NIMLILIE NANI....
Nilishika shavu, nikiwa nimeinamisha kichwa chini, kichwa kikiwa karibu ya magoti...nilikuwa hivyo kwa muda, baadae nikainua kichwa kujaribu kuangalia mbele, macho hayakuweza kuona,...macho bado yalikuwa yakilengwa lengwa na machozi, Lakini machozi hayakuweza kutoka tena...moyoni nilishaapa sitalia tena.....
'Sitalia......inatosha....basi...'
Nilijaribu kugeuza kichwa kushoto na kulia...japo ni kwa shida maana shingo ilikuwa kama imekakamaa...kiukweli sikuweza kuona kitu, zaidi ya ukungu, sio ukungu wa hali ya hewa, nahisi ni ukungu wa macho yangu...
Nilihisi mwili kuishiwa nguvu....moyo kwenda kasi, na kichwa kikazidi kuuma, sasa kikiuma kwa kasi zaidi,....ghafla...giza likanijia, na hatimaye ....
'Vipi kaamuka...?
Ilikuwa sauti ya kwanza kuisikia baada ya kupoteza fahamu, nahisi nilipoteza fahamu, au,...sina uhakika!
'Nahisi hivyo, japo hajafumbua macho...'sauti nyingine ikasema
'Usimsumbue kwanza, ngoja nikamuite docta..,usiondoke hapo,....'sauti nyingine ikasema
Hapo nikajitahidi kufumbua macho....
'Sitalia......inatosha....basi...'
Nilijaribu kugeuza kichwa kushoto na kulia...japo ni kwa shida maana shingo ilikuwa kama imekakamaa...kiukweli sikuweza kuona kitu, zaidi ya ukungu, sio ukungu wa hali ya hewa, nahisi ni ukungu wa macho yangu...
Nilihisi mwili kuishiwa nguvu....moyo kwenda kasi, na kichwa kikazidi kuuma, sasa kikiuma kwa kasi zaidi,....ghafla...giza likanijia, na hatimaye ....
'Vipi kaamuka...?
Ilikuwa sauti ya kwanza kuisikia baada ya kupoteza fahamu, nahisi nilipoteza fahamu, au,...sina uhakika!
'Nahisi hivyo, japo hajafumbua macho...'sauti nyingine ikasema
'Usimsumbue kwanza, ngoja nikamuite docta..,usiondoke hapo,....'sauti nyingine ikasema
Hapo nikajitahidi kufumbua macho....
No comments:
Post a Comment
Changia hoja kwa kutoa maoni yako hapa: Au tuma kwa e-mail> miram3.com@gmail.com