Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Tuesday, May 27, 2025

NIANZAJE

Mambo ya kuandika yapo mengi, visa vipo vingi na matukio halikadhalika, lakini nashindwa nianzaje...Nianzeje, najiuliza

Wakati nawaza hivyo, mara nikasikia binti mmoja anaongea kwa hasira, akimfokea mtu mnzima, huyo mtu kwa jinsi alivyojieleza ana miaka sitini na kitu...

'Wewe binti mimi nina miaka sitini na....kukushika kwa kutaka usogee ndio unanikaripia hivyo
'Kwanini unishike, kwanini usiniambie tu wataka kupita
'Ningekuambia huenda usingelijua kuwa ni wewe....nimekushika...'
'Aaah, nyie wazee hamna adabu, kushika shika tu wanawake...
'Hata nikikushika kuna ubaya gani, au wataka ushikwe na mume wako tu
'Achana na mimi wewe mzee
'Au kwa vile wewe ni mnzungu....'
Nahisi alitumia neno hilo mnzungu kwa vile yule binti ni zeruzeru (matatizo ya ngozi)
Abiria wengi walikaa kimia,...ni asubuhi kila mtu anawazia kuwahi kazini na kwa muda ule ilishafika saa mbili hivi
 Nikiwa nimezama kwenye mawazo mara nikahisi mtu aliyekaa karibu ya anakuwa kama anatoa sauti ya kulia, nikageuka kumuangalia....
Ni yule mdada, zeru zeru....kainamisha kichwa sasa anafuta machozi....nilijua labda kakerwa na yule abiria aliyemshika

'Usijali dada...kwenye gari haya yanatokea....'nikasema
'Mhh....wakati mwingine watu wanataka washushiwe hasira zilizojificha....'akasema
'Polee...na samaahni..'nikasema nikihisi nimemkwaza
'Pole na samahani ya nini...?' akauliza na kunigeukia sasa akitabasamu...

 
Ni mimi: emu-three

No comments :