‘Unajua bro
nilikweda kwa yule mke mtaliki wako, na cha ajabu akagundua kuwa huyo mtoto ni
wake....’akasema akiwa anaongea na kaka yake ambaye alikuja siku hiyo mjini kununua
bidhaa zake za biashara, na akampitia mdogo wake kumtembelea, sio kawaida yake
mara kwa mara kufanya hivyo, ila kwa vile anafahamu mdogo wake huyo ypo na
mtoto, basi akaona apitie ajue kinachoendelea.
Alishapanga
afanye utaratibu wa kumchukua huyo mtoto akaishi naye, na alishajipanga
kuhakikisha anambadili tabia yake, lakini kulikuwa na tatizo kuwa ataweza
kujikuta matatani, kuwa yeye ndiye alimuiba huyo mtoto, na wakati sheria, na
watu wa usalama walishafika kwake mara nyingi, na kuwaambia hajui wapi alipo
‘Ni kweli
nilikuwa sijui wapi alipo....’akawa anajisemeza mwenye kichwani
‘Ni huyu
kichwa maji, sijui kwanini alifanya hivyo, hata aliponipigia simu kuwa akimpata
huyo mtoto afanyeje, nilijua anafanya mzaha, kumbe...mmh, sasa hili ni tatizo,
lakini sijali,..lazima nimchukue huyu mtoto, vinginevyo ataharibika kabisa....’akasema
Basi akaona siku hiyo apitie kwa mdogo wake huyo na alipofika alimkuta mdogo wake akiwa kwenye harakati zake za
kuuza madawa zake, akiwa na wasaidizi wake..
‘Oooh, bro,
umakuje leo kwangu, ajabu kabisa....karibu, ngoja nimuachie huyu muuzaji wangu
aendelee, karibu ndani....’akasema
Na ndipo
wakaanza kuongea
‘Kwanza
mtoto mwenyewe yupo wapi?’ akauliza
‘Kaenda
shule, hatakiwi kukaa nyumbani, japo yupo likizo, lakini nimeoana awe anasoma
soma, hili litamsaidia na yeye kujichanganya na wenzake na ataweza kukifahamu Kiswahili
vyema zaidi..japokuwa ni kichwa, Kiswahili keshakifahamu hutaamini,...’akasema
Tuendelee na kisa chetu
*************
‘Sasa kwanini
ulimpeleka mtoto huko kwa mama yake, mimi nilikuambia kuwa, sitaki wale watu wafahamu
kuwa huyo mtoto tunaye,....kwani ulichofanya ni makosa,....sasa kwanini ulkampeleka
huko bila idhini yangu?’ akauliza
‘Bro, huyu
mtoto amekuwa mikononi mwangu miaka yote hiyo wewe hujui kuwa ninaye, na
nimekuwa nikifanya lolote bila idhini yako, ....sasa kukuambia hilo ndio
imekuwa kosa,....unanishangaza sana bro...’akasema
‘Vyovyote
iwavyo huyo ni mtoto wangu, sikukutuma wewe kwenda kumuiba, mimi pale ni
mjumbe, najua taratibu zote, naaminika, ..na kama taratibu zingelifuatwa, nilijua kabisa mwisho wa siku nitakabidhiwa huyo
mtoto wangu, wewe kwa kiherehere chako ukaenda ukamchukua bila idhini yao,
hujui hilo ni kosa, hujui kuwa taarifa za kupotea huyo mtoto zilifikishwa
polisi ....’akasema
‘Lakini
ningewezaje kumuacha aliwe na mamba au kwa vile sijakusimulia ilivyokuwa,
unafikiri mimi nina akili mbovu ya kuchukua watoto wa watu bila idhini yao....’akasema
akiangalia saa, hakutaka huyo mtoto aje akutane na huyo baba yake.
‘Mimi
sihitaji kujua, kwani haitanisaidia kitu, ....na sitaki ushahidi hapa, cha muhimu
ni kuwa mtoto yupo, ubaya zaidi umemuharibu, huyo mtoto hastahili kukaa na wewe
tena, anahitaji kuja kijijini ili apigwe msasa....’akasema.
‘Sikiliza
bro, siku ile kule porini, nilimuokota huyo mtoto akitaka kuliwa na wanyama
wakali, na mwanzoni sikujua kabisa kuwa ni mtoto wako....’ akasema
‘Hahaha hivi
unafikiri nitakuamini na hadithi zako za kutunga...’akasema
‘Bro hili
ninalokuambia ni la uhakika, ....unaufahamu ule msitu,ungelijua huo msitu ulivyo,na bahati mbaya ni kuwa humo
kuna mto ambao wanakijiji wanautumia kwa kuchota maji, kwa mbele yake kuna
mamba, kuna mikenge mikubwa, ..kuna michatu na wanyama wakali, hebu fikiria,
...’akasema
‘Sasa huyo
mtoto alifikaje huko, kama sio uwongo wako....?’ akauliza
‘Nimekuambia
huko ndipo wanakijiji wanapochotea maji yao ya matumizi, si ndio serikali yako,
kuna vijiji wana taabu ya maji...’akatulia
‘Najua ndio
kauli zenu wapinzani, kwa vile mimi ni mjumbe wa chama changu utanishambulia
kwa poroj zenu, na siwezi kukuamini kwa hadithi zako hizo...’akasema
‘Bro hii sio
hadithi, ni kweli, mimi nilimuona huyo mtoto huyo akitembea peke yake, ...,
huku analia, isingelikuwa ni mimi mtoto huyo angelikuwa ni kitoweo cha wanyama
wakali....mimi kwa macho yangu nilimuona chatu akiwa eneo lile lile alipokuwa
akitembea huyu mtoto....’akasema
‘Wewe
ulifuata nini huko?’ akauliza huyo kaka yake sasa moyoni akiwa kajawa na jaziba,
sijui kwanini ahisi hivyo kwa muda huo.
‘Nilikwenda
kufuata dawa zangu, nilikuwa nimeshamaliza kuzipata dawa, nikawa sasa nachukua
picha za video kwa kumbukumbu....na wakati namalizia, mara nikasikia sauti kama
ya mtoto analia, nikaelekeza kamera yangu hiyo na huku na huku nafuatilia,....’akasema
akionyesha kwa vitendo
‘Nikafuatilia,
ndio nikamuona huyo mtoto akitembea kuelekea barabarani, kwanza nikamtizama kwa
makini, kuhakikisha kuwa ni binadamu, hebu fikiria msitu kama ule unamuona
mtoto mdogo peke yake, huwezi kuamini kwa haraka, ...nilipohakikisha kuwa ni
binadamu sio kibwengo,, nikamwendea,....’akasema
‘Ina maana
hao watu wanaishi karibu na hicho kisima, au ilikuwaje wamuachie mtoto atembee
peke yake na kwenda huko msituni, ndio maana nilitaka nimchukue mtoto nimlee mwenyewe,
....siku nikikutana nao watanitambua, hilo halivumiliki, watu gani hao wasiojua
kulea, hukumuona mama yake....?’ akaulizwa
‘Kwa muda
ule sikumona mama yake, nilichojua ni kukimbia hadi pale alipokuwa huyo mtoto
kabla hajadakwa na hilo lichatu....yaani hata mimi mwili ulinizizima kwa hofu,
sina uwoga kabisa na midudu hiyo maana ninayo dawa ya kuyalewesha manyama
makali kama kama hayo yasiwe na nguvu, huwa naileweshaga nikitaka kuchukua sumu
zake, kwa dawa zangu, lakini kwa kitendo kilee...haaah, ...’akasema
‘Mhh,.....sitaki
uendelee kunisimulia unanifanya nizidi kukasirika, na kuwachukia hao watu, ...
ninachowaza ilikuwaje huyo mtoto awepo huko msituni peke yake.....?’ akauliza
‘Siku hiyo
nilikuwa nimeweka kambi yangu ...kawaida nikitafuta dawa zangu sitaki mtu
afahamu kuwa nipo hapo msituni mpaka nizipate....uzuri wakati namuona huyo
mtoto nilishamaliza kazi zangu, ilikuwa ni bahati ilinijia, kwani ndio ulikuwa
muda nachukua picha, na hizo picha ni biashara huko ulaya...’akasema
‘Unasema ilikuwa ni bahati kukujia, unaona ni kitu
kizuri hicho...!’ akasema kaka yake kwa mshangao
‘Basi bro,
nilipomchukua huyo mtoto, sijui ni wa nani....nikawa sasa nawaza nimpeleke wapi
huyo mtoto. Nilimpa chakula nilichokuwa nacho akala akalala, alikuwa na njaa,
ungeona alivyokuwa anakula...’akasema.
*********
Nilkiwa sasa
nataka kuondoka, mara wakaja watu;
‘Profesa
kumbe leo upo huku....?’ akauliza mmoja wa askari pori huwa nafahamiana naye,
wakati huo mtoto yupo kwenye hema kalala, hawakumuona na kwa muda ule
ningewaambia, lakini haikutokea hivyo....ningewaaminije..., nikaoea nao kwanza
‘Ndio nipo
nilikuwa namalizia kuchukua dawa zangu na nika....’kabla sijamaliza tukasikia
kelele zikiita, walikuwa aksri wenzake, wakiwaita hao askari pori, wananifahamu
sina shida nao sana, basi wakakimbia kuelekea huko walipoitiwa
‘Mhh, hawa
wanatafuta nini, au ndio wanamtafuta huyu mtoto....?’ nikabakia kujiuliza
Baadaye nikaona haina haja, muda wangu wa
kukaa hapo ulishapita, nikamchukua yule mtoto nikaingia kwenye gari langu
nikaondoka, na ni wakati naondoka ndipo nilikutana na mtu akanihadithia tukio
zima, na uzuri, wakati huo mtoto alikuwa kalala kiti cha nyuma, na hakuweza
kuonekana na mtu
‘Unajua sana
kutunga hadithi wewe, na sikuamini katu, na mambo yako ya uganga hayo, ya
utapeli utapeli ni nani atakuamini ..usije kuwa ulitaka kwenda kumuuza huyu
mtoto kwa mambo yako ya kichawi....’akasema kaka yake.
‘Bro...sikiliza
kwanza, waliponisimulia kuwa mtoto huyu ni wa mama mmoja aliye na mtatizo ya
kifafa, nikamkumbuka shemeji,...na kweli alikuwa ndio yeye, nikaona ooh, sasa
ndio muda muafaka wa kufanya kile ulichokuwa ukikitaka
‘Kile
nilichokuwa nikikitaka...wewe hebu acha uzushi, nilitaka kumuiba mtoto...?’
akauliza kwa mshangao.
‘Nakumbuka
ulisema kuwa unataka kuirejesha damu yetu mahali pake , ulitaka mtoto huyo
achukuliwe arejeshwe kwao, yaani kwenye familia yetu...utajifanya umesahau,
mimi nakumbuka vyema, uliwahi kuniambia hivyo....’akasema na kaka yake akabakia
kimia
‘Niliposikia
hivyo nikamchunguza mtoto nikagundua kuwa kweli anafanana na wewe, basi nikaona
kumbe naweza kufanya jambo,....lakini sikutaka wewe uingie matatani...ndio
maana sikukuambia mapema....’akasema
‘Tatizo lako
unajifanya una akili sana, unafikiri ulichofanya ni ujanja na ujasiri, ..huoni
kuwa ndio ulijiweka kubaya, sasa wakija kugundua kuwa wewe ndiye uliyemuiba
huyo mtoto, wakafungua mashitaka unafikiri itakuwaje....?’ akaulizwa
‘Bro, mbona
unakatiza utamu wa maelezo,.....wakati nipo porini mara nyingi ninakuwa na
kamera yangu ya video, siunanijua zangu,...nimekuwa nikipiga picha nyingi za
wanyama wa hapo msituni, sasa hilo tukio hahaha, kwanza liliniingizia pesa
nyingi ajabu ...’akatulia
‘Wakati huyo
mtoto anapita pale alipolala huyo chatu.....ndipo utamu ulipokuwepo, japokuwa
nilikuwa na wasiwasi mkubwa, ikanasa
hilo tukio bara bara...utaliona lile chatu likijitutumua,..bro, unajua hilo
tukio limeniingizia pesa nyingi, mtoto anapita karibu na chatu, na yule chatu
anajitutumua kutaka kummeza....hebu weka akilini,....’akatulia
‘Na tukio
hilo ndilo lililowezesha huyu mtoto kusoma huko ulaya, niliwaambia nilimuokota
huyo mtoto akitangatanga msituni, hana wazazi, ...wazungu wana huruma ,
walipoona lile tukio kwenye kanda ya video, wakatokea wadhamini kibao
wakuhakikisha huyo mtoto anapata elimu na matunzo....’akasema
‘Kwa
ushahidi gani...?’ akauliza kaka yake
‘Ushahidi si
hiyo kanda ya video..sasa nambie kama mimi sio mjanja...mimi ni profesa bro.’akasema
‘Kwahiyo
mtoto wangu anajulikana huko kama mtoto yatima hana baba wala mama...?’
akauliza akiwa kakunja uso.
‘Huko ulaya
ni mtoto yatima aliyetekelezwa msituni, ......na atakuwa hivyo mpaka anamaliza
shule hadi chuo kikuu,,....si umeona mwenyewe anavyoongea kiingereza kile cha
kwao....halafu, alisoma shule yenyewe inayotambulikana, ..’akatulia kuendelea
hakutaka kusema anasoma shule ya watoto yatima.
‘Nakuambia
wewe utafungwa, hayo maisha yako ya ujanja ujanja,mimi siyaungi
mkono,...kumbuka uliponea chupuchupu kunyongwa huko uchina kwa madawa ya
kulevya,karibu mama afe kwa shinikizo la moyo....sasa hili linaweza kukupeleka
kubaya usipoangalia....’akasema kaka mtu
‘Baada ya
miaka kumi na sita, ni nani ataweza kunifungulia mashitaka na kwa kosa gani, ni
nani anajua sheria kwenye ile familia, wote sio waongeaji,.. ni nani pale, wote
wapole-pole, watu wa kukubali tu, na kusema, namuachia mungu...hahaha, wacheza na profesa wewe...’akasema
‘Mimi
sipendi kabisa hiyo tabia, sipendi kabisa...’akasema kaka mtu
‘Sikiliza
bro, nilichofanya kwa muda ule kilitakiwa kiwe hivyo, na nina ushahidi,..., na
kama unanilaumu kwa hilo, basi ..., hilo niachie mimi mwenyewe, mimi nimesoma
naifahamu sana sheria, na mimi ni mjanja, ...’akasema
‘Huo sio
ujanja, ni dhuluma, ujinga, a utapeli, na ukumbuke kuwafanyia watu hivyo, usione
umeshinda....malipo ni hapa duniani, wangapi wangapi waliishi maisha ya namna
hiyo wakajenga, wakatajirika,....’akasema akizungusha macho kuangalia paa la
nyumba na kuzungusha macho kuangalia vilivyomo humo ndani, kweli mdgo wake,
alikuwa kajijenga, nyumba ya maana, na vitu vilivyomo humo ndani ni vya thamani
tupu.
‘Utajiri wa
namna hiyo,...hii, mmh haina mwisho mwema,mwisho wake unakuwa mbaya....,
ukumbuke malipo kama hayo ni hapa hapa duniani, kamwe dhuluma haidumu...na mengie
huenda yakalipiziwa kwa familia yako mwenyewe....sasa mmmh....,mimi namtaka
mtoto wangu....’akasema
‘Hahaha bro,
badala ya kunishukuru, unaanza kunilaumu, kunionea wivu, huuku unasema eti..sasa namtaka mtoto wangu, ungempataje,
kama angelibakia kule, ungempataje kama angeliwa na wanyama wabaya, angewezaje
kufika ulaya..hivi bro, hulioni hilo....na kwanza mtoto mwenyewe hataki kabisa kusikia habari za wazazi
wake....’akasema
‘Eti nini,
kumbe wewe ndiye ulimfunza huyo kijana, atukatae, sisi wazazi wake.....naona
akikaa na wewe ataharibikiwa kama wewe, ...kwanza yupo wapi huyo mtoto, umesema
kaenda shule, anarudi saa ngapi, nataka niondoke naye...’akasema
‘Analala
huko huko.....’akamdanganya
‘Atalalaje
huko huko, wakati umesema anasoma kwa muda,...na kwanii uhangaike kumpeleka shule
hizo, wakati yupo likizo....anatakiwa kuwajua wazazi wake, anatakiwa kujifunza
maadili mema...?’ akauliza
‘Bro unakumbuka
nilikuambia kuwa nikipata bahati ya kumpata huyo mtoto nifamfanyeje, uakumbuka,
na uliniambia nini?’ akauliza
‘Nilijua
unaongea kwa utani wako.....sikuwa na uhakika kuwa umedahamiria kulifanya
hilo,..ningelijua kuwa unaye huyo mtoto, ningekuambia umrejeshe kwa mama yake
haraka, maana najua utaratibu ulivyo....’akasema
‘Hahaha,
bro, sasa unanigeuka, sema ulivyoniambia siku ile...’akasema
‘Nilikuambia
nini...?’ akauliza kwa hasira
‘Hukusema ikiwezakana
nimuibe na nimfiche wasimuona, ....akae mbali kabisa na hiy familia wasije
kumuambukiza huo ugonjwa wa mama yake
‘Kipidi kile
niliongea tu kwa jaziba tu...’akasema kaka mtu
‘Mimi
nilijua umedhamiria na ndivyo nilivyofanya, nikamchukua huyo mtoto nikakaa
naye, na bahati nilikutana na huyo mzungu aliyekuwa akishughulika na watoto
yatima, nikamwambia nina mtoto yatima mkononi mwanagu, nikamuonyesha hiyo kanda
ya video...na akasema tuongzane naye hadi huko kwao, na kwa vile na mimi
nilikuwa na safari ya kwenda huko mambo yakijipa....’akasema
‘Tatizo lako,
ujanja-ujanja na kuongea sana, kunakuzuzua...na ukome kabisa kusema huyo mtoto
ni yatima, huwezi kuniua mimi, kwa kisingizio, hicho,....huna akili kweli wewe,
yatima kwani mimi nimekufa, kwani mama yake amekufa....’akasema
‘Ndio
ilikuwa njia muafaka ya kumweka mbali huyo mtoto na nyie wazazi wake amba
hamualewani, nataka kwanza hl tuelewane, maana ukitoka hapa na kwenda kuongea
ovyo, utaharibu kila kitu, ....’akasema
‘Kwahiyo
yeye mtoto, anafahamu hivyo kuwa hana baba wala mama....?’ akaulizwa
‘Nilifanya
hivyo ili asome, na ili aweze kuishi huko ulaya , na kweli akapata shule nzuri,
na kusomeshwa huko,..tatizo kubwa ndio hilo hakuweza kupata mtu wa kumuongoza
ili ajue asili yake mapema, hilo bro ndilo tunatakiwa tulifanyie kazi,
tuelewane hilo, ....’akasema
‘Unajua bro,
baada ya kwenda naye ulaya, sikuweza kuonana naye kwa miaka kma saba hivi, na siku
nilipokutana na huyo mzungu akaniambia
maendeleo ya huyo mtoto ni makubwa sana...ana akili sana darasani..,
nikamwambia nataka niwe karibu naye, nikitaka ajue lugha yao, na .....hata
asili ayake, akanikubalia, kwahiyo nikawa namtembelea, tukaanza kuzoeana, na
baadaye nikaja kumuambia mimi ni baba yake......’akasema
‘Wewe ndiye
baba yake,....?’ akauliza kaka mtu
‘Mwanzoni....si
alikuwa bado mdogo, kwahiyo nilitaka kumpeleka taratibu, ili anizoee, ilikuwa
ni hatua kwa hatua za kumrejesha kiakili kuwa yeye sivyo kama ilivyo..unielewe
hapo....’akasema
‘Ina maana
hata huyo mzeungu hukumueleza ukweli...?’ akauliza kaka mtu
‘Yeye
anafahamu kuwa mimi ni baba wa kufikia, ...mtu niliyemuokota huyo mtoto
akitangatanga msituni..... hadi sasa inajulikana hivyo, ila ni rafiki yangu
mkubwa, ndiye kaniwezesha kuwa karibu a huyo mtoto, na kwa vile kule nilipata
soko la dawa zangu, nikawa naishi huko na yeye anakuja mara kwa mara kwenye
dula langu,....tumezoeana sana, hana shida...’akasema
‘Nikuambie
kitu, wewe kwanza huna adabu kabisa, ....mimi sitakuelewa, mpaka nimchukue huyo
mtoto, nataka nikakae naye mwenyewe...’akasema
‘Bro huyo
kijana bado anasoma, na anatambulikana huko kama yatima, ukijitia kimbele mbele
utafanya asisome tena,...utamwaribia maisha yake ya baadaye na mimi utanifanya
nionekane ...eeh tapeli...’akatulia
‘Mhh...umeanza
kujileta mwenyewe, kumbe eeh...’akasema kaka yake
‘Bro, wewe
mwache asome hadi tuone mwisho wake..mtot ana kili darasani, ana kipaji sana cha lugha,...ana akili sana, hata
nilipomtembelea hapo shuleni kwao,mwalimu wake aliniambia kuwa darasani ni
miongoni mwa vijana wanaofanya vyema....’akasema
‘Lakini hata
akiwa na akili. Kama hanifahamu mimi, kama hana adabu unafikiri huko mbele
itakuwaje...?’ akaulizwa
‘Bro,
kumbuke kuwa huyu mtoto hadi kwa wazazi wake , mama yake hajulikani wali alipo,
kapotea, ...kafa, na hata wewe uljua huyu mtoto yupo wapi.....na nakuambia hivi
ukilazimisha kumchukua huyu mtoto utampoteza kabisa, ..anaweza kutoroka, na
hata asionekane tena, wewe niachie mimi nitampeleka hivyo hivyo na ipo siku
atakuja kukutambua wewe kama baba yake, sasa hivi usilamishe....’akasema
‘Hilo
sikuoelewi,...mimi naondoka, ila nikirudi tena ujue nitakuja
kumchukua,....’akasema na kuondoka, na wakati anageuka kuondoka mlango
ukagongwa
‘Dad am back....am hungry...’ sauti ikasikika
NB: Haya haya, japo kwa shida, lakini tutafika tu, kwa leo ni
hayo , tuzidi kuombeana heri...
WAZO LA LEO: Kizazi chema ni kile kinachojengwa
kwa maadili mema, elimu yenye manufaa, na msingi mwema wa maisha. Wazazi ni
jukumu letu kujitahidi kwa hilo, maisha ya ubabaishaji, utapeli, kudanganya
tusiyaingize kwenye akili za watoto wetu, kwani baadaye tutakuwa na taifa
lisilojua sheria, na muelekeo mwema.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment