Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, October 11, 2018

CHOZI LA KUTOKA MOYONI-2


‘Ndugu yangu liogope chozi la kutoka moyoni…hili ni chozi la huzuni, chozi la majuto, chozi la kukosewa, chozi la kulalamika…huwezi kulitafsiri, maana linakuja tu..na huja kwa jambo maalumu sio hivi hivi tu..kwa aliyezoea kulia, …hili sio chozi lake..’aliendelea kunihadhithia rafiki yangu.

Hiki ni kisa cha kweli kilichonitokea mimi na familia yangu...’akasema huyo rafiki yangu anayenisimulia kisa hiki....

‘Unajua mimi sikupenda kuyahadithia haya, lakini nataka mlione chozi la namna hii linavyofanya kazi yake maana sio chozi la kawaida,…na  nakuhadithia hiki kisa, sio kwa nia ya kuwalaumu hao walionitelekeza, huenda walifanya hivyo kwa nia ya jinsi walivyoona ni sahihi kwao, ila maamuzi hayo yalitoka kipindi ambacho niliwahitajia sana…maana nilitarajia mengi  baada ya kuwafanyia kazi zao kwa kujitoa kwa moyo wangu wote, na nini walikuja kunilipa sasa,…

'Malipo yangu ndio hayo kuwa mimi sihitajiki tena....'akasema

'Pole sana...'nikamwambia 

‘Yote namuachia mungu…’akasema na kutulia.

'Hebu sasa niambie kwa kirefu, ilikuwaje kwenye hiyo kampuni hadi ikafikia hapo...?' nikamuuliza

Tuendelee na kisa chetu...

*************

 Kwa kuhadithia tu, mimi nilianza kufanya kazi kwenye kampuni hiyo, ikiwa na mapungufu mengi tu, na waliniita hapo kwa vile walisikia kuwa mimi ni mtaalamu kwenye hiyo idara ...ni kweli na nilipofika hapo na kuyaona hayo mapungufu, nikaamua kutumia ujuzi wangu na uzoefu wangu kuhakikisha kila kitu kinakuwa sawa…na nilifanya hivyo nikijua huenda huko mbele kutakuwa na neema. Hayo ndio yalikuwa matarajio yangu.

Katika kuwajibika huko, niliweza kuokoa mamilioni ya pesa, pesa hizo hazikuwa zimejulikana, kutokana na mahesabu yao  na kumbukumbu zao, kutokuwa sawasawa, na bosi aliposikia hivyo alifurahi sana, nikajua labda tutapewa kifuta jasho (bonasi,..lakini haikutokea, sikukata tamaa, nikajua ipo siku.

Kazi zikaendelea, lakini kutokana na hali halisi ya mabadiliko, ya kinchi, nisema hivyo... ambayo sio kwa kampuni hiyo peke yake tu,…biashara haikuwa nzuri sana, kwahiyo kukawa sasa na tetesi kuwa huenda watu wakapunguzwa, mimi sikuwa na wasiwasi na hilo..., maana kama niliweza kuokoa mamilioni ya pesa, kwanini kampuni inipunguze mimi.

Ndio maana baada ya kupata taarifa hiyo, niliumia sana, niliumia kwa vile nilishafika mahali nikawa napanga maisha, nakopa huku na kule ili watoto wasome,..najua mwisho wa mwezi nitapata fungu langu, japokuwa lilikuwa lapatikana kwa nusu nusu...lakini unakuwa na uhakika hata ukikopa utakuja kulipa.. Sikujali, nilijua ndio hali halisi…

 Sasa kilichoniuma zaidi ni pale nilipopigiwa mahesabu ya nini nilipwe,..hapo ndio unaweza kuona jinsi gani haya makampuni ya watu binafasi yalivyo na dhuluma...

‘Wewe mwenyewe unaifahamu hali halisi, kwanza nilikuwa sijakuajiri, kweli si kweli... ulikuwa kama kibarua tu,…kwahiyo kutokana na hali halisi,...sipendi, unaonaee..nifaneje sasa, na sitaki uondoke mikono mitupu, etu usubiria mpaka nikijaliwa, lini sasa..kwahiyo mimi nimeona hivi.. tutapiga mahesabu yako ya mwezi huu…umefanya siku ngapi vile…’akajifanya kama hajui. Mimi nikabakia kimia.

‘Eeeh mwezi uliopita umelipwa pesa yako yote…?’ akauliza kama vile hajui hilo

‘Bado, …nimelipwa nusu mwezi…’nikasema kwa sauti ya unyonge, nimeshavunjika nguvu, nilikua kwa juhudi zangu nilizofanya, angalau...ningelipewa hata asante

‘Ok, sasa..tutachukua hiyo nusu mwezi ilibakia na tutaongeza na siku hizi za mwezi huu ulizofanya, tutakulipa,…nitahakikishe umelipwa hizo pesa zako, sitaki uondoke mikono mitupu…’akasema

‘Ina maana, ndio malipo hayo ya  mwisho…?’ nikauliza

‘Wewe mwenyewe si unaona hali halisi, nitakulipa nini, shukuru kuwa mimi nitafanya juhudi upate hizo…nusu mshahara uliobakia, na siku hizi za mwezi huu ulizowahi kufanya..na..kiukweli sikutegemea kuwa kazii hii itachukua muda wote huu, mimi nilitarajia utafanya miezi mitatu, ..tumalizane…’akasema

Sikutaka kusema lolote kuwa kama ningefanya hivyo anavyodai yeye, asingeliweza kuyapata hayo mamilioni ya pesa, nikabakia kimia, nikiumia kimoyo moyo..

‘Nitamwambia mshika pesa wangu akupigia mehesabu yako, na akulipe, lakini hakikisha kazi zako zote ulizotakiwa kufanya umemaliza…najua sina shaka na wewe, lakini kwa kukumbushia tu, sitaki mtu aondoke hapa kabla hajamaliza kazi zake,..na nitakulipa baada ya kukaguliwa kuwa kweli umemaliza kazi zako…’akasema

Sikuamini hayo maneno, ina maana kafikia sehemu ya kutokuniamini tena…moyoni nilitaka kumuambia, kama ungelinijua nilivyo, usingelisema maneno hayo, hata kama unaniondoa mimi nitafanya kazi yako yote…kimujibu wa taaluma yangu, ..ndivyo nilivyo, sina haja ya kuwa na kisasi na yeye.

Yaliyofuata hapo baadae huwezi amini, nilioanza kuonekana kama mtu ambaye naweza kuharibu kazi, naweza kuiba, naweza kufanya jambo na kukimbia,…sikuamini…

Haya ngoja turudi siku ile…ambayo, nilitakiwa nirejee nyumbani, nikutane na muuza duka,..siku ya kulipa ada..siku ya…mke wangu anategemea nitakuja na mkopo, ili aweze hata kuanzisha duka,…siku ambayo nilipewa hiyo taarifa kuwa kazi sasa basi.

*************
Siku ile naikumbuka sana, kwani ni siku ambayo….nilianza hata kuumwa maradhi ya moyo…

Wakati naondoka kazini, nilipanga nisipitie njia ile ya dukani, kama nitawahi kufika, kama nitafika maduka yamefungwa itakwua ahueni kwangu…na hata hivyo huko kwa dukani nikipita salama, nitakwenda kusema nini kwa familia yangu…kiukweli nilikuwa na wakati mgumu sana.

 Siku ile…, pamoja ya kutoka kazini kwa muda ule ule wa saa kumi na moja, cha ajabu siku ile usafiri ukawa ni rahisi,…hakukuwa na wingi wa abiria, nikapata gari, japo la kusimama, mwili hauna nguvu, lakini utafanya nini..tumbo halina kitu, ningelikula nini, wakati bajeti imebana.

 Cha ajabu siku hiyo nikafika nyumbani mapema sana, tofauti na siku nyingine…akilini nawaza nikifika nitaanzaje kumwambia mke wangu…mawazo hayo yakawa sasa ndio yameuteka ubongo wangu…unajua mkiwa mnaishi pamoja, unajau ni kitu gani uongee na mwenzako kwa wakati gani,…nilimpenda mke wangu na familia yangu sikupenda kabisa ije kuumia, nipo tayari kufa kwa ajili ya famili yangu.

Kwa jinsi nilivyotekwa na mawazo hayo ..ya jinsi gani ya kufikisha ujumbe huo kwa familia yangu,…, nilisahau kabisa lile wazo la kupitia sehemu nyingine kumkwepa mwenye duka, maana njia ya kufika nyumbani ni lazima upitie kwenye hilo duka, lakini kuna njia nyingine ya kuzunguka…wakati natoka kazini, nilipanga nipitie njia ya kuzunguka…lengo ku mkwepa huyo muuza duka.

Ndugu yangu, sio kwamba mimi ni muoga kiasi hicho, ila kiukweli huyo jamaa sifa zake za ukatili, zinajulikana sana, kwanza alikuwa jambazi, na…sio kwamba natania, ipo siku moja alishikwa mwizi, ..kwa macho yangu nilimuona jamaa huyu akionyesha unyama wake kwa huyo mwizi, aliyetaka kuvunja duka lake ili aweze kuiba, ilikuwa alifajiri mimi nawahi kazini

Walikuwa wawili mmoja akaweza kuponyoka na kukimbia, sasa huyu aliyeshikwa, ambaye alijiona ni mbabe, ndiye alikutana uso kwa uso na huyu muuza duka,…mwizi alikuwa mtu kashiba, ana miraba minne, na akaamza kukabiliana na huyu muuza duka, lakini hakuweza.

‘Huyu niachieni mimi mwenyewe, nataka niwaonyeshe kuwa mimi siibiwi..na hakuna atakyefanya hivi hapa tena….sitaki utani mbele ya mali yangu…’akasema, kwanza alikuwa na kisu akakurusha pembeni.

Mwizi kuona hivyo, akajua huyo muuza duka ni rahisi kwake, ,…wakaanza kutupiana ngumi na huyu mwizi kwanza mwizi alionekana kumzidi muuza duka, lakini hakuna aliyeingilia,..watu walikuwa wamesimama  pembeni.

‘Ukinishinda, umepona, ..nikikushinda umekufa….’akasema huyo muuza duka, kifua wazi, na bukuta la kulalia…bukta lake lina sehemu ya kuhifadhia kisu –ala.

Ikawa kila mwizi akipatwa na konde moja usoni, anabwagika chini,…anajizoa hara haraka, kawa sasa kama kalewa… watu wakawa wanacheka…mwizi gani kila ngumi anakwenda chini…lakini mwizi akawa anapmbana akijua ndio kupona kwake, kufa au kupona…

 Ikatokea wakati mwizi akarusha ngumi, mkono ukadakwa na huyo muiza duka, kwa jinsi alivyoshikwa tulisikia mlio wa kooo….mkono ukavunjwa na hapo hapo, huyo mwizi akarushwa hewani, alizungushwa hewani kama mzigo tu, na kubamizwa chini, na watu walishangaa huyu mtu ana nguvu gani ya kuweza kumbinua huyu mwizi hewani, mwizi ambaye kiumbile anamzidi huyo muuza duka…ilibakia historia.

‘Mimi sina huruma na pesa yangu,…pesa yangu ina thamani ya utu, ukinichukulia pesa yangu, umevunja utu wangu na mimi sitakuwa na huruma na utu wako..nitakumaliza tu…hilo nimeapa, sasa wewe  mwizi utakuwa fundisho hapa mtaani, nitakuonyesha kile ambacho watu hawakijui kunihusu mimi…’akasema

Huyo mwizi anagugumia mkono umevunjwa, muuza duka akawa bado hajaridhika,…akasogea pale alipoweka kisu chake, akakichukua mwizi hata hawezi kuinuka, kukimbia, ..muuza duka akamrejea na kumshika huyo mwizi sikio akalikata sikio…

‘Hiyo kwanza ndio alama yako kuwa wewe ni mwizi, mimi nilikuwa jambazi, na jaambazi ukikamatwa ujue ni kifo, sasa mimi nimeacha, sitaki kuibiwa tena, wewe wataka nirejee kwenye wizi…’akasema

Na hapo hapo akakitumbukiza kile kipande cha sikio mdomoni akakitafuna..sasa sijui atakimeza au la,… kwa haraka ageuka kwa kasi ya ajabu, kile kisu, kikapita kooni kwa huyo mwizi, damu zikaruka,…

‘Aaah…’ mwizi akapiga ukelele.

Tukajua koromeo limekatika…bahati mbaya kisu hicho kilkwepa koromeo, kikakata sehemu ya koo … lakini kilifanya kazi yake ..mwizi yule akalala chini, anakoroma kama mtu anayekata roho.

‘Hufwi eeh,..umechafua kisu changu halafu hujafa… ngoja nikuone kama hutakufa…’jamaa akaingia dukani, na kuchukua chupa ya mafuta ya taa…mimi hapo  sikuweza kuvumilia tena…huyo, nikaondoka zangu kuwahi kazini..

 Nilipokumbuka hayo, nikajua huyu mtu hana mzaha kweli kwenye pesa yake, na kweli kwa maana kwa yoyote eliyewahi kumkopa akachelewa kumlipa pesa yake cha moto alikiona.., kwanza akija kwako utapokea  kipigo, na kipigo hicho yeye mwenyewe anakuruhusu upigane naye, halafu anachukua kitu chochote ambacho kinaweza kulipa deni lake,..

Sasa sijui mimi yatanikuta hayo au….kwahiyo sio kwamba niliingiwa na wasiwasi huo bure… jamaa huyo ana visa vingi, akipigana na mtu,..ngumi yake ikikupata lazima utaenda chini, yeye anadai, alishaambiwa asitumie mkono wake kupiga mtu, hasa wa kushoto..alishawahi kumvunja kaka yake mkubwa wake taya, kwenye ugomvi ugomvi

*********

Sasa ghafla bin vuu,..nikawa nipo maeneo  ya duka…nilishasahau, kuwa nilipanaga nitumie njia nyingine ili kumkwepa huyo muuza duka, ..mawazo ni kitu kingine kabisa, na ilipangwa tu , lazima nipitie hapo dukaniu.
.
 Nilipofika hapo , nikawa sina jinsi, nikasema moyoni potelea mbali, mungu atanilinda, nikasogea pale dukani, …sikumuona huyo jamaa, yupo kijana wake, ajabu mara nyingi huyu jamaa hamuamini mtu, nikajua labda yupo chooni, ..hata hivyo nikasema  afadhali.

Nilisema afadhali, ..sio kuwa nitakuwa namkwepa hivyo kila siku, nilikuwa na maana nahitajia kwanza nifike nyumbani,…, nipate muda wa kujipanga, jinsi gani ya kukabiliana naye,..najua ni lazima nionane naye ..hata hivyo akili ilikuwa imechoka sana..nilihitajia nikalale kidogo hadi kesho .

'Bosi wako yupo wapi…?’ nikamuuliza hapo kwa kujiamini kidogo.

'Katoka hapa sasa hivi…, anasema anawafuatilia wadeni wake, kakasirika kweli kweli…’akasema huyo kijana wake.

'Mungu wangu...'nikasema hivyo tu kuondoka pale dukani kwa haraka…, nikikimbilia nyumbani kwangu sio mbali sana na hapo dukani,…na hisia zangu, ni kuwa huenda familia yangu ipo chini ya ulinzi ya huyo jamaa au keshawafanyia kitu kibaya. Pamoja na kumuogopa hivyo, kama atakuwa kaifanyia kitu kibaya familia yangu, tutapambana…

Nafika eneo la nyumba yangu, nasikia sauti ya jamaa akifoka huko ndani, nikajua sasa..kumekucha, sasa naingia vitani, japokuwa nafahamu fika kupambana na huyo mtu siwezi lakini nitajitahidi …

Na kwa namna nyingine nikaona labda kuepusha shari, ni bora nirudi nilipotoka, nikakae sehemu hadi usiku ndio nirudi, lakini je hapo alipo hajafanya chochote kibaya, ikawa ndio wasiwasi wangu huo..

Nikawa sasa natamani nigeuke nirudi nilipotoka, na kabla sijafanya lolote la maamuzi yangu, mara mlango ukafunguliwa,  jamaa huyo katoka. Akaniona, au sijui hakuniona maana kilichofuata baadae ilikuwa ndio jibu halisi…

 Alipojitokeza pale malngoni, uso umebadilika kawa mweusi, …jicho limemtoka nikajua sasa napambana na simba…kurudi nyuma siwezi, kusogea mbele siwezi nikawa nimeganda, nasubiria kitakachofanyika

Jamaa huyu anakuja usawa wangu, nikawa nimejiandaa, huku moyoni nasema, kiukweli ilibidi iwe hivyo, kumuomba mungu, maana sikupenda iwe shari..,…

‘Mungu wangu nisaidie kwa hili, haya yote sio kwa kusudio langu. Je mimi sikutimiza wajibu wangu kazini,.., je mimi nimefanya dhambi gani hadi niondolewe kazini, nimefanya kosa gani hadi nije kuzalilika hivi…najua kabisa ningelikuwa kazini, haya yasingelitokea…naomba msaada wako, ewe mola wangu…’nilijikuta nasema hivyo tu, kwa hisia za ndani,..sijui ila nahisi ilikuja hali ya chozi kama lile la ofisini

Nilishangaa….mimi sina kawaida ya kutoa machozi…na niliona ajabu tukio hilo liniathiri kiasi hicho,…najiona nipo kwenye mabadiliko mengine makubwa.

Basi kwa muda jamaa alishafika usawa wangu…nikitarajia kipigo, najua nitajitetea, lakini najua kiundani siwezi kupambana na mtu kama huyo…

Ajabu kabisa jamaa akanipita kama hanioni,…upepo tu, nikayumba… sikuamini hilo…karibu anipige kikumbo, huyooo kwa haraka akawa anaondoka…

Mimi ilinijia kwa mshangao, sikumini kabisa kama jamaa huyo angeliliweza kunipita bila kufanya jambo, bila hata kunifokea…kwa vile sikuamini, taratibu  nikageuka kwa mashaka, kumuangalia kama kweli ndio anaondoka,...

Ile nageuka, kumbe naye sijui alikuwa akiwaza nini, naye kumbe akagauke, tukawa tumeangaliana, lakini kwa umbeli, alishanipita na kwa vile alikuwa akitembea kwa haraka ilikuwa ni umbali wa hatua kadhaa,..hapo ndio sijui, alikuwa hajaniona au..na kwanini alipogeuka alikuwa akainiangalia kama kushangaa vile…na alipogeuka tulikutanisha macho.
.
Hakusimama na wala hakurudi nyuma…

Ilipita dakika mbili hivi bado nimesimama, na akili iliporejea kwenye msimamo wake, ndio nikakumbuka kuingia ndani kuiona familia yangu…nikatembea kwa hatua za haraka haraka, kawaida nikifika nyumbani nagonga mlango kupiga hodi..

Sikufanya hivyo….nikasita kufanya hivyo, nikajikuta nasita hata kushika kitasa…nahisi mwili ukinisisimuka, …ni hali ngeni kwangu..hata hivyo, nikashika kitasa na kuzungusha , mlango ukawa wazi..

Ile natupa macho ndani, naangalia sakafuni, namuona mke wangu…na mtoto kasimam akiwa kainamisha kichwa…

NB….ILIKUWAJE…Ndugu zangu, nahis kama nisipopata kitendea kazi, kisa hiki na hicho kingine kitechelewa kidogo maana sehemu niliyoitegemea , nilipokuwa nimejishikiza sitakuwepo tena…mniombee tu, nipate sehemu nyingine.


WAZO LA LEO: Yakikukuta matatizo, shida , mitihani, kamwe usikate tamaa, wewe elekeza imani yako kwa mwenyezimungu, kwani yeye anatosha kukuongoza na kukusaidia kwenye hatua nyingine.
Ni mimi: emu-three

2 comments :

Anonymous said...

UPO WAPI NDUGU YANGU

Anonymous said...

Kama umeshindwa endeleza niuzie hii blog...