Matatizo
yaliingilia familia za wakina mama hao, hasa hao wawili, yule aliyenitoa kijijini,
na huyu anayeishi na mdada, ila huyu ninayeishi naye kwasasa hayakuwa makubwa
sana, zaidi ya migogoro yao ya kifamilia hasa kati ya baba na mkewe, mkewe alikuwa
hataki kabisa mimi niendelee kuishi hapo, hata kurudi kuishi hapo, ilitokea
pale wenzake walipomshauri kuwa nirudi kwake niishi kwa muda.
‘Mlishakubaliana,
aje aishi kwako, huku akitafutiwa chumba, basi wewe endelea kufanya hivyo,
nakuomba sana , maana kama unavyosikia, kwangu hakuna amani, mume wangu kawa
kama mtu aliyechanganyikiwa..kijana wangu naye haeleweki…’yule mama mfadhili
wangu wa kwanza akamwambia mwenzake huyu alipopigiwa simu kuhusu mimi.
Walikuja wakakutana na kukubaliana aendelee kunivumilia.
Basi
ikakubaliwa hivyo, nikawa naendelea kuishi hapo, lakini kwa makubaliano kuwa niishi hapo kwa muda,
lakini alisema hatakubali mimi nikae hadi nijifungulie hapo kwake….
Tuendelee
na kisa chetu…
************
Baada
ya tukio hilo, mimi niliendelea kuishi kwa yule mama niliyepelekwa kwake, kwa
masharti kuwa nindoke hapo kitakapopatikana chumba, ili nihamie na kuanza
maisha yangu mapya, na mtu wa kunitafutia chumba alitakiwa awe mume wa yule
mfadhili wangu wa kwanza.
Siku
zikaenda na mimba inakuwa, na hali yangu ilikuwa leo mzima kesho mgonjwa hoi
kitandani, na nikiumwa ndio makelele matusi, mimi nipo hapo kwa ajili ya kula
na kulala tu,…ikabidi nivumilie hivyo hivyo nitafanya nini.
Sikuweza
kuwalamu wafadhili wangu wa kwanza, kwanini hawanitafutii chumba kwa haraka,
kwasababu sikujua kuna tatizo gani huenda bado wanahangaika na matatizo ya
familia yao, maana baada ya kutoka siku ile, huyo mama alipopigiwa simu kuwa
mume wake kachanganyikiwa, mimi sikuweza kuonana naye tena, nasikia tu, kwa
kupitia kwa huyu mama ninayeishi naye kuwa hali ya yule mume imekuwa ya
utatanishi.
Siku moja nikakutana na mdada, nilipokwenda
sokoni, tukapata mwanya wa kuongea kidogo, na ndipo akaniuliza nimefikia wapi
na mpango wa chumba
‘Sinilisikia
kuwa wanakutafuti chumba, imefikia wapi…?’ akaniuliza
'Mimi
hata sijui, kila kukicha wanandoa hao wawili, wanakimbilia kwenye shughuli zao,
jioni wakikutana ninachosikia ni ugomvi, mama mwenye nyumba analalamika, mimi
nitawekwa humo mpaka lini, na mimba ndio hiyo inazidi kukuwa na kila siku
siishi kuumwa umwa.
'Na
mzee anasemaje, baba mwenye nyumba?’ akaniuliza
'Yeye
anasisitiza kuwe na mke wake azidi kuwa na subra, kwani hawataweza kunirejesha
kule kwa familia ile nyingine kwa hivi sasa kutokana na matatizo yanayoendelea
huko, kunipelekea mimi huko kutaizidisha matatizo zaidi, na mpangop wa chumba
haujakamilika….’nikasema
‘Lakini
chumba kiwe ni tatizo kupatikana, mimi hili siamini, nahisi kuna jambo jingine
, labda baba yule kutokana na hali yake, na kazi ya kutafuta chumba na
kukuhudumia kakabidhiwa yeye..si ndio hivyo..?’ akasema na kuuliza
‘Ndio
hivyo…’nikasema
‘Kwahiyo
huyo mama anatakaje, kuwa uondoke, uende wapi, urudi kule au iweje, kama ni
hivyo, kwanini yeye asisaidie kutafuta hicho chumba…?’ akaniuliza
‘Huyo
mama kasema hayo ni mambo ya wanaume waliosababisha hayo yote ,kwahiyo kama ni
chumba, waume ndio watafute, ili waweze kuwajibika, wanachoogopa ni kuwa
wakitafuta chumba wao, waume wao hawatawajibika ndio makubaliano yao, na zaidi
kinachoniuma ni kauli yake tu….’nikasema
‘Kauli
gani…?’ akauliza
‘Hiyo
ya kuwa mimi nikizaa shetani, ni nani atahangaika nalo…’nikasema
‘Lakini
ndivyo alivyosema marehemu au sio, wote wawili hilo walilisema, na hata yule
rafiki wa marehemu alilithibitisha hilo, japokuwa yeye ni mganga tu wa miti
shamba, lakini si alisema ukiwa na matatizo umpigie simu, atakutafutia dawa…?’
akauliza
‘Ndio,
lakini huyo mama ninayeishi naye, kasema hataki kuhangaika na mambo ya
kishirikina, kama ni shetani, niondoke nalo, nikazalie huko huko…’akasema
'Hayo
waliongea lini…maana majuzi walikutana kwenye kikao chao…?’ akaniuliza
'Hata
wiki haijapita, walizozana kweli, hata usiku sizani kama wamelala kwa amani…maana
asubuhi waliamuka kila mtu kanuna, …’akasema
'Basi
hao akina mama walikutana kwenye kikao
chao, wakashauriana kuwa sisi turejeshwe kijijin na kukabidhiwa kwenye familia
za hao marehemu maana sasa familia zao hazina amani tena, na tukiendelea
kuwepo, matatizo hayataisha…’akasema huyo mdada
'Aaah
mimi hilo sikubali, kama hawanitaki, waniache tu, nitahangaika hapa dar, na
najua nitaweza kuishi, lakini sio kunirejesha huko kijijini…’nikasema
'Haya
wakikitupo huko mitaani ndio utaishije, hebu niambie, una mipango gani ya
maisha..?’ akaniuliza
'Mungu
mwenyewe atajua, ….’nikasema
‘Mungu
mwenyewe atajua, ndio mipango yako hiyo, mimi sipendi hata kuongea na wewe,
maana huna ubunifu, huna akili ya kufikiria, mungu atajua, ukiwa umekaa hivi
hivi tu…’akasema huyo mdada
‘Sasa
unataka mimi nifanye nini, elimu yangu imeishia hivyo…sina ujuzi zaidi ya
kufagia na kusafisha vyombo, na kuomba omba mitaani, nitafanya kazi gani…?’
nikauliza
'Tatizo
wewe….hata nikikushauri jambo ni kama nampigia gita mbuzi, wewe ulivyo, huwezi
kuishi na mimi, wewe huwezi kupambana na
mambo ya mitaani…mimi mwenzako ni mjanja, nione hivi hivi tu…’akasema
'Mungu
atanisaidia, najua mungu anajua fungu langu, kama ni hapo hapo au hata
wakinifukuza, ipo siku nitafanikiwa tu, lakini siwezi kufanya mambo nisiyokuwa
na ujuzi nayo…’nikasema
'Mimi
ninachokuonea huruma, wewe una mzigo tumboni, na baya zaidi hatujui huo mzigo
ulio nao tumboni upoje, ushaambiwa sio mimba ya kawaida, je ukizaa shetani,
hebu niambie kutakalika kweli…’akaniambia
'Mimi
sipendi hiyo kauli, kwanini nizaie shetani, …kwani wengine wanazaaje, mbona
hospitalini wanasema ni mimba ya kawaida tu…’nikasema.
'Hiyo
ndio kauli yako,mungu anajua, mungu anajua, haya kaa na kauli yako hiyo tuone
kama mungu atakusaidia kama wewe mwenyewe hujisaidii,..kiukweli mimi nilikuwa
na mpango, lakini kila nikiongea nawe naona ni majanga tu, hutaweza kuniunga
mkono, na sana sana, utaniharibia, naogopa kukushirikisha kabisa…’akasema
'Mpango
gani huo…?’ nikamuuliza
'Niapie
hutasema kwa mtu, kama nikikuambia kuhusu huo mpango wangu, maana ni…..’akatulia
kama kshtuka jambo, akageuka kuangalia kule sokoni, na mimi nikaangalia huko
huko kuwaangalia wenzangu niliokuja nao.
'Niambie
kwanza, ndio niape siwezi kuapa kitu ambacho sikujui, je kama ni dhambi…’nikasema
'Hawa
akina mama si wanajifanya wajanja, hawajui kuwa bado wamekalia bomu….’akasema
'Bomu
gani hilo…?’ nikamuuliza
'Si
yale mazindiko, umesahau, kwani walifanya juhudi gani kuyaondoa, wamepuuza,
angalia yule mama kule tulipokuwa awali anavyopata shida, kwanini hawaelewi,…’akasema
'Si
walishahangaika wakaambiwa yameondolewa, na hayo yanayotokea hivi sasa yawezekana ni mambo ya kawaida tu, mimi hata
sijui, …’nikasema
'Thubutu,
kila siku majanga, nimesikia wakiongea, mume wa kule tulipoanzia, siku nyingine
anakutwa yupo nje uchi, anaweza akawa anatembea hata hajui anakwenda wapi,
usiku amaanuka, anatembea, anafanya kazi, hivi hayo ni mambo ya kawaida…’akasema
‘Lakini
docta alisema huo ugonjwa upo, na kutibika kwake hakuhitajii haraka, …’nikasema
‘Na
huyo kijana wao, umesikia vituko vyake…’akasema
‘Amekuwaje
na yeye…?’ nikauliza
‘Hahaha,
mimi niliwaambia, huyo kijana wao, ana matatizo, wakaniona namchukia, naingilia
mambo ya kifamilia, na unajua mimi walishanichukia mapema hata kabla y ahayo
matatizo, kisa namsingizia mtoto wao, eti mambo asiyoyafanya, wanamdekeza sana
yule kijana, sasa wameshaanza kuipata joto ya jiwe, watanikumbuka…’akasema
‘Amekuwaje
kwani…mbona siyajui hayo?’ nikauliza
‘Sasa
na hilo utasema ni ugonjwa,…hilo sio ugonjwa, pamoja na mengine, mtoto wao ana
matatizo, na ukionamtu anakushauri msikilize, yule mama ni mwalimu, msomi
mnzuri, lakini sijui kwanini mambo mengine anayafumbia macho, hasa yakihusu
mtoto wake..yeye alitekwa na akili kuwa mimi huenda natembea na mume wake,
akashindwa kuangalia mambo mengine…’akasema
‘Mhh,…sijui
kwanini alikuwa akifikiria hivyo, kwanini lakini, mimi wala sikuwa na mawazo
hayo…’nikasema
‘Hukuwa
na mawazo hayo, ushahidi si unao tayari….’akasema akicheka.
‘Naona
wewe unaleta utani, mimi niliwahi kutembea na mume wake…’nikasema
‘Sasa
ndio hapo, wangetuliza kichwa, wakaangalia kiundani zaidi, tatizo, sio sisi tu,
huenda matatizo hayo yameanzia hata kabla yetu, mzee, kijana,…na ni kweli kuna
mamabo yamewekezewa, nayo walitakiwa wayafukue, lakini kwanza wamejiangalia wao
wenyewe, mle ndani kuna tatizi zaidi ya tatizo,…’akasema
‘Mhh..au
wewe unahusika….’nikasema
‘Hahaha,
watamtafuta mchawi, na hawatampata, maana mchawi keshafariki, yaliyobakia, ni
masalio yake, na hayo masalio, watapata shida sana kuyamaliza, ... waache
wahangaike, mwisho wa siku watatutafuta, ila mimi sijui kama nitaendelea kuishi
na hawa watu…’akasema
‘Kwanini
wanasema hivyo watatutafuta,…?’ nikauliza
‘Hivi
unafikiri utaishi na wao milele…na we ngoja tu,…mimi sio mjinga, najua kuishi
na watu, kwanza nilipofika hapo kwa madamu, nikafanya utafiti, kuna mtu
kanifundisha jambo, mjue mtu unayeishi naye anataka nini…nikamtafit madamu
nikajua anataka nini na nini..nikamtafuti mzee, nikajua anapenda nini na nini…mzee
wake hata habari na mimi kabisa…hilo nimelifurahia, tatizo ni mama…’akasema
‘Lakini
si kawaida…mama ndiye mlinzi wa nyumbani…’nikasema
‘Sasa
huyo mama kuna siki atanitafuta….’akasema
‘Utakwenda
wapi…?’ nikamuuliza
‘Wewe
kaa hivyo hivyo, ngoja niondoke, wasije kurudi hao mabosi, madamu wangu
nampenda lakini ..unajua kuna kipindi tunakaa naye ananisimulia mambo mengi,
..lakini kuna kipindi haeleweki, kila unachokifanya hakionekani…akiona mume
wake akinitupia jicho, basi keshabadilika, ni nani kasema anamtaka mume wake
mzee yule..mimi nina mipango yangu, …hahahaha,.’akasema akicheka kwa dharau
‘Lakini
wewe si ulisema, wanakusifia kuwa wewe ni jembe, unafanya kazi sana,…’nikasema
‘Ndio
hivyo, kwa hilo, kila mtu ananisifia, sio madamu, hata mzee mwenyewe, lakini kazi ukimaliza, hawakosie cha kunisema,
mara mimi ni muhuni, mara mimi napendelea mambo ya kishirikina, , mara tumeleta
matatizo kwenye familia zao, yaani karaha,kashfa, sasa mimi sio mtoto mdogo,
nayasikia, yananiuma, mpaka lini…kwa kifupi maisha kaa haya, hayana uhakika, na
alishaniambia, siku yoyote atanitimua kama hanijui…’akasema
‘Lakini
angalau kwako kuna unafuu, sio kama kwangu…yaani kuna muda nafikiria kukimbia,
niondoke kabisa, unaweza ukajitahidi kufany akila kitu, lakini watoto wa pale
ndani, wale mabinti, wanaharibu, wanachafua, maana wao wanataka kula na kulala,
..ndio maana hawaolewi. Na mama yao anawatetea, sasa hata mimi hali kam hiyo
inanikwaza, lakini ndio maisha utafanyaje, hata hivyo, hata mimi nitakimbia,
nitaondoka hapo nyumbani…’nikasema
'Sasa
ukimbie na hali kama hiyo uende wapi …?’ akaniuliza akinikagua tumbo
'Popote,…ipo
siku, mungu atanionyesha njia, yaani hata sijui, hakuna anayenionea huruma kazi
zote nafanya mimi, nachoka sana, kuna muda nahsi kizungu zungu , kutapika,
nakimbia kujificha mpaka hali hiyo inakwisha, najua wakiniona nipo hivyo,
itakuwa njia ya kunifukuza, aah, ni shida kwakweli …’nikasema
'Umeonaeeh,….ndio
hayo matatizo yanayonikuta mimi, ila kwako, haaah, unalo….nilikushauri awali
uiotoe hiyo mimba ukakataa, sasa kazi unayo…sasa sikiza nikuambie mpango wangu….’akasema
'Mpango
upi huo…usiwe mpango mbaya, mimi sitaki matatizo…?’ nikamuuliza na yeye kwanza
akaangalia kule sokoni kama ana mashaka fulani, , halafu akaniangalia na
kusema;
'Unauliza
eti mpango gani, …’akasema na kuaniangalia
‘Sawa
nimekuelewa, niambie sasa…’nikasema
‘Nikuambie
kitu, hawa watu, hata ufanye kazi kama punda, hata uwe mnyenyekevu kama
malaika, hata uwe mtiifu kama …sijui nani, hawatakutahamini kamwe, unanisikia,
hawa watu watakutumia, na wewe hivi wanakulipa shilingi ngapi, aheri ya mimi
mwisho wa mwezi nakinga japokuwa ni kidogo…’akasema
'Hawanilipi
chochote, wanadai mimi sina mkataba na wao,…mimi hapo nakaa kama nimefadhiliwa
tu, kama mgeni, na siku ikifika nitaondoka, yule mama mchungu wa pesa, kila
kitu anakupigia mahesabu, na ole wako usirudishe chenji, kwahiyo maisha
ninayoishi anayejua ni mungu peke yake….’nikasema
‘Sasa
sikiliza nikuambie huo mpango, lakini ole wako ufungue domo lako , huu
nimeshaufanyia kazi na utafanikiwa, ni wewe tu,….’akasema
‘Sawa
niambie…’kabla hajaongea mara nikaitwa, na nikiitwa, nawafahamu watu wangu,
wanataka niwepo mara moja, ikabidi niachane na huyo mdada, kuwakimbilia watu
wenzangu, na mdada akanipungia mkono akisema
‘Kwaheri
ya kuonana….’akaondoka
Niliwaendea
watu wangu na nilipowafikia tu mama mwenye nyuma akaniuliza
‘Ulikuwa
wapi muda wote huo,tunakutafuta hatukuoni, ..?’ nikaulizwa
‘Nilikuwa
naongea na yule mdada wa kule…’nikasema
‘Mumeanza
kudanganya tena eeh, sawa, ongeeni tu, na huyo mwenzako ni mjanja njanja, ngoja
akudanganye uhadaike, shauri lako…’akasema
‘Hakuna
kitu kibaya mama, nilikuwa naongea naye tu.
‘Sawa
ongeeni tu, na nilikuwa sijakuambia, ujiandae, safari yenu ya kwenda huko
kijijini inaiva, wewe na yeye mtandoka, sasa kama mlikuwa mnaliongelea hilo
mlipange vizuri, safari hii hakuna kurudi nyuma, ukazalie huko kijijini kwenu
mlipoyatoa hayo mashetani…’akasema huyo mama
‘Mama
kwanini unamuambia hivyo….’mtoto wake akasema
‘Kwani
uwongo mwenyewe anafahamu tumboni kabeba nini, na akijifungulia hapo nyumbani,
mtaambukizwa na nyie, na hatujui hilo shetani litakuwaje,…kama ni shetani
kweli, si itakuwa ni balaa…’akasema huyo mama
‘Mungu
anajua,…’mimi nikasema hivyo tu, siku hiyo kiukweli sikuwa na raha kabisa,
nikawa kama mgonjwa, kumbe safari imeshapangwa, sasa nitafanya nini…akilini
nikajipanga niende kuonana na huyo mdada, niusikie mpango wake, kama ni
kutoroka tutoroke wote, sasa sijui tutakwenda kuishi wapi.
Basi
siku hiyo ikapita, na nyingine na siku ya tatu sasa, nikiwa nyumbani, wenzangu
walitoka, nilikuwa sijisikii vyema, na nikiwa ndani, mara nikasikia wanzangu
wakirudi, na kabla sijatoka nje kuonana nao, mara, wakaja askari,
‘Kuna tena
jamani…?’ wakaulizwa
‘Tunamuhitaji
huyu mfanyakazi wenu wa ndani…’akasema
‘Kafanya
nini…? Huyo mama akauliza
‘Atuambie
mwenzake yupo wapi, …’wakasema
‘Mwenzake
yupi…?’ mama akauliza
‘Yule
mfanyakazi wa yule rafiki yako,….’akasema huyo askari, huku akinikabili mimi,
pale nilipo nilihis mwili ukinisha nguvu miguu ikawa kama imekatika kwenye
magoti.
‘Kafanya
nini huyu mfanyakazi …?’ akauliza huyo mama.
‘Kaondoka
hapo nyumbani, tangia jana, …na kuna kiasi kikubwa cha pesa hakionekani,
inaonekana ni yeye kazichukua hizo pesa na vito vya thamani vya huyo mama, na
rafiki yake mkubwa ni huyu mfanyakazi wako, tunataka tukamuhoji huyu mfanyakazi
wako kituoni…’wakasema hao askari.
‘Lakini
mna uhakika gani kuwa huyu anajua wapi huyo mwenzake alipokwenda…?’ akauliza
huyo mama
‘Tuna
uhakika, kwa mara ya mwisho , walionekana wakiongea hawa wawili kule sokoni,
NB:
Majanga
WAZO
LA LEO: Tuweni makini kwenye ushauri tunaopewa na watu wengine, kuhusu mikakati
ya maisha, tusikubali kwanza, kabla hatujafiria matokeo ya hiyo mikakati, kuna
watu wengine ni wepesi wa kubuni na kupanga mambo hata kama ni ya shari, na
kuwashikirisha wengine, nia ni kuingiza kipato. Jiulize kwanza kipato hicho ni
cha halali kinapatikana kwa njia ya halali, kama kuna mkono wa shari epukana na
mipango ya namna hiyo. Tumuome mola wetu atupe njia ya heri, na kupata riziki
za halali
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment