‘Binti katoweka…’akasema
mpelelezi akimuangaalia mkuu wake na mkuu wake kwa muda huo alikuwa kaduwaa,
akiwa bado kashikilia simu mkononi, sijui alikwua akiwaza nini, labda alikuwa
akiwaza jinsi taarifa hiyo itakavyofika kwa wazazi wake, na je binti huyo yupo
kwenye mikono salama , na cha muhimu kaenda wapi..kaelekea wapi, na kwanini.
‘Atatokaje pale…mlango
ni mmoja, walinzi wapo mlangoni, haiwezekani, ni lazima kuna jambo la uzembe
limefanyika…, ‘ akasema mkuu kwa hasira.
‘Ni kweli mkuu…huo ni uzembe…’akasema mpelelezi.
‘Hao walinzi watakuwa
wanahusika, natoa amri ukalifanyie kazi hili,, kawaulize, …waseme walikuwa
wapi, wakati huyo binti anatoka, nataka kujua ukweli mara moja …’akasema
msaidizi wa mkuu kwa amri na mpelelezi akatikia amri ya bosi wake akisema
‘Sawa afande,…’akageuka sasa
akitaka kuondoka,… lakini kabla hajaondoka, docta akasema kwa sauti;
‘La muhimu la kujua huyo binti kaelekea wapi, huenda katoka kwa
nguvu za giza za hao watu, hapo alipo hajijui, sasa hiyo inaweza kuwa ni hatari
zaidi, lakini tukumbuke wazazi walitukabidhi huyo mtoto wao wakijua yupo sehemu salama, na kwahiyo ni muhimu sana apatikane kabla wazazi hawajaligundua hilo…’akasema docta.
‘Hahaha unamsikia huyo
mtu wako na imani zake, eti nguvu za giza, kwa vipi….Mkuu huyu mtu inabidi
umuweke chini ya ulinzi, anaweza kutufanya tukashindwa kufanya kazi yetu kwa
imani zake hizo,..halafu umesikia alivyosema, kauli yake ni kama anajua kila
kitu…’akasema mpelelezi
‘Kwanini sasa awekwe
chini ya ulinzi, sijaelewa hapo…?’ aliyeuliza sasa ni wakili na mkuu akawa
kabakia kimia tu.
‘Nyinyi hamlioni hilo
eeh..yeye awali ya yote aliweza kuwatoroka walinzi pale aliposhikiliwa hebu
muulize yeye aliwatorokaje walinzi ndio hiyo nguvu ya giza alitumia,…au..?,…na
hapo hapo, alipotoka, kwa haraka akagundua wapi msaidizi wake alikuwa..nikama
vile alipafahamu kabla…, ‘akasema na kabla wakili hajasema kitu yeye akaendelea
kuongeaa
‘Na sasa binti katoroka,
huyu mtu atajua wapi alipo, hebu atuelezee haraka, ili tusipoteze muda, yupo
wapi huyo binti..au lengo lako tuonekane sisi askari hatujui kazi yetu vyema, si ndio lengo lako au?’ akauliza akimgeukia docta.
‘Kwahiyo kwa kusema hivyo , ina maana wewe unaamini
hizo nguvu za giza au…?’ akauliza docta na mpelelezi akacheka kwa dharau, na
kusema
‘Huyu mtu, ana jambo,
inabidi tuwe makini na yeye, na mimi nimeshamuhisi kuwa anaweza kuwa kikwazo kwenye kazi yetu hii kwa kuleta imani zake, zisizofaa, ...na kama ana amini imani zake hizo, kwanini sasa hatuambii wapi huyo binti alipo, eti docta tuambie sasa huyo binti yupo wapi,.., …?’ akamuuliza docta.
‘Mimi nimetoa ushauri
wangu tu na wala sijui wapi huyo binti alipo, kutoweka kwake kunanipa shida sana, nikijua kuwa mimi ni mmojawapo niliyewahakikishia hao wazazi kuwa binti yako atakuwa salama...na mimi kusema hivyo, ni sehemu ya ushahuri, , au ina maana mimi siruhusiwi kuongea, ina maana gani sasa, mimi kunishirikisha kwa hili jambo,…’akasema docta.
‘Kiukweli wewe hutufai,
na ni vyema, ukawekwa chini ya ulinzi, ili tuweze kuendelea na taratibu zetu,
ukiwa mbali na upeo wetu wa macho..., unaweza ukaharibu…mkuu mimi kwa ushauri wangu huyu mtu awepo hapa,
au sehemu ambayo hataweza kutoka, mpaka tuimalize hii kazi, mtakuja kunikumbuka
kwa hili mkuu…’akasema mpelelezi, huku akijiandaa kuondoka.
‘Lakini mimi sioni
umuhimu wa kumweka huyu mtu chini ya ulinzi, yeye tunasaidiana naye au sio…nia
ni kuwekeza nguvu kwa pande zote, anachokifahamu yeye, na sisi tukichanganya
utaalamu wetu, itakwua rahisi kulishinda hilo kundi,..kama mlivyosema huenda
wanatumia nguvu za giza…’akasema wakili.
‘Sikiliza muheshimiwa,…maswala
ya nguvu za giza, ni hisia tu,..sisi tunatakiwa tutimize wajibu wetu, tuone
kama kweli nguvu za giza zinaweza kutuzuia,..tusiendekeza hayo mambo ya imani
zisizokubalika kisheria...’akasema mpelelezi.
‘Kwahiyo hicho kipengele
cha kuwa wahalifu hao wanatumia nguvu za giza, kisikuwepo..tusihangaike kwa
hilo…tuwekeze kwenye utaalamu wetu wa kawaida, hata tukifungua mashtaka hicho
kipengele kiwe kama ‘kusikia tu’ akasema wakili.
‘Kwanza ni nani kaileta
hiyo hoja hapa, ..ni huyu huyu docta, ndio maana kwenye kazi yangu mimi sitaki
awepo,…anyway, ngojeni nikawajibike…’akasema mpelelezi.
‘Mimi naona tuwe naye,
ili tuweze kuangalia na upande huo pia, na kama mpelelezi huamini hayo, kwanini
sasa unasema, anajua zaidi…atajuaje zaidi wakati mtu mwenyewe, tupo naye
hapa..mimi naona tusaidiane naye na kama anahusika kwa namn moja u nyingine, …ni
lazima tutakuja kumgundua au sio mkuu…’akasema wakili
‘Ok, nimewaelewa
wote,..ni muhimu kwa sasa tuwe timu moja, mpelelezi wewe wahi kulifuatilia hili
swala la kutowekwa kwa huyo binti, kawashughulie hao walinzi, na uwahimize
vijana wako na urudi hapa na taarifa kamili..’ akasema mkuu na mpelelezi akawa
anaondoka, huku akisema;
‘Ok sir…ila huyu mtu
sitaki awe kwenye kazi zangu kama mnamuamini sawa, atawasaidia nyie na imani
zake za kishirikina, lakini sio mimi,…’akasema
mpelelezi.
‘Huyu mtu nitamshughulikia
mimi mwenyewe, usijali….’ akasema mkuu, na mplelezi akaondoka, …na docta
akabakia kimia akisubiria hatua za mkuu huyo.
************
Baadaye wakili akaondoka,
baada ya kuongea kidogo na mkuu, msaidizi wa kituo hicho, Baadae ndio mkuu akamgeukia docta na kusema;
‘Sasa docta sikiliza kwa
hali ilivyo, wewe, inabidi ukae hapa, usiondoke kama kuna kazi ya kufanya
pamoja, tutaifanya pamoja, umenielewa..haya mengine waachie polisi,..natumai
hutaenda kinyume na maagizo yangu tena..?’ akasema mkuu.
‘Hamna shida…’akasema
docta na mkuu huyo akatoka huku ;
‘Docta mimi nipo ofisini
kwangu , kama kuna lolote usisite kuniambia…’
‘Sawa mkuu…’akasema
docta huku akiombea huyo mkuu aondoke haraka kwani kuna zoezi anatakwia
kulifanya haraka iwezekanavyo, na hakutaka mtu mwingine afahamu…
Docta alipoona kabakia
peke yake, na kwa vile ameshaambiwa yeye hatakiwi kuondoka eneo hilo kwa sasa,…alichofanya
yeye ni kuchukua mkoba wake na kuingia kwenye chumba kingine ambacho hakikuwa
na mtu, na alipohakikisha hakuna kitu
cha kuweza kumuharibia mambo yake akaitoa komputa yake ndogo , kutoka kwenye
mkoba wake.
Aliiwasha ile komputa yake, baada ya kuhakikisha
kuwa hakuna kiambata chochote humo kwenye chumba cha kuweza kunasa matukio humo
ndani…, na alipojirisha kwa hilo, ndio akaiwasha komputa yake ndogo, na kuingia
sehemu ya video mbashara, humo pia kuna sehemu yake maalum aliyoitayarisha
ambayo hunasa matukio kutegemeana na jinsi alivyowekeza vinasa matukio …akaanza
kufanya akzi yake huku akiombea awe hajachelewa!
Na wakati huo huo, mpelelezi alikuwa
ameshafika sehemu ya tukio na kukutana na askari ambao walikuwa wakimlinda huyo
binti aliyetoweka…, na wale askari walipomuona huyo mkuu wao, wakiwa na
wasiwasi wakasema;
‘Mkuu huyu mdada
alitoroka kiajabu sana…hata hatuelewi alitokaje humu ndani…’akasema mmojawapo
'Mtanieleza vyema, ilikuwaje?’akauliza
mpelelezi akiangalia upande pale mlangoni;
'Afande tulijitahidi
kufanya kama ulivyotuelekeza, na sijui
ilikuwaje, tuliposimama mwili ulikuwa kama sio wetu, na….baadaye akili
alipokuwa sawa, ndio mwenzangu akaingia ndani, ndio akakuta binti hayupo.
‘Siwaelewi, mlifanya
kama nilivyowaelekeza mimi kwa vipi kuwa mlale, kuwa msiwajibike,,….mimi
niliwaelekeza nini…?’ akauliza akionyesha mshangao, na hao askari wakawa kama
wametahayari, na mmojawapo akasem;
‘Mkuu, sisi tulitii amri
yako,kuwa tuhakikishe huyu binti hatoki humu ndani na tulifanya hivyo, hatujui
ilikuwaje, ..’akasema mwingine.
‘Hamjui ilikuwaje, kama
mlikuwa hapo mlangoni, kwa muda wote…aliwezaje kutoka,..sitaki maneno mengi…?’
akasema mkuu
‘Kama tulivyokueleza
mkuu, muda wote tulikuwa hapa mlangoni,..kuna hal ilitutokea, mwili ukawa
umelegea, huwezi hata kuinua mkono..mara tukajikuta tumesimama, mwenzangu
akageuko huko na mimi huku tukawa tumepeana migongo, na mlango
ukafunguka,..huwezi kugeuka, huwezi kutikisika…’akasema askari
‘Hahaha…hivi kweli nyie
ni askari..’akasema mpelelezi akiwatolea macho ya hasira
‘Mkuu ni kweli kabisa,…tunahisi
kuwa huyo binti alitoka kwa muda huo, na huenda yeey katufanyia kitu au kuna
watu wametufanyia hivyo ili huyo binti aweze kutoka…’akasema mwingine
‘Nyie mna wazimu kweli,
sasa mtaenda kunyea jela,…mtajua ni nini maana ya ulinzi..na ole wenu muongee
kauli kama hiyo isiyoeleweka,…nataka kujua huyo binti akaelekea wapi…kama
hamsemi mtakwenda kusemea chumba maalumu , mnafahamu huko kupoje, sawa..’akasema
sasa akielekea ndani, hakuwawia sana, akatoka.
'Sasa nyie mnakwenda
selo, kama hamuwezi kunieleza huyo binti kaelekea wapi, basi mtakwenda kuelezea
huko kwenye mateso,, …’ akasema mpelelezi.
‘Lakini bosi…’wakaanza
kulalamika, wakaambulia vibao, na kukalishwa kimia, halafu mpelelezi, akasoogea
pembeni na kuchukua simu yake,
.
'Mkuu, ni uzembe
umefanyika, sijui..nahisi walipitiwa na usingizi, yaonekana bint ni mjanja sana..aliwapumbaza
, sijui na kitu gani…watasema wapi alipo..nakuhakikishia hili…’akasema
mpelelezi, akatulia akisikiliza baadae akasema;
'Sawa mkuu nitawawajibisha, lakini hakikisha
huyo docta hatoki hapo maana nimjuavyo anaweza kuharibu hizi harakati zote.. na
mkuu keshakupigia simu, alinipigia ndio,…ok, ok, sijaongea naye lolote…ndio
nimekeulewa mkuu, ni lazima kundi hili
tulisambaratishwe..’akasema.
Alipomaliza kuongea hapo , baadae alisogea pembeni,
akatoa simu yake maalumu, akaingiza alama za siri, halafu akaongea lugha ya
aina isiyo kiingereza au Kiswahili, lakini mwishowe akasema;
'Wapo njiani, sawa mkuu, …wamalizwe tu..ok’
akarusidha simu yake na kugeuka kuwaangalia hao askari, akasema;
‘Inabidi…kwa uzembe wenu
na kushindwa kuzuia midomo yenu, ..sina jinsi, ..’akasema kwa sauti ndogo.
Mpelelezi huyu, yaonekana kuna kitu kikimsumbua
zaidi ya hiyo kazi, akawa anawasiliana na mtu mwingine alipomaliza ndio
akawageukia tena hao askari na kusema;
'Sasa nyie, ok naawamini maana nyie ni askari siwezi
kuwachukua kama wahalifu, na nisingelipenda kuharibu ajira zenu, ingieni kwenye
usafiri huo, mimi nitawafuata nyuma kwa bajaji…’akasema.
‘Sawa mkuu…’hao askari
wawili wakasema sasa wakionyesha mashaka makubwa.
‘Dereva hakikisha
umewafikisha hawa watu kituoni, mimi nawafuata kwa nyuma, hakikisha unapitia
njia hii ya mkato…’akasema akionyesha kwa mkono njia hiyo ya mkato.
‘Lakini afande njia hiyo
ina makorongo, na ni hatari, gari linaweza kukwama, na lolote linaweza
kutokea…’akasema dereva
‘Wewe ndio
unapanga…fuata ninachokuambia, nina maana yangu, unanielewa dereva..’akasema
mpelelezi.
‘Sawa afande…’akasema
dereva.
‘Nazungumza hivyo
kwasababu naogopa foleni,…kwa njia hii ya mkato kama kutakuwa na foleni kwa vile nipo nyuma,
nitajua la kufanya…’akasema na dereva akasema;
‘Sawa afande..’akasema
*********
Wakati hayo yakiendelea mkuu alikuwa naye kwenye
chumba chake maalumu, akiangalia komputa yake, kama alivyokuwa akifanya docta…tofauti
yake ni kuwa alikuwa akitumia komputa kubwa ya mezani…akiwa amechomeka kifaa
chake maalumu ambacho kina nguvu sana ya kunasa matukio.
Mkuu alipohakikisha
msafra umeondoka kwenye lile eneo, kwa haraka akatoka nje, na kwa muda huo
akakutana na docta naye akitokea nje ya kile chumba.
‘Mkuu, kuna watu
wanahitajia msaada wa haraka.., nahisi kuna ambushi …inabidi kuwawahi kabla
hawajakutana na hatari…’akasema docta
'Watu gani hao..?’
akauliza mkuu akikunja uso
‘Wale walinzi waliokuwa
wakimlinda binti, nahis kuna njama za kuwamaliza…’akasema docta na mkuu kwanza
akawa kama anajiuliza ni kwa vipi docta kalipata hilo, akasema;
‘Una uhakika na
unachokisema…?’ akauliza mkuu.
‘Yaonekana hivyo, …’akasema
docta
‘Lakini mpelelezi yupo
huko, na yeye ni mtaalam wa mambo hayo, lakini subiri, nitaongea na dereva, atabadilisha
njia…na kwenye huo msafara kuna watu wetu tayari..’akasema mkuu.
'Mkuu usilizarau hili,
nina mashaka na mpelelezi, ..’ akasema docta na mkuu akamtupia jicho docta,
halafu akasema.
‘Huyo ndivyo alivyo…maneno
yake ya awali yasikutie shaka, mimi amjulia, hata hivyo sizani kama ana lolote
baya…’akasema mkuu.
Docta alitaka kumuelezea
anavyohisi, lakini akaona huo sio muda muafaka, jambo la muhimu kwa hivi sasa
ni kuhakikisha hakuna madhara yanayotokea.
‘Sawa mkuu mimi
nakuaminia…muhimu hao askari wasije kuingia kwenye mitego ha ya hao watu…’akasema
docta
'Docta mm ni mkuu, ndio
maana nimeletwa huku, ukiwa na watu kwenye hii kazi kitu cha muhimu ni kuona ni
nani na nani yupo na wewe, pili,…utaalamu na elimi uliyo nayo inavyoweza
kukusaidia..mimi sijapewa hivyo vyeo bure bure, nimesoma na nimepitia mafunzo
yote…’akasema msaidizi wa mkuu.
‘Ok, sawa…naona
tusipoteze muda…’akasema docta, na mkuu akatabasamu , huku akiangalia simu yake
iliyokuwa ikilia..
‘Ok, sasa ingieni bara
bara kuu, msiendelee na bara bara hiyo ya mkato,..’akamuelezea dereva
‘Lakini…bosi ndiye
katuelekeza hivyo, na nyuma yetu…’akasema dereva
‘Nisikilize mimi mkuu wako
wa kituo, unanielewa, achana na maagizo yake, fuata maagizo yangu,…’akasema
mkuu.
‘Sawa mkuu..’akasema
dereva na kupindisha gari kwa haraka kuingia bara bara kuu na wakati wanapita
ghafla wakaona magari mawili yakigongana, lakini kwa utaalamu wake, akaweza
kuipita hiyo ajali kabla hawajazuiwa..na ikawa heri kwo,…
Huku nyuma,…Mpelelezi
akaona hiyo hali ya dereva kutoka kufuata masharti yake ya kupitia njia ya
mkato, na tendo hilo lilimkwanza , na kwa muda ule simu yake ya dharura ilikuwa
ikiita, na alishajua ni kwanini anapigiwa, …
‘Hawa watu wameharibu…’akasema
mpelelezi, na kosa la namna hiyo linaweza kumharimu, hapo akahisi hatari inayomkabili,
hata hivyo, inabidi kutafuta njia nyingine mbadala, akikumbuka amri aliyopewa
‘Hakikisha hao watu
hawafungui mdomo wao, na wakifungua mdomo wao wakaelezea …ujue sisi tutaifunga
mdomo wako milele..’sauti hiyo ilimfanya mpelelezi ahisi matumbo yake
yakimcheza- cheza,..akijua sasa hivi hata yeye yupo hatarini..
NB: Najua sehemu hiyo
itakuwa haieleweki , haipo wazi …, hata mimi imenisumbua kidogo, lakini ndivyo
ilivyokuwa na baadae utakuja kuelewa zaidi huko mbele.
WAZO LA LEO: Uwongo mwingi, na kujifanya mjanja kuhadaa
wengine, ukachuma jasho lisilo halali yako, kwa hadaa kugushi, veti bandia nk..,
ukajijenga, nk..lkn ukumbuke mungu yupo anayaona yote hayo, na ukumbuke kuwa
hayo unayoyafanya yanaumiza wengine, je wao hawana haki…je wao hawaumii, je wao
hawamuombi mungu wao,..basi ni bora ukaanza kubadilika, ukatubu kabla siku
haijafika, siku ambayo uovu wako, hadaa, nk..vitajulikana,..
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment