Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, August 12, 2016

TUYAENZI YA WAJA WEMA KWA VITENDO



Jamaa yangu kanihadithia ndoto yake ya ajabu …nikaona sio vyema kuiacha kuiweka ndani ya shajara yangu(diary yangu) , ili kila mtu apate kuwaadhika nayo.

‘Ndugu yangu, nimekuwa nikimuoata sana mzazi wangu tangia aondoke hapa duniani,…hutaamini , baba yangu alikuwa mtu wa ibada, mcha mungu wa vitendo, sio muongeaji sana, na kila siku alikuwa yeye ni wa kwanza kuingia msikitini, na kuna sehemu yake maalumu alipenda sana kukaa hapo mstari wa mbeel kabisa..kiasi kwamba kila mtu aliitambua sehemu hiyo kama sehemu yake. Hata alipofariki waumini wengi walimuombea duwa na kuienzi sehemu hiyo kama sehemu yake.

Basi mimi kila nikilala usiku , ikatokea nikamuota mzazi wangu huyo , na mara nyingi namuota akiwa sehemu hiyo amekaa, na hapo namuendea tunaongea ndani ya..na ni pale pale msikitini  kwenye sehemu yake…Nashindwa kuelewa ni kwanini mara nyingi namuota yupo sehemu hiyo na si sehemu nyingine, nikaja kumuuliza kiongozi mmoja wa dini, akaniambia ina maana mzazi wangu huyo anakuwepo sehemu hiyo kila muda wa ibada, ni neema kubwa mungu kamtunuku.

‘Sasa basi ikatokea wiki iliyopita nikaota nimefika hapo msikitini, nikitarajia kumkuta baba yangu sehemu hiyo,…, lakini cha ajabu sehemu ile nikaikuta ipo wazi, na watu wamekaa sehemu zote ile pale pamebakia wazi,…kama vile wamemuachia yeye,.. nikaingiwa na mashaka. Ndani ya ndoto, nikageuka ili kumtafuta, nikamuona baba yangu huyo kasimama mlangoni, huku kainama kwa masikitiko.

Nikamwendea na kumuuliza, kulikoni, akasema;

‘Mimi nasikitika sana, maana matendo yangu mema hutaki kuyaendeleza, nilitarajia wewe kipenzi changu ungekuwa ukikaa ile, ukafanya kama nilivyokuwa nikifanya ili yale mabaya yangu yasafishwe, na mimi nipande daraja kwa kupata fadhila njema huku. Wenzangu wana watoto wao wanaendeleza matendo yao mema na wazazi wao hao wamepanda madaraja, …lakini mimi nipo pale pale…

Basi nilipozindukana nikamuendea imamu, kiongozi wangu wa dini nikamuuliza, akaniambia huo ni ujumbe , na ni ujumbe wa kweli, unatakiwa uufanyie kazi,..’akaniambia na kuzidi kuniasa akisema

‘Kuna wengi wetu hatupendi kuyaendeleza mambo mema ya wazazi wetu waliotangulia mbele za haki kazi yetu ni kusifia tu, baba yangu alikuwa hivi alikuwa hivi..au kiongozi fulani alikuwa hivi au vile lakini kimatendo tupo mbali kabisa na tabia hizo njema....hiyo kuongea tu haitoshi kama ni matendo mema basi tuyaendelezeni, hasa ya wazazi wenu…na kwa kufanya hivyo, tutayafukuza matendo maovu..

Basi kuanzia siku ile nikawa sasa najitahidi kufika msikitini mapema, na kukaa sehemu ile ile…hutaamini nikaja kumuota baba yangu akiwa pembeni yangu sehemu ile ile. Akiwa amefurahi kweli huki akiwa, kava joho la Hariri…

Jamani ndugu zanguni hivi kweli tunawakumbuka waliotangulia mbele ya haki kwa matedo yao mema, au ndio tunasubiria siku ya kuwaombea tule pilau na kuondoka…, kwanini tusijenge tabia njema ya kuwaenzi wapendwa wetu hao kwa kutenda yale matendo yao mema waliyowahi kuyafanya, ….na tukifanya hivyo hayo matendo mema ni hakika yatafuta matendo yao mabaya na wao watapanda madaraja.

Tukiacha kuyaenzi matendo hayo mema, ni dhahiri kuwa matendo mabaya yatashika nafasi, ..ndio maana sasa hivi matendo mabaya ndio yamezidi, mpaka watu wanayapigia debe,..angalia maangamizi ya kizazi cha nabii Nuhu,(sodoma na Gomara)…Sasa hivi yameshamiri, na watu wanachekelea, wanapigia debe, na hata kuyafadhili, nani atayakemea , wakati bwana mkubwa kayafagilia…haya ndio madhara ya kuacha kuyaenzi metendo mema ya waja wetu wema.

Tumuombe Mungu atusamehe na atusaidie, kutuepushia na janga hili ovu, kwa ajili ya vizazi vyetu, tusije kupata maagamizi kama hayo yaliyotokea kipindi hicho, ..tusione hizo ni hadithi, hayo tumeandikiwa ili tujifunze, na tuweze kujihadhari nayo...maana yaliyokuwepo, yatatokea, na sasa yanatokea….hala hala mti na macho..

Tumuombe mola awarehemu wazazi wetu, ndugu na jamaa zetu waliotangulia mbele ya haki, mola awalaze mahali pema peponi. Na tunakuomba ewe mola wetu, na sisi tuendeleze matendo hayo mema, ili vizazi vyetu navyo viyaendeleze hivyo hivyo hayo matendo mema na kuyaepuka matendo maovu…na utujaliwe tuwe na mwisho mwema…Aaamin..
Sote tuitikieni Aaamin…

Ijumaa kareemu


Ni mimi: emu-three

No comments :