Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Tuesday, August 8, 2017

DUWA LA KUKU...31


 Baada ya majadiliano kidogo, mama akaona nipewe nafasi hiyo, mimi nikae faragha na huyo mzee, lakini sehemu ambayo naweza kuonekana ili kama akileta vurugu niweze kusaidiwa, Nilimuangalia yule mzee, , kwasasa akawa anaona aibu hata kuniangalia, sio kama ile awali, ni kama kabadilia, na kule kuona aibu hataki kuniangalia moja kwa moja usoni, kukanifanya nishindwe kumtambua vyema.

‘Haya wewe unaweza kuwepo , maana kwa hivi sasa huyu ni binti yako, au sio, sitaki nikae naye faragha tukiwa wawili tu, walimwengu ni wengi wa kuzusha, naogopa sana kwa sasa…” akasema huyo jamaa sasa akiongea vyema sio kama ilivyokuwa awali, ni kama vile mtu anaigiza, kuongea kwake kwasasa sio kama awali alivyokuja akia kama kachanganyikiwa, kama isingelikuwa hayo mavazi na muonekano wake, usingemfikiria vibaya.

‘Sawa lakini unaona bado tuna kazi za usafi, maana sisi, siku nzima huwa ni kazi tu, na kazi zetu usafi ni kitu muhimu sana, na wewe sasa unatukwamisha, tumekuheshimu tu kwa vile wewe ni mteja wetu mnzuri…’akasema mama.

‘Mimi nitawalipa siku hii nzima, nipo tayari kwa hilo, nipigieni hesabu zenu,…., msijali, hamuwezi kupata hasara kwasababu yangu, najua haya ni kwa masilahi yangu…samahanini sana..’akasema akashika kifuani.

‘Pesa utapatia wapi wewe mzee,  au unaomba omba mitaani..?’ huyo mama akamuuliza kwa utani na huyo mzee, hakukasirika akasema kwa uzuri tu

‘Pesa sio shida kwangu mama Ntilie,…usinione hivi…’akasema akijikagua huku akitikisa kichwa kwa kusikitika.

‘Ukisikia historia yangu utanionea huruma,…hadi nimefikia hii leo naweza kuongea na wewe hivi, namshukuru sana mungu na wanaonifahamu wakiniona hivi naongea na wewe hivi hawataweza kuamini..unajua huko nilipotoka niliondoka siku nyingi hawajui wapi nilipo…’akasema

‘Wapi umetokea…?’ akaulizwa

‘Huko kwa mke wangu…nilitoka siku moja saa kumi alfajiri nikapotea, hawajui wapi nilipo, niliwahi kuona tangazo,…kwenye gazeti, wakati akili inakuja na kupotea, kuwa natafutwa,..lakini kwa hasira nikalichana lile gazeti, walipiga kipindi sina midevu hii…’akasema.

‘Sasa kwanin hunyoi…?’ akaulizwa.

‘Ningelinyoa kama nilikuwa najitambua..sijui…kiukweli nahisi nilikuwa sijijui,..unajua hivi sasa nahisi ni mtu mwingine kabisa…’akasema.

‘Kwani tatizo lako ni nini…?’ akaulizwa.

‘Tatizo langu,!!! ..labda akija mke wangu atawaambia..yeye unajua, tatizo langu limeanzia wapi, ila hajui jinsi ya kunisaidia, mimi nilishajua lakini jinni gani ya kumuelezea ikawa ni vgumu sana ..’akashika kichwa

‘Unajua nikuambieni kitu,..hata kwenye njozi, nahisi hivyo, ni kuwa niliwakosea watu wengi sana, na hilo ndio tatizo langu, hakuna zaidi…mengine sawa yawezekana yapo,…ila nahisi , ni hayo niliyowafanyia watu , na ninayemkumbuka kwa haraka ni huyu binti, hasa nilipomuona ndio nikakumbuka,…’akaniangalia kwa aibu.

‘Nilipomuona tu nikamtambua, najua yeye ndiye nimemkosea sana, mke wangu nilimkosea lakini yeye alishasema kanisamehe, iliyobakia ni huyu..najua ni huyu tu…baada ya tendo hilo la kunisamehe..akakiri moyoni na vitendoni, nina imani mola anatanirejeshea hali yangu, na kila mara nilikuwa naiota hiyo ndoto na nikionywa kuwa, nispofanya haraka sitapona tena, na tumuwahi kabla hajapata matatizo zaidi ….’akasema.

‘Kwenye ndoto ndio unaota hivyo, sio kwa waganga wa kienyeji..?’ akaulizwa.

‘Mimi siwajui waganga wa kienyeji, sio kwamba sijawahi kwenda, nakumbuka mke wangu alinipeleka huko kwenye kunihagaikia…lakini nikaja kumtoroka, unajua hata kutoroka kwangu asubuhi siku hiyo sababu kubwa ni hiyo, walipanga wanipeleke kwa mganga wa kienyeji, kuna rafiki yake mke wangu alikuja akamshauri hivyo, mimi alifajiri hakujapambazuka, nikatoroka mapaka leo ndio wanapata taarifa zangu..’akasema.

‘Sasa kwanini ukatoroka ukijua kuwa wenzako wanakuhangaikia wewe, ili uje kupona…?’ akaulizwa.

‘Mimi sijui kwanini nilifanya hivyo…, ila kuna kitu kiliniambia toroka, huko wanakotaka kukupeleka hutapona, watazidi kukuharibu, dawa ya maradhi yako sio hiyo, dawa ya maradhi yako ni makosa yako mwenyewe, …’akatulia

‘Nikijaribu kuuliza ni makosa gani nimeyafanya, basi nikijiuliza hivyo kuna watu , kelele za watu wanalia, …wakuja kunililia, nimewakosea,..sasa kwa vipi ni nani, siwaoni , sioni ..unajua, kichwani tu kelele za vilio, nikisikia hivyo nakiambia, nikijaribu kuzikimbia hizo kelele, lakini wapi, kwahiyo nimekimbia wee…mpaka wapi huko, …nilikwenda mbali sana..’akasema

‘Sasa huku uliwezaje kurudi….?’ Akaulizwa
‘Hata sijui, nimekua  nikitembea , huku na kule, nalala maporini, majalalani, lakini siachi kumkumbuka mungu, mimi sijawahi kusoma dini, nahisi hili ndio kosa kubwa sana, kama ningelikuwa nimesoma dini, huenda matatizo haya yasingelitokea, nimesoma masomo ya kawaida, nimesoma sana usinione hivi, hadi chuo kikuu…’akasema

‘Wewe…?’ mama akauliza kwa mzaha

‘Ndio, huamini…’akasema
‘Sawa nikiamini aikuamini, haitasiaida kitu, muhimu ni mtu mwingine aje kututhibtishia,…’akasema huyo mama
‘Sasa uliambiwa ni makosa yako, hukuambiwa ufanye nini, utubu au ufanya nini…?’ akaulizwa

‘Unajua hali hiyo ya kuchanganyikiwa,  inakuja tu, na kupotea, kuna muda nakumbuka kumbuka mambo kuna muda hali inakuwa mbaya, wakati mwingine nahisi kama nipo kwenye njozi, ni kweli kuna muda, niliwahi kuulizia, nitafanyaje kuhusu hayo makosa, sikumbuki jibu, lakin….ikaja hiyo hali kuwa nitubu , kama ni makosa unatakiwaje ufanye nini, ni kutubu au sio , sasa kwa nani….’akatulia

‘Kwahiyo ukafanyaje hadi ukafika huku…?’ akaulizwa

‘Kufika huku labda niseme ni miujiza ya mungu,..sasa haivi kidogo nimeanza kukumbuka nipo wapi, na kutoka hapa ninaweza hata kwenda nyumbani kwangu, ni mbali kidogo na hapa, ….lakini nitafika tu….’akasema

‘Ni mke wako unamkumbuka sasa kwa jina wapi alipo, au sio…?’ akaulizwa hapo akakaa kimia kidogo, halafu akasema;

‘Unajua bado, kichwani hakujakaa sawa kabisa, maana sijariskika, nahisi ..lakini nishapona, najua kwa haya mateso, niliyopata nia dhabu tosha, sikuwahi kuambiwa, nifanye nini, ila nahsi hivi ndivyo sahihi, ila jamani nilikuwa nateseka, kichwani kunakuja mambo mengi hili na lile..yaani nikikaa hivi ni kama kuna watu elifu wanaongea kwa pamoja kichwani, wengine wanalia, wengine wanapiga makelele..yaani we acha tu…’akasema

‘Pole sana, mungu atakujalia, utapona kabisa, mimi nimeshakusamehe japokuwa sijui kosa ulilonifanyia ni lipi, maana sijawahi kukutana na wewe, sikukumbuki kabisa…’nikasema na yeye akaniangalia kwa makini nikaona kama machozi yakimtoka, kiukweli nilimuonea huruma nikasema;

‘Usilie baba yangu, wengi tupo hivyo, tunapitia matatizo, maisha magumu, na ukifikiria sana, unaishia kulia, na hasa ukigundua kuwa wenzako huenda …lakini sitaki niongee zaidia, mimi namuomba mungu kama kuna ulilonifanyia mimi, hata nisipolijua akusamehe tu, ..sina kinyongo na wewe…’nikasema.

‘Mungu wangu…hata sijui niseme nini…’akasema.

‘Huna haja ya kujiumiza mzee…bint huyu ni mwema, sana, katika misha yangu ya kuhangaika sijawahi kukutana na binti kama huyu , mwenye adabu, anajua kuishi na watu, muaminifu, ..huwezi kuamini, hata kuonja mboga jikoni mpaka aniombe ruhusa, niliona ni mtu wa ajabu sana…’akasema huyo mama.

‘Namfahamu sana…’akasema huyo mzee.

‘Unamfahamu kwa vipi, unajua unatuweka kwenye mtihani mpaka watu wanatufikiria vibaya wanafikia kuhisi labda, ni  wewe ndiye ulimpa huyu binti hiyo mimba..japokuwa tunajua sio kweli au sio…?’ akaulizwa na hapo akanitizama tumboni, kwa uso wa huruma, akasema;

‘Ana mimba, masikini…sikujua hilo…’akasema sasa akinitizama tumboni.

‘Wewe si unasema unamfahamu, mbona hujui kuwa ana mimba..?’ akaulizwa.

‘Mimi hilo sijui….ooh, yaani labda ..lakini mim isijui kabisa, nisamehe sana …sitaki niongee zaidi hapa, nataka tuongee ukiwa huru…’akasema.

‘Kwahiyo hiyo mimba sio ya kwako..’akasema huyo mama kwa utani.

‘Wewe mama wewe, huko sasa…hapana, …’akasema akiona aibu


‘Niambie ukweli, kama ni wewe ulimbaka au wewe ni baba yake, tuambie maana hata yeye hakufahamu kabisa isije ukawa ni tapeli fulani una mambi yako…?’ mama akauliza hivyo na jamaa akatoa jicho la kushangaa na kusema.

'Ni hadithi ndefu, na kiukweli hivi unavyoniona na hali niliyo nay oleo ina afadhali, nashangaa hata mimi, najikuta nipo hivi, ile hali ya awali imenitoka, na kama mtu kanivua kofia, kofia niliyoizoea, na kuniacha kichwa, nahisi nipo mtu mwingine kabisa…’akasema.

‘Sijakuelewa…’mama akasema.

‘Wakati nipo hapo nje, nililia sana, namlilia mola, kuwa nimempata mmojawapo, basi anisaidie huyu niliyempata anisamahe…najua huyu nilimkosea, najua kwa hayo makosa alishawahi kuinua mikono juu na kumlilia yeye, sasa nimeyaona madhambi yangu, anisaidie huyu mtu anisamehe…nililia mpaka macho yanauma.

Kuna muda nikahisi kama kausingizi…  mara nikahsi kitu kikipiga kichwa, taa..nikasikia nziiiiiii..hujawahi kuhisi hivyo kichwani, mara nikajihisi kama nimetoka usingizi,…naanza kuona watu vyema, nahisi vyema, ..na nilipojiangalia nilivyo nikashtuka, kwanini nimekuwa hivi, unajua nilisimama najikagua kwa muda nikashikwa kichwa manywele mengi, midevu, ohhh, sikuamini, hivi mimi ni nani , na kwanini imekuwa hivi, nikaanza sasa kutafkari, kukumbuka imechukau muda, lakini naanza kukumbuka,…’akasema.

‘Mungu mkubwa, kwahiyo kule kuchanganyikiwa ndio kumeondoka hivyo, nahisi mola mwingi wa rehema kasikia kilio chako,…’akaambiwa.

‘Lakini sijaamini mpaka nisikie kauli ya huyu mdada, najua kanisamehe moyoni ndio maana ikatokea hivyo, natamani niskie kauli yake kuwa keshanisamehe zaidi ya hapo, katamka na kutamka, lakini bado,ni mpaka asikia kuwa mimi nani nilimfanya nini , hilo la mimba mimi sijui, …, najua siwezi kumlipa kwa hayo niliyomtendea, lakini…mungu anajua jinsi gani nilivyoteseka, muulizeni mke wangu atawaambia ukweli..’akasema

‘Sasa mke wako tutamjuaje sisi, maana unasema mke wako mke wako, hutaki hata kututajia jina lake…’akasema huyo mama.

‘Atakuja,…naomba simu yako mara moja…’akasema, na huyo mama kwanza akasita kidogo, jamaa akasema

‘Usiwe na wasiwasi nimekumbuka namba ya mke wangu, nilikuwa najaribu kuiwazia, sasa nahis ndio hiyo, nipe nimpigie, au wewe nikutajia umpigie kama una mashaka na mimi…’akasema na huyo akampa huyo jamaa simu,

Jamaa akaanza kubofya hizo namba na kuweka simu sikioni, akasikiliza kwa muda mara, haloo

Ni mimi mume wako…’akasema

‘Ni kweli ni mimi, umenisahau hata sauti yangu jamani…’akasema

‘Nipo..nipo..hapa ni wapi…?’ akauliza huyo mama, huyo mama akasema

‘Nipe hiyo simu nimuelekeze…’akasema na kupewa akaongea na huyo mke wa jamaa ana kumuelekeza wapi walipo na huko wakasema wanakuja.

‘Wanasema wanakuja, sijui nani na nani…’akasema mama

‘Oh, mungu mkubwa, …’jamaa akasema huku anafuta machozi,

‘Unajua niwaambie kitu, bila ya mke wangu kuwepo hapa hili zoezi halitakamlika, nataka aje ashuhudulie kuwa mimi sio yule tena, mimi ni nani, na nilimkosea nini huyu binti, yeye anajua zaidi yangu…kiukweli namuonea huruma sana mke wangu,..kateseka kwa ajili yangu mpaka ikafika sasa hana jinsi, unajua huwezi kujua ugumu wa jambo mpaka uwe nalo, kuishi na mtu aliyechanganyikiwa ndani ya nyumba, ni mtihani…’akasema

‘Oh, pole sana, sasa…mimi naona utupe muda, sitaki kukukatili na kwa vile umesema mke wako anakuja na ni bora awepo, unaonaje ukatupa muda, tumalizie hizi kazi au sio,…’akaambiwa

‘Sawa, …sasa hivi nahisi nipo binadamu, najua moyoni keshanisamehe ndio maana imekuwa hivyo, …nitawasaidia kazi, ngoja, nipeleke huu uchafu nje…’akasema na kuanza kusaidia kazi za hapo.

 Haikupita muda mara ukaingia ugeni, muda huo tulikuwa tunapanga panga vitu, na kwa vile siku hiyo hatukuwa na kazi za mapishi zaidi, tulikuwa tunafungasha fungasha, na ndio tukaona ugeni wa watu wa dini, wakiwa na mavazi yao, walikuwa kundi, mpaka tukashangaa, kuna nini leo.

‘Salamu salamu, amani iwe juu yenu nyote, hamjambo jamani…,’ mmoja wapo akasalamia na mama alikuwa kwa ndani akatoka nje kukutana na ujumbe huo, mimi kwa muda huo nilikuwa namalizia kazi na yule mjamaa alikuwa kapewa kiti kakaa pembeni na muda mwingi alikuwa akinitupia jicho, sasa hivi anafanya kwa kujiiba sio kama asubuhi alikuwa akinitizama , najisikia vibaya sijui kwanini, na hali hiyo inanifanya nasikia hata kutapika.

‘Sijui kwanini nilikuwa nikimuangalia nahisi hivyo, hadi nilipotapika, ..na baadae nikamuomba munu kama kuna kitu kanikosea basi amsamehe tu mja wake, maana ni mtu mnzima, hastahili kuadhibiwa hivyo, kiukweli nilimuomba sana mungu amsamehe, sasa sijui nilivyoomba hivyo ina mahusiano na hicho kilichotokea anayejua ni mungu pekee.

*************

‘Jamani wapendwa, mtusamahe kwa kuja bila taarifa kwa siku ya leo, ila taarifa mlikuwa nayo kabla , hatukuwa na jinsi, nyingine ila nikuja hivi hivi,...natumai mliwahi kuongea na kiongozi wetu mmoja, kuwa atakuja kuwatembelea baada ya wiki,..yeye kapatwa na dharura hakuweza kufika..., lakini hatukuona haja ya kutokufika kwa sisi, maana viongozi wengine wapo, ndio sisi …’akasema mmoja wapo.

‘Nakumbuka ndio…’akasema huyo mama

‘Basi baadhi yetu hapa tumetokea huko kijijini, kama alivyokuambia huyo mzee awali, na katika harakati zetu za kutangaza dini ya mwenyezimungu tukapungukiwa na sehemu ya ibada, huko kijijini kwetu …na katika kuhangaika ndio tukagundua eneo linalofaa, lipo sehemu nzuri tu, tukataka kulinunua, lakini mwenyewe akawa hayupo…’akasema.

'Mwenye eneo hilo alifahamika, eneo hilo lilikuwa la mama mmoja alikuwa akiishi na binti yake, anafahamika sana kipindi hicho cha uhai wake...'akatulia kidogo

'Sasa kuna mambo yalitokea, unajua huko vijijini kuna mambo yanakua kwa haraka, imani hizi za kishirikina, kuna mambo mengine vijana wanakuwa hawana kazi, basi yanazuka mambo mengi tu, na baya zaidi, watu wanauwana ovyo, ukiuliza sababu ya msingi hakuna, imani ya kumuogopa mungu haipo tena..

'Kwa vile watu wanalifahamu hilo eneo ni la nani, ikabidi sisi tuhangaike, ujue, kuna watu walilivamia awali,lakini hawakuweza hata kujenga, wakapata misuko suko, wakakimbia na kuliacha, wakaja wengine hivyo hivyo, mwishowe likaachwa kama lilivyo, ndio sisi sasa tukaingiwa na hamasa nalo,...'akatulia


‘Kiongozi wetu akafanya juhudi kubwa kutembelea huku Dar, nia na lengo ni kumpata mumiliki halali wa eneo hilo, maana tulisikia mrithi huyo ni binti wa marehemu huyu mama..., na alichukuliwa huku dar, kuja kufanya kazi za ndani, ..tunasema mrithi maana mama aliyekuwa akilimiliki eneo hilo si ndio kalifariki, watu wahuni walimfanyia kitu kibaya sana, mungu awasahemeh tu, hao watu maana nasikia nao wao wamekumbwa na matatizo makubwa, mungu huwalipa watu hapa duniani, tumuogope sana mungu…’akatulia.

‘Sasa nyie mlikuwa wapi mpaka hali hiyo inatokea, nyie si ndio wazee wa huko, tena watu wa dini…?’ wakaulizwa

‘Unajua sisi tuna nafasi yetu kama viongozi wa dini, kazi yetu ni kutoa imani kwa watu, na kazi ya ulinzi ni ya serikali, tumejitahidi sana kwa upande wetu, lakini vijana hawataki kuingia kwenye nyumba za ibada, tukiwafuata mitaani, inakuwa kero kwa wengine, na baya zaidi ila hali ya watu kuamini mambo ya ushirikina imeshika kasi, ni kama watu wtunarudi ujingani, hili ni tatizo kubwa sana,….’akasema.

‘Ni vyema watu kama nyie mkiwepo…, tunashukuru kwa hilo, kwahiyo mnasemaje sasa….?’ Akaulizwa

‘Sasa tulielekezwa hapa na huyo kiongozi wetu, kuwa kuna binti kasema anaishi na wewe, na huenda akawa ndiye huyo tunayemtafuta, kama yupo tumuone, kama ni yeye basi tutapanga siku ya kuja, kama hamna nafasi leo, au kama mna nafasi leo mungu ni mwenye neema, zake, tunaweza kuongea naye, mungu akipenda…’akasema.

‘Mhh, kiwezekanacho leo hakiwezi kusubiria, lakini nashangaa leo napata ugeni na wote mnataa kuongea na binti yangu, kuna ugeni mwingine nao unataka kuongea na binti, hatujajua wana nini, sasa nyie tena…’akasema huyo mama.

‘Lakini taarifa zetu ulizipata mapema au sio, isije kuja kuazima jamvi akaja mwingine kutaka kuliwahi, sisi tulishakuaambia na eneo hilo sisi tulisha…’kabla hajamaliza mama akasema.

‘Wao hawahitajii hilo eneo nijuavyo mimi, wana yao mengine kabisa, …sasa kwa vile hao wengine hawajakamilika, basi ngoja nimuite binti, aje mumuone kwanza isije ikawa sio yeye, nafikiri mkitambulishana itakuwa ni vyema zaidi, au sio…’akasema huyo mama.

‘Hewala hilo neno, …’wakasema na mimi nikaitwa kuja kuonana na huo ujumbe.

Nilitoka nikiwa nimevaa kiheshima, na kiukweli mimi kawaida yangu ni hivyo, huwezi kuniona nimevaa kinyume na maadili yetu, na nilipotoka kuna wazee wawili wakatikisa kichwa kama kukubali, na wengine walibakia kimia.tu wakiniangalia.

Nikawasalimia kama ada, na wao wakaniitikia, na yule kiongozi wao akaniuliza jina na natokea wapi, nikawaelezea jina na jina la mama na natokea wapi, wakasema;

‘Oh mungu mkubwa hatimaye tumekupata..ndio wewe hasa, unafanana sana na marehemu mama yako…’akasema huyo kiongozi wao,

‘Ndio huyu sio..?’ akauliza huyo mama

‘Ndio yeye, bila shaka…’wakasema

‘Sasa muelezeni shida yenu..’akasema huyo mama, na watu wale wakaelezea shida yao, na jinsi gani walivyojpanga, na wapo tayari kunilipa pesa ya eneo hilo, wao walikadria kutokana na bei za huko kijijini, zinajulikana, basi mimi nikawa sina la kusema maana nilichokuwa nikihitajia ndio hicho, kwasababu sikutarajia kabisa.

‘Wazee wangu, nawashukuruni sana, maana sikitarajia hilo, mimi nilijua eneo hilo limeshachukuliwa,. Na nilikuwa naogopa kabisa kurudi huko nikijua yatanipata kama yaliyompata mama,  na ujio wenu umenipa faraja kuwa angalau wapo watu wema katika hii dunia, nimepitia machungu mengi sana, sitaki kuelezea, lakini siku zote kama alivyoniusia mama yangu, alinitaka nisikate tamaa na niwe na mtegemea mungu , kwani mungu pake yake ndiye, ataniondolea mizigo hii ya mitihani..’nikasema.

‘Sawa kabisa, imani imekuiba binti, endelea hivyo hivyo utafanikiwa hapa duniani na kesho siku ya kiamana,…kwahiyo sasa eeh, umekubaliana na kiwango hicho.au.?’ nikaulizwa.

‘Mimi sina zaidi,kama mumeona ni kiwango halali kwa hilo eneo, basi nimeridhia, nyie ndio mnajua na nyie ndio mumelipima,hilo eneo, mimi yote namtegemea mungu tu ni neema zake hizo..’nikasema.

Basi utaratbu wa nyaraka ukapita, na nikaambiwa kwanza nifunguliwe akaunti ya benki, tutasaidiana na wao,  na malipo yatafanyika huko huko benki, ili hizo pesa ziwe salama na niwe nachukua kwa awalmu nikihitajia, tukakubaliana hivyo, ikabakia sehemu ya kuweka sahihi na kupitia sehemu zote za serikali zinazostahiki ili isije kutokea migogoro baadae, nikawa sasa na mimi tajiri, nilijihisi hivyo moyoni.

*************
Ugeni ule baadae ukaondoka, ikabakia kesho waje tuongozane kwenda banki kukamilisha mipango yote iliyobakia, na walipoondoka,  mara ukaja ugeni mwingine , gari likasimama nje, …na tukasikia hodi, baada ya muda,

Wa kwanza kutoka nje alikuwa yule mzee, akasema.

‘Huyo anaweza akawa ni  mke wangu…’akasema akiwa na furaha sana usoni.

NB inatosha kwa leo…nipo kwenye mitihani fulani hivi, lakini nimeona nisiache siki ipite hivi hivi


WAZO LA LEO: Tusichoke kumuomba mola wetu, kwani mola ni mwingi wa rehema anajua ni lini atatutimizia matakwa yetu kwa wakati gani. 

Ni mimi: emu-three

No comments :