Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Saturday, August 1, 2015

RADHI YA WAZAZI-26



Ni siku maalumu kwa Profesa,.....

Ni siku maalumu kwa wenzake, pia,

Profesa alijua sasa ni muda wa kuitwa tajiri, ni muda amao ataipata pesa ambayo hajawahi kuishika kabla...moyo ukawa unamdunda kwa uroho...

‘Sasa hawa watu watanitambua kuwa mimi ni nani....’akawa anaongea, akakuna kichwa

‘Huyu mtaalamu, anajifaya mjanja, ...hahaha hajui kuwa mimi nimeshika mpini, yeye kashika makali, ataniliona vumbi langu....’akasema akitabasamu

‘Najua .....ujanja wake, ....nimeshajua mbinu zake, hajui kuwa mimi ni mjanja....’akaangalia saa yake...

Akiwa yupo sehemu yake maalumu,...alikuwa akivuta sigara, taratibu, huwa akivuta sigara ujue ana tatizo gumu, na tatizo hilo liahitajia kufikiria sana.....

Aliangalia saa yake, akajua sasa ni muda muafaka, akatembea taratibu, hakuwa na haraka, kwani kazi hiyo inahitajia umakini sana, kwanza akatafuta usafri hadi mtaa mwingine, kwenye watu wengi,  akahakikisha hakuna mtu anayemfuatilia

Moja ya kibanda cha simu kilikuwa kinatumika, alisubiri aliyekuwa kipiga simu kutoka,...alipotoka tu, akaingia kwenye hicho kibanda cha simu, akaitafuta namba, akaipiga, na kusubiria,...mara mtu akapokea, akakaa kimia

‘Halloh,....’sauti ikasema, hakusema kitu, akakata simu

Aliondoka pale akaelekea kibanda kingine akapiga simu, na mara mtu akasema 

‘Halloh,....nani mwenzangu...’

‘Subiri kuna mtu anataka kuongea na wewe....’akasema akiigiza sauti ya kike,

Aliondoka hapo na kutafuta usafiri hadi mtaa mwingine, baada ya kuhakikisha hapo hakuna mtu karibu, akavaa kitambaa usoni kinachofunika mdomo, akachukua simu na kupiga namba....

Haikupita muda akasikia sauti, kama kawaida alisikia sauti ya jamaa akihema, halafu kwa sauti ya kukoroma, ikionyesha kuchoka akasema;

‘Halloh...mbona ...wewe ni nani .’akaanza uongea

‘Ongea na ....’akaigiza sauti ya kike

Natumai upo tayari.....’akasema profesa kwa sauti nzito sasa

‘Nani wewe ....mbona namba tofauti tofauti.....’sauti ikasema

‘Wewe wajifanya mjanja sio,....nilikuambia nini....’akatoa sauti nzito ya vitisho

‘Kwani nimefanya nini..’sauti ikasema

‘Najua hapo ulipo unarekodi sauti yangu, hiyo haisaidii kitu, yote haya niliyafanya kukusaidia, sasa umekiuka masharti, kesho mkeo atapata picha mojawapo kuonyesha uchafu wako, na baadaye nitatuma kwa mkweo...’akasema

‘Kwani mimi nimefanya nini, umetaka pesa, pesa nimeshazitafuta, unataka nini zaidi....?’ akauliza

‘Pesa yote ipo kamili....?’ akaulizwa

‘Ipo kamili, .....’akaambiwa

‘Wewe si umetafuta mpelelezi, na unatarajia kuninasa wakati unazipeleka hizo pesa, ....’akaambiwa

‘Mpelelezi, nani kakuambia nimetafuta mpelelezi...?’ akauliza

‘Nilishakuambia wahusika wameshajiandaa kwa yote hayo, kila unachokifanya wanapata taarifa....na hilo ulilolifanya la kutafuta mpelelezi,....na watu wakufuatilia simu zinazopigwa, kuwa unaweza kuninasa...wanaona wewe huna ushirikiano,mimi ni mjumbe tu, na hao watu mimi sikutani nao,unajua kwanini wanafanya hivyo....’akasema

‘Ni nani kakuambia nimetafuta mpelelezi....?’ akauliza

‘Hakuna haja ya kuongea sana,........ najua hapo unatafuta mbinu za kutafuta wapi nilipo,...ila nakuambia mkeo akiona huo uchafu wako, ndio utagundua kosa ulilolifanya, utajutia maisha yako yote....’akasema

No,no...usifanye hivyo tafadhali, nambie nipeleke wapi hizo pesa, na nikampe nani utakayemuamini,au uje uchukue mwenyewe, tukutane wapi ....nitabadili kila kitu, na ...sijatatafuta mpelelezi, sio kweli nipo peke yangu....’akawa anaongea kuonyesha wasiwasi mkubwa.

‘Sasa ni hivi...hizo pesa utazipeleka sehemu ile ile ya awali, ...na utazipeleka wewe mwenyewe ukifika hapo usubiri maagizo yangu...’akaambiwa

‘Na mzigo wangu nitaupateje....?’ akauliza

‘Mzigo gani...?’ akaulizwa

‘Picha ya hiyo video...tulikubaliana nini.....nataka picha zote na kama mnanidanganya nawaambia, ninajua kama ni feki au ni sahihi, kama mkitoa kopi nitafahamu ....’akasema na kutulia

‘Huo mzigo wako utaupata,....lakini ni mpaka hapo wenyewe watakapohakikisha pesa imekamilika,huwezi kwenda dukani kununua kitu ukalipa pesa nusu ukakabidhiwa kifaa, ....umenielewa, pesa kwanza....ikiwa imekamilika.’akaambiwa

‘Ina maana bado hamjaniamini, nimeshawalipa pesa ya kwanza, ....sasa hii ya pili, bado hamjanionyesha dalili ya kunipa huo mzigo, nitawaamini vipi, kama sio mnanidanganya....’akasema

‘Hii yote ni kwasababu huaminiki tena,na ....kwa taarifa yako kila hatua unayokwenda, kila mtu unayekutana naye unaonekana....kosa dogo mke wako ataona kila kitu, na mkweo nasikia anafika huku mjini hivi karibuni....’akambiwa

‘Ni nani kawafahamisha hilo, mbona hakuna anayefahamu  ....?’ akauliza kwa hasira

‘Ndio ujue kuwa kila kitu mnachokifanya kinajulikana.....sasa nataka kesho peleka huko mzigo, ukifika hapo usubiri, utaambiwa kinachofuata...’akakata simu, alijua kuna mtu anafuatilia hiyo simu.

Profesa akamaliza, na kutoa ile kofia ya kuziba mdomo, aliyokuwa kavaa, na kwa haraka akatoka pale kibandani na kutembea kuelekea sehemu nyingine akasubiri, haikupita muda, akaona gari likifika eneo hilo, na mtu mmoja akatoka na kuonekana akiangalia huku na kule...

Profesa akaondoka hapo kwa haraka na kwenda sehemu nyingine ilikuwa ni sehemu ya vibanda vya mitandao, akalipia pesa yake akaingia kwenye mtandao, kwa haraka akatuma alichotaka kutuma kwenye mtandao,...., halafu akaondoka hadi kibanda kingine cha simu.

‘Umeona hiyo picha niliyokutumia....’akasema

‘Picha gani....?’ sauti ikauliza kwa hasira, na wasiwasi

‘Hii ni kukuonya tu, fungua simu yako uone, maana huamini kuwa tuna uchafu wako mbaya zaidi, na picha hiyo ipo tayari kutumwa kwa mkeo...’akaambiwa,

Profesa hakusubiri, akatoka hapo na kuchukua usafiri hadi mitaaa mingine ya mji, na kutafuta kibanda cha simu, akapiga hiyo namba tena.

‘Umeiona hiyo picha...?’ akauliza

‘Kwanini unanifanyia hivyo...’sauti ikauliza ikionyesha kunyong’onyea

‘Kwasababu umejifanya mjanja, umeajiri watu wa mitandao kutafuta simu ninazo piga,....sasa nikiona dalili ya mtu akinifuatilia, naituma hiyo picha mkeo...ipo tayari kwenye mtandao....’akaambiwa

‘Tafadhali, usije kufanya hivyo, na tulikubaliana usiweke picha kwenye mtandao kwanini umefanya hivyo.....?’ akauliza

‘Na tulikubaliana kuwa hilo ni mimi na wewe na hao watu waliokuwa na hiyo video, wewe sasa umefaya nini....?’ akauliza

‘Sikiliza  mimi nimeshaachana na hao watu, nimewaambia siwahitaji tena, kama wanafanya lolote wanafanya kivyao, sio mimi siwatai tena...’akasema

‘Mimi hilo silijui,maana wewe ndiye ulikiuka masharti,. Kwahiyo kitakachotokea baadaye usije kunilaumu...’akasema na mara akasikia sauti kwenye simu ya kike, akajua huyo ni mke wake

‘Mume wangu , upo wapi....Kuna mtu kanitumia ujumbe wa picha lakini haifunguki..’sauti ikasema na huyo mumewe akasema

‘Ufute huo ujumbe haraka usije kuufungua, inawezekana ni virus, hujasikia wakisema ukipokea ujumbe kama wa picha uufute kabisa.....’akasema hakujua simu bado ipo hewani

‘Haufutiki..’sauti ya kike ikasema

‘Oooh, Hebu ilete hiyo simu,.....’kukawa na ukimia fulani, profesa hakupoteza muda, akatoka hapo na kupanda usafiri hadi mtaa mwingine wa mji, na kusubiria muda maalumu.

******

Wakati profesa akihangaika, mtaalamu alikuwa kwenye mitambo yake akifuatilia kinachoendelea, akiwa keshajiandaa kwa hatua nyingine na muelekeo mwingine, alikuwa keshaamua,  alihamia kwenye chumba kingine na kumwambia katibu muhutasi wake, hataki mgeni, hataki usumbufu,....

Akainua simu yake na kumpigia jamaa yake....

‘Umemuona,....eeh,?’ akauliza

‘Ndio nimemuona, yupo mitaa ya kati, ....kavaa kofia pana,...yupo kwenye chumba cha mgahawa anakunywa maji...na kuvuta sigara,....’akasema

‘Ok,nimeshakuona...sasa sogea hadi ....ok, hapo hapo, upo karibu naye sasa sio.....?’ akauliza

‘Ndio yeye kavaa kofia ana mawani meusi,...., na ndevu  yes, ndio yeye,ok ok, sawa tatizo kazima simu yake, angewesha ningemuona, lakini sio hoja, wewe hakikisha unakuwa karibu yake muda wote....’akasema

‘Kwahiyo mimi nifanye nini....?’ akauliza

‘Wewe subiri nitakupa maelekezo....hakikisha unafanya ninavyokuambia, usimsogelee sana, akagundua unamfuatilia, wewe mfuatilie tu kila anapokwenda, kwa umbali huo....’akasema  mtaalamu
Halafu akakata simu na kupiga sehemu nyingine...huku akisema;

‘Lazima hapa nitumie pesa kidogo .....bila hivi,....nikitegemea huu mtandao sitakuwa na uhakika zaidi, hawa ndio watakuwa ishara yangu.....’akasema akisubiria mtu apokee simu

He is too slow,kupokea simu.....’akasema,na mara mtu akawa hewani na yeye akatoa maagizo

‘Hakikisha huyo jamaa akitoka unamfuatilia nyuma,...na hakikisha hapotei usoni mwako,wewe kazi yako ni  kumfuatilia tu,na kila hatua nitakupigia simu.....usije kufanya zaidi ya hapo, ....malipo yako ni kwa kazi hiyo tu.....’akasema na kukata simu.

‘Huyu ni rahisi kumfuatilia maana simu yake ipo hewani, nimeshamnasa,...mmh, hata huyu wa kumfuatilia sio muhimu sana....lakini naona kuna watu zaidi ya mmoja,....mmh, hapakuna tatizo, huyu mtu ana watu karibu....’akasema

‘Inabidi niongee na profesa awe makini, lakini profesa kazima simu,....ngoja nione la kufanya..alisubiria hadi profesa alipokuwa kwenye kibanda cha simu, kwa kutumia huyo mtu anayemfuatilia, akapiga simu kwenye hicho kibanda akitarajia profesa atapokea lakini haikufanyika hivyo

‘Hamna shida ...nitaona la kufanya....ni lazima nipata mawasiliano ya hawa watu waliomzunguka huyu jamaa....ni lazima....ngoja ninase mawasiliano yao.....’akasema akifanya vitu vyake

‘Ok, ....poa,na hapasawa kabisa simu itakayoingia au kutoka nitakuwa nayo hewani, ...test...akasema na mara akasikia sauti ya mtu akipiga ...

‘Hahaha....this is a crazy profesa...anajua kuigisa, hahaha....wanacheza na mtaalamu...’akasema na akiwa kaweka vyombo vya kusikilizia masikioni.

‘Everything now is fine....ni swala la muda...kama profesa atafanya nilivyomuelekeza,pesa yote itakuwa mikononi mwangu, na hapo ataoana vumbi langu..hahaha....

Akaangalia kwenye mtandao wake, akawa anafuatilia kitu...upande mwingine....

‘Na huyu mpelelezi, anajifanya mjanja,ngoja nione yupo wapi....’akasema akitafuta jambo....mmmh, .....yupo wapi huyu mtu.....ok,ngoja nitamtafuta baadaye,hana shida kwangu huyu mtu....’akasema huku akikagua kitu kingine

‘Huyu mtu vipi mbona hatulii sehemu moja....’akawa anasema huku akiangalia saa yake,  akataka kupiga simu kumuulizia mtu wake, lakini akaona asubirie. Halafu akapiga

‘Mbona hukai sehemu moja....?’ akauliza

‘Ni mtu wako, kapanda gari hadi mtaa mwingine ndio namfuatilia....’akasema

‘Ok poa hakikisha humpotezi, nakuona wewe....akiwasha simu tu nitakuwa naye, lakini....ok, ok,endelea kumfuatilia....’akasema na kukata simu

‘Mhh, kumbe mjanja ngoja tuone.....’akasema akiendelea ku angalia kwenye komputa yake,moyoni akiwa na mipango mingi, akijua leo ni siku ya kupata pesa nyingi , pesa ambazo zitamfanya anunue mtambo mwingine mpya wa kisasa utakaomfanya aone mbali zaidi, aone shughuli zote hapo mjini na nje ya eneo lake na hapo ataweza kupanga dili nyingi za kumuingizia pesa

Alishaona pesa hiyo itamfaa kwa mambo mengi, na kwahiyo kinachohitajika ni kuhakikisha inafika mkononi mwake, na yeye ndiye awe na mamlaka nayo, na ikibidi aichukue yote peke yake...

Akajilamba mdomoni,kwa uchu, akawa anaangalia kwenye komputa yake, na wakati anataka kufanya kitu kwenye komputa yake  mara mlango ukagongwa...

Who the hell....’akasema kwa sauti kubwa,na mara mlango ukafunguka...na alipogeuka kuangalia, akajikuta anaangalia mtutu wa bastola..

*******

WAZ LA LEO: Usije ukajiona mjanja kwenye kazi za dhuluma, utafanikiwa leo, lakini jinamizi la kudhulumu litakuandama usiku na mchana, ukumbuke wale uliowadhulumu, wanalalamika, wanaomba, ....familia zao zinateseka, kwa sababu ya dhuluma zako...


Na wengine wanakufuatilia usiku na mchana....na japokuwa wewe utawaona hawana lolote kwako, hawajui kujitetea, sio wasomi.. lakini yupo mwenye uwezo wa kuwasaidia, kuwatetea,...muumba wa mbingu na ardhi, ..kumbuka dhuluma haidumu, ipo siku utaumbuka tu.

Ni mimi: emu-three

No comments :