Saa kumi na moja, jioni ikaingia na jua likawa linatoa miale
yake ya kuaga, na hiyo ndiyo saa waliyotabiriwa kuwa mfalme siku hiyo
atatokezea huko miale inapotokea, na utakuwa muda wa jioni, kuisha kwa muongo wa shida, dhuluma na kuingia siku za matumaini, na neema.
Hili kwa mzee
Hasimu alishajiandaa nalo, kwani siku hiyo mtabiri akiwa anaelezea hayo
alikuwepo na mzee mwenzake, Mzee mtaule....akaona hilo anaweza akalitengeneza;
Alichofanya mzee Hasimu, ni kumpanga kijana, akamsomesha, na jinsi gani afanye, akawatuma yeye na kikosi cha watu waaminfu,waende upande huo wa machweo ya jua, na muda ukifika
wajitokeze na kikundi cha watu wake, huku wakipiga mbinja, au mruzi, na kutoa mlio maalumu
wa ndege mmoja wanyemuheshimu sana,.
Ndege huyo akilia wanasema anabashiria
neema. Na kweli kijana wao na kundi la maaskari walielekea huko, na wakawa
wanasubiri huo muda ufike.
Mzee Hasimu na wapambe wake walipoona sasa ni jioni ya saa
kumni na moja, kwao wao, saa haikuwa makini sana, walichokuwa wakiangalia ni
majira, na mwendo wa jua, na mwezi , na waliweza kusema muda huo ni saa ngapi
kwa kutumia vitu hivyo vya asili bila hata ya kukosea. Kwahiyo Mzee Hasimu
alipoangali jua, na kuona linaelekea kuzama, akawaambia wapambe wake muda
umefika, waelekee njia panda.
Njia panda nis ehemu ya mpaka, kati ya koo hizi mbili kubwa,
ukifika hapo utakuta njia inayoelekea eneo la mzee Hasimu, na nyingina
inaelekea eneo la mzee Mteule, na njia ya kati kato inaelekea sehemu
wanayoitambua kama sehemu takatifu.
Sehemu hiyo na njia panda ndipo vikosi viwili vya mahasimu
hawa vilikutana na kuchinjana kama mbuzi, hapo, hakuna aliyejali kuwa huyu ni
mtoto wa baba mkubwa na mdogo, wote kila mmoja, alitaka kutwaa utawala,
wakauana, na waliobakia walikuwa majeruhi ambao wengi wao walifariki baadaye.
Kipindi hicho wazee hawa wawili ndio walikuwa majemedari wa vita kila mmoja
upande wake.
Walijikuta wamebakia wawili, na wakaanza kupigana,
walipigana mpaka wakaishiwa nguvu, kama vile jogoo, wanaopigana hadi kuishiwa
nguvu, na hapohapo ndipo kikosi maalumu toka uko chimbukoni kwao kikafika, na
kuwatenganisha.
Kila moja alichukuliwa upande wake, na baadaye
wakakutanishwa na maiti zote zilipelekwa sehemu hiyo wanayoiita sehemu
takatifu, ambapo ndipo askari wengi waliuwawa kabla hawajafikia hapo njia
panda, sehemu hiyo ndiyo iliyokusanywa maiti wote na kila aliyebakia hai, ndugu
na jamaa ambao hawakuwepo itani, walifika kuchukua maiti zao.
‘Haya jamani mliyoyataka ndio hayo, hawo ni ndigiu zenu,
toka ni toke, baba mdogo na mkubwa, sasa hivi na maiti, ……naona sas
amumesuuzika mioyo yenu, …je bado mnataka kuuana, ?’ wakaulizwa.
Majeruhi ambao walikuwa wakigugumia maumivu, wakaguna, kila
mmoja akitaka apate sehemu ya kujipumzisha ili aponyeshe kidonda chake, na wale
ndugu waliofiwa na vijana wao, walikuwa wakitoa machozi ya huzuni. Hakuna
aliyetaka vita tena, hakuna aliyetaka huo unaoitwa utawala, wa nini kama utawala ndio huo wa kuuana, hakuna amani. Na wengine
walidiriki kusema kama ni hivyo ni bora warejee huko walipotoka.
Mzee Hasimu ambaye alikuwa kazingirwa na maaskari kutoka
huko chimbukoni kwao, alikuwa katulia, akiuma meno kwa hasira, moyonu alikuwa
na kisasi, na alitaka akiachiwa hapo akakusanye tena kikosi chake na kuja
kummalizia hasimu wake, lakini kila alipotoka kuinua mguu alitulizwa.
‘Jemedari sikiliza, hivi wewe unataka nini zaidi, …unataka
madaraka, unataka kumiliki ardhi , unataka kumiliki mifugo utajiri..au unataka
nini cha zaidi,…kama unavitaka hivyo vyote utavipata, haina haja ya kumwaga
damu tena, hakuna haja ya kuuna tena, kama mtauana wote, huo utajiri, utapatia
wapi, na ni nani utamtawala, ..unataka utawale vilema?’ akaulizwa.
‘Sasa ni wakati wa kushikana mkono, vita basi…kwanza mshikeni mikono, na pili watakuja
wanasheria kuwatungia sheria itakayowatawala,…kila mmoja ni lazima aifuate
sheria hiyo, tutawapa kipindi cha mpito, na kipindi hicho kila atakayekiuka
hiyo sheria hakutakuwa na msamaha…
Wakapewa hiyo sheria, na sehemu hiyo ikawa inatawaliwa
kijeshi na kikundi maalumu toka huko chimbukoni kwao. Kipindi hicho kilikuwa
cha sheria ni msimemo, kila aliyekiuka sheria, adhabu kali ilitolewa, na adhabu
kali ilikuwa kutupwa ziwani na kuliwa na mamba. Na hapo ndipo kulipotokea imani
ya kuamini kuwa mamba ndiye mlaji wa wakosaji. Na imani hiyo ilikuwepo toka
huko chimbukoni kwao.
Kipindi hicho kila raia alitakiwa kufanya kazi, kila ikifik
asubuhi, maaskari walipita nyumba hadi nyumba kuhakikisha kuwa kila raia yupo
kwenye kazi, hakuna kukaa makundi, vijana walitumiwa kwa kazi ngumu, ili wawe
mashupavu, hakuna kulewa kipindi cha mchana,…kila mtu alitakiwa kutahamini
kazi.
Kipindi cha mpito kilipopita, kila mtu akawa kajengeka na
imani, imani ya kupenda kazi, imani ya
kutii sheria, na imani ya kuamini mambo yaliyoelekezwa na wazee wao kutii viongozi wao, na kila mmoja
aliogopa kufanya makosa, kwani ukifanya kosa unatupiwa mamba, familia
inatengwa, na kupelekwa kisiwa cha umauti.
‘Kipindi cha mpito kimekwisha sasa tunataka kuwakabidhi
madaraak yenu, lakini kwa amsharti kuwa yule atakyekiuka sheria, ataadhibiwa,…na
adhabu kubwa itakwua ikiwaandama viongozi, …kama kiongozi unatakiwa uwe mfano,
uwe wa kwanza kutii sheria, …’wakapewa maagizo na sehemu hiyo ya kumbukumbu ya
mauaji ya kivita ikawa ndio sehemu ya kukutania.
Baadaye akaja huyo mtabiri, na kuwaambia sehemu hiyo ni
sehemu takataifu, kwani roho za mashujaa waliokufa kwenye vita huwa zinafiaka
hapo kila siku, na nyingine bado zinadai haki, na haki ni utawala bora. Kila
mmoja atii utawala, atii sheria, mkikiuka sheria, basi janga litawapata.
‘Yupo kiongozi wenu atakuja miaka kadhaa mbele, kiongozi
huyo, ndiye ataibadili hi hali hapa na kuwaletea amendeleo ya kisasa. Kiongozi
huyo atakutana ndiye atamuoa malikia. Malikia mbaye ujaji wake hapa utakuwa wa
miujiza,….malikia huyo hatatokana na nyie, ila alikuwa ni damu yenu.
‘Malikia huyo akija ndiye ataolewa na kijana wenu
shupavu,..kijana wenu ambaye ndiye atakuwa mfalme, mfalme wa taifa teule. Taifa
ambalo litakuwa kuja taifa lenye nguvu, utajiri, aman na matumaini. Hakuna
umwagaji damu tena, hakuna dhuluma, hakuna kuwaonea wanyonge.
Mfalme huyo atatoke
machweo ya jua, atakuja na usafiri wenu wa asili, akiwa na sura ya ajabu….sura
ya ajabu kwa sababu ya mavazi yake, kwasababu ya kuwajibiak kwake, atakuwa
kachoka, na pembeni yake atakuwa na majeruhi ya walioumia vitani…
‘Na huyo ndiye atakaye waleta taifa la amani, taifa teule,
taifa lenye nidhamu, …lakini hayo yote yanahitaji subira, yanahitaji ujasiri, na
hayatakuja kirahisi,….mkicheza mnaweza kuingia vitani tena, na kama kutatokea
vita tena, taifa hili lote litaangamia.
‘Kumbeni siku hiyo, siku maalumu ya mavuono, ndipo atatokea
huyo shujaa, siku hiyoo haitaki kumwagwa damu, siku hiyo, kila mmoja anatakiwa
awe mkarimu kwa mwenzake, na kama unataka baraka, na kama una matatizo, na kama
unaumwa, siku hiyo ndiyo siku ya kupona, lakini kuweza kufanikisha hayo,
inahitaji kwanza ujisafishe moyo wako. Uwe huru, uwe na amani, na kam kuna
watumwa, waachiwe wote..ili muwe na amani.
‘Tadhari siku hiyo, kama kutatokea kumwaga damu, laana kubwa
itawaandama, ….kama kweli mnataka taifa teule, taifa la amani, …kama kweli
mnataka maisha ya raha, kama kweli mnahitaji baraka kwenye familia zenu, vizazi
vyenu, siku hiyo ndio siku maalumu, …..pendaneni, ondoeni chuki,….visasi, na
kila mmoja amuone mwenzake ni ndugu yake. Na kila mmoja we tayari kupma
mwenzake kila alichojaliwa nacho…
‘Mkifanya hivyo, mtafanikiwa, …kama bado moyo wako una
uchoyo, hupendi mwenzako apate, kama ulivyo wewe, utakuwa hujafanikiwa siku
hiyo. Na siku hiyo ikifika, na miali ya juoa ya kuzama ikiwa ainamulika
kuashiria kuisha kwa siku, na kila mmoja akwa huru nafsini mwake,….akajaa
upendo, huruma, unyenyekevu…basi pale kiwingu kitakapotanda kutokana na ugeni
huo, kama una tatizo, kama una shida, omba, elezea shida zako,….hutaamini,
zitaondoka zote kabla siku hiyo haijaisha…
‘Nyie ni ndugu, mkiangalia hapa mlikuja watoto wa babu ba
bibi mmoja, ambaye alizaa watoto wengi, lakini kutoka kwa mama mmoja, ndio nyie
kutokana na watoto hawo mkazaliwa, kizazi cha babu na bibi mmoja au sio”
akauliza, kwani ni kweli watu hawo waliamua kuondoka huko walipokuwepo awali,
wakidai kuwa babu yao alikuwa na eneo na inabidi waende wakaishi huko kwenye
eneo la babu yao.
‘Sasa kwanini mpigeni, kwanini mjengeani visasi, chuki uchoyo
na husuda. Babu yenu na bibi huko alipo kakasirika, roho yake haina amani,…na
sasa anataka amani….ole wenu yule atakayekiuka…subirini mpate mtawala bora,
ambaye ataweza kuwafikisha huko mnapopataka.
Mtabiri huyo aliongea mengi na kila aliloliongea siku hiyo
liliweza kutokea moja baada ya jingine, lililokuwa limebakia ni hilo la
kupatikana kiongozi ….mfalme wa taifa teule…na pale alipotokea huyo malikia
mtarajiwa wakajua kuwa sasa , kile kipindi walichotabiriwa kimefika, kila mmoja
akawa na hamu ya kukifiki hicho kipindi.
Kwa wale wenye pupa….kwa wale walioona siku zinakwenda tu,
na huyo mtawala hapatikani, wakaanza kuzusha fitina,…na choko choko za hapa na
pale zikaanza kutokea, na hata baadhi ya sheria zikaanza kupindishwa. …na ukoo
mkubwa ukawa na haki kuliko ukoo mdogo, sheria ikawa inmsadia yule aliyenacho,
na asiye nacho akawa ananyang’anywa hata kile kidogo alichojaliwa…
Leo hii koo mbili hasimu zimekutana , sio hizo koo mbili tu,
hata zile zilizoonekana kama koo ndogo, zilizojengwa na familia hizo hizo,
zilifika, zilifika sehemu ile ile waliyosuluhishwa , sehemu ile ile
waliotabiriwa kuwa mfalme, atakuja, ….je ni kweli mfalme atatokea siku hiyo
kama ilivyotabiriwa.
********
Malikia hakuwa na jinsi tena, ilibidi akubali, akainuka pale
alipokuwa amekaa, na kunanza kutoka nje, huku akikanyaga maua, maua
yaliyodondohwa ardini kutoka hapo nyumbani hadi sehemu sehemu takatifu, sehemu
ambayo,atakabidhiwa majukumu ya umalikia, sehemu ambayo atakabidhiwa mume wake…..huenda
mume mpya.
Alipowaza hilo kuwa huenda atakabidhiwa mume mpya, akasita
kutembea, lakini kauli ya mzee, babu yake ikamsuta kuwa yeye hapo alipo sio
malikia wa ukoo huo peke yake, ni malikia wa koo zote, na huko anapokwenda
anakwenda kuwa mama wa taifa hilo….akajipa moyo..
‘Huenda nitamkuta mume wangu keshafika huko..’akasema na
kutabasamu, na moyoni akakumbuka kuwa siku hiyo hapo ni siku maalumu, siku ya
kuondokana na shida, siku ya kuomba shida zako, siku ambayo kila mtu anapata
neema, lakini huwezi kupata neema na baraka bila kuwa huru kwenye nfasi yako,
uondoe, chuki, uondoe husuda, uondoe uchoyo, uondoe akili ya kulipiza kisasi,
uondokane na kila baya, ujawe na upendo, na amani….
Akasafisha moyo, na kujenga tabasamu, na moyoni akajawa na
matumaini kuwa lolote linaweza kutokea, na sio kwa mapenzi yake, bali kwa yule
aliye na nguvu, ambaye ndiye aliyeumba kila kitu, hana mfano ….hana uzaifu
wowote wa kibadamu….mwenyezimungu, yeye alikuwa anajua hilo, …
Akaanza kutembea kutoka nje, akahesabu hatua moja, mbili,
tatu..nne,..mara akasikia sauti ya ndege, akakumbuka….mume wake aliwahi
kuwambia kuwa nudge huyo akilia ni ishara ya neema, baraka, na hutoke kweli, ….akasimama,
na kueguza uso wake kutafuta wapi hiyo sauti ya ndege imetokea, akajikuta
akikutana na miale ya jua linalozama…na kiwungi kikatanda, ….
Akakumbuka kuwa muda kama huo alitakiwa kuomba , alitakiwa
kulilia hali yake,….akaomba, kuwa anataka mume wake arejee, ili wawe naye
kwenye majukumu hayo mazito ya kuliongoza taifa kuwa taifa bora walilolitarajia wanachi wote…..
*********
Wakati hayo yakiendelea eneo hilo, mzee mteule, alikuwa kakaa
na kundi la wazee wenzake, ambao bado walikuwa na imani kuwa kijana wao
atakuja, na kila muda ulivyopita ndivyo kundi hilo la wazee lilivyozidi
kupungua, kwani wengine walishakata tamaa na wakajua kuwa kijana huyo hayupi
tena, na iliyobakia ni kusuburi huyo kijana mwingine, na yule aliyekata tamaa
akawa anatoa udhuru, anaondoka, wakabakia wazee wachache sana.
Wale wazee wachache wakawa wanaongea ili kupoteza muda na
kupena matumaini, na mmoja wao akasema;
‘Kama ni kijana wa mzee Hasim ndiye atakabidhiwa hayo
madaraka, basi nahisi mambo yatakuwa bado, nahisi kuwa siku sio leo, pengine
hili linatakiwa litokee mwakani, maana huyo kijana hana sifa zilizobashiriwa
siku ile’akasema mzee mmoja ambaye alikuwepo siku hiyo mtabiri alipoongea.
‘Mbona malikia ana sifa zote zilizobashiriwa, kwanini kwa
upande wa mfalme ishindikane…kuna tatizo hapa, inabidi tusubiri tuone, au
mnasemaje wenzangu?’ akasema mzee mwingine.
‘Mara nyingi mambo kama haya ya wanaume ni magumu kuingia
kwenye muafaka…ukizingatia huko tulipotoka, ujue kuwa kila ukoo unahisi huenda
huyo kijana atatokea sehemu ya ukoo wake. Ni kweli malikia keshapatikana,
lakini huenda pia asiwe ndio yeye, huenda kaletwa huyu kama majaribio tu, ili
tujindae kwa malikia mtarajiwa’akasema mzee mwingine.
‘Mimi sikubaliani na hilo, malikia mtarajiwa ndio huyu huyu,
tatizo ni mfalme,…kwasabaabu sifa zote za malikia mtarajia anazo huyo binti..je
hamjaona karama zake, kwa baraka zake amekuwa akiwasaidia watu, mimi mwenyewe
nilikuwa naumwa na kichwa, nilikuwa na matatizo ya kifamilia, mimi na mzee
mwenzangu mke wangu tulikuwa kama chui na paka, ….mnakumbuka nilivyotaabika,…lakini
siku tulipofika kwake, yote hayo yamekwisha…’akasema huyo mzee.
‘Kweli hata mimi….
Na wengi walitoa ushuhuda, kuwa huyo malikia aliweza mengi,mkono
wake ulijaa baraka, akikushika kichwa, kama kichwa kilikuwa kikikuuma,
kinapona, kama ulikuwa na msongo wa mawazo, yanayeyuka, na kama ulikuwa na
shida, inapungua au kuondoak kabisa….kila mtu aliamini kuwa huyo kweli ni
malikia matarajiwa.
‘Kama ndio yeye, mbona mume wake haonekani kuwa hivyo, na
huyo aliyekuwa ana sifa zinazokubalika tunahisi , kuwa kauwawa na mamba’akasema
mzee mwingine.
‘Hizo ni tuhuma,…hazina ukweli, tatizo ni kuwa tuhuma,na propaganda
potofu, zinatawala sana akili za mwanadamu. Kitu kidogo kikitokea,
kinachotangulizwa mbele na tuhuma, udaku na uzushi na propaganda potofu, …na
hili huchukuliwa kwa kasi kubwa sana, kuliko ukweli wenyewe wa jambo. Na huenda
hata ule ukweli ukija, unakuwa hauna nguvu tena, watu wanaweza hata wasiuamini!
‘Lakini haki, ukweli, ..vina nguvu, ni kama taa ndogo kwenye
giza nene, hata kama, dhuluma, uzushi utagubika dunia, lakini tunaamini kuwa
haki, ukweli utaleta nuru yake, hata kama miali yake itakuwa ni midogo,
kutokana na propaganda potofu, lakini bado, tutaona nuru yake,….kama unavyoona
nuru ya taa ndogo kwenye giza nene, haifichikia…’akasema Mzee Mteule ambaye
alikuwa muda wote kainama akiwa kwenye dimbwi la mawazo.
Aliinuka na kuangalia nje, na miali ya kuchwa kwa jua ikawa
inaonekana, ikammulika usoni…kuashiria sasa siku inakwisha, na usiku unataka
kuingia, na kwa mtizamo huo, ina maana wenzao wameshashinda, akakuna kichwa na
kugeuka kuwaangalia wenzake, akasema;
‘Kama imepangwa iwe hivyo, inabidi tukubali….kumbekeni kuwa
siku ya leo sio siku ya visasi, sio siku ya tamaa ni siku ya kupendana, na
kushirkiana, ….inabidi tutoke nje tukashirikiane na wenzetu, hata kama kijana
wetu hatatokea leo, lakini nina imani yupo njiani….twendeni nje tukaungane na
wenzetu..’akasema na akawa wa kwanza kuinua mguu kutoka nje,
Wenzake wakabakiwa wakiwa wameshangaa, hawakuamini hilo,
wakaona kuwa mwenzao keshakata tamaa na anataka kuwasaliti, wakasita kuinuka,
na mzee alipoona wenzake wamekaidi amri yake, kitu ambcaho hakijawahi kutokea,
akageuka kuwaangalia, na usoni akatoa tabasamu na kusema;
‘Hamkumbuki jamani, kuwa siku kama ya leo, hatutakiwi kuwa
na visasi, kinyongo, husuda na uchoyo,…siku kama ya leo inatakiwa tuwe na upendo
, kushirikiana na kusahau tofauti zetu, ili kama una matatizo, una shida,
unaumwa, uweze kupona,…kweli sisi hatuna hayo…kama kweli hatuna hayo huenda yameshatatuliwa,
lakini hili la kumsubiri kijana wetu hatulioni kuwa ni tatizo…’akasema
Wenzake waliposikia hivyo, kwanza waliangaliana, na wote
wakatingisha kichwa, na bila kusema neno wakainuka, na kwa pamoja wakaanza
kutembea kuelekea nje wakiinua miguu yao kuanza kutoka, kwenda kukutana na
wenzao huko nje, na hatua zao zilikuwa kama zile na askari, yaani kuinua mguu
kwa pamoja na kushusha kwa pamoja na walipohesabu hatua tatu ya nne, sauti ya
ndege ikasikaka kwa nje..
Ilikuwa sauti ya yule ndege, ndege wanayemuamini kuwa akitoa
sauti hiyo anaashiria neema,…kila mmoja akageuza kichwa, kuangalia upande huo
wa machweo ya jua ,wakajikuta wanamulikwa na miali ya jua linalokuchwa….kila
mmoja akawa na hamasa ya kumona kijana , mfalame mtarajiwa akitokea huko, kwani
ishara zote zimeshakamilika, sasa kwanini mfalme mtarajiwa asitokee…
Wazee wale wakaanza kutembea kuelekea sehemu ya makutano ili
kukutana na wenzao, na walipokaribia sehemu hiyo, wakasikia sauti tena ya yule
ndege, na safari hii sauti hiyo iliongezewa na sauti nyingine ya kutoka kwenye
mdomo wa binadamu, wote wakageuka kuangalia huko sauti ilipotokea,
Kiwingu kikatanda, kwani miali ile ilizibwa, na kikundi cha
watu waliokuwa wakija kutokea huko kunapochwea jua….watu kwa pamoja kwanza wakatoa
macho yao kuelekea huko, kutizama ni nani huyo, na baadaye wakakumbuka, na kila
mmoja akaihini na kuanza kulilia shida yake moyoni, na mojawapo ni kupta
mtawala bora, kupata taifa bora, taifa teule, walilolitarajia…..
NB: Sijui nimeandika kile nilichokusudia, kwani sikupata
muda wa kukupitia tena….lakini naona ipo pouwa, mnasemaje?.
WAZO LA LEO: Najua kila mmoja ana imani yake na anamuamini mungu wake, ...hata hivyo kuomba kwa mungu huyo unayemuamini hakuna tofauti. Ila ili
tufanikiwe katika maombi yetu, kwani kila mmoja ana shida, kila mmoja ana
tatizo lake, lakini ili tufanikiwe katika maombi yetu, kwanza tusafishe mioyo
yetu, tuondoke uchafu uliogubika mioyo yetu, ya chuki, husuda, uchoyo, ubinafsi….na
kuzijaza mioyo yetu kwa upendo, na huruma,…na kila lililojema,..na hapo
tukiomba kwa mola wetu,..tutafanikiwa.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment