Wakati mke na mume wanaingia kwenye
mtihani ulisababishwa na kauli y a mume kuulizia kama mke wake anamfahamu huyo
mama aliyeonekana huko nje, mwanamke wa ajabu, mke yeye alitaharuki kwa kuona
kuwa mume anajali jambo jingine kuliko tatizo la ndugu yake.
Na wakatii wapo kwenye majibazano, mara
simu ikalia, na hiyo ikaleta amani,
Tuendelee na kisa chetu…
*******
Simu ile ikavunja
sintofahamu iliyoanza kujitokeza, na wote wakainamia ile simu kuona mpigaji ni
nani,....ilikuwa namba mpya kwenye simu ya huyo mume , kwani haikuonyesha jina
la mpigaji, na mke kuona hivyo, akampa mume simu yake ili aipokee;
‘Haya pokea maana hiyo namba haina jina, labda ni simu zako,
….’akasema mke na mume akachukua simu,
kwanza akaipokea na kuuliza;
‘Habari , ni nani mwenzangu…?’ akauliza mume huku anamuangalia mke
wake, mke wake alikuwa kainama, lakini huku katega sikio, akiombea kuwa simu
hio itoke huko mjini, lakini hata ikiwa inatoka mjini mbona sio namba ya mdogo
wake, hapo akili ikamtuma kuwa huenda ni namba miongoni mwa namba za mabosi wa
mdogo wake, na kitakachofuata hapo ni kauli kuwa mdogo wake amefungwa.
Mume akasikiliza mpigaji, akitoa sauti, na alipogundua kuwa
mpigaji wa hiyo simu sio miongoni mwa watu wake, akamsogelea mke wake,
huku akiweka sauti ya juu ili mwenzake
asikie
‘Shameji ni mimi, simu yangu imeharibika, ilidondoka wakati
nimetaharuki nilipoambiwa nahitajika kuwajibia baada ya tukio lililotokea hapa
hospitalini…na ilipodondoka, ilizimika kabisa, nimepeleka kwa fundi, hii
nimeazima tu kwa muda….’akasema
‘Haya tuambie kuna nini kinachoendelea huko, kwani ilikuwaje…?’
akauliza mume mtu kwenye simu akiwa kaiweka kwa suti ili mkewe naye asikie
anachoongea mdogo wake,
‘Shemeji kuna tatizo limetokea huku hospitalini na kisa kirefu
sizani kama nitaweza kukusimulia tukio zima kwenye simu, …kwa jinsi ilivyo
imefikia maafikiano ambayo yanahitajia mawazo yenu, ila mimi nimekubali kuwajibika
kama walivyoamua, na kuwajibika kwangu kunawagusa na nyie, na nimeamua hivyo
nikijua kuwa hata nyie mtakubaliana na uamuzi wangu huo…’akasema
‘Sawa tunakusikiliza…’akasema shemeji mtu akimuangalia mke wake
kama ana lolote la kusema, lakini mkewe alikuwa kimia naye akisikiliza
anachoongea mdogo wake.
Na kabla mdogo mtu hajaongea, mara kwa nje wakasikia kelele zile zile za
watoto.
‘Mbona kuna kelele kuna hapo nyumbani…’akauliza mpigaji wa simu,
na kweli kelele hizo ziliwafanya hata hawa wanaopkea simu wasiweze kusikia
anachoongea mpigaji wa simu, na kumfanya mume mtu kuchungulia dirishani huku kakukunja
uso, maana kelele zao, ziliwafanya, washindwe kusikia vyema anachoongea shemeji
yake huyo…
‘Kuna kelele za watoto hapa nje, zinafanya tushindwe kukusikiliza
vyema hebu ongea kwa sauti…..’akasema huku akimuashiria mke wake awafukuze hao
watoto huko nje, lakini dada mtu hakutaka kuondoka karibu na simu, alitaka
kujua, au kusikia kauli ya mdogo wake kuwa yupo salama au yupo jela.
‘Ni hivi kwa vile hili tatizo limefikia sehemu kidogo ya maafikiano
, na maafikiano hayo ni sehemu tu ya tatizo lenyewe, na hayo maafikiano yanawagusa
na nyie, ….ndio tukaona tuje huko, ili tuongee vyema…’akasema.
‘Mje…mnakuja na nani….mnakuja na nani…?’ akauliza shemeji mtu
akiwa na wasiwasi.
‘Msiwe na wasiwasi ndugu zangu….’akasema na kukawa na kukatika
katika kwa mawasiliano na shemeji mtu akasema;
‘Kwa kifupi unataka kutuambia kuwa matatizo yaliyotokea huko
yamekwisha kikazi, au sasa hivi upo wapi sijui, …unachotaka kusema ni kuwa
unatakiwa kuja huku kuongea na sisi ili tukubaliane na maamuzi hayo kidogo
mliyokubaliana nayo, kama ni kukuwekea dhamana au….. ?’ akaulizwa
‘Matatizo ya kazi hayajaisha, kwa vile kosa limeshatokea, na
sijajua kiukweli hatima yake ni nini…..na sijui kuhusu kazi…, ila hili ninalotaka kuja kuongea nanyi ni
muhimu kabla kesi haijasikilizwa, kuna kikao kitakaliwa kuliongelea, hata kabla
ya kesi yenyewe ..’kelele zikazidi tena nje
‘Kwanini uwajibike kwanza kabla kesi haijasikilizwa, huoni kwamba
wanakuonea, utawajibikaje kabla ya hukumu, na hicho kikao ni cha nini, kama
kuna kesi tena,…hapo sisi hatujaelewa..?’ akauliza
‘Kutokana na kosa lenyewe…ni lazima polisi wahusike, ..kwahiyo
kikao ni kazini, na kesi ni mahakamani,…kifupi tatizo halijapatiwa ufumbuzi…bado uchunguzi
unafanyika…’akasema
‘Lakini hujashikwa na polisi,….?’ Akauliza
‘Mhh, ndugu zanguni,…. kuna jambo jingine ni muhimu lazima lifanyika,
na kwa vile mimi ndiye niliyesabaisha hayo yote, nikatakiwa kubeba dhamana hiyo
huku uchunguzu ukiendelea, na hilo ndilo limeniokoa nisiende polisi kwa hivi
sasa hadi hapo uchunguzi utakapokamilika, na nikawa sina jinsi,, imebidi
nikubali, kwa vile nahisi pia ndugu zangu tutasaidiana kwa hilo, tutaliongelea
nikija huko…’akasema
‘Mhh, bado unatuweka roho juu, maana hatujajua tatizo ni nini, na
bado unasema kuwa umewajibishwa, ..kuna kesi , kuna uchunguzi,…sasa sisi hapo
tutatoa msaada gani, haya huko kuja kwako unakuja lini….?’ Akauliza
‘Shemeji msiwe na wasiwasi na hilo, ….kuna kikao kitakaliwa
kulijadili hilo kiofisi, ili kufikia hatima yake kuhusu ajira yangu, lakini
swala la kipolisi inategemea uchunguzi wao, siwezi kuelewa itakuwaje, ….’akasema
na kelele zikaanza tena, safari hii shuyu mwanamume hakutaka kusikiliza zaidi
akasimama huku bado simu ipo sikioni na kwenda mlangoni, akafungua mlango ….
Alipofungua mlango akajikuta anaangaliana na mwanamama aliyekuwa
kajifunika uso, na yule mama alipoona mlango umefunguliwa tu, akafunika kabisa
usoni, na kauli yake ilikuwa;
‘Namtaka mtoto wangu…’akasema, kauli ile ikadakiwa na watoto
wakisema hivyo hivyo, na kelele hizo zikamfanya huyu mwanaume amkumbuke yule
mwanamke wa ajabu, huku kwenye simu shemeji mu anaendelea kuongea
Kutokana na ile hali ya mshituko kumuona huyo mwanamke na huku
shemeji ake anaongea na mkewe yupo nyuma akitaka kusikiliza akaona hataelewa
vyema akasema;
‘Sasa sikiliza shemeji, usiwe na shaka, kwa vile wanataka kukaa kikao kulijadili hilo, wewe subiri kwanza, usijiweke roho juu, kwani huna hatia, kutokana na maelezo uliyotupa, hilo lingetokea kwa yoyote…sidhani kwamba wao watachukua hatua kama hiyo ya kukufukuza kazi…na polisi watategemea maamuzi ya kazini kwako, kazini kwako wakiona huna hatia sizani kama polisi watashinikiza kuwa una kosa….’ Akasema.
‘Ndugu zanguni, polisi ni polisi,…na kosa lenyewe sio dogo, kwahiyo hata kama kazini watasema sina kosa, ..je kuna ufumbuzi gani wa tukio lenyewe,…tunachoombea ni uchnguzi ulipatie ufumbuzi hilo tukio kwa haraka…na ikipita muda mrafu, sizani kama nitakuwa na kazi…..’akasema, na maneno hayo ya mwisho yalimshitua sana mke wake.
Mke mtu alifikiria mbali hali yao na wazazi wake ambao walishaona kuwa binti yao huyo atawasaidia kwa vile ana kazi, wao walishapata ahueni, kuwa mshahara anaopta huyo ndugu yake unawasaidia na wazazi wake, kwani wao kipato chao wanachopata ni kidogo, wasingeliweza kuwasaidia wazazi wake, sasa mdogo mtu ndio huyo kafukuzwa kazi, na huenda kutahitajika chochote ili kuizima hiyo keso, watapatia wapi pesa…
Mke wake akamshika mumewe bega, na mume mtu akageuka kumuangalia mkewe na alichoona machoni kwa mkewe ni machozi, hali hii hakuweza kuivumilia, na kabla hajajibu alichoulizwa kwenye simu, kwani mpigaji simu aliuliza swali;
‘Kwani siku hizi kuna shule ya watoto hapo karibu….’akaulizwa kwenye simu na shemeji mtu, akawa anaondoa mkono toka mlangoni, alipokuwa kashikilia, nia yake ilikuwa amfute machozi mkewe, lakini mkewe akawa keshageukia upande mwingine.
Mkewe alimuonea huruma mume wake, kwani anajua kipato chao, anajua jinsi gani mumewe anavyohangaika usiku na mchana kuhakikisha wanakula,…lakini kwa upande mwingina akwa anamkumbuka mama yake alivyoteseka kumlea, akakumbuka enzi mama yake bado mama, hjazeeka, akiwa kambeba mgongoni, hapo akaanza kulia huku akisema;
‘Nani kama mama,…sasa mama nani atawasaidia, baba naye ndiye haishi kuumwa…wakisikia binti yao kafukuzwa kazi wataumia sana,…ooh, hili sasa litamzidishia mumewe wangu mzigo mnzito asioweza kuubeba. Hapo bika kujua akamshika mume wake begani kama kumonea huruma, na alipoona mumewe kageuka, akajigeuza haraka upande mwingine ili sione machozi yaliyokwisha kujaa machoni.
‘Ni watoto tu sijui wametoka wapi na kuna…..’akasema huku anageuka kuangalia nje, pale alipoona mkewe kageukia upande mwingine na alipogauka tu kuangalia nje, akakutana na kauli kutoka kwa mwanamama aliyekuwa kajifunika usoni, akisema ;
‘Na-na-mtaka mtoto wangu…’
‘Mtoto gani….?’ Akauliza huyu mwanaume, na huko kwenye simu akasikia sauti ikisema;
‘Mtoto wa kiume…’shemeji mtu akasema.
‘Na-nataka mtoto wangu, watoto wakajibu kwa shangwe…na akawa kama kachanganyikiwa, maana huku shemeji yupo kwenye simu, huku huyo mwanamke wa ajabu anadai mtoto wake…sijui ni mtoto gani, akasema kumjibu shemeji yake;
‘Nilikuwa naongea na hawa watu huku, ….unasema..?’ akauliza na huku kelele zikizidi na kukawa hakuna maelewano mazuri, maana sauti zawatoto nje, zikawa zimezidi, na baba mwenye nyumba akaona ni kero akampa mkewe simu aendelee kuongea na ndugu yake, na mkewe alipoishika ile simu kwa Bahati mbaya akawa kashika kitufe cha kuzimia simu, bila kukusudia simu ikawa imezima kukawa hakuna mawasiliano hata alipoweka sikioni hakusikia kitu.
Akaiangalia huku akionyesha mshangao, akasema;
‘Mbona hakuna mawasiliano…’akasema na mumewe kwa muda huo alishatoka nje, mke mtu akajaribu kuipiga ile namba kwanza ikasema unayempigia anaongea, na alipopiga tena ikawa haipatikani.
Mume wake kwa hasira akawa katoka nje, kuwatimua hawo watoto na alipotoka nje, hakumuona yule mama, waliokuwepo hapo ni watoto wakipigana, na wenzao wakiwashanglia na kuwashibakia waendelee kupigana,…ikabidi kuingilia kati kuwaamulia hao watoto wanaopigana.
‘Hivi nyie watoto mnatoka wapi, na kwanini mnakuwa hamna adabu…angalia sasa mnapigana mumeumizana..mnataak niwachape…?’akasema akimuona mtoto mmojawapo aliyekuwa akipigana akitoka damu puani.
‘Ni huyu hapa mchokozi, ….’akasema yule aliyemuumiza mwenzake.
‘Ndio umuumize mwenzako kiasi hichoo..’akasema
‘Kanianza yeye mwenyewe ..’akasema kujitetea
‘Haya wewe njoo hapa niambieni kwanini mnapiagana..’akasema akimuita yule aliyeumizwa,.
Wale watoto wakaanza kujielezea, kuwa walikuwa wakimsogelea huyo mama kuitikia wimbo, na huyo mwenzake akawa anamvuta shati kwa nyuma alipomuuliza kwanini anafanya hivyo, akapigwa teke nay eye akajibisha, na ndipo wakaanza kupigana.
‘Kwanini mnataka kumuona huyo mama, hamuoni kuwa mnamsumbua huyo mama wa watu, na huyo mama yupo wapi , anatokea wapi…?’ akajikuta anauliza maswali mengi, akigeuka huku na kule kuangalia kama anaweza kumuona huyo mama, na ghafla wale watoto wakaondoka mbio, hata wale walikuwa wakipigana wote wakawafuatia wenzao huko walikokimbilia, na sauti ya huo wimbo wa aina yake ukawa unasikika kwa mbali;
‘Na-na-mtaka mtoto wangu…’
Huyu mwanaume akawa anawaza sana kuhusu huo wimbo au sijui ni kibwagizo kina maana gani;
‘Mbona wimbo na kauli ya huyo mama vinafanana,…eti anataka mtoto wake, mtoto gani huyo….?’ Akawa anajiuliza, huku akirudi ndani na alimkuta mke wake akiwa kashikilia simu, na machoni alionekana han raha;
‘Mke wangu vipi, ulikuwa unalai, sasa unalia nini tena..?’ akasema
‘Wewe hujiu tu mume wangu, kama wamemfukuza mdogo wangu kazi , wale wazee wangu watalelewa na nani. Mdogo wangu alipopata kazi, ilikuwa furaha kwetu, baada ya kujitolea kumsomesha, akawa ndiye tegemeo la wazee wangu, unaona jinsi gani wazee wangu walivyochoka, mazao hakuna, unafikiri hali yao itakuwaje, na mimi nakuonea huruma wewe mume wangu maana unabeba jukumu kubwa zaidi ya uwezo wako, je kipato tunachopata kitaweza kuwasaidia na wazee wangu….’akasema
‘Mke wangu yote ni kudra ya mungu,..na sioni kwanini ufikie hatua hiyo ya kulia na kukata tamaa, hawajasema kuwa shemeji kafukuzwa kazi, kwani bado wanachunguza, na kama alivyosema shemeji ndio hivyo nilivyoelewa mimi, atarudishwa kazi tu…’akasema
‘Kama ni wakurudishwa kazi, kwanini asema anakuja huku, kwanini kuna uchunguzi wa polisi, ina maana kuna ….kasababisha kifo au,..na kama ni hivyo mpaka uchunguzi ukamilike, ni miaka, nijuavyo mimi, kwahiyo hapo hana kazi, ndio maana anakuja huku kuishi nasi hapa tena,…si ndio maana yake…’akasema mkewe.
‘Kasema kuna jambo anataka kuja kujadiliana nasi, ambalo wamekubaliana huko, ….na ni muhimu, hatujui ni jambo gani, cha muhimu tuvute subira mpaka akifika, ..na sijui anakuja lini, akifika tutajua la kufanya, hayo mengine tumuachie mungu,.usianze kujitwika mzigo kabla haujatua kichwani...’akasema mume mtu.
‘Haya mume wangu nimekuelewa,….’akasema akimkabidhi mumewe simu yake, na mumewe akataka kupiga kuongea na shemeji yake tena ili apate ufafanuzi, lakini mkewe akasema;
‘Unataka kuwapigia tena?’ akauliza mkewe, akitaka kumuambia kuwa kajaribu kupiga lakini hapatikani tena huyo ndugu yake.
‘Ndio ili niweze kuelewa vyema, hawa watoto wameleta zogo hapo nje, wamefikia hadi kupigana, na kuumizana, sijui kuna nini hapa mtaani leo, ….’akasema
‘Nahisi ni huyo mama nilyekuambia mchana, nahisi ndiye huyo huyo watoto wanamfuatilia anapoimba huo wimbo wa ajabu..’akasema
‘Ndiye huyo alikuwa kalala hapo upenuni mwa nyumba yetu?’ akauliza mumewe akonyesha mshangao.
‘Unasema alilala hapo upenuni mwa nyumba yetu?’ akauliza mkewe akionyesha hamsa na mshangao, uso ukimeta meta kama kasikia jambo la furaha.
‘Ndio…sijui ndiye huyo unayemzungumzia au yupo mwingine, ila ….mmmh, sijui sijawahi kuona ….mmh, kwani unajua anatokea wapi..’akawa anaongea mume matu akionyesha kama kushangaa.
‘Atakuwa huyo huyo, hakuna anayejua katokea wapi, na kila mmoja anaongea lake, na kuna kauli kuwa ni mama wa kutoka mbinguni, kaja kuleta neema, na akifika kwako ujiandae kupokea neema…’akasema na mumewe akajizuia kucheka akatabasamu na kusema;
‘Akifika kwako kwa vipi, mtu mwenyewe anadai kuwa anataka mtoto wake… kama analeta neema mbona mwenyewe hana neema, ….achana na imani hizo’akasema
‘Huo ndio wimbo wake, kuwa anataka mtoto wake, na akisema hivyo na wewe unatakiwa kuitikia, usipoitikia utaikosa hiyo neema, ulitakiwa na wewe uitikie hivyo hivyo….’akasema
‘Niitikie vipi…?’ akauliza mumewe huku akionyesha uso wa kushangaa.
‘Anavyoimba yeye, hayo maneno,…na-nataka mtoto wangu, na wewe unaitikia hivyo hivyo. Na mume mtu akajikuta akiitikia, kama kuyafuatilia yale maneno
‘Na-na-na taka mtoto wangu….ndio unapata neema ukiitikia hivyo’akasema na kutabasamu, na mkewe naye akatabasamu kwa mara ya kwanza tangu itokee hiyo sintofahamu siku hiyo, na kabla hawajaendelea kuongea mara wakaisikia mngurumo wa gari ukikaribia hapo kwao, na wote wakatega sikio.
‘Nasikia kama mngurumo wa gari….’akasema mke mtu
‘Yah, …labda kuna mtu kakosea njia, sijui huku anafuata nini,…..’akasema akielekea dirishani kuangalia nje na mara gari likafika na kusimama nje ya nyumba yao, wakajikuta wanandoa hawa wakiangaliana
‘Mhh, tatizo..nenda wewe…sio polisi hao,’akasema mke mtu
‘Kwani unajua ni akina nani,polisi, kwanini, ooh, siwezi kujipeleka tu, subiri kwanza….’akasema mume mtu na mara mlango ukagongwa
NB: Ni nani hao....kuna nini ? tuwepo pamoja
WAZO LA LEO: Kila ukila na kulala kwa starehe, kumbuka kuna ambao hawajapata chakula, hawana cha kula, na hata usingizi hawaupati kwasababu ya njaa. Kila ukiendesha gari lako kwa furaha, huku ukiongea na simu yako kuwalekeza wafanyakazi wako wa nyumbani cha kufanya ukumbuke kuna ambao wanatembea mwendo mrefu kwa miguu, miguuni wamevaa ndala zilizochakaa, wapo kwenye jua kali, kutafuta angalau tonge moja la kupoteza nja, wanatembea mwendo mrefu kutafuta tiba, kutafuta maji, kutafuta….angalau na wao waweze kuishi maisha bora...kwao ni ndoto.
Kila ukihangaika kutafuta shule gani ya kimataifa ya kuwapeleka watoto wako, bila kujali gharama kubwa ukumbuke kuna watoto wanakalia mchanga, wanaogombea kitabu kimoja, hawana walimu,…wansoma huku wanapiga miayo ya njaa, ambao mwisho wa siku wanapambanishwa na watoto wako wanaosomea shule za kifahari, ili kupata mtoto aliyefanya vizuri kitaifa.
Ukumbuke kuwa, pesa ulizofisidi, pesa uliyokwepesha kulipa kodi,....hizo zinatokana na jasho la hao wanyonge…ambao leo hii wanateseka wao na watoto wao, Tujue na tukumbuke kuwa na wao wana haki sawa kama ulivyo wewe na watoto wako.
Ni mimi: emu-three
No comments:
Post a Comment
Changia hoja kwa kutoa maoni yako hapa: Au tuma kwa e-mail> miram3.com@gmail.com