Kwanza ni kumshukuru mungu kuipata siku hii muhimu ya kuungana na mahujaji wenzetu waliojaliwa kutimiza nguzo hii muhimu katika dini. Sisi ambao hatujabahatika tumuombe mungu atujalie tuje kuitimiza , kwani kwake yeye yote yanawezekana.
Siku ya leo wengi wana maandalizi , makulaji mavazi na tamasa za hapa na pale, na nifuraha kwa kwenda mbele, lakini tunasahau kuwa kuna wenzetu kwasababu hizi na zile hawawezi kufanya hivyo, hawawezi kula vizuri, hawawezi kusherehekea, ....je wewe uliyejaliwa unawaonaje
Wapo wagonjwa, wamelezwa, au majumbani, na wao walitarajia kuwepo, lakini kutokana na mitihani hiyo ya maradhi wameshindwa, wanahitajii faraja yako, ukila na kusaza wakumbuke , wapitia, wape zawadi wape faraja, utapata jaza zaidi ya hiyo ya kula na kusaza.
Wapo wasiojiweza, kwa ulemavu, wapo wasiojiweza kwa mitihani ya umasikini, wapo mayatima, wazee, jamani jamani, hawa ni vipenzi wa mungu, ukiwakumbuka na wewe utakuwa miongoni waliomjali mwenyezimungu, na imani yako itakuwa kubwa, utakuwa miongoni mwa waumini..
Blog yako ya diary yangu inawatakia IDD EL HAJ NJEMA
Ni mimi: emu-three
No comments :
Post a Comment