Rafiki yangu
hutaamini , nilipoteza fahamu siku tatu,
‘Siku tatu, kwa
vipi…?’ nikamuuliza msimuliaji wa hiki kisa
‘Yaani … siku nipo
, madocta wanahangaika huku na kule, hadi ikafikia watu wakajua sasa nimeshakufa...na
wakiwa wameshakata tamaa ndio nikazindukana. Na nilipozindukana kwa muda huo
sikujua nipo wapi, mara nikasikia sauti…
‘Docta. Docta…njoo mgonjwa kazindukana…’ hapo nikajua kumbe nipo
hospitalini, lakini kwanini…akili ilikuwa haiweze kutambua, .
Nilijua huyo
aliyeita ni mwanamke, kutokana na hiyo sauti, lakini sikujua ni ya nani…, kuna
wazo liliniambia huenda ni sauti ya mke wangu, nikawa sijielewi elewi,…sijui
nielezeje hapo,…
‘Basi muacheni
atulie msimwambie au kumuuliza kitu chochote…’nikasikia sauti ikisema hivyo,…hapo
nilikuwa nasikia wanavyoongea, lakini ile akili ya kutafakari, ilikwua haipo, nilikuwa
kama buwa, akili haielewi kitu!
Nilikaa hivyo hivyo
kwa siku nzima, nageuza macho tu…na ilionekana kama nimepatwa na tatizo
jingine, mwili hauosegei zaidi ya kutembeza macho, akili haifanyi kazi zaidi ya
kusikia wanavyoongea na kuwasa hapo kwa hapo, baadaye nasahau,..nikawa kama mtu
aliyepooza viungo….
Docta akawa anakuja
na kunipima pima, anajaribu kkuninyosha viuongo, lakini sikumuelewa ni kwanini…akiinua
mkono kuuwek hewani, akiachia unadondoka kama sio wangu….
‘Kwa hali hii
anahitajika mtu wa kukaa naye karibu…’akasema docta na jamaa zangu wakawa
wanashauriana, ilionekana kila mtu alikuwa na shughuli muhimu kwake, na
akabakia binti mmoja , kwa muda huo sikumtambua, yeye akasema;
‘Mimi nipo tayari
kukaa naye…’akasema
‘Lakini huyu ni
mwanamke atamsaidiaje..’wakaulizana
‘Sawa hamna shida
atasaidiana na manesi , ni muhimu tu kwa mtu wake wa karibu kuwepo, kazi
nyingine wapo watu wa kuzifanya..’akasema docta
Basi siku , wiki
,hadi miezi ikapita mimi sijijui, hata ukiniuliza jina langu nilikuwa siijui
ninaitwa nani, na hata wakati mwingine wakiniita kwa jina , nilikuwa siitiki
maana sikujua kuwa wananiita mimi… hapo sasa ikaonekana nina tatizo jingine…
Baadaye nikaanza
kuinuka,..hata kutembea kidogo kidogo…lakini akili bado ilikuwa haijafunguka…
‘Hili ni tatizo
lakini litaisha taratibu…’akasema docta
Docta akashauri nirudishwe
nyumbani lakini mara kwa mara kuwepo na mtu karibu wa kunichunga, na Yule yule
binti ambaye aliyejitolea kule hospitalini akawa tayari kunisaidia sijui kwanini….
Nilikuja
kujua baadaye kuwa huyu alikuwa binti kwa upande wa mke wangu, ambaye kipindi
hicho cha nyuma alikuwa akifika hapo nyumbani kumsaidia mke wangu. Alikuwa
akimpenda sana mke wangu!
********
Siku moja nikiwa nimepumzika ndani, nikiwa
peke yangu, nikaanza kufungua fungua makabati, napekua pekua kwenye droo za kabati,
sijui natafuta nini, mara nikaona
shajara(diary), nikavutika kuisoma,….akilini nilikuwa najisomea tu,…
Sasa kitu cha ajabu
kila nikisoma kilichoandikwa humo ilikuwa kama mtu anayenikumbusha jambo
fulani, akili inakuwa kama inajenga hoja ya kujiuliza na kujiuliza huko kunazua
,maswali mengi, nikiaona nimechoka naiacha naanza kutembea tembea huku na huku nikitafakari,
baadaye nairudia tena.
‘Nikawa kila mara navutika
kuitafuta sajara hiyo na kuanza kuisoma,..ninasema naitafuta , maana nikitoka
pale ninakuwa nimesahau kabisa niliiweka wapi…ila kuna kitu kinanishitua kuwa
niende pale kwenye kabati nitafute tafute halafu nakutana nayo tena naanza
kuisoma, ikawa sasa ndio sehemu ninayopenda kukaa kwa muda mrefu..
Huyo binti akawa
ananishangaa , maana ananiona mara nyingi nipo hapo kwenye kabati natafuta
tafuta baadaye ananiona nimetulia, na nikiwa hivyo sikupenda aniulize jambo,
basi ananicha mpaka mimi mwenyewe niwe nimechoka, nainuka hapo naanza kutembea
tembea..
Siku moja,
nikaisoma sana hiyo shajara ….huku ninawaza sana, mimi ni nani, ilitokeaje,
nikawa nawaza kwa bidii sana…..ikafika muda hata kichwa kikaanza kuniuma sana,
huku najilazimisha kujua, kujiuliza… kuna kitu kinanijia kunaipatia majibu, lakini
hakikai, nikawa najilazimisha kujua….sasa yakawa yanakuja maumivu makali kichwani
mpaka nikapoteza tena fahamu…
Huyu binti anayenisaidia
akanikuta nimelala sakafuni, nimepoteza fahamu, niliambiwa aliwaita watu, wakajaribu
kunihudumia lakini zikuzindukana, wakaamua kunipeleka hospitalini…nikalazwa
tena…
Huku hospiatalini
ilipita siku nzima sizundukani, wanasema kuna muda nakuwa kama nataka
kuzindukana lakini inaishia kutikiswa-tikiswa, halafu natulia…, lakini sifungui
macho, nipo tu..docta alisema ni dalili kuwa akili inaanza kufanya kazi ya
kukumbuka mambo…ndivyo walivyoniambia hivyo baadaye…siku mbili , baadaye
nikazindukana,sasa niipozindukana, mambo
yakawa tofauti.
‘Mke wangu yupo
wapi…?’ ilikuwa kauli yangu ya kwanza siku hiyo, na watu waliokuwepo humo ndani
wakawa wanaangaliana…alikuwepo docta, na baadhi ya ndugu zangu na huyo binti
aliyekuwa akinihudumia huko nyumbani.
‘Ni mimi
hapa….’akasema mdada mmoja..Nikamuangalia kwa makini, nikajaribu kukumbuka
nilimuona wapi,
‘Wewe ni nani…?’
nikamuuliza nikimuangalia kwa mashaka
‘Umenisahau mkeo….’akasema
akionyesha aibu aibu
‘Mhh..mke wangu
siwezi kumsahau, mke wangu yupo wapi..?’ nikauliza na watu wakabakia kimia
‘Si huyo hapo,….’sauti
ikasema na nilimuangalia mzungumzaji alikuwa akimnyoshea huyo mdada kidole,
nilimuangalia huyo mdada kwa makini, na kumbukumbu zikaanza kunijia,
nikakumbuka kuwa ni mdada aliyekuwa akija nyumbani kipindi cha nyuma..lakini
sikukumbuka kuwa muda wote ndiye aliyekuwa akinihudumia.…
‘Acha utani unafikiri mimi simfahamu huyu, …’nikasema
‘Huyo ni nani..umemsahau
mkeo, hukumbuki kuwa ndiye mliyekuwa naye siku zote akikuhudumia…’nikaambiwa
‘Akinihudumia, mimi…hapana..kama
nikuja labda amekuja leo...ila mimi ninamkumbuka kuwa yeye ni shemeji yangu! Mimi
ninauliza dada yake huyu yupo wapi…?’ nikauliza sasa nikijitahidi kujiinua.
Na watu walibakia
kimia, nikamgeukia huyo mdada na kumuuliza
‘Ulikuja lini, je uliweza
kuingia kumuona dada yako huko alipolazwa…?’ nikamuuliza, na yeye sasa akainamisha
kichwa chini kama aibu fulani, na mara nikasikia sauti ya mzee ikisema.
‘Docta unaonaje tumwambieni
ukweli…?’sauti hiyo ilitokea nyuma ya kitanda sikuweza kumuona vyema aliyeuliza,
ila nilijua kuwa ni sauti ya mzee .
‘Mnaweza….’sauti
nyingine ikajibu, ilikuwa ni ya docta , yeye aikuwa pembeni mwa kitanda,
sikutaka kugeuka kumuangalia, kwa wakati huo macho yangu yalikuwa kwa huyu
mdada, ambaye nimeshamtambua sasa kuwa ni yule binti aliyekuwa akija kumsaidia
mke wangu kazi za nyumbani.
‘Tajiri…, tunaomba
uwe mvumilivu, kiukweli ni kuwa mungu keshamchukua
mja wake,…mke wako hayupo tena duniani na sasa ni inakaribia miezi
mingapi..saba au nane hivi,…hatukuweza kukuambia mapema kutokana na matatizo yako uliyokuwa nayo awali….’akasema
‘Nyie waongo, mwaka!...mnasema
nini…, hohoho…acheni utani…., hahaha, leo sio sikukuu ya wajinga, mhh…mnasema
nini, mbona mimi siwaelewi, hebu nisaidieni niinuke, ni- nataka kwenda kumuona
mke wangu…’nikasema nikijaribu kujiinua kitandani lakini sikuwa na nguvu za
kufanya hivyo.
‘Sikiliza
Tajiri…hayo tunayoakuambia ndio ukweli wenyewe…! ‘sauti ikasema
‘Ukweli gani…wewe
unayezungumza ni nani kwanza..wewe ni mwanga nini.., ni jana tu nilikuwa
naongea na mke wangu, nyie mnaniambia nini, aah, hebu acheni utani,…’sasa
nikajitutumua hadi nikaweza kukaa vyema kitandani.
‘Sikilizeni sasa
niwaambie ukweli, mke wangu amepelekwa thieta.kufanyiwa upasuaji, hajarudi …mnajua
hata mimi sikuwa naelewa tatizo ni nini…wamesema baada ya upasuaji wataniambia,
sasa ….hata mimi, ninataka nijue tatizo lilikuwa ni nini, hebu muiteni dakitari
mumuulize, yule jirani yangu, sio huyu…, huyu hajui..muulizeni yule dakitari jirani
yangu anafahamu vyema…’nikasema
‘Mliongea na mke
wako wapi, lini..?’ nikaulizwa nikamuangalia muulizaji kwa macho ya kushangaa
‘Wapi lini..jana,…niliongea
naye Hospitalini,….mke wangu alikwenda huko, akalazwa kwa ajili ya upasuaji,
nia ni kusafisha kizazi, …ninajua baada ya upasuaji huo atakuwa hana tatizo
tena..tutapata watoto…nyie hamjui kwa vile hamukuambiwa hayo..mimi najua,
..yupo thieta…’nikasema
Watu wakabakia
kuangaliana…
Kwakwei ilichukua muda mimi kuikubai hiyo
hali…dakitari alisema nizidi kupewa muda,…
Siku ya pili yake niliruhusiwa
kurudi nyumbani, ilikuwa ni kazi, maana nilitaka kwanza nikamuone mke
wangu..hata hivyo baadaye nikakubali, na kurejeshwa nyumbani…,
Ikawa sasa kila
siku nadamka asubuhi nadai nataka kwenda hospitalini kumuona mke wangu…hapo hakukaliki , inabidi
waniruhusu, tunakwenda hadi hospitalini , nikifika nawauliza madakitari, kuhusu
hali ya mke wangu,…
Ilifikia hatua watu
wakaona kama nimechanganyikiwa…, lakini docta alisema akili yangu ipo sawa, ila
hiyo hali bado haijakubaliana na ubongo wangu.
Na siku moja, jamaa
wakanipeleka makaburini na kunionyesha kaburi la make wangu, hapo ndio kidogo akili
ikaanza kukubali-kukubali…lakini haikuwa kazi rahisi..
Naikumbuka sana
siku ile,..sijui kulitokea nini, na ndio nikaanza kukubali kuwa kweli mke wangu
hayupo tena duniani…, ilikuwa siku niliyoumia sana,… siku hiyo ilikuwa ndio
kama vile msiba umetokea kwangu, nililia sana ..mpaka nikawa sijiwezi…
Basi siku zikapita,
…mwaka na kitu sasa…nikawa siongei na mtu…yule binti au mdada ndiye anafanay
juhudi za kunisaidia,..wakati mwingine nakataa kula..anafanya juhudu mpaka
nakula..nikaisha …mwii ukawa kama sio mimi…
*********
Siku moja….nipo
ninaongea na mke wangu, na katika kuongea mke angu akanituma nikamchukulie
kitabu kidogo kwenye kabati, alisema hivyo, na mimi nikasimama sasa kuelekea
kwenye kabati…mara nikazindukana kumbe ilikuwa ni ndoto…
Nilipoamuka
niliwaza sana hilo..kijitabu kidogo, kijitabu kidogo, ni katabu gani hicho,…basi
nikaenda kwenye kabati, wakati napekua pekua, ndio nikakutana na shajara ya mke
wangu.
Ukumbuke awali niliisoma
hiyo shajara bila kujua ni nini ninachokisoma, na kwa muda ule sikukumbuka
kabisa kama niliwahi kuisoma, …sasa kwa hivi naisoma nikiwa na akili zangu
timamu, naelewa kila kitu,… ndipo hapo nikaanza kugundua ukweli halisi kumhusu
mke wangu,….kumbe mke wangu alikuwa akiandika kia kitu , katika maisha yake….
Hapo nikamjua mke
wangu vyema, nikamjua kwa yale ambayo sikuwa nayafahamu….
‘Mungu amlaze
mahali pema peponi….’ Akasema na sote tukasema kwa pamoja
`Aaamini…’
************
Mke wangu awali
kabisa aliandika wasifa wangu, jinsi gani anavyonipenda,..na aliapa kuwa
hataweza kuishi na mtu mwingine zaidi yangu….aliandika maneno mengi ya
kunisfikia, ila kitu alichokiona ni tofauti, na anakiombea kiniondoke ni
hasira..na kupenda sana mali…
Nikawa naisoma hiyo
shajara kwa hisia ….aliandika jinsi gani anavyotamani kuwa na mtoto, lakini
hampati, akaeleze jinsi gani tulivyohangaika mimi na yeye, ikafikia sehemu
akaona mimi nimekata tamaa,akawa anahangaika kivyeka…ndugu zangu upande wa
kiumeni wakawa wanamsakama sana ….
Ikafikia sehemu ya
ugonjwa,…..aliandika kuwa alianza kuhisi maumivu hasa ikifikia siku
zake..ilikuwa ni mateso sana kwake..hali hiyo iliendelea kumtesa sana….
Kumbe Mke wangu
alianza kuumwa tumbo, muda,…nikakumbuka awali kuwa ni kweli mke wangu alikuwa akilalamika
kuwa tumbo linamsumbau, na kuna kipindi tulikwenda mimi na yeye hospitali, na
akatibiwa, na baadae sikusikia tena hilo tatizo, kuna muda analalamika, mimi
nikawa simtilii maanani…najuata sana nikiliwazia hilo…
Kumbe mke wangu baadaye
akawa anahangaika peke yake, na huko akagundua kuwa ana tatizo kwenye kizazi, lakini
kwa jinsi nilivyokuwa bize na maisha ya kutafuta mali, hakuweza kuniambia zaidi…na
kumbe tatizo hio ilifikia mahali akaambiwa hatakiwi kushika mimba…akishika
mimba itakuwa ni hatari kwake, hakuweza kuniambia hilo…aliongea na docta , na
akamwambia docta asije kuniambia kitu!
Katika kupimwa
pimwa walikuja kugundua kuwa alikuwa na uvimbe kwenye kizazi, akatumia dawa za
kienyeji, na ule uvimbe ukaondoka, lakini kumbe kulibakia tatizo humo humo kwenye
kizazi…shimo au kidonda…,na tatizo hilo lilikuja kuharibu kizazi kabisa, na mke wangu aliposikia hivyo,
alijitahidi sana kutafuta njia za kuniambia lakini alishindwa...
Mimi nilikuwa
nataka mtoto, sasa akiniambia hatanipatia mtoto itakuwaje, ina maana
nitamfukuza, au nitatafuta mke mwingie…alisema kutafuta mwingine sio hoja,
lakini anajau kabisa nitakuwa simpendi tena…basi akawa anamuomba mungu huku
akivuta subira kuwa ipo siku mungu atajali,atapona, au ipo siku ataweza
kuniambia ukweli…
Mtu aliyemtaja kama
dakitari, alikuwa ndiye msaada wake mkubwa, na mshauri wake mkubwa, alisema
kama asingeikuwa yeye, huenda angelikuwa
keshakata tamaa ya maisha kabisa…alimtaja kama mtu ambaye ana deni kubwa kwake
kwa fadhila….docta..docta…akawa anamtaja sana…
Siku baada ya siku
ndio ikagundulikana kuwa kumbe kile
kidonda kimekuwa kikubwa kimekula na mirija ya uzazu..kimekuwa kidonda , na
hakitaki kupona,…na ndipo akaanza utaratibu wa tiba na aliyekuwa akimsaidia ni
huyo docta.
‘Docta..docta..docta….’
alimtaja sana kwenye shajara hiyo mpaka nikaanza kujisikia vibaya, wivu….alionekana
kama yeye ni mtu muhimu sana, hata kuliko mimi, ..mimi nikawa simjali
anayemjali ni huyo docta…
‘Nampenda sana mume
wangu, lakini yaonekana anapenda mali zaidi kuliko mimi, na inafikia muda
najaribu kuongea naye hanielewi, tofauti na ilivyo kwa docta, ..alinijali sana…’kauli
hii iliniuliza sana, na zile hasira dhidi ya docta zikaanza kunijia tena
akilini.
Mke wangu hakutaka
kabisa niambiwe, akijua kuwa nikiambiwa nitaumia sana, na kwa mawazo yake
ningemuacha kwa hasira, kwasababu ananifahamu nilivyo, na kama ningemuacha, asingeliweza
kuishi bila mimi..na akawa anaumia sana pale nilipoanza harakati za kutafuta
mtoto. ….
Kumbe …aligundua kuwa ninatembea na wanawake
wengine ili nipate mtoto , lakini hakutaka kuniambia, aliombea tu, nijaliwe nipate
huyo mtoto, lakini haikutokea…na kwa jinsi alivyohangaika, alijua ni yeye peke
yake anayeweza kulifanikisha hilo..lakini kwa vipi….
Sikutaka hata kumalizia
hiyo sehemu, nikairudisha ile sajara kwenye kabati, haraka nikiwa nimeshaanza
kupaniki, nikatoke nje, moja kwa moja nikaeleeka nyumbani kwa docta, ..docta
alikuwa jirani yangu….
NB: Naishia hapa
kwa leo, nina imani sehemi ijayo itakuwa ni hitimisho…
WAZO LA LEO: Kuvumiliana ni kitu muhimu sana kwenye mahusiano, kwani
akili za kutafakari mambo hutofautiana mtu na mtu, haiwezekani kile
unachofikiria wewe au kukitaka wewe kikawa sawa na mwenzako. Pia tukumbuke
kuwa, uwezo wa kujieleza, hutofautiana mtu na mtu, kwasababu mbali mbali, mmoja
anaweza kushindwa kuelezea jambo, labda kutokana na malezi ya huko alipotoka,
au labda kutokana na sababu mbalimali...
Sasa basi mnapokutana wawili, mnatakiwa hili
mliangalie kwa makini,kwa mfano tatizo
likitokea, mjaribu kukaa, kuulizana na kila mmoja apate nafasi ya kuelezea
aonavyo, na kama kuna ugumu wa kujieleza, au hata kutekeleza, basi kuwa na
namna ya kuvumilia, kuchunguzana tatizo lipo wapi…huenda kuna sababu ..na sio
vyema kukimbilia kwenye jaziba, mkaanza kugombana na wengine hata kuingia
kwenye uadui, na wengine hukimbilia kuachana huku moyoni wanapendana, au
wengine wanateseka ndani kwa ndani, lakini wanashindwa kusema,kama ilivyotokea
kwenye kisa chetu…
Ni mimi:
emu-three
3 comments :
Safi sana mkuu
Lini tena, like a movie
Mtu wangu, hongera sana
Post a Comment