Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, April 9, 2015

NANI KAMA MAMA-55


 Siku ile ilitokea hivyo, wakati nesi anaongea na docta wakibisha kuhusu jambo ambalo nesi alishinikizwa kulifanya na akahisi kuwa huenda docta kamshitakia na mara alipogeuka kumuangalai mgonjwa akamuona kasimama….lakini alionyesha hana nguivu anatetemeka, nesi akamuashiria docta kwa mkono ageuka kumuangalia huyo mgonjwa, ….

Docta alipogeuka akamuona yule mama ndio anadondoka, na hakuwa kumshika, wakasaidiana na nesi na kumrudisha kitandani….

 ‘Hebu tulia, tulia…nesi hebu saidia huko….’docta akasema alipomuona nesi akisita kusmhiak huyo mama.

‘Unaona…, anaonekana ana joto kali sana huyu mgonjwa…hebu tumpime joto mshike mkono asidondoeshe hiki kipimo…’ akasema yule dakiatri huku anahangaika kumkamata.

‘Wanataka kunichoma moto…nakufaaaa, nakufaa…majambazi hawa, hawo wanataka kuniua eti mimi mwanga….oooh, niache, niache…..’ ilikuwa sauti kubwa iliyomfanya yule mgonjwa mwingine aliyekuwa kalala, kuzindukana na kukaa kitandani kutizama nini kinachoendelea.

 Baada ya shughuli za kidakitari za kumweka huyo mama sawa na kumpa dawa za kushusha homa, yule mama akalala.

Leo tena imetokea vile vile… na ilitokea tu pale nesi alipoingia kwenye hiyo wodi nia ni kutaka kuongea na huyo mgonjwa lakini akamkuta dakitari naye ndio anaingia.
Ile wanamsogeela huyo mama, wakahisi kitanda kikitetemeka, kuashiria huyo mama anatetemeka homa

Docta akamsogelea huyo mama, akamtizama kwa uangalifu sana. Na kumkagua kila panapowezekana,…akamweka kipimo cha joto, joto likaonekana lipo juu,…. halafu docta akaangalia kumbukumbu za usiku, walipompima, maana ilitakwia kumchunguza joto kila baada ya masaa sita, akaona usiku joto lilikuwa kawaida,

‘Mpe hizi dawa sasa hivi….akinywa talala, itasaidia….’akasema docta akimpa nesi vidonge viwili na yeye akawa anazidi kumkagua huyo mama.

Akakagua taratibu za dawa alizomuandikia siku za nyuma, na alipoona kila kitu kipo sawa akasogea pembeni na kumuuliza nesi;

Tukio hilo naona ni mara ya tatu sasa….na likitokea mgonjwa anakuwa na homa kali sana…’akasema

‘Majuzi yale ndio ilitokea hivi, sijui kwanini..’akasema nesi

‘Ni kawaida, na …..itakwisha ni dalili za kuonyesha kuwa mwili sasa umeanza kufanya kazi, ubongo unafanya kazi zaidi….hana tatizo la ndani, tatizo kubwa limeshakwisha sasa tunapambana na marejeo kwenye ubongo…’akasema

‘Kwaweli lakini lile la juzi na leo…, naona hii imezidi….anatetemeka hadi kitanda kinatingishika….’,  akasema nesi

‘Hizo ndio dalili za kuonyesha kuwa kumbukumbu zinarudi….na muhimu kuhakikisha hali kama hiyo ikitokea kuna watu karibu wa kumsaidia, vinginevyo anaweza kukimbia na hata kujiumiza….’ Akasema docta.

‘Kama ilivyowahi kutokea….’akasema nesi na kukatisha akajifanya kama anakohoa.

‘Yah..huwa iantokea..’akasema docta akiwa hamjali sana nesi alichokuwa kitaka kukisema mawazo yake kwa kipindi hicho yalikuwa kwa mgonjwa, akawa anaweka vyema kadi ya huyo mgonjwa….mara yule mama akiinuka kutoka kitandani. Ile dawa aliyopewa ilitakiwa huyo mama alale, kwani ni ya usingizi, lakini inavyoonekana haikufanya kazi haraka…

Docta kamsogelea kumshika ili asije kuanguka, yule mama akawa kama anaukwepa huo mkono wa docta kama vile ni kitu cha kumdhurua, akasema;

`Wewe ni nani..?’ akauliza huyo mama kwa sauti inayoashiria kuogopa

‘Mimi ni dakitari wako…umeshanisahau.’akasema docta

‘Ndio wewe eeh…eeh nimekukumbuka….oh, unakumbuka , nilikuambieje…?’ akauliza huku akiwa anamuangalia docta, japokuwa kajifunika kichwani lakini ilionyesha dhahiri kamkazia docta macho.

‘Ulisema unamtaka mtoto wako ….’akasema docta

‘Sasa yupo wapi ndio huyu….’akasema akimuelekezea mkono nesi,  na nesi alikuwa pembeni akiwa tayari kutoa msaada, lakini alipoona anaelekezewa mkono kumbukumbu za kuwa huyu mama sio mtu wa kawaida zikatanda ubongo wake akajiandaa kutafuta nafasi kama itabidi kukimbia.

‘Huyu ni nesi anayekusaidia kila siku umeshamsahau, humkumbuki?’ akaulizwa na huyo mama taratibu akageuza kichwa kumuangalia nesi, akatulia kwa muda, halafu akawa kama anataka kumsogelea nesi, na nesi akajiweka katika hali ya tahadhari

‘Usikimbie..sina nia mbaya na wewe….ila ninachotaka ni mtoto wangu tu..mtoto wangu ,…’akasema na nesi akawa kimia

‘Mtoto wako, hivi kila siku unasema mimi nin mtoto wako, …mimi nilimchukuaje mtoto wako?’ nesi akaona alimalize hata kama hakutakiwa kuongea na huyo mama kwa muda huo, na doct akamtupia jicho la kumkanya huyo nesi, kuwa huo sio muda mafaka wa kuongea na huyo mama.

‘Unakumbuka ile siku…wewe mkiwa na wanzako mlimchukua mtoto wangu,,…mkijua mimi nimekufa, unakumbuka…sasa nimerudi….namtaka nani, namtaka mtoto wangu….nakumbuka kila kitu…..’akasema na nesi akawa kimia

 Docta akabaki kaduwaa akimwangalia nesi na tena akimuangalia huyo mgonjwa….docta hapo alitaka kumuuliza kitu, lakini kwa utaalamu wake huo sio muda muafaka wa kumsumbua huyo mama, alitakiwa kulala na kutuliza kichwa.

Kama alivyotarajia, akamuona huyo mama anayumba, anataka kudondoka, akajua kuwa ile dawa imeshfanya kazi, huyo mama anaweza kudondoka sakafuni na hata kuumia, akamsogelea huyo.

‘Sasa pumzika, nesi ameshakusikia,…. tutalishughulikia hilo tatizo lako, usijali, niamini mimi…’akasema docta

‘Na-na---se…ma …na hivi, na—mtaka  mtoto…wangu…docta , nataka mtotoooo…wa—wa—nguuuuh, unasikia, vi-vi-ngine-vyo, yatawakuta makubwa,msije kunilaumu…..’akasema maneno ya mwisho kwa nguvu, halafu akawa kama katulia lakini mara akainua kichwa na kusema;

‘Nesi ..natum-mai ume-ni-elewa---mtoto-wangu…unakumbuka..yule…namtaka haraka…saaa-na’akasema

‘Mtoto wako yupi wewe mama, mbona hakuna maelezo ya kuonyesha kuwa uliwahi kujifungua hapa…? Akauliza docta

 ‘Muulize huyu nesi wako anajua mtoto gaaani, anajuuu-a-a wapi alim-mm-mm-peleka mtoto , mto-to-to…waaa-ngu, yeye na wenzake walipa-pa-pa-suuu-a tumbo langu na kum…m..mt-oa mtoto ..toto..wangu waka…waka….’  akakaa kimya kidogo

Ilionyesha kuwa huyo mama keshalala,…lakini baadaye kidogo kwa sauti ya kufifia akasema;

‘Nesi nikirudi…nataka uniambie mtot o wangu yupo wapi…namtaka mtoto wangu, na hiyo ndio itakuwa salama yako, sina ubaya na wewe, ubaya wangu kwa hao…hao…walionifanya hivi…’ akanyamaza kimya, na hatimaye wakasikia sauti ya muhemo wa kulala, huku anatafuna-tafua  maneno, kama vile anaota!

Docta akawa anawazia kauli hiyo `…namtaka mtoto wangu, na hiyo ndio itakuwa salama yako, sina ubaya na wewe, ubaya wangu kwa hao…hao…walionifanya hivi…’

Akikumbuka mazunguzmo yake ya ofisa usalama, akageuka kumuangalia nesi, halafu akachukua karatasi na kunadika melekezo kwani alihitajika kwenda chumba cha upasuaji, akatoa maagizo kuwa vipimo vingine vya damu vichukuliwe, ili iijulikane ni kitu gani, isije ikawa ana ugonjwa mwingine kama malaria…

‘Mchukue vipimo hivi, tuangalia tena…’akasema docta na nesi alikuwa kama kapigwa na butwaa, akawa kasimama akimuangalia huyo mama kwa macho ya kuogopa kabisa, na docta akamsogelea nesi na kumshika bega, akasema;

‘Natumai wakati umefika wa wewe kusema ukweli….kama hali unavyoiona, je hayo anayoongea huyu mama ni ya kuchanganyikiwa? ,…hapana nesi hayo anayoongea huyu mama yana ukweli ndani yake…na, wewe inavyoonekana unajua huo ukweli,….sasa naona htuna muda tena wa kupoteza....’akasema docta na nesi akabakia kimia.

Docta alimtizam yule mgonjwa kwa makini,..huku akiendelea kukumbuka mazungmzo yake na ofisa usalama, jinsi alivyoambiwa huko kijijini kuwa mama huyo sio mama wa kawaida;

‘…. kama tukikubaliana nayo ina maana tunaamini ushirikina,..na tukiamini hayo tutakuja kuamini kuwa huyu mama..mgonjwa ni shetani, sio mwanadamu...kaja kulipiza kisasi….

 Hapana huyu ni mtu kamili, ..hayo mengine ni imani tu…’akajikuta akisema na nesi aliyekuwa bado kaduwaa, akamtupia macho docta akakumbuka kile alichokisia akiwa dirishani,

‘Tunarudi kule kule..ndio maana nikakuambia hapa hakuna kesi....ni bora tuyaamini maneno ya nesi,..kuwa huyo mama alikufa...maana kaburi lake lipo...ila kuna kitu kingine kilinitia mashaka..ndio maana nikakuambia kuna utata..’akasema

‘Kitu gani...?’ akauliza docta

‘Kaburi la huyo mama..kule kwenye kijiji nilipokwenda awali lilikuwa limefukuliwa....sikukuambia awali ili nije kuoanisha na sehemu hii ya pili..’akasema

‘Limefukuliwa na nani, uligundua siku ile ile, au baadaye…..na je maiti ipo?’ akauliza

‘Haijulikani ni nani kalifukua....na maiti haipo...ni siku ile ile nilipokwenda, hata wao waligundua siku hiyo, wakawa wanashangaa….’akasema


‘Docta…una uhakika huyu ndio huyo mama….?’ Akauliza nesi

‘Mama yupi?’ akauliza docta

‘Huyo aliyekuwa amekufa…?’ akauliza na docta akamtizama huyo nesi kwa macho ya kumshangaa, akasema;

‘Wewe hayo umeyatolea wapi?’ akamuuliza

‘Aaah, nataka kujua tu….maana wewe ni docta, una uzoefu na haya mambo ni kweli kuwa mtu anaweza kufa akafufuka ….?’ Akauliza nesi.

‘Sikiliza nesi, muhimu ni wewe kuniambia yote yaliyotokea huko nyuma, na mimi nitakuwa tayari kukusaidia kwa hilo…lakini kama utabakia an siri yako, sijui, unasikia kauli ya huyo mama kasemaje?’ akauliza

‘Kwani kasemaje..?’ akauliza huku mwenyewe akikumbuka alichoambiwa na huyo mama;

‘Nesi nikirudi…nataka uniambie mtot o wangu yupo wapi…namtaka mtoto wangu, na hiyo ndio itakuwa salama yako, sina ubaya na wewe, ubaya wangu kwa hao…hao…walionifanya hivi…’

‘Docta lakini huko ni kuchanganyikiwa tu, sizani kama ……huyu mama ndiye yule aliyekuwa amekufa,mimi nina uhakika huo, hawafanani kabisa….au docta na wewe...unaamini hayo mambo, mtu afe afufuke haiwezekani….?’ akauliza

 ‘Chukua vipimo vya damu , na …nitaongea na wewe baadaye, ngoja nimalizie wagonjwa wengine…’ akasema yule dakitari akielekea kwa huyo mgonjwa mwingine, lakini kichwani mwake alikuwa anadadisi mazungumzo yake na ofisa usalama kuhusu huyo mama!

***********

 Nesi akiwa hana nguvu, alifanya alichoagizwa na docta, akachukua sindano na kuchukua mkono wa huyo mama kwa tahadhari huku akiwa kama anatetemeka akajitahdi na kuchukua damu ya huyo amma,

Alipomaliza, akasimama pembeni akimkagua huyo mama kwa macho, alishindwa hata afanye nini, alitamani amfunue kichwa amtizame usoni lakini akaona hilo halitawezekana kwani docta bado alikuwa hapo akiongea na yule mgonjwa mwingine

Basi nesi akachukua vile vupimo vya damu na kuanza kutoka navyo nje huku akiwaza kauli ya huyo docta;

‘Sikiliza nesi, muhimu ni wewe kuniambia yote yaliyotokea huko nyuma, na mimi nitakuwa tayari kukusaidia kwa hilo…lakini kama utabakia an siri yako, sijui, unasikia kauli ya huyo mama kasemaje?’

Halafu akakumbuka kile alichokisikia pale dirishani;

‘Kwa huyo nesi naona ama anapotezea muda,au na yeye anahusika kwa namna moja au nyingine...sasa nilikuwa nakusubiria wewe, kama utatoa kibali, ....tumfikishe kituoani, nahisi ana mambo mengi anatuficha, na hili litatutafanya tushindwe kutimiza wajibu wetu...’

`Ina maana huyu docta anafanya kazi mbili, ya udakitari na ushushu..kaja kunichunguza mimi…lakini anichunguze mimi kwa kosa gani, kwa ajili ya matukio hayo ya huko nyuma, lakini mimi sina hatia, ni kuhusu mtoto…..hapana,….’

‘Kwanza nivifanyie kazi hivi vipimo, nitamuomba docta wa zamani avichunguze vyema, na ikibidi nipate vipimo vya DNA, nipo tayari kugharamia…..siwezi kumtoa mtoto kwa shetani..hapana….’akawa anazidi kuongea kwake hadi alipofika chumba cha maabara.

‘Unasiki achukua vipimo vya damu hii haraka…na nahitajia zaidi, hivi wewe unaweza kutumia ile mashine ya DNA,….?’ Akauliza

‘Naweza lakini kwa kibali cha mkuu wa kitengo hiki, ….si unamfahamu mambo yake..’akasema

‘Nitaongea naye ni muhimu sana, nipata hivyo vipimo,..’akasema nesi akielekea kwa huyo dakitari wa zamani, na bahati nzuri alimkuta hata wagonjwa akamuelezea shida yake na dakitari akamtizama huyo nesi kwa muda, halafu akamuuliza

‘Hebu niambia ukweli, kwani siku ile mlifanya nini ..mpaka uhangaike hivyo, hayo hayakuhusu  yanawahusu wale waliokuwa wamepewa dhamana, kwani wewe kuna kitu chochote kinahusu pale….?’ Akauliza

‘Aaah, docta nakuombaunisaidie kwa hilo, nitakuja kukuelezea mengine ambayo hustahili kuyasikia kwa sasa, wewe niamini tu..’akasema

‘Sawa mimi nitafanya hivyo, ila ujue ile mashine inasoma na gharama, sasa itabidi ugharamie japo kidogo…’akasema

‘Nitafanya hivyo docta…’akasema nesi

‘Kwahiyo itachukua muda gani?’ akauliza

‘Mhh…ngoja nikaone kwanza, ….’akasema na kusimama kuelekea huko maabara

Wakati anasubiri vipimo, simu yake ya mkononi ikaiita, alipoitizama akaona ni dada yake anayepiga, akaipokea haraharaka. Hakutaka kuwaambia nini kinachoendelea hapo  hospitalini, kwa sasa hivi, aliona sio muda muafaka wa kuwavunja moyo, Hakuwa tayari kuamini kuwa huyo mama anaweza kuwa huyo mama aliyekuwa kafa, na sasa kafufuka, halikumuingia akilini.

‘Tunataka kukupa habari njema, …na tumeona tufanye sherehe fupi ya kumshukuru mungu…’ dada yake akawa anaongea kwa raha.

Nesi akatabasamu na kusema moyoni, nyie mna raha, lakini mwenzenu nipo taabuni, mngelijua nini kinachoendelea huku msingekuwa kwenye raha hiyo…nahis mngeliahirisha hiyo raha yenu..nesi aliyesema hayo mawazoni tu, lakini hakujua wenzake wanazungumzia raha gani….!

`Habari gani hiyo njema, …na raha gani hiyo..?’ akauliza nesi akiwa anatizama saa yake kwani aliona hao watu wa vipimo wanachelewa.

‘Nikuambie kitu mdogo wangu, jana tumetoka kuthibitisha kwa dakitari,… ‘akaanza kusema

‘Ehe..ndio ..vipi una malaria tayphoid…?’ akauliza

‘Sina matatizo hayo bhana….unajua nilipima mara ya kwanza, sikuamini…, lakini safari hii ya pili , dakitari kasema maneno yale yale, kuonyesha kuwa ni kweli ..’akasema na nesi kwa vile alikuwa na mawazo yake kichwani hakuwa na akili ya kuweza kugundua dada yake aantaka kumuambia nini.

‘Mhhh, docta akasemaje…?’ akauliza

‘Mdogo wangu nikuambie nini…ni, kweli kabisa, sikuamini maneno yake…maana nilitamani nipige ukulele dunia  nzima isikie…yaani nina furaha isiyoelezeka…kama inawezekana kesho njoo…’ akasema dada yake huku akionyesha furaha.

‘Dada unajau sijakuelewa….’akasema, ni kweli kwa hali aliyokuwa nayo,  hakuweza kuelewa kabisa kuwa dada yake anamaanisha nini, kwani kwa mara ya mwisho kuwasiliana na dada yake aliambiwa kuwa dada yake hajisiki vyema, akamshauri aje mjini wampime vyema. Lakini leo anamsikia kwenye simu akicheka kupitiliza, akajua labda anaongea akichwza na mtoto wake, lakini kasema anafurahia kitu alichoambiwa na docta...

Au kaambiwa anaweza kushika mimba tena...au...hapana mbona hilo alishaambiwa siku nyingi tu...'akawa anajiuliza bila jibu, akauliza.


‘Kwani ulipofika kwa docta uliambiwa nini ?’ akauliza huku akitizama saa yake, na dada yake akawa anaongea kitu huku anacheka, mpaka mdogo mtu akaona hiyo imezidi tena, alitamani sana kujua anachofurahia ndugu ayake, lakini wakati huo huo, akaingia nesi na katarasi mkononina kumuongelesha kwasauti ikabidi asimsikilize dada yake kwanza akaiondoa simu sikioni na kusema

‘Unasema, vipimo….eeh,?’ Akaumuuliza yule nesi aliyekuja kumpa ujumbe

'Ndio..'akasikia sauti ya dada yake, lakini wakati huo simu ipo mbali na sikio

‘Nesi unaitwa wodini, na vipimo hivi vyako hivi hapa…’ akaambiwa,

‘Sawa…wodi gani?’ akauliza

‘Ya yule mama, mgonjwa wako…’akasema na nesi aliposikia hivyo akajua kuna jambo, kuna kitu kimetokea tena huko, basi kwanza  akavipokea vile vipimo na kuirudisha simu sikioni, lakini aliona ipo kimia, kumbe mwenzake hayupo tena hewani..hakuwahi kujua ni furaha gani aliyokuwa nayo  ndugu yake.

Kwasababu ya huo muito ulionyesha wazi kuwa kuna dhahrura, ikabidi nesi aachane na hiyo simu, kwaharaka akaelekea wodini. Wodi ya mgonjwa maalumu, mama wa mitaani…

NB;   Leo tuishie hapa


WAZO LA LEO: Ni muhimu mara kwa mara tuwe na tabia ya kujichunguza afya zetu, hii sio tabia yetu kwani mara nyingi tunasubiria mpaka tuone tunaumwa, na huenda huko kuumwa tungekuzuia mapema kama tungekuwa na tabia hiyo ya kuchunguza japo mara moja kwa mwezi. Najua ni hali za kiuchumi, lakini kinga (kujipima) ni bora zaidi kuliko tiba.
Ni mimi: emu-three

No comments :