Siku
hiyo sikuwa na raha kabisa,…na tofauti na siku nyingine ambayo nilipenda
kumfuata fuata huyo bint kwa siri, nikimuangalia alifanya usafi, siku hiyo
nilijaribu kumkwepa, na hata alipotaka kufanya usafi ndani kwangu, sikutaka
anikute hapo, nakumbuka siku moja alipotaka kufanya usafi, nilidhamiria
kumshika kwa nguvu, lakini nilipomkaribia tu, nikahis kichomi kikali tumboni, nikanywea na kwa haraka nikarudi
nyuma…
Kwa
huyu binti, kila nilipojaribu kumfanya chochote ilikuwa ni kama kuna mtu
anamlinda, kama ilivyokuwa kwa yule binti wa awali, nikakumbuka maonyo, kuwa
huyu binti naye ana mtu wake, na yule halikadhalika alikuwa na mtu wake, na
wote hao ni hao wachawi…
Basi
nikatoka hapo nyumbani, baada ya kuhakikisha kuwa kweli huyo mbwa hayupo, na
kwenda kwenye shughuli zangu na baadae nikampigia simu huyo mtaalamu nia ni kumuulizia kuhusu kijana wangu na je kulifanyika nini huo usiku na je kilichofanyika kimeweza, au kitaweza kumsaidia kijana wangu.
Nilipiga simu ikaita kwa muda baadae akawapokea na kuwa hewani,, nikajitambulisha kwake, akasema ameshanitambua mimi ni nani,...na sauti aliyotoa ilionekana ina uhai, nikamuuliza
‘Vipi
mtaalamu ulifanikiwa…?’ nikamuuliza
‘Nusu
nusu, kama nilivyokuambia, mkeo aliondoka mapema, na kijana wako pia..kwahiyo..mambo mengi yakashindikana kufanyika,..tukajaribu kumtuma mbwa wetu usiku huo, akaone
alipokwenda huyo mkeo, na tuone kama tunaweza kufika huko angalau kwa muda, lakini kilichotokea huko ikawa ni mkosi wa siku …’akasema
'Mkosi !....mkosi wa nini...?' nikauliza
‘ Jamaa alinaswa....'akasema
'Alinaswa na nani sasa…?’ nikauliza
‘Hao
wakwe zako naona safari hii wamejiimarisha, jamaa alifika vyema na alipojaribu kufanya vitu vyake, akajikuta anaonekana...nguvu zake za kinga zikawa hazifanyi kazi, na hakuwa na jinsi, akapatikana,...na alaichukuliwa kwenda polisi na hata hivyo
watayaona maajabu yake…’akasema
‘Maajabu
gani…?’ nikamuuliza kama sijui
‘Tuyaache
hayo,…ila mbwa wanaye bado, nimeacha abakia huko kidogo, atatusadia mambo
mengine ya huko, na usiku atawatoroka, huyo hana shida, hawamuwezi…’akasema.
‘Atawasaidia
nini huko polisi, huyo mbwa…?’ nikamuuliza
‘Tatizo
lako hunijui mimi…lazima nijue wamepanga nini huko baada ya hilo
tukio….’akasema
‘Sawa
nimekuelewa…’nikasema hivyo, nikasikia akipiga miayo halafu akasema;
‘Haya
niambie unataka kujua nini zaidi, hayo mazungumzo mengine tuyaache
kwanza…’akasema.
‘Sawa mimi usiku huo mlipofanya hayo mambo
unajua siwezi kuona yanayotendeka ila wewe ndio unanisimulia, je hmlifanya
nini..na je mlifanikisha hayo mambo maana siku alizo nipa kijana wangu ndio
hizo zinakwisha…’nikasema.
‘Nashangaa
leo unataka kuyafahamu mwenyewe tofauti na siku nyingine,….’akasema
‘Ndio
wewe huoni hali ilivyokaa sasa hivi…..’nikasema.
‘Japokuwa
mke wako alikimbia na kijana wako, lakini tuliweza kufanya baadhi ya mambo yetu,
hasa mambo yetu ya kujilinda, na huyo adui yetu, sasa yaliyotukwamisha ni mambo
yako, lakini mambo yetu yamekamilika….’akasema.
‘Mambo
yenu yapi sasa, na kama ni mambo yenu kwanini mje kuyafanyia hapa kwangu,
hamuoni mnanifanya niwe kwenye wakati mgumu, …na,…na…mke wangu…?’ nikamuuliza
na nilipotaka kuongea zaidi akanikatisha na kusema;
‘Nilikuambia
kitu, huyo binti hapo ndani ametufaa sana, kuanzia sasa kachukua nafasi ya yule
binti wa awali japokuwa sijakata tamaa, maana huyu hatanifaa mimi , kama mimi,…yule
binti mwingine alikuwa ni mke wangu, huyu sio wa kwangu…ila tumemtumia sana,…na
mambo mengi yamefanikiwa, na kijana wako, kama angelikuwepo hali yake ingelijirudia
kama kawaida…’akasema
‘Sasa
kwanini kwani ni mpaka awepo ndio hayo mambo yafanikiwe…?’ nikauliza
‘Sasa
tutamfanyia vipi ili kuhakikisha karejea kwenye hali yake, ilitakiwa yale
matendo ya awali yafanyike, mkabidhiane tena, na …hilo litasubiria, utajua
mwenyewe jinsi ya kumweka sawa, ukitaka tumnyamizishe tunaweza lakin
hamtapendezewa na hiyo hali hasa mke wako…’akasema
‘Na,
na yuleo mbwa wenu atarudi tena hapo nyumbani…?’ nikamuuliza
‘Huyo mbwa , keshamaliza kazi yake kama mbwa…, kuna
kazi alitakiwa kuifanya hapo ndani ya kafara maalumu la kuunda silaha mpya,
kombora litakalomumaliza kabisa huyo adui yangu…na limefanikiwa,….’akasema
‘Kwa
vipi huyo ni mbwa au sio…mumemfanyia nini na huyo binti wa watu…?’ nikauliza
‘Hahaha..huyo
ni mbwa kwa uoni wenu wa macho, huyo ni shetani wetu , yeye anaweza kujigeuza
mbwa, paka, nk…na tumemtumia kwenye mambo hayo makusudi ili kuficha ukweli…, na
yeye kwa hivi sasa ndiye bwana wa huyo binti ….’akasema
‘Bwana
wa huyo binti, binti yupi…una maana gani
kusema hivyo?’ nikauliza nikiwa na mashaka.
‘Binti
yupi tena si huyo hapo nyumbani kwenu, yeye katunukiwa na huyo shetani-mbwa
wetu..kwahiyo hana budi kumtumia huyo binti, na kupitia kwake tutafanikisha
mambo mengi sana nyota yake ina nguvu sana kwenye makafara yetu…usiku huo
tulimchukua huyo binti hadi kuzimuni, akachezewa huko kuwafurahisha hao mashetani ..’akasema.
‘Mungu
wangu, kwanini mumefanya hivyo, huyo binti wa watu ni masikini tena yatima, sio
vizuri jamani…’nikawaambia
‘Sisi
hatuangalii huko, mambo yetu ni kishetani, na yanafuata mkonodo huo…wewe
ulitaka utajiri hukuupata,unafikiri uliupataje, ni njia hizo hizo…..sasa
umetaka mengine…haya tufanyeje…ni lazima mambo hayo yafanyike ili mambo yetu
yafanikiwa, ukiwa na huruma hiyo hawezi kufanikiwa….’akasema
‘Hapana,
hilo mimi sipo na nyie kabisa…’nikasema
‘Hupo
na sie k, kwahiyo unataka kijana wako aendelee kuwa hivyo, maana bila hayo
yaliyofanyika kijana wako hataweza kurejea kwenye hali yake, huyo ndiye
atatusaidia kila hatua,… si ndio unataka hivyo…mtoto wako arejee kwenye hali
yake, au unataka nini…?’akauliza.
‘Kwa-kwa-hiyo
mumefanikisha kuhusu mtoto maana hapo sijakuelewa…?’ nikauliza nikiwa sina hamu
maana kila hatua najikuta naingia kwenye mambo mabaya zaidi,..
‘Tutawezaje
kuanikisha wakatu wahsuika wakuu
hawakuwepo, mke wako, haya kijana wako, ..tulijaribu kuwafuatilia, mtumishi
wangu ndio akanaswa huko,..unajua nikuambie kitu, .sio kila mahali tunaweza
kuingia, …’akasema.
‘Kwahiyo
lini tena, maana siku zimekwisha unajua sitaki kijana wangu anifikiri vibaya,
hivi sasa anaonekana kujua kila kitu sijui ni nani kamuambia…’nikasema.
‘Ndio
maana tunatakiwa kumnyamazisha hadi haya mambo yakamilike…’akasema.
‘Una
maana gani kumnyamazisha…?’ nikauliza.
‘Anakuwa
kama zezeta, hawezi kufikiri wala kuongea , …ni swala la muda mfupi
tu…vinginevyo hiyo hali inaweza ikakujia wewe, na ikikujia wewe ndio basi tena,
kwahiyo ni bora kuifanya hivi sasa kwa kijana wako ili iwe rahisi kwetu
kufanikisha haya mambo, asitusumbue…’akasema
‘Hapana….kwa
kijana wangu sitaki tena, sitaki muiguse familia yangu tena, imetosha…’nikasema
‘
‘Hahaha hapo ulipofikia huwezi kurudi nyuma .
kama nilivyokuambia kuachana na haya mambo ni mmoja wenu afe….hilo sitanii
ndugu yangu…na hivi huoni kuwa ile nyota imeshaanza kurudi kwa wenyewe…wenzako
pia wanahangaika kivyao, usipojitahidi, sio kwamba tu utafirisika kabisa,
lakini pia unaweza kuwa kichaa, na ikitokea hivyo umekwisha..…’akasema.
‘Oh…..mtaalamu,
fany aufanyavyo, kijana wangu arudie hali yake, usijali kuhusu mimi…na mke
wangu arudi nyumbani, …lakini kwa hivi sasa usifanyie nyumbani kwangu…’akasema.
‘Kwangu
hatuwezi kupaacha, labda umuhamishe huyo binti kwenda sehemu nyingine ambayo
tunaweza kumpata kiraisi…umenisikia…’akasema na kukata simu.
Mimi
…pale nilipokuwa nimekaa nilianza kujisikia vibaya, ina maana mimi nimeolewa na
mbwa-shetani, na usiku walinipeleka makaburini,maneno hayo yalinichefua zaidi
na zaidi hapo sikutaka hata kumuangalia huyo mzee, maana hata mimi nilishaanza
kujihisi kama huyo mama, moyo wangu ulishaanza
kumchukia huyo mzee, lakini sikusema neno.
Nikasogea
hadi dirishani kupata hewa, naona wote wakageuka kuniangalia mimi.
‘Upo
sawa…?’ akaniuliza mama Ntilie.
‘Nipo
sawa..hewa ilikuwa nzito…’nikasema
*********************
‘Tuendelee…?’ akauliza huyo mzee, alipoona
mimi nahangaika…
‘Endelea
lakini naomba uongee mengine sio hayo ya kunihusu mimi…’nikasema nikijaribu kutafuta
hewa, maana nilikuwa kama nakabwa, pumzi ilikuwa ndogo.
‘Muache
aendelee ni vyema ukajua walichokufanyia, ili ujue ni kwanini mimi nakataa
kumsamehe huyu mtu, tamaa zake ndio zitufanye tuzalilishwe, unajua ni mangapi
waliyokuwa wakiyafanya kwako na kwangu, na hujui ni nini hatim,a ya iyo mimba
yako , …’akasema.
‘Kwangu
mimi inatosha…’nikasema nikitikisa kichwa nilitaka nitoke nje kabisa
‘Ni
mengi yalifanyika, baadae wakikutumia wewe, na kipaba zaidi licha ya mimi
kugoma kuwa wasifanye hayo mambo yao hapo nyumbani kwangu, lakini waliendelea
kuja, na bado walinitumia nikisimamia …’akasema.
‘Ina
maana kuna mambo mengine yaliendelea kufanywa kwa huyo binti…?’ akaulizwa.
‘Wanasema
walikuwa wakitengeza shetani ambaye atakuwa mlinzi wa kupambana na hayo
yanayoendelea kati yake na huyo adui yake, na wamegundua kuwa huyu binti ana
damu itayowezesha hayo,..kwahiyo waliendelea naye kila hatua, kwani walihitajia
shetani ambalo litazalishwa kupitia kwenye tumbo la huyu binti….’akasema.
‘Oh….’nikajitizama
tumboni, na kuhisi tumbo likianza kuniuma, nikahisi kizungu zungu, kutaka
kutapika…
‘Ina
maana kilichopo tumboni ndio hayo mambo yao..?’ akauliza mama Ntiliye
‘Mimi
kiukweli yaliyokuwa yakifanyika baadae sikutaka kujua, nilishaanza kuogopa,
mambo yalishaanza kuniwia magumu kwangu, na kijana wangu tukawa hatuonani akija
anaongea na hyu binti anaondoka, na mama yake akija anaongea na huyu binti
anaondoka zake kwahiyo, ili niwasiliane nao ni kwa kupitia huyu binti, mimi nikawa kama nimetengwa
‘Hawakukuambia kitu gani kinaweza kupatikana
kwa huyu binti, kuwa atazaaje ….?’ Akaulizwa
‘Hawakuniambia.
Ila walisema iwapo atapata ujauzito kuna mambo alitakiwa kufanyiwa kabla
hajajifungua….’akasema.
‘Je
aliwahi kufanyiwa hayo mambo…?’ akaulizwa.
‘Mhh..hapana
kwa jinsi nijuavyo mimi…’akasema.
‘Ikawaje
sasa..maana ulisema kuwa kijana wako alikupa muda wa kumrejeshea hali yake..au
nguvu zake, iliwezekana au ilikuwaje, kijana wako alipokuja kwako, uliwezaje
kuliweka hilo sawa, na je hajaweza kurejewa na nguvu zake mpaka sasa…?’
akaulizwa.
‘Haikuwezekana
, maana baada ya hapo, huyu mtaalamu alisema mwenzake kaharibu kila kitu chake
alichokuwa nacho, na sasa iliyobakia ni kuweka mitego yake anayoijua yeye
mwenyewe, ili kumnasa huyo adui yake, na
hiyo mitego inahitajika kuwekwa kwenye nyumba ambazo huyo adui wake huwa
anapita mara kwa mara wakiwindana…ndio maana akawa anawaomba hao akina mama,
kwa kusingizia kuwa kuna mazindiko na kitu kama hicho,…’akasema.
‘Kumbwe
hakukuwa na mazindiko kama alivyotuambia sisi, sasa kulikuwa na kitu gani …?’
akauliza mke.
‘Hakukuwa
na mazindiko, yeye ndio alitaka kuyaweka hayo mazindiko kwa ajili ya kupambana
na adui yake, na kama mlivyoona hakufanikiwa, mwenzake alimuwahi…kipindi hicho
yupo huko Ocean road, na huko ndio mlikutana naye…yaliyotokea huko mnayafahamu
zaidi kuliko mimi.’akasema.
‘Sasa
swali, je ina maana hii mimba ya huyu binti ndio huyo shetani wa kupambana na
huyo adui yake na ina maana ni mimba ya huyo mbwa -shetani…?’ akaulizwa.
‘Hapo
mimi sijui, lakini kwa mara ya mwisho kuongea na huyo jamaa aliniambia hivyo,
kuwa ni moja ya silaha zao za kupambana na huyo adui wake, sasa zaidi ya hapo,
mimi sijui, na wala sikuwahi kuongea naye kuhusui kuwa hiyo mimba ni ya nani,
zaidi ya kauli hiyo, kwa kipindi hicho nilikuwa na mawazo jinsi gani nitaongea
na kijana wangu…’akasema.
‘Kwa
kifupi unataka kusema kuwa hii mimba sio ya kawaida, mtoto aliyepo tumboni sio
wa kawaida, atajifungua kioja au sio…?’ akaulizwa.
‘Mimi hapo
siwezi kujua, naomba mnielewe hivyo, siwezi kudanganya, maana sikupata muda huo
wa kuongea na huyo mtaalamu tena…baada ya tukio lililotokea….’akasema.
‘Kwahiyo
hapa tunabakia na mambo mawili makubwa, la kwaza ni hilo la mimba ya huyu binti….,je
atasaidiwaje maana hapo alipofikia hakuna jinsi ni lazima ajifungue, na hatujui
atajifungua kitu gani, je hakuna jinsi gani nyingine ya kumsaidia,…hiyo ni kazi
yako wewe uliyesababsiha hili..au sio jamani….’akauliza mke wake.
‘Ni
kweli, wao ndio sababu na wao ndio wanatakiwa wajue jinsi gani ya kumsaidia huyu
binti…’akasema mama Ntilie, mimi nikawa kimia tu, sikuwa na nguvu ya kuongea
kabisa.
‘Lakini
la pili ni kuhusu kijana wako, je
alikuambiaje mlipokutana baada ya siku saba kupita, na yeye utamsaidiaje
kurejesha hali yake,…?’ akaulizwa.
‘Ni
kweli siku saba zilikuwa zimeshapita, maana hapo kulipita siku mbili tatu hivi
baada ya jamaa kusema mwenzake kamuwahi kaharibu kila kitu chake, na ilitokea
kabla haijafika hiyo siku ya saba.,..’akatulia.
‘Kijana
muda wote huo alikuwa haki hapo nyumbani kama nilivyosema, alikuwa akikaa na
babu yake, na huko hawakuwa hivi hivi, walikuwa wakimuhangaikia, kwa namna
wanayoijua wao,kwani alimuelezea babu yake kuwa kapatwa na mambo ambayo
hayafahamu na yamemuathiri..wakakimbilia kumuambia labda ni sababu ya madawa ya
kulevya..
‘Babu
sio madawa ya kulevya, …’akasema
‘Sasa
unahisi ni nini…?’ akaulizwa
‘Babu
nimepimwa haospitalini, wanasema eti kwa umri huo nina martatizo ya
kisukari…mara shinikizo la damu, ni kweli babu, hayo sio magonjwa ya wazee…?’
akauliza.
‘Hahaha,
mjukuu nikuambie kitu, sasa hivi ni wewe unajiumiza, kwanini unatumia vilevi,
madawa ya kulevya, hujui athari zake ndio hizo…’akaambiwa
‘Babu
mimi sikupenda iwe hivyo..ni hali ya hapo nyumbani …wazazi wangu nawapenda
sana, lakini yanayotokea hapo yananipa mawazo sana, naamua kutumia hivyo
vilevi…’alimuambia babu yake hivyo.
‘Hayo
mazungumzo, niliyapata kutoka kwa huyu mama yake hapa….nashukuru kuwa wao
hawakuweza kukimbilia kusema kuwa kijana kafanyiwa mabaya, kwahiyo ilikuwa ni
swali gumu kwangu, nikijiuliza je kijana wangu aliambiwa na nani hayo mambo…
Nilikuwa
na wakati mgumu sana na siku saba zikapita bila mchezo,…na kijana hajapona, na
aliahidi kama asipopona, atamwambia mama yake na atamwambia mbele ya babu na
bibi yake,…
Ilikuwa
siku ya saba nikiwa nipo kwangu, siku hiyo sikuweza hata kutoka kwenda kwenye
shughuli zangu, siku hiyo mke alikuwa hayupo , na kipindi hicho hata huyu binti
hayupo, maana kuna kikao kilifanyika nyuma ikashauriwa huyo binti aondoke, ni
kipindi hicho hicho, nahangaika….na nashukuri kuwa hata kwenye hicho kikao
kijana wangu hakuweza kuliongelea hilo,
Sasa safari hii sizani kuwa atanisamehe…na
nitamuambia nini, ili anielewe, hapo nipo mimi mwenyewe nawaza na kuwazua,
mtaalamu anaumwa hawezi kunisaidia tena, je akifa kabla hajamsaidia kijana
wangu itakuwaje, nitakwenda kwa nani, ..nikawa najiuliza maswali mengi kichwa …na.mara
nikasikia mlango ukigongwa, maana kwa usalama nilikuwa nimefunga milango,
nikajua ni mke wangu.
Nikakimbilia
kufungua mlango, na mlango ulipofunguka …moyo ukanilipuka utafiri nimeona kitu
gani,...nilibaki nimeduwaa, ….
NB: Ngoja
niishie hapa kwanza
WAZO LA LEO: Familia hujengwa na mshikamano wa
wanafamilia, wote wawe kitu kimoja na lengo moja, kusiwepo na sintofahamu ya
kila mtu anakuwa na jambo lake binafsi, kwa kufanya hivyo ni kumpa nafsi
shetani, ambaye raha yake ni kuhakikisha ndoa hazisimami, ndugu kwa ndugu
hawaelewani…...
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment