RIDHIKI HAIGOMBWI-utangulizi
Baada ya kusikia tetezi kuwa kuna jamaa mmoja alikuwa freemasoni, na akakiukamiiko, na hatimaye kufirisika,mimi nikaingiwa na hamasa ya kumjua na kujua ni nini nyuma ya pazia
Ndio chanzo cha kisa chetu
Siku hiyo ndio nikaamua kumuendea huyo mtu, ajulikanaye kama Mzee
tajiri, lakini kwa siri walikuwa wakimuita mzee wa freemasoni , kwanini walimuita hivyo, kwanini ilikuwa hivyo, ndio chanzo cha kisa chetu,..
Na tulivyofika kwake ndio akaanza kunisimulia kisa cha
maisha yake, akianza hapa kama utangulizi tu, alianza kwa kusema,
'Wengi walihisi mimi ni freemason, lakini hapana...’akaanza
kusema.
'Kwanini walikuhisi
hivyo?' Nikamuuliza kwani hata lengo la kuja kuonana naye ilikuwa hivyo,kuwa
tumesikia kuwa yeye alikuwa ndani ya taasisi hiyo, na mimi nikavutika kutaka
kujua zaidi ndio nikafika hapo nikielekezwa na rafiki yangu
'Walifikia kusema eti utajiri
wangu niliokuwa nao ulitokana na taasisi hiyo na imani zao, eti baadaye
nikakiuka masharti ndio maana nimefirisika,...' akasema na mwenzangu aliyekuwa
karibu akanifinya kuniashiria kuwa huyo mzee anadanganya
'Ni kweli nilikuwa tajiri sana,..nikafikia kumiliki kampuni
kubwa tu,.., na sio kampuni moja.kampuni hiyo kubwa ilikuja kuzaa kampuni
nyingine zikiwa zipo chini ya kamuni hiyo tanzu....'akasema.
Nilimuangalia huyo mzee jinsi alivyo, akiwa kavalia shati
kuukuu, iliyogimbaa kwa jasho, tai shingoni,..kuashiria alikuwa akijpenda, au
...ndio hivyo, kama walivyosema watu alikuwa mtu mkubwa, mashuhuri,..lakini
nilipotupa macho miguuni, nikakuta kavalia kandambili, zilizokwisha na zikiwa
na rangi tofauti...
'Sasa sina utajiri tena., sina cha kampuni wala dalili ya hizo
kampuni, ukifuatilia utagundua ni kampuni yenye madeni yasiyolipika,ikiwa na
maana nilifirisika.., sasa sina mbele wala nyuma, nimekuwa masikini wa kutupwa,
hata pesa ya kula naipata kwa kuomba omba...'akasema kwa uchungu
‘Ilinichukua muda
kuamini hivyo, kuwa sasa sina kitu,...huwezi amini, mimi aliyekuwa tajiri,
nijifunika ili nisionekane, nakwenda barabarani kuomba...kweli hujafa
hujaumbuka..’akasema kwa uchungu
Unaweza ukafikiria kuwa huyu mtu ni muongo, ukimuona kwa hali aliyokuwa nayo,unaweza
ukafikiria anajitukuza tu, kuwa alikuwa tajiri , akawa anamiliki kampuni,
alikuwa mkurugenzi, ..lakini mimi mwenyewe niliona kwenye gazeti, likionyesha
enzi zake, akiwa mkurugenzi, akiwa anaongea na mawaziri, akifungua vituo mbali
mbali vya watoto mayatima...leo hii ukimuona unaweza kusema ni kizee cha wapi.
'Mimi nilikuwa mkurugenzi, naheshimika, najuana na mawaziri...na
hata mkuu wa nachi' Akasema sasa akinitupia jicho na kuangalia chini kama
anaona aibu.
'Lakini, leo, unavoniona ndio hivi,...natamani hata
kujiua...lakini kwanini nijiue, nilijiuliza mara mbili tatu, nijiue, wakati
siku yangu itafika, nitakufa tu...'akasema kwa sauti ya unyonge.
'Mimi nilikuwa na mke wangu mrembo kweli..nikisema mrembo ni
mrembo kweli, kila nikipita naye mitaani, watu hugeuza shingo kumtizama, na
alivyokuwa na maringo, basi ikawa hata waandishi wa habari wanamfuata kila
anapokwenda ili kupata picha zake....' akasema
'Lakini leo hii unavyoniona hapa nilipo sina cha mke wala
mtoto...’akasema
‘Wamekwenda wapi...?’ nikamuuliza na hapo akainua uso kunitizama
na machozi yakaonekana yakimlenga lenga.
‘Usinikumbushe mbali...mke hayupo na wala sijui katoweka wapi,
.....na aliondoka na mtoto wangu, ...’akasema
‘Kwanini aliondoka...?’ nikamuuliza
‘Hivi hali niliyo nayo unaweza kuishi na mke mrembo kama
huyo...mtu aliyekuwa kazoea kula chakuala kutoka ulaya , maji kutoka ulaya, na
kila upande kazungukwa na wafanyakazi wa ndani, akikohoa anaulizwa ‘madame
unataka nini...’akasema kwa mikogo.
‘Mke wangu nilimpenda sana, ...kila alichotaka nilimpa, na
alikuwa mshauri wangu mnzuri sana, alijua jinsi gani ya kunifanyia...lakini
ooh, jinamizi likavamia maisha yetu, balaa ikatuvamia,..kisirani
kikatuvamia...furaha, amani..upendo vikapotea...’akasema
'Lakini mzee kwanini ikatokea hivyo...?' nikamuuliza nikipoona
anazidi kulalamika tu, kwani nilivyosikia kwa watu ni kuwa jamaa huyo utajiri
wake ulikuwa unahusishwa na taasisi hiyo inayojulikana sana duniani....ya
freemason.
'Lakini mzee mimi nimesikia kuwa wewe ni mwanachama wa taasisi
ya frimasoni, ila ulikiuka masharti...'
'Wengi wanasema hivyo, lakini kiukweli hawafahamu kitu....'
akasema.
Na jamaa yangu akanifinya na kuninong'onezea sikioni, akisema;
'Alikuwa frimason huyo, asikudanganye, kakiuka mashart, ndio
maana kafirisika,...'
'Mke wangu alinikimbia, nilimpenda sana, alinikimbia na mtoto wangu
kipenzi changu, ua la moyo wangu nikabakia mkiwa, hata sijui wameenda wapi,
angalau ningejua wamekufa, angalau ningejua wamekimbilia wapi, lakini hata
fununu hakuna,....’akasema kwa uchungu
'Siku wameondoka nilitaka kujiua....nililia usiku kucha, na
niliendelea hivyo hadi mwaka ukapita...nikawa sina machozi tena, ikabakia kulia
moyoni...' akasema kwa uchungu
‘Najiuliza kwanini...umasikini sio kilema,...eti ukiwa masikini
hutakiwi kuwa na mke, wangapi ni
masikini lakini wanaishi mtu na mke wake, ...ina maana mimi kuwa masikini ndio
wanikimbie...’akasema kwa uchungu.
'Samahani mzee unaweza kunisimulia ilivyokuwa, kwanini ulipanda
kuwa tajiri na baadaye ukashuka kuwa masikini kwa kiasi hicho kikubwa...'
nikamuuliza.
‘Mengi nilikuwa siyajui,...kwani nilikuwa nimetekwa na anasa,
nimetekwa na ile hali ya utajiri,..nikajua mimi ndio mimi, utajiri huo ni kwa
ujanja wangu,...lakini baadaye nilikuja kutambua kuwa utajiri huo ulikuwa sio kwa
ujanja wangu...’akasema
‘Ina maana utajiri huo ulitokana na nini...?’ nikamuuliza, na
mwenzagu akanifinya na kusema unasikia
‘Huwezi amini, hata mimi sikuwa naamini hivyo, maana nimesoma,
unajua mimi maisha yangu mengi yalikuwa ulaya, nilikulia huko nikasomea huko,
nilikuja huku nikiwa mkubwa tu, ndio nikawekeza...’akasema
‘Ila nilipokuja nilianzia chini sana.nilikuwa mtu wa kawaida tu,
biashara ndogo ndogo, nikawekeza..huwezi amini hilo, nilianza na wafanyakazi
wachache ambao nilikuwa nawalipa mshahara midogo sana, kutokana na kipato, na
tulipanda tukiwa nao...’akasema
‘Walirizika na kipato chao.., na nilikuwa nao, kuanzia naanza
biashara hadi nakuwa tajiri, na sikuwa nawalipa mishahara mikubwa sana
kiukweli, walikuwa hawana makuu, hata nilipofikia kuwaajiri wazungu,
wafanyakazi waliosoma,, mishahara yao haikuwa mikubwa sana...’akasema
‘Ni kweli ilibidi niwaajiri mameneja utawala,...mameneja fedha,
masoko, na nikawa nawalipa mapesa mengi tu, lakini hawa nilioanza nao,...aah,
sikuwakumbuka tena...unajua..’akasema
‘Sijakuelewa, kwanini ikawa hivyo, wakati mulianza pamoja, na
ungeliweza kuwaendeleza,...?’ nikamuuliza
‘Ukitaka uyafahamu hayo, inabidi nianza kukusimulia maisha yangu
toka mbali....ili uje kuoana kuwa kumbe utajiri wangu haukuwa ni ujanja
wangu,...utajiri huo niliupata kwa kupitia kwa watu ambao hata sikuwathamini, ,
...mungu alinipatia utajiri huo kwa vile nilikuwa na hao watu, ...’akasema
‘Mhh, hata sikuelewi,labda unisimulia ilivyokuwa ...kama
hutojali....’akasema na mwenzangu akanifinya akiniambia tuondoke
‘Unajiingiza hivyo..’akasema huyo rafiki yangu
‘Hutaweza kuamini hayo mpaka na wewe ya kukute, kwani hata mimi
sikuamini hayo hata sasa inaniwia vigumu kuamini...,kuwa kumbe kweli,..usije
ukajiona wewe ni tajiri, ukajisifu, ukawazarau wale uliokuwa nao,...huwezi
kujua kuwa kumbe utajiri huo ni kutokana na wao
‘Unajua nilikuja kuyafahamu hayo, wakati nimeshafirisika, wakati
sina kitu, wakati mke keshanikimbia wakati nilipoiona barua ya mke wangu
ikielezea kilakitu, niliumia sana,....' akatulia.
Ndio maana nimeamini kuwa riziki mtoaji ni mungu, mambo mengine,
ni sababu tu, na riziki unaweza kuipata kwa kupitia mtu mwingine usiyemthamini
kabisa, usiyemtegemea kabisa, unayemdharau tu, na kumuona si chochote kwako,
kwanza hana hadhi kuishi na wewe,....
‘Kiukweli nimegundua kitu, hata siku moja riziki haigombaniwi.,
kuwa wewe ni mjanja sana, utaipata riziki kwa ujanja wako,kuwa wewe utashindana
na wengine upate zaidi,...utawadhulumu watu jasho lao,kiujanja ujanja ili upate
zaidi,... ‘akatulia
‘Ndio ni kweli, kwa muda huo utapata uteneemeka , utajijenga,
utakuwa kama nilivyokuwa mimi,majumba ya kifahari, magari...,lakini itafika
muda riziki hiyo itakukimbia...’akasema
‘Maana wewe si utajiona wewe ni mjanja,...wewe unapata kwa
ujanja wako, kumbe sio, kuna jinsi fulani mungu anakua hiyo riziki, .....huwezi
kujua na huwezi kuelewa, inaweza kuna sababu, kuna mtu, mungu aliyemuweka hapo
ili iwe sababu ya riziki yako huwezi kumjua, anaweza akawa mtu hohehahe tu, mtu
usiyemjali tu, na hata huyo mtu hajijua kuwa ndiye sababu ya riziki yako, huwezi
amini hilo, hata mimi sikuamini hilo..,' akasema.
‘Huwezi amini hilo, kamanilivyokuwa siamini mimi,maana nimesoma,
mimi ni mjanja, ...utaniambia nini,ila kiukweli, nikuambie kitu...hata siku
moja 'Riziki haigombwi.....' akasema.
‘Riziki haigombwi, kwa vipi....?’ nikamuuliza
‘Nitakusimulia kisa cha maisha yangu, lakini kwanza nina
njaa....’akasema
NB: Huo ni utangulizi wa kisa kipya, ambacho nitakuwa nikItoa
ndogo ndogo kwenye facebook, lakini kwa marefu na mapana utakipata kwenye blog,
ndani ya diary yangu....na hili ni kutokana na maombi ya wapendwa wengi, kuwa
pia sasa niwe natoa visa moja kwa moja kupitia hapa FACEBOOK, mnasemaje?
Najua wapendwa mpo tayari na mimi, ili nijua hayo, naomba mlike
diary yangu,.....
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment