‘Ni
shahidi gani huyo manataka afike hapa mbele?’ akaulizwa.
‘Ni
Kigagula binti Mzimuni, mama wa mmiliki wa hoteli Ya Paradise….’a
'Kigagula,
ni huyo mama anayeishi hapo Paradise Hoteli, lakini anafahamika na jamii
inayomzunguka kuwa kachanganyikiwa, na unafahamu vyema sheria haimruhusu mtu wa
namna hiyo kutoa ushahidi, unalielewa vyema hilo sitaki kukumbusha..’ .
‘Huyu
mama hajachanganyikwa kihivyo, muheshimiwa hakimu….’akasema muendesha mashitaka
‘Mna
uhakika na hilo, ni ajabu basi ….mnaweza kulithibitisha hilo?’ akauliza hakimu
akionyesha wasiwasi na mshangao.
‘Ndio muheshimiwa, tunataka kulithibitisha hilo mbele ya mahakama yako
tukufu muheshimiwa, na ndipo utakapojua njama za hawa watu, wapo tayari hata
kuwaua wazazi wako kwa ajili ya tamaa ya mali…'
Tuendelee na kisa chetu..............
***********
Mahakama ilikuwa kimiya…
Mara
kikaingizwa kigari cha kukokotwa na mkono, na ndani yake akiwemo mama mzee,
ambaye ndiye shahidi aliyetakiwa
kuhojiwa. Mama huyu alionekana kutulia
kwenye kiti chake akiwa kama kajiegemeza upande mmoja, na kofia pana kichwani lenye rangi sawa na gauni lake,
Alivyokaa kwenye kle kigari, alikuwa kama kakaa upande upande, labda ni kutokana na
matatizo alio nayo ya kiafya, na muda wote alikuwa kainama chini,
hukuinua uso kuwaangalia watu hadi alipofikishwa mbele ya mahakama, sehemu wanaposimama mashahidi wanapohojiwa.
Akainamisha
kichwa kama kusalimia, na hapo watu wakacheka, hata hakimu akatabasamu, huku
akimuangalia mama hayo kwa macho ya mshangao na alionekana kuwa na hamu kubwa
kumsikia mama huyo atakachongea, maana amjuavyo yeye huongea kwa jaziba na
matusi juu.
Akawa
anamuangalia huyo mama , na pia kugeuza jicho kumuangalia muendesha amshitaka,
huku kichwani akikumbuka siku ambazo aliwahi kukutana naye, japo kwa sio mara
kwa mara lakini mara chache, alizokutana naye, alipofika kwenye hiyo hoteli
kikazi na kufahamishwa kuwa huyo mama ni nani…
‘Huyu
mama ni nani mbona namuona akitembea huku na kule na anaonekana mkali kweli?’
akauliza huyo hakimu siku ya kwanza kumuona.
‘Huyo
mama inasadikiwa ni mama wa mtoto ambaye alikuwa mumiliki wa kwanza hoteli
hii?’ akaambiwa na watu aliokuwa nao.
‘Anaonekana
hayupo sawa….’akasema
‘Kachanganyikiwa,
..akianza kutukuana hapo utakimbia,….’akaambiwa, na mara mama huyo akawaona
wakimuangalia.
‘Na
nyie mnashangaa nini hapo, mumekuja kushangaa hapa, kwenu hakuna wazazi kama
mimi,….au niwaonyeshe kuwa mimi ni mzazi na nimewaza nyie….’akawa kama anataka
kuvua nguo, na walinzi wake wakamzuia.
‘Acheni
niwaonyeshe wajue kuwa mimi ni nani, mijitu mizima ovyo,...eti hakimu , hakimuhata mimi naweza kuwa hakimu, hakimu watakuwa hawa bwana,... haya wasikilizeni
waende zao huko juu wakafanyae ufusuka wako na kulewa, unafikiri kuna cha zaidi
walichofuata hapa...'akasema akiwaangalia hao wageni.
'Waone kwanza, hivi kweli nyie mnaweza kunihukumu, mimi, nisimame mbele ya mahakamayenu mseme, utafungwa, thibutu, maweee...semeni mlichofuata hapa kama si hayo hayo, mmmh, ngoja ninyamaze maana mteja ni mfalme, yaani hata kama ni mzinzi, anatakiwa awe mfalme..hahaha , karibuni ndani ya dunia…hahaha….’akawa anacheka na
kujizungushazungusha, kipindi hicho alikuwa anaweza kutembea mwenyewe
'Mimi hata siku moja siwezi kusimama mahakamani kwako nikakusikiliza, mnasikia, kamwe, niikija huko mjue mimi ndio hakimu wenu,...haya nendeni wazinzi wenzenu wanawasubiria huko juu.....hata hamuoni haya, mumeacha wake zenu huko mnakuja kufuata maradhi...'akasema huyo mama
Hakimu alipokumbuka hayo akatabasamu, maana yule yule aliyekataa kuwa hawezi kuja kusimama mbele ya mahakama yake leo yupo mbele yake na yeye anatakiwa kuhakikisha haki inatendeka, .`.na sheria
haimruhusu mtu ambaye kachanganikiwa kutoa ushahidi, ….lakini anayway, ngoja
tuone..’ akawa anajisema kimoyo moyo.
Baadaye
alipofika tena, akawa hamuoni, akawauliza watu wanaofika hapo mara kwa mara
aliokuwa nao;
‘Yule
mama aliyekuwa mkali kweli siku hizi yupo wapi?’ akauliza.
‘Yule
mama anaumwa, wanasema alipatwa na kiharusi, na hata alipopona hajaweza
kutembea mwenyewe, anatembea kwa msaada wa kigari cha kusukuma kwa
mkono…’akaambiwa.
‘Oh,
alikuwa maklo kweli na kila mtu alikuwa akimuogopa, niliona wafanyakazi humu
ndani wakiwajibika kweli wakimuona yeye….sasa kumepooza…’akasema.
‘Nasikia
anataka kuja hapa, lakini wanamzuia, wameamua kumfungia kwenye eneo la nyumba
yao iliyokuwepo hapo pembeni mwa hiyo
hoteli…’muheshimiwa hakimu akaambiwa siku hizo.
Muheshimiwa
hakimu akaondoa yale mawazo ya nyuma na kuendelea kumuangalia vyema, na akilini
mwake akawaza;
‘Lakini
leo mbona anamuona yupo tofauti, utafikiri sio huyo mama ninayemfahamu mimi…’akawa
anawaza na hapo akawageukiwa wasaidizi wake kuaona na wao wana taswira gani usoni
mwao kuhusu huyo mama, na wenzake walionekana kuwa kama yeye.
Baadaye
hali ilipotulia vyema, na watu ambao walishaanza kunong’ona, na minong’ona ya wengi hugeuka kuwaa ngurumo. Taratibu
zikaanza, yule mama akawa anahojiwa na kulishwa kiapo, na baadaye muendesha mashitaka akawa kasimama
karibu na yule mama akaanza kumuhoji.
‘Tuambie
tena jina lako ni nani mama yetu?’ akauliza huyo mama.
‘Hilo
swali mnaniuliza mara ngapi, msinichezee akili yangu, mimi sio tahira kama
mlivyozoea kuniita, mimi nina akili zangu timamu, ni hawa vichaa wachache
wanaonidunga sindani za kunipoteza akili yangu ya asili….ole wao,…..’akasema
akiwa kamkazia macho muendesha mashitaka.
‘Ndio
maana nakuuliza jina lako tena tuone kama kweli unayosema ni kweli, kuwa wewe una
akili zako timamu, wanafanya kukuzulia tu kuwa umechanganyikiwa….’akasema
muendesha mashitaka.
‘Hahaha,
na hata wewe pia, unanipima, hahaha, haya mimi naitwa Kigagula….’akasema huyo
mama akiinua uso na kumuangalia muulizaji wa maswali, na watu wakacheka, na
akageuka kuwaangalia watu, watu wakakatiza kucheka na kukaa kimiya utafikiri
katamka neno la kuwanyamazisha.
‘Hilo
ndilo jina lako halisi au una jina jingine ?
‘Hilo
ndilo jina langu la urithi, majina mengine nimeshayaandika hapo mlipokuwa
mkinihoji, sitaki kuyarudia tena, maana yana nuksi, jina langu ni Kikagula binti Mzimuni, hilo nilipewa na bibi yangu,na
niliambiwa nisilje kulibadili, hayo majina mengine ya kisasa mimi siyataki kuyasikika
kabisa…’akasema.
‘Kwanini
wanakudunga sindani , huoni ni kwa vile wanahisi una matatizo ya kiakili?’
akaulizwa.
‘Wao
ndio wana matatizi ya kiakili sio mimi, wamegundua kuwa ninataka kongea mambo
wasiyotaka yaongelewe,..wakaona dawa ni kunimaliza kwa kunipiga madawa ya
kulevya, lakini wameshindwa, wewe huoni, wapo wapi….wanacheza na
Kigagula….watakwenda na maji,….wote, na hata huyo anayejifanya sasa kakua na
kunizidi mimi mama naye, watajuta kuzaliwa….’akasema akitingisha kichwa.
‘Mama
kwani wewe una watoto wangapi?’ akulizwa.
‘Mimi
nina mtoto mmoja tu, wa dawa….hahaha, wa dawa, na ana makarama yule mtoto,
usiombe kukutana naye, ni jembe dunia yote kaiweka hapa….’akasema akionyesha
kiganya cha mkono.
‘Na
mume wako yupo wapi?’ akaulizwa.
‘Mume
wangu, ….’hapo akatulia kidogo, halafu akasema.
‘Mume
wangu hayupo duniani, alishafariki, ila sasa anajifanya kunijia na kudai eti na
mimi nife nimfuate huko alipo, hahaha mimi sifi, nitadunda mpaka kieleweke…’akasema
na kuanza kuangalia huku na kule.
‘Mume
wako alipofariki, wewe na mtoto wako mlikuwa mkiishi wapi?’ akaulizwa
‘Hapo
hapo ilipojengwa hiyo hoteli kubwa ya kitalii, unajua hapo mwanzoni hapakuwa
hivyo, kulikuwa na nafasi kubwa ilikuwa wazi, mume wangu alikuwa mjanja,
alinunua sehemu kubwa sana…sio kwamba alinunua, sehemu hiyo yote ilikuwa ya
mababu na mababu zake…basi tena mambo ya pesa na serikali tena, basi, sehemu
nyingne ilikuja kuchukuliwa na jiji, lakni hata hivyo bado kulikuwa na nafai ya
kutosha, …’hapo akawa anaongea vizuri.
‘Una
maana ni hapo kwenye hiyo hoteli ya Paradise?’ akaulizwa
‘Ndio
hiyo hiyo pepo ya ndoto ya mwanagu, usiniulize maswali ya kijinga, uliza swali
la moja kwa moja, kwani tulikuwa tunaongelea nini mwanzoni mpaka uulize ni hapo
ni hapo..nyie vijana wa siku hizi akili zenu ni ndogo sana, mnashindwa
kupambanua mambo, ndio hapo hapo
tunapopaongelea …..’akasema kwa sauti ya ukali.
‘Kwahiyo
hiyo hoteli ilijengwa baada ya mume wako
kufariki?’ akaulizwa
‘Ilikuwa
imeshaanzwa kujengwa bwana….’akasema akibenua mdomo, kama kikerwa, halafu kama
vile amekumbuka yupo akasema;
‘Ilianzwa
kujengwa zamani sana, … asikudanganye mtu, mimi mwenyewe niliwahi kusimamia
nikiwahimiza mafundi, na taratibu za
ujenzi zilianza zamani sana, lakini sio
kwa ukubwa huo, hapo nakubali, ramani ya awali ilikuwa ndogo tu, wao ndio
wakaongezea kwenye ramani yao na ndio ikawa hivyo....’akasema.
‘Ni
akina nani waliongezea ukubwa huo,..?’ akaulizwa.
‘Ni
mtoto wangu akishirikiana na wenzake, …wenzake sasa wanajifanya eneo hilo ni la
kwao, eti na wao wa hisa, eti..eti… thubutu, nitawateketeza mmoja baada ya
mwingine, nimewaambia sitaki kusikia kauli hiyo tena, ….sijui wapo wapi hao
watu mbona hamjawakamata. Mmmh, ndio hao hapo, waulizeni , lakini wengine
hawapo hapo….?’ Akauliza na kugeuka kuangalia huku na kule.
‘Kwani
wale pale sio wenyewe, wadhamini wa hiyo hoteli,….?’ akaulizwa
.
‘Hao
ni vibaraka wao tu, wapo wenyewe, matahira fulani, wanajifanya wana akili kupindukia,….vichwa
maji kama mwanagu, wengine wanaishi nje, kuna mmoja tu yupo hapa, ananikera
kwelikweli yule mtu,…yeye, anajifanya anajua sana, huyu ….hebu ?’ akageuka huku
na kule kama kumtafuta mtu.
‘Ni
nani huyo unayemtafuta?’ akaulizwa
‘Achana
naye, mtamuona huko makaburini….’akasema
‘Makaburii!?’
akauliza muendesha mashitaka kwa mshangao
‘Huna
maswali mengine ya maana…?’ akauliza huyo mama akionekana kukerwa.
‘Kwahiyo
mtoto wako na hao unaowaita vichwa maji ndio waliobuni huo mradi wa hoteli hiyo
kubwa ya aina yake katika bara hili la Afrika?’ akaulizwa
‘Yah,
exactly muheshimiwa …..ndio ndoto
yao, ndio wao waliobuni mradi huo mkubwa na matarajio yao iwe ndio hoteli kubwa
duniani, watu wawe wanakuja kutoka mbali, kumtembelea mtawala……’akasema.
‘Huyo
mtawala ndio nani?’ akauliza.
‘Mtamuona
siku ikifika,…siwaambii, kamwe, uliza swali jingine….’akasema
‘Kwahiyo
mume wako alikuwa tajiri sana, mali hiyo alipata wapi?’ akaulizwa
‘Mume
wangu alikuwa mrithi wa utawala , utawala wa kijadi, na mtawala wakati huo
alikuwa akipata ruzuku toka kwa watu wake, ila wao waliwahi kumuliki eneo lenye
madini…siunajua madini yalivyo na pesa, wakawa matajiri kweli, enzi hizo, hata
wazungu walikuwa wakiwaheshimu,…mababu hao wakapita, wakaja sasa enzi za mume
wangu, mambo yakaanza kulega lega….’akatulia kidogo.
‘Unajua
kuna mambo mengine ya kijadi hayana maana, mume wangu akawa anayapuuzia baadhi
yao, na kuna mambo yakawa yanaharibika,…siwezi kuwaaambia yote hapa, maana nyie
mtajifanya hamyaamini, ila kiukweli yalikuwa na nguvu sana na
yanatisha….’akasema akimuangalia muendesha mashitaka.
‘Baada
ya mume wako kufariki, utajiri wote wa
mume wako ulibakia mikononi mwa mtoto wako,kwani mume wako hakuwa na watoto
wengine?’ akaulizwa.
‘Walikuwepo
watoto wengine..ndio hivyo, usasa mume wangu hakutaka sana kuonekana ana nyumba
ndogo nyingi, lakini mimi nilikuwa nazifahamu, kisiri,….unajua tena, yeye
akijifanya mjanja, akakutana na mjanja mwenzake, lakini tukawa tunaenda hivyo
hivyo,…ndio kifupi alikuwa na watoto wengine , kwa wanawake wengine…’akasema.
‘Sasa
wao ikawaje, hawakupata urithi wa utajiri wa mume wako?’ akaulizwa.
‘Mhh,
sasa wewe unanichimba, …waulize kwanini walikimbie, sijawakataza kuja kuchukua
kile wanachoona ni chao, walikimbilia huko kijijini wakawahi mashamba, mimi
sikuwafuta kuwanyang’anya, kama wao walichukua huko, basi huku na wao hawana
chao, unasikia vyema…hata hivyo ni nani angeweza kushindana na Kigagula …’akasema.
‘Labda
wewe uliwatisha, ukawaambia waondoke?’ akaulizwa.
‘Waliondoka
wenyewe kwa uwaoga wao,sikuwahi kuwaambia waondoke……’akasema
‘Ni
kwanini walifanya hivyo, mpaka waogope, je walikuwa wakikuogopa wewe…..?’
akaulizwa.
WAZO LA LEO: Dhuluma
inapozidi, watu hufikia kutokuogopa, na wengine bila aibu wanaweza hata
kuchukua mali ya mayatima, mali ya watoto wanyonge ambayo wazazi wao
walihangaika, na kwa vile wazazi hao hawapo, basi wadhalimu huichukua bila hata
aibu. Hio ni dhuluma kubwa sana , na hilo deni lna mnafahamu hakimu wake ni
nani, hakimu muadilifu anayefahamu undani wa kila jambo.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment