Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Monday, April 20, 2015

NANI KAMA MAMA-61


Mama wa mitaani , mama ambaye kalazwa hospitalini, kwa tatizo la kukatwa na mapanga na kuungua kwa moto, moto uliochuma sehemu aliyokuwa akiishi kwa nia ya kumuangaliza kisa ni kuwa mama huyu ni mchawi.

Mama huyu hana kumbukumbu za nyuma, huenda ni kutokana na matatizo aliyokutana nayo, madakitari wamekuwa wakijaribu kila njia kuzirudisha kumbukumbu zake na pia kujua chanzo cha matatizo yake.

Dakitari anayemshughulikia ni moja watu waliotumwa kuchunguza matatizo yanayoikumba hiyo sehemu hadi kutokea wazee akina mama kunyanyapaliwa, kuteswa na hata kuuwawa, kwa visingizio mbali mbali ikiwemo imani za kishirikiana.

Mama huyu keshaanza kurudisha kumbukumbu, na kumbukumbu zake zimeanza kumrejea kwa njia ya njozi, kila anchoota ndio kilichowahi kutokea huko nyuma, japo njoiz hizo hutokea kinamna , isiyo moja kwa moja, lakini ukiziunganisha na kutumia hekima unajua ni kitu kilichokuwa kikielezea kwenye hizo njozi.

Mama akawa anaendelea kusimulia hicho alichokiona kwenye njozi zake,  je njozi hizi zitatufikisha kwenye ukweli wa huyu mama, je huyu mama ni mama kutoka mbinguni, au ni mzimu, au shetani kama walivyodai watu,

Tuendelee na kisa chetu…

‘Mama yetu, ndoto ndio njia ya kukuelekeza yaliyopita, na kutokana na hiyo ndoto tunaweza kugundua wapi ulipotoka,…mpaka sasa hatujui mume wako ni nani, au sio, hatujui ndugu zako halisi ni nani…ndio maana watu wanafikia kusema wewe ni mama kutoka mbinguni,na wengine wanafikiria vingine….’akasema docta

‘Wanafikiria kuwa mimi ni mchawi, mzimu au sio..’akasema huyo mama

‘Ndio maana tunahitajia ukumbuke, utuambie kuhusu ndoto yako,..hata hizo za nyuma, hapo umesema ndoto zako zilianzia siku ile ulipotaka kuchomwa moto, na hebu kumbuka ndoto hiyo ya mwanzo….’akaambiwa

Siwezi kuikumbuka vyema…ila ninachokumbuka, mmh ehe, ilianzia kama hivyo tukioa lenyewe, kuwa nipo kwenye moto, nataka kuungua, mara akaja huyo rafiki yangu..’akasema

‘Nani huyo rafiki yako…?’ akaulizwa

‘Nazungumzia rafiki wa ndoto, sio ukweli, mnielewe hapo…ilionekana kuwa huyo ni rafiki yangu, maana alikuwa  karibu sana na mimi, ndivyo ninavyokumbuka

‘Ilivyotokea ni kuwa nilikuwa kati kati ya moto, nguvu zimeniishia..nikawa siwezi hata kuinua mkono,..moto ukawa mkubwa kweli unazunguka unanisogelea..nikaanza sasa kuungua mguu, …’akasema

‘Mguu uliungua kabisa kama nyma ya kubakika, moto ukazidi kuongeza, kwahiyo nikajua sasa nakufa….nikahisi mtu ananisaidia kuinuka, nikajua ni wale wale waliotaka kuniunguza, lakini mkono wa huyu mtu ulikuwa ni baridi sana, na aliponishika ukawa unaondoa ule ukali wa moto…ni kama maji ya baridi yamekuja kuuzima huo moto mwilini mwangu, …’akatulia

‘Mhh, hapo siji ilikuwaje, ila baadaye nikapiga ukelele, wa kuomba msaada nikihidi huyo mtu ni miongoni mwa hao waliotaka kuniua…lakini sauti haitoki, nikapiga kelele…kelele…kelele…na mara nikahisi nazama kwenye shimo refu, na kuelekea dunia nyingine...yenye giza....sikumbuki zaidi.

‘Kwahiyo huyo rafiki uliyemuona hhukumuona kwa sura , yaani kukumbuka kuwa ni mtu gani?’

 ‘Mhh,…sikumjua kabisa,…kwa muda huo kwenye ndoto sikujua ni nani, ila nilimuona sura yake,..lakini cha jabu sikujua ni nani…ila nilipozindukana nikamuona huyo mtu…’akasema

‘Ukamuona kuwa ni baba wa nyumba, baba wa mtoto unayemlea…au sio?’ akaulizwa

‘Ndio ajabu yenyewe, kwenye njozi sikijua kuwa ni yeye alionekana mtu tofauti, mtu nisiyemfahamu, ila nilipozindukana na kumuona kuwa ndio yeye ndio nikakumbuka kuea ndiye huyo niliyemuota kwenye njozi..’akasema

Nesi ambaye alikuwa akijifanya kufanya usafi bado alikuwa akiliwazia hilo na alitamani dada yake awe hewani asikili anachooongea huyu mama, ..akakumbuka jinsi alivyoambiwa na dada yake..

‘Yaani shemeji yako kabadilika sana, …amekuwa mpole, ..’

‘Kwa vipi..?’ akauliza

‘Hata sijui,..’dada yake akasema

‘Labda na mawazo yake ya kimaisha, muulize  maana huyo ni mume wako unatakiwa ujua kama kuna tatizo msaidiane, vipi kuhuus mtoto…’walipofikia kwenye mtoto wakasahau kuendelea kuhusu huyu baba mwenye nyumba, na kipindi hicho mawasiliano yalikuwa madogo, na hawakuweza kuwasiliana tena hadi aliporudi kwenye kozi yake.

Anakumbuka aliporudi, ndio wakakutana na tatizo la huyo mama, na siku moja dada yake alimuambia tena kuwa shemeji yake amekuwa kama kachanganyikiwa na hataki kabisa kusikia lolote kuhusu huyo mama…

Unamjua shemeji yako, hapendi kuongea kitu kwa kubahatisha, anaweza akasikia jambo au akahisi jambo…akakaa kimiya… lakini nina uhakika kuna jambo ambalo linamkera na huenda linahusiana na huyu mama…maana kuna muda nilimuona kiongea pake yake..na akaonekana ana jaziba kweli kwelii…mmh mpaka niliogopa…lakini ngoja tusubiri tuone…

 Nesi akakukumbuka swali aliloulizwa mama, …

‘Unahisi ni kwanini ulimuota huyo mwenyeji wa hiyo nyumba….je ulimpenda, au yeye unahisi alikupenda…’swali hili lilipoulizwa akatega sikio kupata jibu, lakini jibu lililotoka halikusaidia kuondoa duku duku lake

‘Hahahaha, hivi mimi kwa hii hali, …hapana…akili na mawazo yangu muda wote ulikuwa kumtafuta mtoto wangu mapenzi yangu yote yapo katika kumpata mtoto, sio vinginevyo, na sijui kwanini ikatokea kumuota,..siwezi kujau hilo..’

‘Hebu tauambie maisha yako ulipokuwa hapo nyumbani , kwa wafadhili wako ilikuwaje, hukuwahi kuota kuhusu hilo, je hukuwahi kukutana na baba mwenye nyumba mkaongea, hukuwahi kuota lolote kuhusu kukutana na huyo baba..?’ akaulizwa

‘Kwakweli sikumbuki…..maisha ya hapo siyakumbuki sana, zaidi ya tukio hilo la moto na jinsi nilivyo fika hapo, na kuwa mtu wa kuletewa watoto, lakini mengine kuhusu huyo mwenye nyumba, mama na baba,..mmh, hata sura zao naona kama zimenipotea..’akasema.

 ‘Huyu mama nahisi anaficha kitu, sizani kama hakumbuki yote…mimi nikipata muda wa kuongea naye nitamuuliza…nahisi kuna jambo..., nahisi huyu atakuwa katumwa kuchunguza..huenda ni kuhusu huyo mtoto, akapewa maneno ya kutungwa kwa watu waliowahi kusikia historia ya tukio hilo, ndio maana akajifanya hakumbuki..’akawa nesi anawaza akilini.

‘Vinginevyo huyu ni shetani, ….lakini siwezi kuamini hayo moja kwa moja... sikubaliani na kuwa huyo mama ni yule aliyekuwa kafa na sasa kafufuka....mimi msimamo wangu ndio huo huyu mama simjui , na siwezi kukubali lolote kuhusu huyo mtoto,…’akaweka msimamo huo.

Na siku hiyo ikapita hivyo

*********

Nesi alipofika kazini akawa na nia ya kumuona huyo mama, lakini alipofika aliambiwa na manesi kuwa huko wodini hakuna usalama huyo mama kachachamaa, asiende kuonana naye

‘Eeeh, anasemaje?’ akauliza

‘Hatujui…lakini inavyoonekana kuna tatizo walikuulizia,. Wakasema ukifia uende ofisi kwa mkuu, ..’akasema

‘Mhh…na huyu docta hapatikani kabisa..’akasema

‘Docta yupo ..?’ mwenzake akamuuliza

‘Aaah, we acha tu…’akasema na kutembea kuelekea kwa mkuu , alipofika ofisini kwake, akaambiwa yupo wodini, na maaigizo ni kuwa akifika hapo aelekee wodini.

********

‘Unajua  huyu nesi anajua mengi…na katuficha mengi….nilimwambia yule mpelelezi ajaribu kumhoji huyo nesi, lakini huyo mpelelezi anasema muda wa kufanya hivyo bado, anashindwa kumuhoji kwasababu atamwambia anamuhoji kwa kosa gani….’akasema

‘Lakini tatizo silimeshaonekana, mimi sioni kwanini ashindwe kumuhoji,….’akasema mwenzake.

‘Sasa sisi kama utawala inabidi tuchukue hatua..maana kama unavyoona huyo mama kachachamaa…na zipo kila sababu kuwa kweli alikuwa na mtoto, lakini sasa cha gujiuliza ni kwanini hakumbuki maswala ya mume wake…’akasema mwenzake.
‘Hilo naona limejifunga sana..kama angefunguka akakumbuka ya nyuma, tungekuwa na ushahidi wa kutosha, maana mpaka sasa hatujui wapo alipotokea, na hili linatia mashaka,…na kiukweli hata sisi japokuwa tunatafuta ukweli, japokuwa tunakubaliana kuwa huyu mama madai yake yanaweza kuwa kweli, lakini hatuwezi kufanya lolote maana mfano huyo mtoto anapatikana…tunaweza kweli kumkabidhi mtu wa namna hiyo?’ akauliza mwenzake.

‘Mhh, bado..hatuwezi, japokuwa vipimo vyangu havionyesho kuwa huyu mama kachanagnyikiwa vinaonyesha kuwa huyu mama kapoteza kumbukumbu…kwahiyo …kwa tahadhari kwanza ni kujua ukweli tu, ..na huu ukweli tutaupaat kwa nesi, sasa kwa vipi, na kwanini nesi hataki kutuambia ukweli…’akasema

‘Ngoja akija inabidi tumbane, ikibidi sheria ya utawala ifanya kazi yake..’akasema

‘Utafanyaje, maana huwezi kumtungia kosa, ana kosa gani , na huwezi kujua kwaninia nafanya hivyo huenda ni kwa masilahi ya hospitali…’akasema

‘Tutaona….’akasema na mara mlango ukagongwa

**************

 Nesi alipoingia na kuwakuta wakubwa zake akajua swala ni lile lile, akasalimiana nao na kutulia kusubiri atakalo ambiwa…

Nesi  hata iweje usije kuliongelea hilo kwa yoyote yule hadi muda muafaka ufike, hiyo kwa ni kwa masilahi ya mtoto na usalama wake..kama mama yake amfariki basi wewe ndiye unabeba hiyo dhamana..’akakumbuka kauli ya docta kijana

‘Mhh, sasa ina maana muda muafaka ndio huu… na kama muda mufaka wa kutoa hiyo siri umefika,ni nani wakuamua kuwa lifanyike nini,..’ akajiuliza nesi, huku akitizama dirishani kukwepa macho ya mabosi wake ambao walikuwa wametulia wakimtizama yeye.

‘Nesi naona umepita hapo na kuiona hali halisi ya huyo mama, ina maana hakuna muda tena wa kusubiria…’akaanza kusema bosi wao.

‘Kwahiyo nyie mnataka nifanye nini…?’ akauliza nesi, baada ya kufikiri kwa mapana na kuona kazi inaweza ikaota mbawa. Bosi wake akakunja uso, akageuka kumuangalia mwenzake halafu akamuangalia nesi, akasimama na kuanza kuongea kwa sauti ya ukali.

‘Hivi wewe una akili kweli,..unauliza swali kama hilo eti nyie mnataka nifanye nini, unamuona yule mama alivyo,…’akasema akionyeshea kidole kuelekea kule waliokolzwa huyo mama na mgonjwa mwingine akaendelea kusema;

‘Mimi ni dakitari,…mimi ni bosi wako wa kazi, … nahitaji maelezo, ili niweze kumtibu mgonjwa,…imefikia hatua kumkawiza huyu bingwa, unajua na majukumu mngapi, anahitajika kwenda kwenye hospitali nyingine, lakini siku ya ngapia nafika hapa kwetu , ni kwa ajili ya huyo mama…’akasema

‘Na wewe kama nesi wangu ni msadizi wangu wa karibu, siri za kazini hapa unazijua wewe, leo hii unanificha maelezo ambayo yataweza kumsaidia mgonjwa, kwasababu zenu za kibinafsi…nesi mimi sasa nakuonya kwa mara nyingine, kabla sijachukua hatua za kinidhamu,…niambie yote unayoyajua kuhusu huyo mama....na huyo mtoto yupo wapi….’akasema docta kwa ukali

‘Docta….hapa unaulizia mama yupi, huyu mama au huyo mama ninayemtambua mimi…?’nesi naye hakutaka kukaa kimia kwa vile bosi wake kaja juu akajitetea hivyo.

‘Nesi hebu mwangalie yule mama, pale tumemnyamazisha kiaina akipandisha hasira zake itabidi ukapambane naye wewe mwenyewe, hili sio swala la kusubiri, ni swala la kujua ukweli, na ulivyosema inaonyesha wazi unajua kitu, kuhusiana na huyo mama, na huyo mama anaweza akawa ndiye huyu mama. Nakuuliza tena huyo mtoto ambaye alizaliwa hapa wa huyo mama,….wewe si una mashaka na huyu mama,  lakini unajua wapi mtoto alipo au sio, hata kama sio wa huyu mama kama unavyodai wewe, huyo mtoto wa huyo mama unayemjua wewe yupo wapi..?’ akaulizwa

‘Alikufa..’akasema na kuwaacha wale madakitari wameduwaa. Docta bingwa akageuka kumuangalia nesi, kwa mshangao na huyu mkuu wa hospitalia akawa kamkazia nesi macho sasa kwa kuonyesha mshangao akasema;

‘Eti nini..nesi unajua unachokisema….na kama ni hivyo, kwanini hukutuambia hilo muda wote huo, tukamwambia huyo mama, ..hivi kwa hivi sasa unaweza kumwmbia huyo mama kitu kama hicho akakuelewa..’wakasema.

‘Ndio maana sikutaka kusema, nilijua nikiliongea hilo mtamuambia huyo mama, na huyo mama ataumia sana, na huenda asiamini…’nesi akasema na wakati anaongea hilo alisema alikuwa akiiona sura ya dada yake akiwa kalala na kitoto akionyesha furaha, na aliona huruma kuja kuikatisha hiyo huruma kwa mama asiyetambulikana na huenda kwenda kumtesa mtoto kwa mama ambaye huenda sio kweli mama wa huyo mtoto.

‘Mimi siamini kuwa mtoto huyo alikufa, nesi usitake kuharibu ushahidi, sema ukweli kwanini unaficha hilo tukio je ulimuiba huyo mtoto..?’ akasema docta huyo mwingine, akionekana kweli haamini kauli ya huyo nesi, na docta mwenzake akamtupia jicho halafu akamuangalia nesi.

‘Ina maana mumefikia hatua hiyo ya kutokuniamini mimi, mnamuamini huyo mama, mama ambaye hajulikani wali alipotokea,…mama ambaye hana kumbukumbu, inaonyesha anayoyaongea ni ya kubahatisha tu…hivi mfano kama ningelikuwa na huyo mtoto tunamkabidhi huyo mama, mtoto huyo anakwenda kuwawa, mtakuja kusema nini….mimi, nawashangaa sana mabosi zangu au ndio mnatafuta visa vya kunifukuza kazi..’akasema

‘Nani kazungumza maswala ya kufukazana kazi hapa…, hili ni jambo la utendaji na kama itafikia huko basi mahakama ndio itaamua, maana kuna madai, na haya madai yamekuja hapa kwenye utawala, na huyo mama keshasema akitoka hapa anakwenda mahakamani kushitaki,…sisi tumeamua kwanza kumzuia kiaina tukijua kuwa bado yupo kwenye mamlaka yetu yupo kwenye matibabu..’akasema

‘Kwanini mumuzuia muacheni aende mahakamani, na huko ukweli utajulikana…’akasema nesi, moyoni akijua kuwa hilo kalitamka tu ili kuonyesha msimamo lakini aliogopa hilo lisije kutokea.

 ‘Nesi unatupotezea muda, mimi ni mtaalamu wa mambo ya akili, huyo mama alikuwa kapoteza kumbukumbu, na sasa kumbukumbu zake zinaanza kurejea hatua kwa hatua, na ili kuweza kumsaidia zaidi ni kumpata huyo mtoto, hili litampa faraja na ataweza kukumbuka yote ya nyuma…unanielewa..’akasema docta.

‘Nimekuelewa bosi haya niambia huyo mtoto mnayemtaka nyie yupo wapi ili tumuambia huyo mama, maana mimi nimeshawaambia ukweli..’akasema nesi na wale madocta wakaangaliana na mkuu akasema;

‘Nesi, chunga sana hiyo kauli yako unajua nikiiweka kwenye maandishi ni jambo jingine…’akasema

‘Nesi wewe hapa, ni mwenyeji kuliko sisi, na huyo mama keshakunyoshea kidole wewe kuwa ndiye uliyemchukua mtoto wake, na lile kovu tumboni linadhihirisha ukweli kuwa alijifungua kwa upasuaji ,je kwani kuna siri gani iliyopo kuhusiana na huyo mama uliyesema unafahamu tukio lake…? ‘ docta akawa anasema kwa sauti ya chini.

‘Docta ndio ni kweli mimi nipo hapa kwa muda ukilinganisha na nyie…na nilisema kuwa kulikuwa na tukio la mama moja  lilitokea miaka iliyopita, nakubali na nilikuwepo,na mama huyo alikuja kufariki.. ..lakini mimi sikuwa mhusika mkuu, wahusika wakuu waliokuwepo kipindi hicho, akiwemo docta bingwa wa akinana mama. wote hao kwasasa hawapo hapa kwanini mje kunitupia lawama hizo, kwanini mnanibebesha mzigo ambao sio wangu…, ‘nesi akasema.

‘Ok, hata hebu tuambie huyo mama unayemzungumizia wewe alijifungau mtoto kwa upasuaji, mtoto wake akachukuliwa na nani?’ akaulizwa

‘Watakujibu wahusika, mimi sio msemaji wao..’akasema nesi

‘Wewe unajua fika kuwa madocta waliokuwepo hapa hawapo, aliyekuwa mkuu kakimbilia nchi ya jirani kutokana na makosa mbali mbali..tunafanya taratibu za kumrejesha kuja kujibu mashitaka…..na wewe mama kakunyoshea kidole akuwa ndiye uliyemchukua mtoto wake, hata kwenye ndoto kakuona….’akasema

‘Unasema anaitwa kuja kujibu mashitaka!?’ akauliza kwa mshangao.

‘Ndio ulijue hilo…uliwaona watu wa usalama walikuja hapa, hujiulizi kwanini…kuna mambo mengi yalifanyika hapa ubadhirifu, na kushiriki katika kuficha ukweli kwa matukio yanatokea huko kijijini yakiwemo ya mauaji…ni mambo mengi kidogo, na hayo yanafanyiwa uchunguzi, huyu mama anadhihirisha hayo…sasa je upo tayari kuwalinda wahalifu…?’ akaulizwa. Nesi kwanza akabakia kimia akiwaza, lakini akakumbuka kuwa hilo analolifanya ni kwa masilahi ya mtoto, ni masilahi ya dada yake….na huyo mama siye muhusika, kwahiyo akikubali basi atakuwa kavunja ahadi na litakalotokea kwa huyo mtoto atakuja kujialaumu maisha yake yote..hapo akasema;

‘Mnaposema mashitaka, na mimi mkaniunganisha, si mlitakiwa kunifahamisha kwa maandishi,…kuwa nashutumiwa..mbona hamjaniambia hilo….halafu mimi nitajuaje hayo….kuwa kuna mashitaka…je mimi name nimo kwenye kundi la washitakiwa..?’ akauliza?’akasema

‘Kwahiyo wewe unataka uarifiwe kwa maandishi kuwa ni mshukiwa…unataka hilo sio….?’ akaulizwa

‘Lakini mabona wangu mbona siwaelewi, mumesema kuma mashitaka,ndio maana hawa watu wa usalama  walikuja, na kiutaratibu kama kunamshitaka, ningelifahamishawa ki maandishi….’ akasema yule nesi huku akikunja uso kwa kutafakari.

‘Kama ndivyo unavyotaka sawa..lakini usije kutulaumu kuwa hatukukusaidia, mimi naona tuachie sheria ifanye kazi yake ..si ndivyo unavyotaka nesi….?’ Akauliza docta

‘Hapana mkuu, tusikimbilie huko, hili tunaweza kulimaliza kwanza hapa,..muhimu tuone tutamsaidia vipi huyu mama, tukikimbilia huko…nahisi hata nafasi ya kumsaidia huyu mama itakuwa ni ndogo..’akasema bingwa

‘Lakini si mumesema mashitaka tayari kinachofanyika kwa sasa ni uchunguzi au sio,…basi mimi naomba nikamtafute wakili ..’akasema.

‘Ok, nesi wewe unaweza kwenda, tuache tuangalia tutakachoweza kukifanya, ila kaa ukifikiria kuwa wewe ni mwanamke, hebu fikiria umejifungua na yakakutokea kama ya huyo mama, unatafuta mtoto wako,…..’akawa anaongea dakitari

‘Naombeni muda nikalitafakari na kama limefika mahakamani niweze kutafuta wakili maana naona mnanibebesha mzigo ambao sio wangu…..’akasema

 Na wakati nesi anatoka, akaona mama mmoja akitokea kwenye ile wodi ambayo alilazwa yule mama na kukimbilia wodi ya wazazi , mama huyo alijifunika kama yule mama wa mitaani, nesi  akaamua kumfuatilia huyo mama kwa nyuma akihisi ni yule mama katoka. Alikimbia hadi kwenye wodi hiyo ya wazazi, na kukuta mhusika pale naye katoka, akaaanza kuhisi wasiwasi.

‘Vipi mbona upo mbiombio…’ akagutuka na kugeuka nyuma, na nesi aliyekuwa zamu kwenye wodi hiyo ya wazazi alikuwa kabeba sinia la dawa na vifaa vingine.

‘Nahisi kuna mama kaingia humu, ambaye hastahili kuingia humu, na…’ akasema nesi mkuu kumuelezea huyo nesi mwenye zamu na wodi hiyo, na kabla huyo nesi hajajibu kitu mara wakasikia sauti ikiita kutokea ndani kwa ukali...

‘Wewe nesi upo wapi, nataka mtoto wangu…’

NB : Hapa tulikuwa tunamalizia sehemu iliyokuwa imebakia, kabla hatujaingia sehemu nyingine muhimu, tuwepo pamoja.

********

WAZO LA LEO: Maswala ya dini na imani ni kama sheria, huwezi ukayajua mpaka uyasomee na ujue mantiki yake. Watu siku hizi hujifanya kujua maswala hayo ya dini wakawa wasemaje wakuu, na hata kuzua mambo bila kujua athari zake,….


Tukumbuke kuwa kila fani ina namna zake, masharti yake,  na maana zake, ndio maana kuna wataalamu wa hiyo fani, tunapoingilia dini nyingine na kujifanya tunajua zaidi kuhusu hiyo dini, na hata kuweka uwongo ili dini hiyo ionekane  mbaya sisi tunakuwa waongo, tujiulize tunamdanganya nani, na kama ni kiongozi au wa imani nyingine ukaweka uwongo kwa dini nyingine, huoni kuwa unakiuka uadilifu wako, wewe sio mkweli hata mbele ya mungu, …..
Ni mimi: emu-three

No comments :