Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Tuesday, February 23, 2010

Mama wa Kambo

                                            Na kisa cha Msamaria mwema

Tukio hili linanikumbusha ile hadithi ya nani kama mama, ipo siku tutaimalizia;-


Ilikuwa saa tano za usiku, wakati tunajiandaa kulala, mara tukasikia hodi nje! Kwa muda kama huo hodi inaashiria mawili jema au baya. Ingawaje sauti ya huyo mtu aliyepiga hodi haikuwa ngeni kwangu, ilikuwa sauti ya kike, na ili tuwe na uhakika vyema, tukauliza `ni nani wewe?’

‘Mimi jamani, mama nani hii huielewi sauti yangu’ Nikamuangalia mwenzangu kuwa kweli ana uhakika na mpiga hodi. Mama nanihii akamtambua na kuelekea huko nje. Maongezi yao yalichukua muda mrefu mpaka nikaingiwa na wasiwas,i huenda huyo mgeni ana masahibu makubwa na alihitaji msaada wetu! Nikaona nami nitoke nje nikasikie mwenyewe. Nilipotaka kutoka nje, mara mama nanihii akaniita toka dirishani, nikabaki nimeduwaa, vipi tena ya kuongelewa dirishani, tena upande mwingine wa nyumba, ina maana haya mazungumzo hayakutakiwa huyo mgeni ayasikie?

‘Hapa kuna mtihani, huyu mama anasema ndugu zake wamemfukuza, na hana pa kulala, sasa mimi naona nikaongee na hao ndugu zake, kwasababu hao ndugu zake ni jirani zetu, tukimlaza huyu mama hapa watatuelewaje, Na ya Mungu Mengi, huwezi jua la kutokea’ Nikaduwaa kusikia hivyo, mtoto anamfukuza mama yake!

Baada ya muda mama nanihii akarejea kuwa mtoto wa huyu mama hataki kusikia kuhusu huyo mama.Mimi nkaona niende mwenyewe kuonana na huyo mtoto wa huyu mama na hadithi ikawa ile ile, na mengi waliyosema, yaani binti wa huyu mama na mumewe yalinitia wasiwasi, kuwa huyu mama anapenda kunywa, na akinywa ni mkorofi na isitoshe yeye ana ndugu zake wengine kwanini ang’ang’anie hapo. Nikawauliza sasa mimi nifanyeje kwasababu kaja kwangu na anahitaji msaada wa kujistiri huu usiku,na sio ubinadmu kumfukuza, yeye ataenda kulala wapi saa hizi. Jibu likawa nimfukuze atajua pa kulala!

Niliporejea na kuongea na mwezangu tukaona si jambo jema kumlaza huyu mama hapa kwetu bila taratibu za msingi. Wakati nawaza haya nikaikumbuka kisa kimoja cha msamaria mwema, jamaa iliyeamua kutenda wema kwa kumuhifadhi mke wa mtu ambaye aligombana na mumewe. Na katika ugomvi huo, mume mtu akamfukuza mkewe, usiku wa manane. Mke huyu ikabidi akimbilie kwa jirani kuomba hifadhi.

Jirani aliyegongewa, akashindwa afanyeje usiku kama huo na kwa mjumbe ni mbali kidogo, wakaona, huyo mke-wa- mtu alale hapo hadi asubuhi, na mapema waende kwa mjumbe. Wakampa huduma zote chumba na kupata chochote na baadaye wakaagana kuwa kesho asubuhi wadamkie kwa mjumbe ili kuondoa shari, na pili kusuluhisha hilo tatizo kwani kama huyu mume mtu atagundua kuwa wao wamemuhifadhi hapo itazua mtafaruku mwingine!

Asubuhi na mapema baba mtu akawahi kwa mjumba na kumwambia mkewe amuamushe mke- wa -mtu, ili ajiandae vyema, na waje huko kwa mjumbe. Mkewe akakubali akijua kuwa wanawake wanahitaji maandalizi ya asubuhi sio kama wanaume. Na mumewe alipoondoka, mkewe akamgongea mwenzake ili aamuke na kujiandaa, akaona kimya. Akagonga kiasi cha muda, na kudhani huenda huyo mgeni kwasababu ya uchomvu, kalala sana, kimya…!Akaona ampe muda kidogo huku yeye akijiandaa na kufanya kazi ndogondogo.Baadaye akagonga tena kimya...!

Kule kwa mjumbe baba mtu alifanya kazi ya ziada kumwamsha mjumbe, siunajua tena asubuhi na mapema, na kazi za ujumbe ni wito, pamoja ya kuchoka na shughuli za mchana kutwa ilibidi mjumbe aamuke tu huku akilalamika lakini kwa vile amekubali majukumu ikabidi amsikilize mtu wa shina lake. Baada ya maelezo ikabidi mjumbe amuendee msaidizi wake na wazee wengine , halafu mmoja akatumwa nyumbani kwa mume-wa- mtu ili aje naye kwa mashauri ya usuluhishi!

Huku nyuma mama-msamaria mwema akawa kachanganyikiwa kwanini mgeni wao haamuki licha ya kugonga kote huko. Mwishowe, akaamua ampigie simu mumewe kumueleza kuwa mgeni wao bado kalala, na licha ya kugonga kote haamuki. Ikabidi mjumbe aambiwe na wote wakaamua wafuatane hadi kwa msamaria mwema. Walipofika hali ikawa ile ile. Mjumbe na wazee wakashauri mlango uvunjwe, kwasababu ulikuwa umefungwa kwa ndani.

Kumbuka kuwa mume-wa- mtu alishaitwa kwa mjumbe na alishangaa alipofika kwa mjumbe anaambiwa asubiri kwani mjumbe katoka kidogo na kumbuka kuwa walioleta shauri hili walitaka isijulikane kuwa huyo mke-mtu kalala kwao. Yule mume-wa- mtu alisubiri kiasi cha kukata tamaa na akaamua arudi nyumnani kwake. Njiani akaamua apitie njia ya kwa rafiki yake ambapo mkewe alihifadhiwa,lakini alikuwa hajui kuwa kahifadhiwa hapo. Aliona kuwa ndio njia ya mkato ili afike kwake haraka. Alipofika karibu na nyumba ya huyu rafiki yake akakuta watu kadhaa wamesimama nje, akashangaa , akasema moyoni huenda jirani kapatwa na matatizo ni heri afike aulize kwani ujirani ni kusaidiana.

***********

Naona muda niliolipia intenet café umeisha, tutaendelea siku nyingine. Tubakie na kujiuliza maswali haya yafutayo:

-Je mimi nilikubali huyu mama alale  kwangu, na kama nilikubali ilitokeaje

-Je ni masahibu gani yaliyowakuta wasamaria wema kwa kumhifadhi huyo mke wa mtu. Kuna mafundisho ndani ya kisa hiki naomba tuwe pamoja kama hutajali
From miram3

1 comment :

Anonymous said...

Ukikubali umekwenda kwako, kama si tapeli anaweza akakufia, kwanza jiulize kwanini wamemfukuza