Ikapita miaka kumi na
sita baada tukio hilo la kupotea mtoto, na wakati wengi wameshasahau, isipokuwa mtu mmoja tu...mama wa mtoto
aliyepotea, mama huyo alikuwa siku zote akimtaka mtoto wake, akilia...na alikuwa
akisema anajua mtoto wake yupo hai,..
'Nina uhakika mtoto wangu yupo hai...kuna mtu kamuiba mtoto wangu...'akawa anasema, lakini tofauti na mawaz yake hayo ndugu na jamaa
wao walijua kuwa mtoto huyo hayupo tena duniani, walishakata tamaa na kusema mtoto huyo hayupo hai tena, wakawa wanampuuza huyo mama.
Basi siku moja
akaonekana jamaa mmoja anayeitwa profesa, kutokana na utaalamu wake wa madawa,
na kuongea lugha nyingi, alionekana akiwa kaandamana na kijana, wakiwa wameteremka
kwenye basi na kwa muda huo walikuwa wakitembea kuelekea kwenye nyumba mojawapo,
kijana yule alionekaa mtanashati akiwa kavalia kisasa , mawani ya jua, unajua
tena vijana....
‘Dad where are we going...?’ kijana akauliza akiangalia huku na kule
huku akikunja pua kuashiria kuna harufu asiyoipenda
‘Nilikuambia nataka
kwenda kukuonyesha asili yako,...ambapo baba yako yupo, na ikibidi
nitakuonyesha mama yako...’yule profesa akasema
‘But you told me before, I don’t have a real parents, and even in school,
I registered that way, you know what I mean..., then to day....hahaha dad!’akasema
akionyesha mshangao
‘Yah, it supposed to be that way,.... but in
reality you have your own parents, and me, am not your biological father..’akasema
huyo profesa, na kijana japokuwa alikuwa
anafahamu Kiswahili lakini hakupenda kabisa kuongea Kiswahili, ...
Kijana huyu miaka mingi
alikuwa akisoma huko nje, kwenye shule maalumu ya watoto mayatima, kuna muda
walikuwa wakija likizo, na huwa anapelekwa shule za hapa nchini ili kukijua Kiswahili,
lakini hakukipenda, japokuwa alikuwa mwepesi kujua lugha yao, kwani kwa muda
mfupi akawa anakijua Kiswahili,, na alishaambiwa kabisa akifika kwao ajitahidi
kuongea kiswahili ili aweze kuelewana na jamaa zake.
‘Mhh samahani mzee, ngoja
kwanza...’nikataka kumkatiza, msimualiaji, lakini hakutaka kukatizwa akaendelea
kuongea
‘Profesa na yule kijana
wakaingia kwenye eneo lililozungushiwa miti ya michongoma kama ukuta kuzunguka
eneo hilo na ndani yake kulikuwa na nyumba za miti zilizokandikwa kwa
udongo,..., na kijana akawa anaangalia yale mazingira kwa macho ya udadisi huku
akikwepa asichafuliwe na mavumbi, na uchafu uliokuwa umetapakaa , siunajua tena
kijijini.
‘Kuna harufu
mbaya....’akasema na kipindi hicho profesa alishapiga hodi na aliyefika
kumpokea alikuwa mtu mzima, na wakaanza kuongea
‘Oh, bwana mdogo ndio
umefika...nilijua unatania, maana kila mara ukifika unaishia huko mjini, sasa
naona umetimiza ahadi yako, haya nambie kilichokuleta, maana huji hapa bila
sababu?’ akaulizwa
‘Ndio nimefika kama
nilivyokuambia, nimeteremka hapo kwenye bas, na kama nilivyokuelezea kwenye
simu, leo nimeamua kutimiza ahadi yangu, tumefika...’akasema na yule mtu mzima akawa
anamkagua huyo mtoto, na mtoto akawa anaangaza macho huku na kule wala
hakusalimia
‘This is your dad,....’professa akasema
‘My Dad!...gosh....’akasema yule kijana akionyesha ishara ya kukata
tamaa, alimtupia jich huyo mtu mzima halafu akageuka kama anataka kuondoka.
‘Huyu ndiye huyo kijana
wako niliyewaambia, ana miaka kumi na sita tu hapo, sema li-mwili limekua
haraka tu...kachukua mwili wako,....huwezi kuamini kuwa ana umri huo, ...sasa
kama unavyomuona keshakuwa mkubwa, msomi, hapo ni kiingereza tu...si ulitaka
awe msomi....huyo hapo, kuna kazi kidogo ya kumbadili badili, si unajua muda
mwingi alikuwa huko nje...’akasema profesa
‘Sasa mbona hasalimii,
ina maana hajui Kiswahili....halafu naona kama katoboa masikio, au macho yangu...hapana,
...mwanaume umetoboa masikio...wewe mtoto hebu kuja hapa...eti au...?’ akauliza
huyo mtu mzima huku akikunja uso kwa hasira
‘Hahaha bro, ujana huo...usijali,
nimehakikisha havai maherenai, ni kuiga tu, lakini nimeshaanza kumbadilisha,
....na kiswahili anafahamu kwa shida, lakini unajua bro, hawa vijana wakiwa
shule, Kiswahili hakitakiwi, kwahiyo kazoea kuongea kiingereza...’akasema huku
huyo mtu mzima akiwa anaendelea kumkagua huyo kijana, akaona sura yake kabisa
akatikisa kichwa kukubali kuwa hiyo ni damu yake, halafu akasema;
‘Kweli ni damu yangu,
ila...mmmh, sijui kama nitaelewana naye, kwa tabia hiyo..mmmh, ...’akatikisa kichwa
‘Atabadilika tu,
...usijali bro...ila kwa vile bado anasoma na natakiwa niwe naye, ..namfudisha
fundisha ili akirudi shuleni, awe hajasahau...ualimu kwangu bado upo kwenye
damu japokuwa niliamua kuukimbia...’akasema
‘Wewe mtoto hebu
salimia, hujui mimi ndiye baba yako...’akasema huyo mtu mzima kwa ahsira akimsogelea
kutaka kumshika mkono, na yule kijana akasogea
pembeni kama vile anaogopa kuchafuliwa
‘Sorry...... ‘ akasema na kugeuka kumuangalia profesa
‘Dad, lets us go...’akasema
huyo kijana akimuashiria profesa kwa mkono
‘Hapa ndio nyumbani
kwenu, unataka kwenda wapi, ...’akasema huyo profesa
‘Lets us go dad, I don’t feel well, y’know what I mean, its ....harufu mbaya....’akasema akianza kuondoka
‘Unasema nini, harufu
mbaya, huna adanu kabisa wewe, huku ndio kwenu, hata kama kuna kunanuka...wewe
bwana mdogo, meniharibia mwanangu...’akasema huyo mtu mnzima akiwa katahayari,
katika maisha yake hajawahi kukutana na hali kama hiyo, kijana mdogo kuoyesha
kiburi na zarau kiasi hicho, alitamani kuonyesha ukali wake lakini akasita,....
‘Hahaha bro, ndio
utandawazi huo, kijana kakulia shuleni...na kabadilika sana tu, ningekuja naye
mapema, mbona igekuwa kazi,...tulipokuwa huko nje walikuwa wakifuata taratibu za
huko, huko watoto wana haki zao, hawatakiwi kuchapwa..na vitu kama hivyo....,unajua
tena, kwahiyo ameshabobea maisha ya huko- kizungu, si unajua tena..., usijali,
mimi nitamweka sawa, ila kwasasa mvumilie tu...’akasema profesa
‘Sikiliza, bwana mdgo, nakupa wiki moja,...mbili, nataka huyo mtoto abadilike, ajue kuwa mimi ni
nani....unasikia, huwezi kuniletea mtoto ambaye ananiona mimi kama kinyaa,
ulimuona alivyofanya,..ananikunjia pua mmi....mmmh, yaani hapa ningeshamcharaza
viboko....nyie watu nyie ..ondokeni hapa....’akasema akinyosha kidole cha onyo.
‘Sawa
bro....lakini...’akawa anajitetea.
‘Sitaki
kujitetea,....huyo mtoto hana adabu, na
nakuambia akileta huo upuuzi wake hapa kwangu, nitamuua, unasikia,...’akasema
huyo mtu uzima kwa hasira huku akimuangalia huyo mtoto kwa jicho la ukali, na
yule mtoto akashika kiuno
‘Whats,...you want to kill me, go ahead....dad, you hear that, ....lets us go...’akasema huyo kijana akianza
kuondoka
‘Umenisikia bwana mdogo,
....nakupa wiki hizi mbili ukija naye hapa nataka ajue kuwa mini ni nani
kwangu...vinginevyo, uniachie mwenyewe, kama nikufungwa nifungwe,..na hizo
sheria zenu, mtoto nizae mwenyewe halafu nitungiwe shera, ai kakuambia....’akasema
na kugeuka kurudi alipotoka, na huyo professa akasimama akishika kichwa.
‘You..., sikiliza, nilikuambia nini,...ukija huku ukijitahidi kuwa
mtoto mwema, nilikuambia ukifanyay hivyo, nitakununulia pikipiki, sasa
umeharibu...’akasema huyo profesa
‘I don’t care, ...sitaki pikipiki yako, sitaki cha huyo baba, lets go...home...’akasema na kweli
ikabidi warudi na kwenda kwa huyo profesa....
********
‘Huyo profesa ni nani,
na huyo mtoto ni nani?’ nikauliza nilipona jamaa katulia
‘Mhh, huyo profesa
alikuwa mtaalamu aliyetokea uchina,...na alishaingia nchini akitangaza dawa
zake, alipotea kwa muda,... tangu aliporudi na kipindi hicho ilipita kama miaka
kumi na sita hivi ndio akaonekana tena,....’akasema
‘Pale kijijini ndiye
aliyekuwa na nyumba ya kisasa, yenye kila kitu muhimu na zahanati yake ya dawa
za kienyeji na dawa zake nyingi zlitoka nje, uchina...na nyingine alikuwa
akitengeneza mwenyewe....’akasema
‘Alikuwa profesa kweli
au ndio jina kutokana na utaalamu wake....?’ akaulizwa
‘Hahaha, kwani uprofesa
ni nini, hebu fikiria mtu anajua lugha saba, Kiswahili kiingereza, kifaransa,
kichina...eeh, kihindi..kitaliano, kireno na yinginezo, mtu anajua madawa,
...mazingaumbwe....katembea nchi mbali mbali, ulaya , bara asia,...hapo utasema
nini, nyie mtu akijua kiingereza kidogo tu mnamuita msomi, sasa mimi ni zaidi
ya kiingereza....’akasema
‘Ina maana alikuwa ni
wewe...?’ nikauliza
‘Alikuwa profesa...elewa
hivyo, sio mimi, ...usitake kuvuruga utaratibu wangu...’akasema
‘Haya endelea....nimekuelewa...’nikasema
‘Ukumbuke kauli ya huyo
baba wa huyo kijana, profesa alipewa, wiki moja au mbili ili huyo mtoto abadilike
na aweze kumtambua baba yake, awe na adabu, tena adabu zile za kjijini, na profesa
aamtambua sana kaka yake, kuwa ni mtu wa namna gani, hawaivani kwa ukali wa
kaka yake huyo,....alijua kabisa akimpeleka tena huyo mtoto kwa jinsi alivyo, ataumizwa,
kwahiyo akawa anavuta muda, huku akijaribu kumfundisha huyo kijana jinsi gani
itakiwavyo, lakini ilikuwa kama kutwanga maji kwenye kinu, kijana akawa mtu wa madharau,
....’
Basi profesa akaendelea
kuishi na huyo kjana kwake, huku bado akiendelea kumuelekeza huyo kijana kidogo
kidigo, wiki ya kwanza, ya pili , ya tatu, kijana bado hana muelekeo, na hataki
kusikia habari za baba yake...ikafika muda akaona huenda sasa kijana atakuwa
keshaelekea elekea akaona afanye majaribio, akaona sasa ampeleke huyo mtoto
sehemu nyingine sio kwa huko kwa baba yake kwanza
‘Leo nataka ukamuone a real mother of yours...’akaambiwa
‘My mom, ...mmh, dont tell me, in all years you never told me about a
real mother , a mom,,,,leo waniambia yupo mama...kama ni kama yule dad,....never, I don’t want to see her....’akasema hivyo
‘Unakumbuka nilikuambia
usome kile kisa cha `nani kama mama’ ulikisoma ukamaliza...?’ profesa
akamuuliza
‘Its real a hot story....nimesoma, lakini mmmh, ni story
tu...unataka kusema nini?’ akauliza
‘Katika hii dunia
hakuna kama mama, ..unajua baba unaweza kumchezea, uka...mdharau kwa vile
hakuwa na machungu nawe sana, lakini, mama yako ni kitu kingine...usije
ukamdharau mama yako....’profesa akasema
‘Nimekaa miaka kumi na
sita, simjui mama, wala baba, mama na baba yangu ni wewe...leo ndio waje
kunitaka mimi....walikuwa wapi muda wote huo...kwanza niambie kwanini wewe
huishi na mama yangu...?’ akauliza swali ambalo profesa hakutaka kuulizwa
‘I told you before, usiniulize kuhusu mama ....mke
wangu...nilikuambia mke wanguu alinikimbia,...eti ...sikuwa na pesa, nilimpenda sana, na nikaapa kama sitampata
yeye sitaoa tena....ndio nikaanza kutembea duniani, ili nimuonyeshe kuwa mimi
niazo, nimerudi nasikia eti kaolewa...so, ...tuyaache hayo, hayauhusu...’profesa
akasema
‘Hahaha....dad, dad....your real very fun...all mothers
wanaokuja na kukaa na wewe, leo huyu kesho huyu, ni nani hao.....si uoe tu
mmojawapo....’akasema na professa akashika kichwa akimuangalia huyo mtoto
Profesa na huyo mtoto
wamezoeana sana, na wakati mwingine wanakaa pamoja na kuongea maisha ya
kawaida, na huyo mtoto amekuwa karibu sana na huyo profesa, ni msiri wake
mkubwa, na mengi yake anayafahamu....
‘Sikiliza, ....mimi ni
mwanaume unasikia, ulitaka nikae hivi hivi, ...wewe subiri ukue, utayaoa,
kwanza hebu kajiandae twende huko kijjijini, nataka nimuone huyo mama yako ana
tatizo gani , kama naweza kumsaidia dawa...ni mbali kidogo, tunakwenda kumuoa
mama yako,...your biological mother,
forget, about this temporary mothers, wanaokuja mara kwa mara hapa kwangu, they are nothing to me, one day I will mary
my ....’akasema profesa huku akionekana kuwa mbali kimawazo
‘Hahaha dad, every time, unasema utamuoa huyo mama umpendaye, yupo
wapi huyo mbona haji,....?’ akauliza
‘One day utamuna, atakuja....’akageuka kuingia ndani, halafu
akasimama kama vile kakumbuka jambo, akasema;
‘Ni lazima leo twende
ukamuona mama yako....ni muhimu sana, watu wasije kunielewa vibaya.....kabla
matokea ya mitihani haijatoka, nataka ujuane na wazazi, ukirudi kusoma huko
ujue wapi ulipotoka...wewe sio yatima, ...’akasema
‘Usije ukasema
sikukuonya dad, unanielewa dad,...ulinipeleka kwa huyo unayesema ni baba yangu,
uliona ilivyotokea...that old man, he is not my dad, ...mimi, naweza kuwa
na baba kama yule, hahaha, hebu kwanza angalia hii sura,..handsome boy..hahaha...’akasema akijiangalia
‘Mhh, hapa eeh,
tumepoteza mtoto,.nilijua shule itamtengeneza kumbe..oh, sasa hii ni lawama, ..huu
ujanja ujanaj mwingine hausaidii...nilimpeleka shule ya misaada akijulikana
hana wazazi....kumbe nimeharibu, lakini ningefanya nini..hili sasa ni garasa,garasa....’akasema
profesa huyo akimuangalia huyo kijana, yule kijana akiwa anajiangalia kwenye
kiyoo cha simu ya mikononi
‘Be ready..., ni lazima uende ukamuoe mama yako, mama yako anaumwa,
na nimesikia siku zote anakutaja wewe, ....’akasema profesa
‘My mother, who one,
ok, Ok, dad....siwezi kukataa kwenda, lakini ....usije kunilaumu....’akasema
huku akiendelea kubonyeza boyeza simu yake....
Nb Ni nini kitatokea? kidog kidogo, si mnajua tena....
WAZO LA LEO: Ulezi bora wa watoto wetu ndio
upendo wa dhati, kama ukimdekeza mtoto, ukaona ndio unampenda, ujue uafanya
makosa makubwa, na labda ukataka aishi kijinsi maisha yanavyokwenda...kwenda na
wakati, kitu ambacho hukufanyiwa wewe hivyo, ujue unamtengenezea mazingira
mabaya huko baadaye. Mtoto alewavyo divo akuavyo.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment