‘Na mimi siwezi kuondoka bila kukuambia yote
aliyotuagizia mkeo…maana hayo maagizo hayataki kuchelewesha, kama ni kucheleweshwa
iwe ni juu yako….na lolote likitokea tusije kuja kulaumiwa sisi kuwa hatukuweza
kukuambia, na hata mbele ya mungu tuwe tumenawa mkono, yeye ndiye atakuwa
shahidi wetu…’hayo
yalikuwa maneno ya docta, yakiwa yananielea akilini
Nilifika nyumbani kwangu
nikiwa nimejaa hasira, na sijui kwanini,…kwa muda huo sikujijua, na sikujua
sababu, zaidi ya kuwa hivyo.
Nilifungua mlango
kwa haraka, na kama mtu angejitokeza hapo kwa muda huo, sijui ningemfanya
nini.. akili ilikuwa imesahau kabisa kuwa nilikuwa na jukumu la toba,…toba
ambayo masharti yake ni kuwa uwe mbali na jaziba, uwe mbali na husuda, chuki…visasi..kwa
kifupi ilitakiwa moyo uwe safi, lakini kutokana na hayo waliyoniambia docta na
mkewe, vikanifanya nisahau kila kitu…
Niliingia ndani kwangu na kujipweteka kwenye
sofa, nikiwa nimeangalia juu, kama
nahesabu vilivyopo huko juu, japokuwa akili haikuwepo hapo, ilikuwa mbali
kimawazo…na mara nikahisi kuwepo kwa mtu mwingine, ..
ILIVYOTOKEA, wakati nikiwa nimelala hivyo,.. ilikuwa kama nimeshikwa na
usingizi , au ganzi fulani hivi, na hii
hali imekuwa ikinijia vipindi hivi vya majaribu, yaani kinakuja kitu kama kausingizi , halafu mwili unalegea kabisa, na baada ya hapo
kunatokea kitu kisicho cha kawaida…
Sasa,..ninachokumbuka
mimi ni kuwa, macho yangu yalikuwa
mazito, na mwili ukawa umeshikwa ulegevu, kwa hali kama hiyo unachopweza
kukifanya ni kuyazungusha macho kutizama
huku na huku, lakini viungo vinakuwa havina nguvu ya kuinuka, ila unaweza
ukajiwa na hisia ya kuwa umeinuka, ukafanya jambo…
Haya….hali hiyo
ilipotokea kwa muda huo, ndio nikaona jambo la ajabu..
Nilimuona mtu kaja kusimama mbele yangu, kwa
mbali kidogo,..na haraka nikatambua kuwa ni mke wangu, yaani ndivyo nilivyoona
kitaswira na kiakili…!
Sikuwa na haja ya
kujua mke wangu katokea wapi, ila nilichojiwa nacho akilini, ni kutaka kuinuka
na kwenda kumpokea, kumkumbatia..lakini mwili hauwezi kuinuka,…hata hivyo akili
ikanivuta kuwa nimeshasimama…sasa namsogelea, lakini simfikii…nikawa namkodolea
macho t.
Mke wangu hapo
alionekana wa ajabu kabisa, alikuwa kavalia vizuri, nguo nyeupee na nyepesi
ambayo niliweza kuona maumbile yake ya ndani…kwanza nikataka kumuuliza kwanini
mke wangu kavalia hivyo, sio kawaida yake, lakini nikasema moyoni, hizo labda
ni nguo za kulalia, haina shida,…lakini kulikuwa na kitu kingine cha ajabu…..
Pamoja na y a kuwa
mke wangu kavalia hivyo, na niliweza kuona maumbile ya ndani, lakini sikuweza
kuyaona yalivyo, maana, yalikuwa yakimeta meta, kwahiyo huwezi kuona mwili,
unachoona ni kama mchoro wa mwili wake wenye miale kama ile ya jua na macho
yanapata shida kumuangalia , nikainua uso ili nimuangalia usoni,…alikuwa ndio
yeye…, nikahema
‘Sasa kwanini
simfikii mke wangu…’nikasema huku nikimsogelea kihisia, lakini kila
nilivyosegea alionekana kwa umbali ule ule….
Sasa yeye akawa ananiongelesha jambo…, lakini
sikusikia anachosema,..ni kama ananionya au kunisuta, au kuniashiria nifanye
jambo fulani ..na kuna muda alionyesha kama kukasirika,…na ghafla nikasikia
sauti…
‘Shemeji
nikutangenezee chakula gani…’ Ilikuwa sauti iliyonishtua, …na hapo hapo ile hali
ikaisiha, na haraka nikazindukana na nilipogundua kuwa aliyekuwa kasimama mbele
yangu ni yule mtu nisiyetaka kuongea naye, kwa haraka nikasimama,..hasira
chuki, vikauteka tena ubongo wangu…
‘Aaaha, …kumbe ni huyu mshe—nzi,….’ nilisemea akilini
haku nasonya..nikatembea kuelekea chumbani.
Nilipofika chumbani kwangu, nikajitupa
kitandani, na wakati nafanya hivyo, maneno ya docta yakatanda kwenye ubongo
wangu:
‘Na mimi siwezi kuondoka bila kukuambia yote
aliyotuagizia mkeo…maana hayo maagizo hayataki kucheleweshwa, kama ni
kuchelewesha ucheleshe wewe mwenyewe….na lolote likitokea tusije kuja kulaumiwa
na mbele ya mungu, ….’.
Nilijiunua kichwa
changu na kuangalia darini, sasa nikaogopa ile hali ya kuona taswaira isije
ikanirekjea tena,…nikajiinua kwa haraka, halafu nikasimama na kutembea kuelekea
dirishani, na wakati natembea akili yangu ikawa inaendelea kukumbuka mazungumzo
ya docta na mkewe,….maneno waliyokuwa wakiongea wakati huo mimi nilikuwa natembea
kutoka nje kwa hasira, lakini niliyasikia, baadhi…
‘Mkeo alikupenda sana…hakujijali yeye
mwenyewe…sikia kwanza usiondoke…yeye alikujali sana..hakuijali nafsi yake kama
wewe… kwani alifiki hatua ya kukutafutia hata mke gani umuoe,….’ Hayo aliyasikia, lakini sikutaka kusikia
zaidi, ila kuna neno la mwisho lililonifanya nikimbie kabisa humo ndani…
Mara nikasikia mtu
akigonga mlangoni, nikajua ni nani, sikuitikia nikakaa kimia, na mara simu
yangu ikaita….
Nikabakia kujiuliza
niitikie huyo wa mlangoni au kwanza niangalia ni nani anayepiga simu, ….mara
yule mlango akaacha kugonga, na mimi nikaisogelea ile simu, ilikuwa namba mpya
kwenye simu yangu…nikaiangalia ile simu, moyoni sikupenda kuipokea, sikutaka
kuongea na mtu……..lakini ikaonyesha mpigaji , kweli kadhamiria kuongea na mimi
Nikaiweka
hewani..na sauti ya docta ikasikika,…. alikuwa ni docta, alikuwa katumia namba
ngeni,..huenda alijua akitumia simu yake, nitagoma kuipokea.
‘Jirani nisikilize kwa makini usikate simu
kwanza, hili ninalokuambia ni la muhimu sana, mimi nipo safarini, lakini
sitakuwa na amani kama hutalisikia hili jambo, uliondoka kabla sijakumalizia,….’
Ni kweli nilishajiandaa kuikata simu,lakini nikaona nisikilize tu…
‘Nimekuambia kuwa
mkeo, alituambia ni nani uje umuoe… na sio
mimi au mke wangu, hilo lielewe wazi, na ni vyema ukamsikia huyo mtu…najua kwa
hivi sasa huna unayemfikiria, lakini tuna uhakika ukituliza kichwa chako
utagundua kuwa kweli huyo aliyemtaka mkeo umuoe ndiye stahiki yako,…kwahiyo
usije ukakasirika ukiona labda sisi ndio tumempendekeza, labsa kwa masilahi
yetu…
Akilini nilitaka
kusema sitaki kumsikia, lakini kwa namna nyingine iliuliza ni nani kwa nini
anachukua muda kumtaja,…
‘Mkeo aliona mbali
, anakufahamu na yeye aliliona hilo kwenye njozi zake, anakujua kitabia, anajua
unahitajia nini…kama nilivyokuambia awali kutokana na imani aliyokuwa nayo mkeo
kwa mungu wake, mwenyezimungu alimpa dalili fulani fulani..na mojawapo ni hiyo
kuwa hatapona,..na nyingine ni nani anayekufaa kuwa awe ni mke wako…
‘Sasa ….mkeo
alituambia kuwa, wewe una hasira sana, wewe una hamaki, wewe una tamaa, na wewe
unataka kile ukitakacho ukipeta, kwahiyo unahitaji mke mwenye subira….na ndio
maana akaona kuwa, mke anayekufaa, si mwingine ni huyo huyo unayeishi naye humo
ndani ya nyumba,…
‘Unasema nini…’hpao
nikajikuta ninaongea
‘Ndio alisema mke
anayekufaa … ni huyo huyo binti
anayekusaidia kila siku hapo nyumbani kwako, mkeo anamfahamu sana, mkeo
alishampima, lakini hakuwhi kumwelezea huyo binti kuwa wewe ndiye unayefaa
kuolewa na mume wangu, ila alimuomba awe karibu nawe, akusaidia mpaka uwe
umejiweza mwenyewe, tatizo ni je atakubali, hiyo ni kazi yako……’akaendelea kusema.
Hebu fikiria
mwenyewe…mwanzoni ilikuwa nikimuona huyo binti na hisi hasira, nahisi kama
ndiye mbaya wangu, ndiye…aliye..oh, sasa naambiwa kuwa ndiye mke wangu alitaka
nimuoe…..haiji akilini, na upendo utatoka wapi wakati chuki zangu zimejaa tele
dhidi ya huyo binti, …haiwezekani….hapo, nikasema;
‘Nyie watu kweli mumenichoka,…,kwanini
mumenidharau kiasi hiki,hata kama sasa nimeishiwa kiasi hiki,….lakini hamuwezi
kuni, eti nimuoe mfanyakazi wangu wa ndani mnahisi kuwa labda mimi natembea
naye, au sio, sitaki kusikia zaidi, nakata simu….!’ Nikawa sasa nikitaka
kuikata ile simu,lakini kila nikibonyesha kitufe cha kukata simu ikawa
haizimiki na sauti ya docta ikawa inaendelea kuongea;.
‘Hili ninalokuambia
mimi sio uwongo, ni mkeo mwenyewe, alituambia hivyo, kuwa huyo ndiye chagua lake
na huyo ndiye anayeweza kuishi na wewe, wengine hawatakuweza, kutokana na tabia
yako..na zaidi ya hayo, yeye kwa njozi zake, alivyoonyeshwa kwa ishara huyo
ndiye atakupatia kile ulichokuwa ukikitafuta siku nyingi….’akasema docta.
‘Huyo ndiye ataweza
kukupatia mtoto…’akasema na mimi hapo nikahisi kama kitu kimemwagiwa kichwani ,
kitu cha baridi.
‘Jirani mimi kama
nilivyokuambia, huwa naota tu, na ndoto kwangu ni ndoto tu, lakini ndoto ya
jana imenifanya nifikiri sana… jana usiku, hutaamini mkeo ainijia tena kwenye
ndoto,…ndoto kwangu ni ndoto tu, lakini kwa hii nimelichukulia kuwa ni kweli…alikuja
akiwa kavalia vaza la ajabu, anameta meta mwilini…..sijui nikuelezeje…’akasema
docta
Baadaye nikawa sina
mawasiliano na docta, nahisi walifika sehemu hakuna mtandao…nikaiweka simu
kitandani na sikutaka kulala tena, nikatembea hadi dirishani na kuangalia nje
Nikawa najiuliza
ilikuwaje, ina maana ,..ndoto ile ile niliyoota mimi, na docta naye kaiota
hivyo hivyo…maana docta kanisimulia vile vile kama nilivyoona mimi…alimuona mke
wangu akiwa na vazi lile lile, akiwa na maumbile yale yale….hapa sasa kuna
jambo, nikahema kwa nguvu…
**********
‘….na ndio maana akaona kuwa, mke anayekufaa,
si mwingine ni huyo huyo unayeishi naye humo ndani ya nyumba,…’ maneno haya yakawa yanajirudia sana kichwani
mwangu, mpaka nikahisi vibaya, …
‘Mimi siwezi kumuoa
huyo….sitaki sitaki….’nikawa nasema huki najikuna kuna kichwa kama mtu
aliyechanganyikiwa. Baadaye nikatulia, na kuanza kuchanganua hilo jambo, kwanza
nikajiuliza kulikoni..
‘Kwanza sitaki
kuoa, ..pili simtaki aliyependekezwa, tatu….’hapo nikasikia mlango ukigongwa,
nikajua ni nani..sikutaka kuitikia nikakaa kimia, huku nikizama kwenye mawazo…
‘Mfano..nasema
mfano, naamua kumuoa ili kumrizisha mke wangu, nitauweka wapi uso wangu…’nikasema
kimoyo moyo
Niliwaza mbali
nikikumbuka maneno ya watu, walivyokuwa wakinihsi vibaya kuwa mke wangu
kafariki, na sasa nakaa na kimada, najifanya ni mfanyakazi wangu wa ndani kumbe
ni kimada wangu…najifanya naombeleza kumbe naendekeza zinaa…., sasa wasikia
kuwa nimemuoa, si ndio watasema, `mnaona tulisema…huyu jamaa anatembea na
mfanyakazi wake ndani sasa kathibitisha kabisa, ….’ Nikawaza hivyo.
‘Ndio….kaniambia uoe, na usioe mtu mwingine
zaidi ya huyo binti mnayeishi naye huyo ndiye chaguo lake, sasa kama unataka
kumkaidi mkeo sawa, na huyo ndiye atakaye kupatia mtoto…..’nikakumbuka maneno ya mke wa docta.
****************
Siku hiyo ikapita, na nyingine na nyingine,
mawiki , mwezi..miezi…
Kiukweli sikupenda
kuoa tena..lakini hata mimi ndoto za mara kwa mara za kunijia mke wangu kuwa
nifanye kile alichokita zikawa zinanitesa sana, siku zikawa zinakwenda, nikawa
natokewa na ndoto hizo zingine mbaya, mpaka napiga kelele, kama mtu
aliyechanganyikiwa.
Hali hi iliendelea
mpaka siku moja huyo binti akamuita docta wa akili, huyo docta alifika, nikiwa
hata sina habari…na akaja kujitambulisha kuwa yeye ni docta wa mambo ya akili,
na amefika hapo kuja kunisaidia..
‘Nani kakuambia
ninaumwa akili..mimi sijachanganyikiwa…’nikasema
‘Unaweza kusema
hivyo, lakini ukijiangalia kwenye kiyoo utagundua kuwa wewe haupo
sawa..unahitajia matibabu…’akasema
Sikutaka kubishana
naye sana, nikatulia, na yeye akaanza kunihoji, kwanza nilimtolea nje kuwa mimi
siumwi, lakini baadaye akaniweka sawa, nikamuelezea mengi yanayonitokea…mengi
kuhusu maisha yangu..lakini sikumuelezea hilo la kuwa natakiwa nioe, na …nimuoe….
‘Sikiliza..hali
uliyo nayo, unahitajia mke,..labda nikuulize ni kwanini huoi…?’ akaniuliza,
‘Mimi sitaki kuoa…aliyekuwa
mke wangu ndio huyo kafariki, na mimi nilishakufa kimwili, kihisia…sina hisia
za mke mwingine yoyote….’nikasema na docta kwa utaalamu wake, akanielezea mambo
mengi, kuwa hayo yanayonitokea ni kuwa akili yangu haitaki kuondokana na
kumbukumbu za mke wangu na kwahiyo ili hizo kumbukumbu ziondokane na mimi dawa yale
aliyoiona yeye, ni mimi kuoa.
‘Oa mke ambaye
atakuliwaza, wake mungu kawaleta humu dunia, kutusaidia, na kutuliwaza sisi
wanaume..mchague ambaye atakupendezesha, ambaye anaweza kuchukua nafasi ya mke
wako…vinginevyo, hali hii haitakwisha, na huko unapokwenda ni kubaya tena kubaya zaidi, umeshafikia hatua mbaya
sana, chukua hatua kabla hujachelewa…’akasema docta na baadaye akaondoka.
'Na ningeshauri, awepo mwanaume....huyu binti..ni hatari kuendelea kukaa na wewe humu ndani....'akasema docta, na nilimuangalia yule binti, akionyesha wasiwasi machoni.
Docta baadaye akaondoka....
Docta alipoondoka tu,
nikamvaa huyo binti, nilimfokea sana huyo binti mpaka akawa analia.., na hata
nikafikia hatua ya kumsema vibaya kuwa hizo ni mbinu zake,..
‘Kama ni mbinu zako
za kutaka kuendelea kukaa hapa …basi utaondoka tu, sikutakia humu ndani, uondoke ...nani kasema anakuhitajia humu, uondoke..…’na huyo binti alibakia kimia,a yeye akabakia kimia
hakujibu kitu zaidi ya kulia tu.
Ikapita miezi, hali
ile ikawa inaendelea kunitesa, na kweli kila mtu aliyeniona alijua kuwa mimi sasa nimechanganyikiwa, haikupita muda wakawa wanakuja ndugu zngu , hata wazazi wangu, na kila mmoja aliyefika aliishia kunishauri nioe..., lakini
sikuweza kuwasikiliza,…
Sasa siku moja ndio
niliota ndoto mbaya zaidi….ndoto iliyonifanya nipige ukulele sana,…na
nilipozindukana, nikahisi moyo kama unatolewa pumzi ..ikawa kama
nimebanwa..ilichukua muda mpaka kujisikia vyema, nikatulia. Na ujue kwa muda
wote huo anayenisaidia ni huyo binti.
Hata sijui ilitokeaje…nakumbuka tu...ilikuwa siku
huyo binti keshaamua kuondoka, …alikuwa ameshafungasha kila kitu,…akawa sasa anaiga, nilishamkubalia aondoke, kwangu mimi kwa uoni wangu huo wa kuchanganyikiwa,....sikuwa naona umuhimu wake, ..
NAFSI, AKILI,…ile
kuwaza kuwa huyo binti sasa ndio anaondoka kabisa, maana alishasema yeye
anaondoka na hatarudi tena,na nilimwambia ni bora afanye hivyo maana akifanya
hivyo itanisaidia hata mimi...huyo binti alisema sawa kwa sauti ya unyonge, hakuwa na jinsi...
Sasa ndio huyu kweli....keshafungasha, ananiaga.
Sijui ilikuwaje,nilihisi upweke fulani ghafla. nilihisi kumkosa mtu muhimu kwangu …ilikuwa
kama vile namuona mke wangu ananiaga, ghafla nikajikuta nimemkumbatia huyo binti….huku
nasema;
‘MKE WANGU
USIONDOKE,…usinieche peke yangu…..’ Huyu binti alibakia kaduwaa, na kwa vile
alishanizoea kuwa nimechanganyikiwa, yeye alitulia tu, akiwa anaogopa, unajua huyu binti japokuwa anaishi hapo lakini ananiogopa kweli, hasa akikumbuka siku zile za zamani nilipotaka kumbaka....
Baadaye huyo bnti akasema;
‘Shemeji mimi sasa naogoa kwa hali uliyofikia,...hata hivyo, pia haifai wewe kubakia peke yako, hutaweza, ni bora nipitie kwa ndugu
zako mmoja aje kukaa na wewe hapa…’akasema
Oh….nikakumbuka,
kumbe sio mke wangu… nikakurupuka, nikasimama pembeni,nilikaa kimia kwa muda,
na ghafla machozi yakaanza kunijaa machoni, nikajikuta nikilia..nililia sana,..unajua kulia..., nililia sana
siku hiyo…mpaka nikawa sina nguvu tena..halafu nikasema;
‘Mke wangu…nakupenda
sana, haya yote ni kwa ajili yako, sijui nifanyeje nini, kukuonyesha pendo langu
kwako, namuomba mungu aichukue roho yangu, ili nije huko ulipo…ooh,…’nikatulia ..na nilihisi yule binti akiwa karibu yangu, alifanya kama vile mama anavyofanya kwa
mwanae..akawa kaniwekea mkono wake begani, kama kuniliwaza akasema;
‘Shemeji,..mungu
atakusaidia, utapona tu,..haya yana mwisho, lakini usifikie hatua ya kumkufuru mungu,
kwani yaliyotokea ni kwa mapenzi yake, sio kwa mapenzi yetu, mimi na wewe hatuna la kufanya, ila shemeji inabidi mimi niondoke...ila nakuahidi nitajitahidi mmoja wa
ndugu zako waje..'akasema
'Mimi ...najua nakwenda kinyume na maagizo ya mke wako, alisema niskuache peke yako, maana hakuna anayekuweza.... lakini mimi
sasa naanza kuogopa…ninaogopa chochote chaweza kunipata, ..samahani sana
shemeji, kwa kweli kwa hali kama hii sina jinsi, ni lazima niondoke, kwaheri shemeji…’akasema sasa kiwa keshabeba mizigo yake.
Nilibakia
nimeshikwa na butwaa…na nilianza kuhesabu hatua za yule binti, akiondoka... moja , mbili
tatu,..huyo anaondoka…alipofika mlangoni, sikuweza kuvumilia, nikajiinua , na
kwa haraka nikaanza kumkimbilia huyo binti, kabla hajavuka kizingiti cha
mlango..nikamfikia na kumshika begani.
Huyo binti alishtuka sana, mpaka akadondosha lile begi, na karibu apige yowe....
‘Binti tafadhali,
nisamehe….kabla hujaondoka nakuomba unisamehe..nipo chini ya miguu yako….' nikasema sasa nikimpigia
magoti.
Huyo binti akawa anatetemeka kwa uwoga,..akabakia kuniangalia macho yalikuwa na wasiwasi, kaduwaa, hajui hata fanye nini, lakini mimi
niliendelea kumuomba msamaha….na mara nikasikia gari nje likisimama, na mara
nikasikia sauti ya mtu akipiga hodi…. Na kabla sikajaa sawa,…. huyo binti, akalegea, na kudondoka chini, sakafuni na kupoteza fahamu…
NB: Nashindwa
kuimalizia leo, kuna mambo mengi hapo yalitokea na ili kisa hiki kiishe vyema,
ni wajibu kuyaandika, samahani sana tukutane sehemu ya mwisho
WAZO LA LEO: Akili
zetu za kibinadamu zinapokutwa na mitihani , iwe ya misiba, iwe ya njaa, shida,
au matatizo mbali mbali kama ya kukataliwa, …kumkosa uliyempenda, nk..hufikia
kujilaumu sana, na hata kujiona hatuna faida,..na wengine hufikia kubaya na
kusema bora waafe…hii sio sahihi, tujue kuwa mambo hayo hutokea kwa mapenzi ya
muumba.
Tujue kuwa mola
wetu, yeye ndiye anayejua ni kwasababu gani, hayo yanatokea, huenda mengine
hutokea ili iwe ni heri kwetu, na mengine hutokea maana muda wake umefika. Sasa
sisi kama wanadamu watiifu kwa mola wetu kinachowajibika kwetu kwanza ni kumshukuru
mola wetu…na, pili ni kuzidi kuomba rehema zake, maana yeye ndiye mjuzi wa yote.
Ewe mola wetu, tupe subira , tuondolee mitihani
hii ya maisha na ikitukuta tupe moyo thabiti wa kuweze kusubiria, na utujalie mafanikio
mema…bila wewe mola wetu, sisi hatuwezi kitu, …sote tuseme Aamin….
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment