Basi niliondoka hadi nyumbani, namkuta mume wangu kazidiwa
shinikizo la damu, ikabidi nifanye jitahada nyingine za kumuita docta, hakutaka
nimpeleke hospitalini, akaja docta, akasema kweli shinikio la damu lipo juu,
kwahiyo apate dripu…
Baadae hali ikawa shwari, ikabidi nikae naye kumuhoji hili na lile,
nilichelea kuongea naye maswali yanayoweza kumtatiza hata docta alinionya kwa
hilo, lakini kuna swali lililokuwa kichwani mwangu;;
‘Nikuulize kitu samahani lakini..kwani
shemeji ana tatizo gani?
‘Ndio mume wako, naona kama …ana matatizo,
wewe ni rafiki yangu, na lako ni langu, niambie ukweli …?
‘Hapana, mimi si ninaona tu…alivyo, sio
yule shemeji niliyemzoea, anaonekana hana raha kabisa…’akasema
‘Mhh, nahisi kuna tatizo kubwa sana
linamsumbua, jaribu kuwa naye karibu, sio vizuri rafiki yangu, mimi nawajali
pia..
Kumbukumbu hizo ziliuteka ubongo wangu, na kiukweli sikuwa na
amani kabisa..,Japokuwa mpaka hapo sikuwa na wazo baya dhidi ya rafiki yangu…ila
nilianza kuamini kweli mume wangu ana
matatizo..na hilo ndilo nililipa kipaumbele, vipi nitaweza kumsaidia mume
wangu, maana hiyo hali iliyojitokeza ikiendelea hivyo, kweli naweza kumpoteza
mume, …niliwazia zaidi kwenye afya yake
Basi nilipoona mume wangu katulia, na anaongea vizuri, nikamuuliza
‘Hivi mume wangu, hebu
niambie,…. kuna tatizo gani linalokusumbua…?’ nikamuuliza
Mke wangu matatizo ni ya kawaida tu, …tulishayaongea haya,…na
mimi sitaki ukwazike kwa hilo, na sijui
kwanini leo hali yangu imekuwa hivi,..nijitahidi isitokee tena, lakini kuna
mambo mengi yamenizonga, lakini yataisha tu, nitayamaliza kwa vyovyote iwavyo…’akasema
‘Huo ni ugonjwa, halafu unasema utajitahidi isitokee tena, na
tatizo hilo, ninavyoona sio bure, nahisi kuna kitu kinakusumbua,…sasa usipotaka
kunishirikisha mimi, eeh, hebu niambie,…ni nani mwingine anaweza kukusaidia,
zaidi ya mkeo …’ nikamwambia.
‘Usijali mke wangu,…wewe endelea na kazi zako tu, najua una mipangilio
yako mingi sana, …, na sitaki mimi niwe sababu ya kukukwamisha…’akasema
‘Hujanisaidia kwa hilo, maana sasa sitaweza kufanya kazi zangu kwa
amani, nitakuwa na mashaka muda wote, usiponiweka wazi…utanifanya na mimi
nianze kuumwa.
Basi nikaanza kuwa karibu na mume wangu na kumuomba samahani kama
mimi ndiye chanzo cha hayo yote, na siku moja akaniambia;
‘Mke wangu, uwe na amani, najua yametokea mengi, ambayo huenda
hata mimi sikupenda yatokee, lakini isiwe sababu ya wewe kukatisha shughuli
zako, muhimu ufahamu sijapenda yatokee, na kuumwa kwangu hata mimi ninaanza
kuogopa, inabidi nibadilike..’akasema
‘Ni kitu gani kinachokusumbua, hebu niambie kwanza…?’ nikamuuliza
‘Kifupi hakuna…nimeshazoea, na…hakuna tatizo, …’akasema na
sikuweza kuwa na amani tena…hasa nikikumbuka zile kauli za rafiki yangu, na
sasa ninaona kweli mume wangu ana matatizo,…
Kwasababu ya hayo matatizo, nikawa sina muda wa kumfuatilia rafiki
yangu tena, kumbe alishaondoka kwenda Zanzibar.
Na siku baadae nikamtembea rafiki yangu, katika kupoteza mawazo,
na katika kuongea tukajikuta kwenye yale mazungumzo yetu, tukafikia pale
pale…nikamuuliza
‘Unajua siku ile tulipoongea ukanipa ushauri kuwa niwe makini
naweza kumpoteza mume wangu, imenifanya nianze kujirudi, nimewaza sana, naona
kweli nitakuja kuumiza mume wangu…’nikasema
‘Nilikuambia lakini…sasa kwanini unaendelea kufanya hivyo, na je
mume wako anaendeleaje…?’ akaniuliza
‘Hajambo hajambo kabia…na huwezi kujua ni yule siku ile nilimkuta
kitandani akiwa kama kapoteza fahamu, ..shinikizo la damu ni baya… siku ile
hata mimi niliogopa, maana alikuwa kama anataka kukata roho…’nikasema
‘Oh,… lakini ni nini tatizo…?’ akaniuliza
‘Mpaka leo sijafahamu…na hata sielewi, unajua kuna kauli alisema…lakini
sio sababu nahisi kuna jingine..lakini hizo kauli zimenifanya niwaze tu, …japokuwa
sizani kama zinaweza kuwa ndio sababu..’nikasema
‘Kauli gani hizo mbona huzitaji…?’ akaniuliza
‘Unajua kuna kitu, …mume wangu anatamani sana, kimojawapo ni
hicho, ya kuwa anatamani kupata mtoto wa
kiume…na kingine ambacho hatusikilizani, yeye bado, anapenda ujana ujana,….hajui
kuwa umri umekwenda…hilo sijui wanaume wengi kwanini haalioni…mzee mzima bado
upo na mambo ya vijana.., mimi namemuambia sina muda huo…’nikasema
‘Mhh kwanini unafanya hivyo, unafanya makosa, maana mume wako ni
mwenza wako mwatakiwa mshirikiane, mfurahishane, sasa kama anataka hivyo
akaende wapi, ndio maana wanakimbilie mitaani, ..hili hulioni wewe…?’
akaniuliza
‘La kujiuliza ni hili mambo hayo, eeh yana faida gani kwetu, kwa
umri huu…sawa kama ni watoto tutapata tu,….mungu akipenda, … ila nilitaka
nimalizane na mipangilio yangu ili tukianza kuzaa, nisiwe na hangari hangari
nyingine ndio mpangilio wangu, nimejifunza kwnye mimba hiyo ya kwanza, …na hilo
nilishamuambia…’nikasema
‘Ina maana hilo ndilo la kufanya usiwe karibu naye,…hilo ndilo
linakufanya usitimize haki za ndoa,
ambazo ndio msingi wa ndoa au …’akasema
‘Unasema nini.., nani kakuambia kuwa sitimizi haki za msingi za
ndoa..?’ nikamuuliza kwa mshangao.
‘Nakuuliza sio nasema mimi, nakuuliza wewe, na …’akasema na kabla
hajamaliza nikasema;
‘Umeyajuaje hayo,….!! Kwani aliwahi kukuambia hivyo, kuwa
sijamtimizia hayo…aah, naona sasa unaingilia mambo yasiyokuhusu…’nikasema
‘Lakini rafiki yangu rejea mazumgumzo yetu tuliyofanya siku ile, kwani hukuwahi kunigusia hilo,…. au
unafikiri mimi nakuzulia au urafiki wetu una mipaka sijakuelewa, …’akasema
‘Ok,…ok… basi labda niliwahi kukudokezea hilo.., sawa, nimekumbuka
nilikuambia …hata hivyo hilo mimi nimeshaliona, na nilikuwambia nitalifanyia
kazi, kwahiyo lisikuumize kichwa, umenielewa…’nikasema
‘Sawa, ….ni heri ulifanyie kazi, na kiushauri, kama kuna
yaliyotokea yakakukwaza, au kama kuna kitu, jaribu kukiweka kapuni, kitupe…
nakuomba uyasahau yote mabaya ya nyuma,…hali umeshaiona, hali hiyo inaashiria
kuwa , sasa hivi uwe karibu naye,
na…nahisi inaweza ikaleta heri ukifanya hivyo.., tusameheane tu, maana mengi
yanafanyika ili tu, kutimiza adhima…’akasema
‘Nimekuelewa,…’nikasema
‘Unajua nilitaka nikisafiri niwe na amani, niwe nimeacha kiula
kitu ni shwari..nisiwe na kitu moyoni mwangu kwako, na wewe kwangu…’akasema
‘Hilo lisikutie shaka, hebu kwanza nikumbushe, siku ile tuliishia
wapi…’nikasema
‘Siku ipi tena….mmh, yale tuachane nayo bwana…ndio maana nataka
tuhakikishe tumeridhiana, hakuna …jambo la kuumizana kichwa, na ukweli wote,
nshakuambia au sio…’akasema
‘Hapana hujambia,..ukweli wote.., maana nakumbuka siku ile
ulisema…, alipokuja kwako,…kuna kitu alikuambia ndio kikafanya yeye agundue
kuwa una mimba, ni kitu gani miliongea…?’ nikamuuliza
‘Hahaha, na wewe bwana,….hahaha, unajua wakati mwingine nacheka,
lakini wakati mwingine najiuliza hivi hili jambo litafikia mwisho tusahau ,
isije kuleta matatizo huko mbeleni,…na ikileta .. itakuwaje…maana nimejaribu
kila njia unielewe, lakini sizani kama utanielewa, kwa hali kama hii…unakuwa
mdadisi kwa kitu ambacho ulikanya wewe mwenyewe kuwa jambo hilo liwe siri….sasa
labda mimi naona nikuambie kila kitu iwe iwavyo…’akasema
‘Sawa lakini hapo …kuna kitu sijakuelewa…’nikasema
‘Rafiki yangu, hebu nikuulize kwani unataka nini zaidi,..unataka
matatizo, unatakaje ili iweje, …wakati mwingine naona ni bora tukae kimia,
wakati mwingine naona ni bora niweke kila kitu kwenye meza, ..lakini
sitaki kuumizana , sipendi kabisa…’akasema
‘Kwa hivi sasa bora uniambie kila kitu tu, maana ukiacha ndio
utanipatia shinikizo la damu, maana nimekuwa nikijiuliza, na…nilitaka hata
niende kuonana na mdogo wa shemeji ili niwe na uhakika fulani, kuna maswali
yana nijia, na mimi nataka nimuulize, lakini siwezi kufanya hivyo mpaka nipate
ridhaa yako,…wewe huelewi tu, …wewe ni kama mdogo wangu lazima niwe na uhakika
na ulichokifanya, ili likitokea la kesho, niweze kuwa na majibu, ukumbuke kuna leo na
kesho…’nikasema
‘Kwahiyo unataka nini hasa, na upo tayari kwa …mimi siwezi kuwa na
uhakika na wewe, maana hili linaweza likawa sababu, na mimi sitaki, unielewe
hapo, eeh, mmh…nasita kidogo hapo…’ akasema
‘Swali lipo pale pale… ikawaje, usitake tuzunguke,…. huyo shemeji
alifahamu vipi kuwa wewe una mimba, na ni kauli gani ilikyokufanya hata wewe
ufikie kumwambia, au ilikuwaje…unajua, nimeanza kuandika kitabu changu, natunga
true story ya maisha yetu mim na wewe
vyema…hahaha, huwezi amini mengi yaliyotokea kati yangu na wewe nimeshayaandika…’nikasma
‘Unasema kweli…?’ akauliza
‘Ndio..ni pale ninapokuwa sina kazi,..akili imetulia huwa
naandika, yale yaliyotokea kama hadithi fulani hivi,…sasa hivi nipo kwenye hilo
tukio, naona lina maswali mengi yasiyokuwa na majibu, na sehemu hiyo nimeiita,
‘ukweli baada ya ushauri kwa rafiki yangu..’.
‘Mhh, ushauri kwa rafiki yako, ambao umeleta matatizo au,
itakuwaje sijui….’akasema
‘Matatizo aah, nani kasema, hakuna kitu kama hicho, ni ushauri
ulioleta matunda ya kuleta faraja…huoni sasa una mtoto, usiseme
hivyo….’nikasema
***********
‘Kama nilivyokuambia, kuna muda nilikuwa natamani yeye awe
anakuja, au nimpigie simu tuongee naye, nikifanya hivyo, nikasikia angalau sauti
yake, kama hakuweza kufika, najihisi raha, nakuwa na amani fulani… lakini
wakati huo sikutaka hayo yajulikane na watu.., sikutaka watu wanione nikiwa
naye tena, naona aibu kuliko wakati wote, nilihisi kama watu watanigundua kuwa
ndio yeye…’akaanza kusimulia
‘OK…sawa endelea…’nikasema
‘Siku hiyo alifika akiwa hana raha, nikamuuliza tatizo
nini…akasema hakuna kitu ni mambo ya kawaida tu,..ni mambo ya kifamilia
zaidi…’akasema
‘Kama huniambii, sitakuwa na amani, siku hizi sijisikii vizuri,
nataka wewe ukija uwe na furaha, na kama huna furaha ..ni bora usije ,..na
usiponiambia tatizo lako, ni bora uondoke..’nikasema na moyoni nijiuliza hivi
kweli akifanya hivyo si nitaumia sana, na mimi nataka awe karibu yangu.
‘Ina maana muda huo mimba bado imejificha,..bado mapema au sio..?’
nikamuuliza
‘Kitumbo bado ile yasana,… ila kimeshaanza kutuna, na mimi sijui
kwanini, nilianza kuvaa nguo pana mapema, ..kama Madera…kitu ambacho wengi walianza kunihoji
nakawa nawapa majibu yao, na nikazoeleka hivyo kuwa nimebadilika, siku hizi sio
yule mdhungu tena…ilinisaidia, hata dalili zozote zisionekane mapema, na siku
baada ya siku …tumbo likaanza kukua…’akasema
‘Safi kabisa, ulicheza hapo maana hata mimi sikuwahi kukushuku
awali…’nikasema
‘Nataka unizalie mtoto wa kiume…mjamaa alipofika alisema hivyo…’akasema
‘Mungu wangu alikuambia hivyo…?’ nikauliza nikihema, muhemo, kama
vile kauli hio inanihusu mimi.
‘Ndio alisema hivyo na mimi kauli hiyo ilinishika kwa mshangao,
lakini sikutaka kujionyesha, nikacheka kweli
‘Kwanini unacheka, akaniuliza…?...’akasema
‘Unanishangaza, ina maana kukuita hapa, umenifanya mimi kama
hawara wako,..nilishakuambia yaliyotokea siku ile, mimi sikuyataka na yaninipa
wakati mgumu sana, na..na..kwanza ole wenu nilitaka kuwashitaki, mlichonifanyia
wewe na ndugu yako, sitaweza kuwasamehe..’nikasema
‘Kitu gani, mbona sikuelewi…?’ akasema
‘Tuyaache hayo…na umesema nini…?’ nikauliza kama vile sijasikia
‘Natamani wewe unizalie mtoto, lakini awe wa kiume..’akasema
‘Nikuambie kitu, hilo kamwambie mkeo, sio mimi…’nikajifanya kuwa mkali,
‘Sikiliza,..najua hata wewe unataka mtoto, nimesikia hivyo..,..unatamani
uwe angalau na mtoto, hata mimi naliunga
mkono, maana umri unakwenda au sio, sasa hebu tulia basi…’akasema na mimi muda
huo nilikuwa nasimama nahisi kichefu chefu
‘Ni nani kakuambia upuuzi huo…’nikasema nikigeukia upande wa pili
leso mdomoni.
‘Wakati mwingine wanawake mpo hivyo, kama hujaolewa kwa muda..umekaa
na unahisi umri utakusuta..na sio siri kila mtu anatamanikuwa na mtoto, hata
wewe itakuwa hivyo,…hilo lipo wazi, sasa nisaidie na mimi nikusaidie…’akasema
‘Nikusaidie..wewe si mume wa mtu jamani, unataka nini…?’
nikamuuliza na mengi yakaendelea hapo ikawa tena hatuelewani…’akasema
‘Mengi yapi..?’ nikauliza
‘Tulibishana sana kuhusu hilo la mimi kumzalia mtoto, eti tena wa
kiume,…hivi hilo si alitakiwa aongee na mkewe…anyaway, tulibishana hapo, na sijui ikatokeaje, nikaanza kujisikia
vibaya, kutapika, nikakimbilia washroom,
kumbe alinifuatilia kwa nyuma, sasa wakati natapika, ikafikia muda, nikasema;
‘Kama mimba ni hivi, bora …nizae mapema tu..hiki kikombe kinipite…’nikasema
na huku nyuma yangu nikasikia akisema;
‘Kumbe una mimba…’akasema,..nilishtuka, karibu nizimie, na akaja
haraka kunishika ili nisidondoke, na alipohakikisha nipo salama akasema;
‘Oh, sasa niambie ukweli,…kumbe una mimba , kumbe ni kweli…mmh,
nishathibistha inatosha, sasa niambie ukweli ni yangu au kuna mwingine…’akasema
‘Mimi sio Malaya bwana…’nikasema
‘Ndio maana nauliza isije kuleta matatizo..najua mimi
nimeshatembea nawe, sina uhakika na mwingine je ni ya kwangu au kuna
mwingine…?’ akaniuliza
‘Mimi sijui, maana mlichokifanya wewe na ndugu yako siku ile mimi
sijui, mimi sijui na sitaki kujua, niache, ushaiharibu siku yangu , ondoka…’nikasema
‘Basi natosha, ninachoomba kwa mungu awe mtoto wa kiume…’akasema
hivyo, na hakutaka kukaaa sana, akaondoka akiwa anaonekana ana furaha usoni ,
sio kama alivyokuwa amekuja.
‘Kwahiyo hebu kwanza nikuulize kuna jambo nilitaka niwe na uhakika
nalo..hivi ulipogundua kuwa una mimba, ulikwenda kupima wapi, maana nataka
mambo haya yawe kwenye kumbukumbu zangu, hapo kasema, ‘kumbe ni kweli’…’nikasema.
‘Kwanini unauliza hivyo…ina maana kweli kuna kitabu unatunga, au
unataka jambo kama ushahidi fulani, ushahidi wa nini…?’ akaniuliza.
‘Nimeshakuambia naandika tu kujifurahisha, nilianza kama mzaha tu, lakini
kadri siku zinavyokwenda naanza kufurahia,… na hasa hii kadhia, kuna muda..
inaniacha kwenye maswali mengi ya kutaka kujua zaidi,..unajua tena…na hata
hivyo ni kawaida yangu kuwa na kumbukumbu, na usinifikirie vibaya, kwanini nafanya hivyo, au
hupendi, niwe naandika, kama hupendi nitaacha tu…’nikasema
‘Ok.. nilikwenda kupima kwenye ile hospitali iliyopo karibu na kazini,…na nilifanya
hivyo kwa vile sikuwa na amani, nilikuwa sijisikia vibaya vibaya, hali ambayo
sijawahi kuihisi kabla, huko kupoteza siku zangu , inatokea mara kwa mara
kwahiyo haikuwa ni sababu…hata hivyo wakati naenda kupima, nilikuwa kama
siamini, maana …kama tukio lilivyokuwa ilikuwa kama ni ndoto…na sikuweza kuwa
na uhakika, niweke hivyo tu…’akasema
‘Hukuwa na uhakika gani kuwa ni nani kati ya hao ndugu wawili au
si..…au hukuwa na uhakika kwa vile..haiwezekani ulisema ..kitendo kilikuwepo au
sio, … hapo usinidanganye kitu…mpaka hapo nahisi kuwa kuna kitu unanificha,
halafu unajinasa mwenyewe hiyo kauli ‘sikuwa
na uhakika..’nikasema
‘Nimekumbuka kitu…siku ile nilipokwenda kupima nilikutana na docta
ambaye nafahamiana naye, naye kuna kipindi tulikuwa naye karibu baadae ndio
akaoa, nikaachana naye,…sasa nikuchekeshe kitu,....’akasema.
‘Nichekeshe…’nikasema
‘Kumbe yule docta ni best sana wa shemeji….’akasema
‘Shemeji,…una maana huyo bwana’ko…?’ nikauliza
‘Na wewe bwana…sio bwanangu huyo..,..mwishowe utazoea hiyo kauli,
mimi siipendi…’akasema
‘Samahani, naongea hivyo kwa vile tupo wawili wala usiwe na
shaka…’nikasema
‘Sasa nahisi..au nilihisi huenda waliwahi kuongea kuhus mimi, kuwa
nina mimba, nahisi hivyo kwa vile siku nilipokwenda kupima,..jana yake, au siku
baada yake, nakumbuka, mjamaa aliniuliza….
, japokuwa hakuwahi kuniambia kuwa kagundua kuwa nina mimba..na nijuavyo aligundua
hilo baada ya siku hiyo wakati alipokuja, na kuanza kuongea hayo kuwa anataka
nimzalie mtoto…’akasema
‘Mhh, ...mambo ya huyo shemeji hayo….yanafanana sana na mambo ya mume wangu, ,
unajua hata wakati naandika, nikawa najiuliza huyo mtu ni nani, sura ya mtoto inafanana na familia yangu, ina
maana huyo baba yao, eeh, atakuwa anafanana na mume wangu, …na na…hili tena,….unajua
mume wangu ni rafiki mkubwa wa huyo docta wa pale…walisoma wote…’nikasema.
‘Ndio hivyo….mmh, sasa…mmh, unajua yote haya ni kutokana na ushauri wako,
nisingelifikia hatua hiyo, wakati mwingine nafikia kujilaumu ni kwanini
nilikusikiliza, ….usinielewe vibaya hapo kuwa sikuupenda huo ushauri wako..,
ila nasema haya kwa vile naona kila hatua kuna mtihani fulani na naona inaweza
ikafikia sehemu…hata sijui itakuwaje……’ akasema
‘Ni wasi wasi wako tu….unafikiri, unajua hayo yote nayafahamu na
…kukushauri kwangu sikuwa na nia mbaya, nilijua haya yanaweza kutokea hivyo..na
mimi nitayapokea kwa jinsi yalivyo, siwezi kukulaumu kwa lolote lile,
unasikia,.., kwahiyo, wala usiwe na shaka kabisa…’nikasema
‘Kwahiyo unataka kusema nini hapo.., kuwa unajua ni nani, na huna
shaka lolote kwa hilo…yaani hutanifikiria vibaya , tukaja kukosana…?’
akaniuliza
‘Hebu nikushauri kitu, hebu
kwanza nihakikishie kwa huyo shemeji ni nani , ili niweze kupanga jinsi gani ya
kumweka sawa, mimi nataka nije kuonana naye, ili niliweke hili jambo sawa,
sawa..’nikasema
‘Mhh..kumbe bado…’akasema
‘Ni hivi…ninachoogopa ni wewe unaweza ukavuruga huu mpango kabisa…,
wewe unachukulia hili jambo kirahisi tu, hujui ni jinsi kwenye mwenye mume
atakavyojisikia akiligundua hilo, unataka mim nije kujuta kwanini nilikushauri,
sitaki itokee hivyo kamwe, unasikia,...sasa nataka uniambie ukweli huyo shemeji
ni nani?’ nikamuuliza.
‘Na wewe bwana , hapa nilijua unasema umeshamfahamu, na ulijua
kitu kama hicho kinaweza kutokea,…ulikuwa na maana gani,..mimi naona haya
tuyaache tu, yasije kukutia presha?’ akasema
‘Mimi nishakuambia ..kwa hisia zangu ni huyo mdogo wake mume
wangu, kwasababu nyingi tu, kuanzia kufanana watoto na tukio zima kama
ulivyoliezea, na , naaeeh…sioni mtu mwingine anayefanana na hivyo,… labda
uniambie wewe, ni nani huyo, na kwanini…eeh, unaona ugumu kunihakikishia kuwa ni yeye, …mimi
siwezi kufanya lolote, maana hanihusu kwa sana, japokuwa ni mume wa mtu,…hawa
wanaume jaman…’nikasema.
‘Lakini…mbona umesahau kuwa ulinishauri hivyo, ukisema hawa waume
jamani, unanishutumu na mimi au…’akasema
‘Ndio hivyo, ila …ukweli upo pale-pale, inauma sana, tena, sana,
sijui ikitokea kwangu kama nitaweza kuvumilia, mimi aah, ..mimi siwezi,…ndio
maana nilitaka nimfahmu huyo mtu ili madhara yasizidi kuendelea, umenielewa
hapo…nataka niongee naye,nitajua jinsi gani ya kumweka sawa,…haya niambie ni
nani huyo mtu….?’ nikamuuliza
‘Ni shemeji jamani…nimeshakuambia ni shemeji’akasema, na kusimama,
kama anataka kuondoka,…sijui kwenda wapi, akageuka kuniangalia na mimi nikawa
nimemuangalia, tukawa tunatizamana…
Kiukweli mpaka hapo bado mimi
sikuwa na tashwishwi yoyote mbaya, maana kwa hilo neno ‘shemeji’ ndivyo alivyo
kuwa akimuita huyo jamaa yake tangia awali, na nikajua anamuita hivyo kutokana
na mimi, kuwa ni mdogo wa mume wangu…lakini bado naona kama anaogopa
kunibainishia hilo, na kwa namna hiyo akazidi kunipa hamasa.
‘Hahahah, nilijua tu, kwahiyo sasa umenihakikishia, kuwa ndio
yeye, au sio….marafiki wawili wana waume kutoka familia moja, japokuwa…wewe
unapita tu, hahaha…kiukweli, nimefurahi, japokuwa,…mmh, namuonea huruma sana
mke wake….’nikasema na mara ujumbe wa simu ukaingia kwenye simu yake, akausoma,
na mara kwa haraka akasimama, akiangalia kule mlangoni, sikusikia sauto ya
gari…kwahiyo sikuwa na mashaka kuwa kuna mtu kaja…
‘Unajua, …kuna mgeni anataka kuja, na sikutaka akukute hapa, wewe
au mtu mwingine, na huyu mtu kawahi kabla ya muda,ujuo wako sikuwa na …..sasa
sijui kwanini, mbona hivi…’akasema akijaribu kupigia simu, nahisi kwa huyo mtu,
lakini naona simu ilikuwa haipokelewi..
‘Kwani una nini, mbona huna amani , ni nani huyo mtu…?’
nikamuuliza
‘Hata sijui itakuwaje…na nilishamuambia asije hapa mpaka nimpe
nafasi, au aniambie kabla, sasa anajileta tu, mbona huu mtihani.’akasema sasa
akiangalia mlangoni
‘Kwanini, mimi si rafiki yako…na huyo shemeji,…niambie
ukweli..’nikasema
‘Ndio yeye….’akasema
‘Safi kabisa, …hilo sasa niachie mimi, wala usiwe na shaka,…na kwa
vile mume wangu hajui kuwa nipo hapa, ..nitamtumia ujumbe kuwa nimepitia mahali,
sitamwambia kuwa nipo hapa, nataka hili jambo tulimalize leo hii, au sio…’nikasema
‘Ina maana mume wako, hajui kuwa upo hapa, umekuja huku bila
kumuambia, kwanini lakini, …?’
akaniuliza kama ana hamaki
‘Nilikuwa na kikao na muwekezaji mmoja, na bahati kikao
hakikufanyika kwahiyo yeye anafahamu nipo kazini..mimi kwa hasira…maana huyo
muwekezaji kanipotezea muda wangu maandalizi, halafu analeta ujumbe mwishoni
kuwa kaahirisha kuja..ameniboa kwa kweli,…’nikasema
‘Mhh….’akasema akiangalia simu yake naona alitarajia kupata majibu
fulani lakini hayaji.
‘Sasa sijamfahamisha mume wangu kuwa nimetoka, ngoja…nimtumie
ujumbe…’akasema akiandika ujumbe kwenye simu…akatuma na kusema
‘Leo simu ya mume wangu haipo hewani, kulikoni…’nikasema
‘Labda kwa vile…’akasema na kusita….kwani mlango uligongwa
‘Huenda ni shemeji,...mungu wangu…’akasema
Nikiwa natabasamu tele mdomoni macho yangu yakaelekea kule mlangoni,
nimuone huyo shemeji, akilini kwangu najua ni huyo huyo, mdogo wa mume wangu….shemejiiiii…
Nikamtupia jicho la pembeni rafiki yangu nikamuona akiwa anahangaika hana amani kabisa,
sikuelewa ni kwanini, labda ni kwa vile hakutaka nikutane na huyo shemeji,
lakini kwa muda huo sikujali, nilijua nitalimaliza nikikutana na huyo mtu, sasa
nilimuona kama anataka kwenda kule mlangoni,...huku mkono mmoja kashikilia
mdomoni…!!!
WAZO LA LEO: Tunapopeana ushauru, au tunapotoa ushauri
tuhakikishe hicho tunachokifanya tuna uhakika nacho, kiimani ya kweli(kwenye
dini zetu), au kiutarataibu uliokubalika na jamii zetu, ili matokeo yake yasije kutuathiri sisi
wenyewe au kuonekana watu wa ajabu katika jamii zetu. Lakini muhimu tuangalie
je mola analiridhia hilo, je ningelifanyiwa mimi ningerizika nalo…
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment