‘Ni
nani hao waliingia …mbona huwataji?’ akaulizwa mama Ntilie akiwa na hamasa ya
kujua kilichotokea, lakini mume wa mtu hakujibu swali hilo kwa haraka, ….kama
vile anaogopa, kama vile tukio hilo lipo mbele yake.
‘Unajua
siku ile nilitarajia kuwa kijana wangu atakuja, kama alivyopanga,..kuwa ikipita
siku saba, hajapona basi atamwambia mama yake, na sio mama yake pia na babu
yake,…mimi sikutarajia kuwa kijana atakuja mapemda hivyo,…. namfahamu sana
kijana wangu, pamoja na hayo yakliyotokea, lakini yeye, ana mapenzi sana kwa
wazazi wake.
'Baba
naona umegoma kuniondolea hilo tatizo ,ambalo nina uhakika ni wewe uliyelisababisha….’kijana
wangu akaanza kuongea, tulipokaa kwenye viti, huyo mwanamke mwengine alikuwa
bado nje akiongea na simu. Nilimtupia jicho huyo mgeni, ambaye sikuwa
nimemtambua vyema, na sikupenda mambo hayo yaongelewe mbele ya mtu mwingine.
'Subiri
kijana wangu tutaongea mambo hayo baadae, huoni kuna mgeni hapa…..'nikisema
nikiwa na maana asiongee hayo mambo mbele ya huyo mgeni , lakini ilikuwa kama
nampandisha jaziba za kuongea zaidi.
'Mzee
hili halina kusubiria, maana nipo kwenye hali mbaya, natamani ninywe sumu tu,
kuliko hii aibu ninayokumbana nayo ambayo wewe ndiye chanzo chake….’akasema
kijana wangu.
'Kwanini
unasema hivyo mwanangu, mimi sikupenda yakukute hayo…na hata mimi linaniumiza
sana, lakini bado nalihangaikia hilo swala, tatizo mama yako haamini mambo haya
ya kienyeji, kama angetoa ushiriakiano wa kutosha tungeshalimaliza kabisa hili
tatizo…, wewe hujui tu…’nikasema
'Najua
, usijaribu kukwepesha ukweli, najua haya yote yametokea kwasababu ya kuutaka utajiri…’akasema
‘Mwanangu
nielewe hapo..mimi sifanyi mamabo kwa masilahi yangu mwenyewe…kama nilifanya
jambo ujue ni kwa ajili ya familia yetu..kama ni utajiri, lakini uwe kwa
familia yetu…’nikasema.
‘Ina
maana baba kweli unathamini utajiri kuliko mimi mwanao, upo tayari kuizalilisha
familia yako, ili tu utajirike, upo tayari kumfanyia mama mambo mabaya ili…..’hapo
kijana akashika kichwa kwa kusikitika.
'Wewe
unaongea nini mambo hayo, kwanini,…huoni kuna watu hapa hawafai kusikia mambo
ya kifamilia, ….’nikasema na kijana bado alikuwa kashikilia kichwa na
kuinamisha kichwa kabisa, hataka kuniangalia.
'Huyu
anajua kila kitu, bila ya yeye nisingeliweza kuyajua haya yanayoendelea humu
ndani, nimemuamini kwa vile kila alichonielezea kimetokea humu ndani,
ninavyoteseka usiku na zaidi ni kuwa huyo mtu anayemuelezea kuwa ni adui yake
nimeshamuona mara nyingi mkiongea naye, na simuamini huyo mtu kamwe…hata yule
mdada wa kwanza alinisimulia kuhusu habari zake…’akasema huyo kijana.
'Ni
nani huyu kwani…?’ nikauliza sasa nikianza kuingiwa na mashaka naye, nikamtupia
jicho, na yeye akawa kanikazia macho, ..mimi nikagwaya na kuangalia pembeni.
'Baba
usitake nifanye kitu kibaya, na kabla ya kukifanya hicho kitu, nitahakikisha
mama ameyafahamu hayo yote uliyoyafanya humu ndani, najua ana wakati mgumu na
yeye najua na yeye anahangaika kujua humu ndani tumeingiliwa na kitu
gani..hajui kuwa adui anayemtafuta wanaishi naye chumba kimoja…’akasema
'Sikiliza
kijana wangu, hawa watu ndio wachonganishi,usiwasikilize, hawa ndio wanaovunja
ndoa za watu, hawa ndio waoingia kwenye familia na kuzifanya zisiwe kitu
kimoja, usiwasikilize kamwe..’nikamwambia kijana na kijana ni kama hakunisikia
akasema;
'Baba
sio swala la kuambiwa, kwani hali halisi haijionyeshi, kwani mimi sina matatizo,
je haya matatizo yametokea wapi, hebu niambie wewe baba, si nilikuja
nikakuambia nina matatizo hayo, umenisaidia nini mimi, zaidi ya kuhangaikia
utajiri wako unaoutaka …kama ni utajiri sawa, utafute kwa njia zako, kwanini
unaniumiza na mimi, kwanini unamutesa na mama, kwanini unawatesa watu wengine
baki…binti wa watu kawakosea nini…’kijana akasema.
'Hayo
matatizo yako nitayashughulikia, kuna mtu namuamini sana, tutayamaliza, usiwe
na wasiwasi ,haina haja ya kutefuta watu wa pembeni, watu ambao hawana huruma
na familia yako..haya yataisha, nakuahidi mwanangu..’nikasema
'Huyo mtu
unayemuamini ndio huyo mchawi wako wa usiku…’kijana akauliza na kunifanya
nishtuke, na kumtupia jicho huyo jamaa, huyo jamaa alikuwa habandui macho
kwangu, unafikiri ana kitu hataki akikose kwangu.
Hapo, hapo nikahisi kuwa huenda huyo jamaa
ndiye kamuambia kila kitu huyo kijana yawezekana ni mganga wa kienyeji,..au
hata sijui ni nani,niliiona ni sura ngeni kwangu, sikuweza kuvumilia, nikasema;
‘Hebu
kwanza tutambulishane huyu ni nani, na huyo huko nje anayeongea na simu muda
wote huo ni nani…?’ nikaulizai
'Baba
kwanza tumalizane na hili langu, nilikupa siku saba, na siku saba zimekwisha,
sioni mabadiliko yoyote,…niambie unataka nini kwangu, unataka nijiue…au………?’
kijana akauliza
'Samahanini
kidogo, naombeni niwakatize kidogo, samahan sana mzee mwenzangu, unajua kijana
kakimbilia kukulalamikia badla ya kunitambulisha mimi kuwa ni nani..ndio
utaratibu ulivyo, lakini naona matatizo aliyo nayo yanamnyima amani…’akasema
huyo mgeni.
'Wewe
ndiye umemdanganya kijana wangu kuhusu hayo anayoongea…?’ nikamuuliza sasa
nikiwa nimekunja sura ya hasira.
'Nimemdanganya
au ni kweli, hayo aliyoongea ni kweli tupu, niambie uwongo wa hayo aliyoyaongea
ni upi,…yeye, alikuja kwangu akiwa na shida zake, kaelekezwa kwangu, kwanza
tuliwasiliana kwa simu, nikamwambi akarubuni nitakuja huko….na nikawa
nimefika..’akatulia kidogo.
‘Basi
nilipofika hapa nikawasiliana naye, nikamwambia aje tukutane, akaja akanisimulia matatizo yake, na kwa bahati
nzuri, alikuja sehemu sahihi, kwasababu huyo mtu anayekusaidia hadi mkaingia
kwenye matatizo hayo, mimi namfahamu sana….’akasema
'Sina
mtu anayenifanyia mambo yoyote kama aliyoyaongea huyu kijana, hizo ni hisia
zake tu,..na wewe ndiye umemjaza maneno yenu ya kiganga ya uwongo…’nikasema.
'Huyo
mtu unaye…sio kwamba na kisia, au ramli au nini…huyo namfahamu ilivyo maana alikuwa
mwanafunzi wangu , aliletwa kwangu nimfundishe mambo ya uganga,… akaasi,
akaniibia hata mikoba yangu ya uganga…, na kwenda kujihusisha na mambo ya
kichawi badala ya kufuata yale niliyomfundisha,…huyo ndiye anayekutumia, lengo
lake sio zuri, anawatumia kwa masilahi yake binafsi….’akasema.
'Tafadhali,
hayo unayoyaongea ni uwongo, na sijui
yametokea wapi, nakuomba tafadhali tena sana, usimpoteze kijana wangu kwa mambo
yenu hayo ya kishirikina, …’nikasema.
'Sio mimi
ninayempoteza kijana wako…, tatizo wewe umeshatekwa akili, na huyo mtu, wewe ndiye unayempoteza kijana
wako kwa kumharibia maisha yake… na usipofanya juhudi utakuja kujuta, utakuja kumuharibu
kijana wako kabisa kabisa…, na maisha yake ya baadae yatakuwa ni ya
giza…atakuwa punguani…, na pia umeiharibu familia yako mwenyewe, , kwa kutumiwa
na huyo mtu, huyo mtu hana wema kwenu, akimaliza kuwatumia, atarudi kijini
kwake na ukimtafuta ataishia kuwazidishia mavumba ya kuwaharibu kabisa…’akasema.
'Sasa
wewe unataka nifanye nini…maana naona umeshamuhadaa kijana wangu na amekuamini
kuliko hata mimi baba yake..umefanya vibaya sana, fikiria kama angelikuwa
kijana wako kakufnyia hivyo ungelijisikiaje…na ni nini lengo lako,…, unataka mimi
nifanye nini …?’ nikauliza.
'Huyo
mtu.unayeshirikiana naye haaminiki, anachojali ni masilahi yake, anawaharibu
mabint za wenzake, ..uchawi wake unategemea sana kuwatumia mabinti, kweli si
kweli…kila siku mabinti wanaokuja hapa wanatumiwa kwenye mambo yao ya
kishirikina ya usiku, na mashetani na wachawi wenzake, hebu fikiria hilo kama
mzazi…’akasema hyo mzee.
'Mimi
sijui unachokiongea…’nikasema nikiangalia pembeni, lakini moyoni nilishaona
kuwa sasa nimepatikana.
'Kijana,
kama nilivyokuambia, huyu baba yako keshalishwa kiapo hawezi kusema ukweli, na
usipofanya kama nilivyokuambia, hutaweza kuokoka na hilo tatizo ulilo nalo, hili
tatizo lako asili yake ni kutoka kwa baba yako, wewe mpigie simu mama yako, aje
na babu yako apa, kabla muda haujakwisha, hao ndio watakaoweza kukusaidia
kutoka kwenye hili tatizo, huyu hataweza kukusaidia…’kijana akaambiwa.
Kijana
akamuangalia baba yake kwa amcho yaliyojaa hasira huku akitoa simu yake kwenye
mfuko wake, nikajua sasa keshatekwa na huyo jamaa, anamsikiliza yeye kuliko
mimi na nisipojitahidi kulizuia hili mapemaa, basi mimi nitafukuzwa kwenye
nyumba hii kama mbwa…
'Wewe mwanangu
ina maana umefikia hatua hiyo ya kumuamini mtu wa nje kuliko hata mimi baba yako, unataka kumuua mama yako kwa
shinikizo la damu, maana akisikia haya mambo ya kizushi ataishia kudondoka, kwa
shinikizo la damu, unajua jinsi alivyo…’nikamwambia huyo kijana wangu.
‘Baba
wewe ndiye unataka kumuua mama kwa shinikizo la damu, nimegundua kuwa wewe
hutujali tena…kwahiyo ngoja nimuite mama, maana yeye ana uchungui na familia
yake, yeye hawezi kuniumiza mimi kwa masilahi ya utajiri, au ubinafsi…’akasema
sasa akiwa anaanza kubonyesha simu yake kutafuta namba ya mama yake. Na huyu
mzee akawa ananiangalia mimi usoni.
‘Subiri
kwanza mwaanagu, niongee naa huyu mchonganishi…’nikasema, nikimuangalia huyo
jamaa machine, na huyu jamaa akawa ananiangalia bila kupepesa macho..
‘Wewe
mtu wewe….hebu niambie unataka mimi nifanye nini, maana hujaniambia
unachokitaka, zaidi y kuziei kutaka kuiangamiza familia yangu….’nikamwambia
huyo jamaa. Na kuwa muda huo kijana akswa kaishikilia simu yake tayari kumpigia
mama yake. Niliangalia kuhakikisha kuwa simu hiyo haipo hewani.
'Lengo
la kuja hapa ni kutaka kumsaidia kijana wako, aondokane na hilo tatizo alilo
nalo, ukiangalaia utagunduaa tatizo hilo ndilo ulikuwa nalo wewe, sasa
limehamia kwa mtoto, iweje matatizo yako ya kizee, yahamie kwa kijana mdogo
kama huyu, kama sio hayo mliyoyafanya wewe na huyo mwenzako…’akasema huyo
jamaa.
‘Sasa mimi
nimekuja kumuokoa huyu kijana na kuikoa hii familia kutoka kwenye mikono ya
huyo mchawi ambaye anajifanya kuwa anakusaidia kumbe anakutumia tu….’akasema.
'Kumsaidia
kijana wangu, safi kabisa, kama ni hivyo basi kwani kuna tatizo gani hapo, mimi
sijakukutaza, sikuelewa dhjumuni lenu, haya niambia mimi nifanye nini,…ila kwa
maoni yangu, tatizo hili la kijana ni letu tu hapa, tusimuhusishe mama yake
kwanzaa, huyo mama yake kwa hivi sasa yupo kwenye matatizo makubwa…,
ukimuongezea na hili utamuua kabla muda sio wake…wewe humjui mke wangu
…………….’nikasema.
'Ni
hivi ili niweze kumsaidia huyu kijana, natakiwa nipambane na huyo mchawi, nim-malize
kabisa, ili niweze kuchukua mikoba yangu ya uganga wangu ambao aliniibia na
humo ndio nitapata mwongozo wa kuweza kumtibia huyu kijana, hayo ni mambo ya
kimizimu, yanahitajia kibali cha huo mkobwa, na hilo tatizo limefungwa kwenye
huo mkoba, huwezi kwenda kokote, ukatibiwa, …’akasema.
'Kwahiyo
kumbe, nimekuelewa wewe lengo lako ni kutaka kumtumia mtoto wangu kufanikisha
mambo yako…wewe unautaka huo mkoba wako, lakini hwezi kuupata mpaka umtumie
mtoto wangu, kwanini unafany ahivyo…’nikasema kumuambia huyo mzee.
‘Mambo
gani, ya kunifanikisha mimi, hapana, wewe sasa unataka kupotza muda,..mimi
nayafahamu sana hayo mambo, najua kabisa, wewe ulishalishwa amini kuwa usiseme
kitu…., ni sawa kwa mfumo huo, lakini amini uliyokula ni ya ulaghai,haita fanya
kazi, muhimu kwa sasa ni familia yako, usipoijali familia yako ukajali mali,
ukajali nafsi yako, wewe sio mzazi mwema…’akasema.
‘Wewe
ni mchonganishi, wewe ni mchawi kuliko hao wachawi unaowasema wewe…’nikasema
kwa hasira
'Kijana
piga simu kwa mama yako, kwa haraka, muda unakwisha….usipoteze muda zaidi,…huyu
mtu haelewi ninachotaka kukufanya, na haelewi ugumu na hatari ya hilo jambo,
unavyozi kuchelewa huyo jamaa huko alipo anazidi kuficha makucha yake..tatizo
linazidi kuwa kubwa, sasa hivi keshagundua kuwa anakaribia kushindwa,
nimeshamzunguka, ukichelewa ataficha kila kitu, mimi sitaweza kukusaidia baada
ya hapo….’akasema huyo mzee, na kijana akawa anataka kubonyesha kitufe cha
kuita kwenye simu.
Nilipoona kijana anataka kupiga simu nikamzuia…na
kumshika ule mkono alioshika simu, na mzee akataka kusogea kunizuia, hapo
nikasema kwa haraka;
'Sikilizeni
kwanza niwaambie, mwanagu usipige simu, kama kweli unampenda mama yako, kama
huyu mtu kaja kwa nia ya kukusaidia kweli , hata mimi nitafurahi, nitatoa
ushirikiani wote kuhakikisha wewe unapona,..lakini haya mambo akiyasikia mama
yako utamchanganya kabisa, mimi namjali sana mama yako huyu hamjali, hata
akipatwa na matatizo…’nikasema
'Kijana
piga simu, muda unakwenda sijaja hapa kupoteza muda wangu, nina mambo mengi ya
kufanya, kama hupigi mimi naondoka, na usije kujilaumu kwa hilo,….’akasema huyo
jamaa na kijanaa sasa akabonyesha kitufe cha kuita simu.
Mimi
kwa haraka nikaibetua hiyo simu mkononi mwa kijana, na ile simu ikadondoka
chini,..na nikasikia sauti ya mama yake akisema;
‘Halloh,
unasemaje, mbona huongei….’ Na simu ikatulia.
Kijana
akawa anainama kutaka kuichukua, nikasema;
‘Izime
hiyo simu tuongee,… maana mama yako alisema atakwenda hospitalini, huenda sasa
hivi yupo na docta, na wewe unataka kumsumbua, tusitake kumchanganya kichwa,
niambia wewe mchonganishi ulitaka mimi
nifanye nini, nipo tayari kutoa ushirikiano…’nikasema.
‘Kwanza
mkaribisheni huyo mama huko nje, yeye atatusaidia sana kwa hili jambo…’akasema
*************
Aliingia
mama mmoja na kusalimia, nikamkaribisha kiti, na alionekana kuwa na wasiwasi
kweli, akawa anaangalia huku na kule, na yule mzee akasema;
‘Huyu
ni mke aliyatalikiwa na huyo mchawi anayekutumia, huyu anamfahamu huyo mtu
kuliko mwingine yoyote, aliishi na huyo mchawi kwa muda, na kipindi kirefu
amekuwa akiona alichokuwa akikifanya huyo mtu, yeye akajaribu kumvumilia, kwa
tabia zake mbaya, lakini baadae alipoanza kutaka kumuingiza na yeye kwenye
uchawi wake, ndio akaamua kuondoka….’akasema na mimi nikamkagua huyo mwanamke
kwa makini,
‘Sasa
mbona unapoteza muda tena, unaona ulivyo muongo….’nikasema
‘Sio
muongo, huyu ndiye anaweza kukitafiti hicho kitu tunachokitafuta kwa maana yeye
anakijua wapi kilipo kutokana na mizimu ilivyo…tutaweza kukipata…?’ akamuuliza
huyo mwanamke, na huyo mwanamke akawa ananusua nusa kwa pua…baadae akasema;
‘Hapa
kuna kitu…’huyo mwanamke akasema sasa akiangalia muelekeo wa chumba anacholala
yule mfanyakazi wa ndani.
‘Huko
ndani au…?’ huyo mzee akauliza na huyo mwanamke akakubali kwa kichwa…na mzee
huyo akasema;
‘Yaonekana
huko ndipo mambo yalikwua yakifanyika, …sasa ndugu yangu tusipoteze muda, kuna
kitu tunakitafuta, kakiacha humu ndani, tukikipata hicho, tutaweza kupambana na
huyu mtu kirahisi tu, na hatimaye nitapata mkoba wa kuweza kumtibia
mwanao…’akasema.
‘Kitu
gani mbona mimi sikijui…’nikasema nilimuangalia huyo mzee na hatimaye huyo
mwanamke.
‘Unaweza
usikijue, lakini kumbuka siku ya kwanza alikuambia anataka kufanya nini ndani
ya hii nyumba….mimi nimeshaanza kujua wapi kilipo, lakini wewe mwenye nyumba,
unaweza kuturahisishia kazi…’akaambiwa, na mimi nikakumbuka huyo jamaa
alichimba shimbo nyuma ya nyumba, na huko chumbani anapolala mdada kuna kitu
alikipandikiza..juu ya kona ya chumba,…
‘Huku
ndani ni chumba cha msichana wa kazi,sasa hivio hayupo…’nikasema na mama
akatikisa kichwa kukubali, na huyo mzee akatoa kitu chake kwenye mkoba, kama pembe
ya mnyama, akawa anakiielekeza huko,
‘Unaturuhusu
kuingia huko ndani..?’ akauliza
‘Sawa
ingineni, mimi sijui kitu…’nikasema
Wawili
hao wakaingia ndani, na baadae wakatoka, na kusema;
‘Kuna
vingine havipo humu ndani, vitakuwa nje….’akasema na wakatoka nje baadae wakarudi,
na kusema;
‘Kuna
sehemu mbili hazipo kabisa humu ndani, kwenye eneo lako, kuna sehemu
kaziweka,…sasa ni hivi, hapa tupo kwenye mapambano, huyo jamaa siku zake
zinahesabika, sijui, kama ataweza…ngoja kwanza tuvitafute hivyo vitu vingine
kabla hajavificha, tunakwenda na muda,..’akasema na wao wawili wakatoka.
‘Sawa
fanyeni muwezavyo, ila mimi sijui kitu…’nikasema
Wakatoka na baadae huyo jamaa akarudi na
kusema;
‘Wewe
kijana ngoja tutafute hivyo vitu vingine, sisi tunaondoka ubakie hapa na baba
yako, usiondoke,..hakikisha baba yako hatumii simu, maana anaweza kumpa taarifa
ya kinachoendelea, akaharibu kila kitu,… kama tukifanikiwa tutarudi, ukituona
kimia ujue bado tupo kwenye mapambano…’akasema na wawili hao wakatoka mimi
nikabakia na kijana wangu.
Tulikaa
kimia, bila kusema neno baadae nikasema;
‘Kijana
wangu usiwaamini sana hao watu, kama wana nia ya kukusaidia kweli…., sawa, mimi
sina tatizo na hilo, ila hilo la kusema mimi nahusika, sikubaliani nalo kabisa,
ni waongo na lengo lao ni kuisambaratisha familia yetu….’nikamwambia kijana na
yeye akabakia kimia tu, nikataka kutoka nje , hapo akasema.
‘Umesikia
walivyosema, tusitoke humu ndani…, kuna mambo wanayafanya, usitake wakaharibu
hayo matibabu, mimi hapa nilipo sina raha, nateseka,..hivi wewe baba hunionei
huruma, nimefikia kutumia madawa ya kulevya, bila kupenda, ili kuondoa mawazo,
kumbe ndio yamezidi kuniharibu, baba unataka nini, unataka mimi nife kwanza nio
urizike,..kama hili halitafanikiwa, sina budu nitafanya hivyo unavyotaka wewe…’kijana
akaongea huku akitaka kulia.
‘Mwanangu
unataka nikuambie nini ili unielewe, hivi nikuulize kipindi kile unatumia
utajiri, unafurahi, ulijua huo utajiri umetokea wapi..mbona muda ule hukuja
kuniuliza, hujui ni vipi nateseka kwa ajili yah ii familia, tatizo wewe
unamsikiliza huyo mtu bika kuataka kunisikiliza mimi…niamini mimi, mimi ni baba
yako siwezi kufanya jambo baya kwa mtoto wangu mwenyewe…umenielewa…?’ nikasema
na kumuuliza.
‘Najua
ni wewe ulifanya hayo mambo ya kishetani, ukaniwekea mimi, na mimi sikujau,
sikuwa na akili yakuyatambua hayo, lakini baadae ndio ukaamua kuyachukua hayo
mambo , ili utajiri uhamie kwako, hayo nayafahamu yote, …ila ulichokosea ni
kuchukua na hali yangu,….unanifanya mimi niadhirike, nionekane sina maana ,
mabinti wengi sasa wananidharau, mchumba wangu kani….’akashika kichwa.
‘Sikiliza
kijana, hayo mimi nitahakikisha yanakwisha, hilo nakuahidi ilimradi uhai uwepo,
mimi nitakusaidia utapona, hata kama ni kuchukua sehemu ya viungo vyangu, hata
kama ni mimi kuharibikiwa, hata kama tutakuwa masikini, mimi ni baba yako mimi
ni mzazi wako,…lakini tuwe na subira..maana haya mambo sina uwezo nayo mimi,
ila yupo mtu ambaye ananisaidia…’nikasema.
‘Huyo
mtu si ndio huyo mchawi , huyo anayekutumia, huyo mchawi kawaharibu wasichana
wa watu, wewe hujiulizi, kama anawatumiwa watoto wa wenzake, anawaharibu bila
kuwajali, huoni jinsi gani alivyo mnyama,.. ..hata huyo mdada alikuwa akikaa
humu ndani kamfanyia mambo mabaya sana…’akasema
‘Mambo
gani..ambayo unayajua wewe aliyomfanyia huyo mdada, usiamini mambo hayo, ..au ni
nani kakuambia hayo mambo..unaona ilivyo, …keshakuingiza kwenye mambo ya
kishirikina, …ni mangapi kakuambia, hebu niambie..?’ nikamuuliza.
‘Huyo
mjaamaa ni adui wa huyo mchawi, wamekuwa wakiwindana tokea huko kijijini, na
wamefukuzana hadi hapa, na kaniambia huyo mdada aliyekuwa hapa kapandikiziwa
shetani,…’akasema
‘Kapandikiziwa
kwa vipi…uwongo huo…’nikasema
‘Sio
uwongo baba,..hayo ya kupandikiza shetani, hayakuanza leo,…wamekuwa wakimfanya
huyo mdada mambo mengi mabaya…hiyo mimba ya huyo mdada akikua, na hayo mambo
yao yanakuwa, yanamuingia huyo mdada, na huyo mtoto akizaliwa hatakuwa na hali
ya kawaida…’akasema
‘Unataka
kusema nini , kuwa huyo mdada, ohoo, nimegundua, kumbe wewe ulimpachika huyo
mdada mimba na lengo lenu ni kuiharibu au sio, niambie ukweli, mimi baba yako
nitakusaidia…’nikatulia.
‘Ukweli
upi baba, mwenyewe unajua, sina uwezo huo…labda ni wewe, labda ni wao, …ila
nijuavyo, kwa jinsi alivyoniambia, huyo mdada ni mke wa shetani –mbwa, na
wamekuwa wakimfanyia mambo mengi, wewe ukihusishwa PIA….’akasema.
‘Na wewe
pia…’nikasema halafu nikashtuka kuwa nimeropoka, nikasema
‘Na
wewe ukiamuamini…Ina maana kakuambia
hayo, kwanini akuambie wewe, sije kuniambia mimi,……?’ nikauliza
‘Akuambie
wewe wakati wewe unashirikiana na adui yake…..’akasema
‘Muongo
huyo anataka kukutumia wewe ili kupambana na adui yake, tunatakiwa hapa tuwe
makini…’nikasema
‘Baba
huelewi, naona wewe hutaki mimi nipone, kwa hivi sasa nipo tayari kufanya
lolote lile, ili nipone, najua wewe unachofanya ni kujiangalia hali yako,
lakini ukumbuke mimi sikuwa na matatizo, matatizo yako umehamishia kwangu, uone
baba ulivyo, kwanini unichague mimi, kwanini unanichukia hivyo,…’akasema
‘Nikuchukie
kwanini nikuchukie, hapana usifikirie hivyo mwanangu,na wala usije kuliongea
hilo, hakuna mzazi anayewachukia wanae…’ akasema.
‘Unaweza
kusema hivyo usoni kwa watu, lakini moyoni ikawa tofauti na ikipatikana nafasi
kama hii huwezi kusita kufany akama ulivyonifanyia mimi, lakini baba, hata kama
wewe hunipendi, lakini mimi nawapenda sana wazazi wangu, nimejitahidi sana
kuombea nyie na mama muishi kwa amani, na upendo, lakini sijui kwanini, na hili
sasa limetokea, yaonyesha kuwa wewe ndiye una matatizo baba….’akasema.
‘Kijana
wangu haya ni mambo ya kikubwa hutakiwi kuyaingilia,…utaumia muda sio wako,
nisikilize, mimi na mama yako tumekuwa hivi, ..kuna kukosana , badae
tunapatana, ni hali ya kawaida ya ndoa, hilo lisikuumize kichwa kabisa, unajua
nimekuelewa, mawazo hayo ndiyo yamekufanya upatwe na matatizo hayo uliyo nayo,
sio hayo anakudanganya huyo mtu,…umenielewa hapo…?’ nikauliza
‘Baba
mimi sijui…usitake kunificha …mimi ninachotaka nipone, kama huwezi kunisaidia
wewe, najua mama atanisaidia, …..’akasema
‘Hilo
mwanangu lipo mikononi mwangu haya ni mambo ya wanaume,mama yako hawezi
kuyafahamu, ngoja tuaone huyo mtu wako atafanya nini, akishindwa mimi nitalifuatilia
mpaka utapona, yatakwisha tu….’akasema
‘Kwahiyo baba, kama nisipopona hili tatizo ina
maana mimi sitaweza kuoa tena…?’ kijana wangu akaniuliza
‘Kwanini
usipone, ..tatizo huyo mtu kakuvuruga akili tu…mimi najua hayo mambo yapo na
yanapona,…niamini mimi utapona,…mimi nitahangaika kumtafuta bingwa wa hayo
mambo, tutayamaliza, kitu muhimu, iwe siri kati yangu mimi na wewe..hakikisha
mama yako halijui hili…’nikasema
‘Babu
nilimuambia ..kuwa nahisi kuwa nina tatizo la namna hiyo sikumfafanulia jinisi
ilivyo, akasema ni sababu ya madawa na
ulevi, niache nitapona, lakini sio kweli, najua kuna tatizo zaidi ya hilo, na
huyo mtu ndiye kanifichulia ukweli,……’akasema.
‘Hata
mimi naamini ni kwasababu ya madawa na ulevi,…muhimu wewe na subiria tu,…niamini
mimi haya mambo, nitayamaliza mimi mwenyewe…’nikasema huku moyoni nawaza
nifanye nini kumthibitishia kijana wangu kuwa mimi namjali kama mzazi wake, je
ni yupi nimuamini kati ya hao watu wawili, huyo mtaalamu wangu au huyo adui
yake.
‘Baba
mimi nakuahidi hapa, kama hili tatizo halitatafutiwa ufumbuzi mimi nitafanya
jambo…mtakuja kujuta wenyewe, lakini kabla ya kulifanya hilo jambo,
nitahakikisha familia nzima inafahamu kila kitu kilichowahi kutokea hapa kwenye
hii nyumba nitakiweka wazi,,…kuanzia yule binti wa awali, hadi huyu wa
sasa…kuwa wewe ndiye unayehusika, hilo baba sikufichi, …’akasema.
‘Kwanini
mwanangu unasema hivyo…kwanini huaniamini mimi….’akasema
Kabla
hatujaendelea na maongezi, mara simu ikalia, ilikuwa simu yangu nikaichukua,
alikuwa anapiga mke wangu,…
‘Halloh,…?’
nikaita na kusikiliza kwa makini…
‘Unasema
nini…kwani wewe upo wapi, hospiatalini …mmh, nakusikiliza…?’ nikauliza kwa
mshangao huku jicho limenitoka…..nikawa namsikiliza huku namuangalia kijana
wangu ambaye naye alivutika kusikia hicho ninachoambiwa na mama yake, lakini
asingeliweza kusikia kile mama yake anachokiongea.
NB: Ni
kitu gani kitakachoendelea.
WAZO LA LEO: Usimuombee mwenzako ubaya hata kama
ni adui yako, maana huwezi kujua , huenda huo ubaya anaokufanyia wewe unaweza
ukawa ni neema ambayo mola wako kakukadria kukupa huko mbeleni, muhimu ni
kuvuta subira na kuendelea kutenda mema.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment