Wawili hawa
yaani mke na mume wa mhanga wa mlungula walikuwa na kawaida ya kila mwezi kukaa
na kupiga mahesabu ya mwezi, kila mmoja analeta matumizi yake na mahitajio ya
nyumbani kwa ujumla.
Kwahiyo kama kawaida mke akaleta mahitajio yake
ambayo hayakuwa na utofauti na miezi mingine, lakini mume alipoleta mahitajio yake ikawa karibu
mara tatu ya yale ya kawaida, mke ikabidi ashituke, na kuulikza kulikoni, na mume
akatoa mlolongo wa madai yake na yote hayakuwa ya ukweli,ilimradi tu apate fungu lakutosha kulipia pesa anayohitajiwa kuwalipa watu wa mlungula.
Ni kwanini aje kukubali kulipia pesa zote hizo,na je kweli zitapatikana..mke atakubali,....
Tuendelee na
kisa chetu....
*******
‘Pesa yote
ya nini....?’ mkewe akauliza akionyesha uso wa kushangaa ,na mume akiwa anamkwepa mkewe wasiangaliane akasema;
‘Nina
matatizo mengi kwa kweli mke wangu...sikutaka kukuambia, ila niamini tu....'akasema
'Haa,nitakumini vipi,..wakati unajua hapa tunakwenda kwa mahesabu kama kawaida yatu,mimi siwezi kukubali pesa yote hii itumike kwa mambo yasiyo na msingi....'akasema mke
'Yana msingi mke wangu ndio maana nimeyaleta hapa..viginevyo nisingeyaleta niamini mke wangu....'akasema
'Niambie ni kwaajili ya kitu gani...?' akauliza
'Mke wangu tatizo lilianzia kwenye uharibifu kutokana na tatizo la umeme,na mimi nikaonekana ni mzembe,ili nisifukuzwe kazi nikakubali kubeba hiyodhamana, nilipe...'akatunga uwongo
'Haiwezekani...'akasema mkewe
'Ndio hivyo mke wangu, tatizo hilo liliharibu hadi vitu vya watu, kwa umeme,na ikabidi niingiziwe
kwenye deni,na kwa vile vifaa vingi vilikuwa vya wateja, nikatakiwa
kulipia kwa haraka, ...nikaona niwakope wenzangu kwa riba, ....unajua tena
riba, ....nikachelewesa kulimalizia deni, sasa deni limakuwa kubwa, ila kasema
naweza kumlipa kwa awamu mbili, au tatu...’akadanganya
‘Mbona
hukuniambia, na ni kifaa gani chenye gharama yote hii....’akauliza mkewe,
akionyesha mashaka.
‘Ni kifaa
chenye thamani kubwa..usijali mke wangu nitalipa halafu nitaangalia jinsi ya
kufidia haya matumzi baadaye...’akasema
‘Hapana
tatizo sio jinsi ya kuja kulipia hizi gharama, tatizo ni uhakika..na nauliza
kwanini hukuniambia mapema, kama kuna tatizo kama hili..?’ akauliza mke mtu
‘Nilijua
nitalimaliza mwenyewe,...huoni nilishaanza kulipa, nikaona mwenzangu atanidai
pesa ya kawaida, kumbe kawezeka na riba juu,..kiukweli sikutaka kukusmbua mke
wangu, ila sasa hali imekuwa ngumu.....’akataka kujitetea
‘Mume wangu
naona kuna kitu unanificha,...kwanini huniambii ukweli, kwani mimi ni nani
kwako?’ akauliza na mume akawa mtizama mkewe kwa macho ya kujiiba, na kuuliza
‘Kwani mke
wangu kwanini ..ina maana huniamini au...?’ akauliza
‘Nimekuuliza
swali mimi ni nani kwako...?’mke akauliza kwa sauti ya msisitizo
‘Wewe ni mke
wangu....’akasema
‘Je mke na
mume wanahitajika kufichana mambo yao,..?’ akauliza
‘Hawahitajiki
kufichana, lakini kuna wakati mwingine unatumia busara kuangalia jambo
lenyewe,...kwa mfano hilo la kazini inatokea mara kwa mara, na nasawazisha mwenyewe ,sio
lazima mke ajue hayo ya kazini....’akasema
‘Mume
wangu...usinione kuwa mimi ni mtoto mdogo,tumeishi miaka mingi, na huwezi
kunidanganya kwa lolote lile,...unakumbuka kipindi tunakuja huku ulaya
nilikuwambia nini....?’ akauliza
‘Uliniambia
nini...mmh, hebu niambie tusizungushane....’akasemahuku akiangalia saa
‘Ok,...hebu
niambie hii barua inatoka benki,ni ya kwako,au sio...?’ akauliza mkewe akiwa
kashikilia hiyo barua mkononi...na mume wake alipoiona akashituka kidogo,lakini
akajisawazisha, na kusema
‘Mhh,nani
kaileta hii barua huku nyumbani...?’ akauliza kwa hamaki huku akichukua kwa
haraka kutoka mkononi kwa mke wake.
‘Mtu wenu
kazini alipitia hapa,akanikuta, akasema ukija nikupe,....’akasema huku
akimtathimini mumewe, kwa kumuangalia usoni,na mumewe akijua mkewe haijaifungua
akaweka mfukoni
‘Kwanini huisomi
hiyo barua, ...na benki nijuavyo, wasingeliandika jina lako moja kwa moja kama
sio akaunti yako, ina maana una akaunti yako binfasi,...? Mbona hujaniambia
kuhusu hiyo akaunti...?’ akauliza mkewe
‘Nilikuwa
nayo zamani, haina pesa, ndio maana benki wanataka kujua kwanini, kama nitaweza
kuiendeleza....waifunge tu, nilipokuja, nikaona niiendeleze, kwa kupitishia
pesa za kampuni, wakati nikipokea kwa dharura...’akazidi kudanganya
‘Una uhakika
na unachokisema mume wangu...’akauliza mkewe,akimuangalia mumewe kwa mashaka.
‘Kwanini
unasema hivyo mke wangu, yaonyesha kama huniamini, au...?’ akauliza
‘Nakuuliza
una uhakika na unachokisema,...mume wangu kuna tatizo gani, mbona uwongo
unazidi siku hizi, tangia tuje huku ulaya nakuona umebadilika, ni nini tatizo
lako,niambie nikusaidie...’akasema mkewe
‘Hakuna
tatizo kabisa mke wangu,niamini, ni hayo ya kazini, nikiyamaliza, nitakuwa na
amani...tusaidiane kwa hilo...’akasema
‘Sawa,....mimi
nitakusaidia nitakachofanya, nitapitia kazini kwako niongee na bosi wako nione
jinsi gani ya kulimaliza hilo deni, maana ni ajabu mfanyakazi aharibu kitu kwa
bahati mbaya, halafu abebeshwe deni...’mkewe akasema
‘Haina shida
mke wangu,..., wala usifanye hivyo,hayo ni maswala ya kikazi, nitaonekana natoa
siri za kampuni, usifanye hivyonitalimaliza tu, muhimu nipate hizo pesa....’akasema
‘Ok,
nimekuelewa,sasa unataka shilini ngapi kupunguza hilo deni...?’ akaulizwa
mkewe, akimuangalia mumewe kwa macho ya udadisi
‘Basi
angalau nusu ..niweze kupunguza punguza...’akasema
‘Pesa tuliyo
nayo tasilimu hapa ni kwa ajili ya kutuma nyumbani, hii haiguswi, nimeitoa tu kwa vile inahitajika...’akasema
‘Sawa mkewe
wangu...’akaitikia lakini akili haikuwa sawa...
Basi mkewe akakubali hiyo nusu ya kile kiwango
alichoomba, na kiwango hicho ndicho alichotuongezea na pesa aliyokwisha kuitoa
kwenye akaunti yake na kutupa sisi lakini ilikuwa sio nyingi....’akasema
‘Lakini sasa
kilichoharibu, ni kuwa jamaa alikuwa kama kachanganyikiwa, maana na sisi
tulishamkaa kooni, ....akawa hatulii, sisi tuliweka shinikizo zito...’akasema
‘Kama
hatukupata hizo pesa kwa kiwango hicho mkeo atajua kila kitu kilichotokea huko
kwenye bar, kwanza umefanya hata binti wa watu afukuzwe kazi, ...’nikazidi
kutilia msumari
‘Lakini...sija..mlazimisha....hata
sijui ilikuwaje,...nahitaji kuongea na huyo binti nijue ukweli,nahisi kuna kitu
kanifanyia....’akasema
‘Kakufanyia
nini,...picha zinaonyesha kila kitu, ukitumia nguvu,...kuna kanda ya video,haifichi kitu,...na kwanini aje kukufanyia sasa hivi, je hukuwahi kumtongoza kabla,je ulipofika
hapo siku hiyo, wewe hukua umelewa,halafu ukaongeza pombe nyingine,kama ulikuwa huwezi kunywa
zaidi kwanini uliongeza, ina maana ulidhamiria...’sauti ikamwambia kwenye simu
‘Mimi
najijua, najua kiasi cha kunywa, ila binti aliniomba nifike kwenye sherehe yao,
na huko ndio nikanywa,...sizani kama
kinywaji kile ningeliweza kulewa kupita kiasi....nilikunywa chupa
mbili....oh,hata sijui ilikuwaje...’akasema
'Kwahiyo kumbe hukuwa umelewa...?' akaulizwa
'Sikumbuki,ilikuwaje...'akasema
‘Ndio
hivyo..ulichokifanya ni kitendo cha aibu,hiyo picha ni moja ya vitendo vyako,na
ukatumia nguvu...mtu mzima kama wewe unabaka...huna aibu,una mke na
watoto,unatumia nguvu, ina maana mkewe hakutoshelezi,....sasa sikiliza ili aibu
hiyo iishie huko huko..sisi tunajua lakufanya, tayarisha dola laki
mbili..tulimalize kabisa...tutafuta kila kitu kwenye mitambo ya hapo .....’akaambiwa
‘Dola lakini
mbili..!?’ akauliza kwa mshangao
‘Tunahitaji
kuondoa picha zote kwenye mtandao wa hiyo bara, unajua wanamitambo yao inachukua
matukio yote, sasa kufanya hivyo gharama yake ni kubwa sana...,pia tunahitajika kuwafunga mdomo walinzi...na wale
wote walioona hilo tukio...na gharama nyingine ....’akaambiwa
‘Lakini
kulikuwa hakuna watu...’akasema
‘Ile ilikuwa
sherehe,..au sio..?’ akaulizwa
‘Ndio lakini
baadaye nakumbuka tuliondoka na binti ....tukawa peke yetu wawili...’akasema
‘Ehee,umekumbuka
eeh,mliondoka na binti,...mkabakia wawili,..mke akisikia hivyo atalichukuliaje,
kwanini mliondoka...?’ akaulizwa
‘Oh...sijui....lakini
ndio nasema hakuna aliyeona kilichotokea...’akasema
‘Kitu gani
...kiseme hicho ambacho watu hawakuona,au tukutumie picha nyingine...unaona kumbe ulikua na akili
zako timamu unakumbuka ulichofanya, halafu unasema ulikuwa hujitambui, ....’
‘Ni
kweli....sikuelewa nilichokifanya...’akajitetea
‘Hahaha, ulikuwa
umelewa, siku zote si unalewa wewe...sema ukweli wako,...ulifanya makusudi
...ulikuwa unatafuta mwanya kama huo..ulishamtamani binti wa watu...ndio
ukatumia nguvu...au sio...’akaambiwa
Basi akatishiwa mpaka akaingia kwenye mtego,
akawa hana amani, akawa sio muangalifu, na kila baada ya muda fulani akawa
anapata barua yenye picha za matendo yake...
‘Wenyewe wamesema watasubiria masaa matatu tu...,baada ya hapo,usije kuja kulaumu, ikifka kwa wamiliki sio rahisi tena kufuta,...na wao kamaunavyojua, wameshalinakili hilotukio kwenye video, na ndio nikaipata nakala....sasa, kabla barua mojawapo haijafika kwa
mkeo,hatutaki kumtumia kwenye simu maana itakuwa ni hatari kwako...’akaambiwa,
kumbe sisi wenyewe hatukutaka kutumia simu za mikononi, kwani ikifikia kubaya,
simu huku hazina siri.
'Kwani wewe ni nani....?' akauliza
'Usitake kujua mimi ni nani...utaumia zaidi, nikikuambia ni mwandishi wa magazeti ya udaku utasemaje....'akasema
'Sasa nitaaminije kuwa habari hizo hazitakwenda mbali zaidi hadi kumfikia mke wangu..?' akauliza
'Mimi nakuhakikishia ukilipa hizo pesa nakala zote utazipata,vinginevyo kamahuamini sawa,usije kunilaumu....'akasema
Kwahiyo kwa
haraka ndio akaenda kuchukua hizo pesa kwenye akaunti yake, na huko nako benki
wakamgomea,hadi akamlishe hizo nyaraka zinazohitajika, akaomba sana na kubahatika
kupata kisi hicho kidogo,na akajua atamshawishi mkewe, aongezee, angalau
ifikie, dola laki moja,lakini hata hiyo haikuwezekana.
‘Usipolipa
hizo pesa uchafu wakoutamfikia mkeo...’kauli hiyo ikawa inamuandama
Kwahiyo alipochukua
hizo pesa, kwa vile zilikuwa kidogo hakupitiliza moja kwa moja sehemu aliyopangiwa
kuzipeleka, sababu mojawapo ni kuwa kiwango kilikuwa kidogo, lakini pia alitaka
kucheza na muda, ili ikiwezekana apate kujua jinsi gani ya kujiokoa, hakujua
kuwa anapambana na wataalamu.
Alipofika
nyumbani kwa haraka mkewe alikuwa hayupo, si yeye anafanyia kazi karibu na
kazini kwake,kwahiyo angeliweza kufika nyumbani na kuondoka, bila kuchelewa
kazini, na bila hata mkewe kujua, hapo wazo laharaka likamjia...
‘Hii akiba
ni kwa ajili ya kutuma nyumbani kwa ajili ya shughuli za huko, usije kuigusa....’akakumbuka
kauli ya mkewe, lakini kwa upande mwingine akikumbuka kuwa kuna uchafu
utamfikia mkewe,akaona heri fedheha kuliko hiyo kashifa.
Akalisogelea lile kabati la akiba, akafungua
droo ya pesa, na kuongeza kiwango, angalau, ifikie kiwango fulani, alichoona
kinatosha japokuwa bado kilikuwa kidog sana, alichukua akijua kuwa benki
watamruhusu kuchkua pesa nyingine akikamilisha hizo nyaraka na atakuja kuzirejesha hizo pesa kabla mkewe
hajafahamu...
Wakati bado anafikiria zaidi, kwani pesa
ilikuwa bado ndogo, mara akasikia simu ya hapo ndani ikiita, akajiuliza ni nani
anaweza kupiga simu nyumbani kwake,wakati wengi wanajua muda kama huo wote wapo
nyumbani, kwanza akaogopa kupokea,...lakini ilipoita zaidi na zaidi, akajua
huyo mpigaji atakuwa anafahamu kuwa yeye yupo nyumbani, akaamua kuipokea,
lakini kwa mashaka.
‘Wewe mtu,
kuna mtu tumemtuma kazini kwa mkeo akiwa na moja ya uchafu wako, si ndivyo
unavyotaka wewe, unajifanya kichwa maji, je upo tayari uchafu wako ufike kwa
mkeo....’simu ikamwambia
‘Kwanini
mbona tulishakubaliana, kuwa nikachukue hizo pesa...’akaanza kujitetea
‘Tulisema
ukitoka benki tu, uhakikisha hizo pesa unazipeleka wapi..?’ akaulizwa
‘Ndio nataka
kuzipeleka sasa hivi...’akasema huku akihaha...unajua kuhaha,...usiombe ukutane
na mtu kama profesa akiwa kwenye hizo anga zamlungula,... hasa akishakufahamu
ulivyo..
Na sauti hapo
ilikuwa sauti nzito ya jitu kubwa, lakini ukiniona sijai hata kiganjani kama
yule mama alivyosema, mwili wa profesa sio mkubwa,ni mwembamba tu,lakini sauti
iliyotoka hapo ni ya jitu lamiraba minne...
‘Nakupa
sekunde sifuri, ziwe zimeshafika sehemu husika,..na ole wako ufanye makosa,
maana makosa hayo yatasababisha siri zako kufichuka, siwezi kubeba dhamana ya
kufuta uchafu wako, wakati wewe husaidii lolote, nitaonekana mungo kwa
wataalamu wa huo mtandao, ambao wanahangaika kufuta kila kitu,..., wewe
unachelewesha...’akaambiwa
‘Japokuwa kuna
tatizo kidogo, lakini ndio nipo mbioni kuzipeleka hizo pesa...’akasema sasa
akiwa anaangalia kupitia dirishani kama ataona mtu,....angemuona nani.
‘Tatizo...!,
tatizo gani,...unataka kuleta mzaha sio...’sauti ikasema,na hapo akaanza
kujielezea, ilivyokuwa, kuwa ana tatizo na benki,wanahitajia maelezo, na mkewe
aliipata hiyo barua, ...kwahiyo benki wakampa sehemu ndogo tu, mpaka hapo
atakapokamilisha hayo maagizo...’akasema
‘Kwahiyo una
dola kiasi gani hapo ulipo?...Mimi naona nisipoteze muda wangu na uaminifu
wangu, naona niache, maana huo sasa ni utani, ...’nikasema kwa hasira
‘Ni kweli
kabisa kama unataka kuthibitisha nenda benki watakuleza maelezo hayo,sasa hivi
kuna uhakiki wa dhamana zote ....’akasema, ni kweli hiyo taarifa ilishatoka,
nalifahamu hilo, hatujua kuwa huyo jamaa hajalifanikisha hilo.
‘Naona
unapoteza muda, hakikisha unafikisha hizo pesa zote ulizo nazo,mimi nakuona
hapo nyumbani, na kila unalofanya nakuona...’nikasema ni kweli pale nilipo
nilikuwa namuangalia na kiona mbali...tulikuwa tumejiandaa..bro,usinione
hivi...’akasema
‘Na..na..zileta...sasa
hivi...’akasema na kwa haraka akakurupuka na zile pesa, akawa anatoka hapo
nyumbani kuelekea hiyo sehemu,...huku akihaha,..jamaa alichanganyikiwa vibaya
kweli, na wakati anatoka ndio hapo mambo yakaanza kumuendea kombo, kwani
alikutana na mshituka asioutarajia,....
‘Mshituko
gani...?’ akauliza kamamtu alipoona mdogo wake katulia haendelei.
‘Bro....hayo
utayasikia sehemu ijayo,ila kwa kukudokezea,...ni kuwa wakati anafungua mlango,alijikuta akikutana
uso kwa uso na mkewe....
‘Mkewe...???’
akauliza kaka mtu
WAZO LA LEO: Jambo lolote lisilo halali, halina
amani , tuache kujitafutia magonjwa ya shinikizo la moyo kwa kufanya makosa
yasiyo lazima, kwa nia ya kujichumia kipato kisocho halali,
kudanganya,..kufisidi..nk.Muhimu ni kujitahidi katika matendo yetu yote
kusimamia kwenye kweli na haki.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment