Yule
jamaa aliposikia gari limesimama nje, akatoka mbio mbio uso wake ukionyeha
furaha sana, sisi tukabakia ndani tukimaliza kupanga vitu vyetu, na ilichukua
muda , jamaa akawa anaongea na huyo mgeni ambaye bafo tulikuwa hatujafahamu ni
nani, japo tulihisi huenda akawa ni huyo mke wa huyu jamaa kama ni kweli, ..
Tulisikia
sauti sauti za kuongea lakini hatukuweza kufahamu wanaongea nini hasa, na
baadae mlango ukafunguliwa , aliyeingia alikuwa huyo jamaa akiwa na tabasamu
tele mdomoni. Aalipofika ndani akasimama na kugeuka nyuma, hamuoni mwenzake,
akasita kidogo, lakini akawa anaongea hivi;
‘Jamani,
natumai muda umefika, najua nimewasumbua sana, na pia nimemsumbua mke wangu,
kumbe alikuwa kwenye kikao muhimu cha matatizo ya familia ambayo kisa ni mimi,
madeni yamekuwa mengi, matatizo ni mengi kweli kweli, na ..aah, kisa ni mimi,
lakini nina imani sasa, kwa vile nitakuwa nimepona natumai hivyo, nitayalipa
hayo madeni kwa mikono yangu hii..’akasema akionyesha mikono yake miwili.
Sasa
akawa anaangalia nje, akimsubiria mwenzake lakini kukawa kimia, huyo mwenzake
hakuonekana, sisi tukabakia kuangalia mlangoni kwa hamasa, na huyo jamaa
alipoona kimia, akaita
‘Mke
wangu mbona unasita kuingia ndani, ingia, umuone huyo bint, ninayekuambia,
ndiye sababu ya kupona kwangu, na ndiye sababu hal zetu zitarejea tena, nina
imani hiyo, ingia, mbona …..’akanigeukia na mimi nilikuwa nimesimama
nikiangalia huko mlangoni, na huyo anayesema ni mke wake hakuingia mara moja, ikawa twajiuliza kuna nini tena huko nje mbona
huyo mtu haingii. Nikaona niendelee na kazi zangu…nikawaacha, nikiendelea
kuingiza vitu sehemu tunapovihifadhia.
Wakati
narudia kuchukua vitu vingine mara nikamuona huyo jamaa akielekea huko nje,
kumfuata huyo mke wake, sijui kwanini huyo mke wake, amegomea huko nje,…
Mara
nikasikia huyo jamaa akisema;
‘Mke wangu unalia nini, yote hii ni mitihani
ya mungu haya yametokea kuwa fundisho kwetu, hasa mimi, kwanini unalia, ingia
kwanza tulimalize hili, na nina imani mengine yatakwisha tu kwa mapenzi yake
mola, nisamehe sana na nakuomba tuendelee kuwa pamoja, usichukulie hasira, na
mimi ni binadamu, kutelekeza kupo, nakuahidi hayo hayatatokea tena…’akasema.
;Hayo
hayatatokea, ni rahisi kusema hivyo au sio…lakini madhara yake utayalipaje, umwaumiza
watu wengi, hadi familia yako,..najua utasema hivyo kwa vile wewe unaitetea
nafasi yako, au sio,…aah, sijui kama nitaweza hili na hali irejee tena kama
awali,..sijui….’ilikuwa sauti ya kike.
‘Mke
wangu ulisema umenisamehe, sasa hayo yanakujaje tena…ingia kwanza tuyamalize
haya ya hapa, najua baada ya hapa hakutakuwa na matatizo tena, nakuahidi
hilo…’akasema huyo mume mtu.
‘Sawa,
..nakuja….’akasema
Baada
ya muda nikasikia hodi ya kike, nikajua wawili hao watakuwa wameshaingia ndani.
Kwa muda huo nilikuwa kwa ndani nikipanga vitu vizuri, moyoni nilikuwa na
hamasa sana nimuone huyo mke wa huyo jamaa yupoje, na yawezekana ni watu
wanaojiweza maana kaja na gari…
Nikawa
naharakisha kupanga viitu vyema, ili sije kuwa usumbufu wakati wa kuvichukua, sikutaka
kuharibu kazi yangu japokuwa nilikuwa na hamu ya kumuona huyo mke wa huyo jamaa,
nikamaliza, na niliskia huyo jamaa akimtambulisha mkewe kwa huyo mama, hapo
nikaamini kuwa ni kweli, maana bado tulikuwa tunamtilia mashaka, huenda hata
mke hana….
‘Huyu
ndiye mke wangu, niliwaambia nina mke mnzuri, unamuona..kakondoa tu kwasababu
ya matatizo, lakini …atarejea hali yake hivi karibuni…’akasema huyo jamaa.
‘Mke
wangu huyu ni mama Ntilie amenifaa sana, chai nzuri,…na chakula, lakini mara
nyingi niliwa sili chakula hapa, maana nilikuwa natimiza wajibu wa kuzunguka
kuwatafuta niliowakosea,..na sikupenda kula mchana,…huwa nilikuwa nakunywa chai
ya nguvu, nikishiba mpaka kesho tena,..kwangu mimi, kiukweli ulikuwa mchana wa
toba, wa kuomboleza, ndivyo maisha yangu yalikuwa hivyo, baada ya kuwakimbia,
hayo nakumbuka sana….’akasema huyo mbaba.
‘Oh,
nashukuru sana, mama Ntilie, kama alivyokuita mume wangu maana tumehangaika
sana kumtafuta huyu mtu, mpaka ikafikia muda, tukasema basi huenda huyu mtu
hayupo tena duniani, jana tu tulikuwa kwenye kikao cha wanandugu kuamua hatima
yake, unajua tena mtu akipotea siku nyingi wengine hufikiria vibaya, na leo
ilikuwa kutoa maamuzi,…bahati ndio nikapata hiyo simu, sikuamini….’akasema huyo
mwanamke.
‘Walijua
nimekufa ee, watakufa wao kwanza…watu wengine bwana wanakimbilia kuona wenzao
wamekufa….walifurahi nimechanganyikiwa hawachakoma, sasa wanazua nimekufa,
wajinga sana hao watu…sasa nipo hai, na nkuja kivingine,…hivi hapa kuna slooni
karibu..eeh, ngoja…’jamaa akasema sasa akishika shika maywele yake akihis
vibaya
‘Sio
hivyo wewe mwanaume, ilikuwa, ni…ni namna ya kutafuta njia ya kuhakikisha upo
wapi na je upo salama…wewe fikiria umepotea muda gani, hujulikani wapi ulipo,…hivi
hata ingelikuwa wewe unaglifikiriaje,..na yote umayataka wewe mwenyewe…’akasema
huyo mwanamke.
‘Sawa,
mke wngu… mimi nipo salama kama unavyonioana na ni kwa mara ya kwanza leo
nimeweza kujitambua, waulize hawa watu ambao walikuwa wakiniona kwa siku chache
nilizoweza kufika hapa,…siku nyingine zote ilikuwa kama nipo gizani, sijijui
sijui nipo wapi,…na najua huku kupona sio bure , ni baada ya huyo mdada
kukubali kunisamehe, vinginevyo sijui ingekuwaje…’akasema.
‘Mdada
yupi huyo maana na wewe ulikuwa mwingi sana, umewakosea mabinti wa watu wengi
tu, sijui wangapi, kiukweli inatakiwa uwaendee wote mmoja baada ya mwingine,
maana bila hivyo…utakuwa bado, hujafanikiwa,..na ni kweli haya yote
yaliyokupata ni sababu ya uzandiki wako,, na tatizo ni kwamba madhara yake
yametukumba na sisi tusio husika na madhambi yako, yupo wapi huyo binti jamani
natamani nimuone …’akasema huyo mama akiangalia huku na kule.
‘Anakuja…’akasema
huyo mama na mimi ndio nikatokea..
**************
Unajua
ni maajabu sana, wakati natokea huyo mama mgeni alikuwa kageukia mlango
mwingine, akijua huko ndio nitatokea, sasa mimi nikatokea mlango mwingine uliopa
nyuma yake, aliposikia sauti ya nyayo zangu, ndio akageuka, macho yake
yakakutana na yangu…hata mimi mwenyewe nilipigwa na butwaa, kuachia yeye ambaye,
akabakia mdomo wazi, na macho kayatoa, ananiangalia tu…na kuniangalia, akawa
hanimalizi…
‘Ndio
wewe ….mungu wangu, ni wewe au ..hapana siamini…’akasema sasa akishika kichwa,
na hakuishi ahapo akapiga magoti, akasimama, akasogea , ikawa kama anatafuta
hewa, au siju anataka kukimbia…
‘Hata
mimi ilikuwa hivyo hivyo mke wanguu nilipomuona huyu binti…sikuamini kuwa ni
yeye….kabadilika eeh…lakini sura haipotei, unamuona alivyo, na nasikia….’akasema
mume wake, na kabla hajamaliza mke wake akamkatili na kusema;
‘Mungu
wangu,..ooh, unajua hii dunia, …samahani sana binti…niliambiwa huyu binti
kafariki…’akasema na akawa anatikisa kichwa, sasa akimuangalia huyo mama
Ntilia. Na kauli hiyo ikanifanya hata mimi nishutuke.
‘Nani
alizuia hivyo…unaona watu walivyo, mimi wanafikiria nimekufa, na huyo binti
naye walimzulia kuwa amekufa, kwanini wao hawajifikirii kuwa wamekufa…watu
wabaya kweli…ni nani huyo alikuambia hivyo…?’akaulizwa na mume wake.
‘Yaani,
akili hapa haipo sawa, na unajua aliyesema hivyo ni nani, alikuwa yule rafiki
yake, yule binti mwingine aliyeiba na kutoroka…na yeye anasema kasikia kwa watu…’akasema
‘Kwani
keshapatikana..?’ akauliza mume wake sasa akimuangalia muke wake kwa macho ya
hamasa.
‘Unacheza
na serikali wewe..na hata hivyo za mwizi ni arubaini, walitegwa wakanaswa,
utaiba utatumia zitakwisha, lazima utatoka tu…na cha wizi hakidumu, kamwe,…’akasema
huyo mama.
‘Oh
afadhali …kama wamepatikana eeh, sasa wataenda kunyea debe, si wameshafungwa au….?’akasema
mume wake, na kuuliza.
‘Basi
huyo binti aliniambia hivyo, nilipokwenda kuwaona, wakiwa jela …yeye sijui
alisikia wapi, akaniambia ana masikitiko sana, kwani kapata taaarifa kuwa
rafiki yake, yule binti aliyekuwa kwangu, akaondoka, kafariki,, aliumwa sana akalazwa
na kutokana na yale mazindiko, na masharti aliyopewa ambayo aliyapuuzia,
akaacha kuyafuatilia, yalianza kumpatiliza…’akasema huyo mama.
‘Waongo
hao…’akasema huyo baba.
‘Sasa
sikiliza …, basi huyo binti alipokuwa
huko hospitalini, alizidwa sana, uamuazi ukawa afanyiwe upasuaji, na kabla
hawajafanya hivyo, akafariki, na mtoto alifarikia tumboni…na alipopasuliwa
kumtoa mtoto, akatokea kiumbe wa ajabu sana…’akasema huyo mama.
‘Mungu
wangu ni nani huyo alitengeneza huo uzushi..?’ akauliza huyu mama Ntilia.
‘Aaah,
tuyaache hayo, mungu akupe maisha marefu binti….na kiukjweli, huyu mwanaume
kanieleza mengi hapo nje, kuwa kakuomba msamaha, na mimi sitakuwa mbali na yeye
na mimi nakuomba unisamehe sana, najua mengi yaliyotokea…eeh,…’akawa
ananisogelea kunipigia magoti.
‘Mama
usifanye hivyo, hustahiki kunipiga magoti mimi, wewe hujanikosea kabisa hata
huyu baba, mimi sijui kanikosea nini, mpaka sasa hajatuambia nilichomkosea, nashangaa
tu kaja anasema nimsamehe, nimsahemeh anini sasa, hata hivyo mimi nishamsamehe,
kama kuna lolote alinifanyia, mungu amsamehe tu maana yeye ni sawa na mzazi, …’nikasema,
na huyo mama akaniangalia kwa macho ya kushangaa na huruma
‘Kakukosea
sana tu…na ni kwa vile hakujakusimulia….’akasema huyo mama, na akashika kichwa
kama anawaza jambo, na kama vile kakumbuka kitu akasema
‘Unajua,
...usije kumdharau mtu katika hii dunia, hata kama unacho, una uwezo, lakini
hujui ni kitu gani kamtunuku mja wake, ambacho wewe huna…huyu binti mungu
kamtunuku jambo ambalo wengi hawana,…hata wakijifanya wanalo, lakini ni gumu
sana kuwa nalo….’akasema
‘Nakushukuru
sana binti yangu,…maana kwa uoni wangu, mimi najua nimekukosea sana, hivi sasa
ndio naanza kulitambua hilo, lakini muda ule ambao nilikuwa na uwezo wangu,
maisha mazuri, nilikuwa silioni hilo kabisa…kwa muda ule ilikuwa rahisi
kuchukua maamuzi ya haraka, hasira, dharau, vilinitawala sana, njia rahisi ni
kufukuza, si nitapata mfanyakazi mwingine,..nilijiona nimesoma, pesa ninazo, watu kama hawa hawawezi kunibabaisha,…sasa
mitihani iliponizidi, nikaanza kuchanganyikiwa, vyote nilivyokuwa navyo
havikuweza kunisaidia…’akasema.
Nilimuangalia
huyu mama akiwa anaongea na akilini nikawa nawaza sana maisha ya mwanadamu
yalivyo, jinsi gani mwanadamu anavyoweza kubadilika kwa muda mfupi, maana huyu mama
alikuwa kibonge siku zile, mwenye nazo, anajiamini , leo hii anaonekana
kakonda,kazidi kuzeeka, ..mvi zinameta meta, kichwani, anaoenakan hana raha
kabisa, ni kwa muda mfupi tu,….moyoni nilimuonea huruma sana.
‘Najua utanisamehe, lakini moyo unanisuta kwa
maana ni mimi ndiye nilikutoa kijijini nikaahidi kuwa nitakutunza, nikachukua
dhamana hiyo kwa mama yako, na hadi anafariki alijua mtoto wake yupo mahali
salama, lakini sikuikumbuka dhamana hiyo na adhabu zote zimenishukia mimi,…adhabu
za familia nimezibeba mimi, kila nikiwazia hilo, naona nimekukosea sana, unajua
niliwahi kumuota mama yako alinilaumu, ananiambia saa umefany anini..hivyo,
sasa nimefanya nini, ina maana ananisuta, ananilaumu….’akasema.
‘Mama kiukweli
mimi sina kinyongo na wewe, najua hata ingelikuwa mimi nipo kwenye hiyo sehemu
yako labda ningelifanya hivyo hivyo,..na una maana huyu baba ndiye yule mume
wako, mbona kabadilika hivi, .?.’nikasema na kuuliza
‘Ndio
yeye, ni hiyo midevu na hali ngumu, ndivyo vimemfanya usimkumbuke, ndiye yule aliyekusababishia hayo yote, huku
sasa akinichunguza tumboni na mimi nikajitahidi kujiminya kwa ndani ili ile
mimba isionekane kwa vile nimevaa dera, lakini haikuwezekana, yeye akasema
‘Ina
maana hiyo mimba ndio imekuwa hivyo, jamani watu waongo, hata siwezi kumuamini
mtu tena, ..hapana…’akasema sasa akificha uso wake na mikono.
‘Ndio
hivyo mama, nasubiria kudra za mungu, nina
imani mimi nitajifungua salama na mtoto wangu atakuwa mwema tu, sizani kama
yale waliyoongea watu yanaweza kuwa ni ya ukweli, hata asipokuwa na baba, mimi
sijali, nitamlea kama mtoto wangu….’nikasema
‘Safi
kabisa, utazaa na utazaa mtoto mwema kabisa, hiyo ndiyo imani sahihi, nikuambie
ukweli kwenye matatizo unakutana na vishawishi vingi, mimi walikuja watu wakanishawishi
niende kwa waganga wa kienyeji kwa matatizo ya huyu mwanaume….’akasema
nilishangaa kwa nini hasemi mume wangu kama zamani,
‘Ilibidi
nikubali tu maana nipo na mtoto wa watu, ni mume wangu, ningefanya nini, lakini
kwa bahato nzuri sijui ilikuwaje mwanaume huyu akatoroka, na akapotoea hadi leo
ndio tunampata…sasa kumbe ndio alikuwa akikutafuta wewe…’akasema
‘Mimi
sijui kama alikuwa akinitafuta mimi..’nikasema nikimtupia jicho huyo mzee, yeye
alikuwa kainamisha kichwa chini, …
‘Hisia
ndizo zilikuwa zinamtuma hivyo, nakumbuka alipoanza kuchanganyikiwa ni pale
nilipokuwa namuuliza, je atakuja kusema nini mbele ya mungu kwa hayo aliyokufanyia wewe..baada ya kuanza
kuugundua ukweli,.. unajua nimekuja kugundua mengi yaliyokuwa yakitendekea pale
ndani, na kumbe kisa ni huyu mzee,…’akatulia akimuangalia mume wake.
‘Waambie
tu, ukweli mke wangu mimi nipo tayari, maana nilitaka wewe uje uyaseme yote, maana nikisema
mimi watafikiria bado nimechanganyikiwa, waambie ukweli wote kunihusu mimi..ila
sasa aujue na akisamehe ajue ni kwanini nimehangaika hivi na kwanini namuomba
huo msamaha…’akasema.
‘Nina
imani nikisema kila kitu huyu bint hataweza kukusamehe kamwe…’akasema huyo mama
‘Hapana
mwambie tu…nipo tayari ..’akasema huyo mzee
‘Kwani
ni lazima kuniambia…kama mnaona kuna utata, na huenda nika…lakini mimi vyovyote
iwavyo, siwezi kuwa mbaya kiasi hicho, furaha yangu ni kuona nyie wawili mnarejeana
kama mlivyokuwa awali,…familia yenu iwe na furaha…’nikasema.
‘Kiukweli…ni
ngumu,…’akasema.
‘Ina
maana mlifikia hatua hiyo, mpaka wewe na yeye mkataka kuachana,au mumeshaachana
tayari…?’ nikauliza
‘Hatujaachana…’akasema
huyo mzee
‘Sasa
tatizo ni nini hapo….?’ akauliza mama Ntilie
‘Sijaachana
na yeye kisheria, mnielewe hapo, lakini upendo wa kweli ni kutoka moyoni,
huwezi ukaishi na mtu mpo mpo tu…ni kama unafuga nyoka,…maana mtu kama alifikia
hapo, akayafanya mambo mabaya kiasi hicho, ni sawa na nyoka tu, siku yoyote
angeliweza kuniua,…ohooo, hapana nyie hamjayasikia aliyoyafanya….’akasema.
‘Sasa mimi
na kushangaa..ina maana wewe hukutaka mume wako apone au..?’ akauliza huyo mama
‘Kupna
ni kitu kingine,.sawa nimefurahi kapona, kama binadamu maana hakuna binadamu
eliyekamilika anayeweza kumuombea mwingine mabaya, akitokea hivyo, huyo ni
shetani,..mimi sio shetani…ila moyoni, nikiyawazia yaliyotokea, nilivyoteseka,
na walivyoteseka wengine unaaambiwa chanzo ni mtu mnayeishi naye,….’akasema
‘Na ni
kweli ….?’ Akauliza huyo mama Ntilie
‘Ni
kweli si huyu hapa, …muulizeni…..’akasema
‘Lakini
hata hivyo, kupona kwake, ni kupona kwa familia, na haya yakiisha ni mafamikioa
ya familia yenu au sio…sasa kama wewe upo hivyo, mnatarajia nini kwa huyu
binti, kama wewe umeshindwa kumsamehe mume wako, huyu binti afanyeje sasa…?’
akauliza huyo mama Ntilie.
‘Hapana,
yeye, ni kwa utashi wake,hilo siwezi kumuingilia na nashukuru kwa moyo wake
huo, ni mtu wa pekee katika hii dunia,na sijui labda nahisi ni kwa vile
hajausikia ukweli wote, kuhusu alichofanyiwa na huyu mwanaume…sijui kwanini
watu kama hawa ..wanaoa…’akasema akimuangalia mume wake kwa hasira.
‘Lakini
mama, mimi sioni kosa, kukosea kupo, ina maana wewe hujamkosea mtu, akakusamehe…?’
nikamuuliza
‘Si
kama hivyo nilikukosea wewe, na umenisamehe lakini sio kama hayo aliyonifanyia
huyu mtu…’akasema
‘Lakini
mimi nimekusamehe sijaona kosa kubwa ulilonifanyia yeye, ..muhimu, nionavyo
mimi, ni kuliona kosa lolote ni kosa tu
la kibinadamu, na wanadamu tunateleza, ten asana, muhimu ni kusameheana,na mimi
nimemsamehe kwa lolote lile alilonifanyia nimemsamehe…’nikasema.
‘Hapana
kabla hujasikia hayo aliyokufanyia, usiseme hivyo kuwa umemsamehe, nafsi
itakuja kukusuta baadae, subiria kwanza, ngoja nikusimulia tu… na ukiyasikia
ukimsamehe na mimi , labda…nitaweza kuingiwa na nguvu hiyo labda na mimi mungu
atanijalia niwe na moyo kama wa kwako, ili niweze kumsamehe…’akasema.
‘Oh,
kama unaona ni lazima kunisimulia, lakini…sawa, ….lakini mimi vyovyote iwavyo, nimeshamsamehe
huyu baba, yeye ni baba yangu, na alichukua jukumu hilo, kama baba yangu, na
wewe ni mama yangu ulinichukua kijijini kwa wema wako, yaliyotokea ni mapito
tu, …’nikasema.
‘Huyu
ndio binti yangu, natamani ningelikuzaa mimi…’akasema mama Ntilie
‘Hata
kama hujanizaa nakuona sawa na mama yangu, sitakusahau maisha mwangu …’nikasema
kumuambia huyo mama Ntilia, na huyo mam Ntilia akainua mkono juu wa ushindi.
‘Haya
tuambie hayo ambayo huyu mbaba alimfanyia huyu binti…..’akasema huyo mama
Ntilie,na huyo mama akamgeukia mume wake na kusema.
‘Upo
tayari mume wangu niyaseme madhambi yako yote…?’ akaulizwa
‘Ndio
maana nilisubira uje uyasema yote wayasikia,usifiche kitu hata kimoja..nipo
tayari…’akasema
NB: Haya
yale maswali yote yatajibiwa humo…
WAZO LA LEO: Tukikoseana ni wajibu wetu
kusameheana, ni mangapi tunawafanyia wengine, mabaya zaidi, lakini
tunasamehewa, ni mangapi tunamkosea mola wetu anatusamehe, tunaiba maofisini,
njiani ..kwa dhahiri na kwa kificho, tunafanya makosa mbali mbali, pasi na
kuonekana, lakini tukitendewa sisi ni wepesi, kutumia mikono yetu hata kuua,..chuki
zipo mbele kuliko upendo, je ingelikuwa
hivyo, tunafanyiwa sisi, tungelikuwa hai……tusamehe ili na sisi tuje kusamehewa.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment