Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, May 20, 2011

Dunia ya leo sio ile ya jana



Wakati napita kwenye shamba moja lenye miti , niliona kitu cha ajabu sana, nikakumbuka ile hadithi na juha, lakini hii sio hadithi, hii ni kweli, nikapikicha macho yangu kuhakikisha kuwa hili nionalo ni kweli au naota, au nakumbuka kichwani ile hadithi ya juha.
‘Halooh hapo juu ya mti, mbona unafanya kitu cha hatari..wewe huoni kuwa hiyo ni hatari..’ nikamwambia yule jamaa
‘Hatari gani wewe, hebu pita la lako maana nyie watu mna midomo mibaya mnaweza kumfanya mtu  kweli akadhurika kiukweli’ akasema yule jamaa huku akiendelea kukata lile tawi.
 ‘Nakushauri hivi, kaa upande huo wa shina, wakati unakat hilo tawi maana ulivyokaa hivyo, tawi likianza kukatika utaanguka nalo…’ nikamwambia.
‘Hahahahah…wewe wafikiri kazi hii nimeianza leo, huu ni mwaka wa kumi tano, na utaalamu wangu ni huu, huu wa kukata miti, naitwa kukata matawi yaliyohatarini, kama haya, hapa kinachohijika ni `timing’ tu…likifikia mahala fulani mbio naelekea upande wa shinani….sina wasiwasi na kazi yangu..’ akasema huku anaendelea kukata tawi.
 Hutaamini niliyoona, jamaa alikuwa akikata tawi la mti halafu amekalia kule ambapo likianguka anaanguka nalo, hana wasiwasi anasema anajua kazi yake. Nikacheka na kusema kumbe majuha wapo wengi, kwanini uweke rehani maisha yako kwa kitu kama kile, kuwa umzoefu na tawi likiaanza kukatika utakimbilia upende wa shinani, je likikuwahi utamlaumu nani…wakati nasema haya nikasikia mlioo wa tatatata….hilo tawi likiaanza kuvunjika, nikageuka haraka nione uzoefu wa yule jama…wapi, ikawa purukushani, …
Loooh, toba walahi, nilimuiona jamaa akielea hewani na lile tawi huku akihangaika kushika tawi ambalo lilikuwa likielea hewani nay eye….duuuuh! Bahati nzuri jamaa akadondokea kwenye jalala lilo na majani mengi hakuumia sana. Nikamsogelea kumpa pole kama anahitaji msaada nimsaidie.
‘Wewe nuksi kweli…haijawahi kutokea tangu nianze kazi hii ya kukata miti…wewe umesema nitazurika, nitaanguka na tawi na kweli imetokea hivyo…ina maana wewe unaweza ukasema nitakufa na kweli nikafa..ondoka katika upeo wa macho yangu kabla sijakumaliza na hili panga…nuksi mkubwa wewe’ akainuka na kunionyeshea panga, ikabidi kweli nikimbie maana jamaa alishapandisha hasira.
 Wakati nawaza tukio hili huku natembea nikiwa na wasiwasi jamaa asije akawa anakuja kwa nyuma mara nikawaona vijana watano wamejificha kichakani, na nilivyowaona wakajifanya hawanijali, walikuwa wakivuta bangi, na mmoja kashikilia sindani ya kujidunga…oooh, nikashituka nikataka kuwasemesha , lakini wakajifanya hawanisikii, wao waliendelea na kazi yao kama vile hawanioni,  nikajisemea mwenyewe  moyoni kumbe majuha wapo wengi, yule alikuwa akikata tawi huku kalikalia huyu anakata nguvu za mwili wake na kuumaliza uhai wa maisha yake huku anajiona…kumbe wapo wengi hawa, nikajisema mwenyewe.
 Ama kweli, kila mji una juha wake na mchimba kisima huingia mwenyewe, maana  maisha yetu yalivyo, kila mmoja ana njia yake ya kuumaliza uhai wake  mwenyewe, na mbaya zaidi kwa mikono yake mwanyewe. Huyu anavuta sigara kama gari moshi, yule anavuta bangi, yule anakula madawa ya kulevya, yule mzinzi na musherati…ilimradi kila mmoja ana bididii ya kumaliza uhai wa maisha yake mwenyewe, ole wako umkanye…! Umesikia wale wanasiasa wanalalamika pale wanapoonywa kuhusu udhaifu na utendaji wao, au wale wanaofisidi dhamana waliyopewa, …nini kitakachofuata kama sio kuja juu, na hata kutoa vitisho, hebu angalia sasa hivi shida ya usafiri ilivyo, tatizo sugu au tuseme donda ndugu la mgawo wa umeme…jamani ina maana tunashindwa kujua kuwa  tufanyacho ni sawa na kulikata tawi huku umelikalia…angalieni sana dunia inavyobadilika, dunia ya leo sio ile ya zamani…
Huu ndio ujumbe wangu wa Ijumaa ya leo. 

Ni mimi: emu-three

3 comments :

Anonymous said...

Tunasubiri muendelezo wa stori bwana, haya usemayo ni kweli lakini siunajua kwamba Tanzanian ,they are sleeping!

EDNA said...

Asante M3 kwa ujumbe mzuri siku hii leo.

Simon Kitururu said...

Bonge la Ujumbe Mkuu!