Yule mama alipofika pale mlangoni akasimama, hakushika mlango,...alishika kichwa , halafu akashusha mkono, dakitari akasogea na kushika kitasa cha mlango, akafungua mlango na kusema;
‘Haya unaweza kuingia,usiwe na wasiwasi….'akaambiwa
Yule mama alionekana kusita, kwanza akabakia amesimama, …dakitari
akamshika mkono, wakaingia wote …
Walipoingia ndani jicho la kwanza la huyo mama lilitua pale alipokaa nesi, na ghafala akasimama..., akaupachua mkono wake kutoka kwa yule dakitari, akawa
kasimama na na taratibu akaanza kutembea kuelekea pale alipokaa nesi…
Mkuu wa hiyo hospitali akasimama, na yule ofisa usalama naye
akafanya hivyo, ambaye hakuonekana na wasiwasi alikuwa dakitari aliyekuja naye
alikuwa kasimama mlangoni akimuangalia nesi,
Nesi, akawa anaonyesha wasiwasi, macho ya woga yakamtanda …..
Nesi alipoona huyo mama anamjia yeye, huku akijaribu kumuangalia
macho yake kwa kupitia sehemu ile iliyoachwa kwa ajili ya macho, na kujaribu
kuhidi kuwa macho ya huyo mama yalikuwa yamebadilika kwa hasira...na macho hayo,
yaliweza kupenya hadi nyoyoni mwake, na kujua kila anachokiwaza....ndivyo
alivyohisi huyo nesi kwa sekunde chache zile, akahis yupo hatarini..
Tuendelee na kisa chetu...
Nesi akiwa katulia akajipa moyo,...kwa uapnde mmoja hakuamini kuwa
huyo mtu , kama kweli ni huyo mama, ambaye alikuwa kafa na sasa kafufuka basi
huyo ni shetani na kama ni shetani hamuwezi mwanadamu mwenye udhabiti, ila
anaweza kumshinda mwanadamu kama moyo wake ukiingiwa na hofu, na yeye hapo
akajitahidi kujidhatiti, akaiondoa hofu
Nesi akamnyoshea kidole huyo mama na kuanza kuongea kwa sauti...
‘Hata kama wewe ni shetani sikuogopi, mungu atanilinda, hata kama
wewe ni mwanga umekuja kutaka kunidhuru, sikuogopi , mungu atanilinda ...
'Wewe ni mwanga, au shetani au mzimu, angamia kwa jina la mwenyezimungu....najua wewe ni mzimu, umekuja kutaka kumchukua mtoto
ambaye sio wako, ukamnyonye damu yake..., mimi siwezi kukubali...mungu
atanilinda, mungu atamlinda huyo mtoto unayemdai......’nesi alijikuta akiongea, na kuwafanya waliokuwepo humo ndani
kumuangalia kwa mshangao.
‘Kwa nguvu za muumba kama wewe ni shetani, kama wewe ni mzimu,
rudi huko ulipotoka,...angamia na tokomoea huko ulipotoka...’nesi akawa anaongea
akinyosha mkono kama anakemea, wakati huo wengine wote walikuwa kimia.
Yule mama aliyekuwa akimsogelea, amabye sasa alishakuwa karibu na huyo nesi, akawa anainua mikono kumkabili nesi,...sijui ni kutokana na hayo maneno, au sijui ni kitu gani kilimfanya asite, kwani ghafla alisimama...
Ghafla akatulia na
mikono iliyoanza kuinuka kutaka kumshika huyo nesi,ikarudi chini,....na mara
akainua mikono na kushika kichwa na haikupita muda akaanza kuyumba, na kama
asingelikuwa yule dakitari kuwa karibu naye huyo mama angelidondoka , lakini
dakitari akamshika na akawa anahangaika naye kumweka sawa
‘Vipi tena....’aliyesema hivyo alikuwa ni askari, na wote
wakasimama sasa wakihangaika kumshika huyo mama, ambaye alionekana kama hayupo
sawa...
‘Mnaona...mnaoona.......’ilikuwa auli ya nesi ambaye alikuwa
kasimama pale akiwa haamini, japokuwa aliyatamka hayo maneno, lakini bado
akilini alikuwa hayaamini hayo aliyoyasema, lakini kwa namna nyingine akajua
yamefanya kazi,.....
‘Ina maana huyu mama ndiye huyo mama...ni mzimu wake,.....kama ni
yeye sikubali hata mara moja kumchukua mtoto wetu...’akasema kimoyo moyo
‘Naona hali sio nzuri..’akasema dakitari aliyekuja na huyo
mama..., na ikawa kazi ya kumweka huyo mama kwenye kiti, lakini
haikuwezekana....wakamlaza sakafuni, na haraka dakitari mwingine akaitisha
kitanda maalumu cha kubebea wagonjwa, ....na baadaye yule mama akabebwa na
kurudishwa chumba maalumu cha wagonjwa wa dharura...
Yule mama akafanyiwa huduma
ya kwanza, na alionekana kama kapoteza fahamu....waliokuwa wanahangaika
walikuwa madocta, kwani kwao wao walijua kuwa huyo ni mwanadamu tofauti na
dhana iliyjijenga, ...
********
Nesi , docta wa magonjwa ya akili na mkuu wa hospitali, walikuwa
wamekaa kukizungua kitanda, alichokuwa kalala huyo mama, na wale watu wa
usalama bado walikuwa kule ofisini kwa huyu mkuu wa hiyo hospitali, wakisubiria
taarifa kwa hamu kutoka kwa wataalamu hawa;
Wao kama watu wa usalama wasingelwieza kuingia chumba hicho
maalumu cha wagonjwa mahututi, lakini pale walipoachwa kila mmoja alikuwa na
lake kichwani, hasa walipona nesi anakemea, …kama vile huyo mama ni shetani au
mwanga, na ghafala mama huyo akadondoka, basi kila mmoja alipeleka akili yake kwa
runinga jinsi watu wa dini wanavyokemea mashetani na watu kudondoka..
‘Yawezekaan huyu mama kweli alitekwa na shetani….’akasema ofisa
huyo wa polisi
‘Kwanini…?’ akauliza mwenzake
‘Huoni nesi kamkemea, kasema kama ni shetani lishindwe..na ghafala
mama akayumba na kudondoka..wewe huoni kuwa huyo mama ana mtindio wa namna
hiyo..’akasema
‘Unaamini hayo mkuu..?’ akauliza
‘Aaah,unajua kuona kunaweza kukupelekea kuamini,nimekuwa
nikifuatilia tatizo hili na nimesikia mengi…na kama nilivyokuambia niliambiwa
huyu mama katekwa na shetani, sasa kwa hili linanionyesha kuwa kunaweza kukawa
na ukweli..’akasema
‘Mhh, mimi sijui…sina uhakika,…lakini ..mmh haya mambo siyakuamini
sana,…ngoja tuone wanasema nini hao watalaamu, lakini ulisema huyo mama hilo
shteni likimtoka anakufa, au sio…’akasema
‘Ndio wasiwasi wangu huo..’akasema
‘Sasa kama hakufa, …’akasema
‘Ina maana …kuna uwongo, ina maana halijatoka, ina maana..oh,
unajua mambo kaam haya ya kiimani, yasiyo naushahidi, mmh hayatufai, kama
wataalamu wa usalama, cha muhimu tusubirie..ila nataka nipate muda wa kuonana
na yule mama tena..’akasema
‘Mama yupi?’ akauliza
‘Yule niliyeongea naye na kuaniambia kuwa huyu mama sio binadamu
wa kawaida,…’akasema
‘Kwanini, atakusaidia nini mama kama huyo aliyetekwa na imani za
kishirikina..?’ akauliza
‘Mimi nahisi yeye ndio hao hao, wale watu wanaodanganya wenzao
kuwa ukipata mwili wa mwanadamu unaweza kuwa tajiri….’akasema
‘Oh…umefikia kuamini hivyo lakini yeye sio mganga wa
kienyeji….utamshukuje…?’ akamuuliza
‘Lakini watu wanakwenda kwake kutabiriwa mambo yao, keshakuwa
mpiga ramli yule..na anachowaambia watu wanaamini….kwa vile mengi aliyosema
ynakuja kuwa kweli…kibahati nasibu na huenda..ndio nguvu za giza…na anaweza
kutumia mwanya huo kufanya lolote…’akasema
‘Mhh…, ngoja tuone, ngoja tusubiria huyu mama atakuwaje, ..’akasema
‘Ni sawa..ila hayo ndio malengo yangu, nataka haya mambo
tuyaangalai kiundani zaidi nahis yanajengwa kuanzia mabli sana, kuna mtu, kuna
kitu…..’akasema
‘Ok, nimekuelewa, sasa na huyu nesi, unamwamini…?’ akauliza
‘Mhh,… nahisi kuna jambo anaficha…na leo tulitaka tulibaini
kwakupitia kwa huyo mama,....lakini naona haliimevuruga, na sijui kafanya hivi
ili kuvuruga huo mtegoo…ila kwa vyovyote iwavyo,...na yeye ni lazima afike
kituoni huko tunaweza kumbana vyema, nahisi ana jambo anaficha…’akasema
‘Yah…nahisi…..’akasema mwenzake.
************
Huku kwenye chumba maalumu nako kulikuwaje…
‘Naona keshazindukana....’akasema docta bingwa wa magonjwa ya
akili na mwenzake akathibitisha hilo, wakamsogelea huyo mama, nesi akawa
kasimama pembeni, kdogo akiwaachi hao wataalamu wafanya kazi yao, na kama kuna
kitu cha kufuatilia awajibike.
Nesi alikuwa amesharizika kuwa huyu mama sio mtu wa kawaida na
kama ni mtu wa kawaida basi atakuwa alitekwa na mapepo… na akili ya kusema huyo
mama ni mzimu, haikuwa ikikubali.
‘Lakini kama ndio yeye, ….kama anavyodai, basi huu ni mzimu, huyu
ni shetani na akianza kuniandama tu, nitamkemea,..nitamuomba mungu amuangamize,
akawa sasa anakumbuka mengi jinsi ya kuomba kinga kwa mungu kwa mambo kama haya…moyoni
akawa anaomba, anamuomba mungu ampe kinga…
‘Mama hebu tuambie..unajisikiaje....?’ akauliza docta akimuangalia
huyo mama, nesi akshituka kutoka kwenye maombi yake, ina maana huyo mama
keshazindukana, na sasa anaweza akaanza kumuandama tena,…..hapana…
‘Kichwa .....kichwa kilikuwa kinaniuma sana...na kilianza pale tu
nilipoingia kwenye kile chumba, sijui ni harufu ya madawa, sijui …hata sielewi…na
hata huyo nesi alipoanza kuongea…, yaani alikuwa kama anakizidisha kichwa kwa
maumivu, na maneno yake yakazidi kunipandisha hasira, …’akasema
‘Hasira za nini?’ akaulizwa
‘Hasira za nini, ina maana hamjaniamini…’akasema
‘Tunataka tusikie ukweli wote, ..sio kwamba hatujakuamini, lakini
ni vyema ukatupa ushahidi ili tuweze kutimiza wajibu wetu…’akasema
‘Najua huyo ni mwenzenu, na ni lazima mumtetee, lakini mimi
sitakubali,…tutafikishana mbali....’akasema
‘Tunakuomba utilize kichwa chako, unajua ukizidi kupandisha hasira
na ndio kichwa kitazidi kuuma, hebu tuambie sasa unajisikiaje?’ akaulizwa na
alikaa kimia kwa muda, halafu akasema;
‘Mhh.....bado....’akatulia
‘Unasikia maumuvu wapi,kichwa au unajisikiaje..?’ akaulizwa
‘Maumivu hapana…kichwa kimepoa,… lakini nahisi kama sipo sawa,
nahisi kuna kitu bado hakipo sawa… akili inaniwanga ....’akatulia
‘Akili inakuwaje, unakumbuka vyema yaliyotokea…?’ akaulizwa
‘Mmmh nayakumbuka sana, ndoto imenisaidia,…ndoto imenipa
imenikumbusha mengi sana, nilijua tu hiyo ndoto inanielekeza jambo.....na ni
kweli ilikuwa hivyo.....’akasema
‘Hiyo ndoto imekuelekeza nini?’ akaulizwa
‘Ni kweli kuwa....nina mtoto....na kitu kinachonisumbau ni kama
nilikuwa na mtoto , mtoto wangu yupo wapi, nilimuona nesi akimchukua, huyu nesi...nesi...nesi...kwanini…nitamfanya
kitu mbaya…’akasema akionyesha kukasirika, na nesi pale aliposimama, akawa hana
amani, yule mama alikuwa hajamauona kwa jinsi alivyolala.
‘Kwani hiyo ndoto ni ndoto gani,.....?’ akauliza docta mwingine, akiwa
anamuangalia huyo mama kwa mashaka, akamtupia mwenzake jicho, kutaka uhakika
kwani waliona huyo mama anastahili kupumzika, lakini kwa hali aliyo nayo hatakubali
kufanya hivyo.
‘Au upumzike kidogo, tutakluja kuongea vyema baadaye….’akaambiwa
‘Ni pumzike,…nyie mna akili kweli, nimewaambia akili hapa
inaniwanga, nataka …..namtaka mtoto wangu…hilo ndilo la kunifanya nipumzike, …ndoto
itanirudia tena na tena…mpama nimpate..’akasema
‘Basi hebu tuambi kuhusu hiyo ndoto yako….’akasema docta
‘Hiyo ndoto hahahaaah…ni ndoto ya ajabu, na nimekuwa nikiiota mara
kwa mara.... , na hayo niliyoota japokuwa yanakuwa katika hali ya kimaajabu,
kinamna ya tofauti ...lakini yananionyesha ukweli fulani,...na imenisaidia
kukumbuka mambo yangu ya yanyuma….kutoka na hiyo ndoto sasa nimeamini...’akasema
akawa kama anataka kuinuka.
‘Wewe tulia tu,...wala usisumbuke kuinuka, mwili bado unahitajia
kupumzika... hebu tuambie umeota nini…?’ akauliza dakitari wa magonjwa ya
akili....na nesi aliyekuwa kasimama akashika kidole shavuni akitabasamu
kuonyesha dalili ya kutokukubaliana na hayo anayoongea huyo mama.
‘Unajua hata nikiwaelezea ilivyokuwa mnaweza hata msinielewe
‘ akasema
‘Wewe tuelezee tu...tutakuelewa....sisi ndio kazi yetu mimi hapa
ni docta mtaalamu wa mambo hayo …’akasema docta na huyo mama akatulia kama
anawaza jambo
‘Ilianza ghafla tu…nipo sehemu... nipo sehemu yenye ubaridi sana,
...sijui ni wapi, lakini kwa akili yangu nilijiona kama nipo kati kati ya msitu
mkubwa....maana kulikuwa kumetulia kimya,...’akasema na kutulia kidogo kama
anajaribu kukumbuka kitu.
‘Msitu!,. Msitu gani huo....?’ akaulizwa
‘Sijui...nilihisi hivyo tu, akili ilinituma nifikiri hivyo...’akasema
‘Ehe, hapo msituni ulikuwa unafanya nini…?’ akaulizwa
‘Ni kama nimelala….sasa sijui ni kitandani aua kwenye
majani..lakini nimelala
nimenyooka,...siwezi kuinuka....ilikuwa kama ...sijui lakini nilijua
kuwa nimelala hivyo, na siwezi kufanya chochote zaidi ya kulala, na kuwaza
tu...kuna muda nilitamani niinuke, lakini mwili ulikuwa kama sio wangu.....kiwili
wili kilikuwa kama sio change, change ni akili ya kuwaza tu..’akatulia
‘Lakini ulijiona ukiwa mtu kamili, au ulikuwa mfu, au
ulikuwaje....?’ akauliza docta
‘Hapana, sio mfu....sikuwa nimekufa,labda nilikufa, lakini hapa
sijui......sio hivyo kutokana na hiyo ndoto nilikuwa nimelala...mwili ulikuwa
hauna nguvu ya kufanya chochote..., nilichokuwa nacho ni akili, kuwaza tu...’akasema
‘Ulikuwa peke yako..?’ akaulizwa
‘Ndio nataka kukuelezea ilivyokuwa baadaye…’akasema
‘Ehe….’akasema docta
‘Nikiwa hapo nimelala, ghafla nikajiona nimezungukwa na watu
warefu waliovalia majoho ya rangi…kama hayo mnayovaa mkienda kufanya upasuaji
na usoni wamejifunika kuficha sura zao, na kuachia sehemu ya macho tu,... na
wote walinizunguka mimi.
‘Hao watu uliwaona..ina maana ulikuwa macho...unawaona kwa macho
yako hao watu...au ndio ukiwa nusu mfu...au ..unawaza?’ akaulizwa.
‘Hapana, sio kuona kwa macho haya...usiseme neno mfu, sikuwa
nimekufa bwana..mnielewe, hakuna cha kufa hapo, ...ila, macho yalifumba, si
nipo usingizini,... naota..kinachofanya kazi hapo ni akili, mwili umetulia
kabisa..lakini unajiona kwenye matendo, ila mimi kwa upande wngu sikuweza
kufanya matendo...naona kama mwili ulifungwa, sio kwamba hapana hauwezi kufnya
kitu....hauna nguvu ya kuinuka...ila naona kila kitu kwa macho ya ndani akilini
...na ninaowaona watu wanavyofanya kazi, wanatenda, ila mimi sikuweza kufanya
lolote.....’akasema
‘Ina maana wenzako uliowaona kwenye ndoto wanafanya kazi kama
kawaida, na vitendo kama kawaida, ila wewe huwezi kufanya hivyo, ....na hao
watu walikuwaje...?’ akaulizwa
‘Watu hao...wao walikuwa wanafanya
kazi, vitendo kama kawaida...ila sasa maumbile yao, ni ya ajabu kabisa.....’akatulia
kidogo
‘Wao walikuwaje, ni binadamu au mashetani…?’ akaulizwa
‘Wao walikuwa warefu, wakubwa,..ni mijitu.....na siweza kuwaona
kwa ukamlifu,..kwa muda ule kwanza sikujua ni nani na wanataka kufanya nini
kwangu, lakini zikanijia hisia,...kuwa hao ni wachawi, au ni mjitu tu....na
wanachotaka kwangu ni kula nyama yangu, ....’akasema
‘Kwanini wale nyama yako....au ulihisi tu hivyo?’ akaulizwa
‘Nilihisi hivyo tu....lakini kitu kingine kilichonifanya nihisi
hivyo ni kwa vile walikuwa na vifaaa, kama mavisu na mikasi mikubwa
sana...masindano makubwa sana..yaani kila kitu kilikuwa
kikubwaaaa.....’akatulia
‘Sasa kwanini ulihisi kuwa ni wachawi...?’ akaulizwa
‘Hata sijui, nahisi ni akili za kibinadamu zilivyo,...jambo la
ajabu akili zetu zinakimbilia huko, kwahiyo kwa hisia zangu nikajua ni wachawi,
au mashetani....au mijitu kama nioliyowahi kusoma kwenye vitabu vya Sinbad…’akasema
‘Walikuwa wanavitu gani zaidi ambavyo wachawi wanavitumia....?’
akaulizwa
‘Mhh, zaidi ya kuvaa nguo nyeupe, na kujifunika nyuso zao...sikuona
kitu kingine ambacho wachawi tunaambiwa ndivyo walivyo....hisia tu ndizo zilinituma hivyo.....zaidi walikuwa na
mamikasi makubwa....mavisu...yaani kwa ukubwa naona kama mapanga....’akasema
‘Ehe,...walifanya nini?’ akaulizwa
‘Kwa hisia nilijua wanataka kugawana mwili wangu....’akasema
‘Walifanya nini mpaka ukahisi hivyo..hebu elezea walivyokuwa
wakifanya?’ akaulizwa
‘Kuna mmoja wao alikuwa karibu yangu akiwa kainamia upande wa
tumbo langu...tumbo lenyewe nilikuwa silioni, nahisi tu kuwa nina tumbo..., na
ilionekana kama anaagiza visu na vifaa vingine ambavyo vilionekana kama mapanga
yenye ncha kali, ...akilini mwangu nilijua ndiye kiongozi wa kugawa nyama kwa
wenzake...’akasema
‘Nilimuona huyo aliyeinamia
kwenye tumbo langu, kila mara alikuwa
akikirudisha kifaa au kukisogeza pembeni kifaa alichotumia kikiwa kimejaa damu.
Nikajua ni damu yangu, inatokea sehemu anazokata nyama yangu...Niliwaona ni
watu wasio na huruma...walionekana hivyo, japokuwa walikuwa wameficha nyuso
zao....niliyemuogopa zaidi ni huyo aliyekuwa kaniinamia, maana niliona hasiti
kufanya anachokifanya...’akasema.
‘Wakati wanakata nyama, ...ulihisi maumivu....?’ akaulizwa
‘Hapana..hakuna hisia yoyote ya maumivu....hakuna ninachokisikia
kama kagusa kitu, hapana, sihisi kitu,akili tu inawaza hivyo...’akasema
‘Kuna muda nilijaribu kuinua kichwa kuwaomba wanihurumie na
kuniacha huru, lakini sikuweza kuinua hata sehemu ndogo ya mdomo wangu, nilikuwa nimelegea
mwili mzima, na hata akili ilikuwa ikiwaza tu kuwa sasa wanafanya hiki au kile,
kwa macho naona, lakini sio kwa macho haya, ni macho ya akilini.
‘Nilijua kabisa huko tumboni au sehemu yote ya chini kutakuwa
hakuna kilichobakia tena, na sikuweza kuhisi maumivu, kwani ilikuwa kama sio
sehemu ya mwili wangu, akili tu ndio ilikuwa ikifanya kazi....mnielewe hivyo…’akasema
‘Muda ukawa unapita, nikajua sasa labda wameshatoa utumbo na kila
kitu sehemu ya tumbo langu..., maini, na sehemu za ndani, lakini sikuona hizo
nyama, au utumbo vikitolewa nje, ial nilihisi tu kuwa wamefanya hivyo
‘Na kuna muda niliona kama wanatafuta kitu ndani ya tumbo langu
ambalo nilihisi kwasasa hakuna kitu, ni kama boksi tupu....nikaona kama
wanatizama na kuonyesha hali ya
kushangaa,...nikaona wakibadilishana vifaa!
Wakati wanaendelea hivyo,
nikaoana jambo la ajabu,....’akasema na kutulia
‘Uliona kwa hisia au kwa macho ya hisia...ehe hebu tuambie uliona
nini.....?’ akaulizwa na docta akitabasamu kuonyesha ni jambo lisiloingia
akilini lakini yeye alishaelewa anachokiongea.
‘Mhh...unajua kipindi chote nilijua wanatoa utumbo, maini, sijui
na vitu gani tumboni mwangu ..lakini sikuona hivyo vitu vikitolewa na kuwekwa
pembeni, labda kwa vile nilikuwa siwezi kuinua kichwa...’akatulia
‘Lakini safari hii kwa mara ya kwanza nikaona wakitoa kitu
nilichokiona,...’akasema
‘Ulikiona kwa macho au kwa hisia?’ akaulizwa
‘Ni kwa hisia,...yaani macho ya hisia yanaona hicho kitu,.....yote
hayo yanafanyika kihisia, kindoto-ndoto naona wanatenda...’akasema
‘Ok, ukaona nini cha ajabu....?’ akaulizwa
‘Maana mwanzoni nilikuwa nahisi kuwa wanaukata mwili wangu na
kugawana nyama au vitu vya ndani, lakini sikuona hivyo vitu kama nyama au vitu
vya ndani vikipewa hao waliokuwepo pembeni yangu...’akasema
‘Safari niliona kitu kikitolewa tumboni mwangu,...’akasema
‘Kitu gani ulikiona , utumbo, maini au kitu gani?’ akaulizwa
‘Niliona wametoa kiumbe cha ajabu...’akasema na nesi akashika
mdomo kama anashuhudia uwongo wa huyo mama, lakini madocta walikuwa
hawamuangalii yeye, wao walikuwa wanamuangalia huyo mama tu.
‘Kiumbe cha ajabu...?’ wakauliza mdocta wote kwa mshangao.
‘Ndio nasema kiumbe cha ajabu ,kwa uonekavu wake....kilikuwa kama
mtoto mchanga, lakini ukubwa wake ndio ulinitisha...kama nilivyosema, kila kitu
humo kilikuw akikubwa sana, kwahiyo hata huyo mtoto mchanga, alikuwa mkubwa...kupita
hata mimi….’akasema
‘Kwa uoni wangu asingeliweza kukaa tumboni mwangu, ila kwa haraka
nikajua ni mtoto wangu..kiumbe hicho kitakuwa kimetokea tumboni mwangu...na
nikahisi kinafanana na mimi...hasa macho....’akasema
‘Kwanini macho...?’ akaulizwa
‘Hata sijui maana kilikuwa kimefumba macho...hadi kilipofikia ile
hali ya kulia,...nikaona macho yakitembea kuonekana kuwa kipo hai...nikayaona macho
yake kama yanafanana na macho yangu....kwasabbu ya ukubwa unaona kila kitu
wazi..macho makubwa, pua kubwa…unaonaeeh…’akasema
‘Hebu nikuulize kwanza, je hapo ulipokuwepo ulijua kuwa una mtoto
tumboni...au ndoto yako ilianza ghafla upo sehemu hujui kama upoje...kwani
ulikuwa mja mnzito kabla?’ akaulizwa
‘Sikumbuki ya nyuma,..ninachokumbuka ni hivyo tu, kuwa nipo
porini...nimezungukwa na hiyo mijitu...na hiyo mijitu ikatoa kiumbe cha ajabu
tumboni mwangu....na kiumbe hicho kinafanana na mimi hasa macho....’akasema
‘Yule kiumbe, ambaye ni mtoto mchanga, mkubwa tu, lakini kwao wao
kwa vile walikuwa wakubwa vile vile, walimshika kama vile unavyoshika
kichanga..., na kichanga hicho kilikuwa na damu-damu hivi, niliogopa … ‘akasema
‘Kwa uoni wangu alikuwa mtoto wangu, lakini nilijiuliza aliwezaje
kukaa tumboni mwangu maana ni mkubwa....’akasema
‘Huyu jamaa aliyekuwa muda mwingi akifanya jambo kwenye tumbo
langu akawa kashika hicho kiumbe mkononi akawa anafanya jambo....akawa kama
anakata kitu kama mnyororo mkubwa uliotokea chini, nilihisi utakuwa umetokea
tumboni kwangu.....’akasema
‘Yule jamaa akawa kashika kile kiumbe kama mtoto anakata vitu
fulani, sijui ni nyama zilizomzunguka yule mtu-kitoto au nini, halafu
akamkabidhi mtu-jitu mwingine, ambaye alikuwa kashika mavitambaa makubwa, huyo
mtu-jitu mwingine alikuwa ni mwanamke
‘Ulijuaje kuwa ni mwanamke....?’ akaulizwa
Nilimjua kuwa ni mwanamke kutokana na nguo zake japokuwa alikuwae
kajifunika uso, lakini gauni....mavazi ya kike yalimtofautisha na hao
wengine...na huyu mtu-jitu akakizungushia kile kitoto-mtu na kukiweka kwenye
chombo kikubwa kama beseni kubwa, halafu wakaendelea kufanya wanalolifanya
kwenye mwili wangu.
Na wale wengine wakawa wanahangaika na huyo mtoto.... Nilitamani
kuwaambia wanirudishie hicho walichokitoa tumboni mwangu, ingawaje sikujua ni
namna gani mtoto mkubwa hivyo aliweza kukaa tumboni mwangu na ukubwa wote
ule...yaani ni mkubwa.... Nikataka kusema `nipeni mtoto –jitu wangu’ lakini
mdomo haukuweza kufunguka!...’akasema akicheka.
‘Kwa bahati, yule mwanamke-jitu akafunua uso , sijui ilikuwaje
nikamuona sura yake, halafu kwa haraka akajifunika, ni wakati anakipokea hicho
kitoto –jitu kutoka kwa wale wengine waliokuwa wakifanya jambo kwa huyo
mtoto.....na akawa kama anasikiliza jambo kwa wenzake, halafu akaondoka na
hicho kitoto-jitu...nilitamani kuiga ukelele wanirudishie mtoto wangu...
‘Huyo mwanamke uliyemuona ni nani, unaweza kumkumbuka….?’
Akaulizwa
‘Ndio nikimuona nitamkumbuka tu…..hata huyo mwanaume, …nikimuona
nitamjua…’akasema
‘Hujawahi kumuona hapa hospitalini tena?’ akaulizwa
‘Hapana tangia nije hapa sijawahi kumuona, ila nikimuona
nitamtambua, anaonekana ni kijana kijana, japo pale walikuwa na maumbo makubwa…’akasema
‘Je na huyo mwanamke ni nani…?’ akaulizwa
‘Si ndio huyo nesi,….’akasema na docta wakasita walitaka
kumtambulisha nesi ambaye alikuwa pembeni na kwa jinsi huyo mma alivyolala
asingelwieza kumuona. Nesi alikuwa kimia, moyo akiomba huyo mama asije akasema
ni yeye, na kukatokea mtafaruku mwingine,
akawa katulia, akiwasikiliza wakubwa wake watasema nini… na maneno ya
huyu mama yalimchanganya, kuna muda naona kama katunga uwongo, lakini kuna muda
anahisi …ngoja asubirie huko mbele atasema kitu gani..
‘Hapa hospitalini kuna nesi wengi….ni yupo huyo ambaye ulimuona?’
akaulizwa
Yule mama kwanza akajinyosha halafu akawa kama anataka kuinuka, na
docta wakamuambia;
‘Wewe usiinuke, wewe tuambie ni yupi kwa sifa kwa jinsi alivyo…na
kama ukimuona uanaweza kumtambua….’akaambiwa
NB: Tuachie hapa kwa muda,….kuna wazo muhimu la leo nataka
kuliandika
WAZO LA LEO: Ajali za barabarani zimekuwa
zikiongezeka, watu wengi wanapoteza maisha na wengine kuwa na vilema vya
kudumu,…Tunapoteza nguvu kazi ya taifa, na ukiangalia sana na hili limekuwa ni tatizo
sugu, …imeonekana kuwa tatizo kubwa ni madereva na mwendo kasi, ..pia miundo
mbinu, barabara zetu bado ni ndogo.
Lakini pia kuna udhaifu wa watendaji wetu katika kusimamia sheria,…na
ushahidi kuwa mdogo kuwabana hawa watu…. kama sheria ingelifuatwa vyema adhabu
kali ikatolewa, madereva wangeliogopa….lakini pia kunahitajika utaalamu wa
ziada ili kuwabana hawa wakosaji na wasimamizi wa sheria wasiowajibika vyema.
Sasa hivi kuna utaalamu wa kuona matukio kuna vifaa na tekinolojia
hiyo,…vifaa hivyo vinawekwa majumbani na maofisini,… hili ni muhimu kuwepo kwenye
haya magari pia…, kila gari lihakikishe lina hicho kifaa kwa hivi sasa. Kama
simu inaweza kugundua wapi mtu alipo, kwanini haya magari yasiwekwe vifaa
vinavyoonyesha wapi gari hili lipo,..kukawa na mitambo ya kunasia mienendo ya
haya magari, utaalamu huo upo…
Ni kiasi cha kuhakikisha kuwa magari yote makubwa ya kwenda
mikoani, yamewekewa hivi vifaa, na kuwe ni kitengo maalumu cha kuchunguza hizi safari,
maana watu wanapoteza maisha na maisha ni bora kuliko hizo gharama za kuweka hivyo
vifaa ….tujalini raia wetu kwa vitendo ili kuwe na maisha bora yenye usalama.Ni
wazo langu la leo
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment