‘…Jana asubuhi uliponiona ulionekana kama
unashtuka,..kweli si kweli kwanini ulikuwa unashutuka, si ina maana hukutegemea
kuniona nikiwa hai, au sio… au unajifanya hujui mlichokipanga wewe na kaka
yako, vinginevyo uniambie ukweli…mlipanga nini wewe na kaka yako,…?’
nikamuuliza hapo kwa ukali…
‘Shemeji hapana, hatujapanga kitu kama hicho, na wala sielewi
kwanini kaka alifanya hivyo....kwanini tupange kuku-ua shemeji, mimi nakujali
sana, kuwepo kwako ni muhimu sana kwangu…, ’akalalamika huku akishika kichwa
akionyesha masikitiko.
‘Sasa mimi nimeamua, nichukue hatua, nakuambia wewe kwa vile kaka
yako ni mgonjwa, na kwa vile wewe ni mzima, na inaonekana mpo shirika, basi
wewe utaisaidia polisi ili ukweli uweze kupatikana,…kwasababu mimi nimeyavumilia
haya mambo mpaka watu wananiona mimi ni mjinga…’nikasema na mara simu yangu
ikaita
Shemeji akawa ananiangalia kwa mashaka, akihisi labda ni polisi
wananipigia na nilipoitizama hiyo namba nikaona ni ya yule mpigaji
asiyejulikana, nikaiweka hewani na kusema;
‘Niambie…?’ nikasema
‘Polisi wananitafuta sana ili niongee nao, na naogopa nitaongea
nao kabla sijakutana mimi na wewe, nahisi ni wewe umewaambia, sasa litakalo
tokea mimi sina lawama …’akasema
‘Sasa kwanini huongei nao, mimi siwezi kukulaumu, kama una
ushahidi huo kawape polisi, si una uhakika nao, kwanini unaogopa kuwaopatia
polis, lakini kama nia yako ni kupata masilahi, kwangu hupati kitu…’nikasema
‘Tatizo wewe hujui kitu gani nilicho nacho,..sawa…kama unasema
hivyo, sawa, lakini namuonea sana mume wako huruma, na zaidi nashangaa kwanini
mke wake hana huruma naye, huyo akienda jela atafia huko, ndio unalolitaka au
sio…’akasema
‘Hayo ni maneno yako na hisia zako, hayawezi kubadili sheria za
nchi…’nikasema
‘Unajua madamu, mimi nilitarajia leo ningewakabidhi kila kitu, ili
mjua wenyewe jinsi gani ya kufanya, lakini mpaka sasa naona muda unakwisha
tu..sipati marejesho…’akasema
‘Marejesho gani, kutoka kwngu, mimi na wewe tulikubaliana kitu
gani, wewe ulisema tukutane unionyeshe huo ushahidi, mara eeh, unatafutwa na
polis, kumbe na wewe ni mhalifu unatafutwa na polis, eeh, sasa kajisalimishe
huko na huo ushahidi wako…’nikasema
‘Mimi nimeongea na mume wako nikamuelezea yote , na pamoja anadai
kuwa hakumbuki, lakini ushahidi kidogo niliomuonyesha kakiri kuwa yupo
matatani, hata kama anaumwa,…na kasema nimuachie huo ushahidi, akasema kuna mtu
atamtuma,…ili nimkabidhi…’akasema
‘Sawa kama mumeongea na mume wangu basi mtamalizana naye, mimi
sihitaji sana kuongea na wewe, kwani msimamo wangu ni ule ule, na huyo mtu ni
nani..?’ nikamuuliza sasa nikimtupia macho shemeji yangu akawa ananiangalia kwa
mashaka.
‘Anamfahamu yeye mwenyewe huyo mume wako…’akasema
‘Alishawahi kutumwa kwako kabla, au umesahau kuwa wewe ulikuwa
tarishi wa marehemu, ….au sio..’nikasema
‘Sawa tuyaache hayo, ila nilifanya hivyo kwa manufaa yenu, kama
umefikia kunidharau hivyo, basi mimi nitawakabidhi polisi, itakwua usumbufu
kwako mkurugenzi mnzima ukishitakiwa wewe na mume wako, maana huo ushahidi
unaonyesha kama nyie wawili mlishirikiana …’akasema
‘Kwa vipi…?’ nikauliza
‘Yeye alifika akamaliza kazi, na wewe ukaja kuhakikisha,..bahati
mbaya wewe ukakamatwa, lakini mume wako bado yupo mafichoni, kwa maana ya kuwa
polis bado hawajamtambua, …wameshatambua hilo, ila wanahitajia ushahdi zaidi na
shahidi muhimu ambaye ni mimi…’akasema
‘Sawa nimekuelewa sasa unataka nini..?’ nikauliza na mara yeye akakata
simu.
************
Niligeuka kumuangalia shemeji yangu aliyekuwa akisikiliza kwa
makini, akasema
‘Nahisi ni….nilijua ni polisi..’akasema
‘Ni mtu wenu huyo…nahisi kaka yako alitarajia kukutuma kwake
kumpelekea pesa ili asitoe ushahidi kuwa kaka yako anahusika kwenye mauaji ya
Makabrasha, na inaonekana kazi yako ndio hiyo ya kutumwa na kaka yako, au
sio….’nikasema
‘Sasa shemeji ngoja mimi niondoke…’akasema
‘Nimekuambiaje..maana hata ukiondoka sasa hivi utakutana na polis
njiani, ..’nikasema
‘Kwani mimi nina kosa gani…?’ akauliza na kabla sijamjibu simu
ikapigwa tena
‘Hebu subiri kuna huyu tena anapiga simu…’nikasema na kuipokea
hiyo simu, ilikuwa namba ambayo sijaiweka kwenye kumbukukumbu zangu.
‘Halloh nani mwenzangu..?’ nikauliza
‘Ni mimi yule mtoto wa marehemu…nilikuwa nauliza kama upo tayari
ya kikao chetu, ni kesho au sio…?’ akauliza na kabla sijamjibu akaendelea
kuongea
‘Japokuwa baba mdogo, nikiwa na maana mumeo kalazwa, lakini sizani
kama hilo litasumbua kitu au sio maana tulishaongea iliyokuwa imebakia ni sisi
kurejesha maelezo kutoka kwa mawakili wetu..je kesho upo tayari..?’ alikuwa
Yule mtoto wa Marehemu ambaye ni kiongozi wa familia.
‘Mimi sina shida ya hicho kikao , ila msimamo wangu ni ule ule, je
mumeupata ule mkataba wa zamani…?’ nikauliza
‘Hilo ni tatizo madam , hatujaweza kuupata huo mkataba unaosema ni
wa zamani.., ni kama vile haupo..’akasema
‘Sasa tutajadili nini, iliyobakia ni mimi nifuate sheria, ili
ijulikane kabisa kuwa mkataba huo mlio nao ni wa kugushi..’nikasema
‘Mimi nataka kuondoka, na ..natarajia kukaa na familia yangu, ili
majukumu yote niyaache kwa huyo msaidizi wangu siwezi kuendelea
kusubiria…’akasema
‘Mimi sina shaka, yoyote Yule nipo tayari kukabiliana naye,
ilimradi tu, huo mkataba wa awali uwepo..’nikasema
‘Kiukweli madamu, kwa hilo, itakuwa ni vigumu sana, maana wakili
wetu amefanya jitihada zote ameshindwa kuupata huo mkataba unaosema ni wa
zamani, sasa tufanyeje..?’ akaniuliza
‘Hilo ni swali ambali unatakiwa umuulize wakili wenu au
sio..’nikasema
‘Yeye kashauri hivi, wewe
ukubaliane na huu mkataba tulio nao sasa, maana swala sio kuufuata, swala ni
kuhakikisha kuwa haupo tena, na kuufuta ni lazima taratibu za kisheria
zifuatwe…umeliona hilo…’akasema
‘Kwangu mimi siwezi kufanya hivyo, huo mkataba siutambui, na najua
dhumuni la hayo yote, kwahiyo msimamo wangu bado ni huo huo…’nikasema
‘Basi hilo nitawaachia nyie mpambane na huyo msaidizi wangu… ,
kiukweli siwezi kuendelea kusubiria tena, hata mama naye anataka kurudi huko
kijijini, akahangaike na shughuli zake,…, ngoja nikae na wanafamilia, ili hili jambo
sasa liwe bayana kwa wanafamilia wote, kitu ambacho sikukipendelea, unajua kila
mmoja anamtizamo wake…’akasema
‘Hilo ni juu yenu nyie kama wanafamilia..ila ninacho kushauri,
hata mkikaa na wanafamilia usije kuwaficha kuwa huo mkataba ni batili,
unasikia..vinginevyo, hata kama utakwenda huko unapokwenda, ujue unaweza kuitwa
kama shahidi kwenye kesi nitakayoiwakilisha mahakamani…’nikasema
‘Sawa..ngoja tuone, nitakujulisha baada ya kikao cha wanafamilia..’akasema
na kabla hajakata simu nikasema ;
‘Nikuulize kitu, ulisema wewe kwenye ile video ya matukio kwenye
ofisi ya Makabrasha uliona Yule aliyemuua baba yako, au sio..?’ nikamuuliza
‘Sikumuona, nilikuambia sura haikuonekana,..alitokeza kichwa tu,
na kichwani alivaa kitu kama soksi, ya kuziba uso na kichwa kizima akaacha
macho na pua..’akasema
‘Na wakati anamlenga marehemu risasi, mume wangu alikuwa amekaa
mbele ya huyo marehemu au sio, sambamba, au sio ,..?’ nikauliza
‘Ndio walikuwa wamekaa wawili mmoja huku na mwingine kule, meza
imewatenganisha, kama ilivyo kwenye ofisi…sio sambamba ya kukinga..lakini
walikuwa wanaangaliana na huyo mpigaji alipiga risasi akiwa mlangoni, akimlenga
marehemu, naelewa unachotaka kukisema hapo, kuwa labda isingeliwezekana mtu akiwa mlango
kumlenga marehemu…angalia mlango ulipo, na meza ilipo, na muuaji ana shabaha..’akasema
‘Kwahiyo kwa vyovyote vile, kutokana na huo ushahidi mume wangu
hawezi kuhusika na hayo mauaji au sio…?’ nikamuuliza
‘Hawezi kuhusika,..hao ni polisi wanatapa tapa tu, nimelisikia
hilo, kuwa wao wana ushahidi wa kutosha kuwa mume wako kahusika, ni waongo..au
kama wana ushahidi mwingine mimi siujui..ila nilio nao ndio huo, na kama mume
wako angelihusika mimi mwenyewe ningehakikisha anakwenda kuhukumiwa…’akasema
‘Kwanini sasa hutaki kuwaonyesha polisi huo ushahidi ulio nao wewe…?’
nikauliza
‘Kwasababu utamtia hatiani mume wako kwa jinsi unavyoonekana , kwa
namna moja au nyingine, ataonekana anahusika, ama kwa kushirikiana na hao watu,
au kujua ukweli halafu akauficha, halafu nimeshachelewa kufanya hivyo,
nikifanya sasa unajua ni nini kitatokea,
its too late! …’akasema
‘Lakini kwenye maelezo yako ya mwanzo hukusema hivyo…’nikasema
‘Nilisemaje..?’ nikauliza
‘Ulisema hutaki kuonyesha huo ushahidi kwa polisi kwa vile
unaogopa kuwa polisi watajua kuwa mume wangu alikuwepo kwenye hicho chumba
kwahiyo atashukiwa,..ni kitu kama hicho..’nikasema
‘Ndio,… hiyo pia ni sababu moja wapo, na hilo la kuwa mume wako
alionekana hapo ofisini, bado halina nguvu, hakuna mtu wa kulithibitsha hilo,
…’akasema
‘Una uhakika na hilo kuwa hakuna mtu anayefahamu kuwa mume wangu
alikuwepo huko…?’ nikauliza
‘Aaah, uhakika gani, mimi nilijaribu kuulizia, hata mpelelezi
wangu alijaribu kufanya uchunguzi , hakuna mtu aliyewahi kumuona mume wako hapo
kwenye hilo jengo, pili hospitali wanatambua kuwa mume wako alikuwa mgonjwa,
alilazwa, na hali yake isingeliwezesha yeye kufika huko..’akasema
‘Sawa nashukuru..’nikasema na kukata simu.
Nikageuka kumuanga shemeji
yangu , na alionekana akitabasamu kidogo
‘Umefurahi nini..?’ nikamuuliza
‘Nimesikia kama umesema kaka hahusiki, ni kweli itakuwaje, mtu
alilazwa hospitalini angeliwezaje kufika huko…’akasema
‘Wewe ungeliweza kumsaidia, wewe si jembe lake..wewe si anakutuma
mara kwa mara kumfanyia kazi zake…’nikasema
‘Nini ..!!’ akasema akionyesha mshtuko
‘Wewe sio jembe lake, wewe si ndio anakutuma mara kwa mara, na
akitaka kufanya jambo anakuita wewe, je siku hiyo sio wewe aliyekuita ukampeleka
huko, ..?’ nikauliza
‘Wapimwishowe nimeona ni muhimu kuwafahamisha watu wa usalama, ili
baadae nisije kualaumiwa,unaona, ..wao wanakuja, ..sijui kwanini hawajafika mpaka
muda huu, na wewe watakiwa kuonana na kaka yako…’nikasema
‘Shemeji, kwanza nimeshachelewa, kaka atakuwa ananiulizia
huko…’akasema
‘Huwezi kuondoka, mpaka uonane na polisi,…acha akupigie simu, na
polis watajua jinsi gani ya kumjibu, wanajua kuwa kaka yako yupoje...kwani
wakati anakutuma, ilikuwaje, alikupigia simu au..?’nikauliza
‘Mimi sijui lakini yeye alinipigia simu niende hospitalini, kuna
kitu anataka kunigaiza, ndio nilipofika akaniagiza nije kuvichukua hivyo
vitu…’akasema
‘Ni kimojawapo ni mkataba, au sio mkataba ambao bado anahangaika
nao, mkataba wa kugushi, mkataba ambao utampa mamlaka ya kumiliki mali ili na
wewe ufaidike au sio?…yeye anafikiria kuwa huo mkataba utamsaidia..na kingine
ni nini alichokuagizia…?’ nikauliza
‘Ni hizi nyaraka tu za ofisini kwake…’akasema na kunionyesha, sasa
alionekana kuwa huru kufanya ninavyotaka, na ndicho nilikitaka,…nikachukua zile
nyaraka na kuanza kuzikagua, nikakuta kuna mkataba wa kuuza gari…
‘Kwanini anataka kuuza gari…?’ nikauliza
‘Mimi sijui, yeye wakati ananituma alisema, kuna mkataba wa mauzo,
anatakiwa aufanyie kazi haraka maana kuna watu wanahitajia pesa kwa ajili ya
kuimaliza kesi ya mauaji, hataki wewe usumbuliwe tena…na asipowalipa hizo pesa wanazomdai, unaweza
kufungwa..’akasema
‘Mimi au yeye…?’ nikauliza
‘Yeye alisema ni wewe…’akasema
‘Kwanini mimi nifungwe wakati sihusiki na hayo mauaji..?’
nikauliza
‘Mimi sijui…’akasema
‘Kuna jingine alikuagiza..?’ nikauliza
‘Hapana…’akasema kwa kusita
‘Una uhakika, hakuna kitu kakuambia uweke…au uchukuze zaidi ya
hivyo…kama anavyokuagiza kila mara , hujawahi kuagizwa kule ofisini kwangu
kuchukua kitu..?’ nikamuuliza
‘Hakuna shemeji…zaidi ni karatasi za madeni,hakuna,..hapana
shemeji, ofisini kwako, hapana, mimi kama niliwahi kufika huko, ni wakati upo
ofisini, sijawahi kufika wewe ukiwa haupo …’akasema
‘Wewe unahisi hizo pesa anataka kumlipa nani..?’ nikauliza na hapo
akaniangalia kwa mashaka, halafu akasema;
‘Hapo sijui…lakini jana nilisikia wakati anaongea ovyo, kuwa una
mtu kasema asipomlipa pesa anaweza kutoa siri, siri ambazo zinaweza kukufunga
na hata yeye anaweza kuwa hatiani…, nikamuuliza siri gani, akasema ni vyema mimi nisijue itakuwa bora kwangu….’akasema
‘Unahisi kweli kaka yako hajaua..huoni kama vile kafanya yeye hayo
mauaji ndio maana anajaribu kuuficha ukweli…na kama hajaua kwanini ahonge,
unaona eeh, na wewe unaingizwa kwenye janga hilo…’nikasema
‘Lakini atauwaje na wakati alikuwa mgonjwa, mimi nahisi anaongea
kwa kuchanganyikiwa…’akasema
‘Kuchanganyikiwa mpaka leo, si sasa hivi ni mzima, ana akili zake
sawa sawa, mbona analikumbuka hilo, …kwanini kakuagiza huu mkataba, kwanini
analikumbuka hilo la huyo mtu, anayedai pesa, kuwa ana ushahidi..? ..na docta
kasema mara nyingi mtu akiwa kwenye hiyo hali anaweza asikumbuke alichokifanya
akiwa kachanganyikiwa, hebu acheni hayo maigizo..?’ nikamuuliza
‘Lakini shemu yawezekana ni kweli…maana alivyoongea leo sio sawa
na alivyoongea jana usiku…’akasema
‘Leo kaongea vipi…?’ nikamuuliza
‘Nilipofika, nilimkuta kama yupo kwenye dimbwi la mawazo, halafu
akaniuliza, jana nilifanya nini..mimi sikutaka kumuambia, ukweli wote, halafu akasema hivi,..leo kuna mtu kampigia
simu, kuwa ana ushahidi ambao akiwaonyesha polisi yeye na wewe mnaweza kuwa
hatiani, lakini hakumbuki huyo mtu ni nani, akasema kwa kuepusha shari ni bora
ampe huyo mtu akitakacho na ili huo ushahidi upatikane uharibiwe,..…’akasema
‘Mbona hukuniambia awali hivyo, mpaka nimekubana kwa njia hiyo,
wewe kuna kitu unaficha,..unamficha nani,…sikiliza mimi sitaweza kukubeba kwa
hili, unasikia…kama hutaniambia ukweli wote, basi, …’nikasema
‘Ukweli upi tena huo shemeji…’akasema kama kukereka
‘Hapa unaona nakukera, lakini polis ni mara ya ya hapa,
watakuuliza kitu kile kile, hadi wakuchanganye kichwa, na mwisho wa siku
wataubaini ukweli wanaoutaka, sasa niambie, jana aliongea nini…?’ nikamuuliza
‘Shemeji nimeshakuambia jana alikuwa anaongea mambo mengi tu, ovyo
ovyo, wakati mwingine anachanganya mada, …’akasema
‘Kwahiyo unavyohisi wewe ni kweli hajui alichokifanya jana…nataka
useme ukweli ili tuweze kumsaidia kaka yako, na pili ili tuweze kumshika huyo
tapeli anayetaka kupata pesa kwa njia isivyo hali, wewe huoni kuwa kaka yako
anatumiwa tu…’nikasema
‘Mimi namfahamu kaka vizuri sana, …anavyoongea leo, sio kama
ilivyotokea jana, mengi nikimuuliza hakumbuki kabisa…anahisi kama likuwa anaota
tu shemeji….’akasema
‘Ngoja polisi waje natumai wakija wewe utakuwa na habari nzuri ya
kuwaeleza, wao ndio watayapima hayo maelezo yako, lakini kwa kukutahadharisha
tu, hayo maelezo yako yanaweza kukufunga, unageuza geuza maneno, hata mimi
naanza kukushuku kuwa wewe una mpango mmoja wewe na kaka yako…’nikasema
‘Mpango gani shemeji, ..mimi siwezi kufanya hivyo,….ninachofanya
sasa ni kujaribu kumsaidia kaka ili aondokane na haya mambo, kiushauri pia..ili
muishi wawili kwa amani…’akasema
‘Wewe na kaka yako, mlipanga jana kuniua,..hilo huwezi
kulikwepa..hata kama …lakini kaka yako alikuwa na nia hiyo…’nikasema
‘Sio kweli shemeji, hilo …nakuapia, mimi siwezi kufikiria hilo,na
kama ningelifahamu kuwa kaka anataka kufanya hivyo, ningekuarifu…’akasema
‘Na hayo mauaji mengine..?’ nikauliza
‘Mauaji gani, ..shemeji, hivi kweli mimi naweza kumuua
mtu…’akasema
‘Umeshirikiana wewe na kaka yako kulikamilisha hilo..hata kama
wewe hujafanya, ila unafahamu hizo njama kwahiyo mumeshirikiana naye…’nikasema
‘Hapana…mimi sijui lolote ..’akasema
‘Haya, nakupa muda wa kuliwazia hilo, hapa hapa, kabla polisi
hawajafika, maana wao wakifika utawaelezea vyema, kwanini kaka yako alitaka
kuniua hilo lazima watakubaba mpaka useme, …’nikazidi kumshinikiza kwa hilo, nia ni
kumjenga hofu ili aweze kuja kuniambia kila kitu ninachokitaka
‘Pili, kaka yako nashukiwa kuwa kashiriki au ndio yeye kamuua
Makabrasha, aliwezaje kwenda huko wakati anaumwa, ni lazim akuna mtu
alimsaidia, ni nani, kama sio wewe jembe lake, kwahiyo alikuita ukampeleka au
sio…?’ nikamuuliza na hapo akashtuka na kuangalia kule getini.
‘Sema ukweli shemeji, …ukweli ndio utakusaidia..’nikasema
‘Kaka alikuwa mgonjwa, huenda ugonjwa wake ndio uliomfanya
akafanya hivyo, mimi sijui lolote utanionea bure tu shemeji…’akasema
‘Haya…, kama ni ugonjwa, angwezaje kufika huko….ni lazima kuna mtu
alimsaidia,…hapo huwezi kukwepa…’akasema
‘Shemu mimi naomba tafadhali..usiwaambie polie lolote kwa hivi
sasa, subiria kaka apone kwanza…’akasema
‘Haya ni lazima yawekwe kwenye kumbukumbu za polisi, kuna leo na
kesho, je ikitokea akafanikisha dhamira yake,..kutapatikana wapi ushahidi wa
rejea…hapa ni kauli yangu na yako, ni lazima watu wa usalama wawe na habari
hizi..’nikasema
‘Hapana, sio vyema shemeji, na kwanini mimi nihusike hata hivyo..?’
akauliza
‘Kwasababu hata wakati anataka kuniua, alikutaja wewe, na kakiri
kuwa wewe ndiye jembe lake…, kwanini akutaje wewe kuwa umsaidie hebu jiulize
hapo…’nikasema
‘Mimi sijui labda ni kuongea tu, …’akasema
‘Docta anasema mengine anayafanya kutoka na kumbukumbu alizokuwa
nazo kichwani, na moja ya kumbukumbu zake ni wewe. Mlivyoongea , mlivyopanga…ndio
maana nakutilia mashaka, hata polis wanakutilia mashaka, ndio maana wanataka
kukutana na wewe, mimi nimetaka kukusaidia, lakini hutaki kuniambia ukweli,
basi nanawa mikono...’nikasema
‘Shemeji mimi jana nilipokuja nilienda chumbani kwangu, kweli si
kweli, na kiukweli mimi nilichelewa kulala , kwahiyo hata usingizi uliponishika
nilala fofofo, ndio nikaja kuamushwa na huo mlio wa bunduki, sikujua kabisa ni
nini kimetokea, na nilipoamuka ndio nikakimbilia kuja kuwaona, nilijua kua mtu
kaumizwa, nilipokuona upo sawa, ndio nikashikwa na butwa, nikijiuliza huo mlio
wa bastola ulikuwa wa nini,.....’akasema
‘Kwahiyo kwa kauli yako hapo, ulijua kaka yako kaniumiza..au
kaniua…?’ nikamuuliza
‘Kaka nimemuona yupo vile, hajaumizwa, hana jeraha, kwahiyo
iliyokuwa imebakia ni wewe..ndio nilipokuona nikawa na hiyo hali, unayosema ni
ya kushangaa…’akasema
‘Haya sawa, kuna jambo nataka uniambia maana ukitoka hapa,
hutakuwa na mimi tena, utakuwa mtu wa polisi, huyo mwanamke aliyezaa na kaka
yako ni nani, umesikia akisema kuna mwanamke wake, huyo mwanamke anampenda sana
kwa vile kamzalia mtoto wa kiume, jembe jingine…, ni nani huyo
mwanamke?’nikamuuliza.
‘Mimi simjui huyo mwanamke, ...naona alikuwa anaongea tu
kama mtu aliyechanganyikiwa...huoni hata sauti yake inasikika kama mtu
aliyelewa, kama teja, kama mtu yupo usingizini, na shemeji kwanini unasema
hutakuwa na mimi, nitakuwa na polisi kwa kosa gani...?’akasema sasa akijua
simtanii…
‘Kila kitu nikikuuliza mimi unasema hujui, …nitakusaidiaje eeh,
hebu niambie,na wao wanataka kukutana na wewe, kukuhoji..kuujua ukweli,..na kwa
maelezo yak ohayo, ni nani atakuamini, unaichanganya…wewe...utakwenda kulala
jela...’nikasema sasa nikichukua simu yangu, hapo akawa ananiangalia huku
akionyesha kuogopa
‘Shemeji mimi nina uhakika , kaka anakupenda sana asingeliweza
kufanya kitu kama hicho akiwa sawasawa, mimi nahisi kafanya hivyo, kutokana na
kuchanganyikiwa...na unataka nikuambie kitu gani ili uniamini, ..mimi sijui
zaidi ya hayo, msubirie tu kaka akipona utamuuliza’akasema
‘Ngoja polisi waje…, naona wamechelewa sijui kwanini..natumai ukiwaona
ndio utajua kuwa wewe upo matatani. Kwa maelezo yako tu, mimi nimethibitisha
kuwa kuna kitu mpo ushirika na kaka yako, na haya yaliyotokea na wewe
unahusika, sasa..wewe utaweleza yote jinsi gani unavyofahamu wewe, ili
ibakie kwenye kumbukumbu zao, unasikia....’nikasema.
‘Shemeji, acha usiwapigie simu polisi…,’akasema
‘Nikiwapigia, nisiwapigia ni hali moja, wewe utahojiwa na wao, na
wao walisema watakuja hapa,..na nimeoa ni bora wakuhojie hapa, kuliko
kukupeleka kituoni, ili nisikie wanachokuhoji…’nikasema
‘Shemeji, nisaidie, na msaidie kaka..huyo ni mume wako, kwa hili
utamtia hatiani, ..kama kuna kitu kingine niulize tu, nitakuambia kila kitu
utakavyo, lakini waweke mbali polis na kaka,, utamchanganya kichwa kabisa ..’
akasema na mimi nikawa tayari nimeshampigia simu ofisa mmoja wa upelelezi
ninayemfahamu..
NB: Sehemu hii nimeandika kwa haraka haraka, naweza nikawa
nimerudia rudia, naomba ipite hivyo, ili tusonge mbele.
WAZO LA LEO:
Moja ya rehema za mwenyezimungu, ni mapenzi kati ya mume na mke, kuhurumiana na
kujaliana. Wawili hawa wanakuja
kujenga familia , na huenda walikutana tu bila hata kujuana, ni nani alijua
wewe utamuoa huyo uliye naye au kuolewa naye, ni kwa rehema za mola wetu….sasa
kwanini tunakuja kuliharibu hilo, watu wanakuwa hawaelewani tena, ndoa zinakuwa
ndoana. Tumuombe mola wetu azijalie ndoa zetu, ziwe za upendo, na furaha, na
wale ambao hawajajaliwa kuwa na ndoa, mola awajalie walifanikishe hilo, kwa
rehema zake. Aamin.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment