Tuligeuka
kuangalia kule mlangoni, mioyo ikitudunda, ni kwanini mlango ukagongwa kwa fujo, kama ni docta anajua jinsi gani y akuufungua nlango wake...sasa ni nani huyo, ni maulizo ya sekunde kadhaaa kabla mlango hauajafunguliwa,
Lakini tendo hilo la kutaka kufunguliwa lilitaka kuzuiwa na sauti ya nguvu huku kwa mgonjwa, akisema usifungue,..ni vitendo vilivyotokea kwa muda mfupi sana, na kitendo cha usifungue kilikuwa kimechelewa, kwani mama yule aliyekwenda kufungu amlango alikuwa ameshakinyonga kitasa cha mlango ili mlango uweze kufunguka.
Na huyo aliyekuwa huko nje, akawa keshausukuma mlango, na kwa haraka akaingia ndani, na kitendo kile cha yeye kuingia ndani kwa haraka kikasindikizwa na mlio mwingine kwa mgonjwa, akigugumia kwa maumivu,
'Aaagh,....Aaagh....'halafu kukawa kimia
Tuendelee na kisa chetu
*******************
‘Nimesikia
yote uliyokuwa ukiyasema, kumbe kweli wewe ulishiriki katika kumuua, mwanangu..’ Ilikuwa sauti ya mwanamama aliyeingia
Alikuwa mama mtu mnzima, kama sio kwa uchakavu wa maisha magumu, basi huyu mama atakuwa mtu mnzima, pamoja na hali hiyo, mwili wake ulionekana shupavu, na alipoingia, aliingia kwa kasi, akitembea pale alipokuwa kakaa mgonjwa.
Ujue vitendo hivi vilitokea kwa muda mfupi, kiasi kwamba, hakuna aliyekuwa na wazo la kumzuia huyo mama, kwani ile akili inaanza kufanya kazi, kua tufanyeje, huyo mama alikuwa tayari keshafika pale alipokaa mgonjwa na kumvamia,huyo
Na kwa vile yule mgonjwa alikuwa kakaa kwenye kiti, na uzito wa huyo mama, basi wote wakaporomoka
chini sakafuni, mama juu, mgonjwa chini...sasa ikawa ni kazi ya kuamulia,...lakini unaamulia nini sasa, kwani, cha ajabu kabisa,wakati huyu mama anaondolewa
kwa huyo jamaa, jamaa alionekana kutulia tu.. , hakufanya juhudi yoyote ya
kujitetea, au kuinu amkono wake,..japokuwa macho yalionekana kuwa na uhai yakipepesa na machozi yalikuwa yakimtoka.
Yule mama akaachanishwa na huyu jamaa, na huyu mama akawekwa pembeni, jamaa alikuwa kalala
chini, hatikisiki.
‘Mhh,
jamani muiteni docta…’aliyesema hivi sasa alikuwa yule mama aliyekuwa akiiuliza maswali,..huyu mama cha ajabu yeye alikuwa karibu na hao mabondia wawili lakini yeye hakushughulika kabisa kuamualia, alikuwa kasimama kimia akiangalia hilo tukio, mimi niliingiwa na mawazo ni kwanini, nikahisi kuna jambo,...
Na
hata kabla mtu hajaenda kumuita docta,
mara docta akaingia, na kwa haraka docta akaenda pale alipokuwa kalala huyo jamaa sakafuni, akamuweke
vizuri, akawa anahangaika kumpa huduma ya kwanza.
Madocta
wengine wakaja na vifaa, sisi tukaambiwa tutoke humo ndani, na yule mama
aliyemvamia huyo jamaa sasa akawa kashika kichwa, hasa pale tulipotoka nje, na akaanza kwa kusema;
‘Sijui
nimeua…, hata kama nimeua ni bora tu, kwanini yeye alimuaa mtoto wangu, kaua
wangapi, muacheni nay eye afe…’huyo mama akasema.
‘Wewe
mama kwanini umeingia bila sisi kukuita, unaona sasa umeharibu kila kitu,…’alianza
kulaumiwa huyo mama, na haikupita muda tukaona kitanda maalumu kikingizwa humo
ndani na baadae kikatolewa, jamaa akiwa kalazwa humo, na chupa ya kuongeza maji
mwilini ikiwa inaning'inia .
Tukawa
hapo nje tunasubiria, tuliambiwa tusiondoke kwanza, na haikupita muda, akaja
askari, huyo alikuwa mlinzi wa hapo hospitalini, akawa anamlaumu huyo mama,
kwanini aliingia huko ndani bila kibali chake, sijui huyo mama aliingiaje ndani
…lakini yawezekana, maana ilikuwa ni muda wa kuona wagonjwa, kwahiyo huyo mama alitumia mwanya huo na kuja kuingia chumba hiki cha docta.
‘Huyu mama
tulimuhitaji sisi, kwa ajili ya kutoa ushahidi, kuna tatizo lilimuhusu mgonjwa, na mtu wake wa karibu anayemfahamu vyema ni huyu mama, kama ni lawama
utulaumu sisi…’akaambiwa.
‘Lakini
hakuruhusiwa kuingia chumba hicho cha docta, mimi nalaumiwa kwa hilo, hamjui , ni kosa kubwa sana limetokea linaweza kugharimi kibarua changu…’akasema huyo
mlinzi.
‘Basi
wanaokulaumu waelekeze kwetu, sisi tupo tayari kukutetea kuwa ni sisi tuliomuita huyo mama kwa dharura, sawa…’akaambiwa na yule mama muuliza maswali. Yule
mlinzi akamuangalia huyo mama , huku akionekana kuwa na wasiwasi, yaonekana alikuwa kafokewa na wakubwa zake, na hapo alipo ana wasiwasi na ajira yake.
Baadae
docta akaja, na kutuambia…
‘Mgonjwa
kapoteza fahamu…hata baada ya juhudi zote tulizofanya, jamaa hajaweza kuzindukana, inavyoonekana mgonjwa alipatwa na
mshtuko mkubwa, sijui ni kitu, ilikuwaje wakati mpo naye…?’ akauliza, ikabidi
aambiwe ilivyokuwa, lakini hawakusema kuwa huyo mama alimvamia huyo mgonjwa
‘Ok,
bado tunahangaika naye, ngoja tuone itakavyokuwa, …ni nani ndugu yake wa karibu…?’
akauliza.
‘Huyu
hapa, …?’ akaambiwa, na huyo mama, akaambiwa amfuate docta, na kabla hajaondoka
na docta, yule mama muuliza maswali,akamshika huyo mama mkono, na kumnong’oneza
kitu masikioni, docta hakuona kwani yeye alishaanza kuondoka.
‘Sawa
nimekuelewa…’yule mama akasema na kumfuata huyo docta.
*****************
‘Hili
sasa ni balaa…’akasema mama mmojawapo katika wale mama.
‘Ulimuona mgonjwa alivyokuwa, kulikuwa na damu mdomoni..mliiona hiyo damu...’akasema mwingine.
‘Mimi niliiona hata puani kulikuwa na damu…’mimi nikasema.
‘Ina
maana huyo mama alimvyomvamia, alimpiga puani, mimi sikuona akiinua mkono
kumpiga, tulimuwahi kabala hajaanza kumpiga…’akasema mama huyo mwingine. halafu wewe ulikuwa karibu hukuahangaika kuwatenganisha..'akasema huyo mama
‘Oh..hiyo
ni dalili mbaya kwa mtu mwenye shinikizo la damu…nahisi ni kiharusi hicho…’akasema
yule mama mwingine aliyeonakana kufahamu mambo ya udakitari.
‘Ngojeni
tusubiria maama ni ajabu kabisa, mimi najiuliza kwanini alisema `usifungue’ kwa nguvu, kama vile alijua ni nani anakuja,
hata hivyo, kama ni mkewe kwanini asema hivyo…?’ akauliza huyu mama aliyekuwa muuliza swali, hakujibu swali la kwanza aliloulizwa ni kwanini yeye hakuwaamulia wakati alikuwa karibu nao.
Baadae yule mama mtalaka, akarudi, na usoni
alionekana na huzuni, akatusogelea na kusema;
‘Mhh,
jamaa, yupo kwenye hali mbaya, hajazindukana, na docta naona kama ni hataki kusema tu,
sizani, kama huyo jamaa atainuka, lakini wanasema bado wanajitahidi, mimi namfahamu sana huyu jamaa ana roho ya paka anaweza akainuka mkashangaa…’akasema.
‘Ndicho
walichokuitia hicho, au kuna jambo jingine wamekuambia.?’ akaulizwa.
‘Ndio hicho, ila wameniuliza maswali mengi kumuhusu mgonjwa, kutaka kujua historia yake kabla,…waliambia,
mshtuko huo, umesababisha mwili kupooza, na inavyoonekana kuna damu imeingia
kwenye ubongo, na sasa hivi wanasubiria vipimo walivyomchukua, kuna gharama kubwa zinahitajika kuchangia...'akasema
'Ok, hilo la gharama usijali, tutalifanikisha,...'wale akina mama wakasema.
'Kwahiyo docta akakushauri nini,...?' akaulizwa
'Alisema tuendee kusubiria, lakini mimi nikamuuliza, ina maana kwa hali kama hiyo jamaa hataweza kuinuka tena, na docta akasema;
‘Subiria
vipimo, na mengine nitakujulisha baadae, …’akasema akiigiza sauti ya kiume
‘Ok,
sawa, sasa usije kuchanganyikiwa hapa, sisi hatutasema wewe ulimvamia huyo mgonjwa..., najua kwenye
video ya mahojiano tutakayoiomba kama ushahid ikibidi, itakuwa imeonyesha hilo tendo, lakini kwa hivi sasa,
hatutaki mtu aseme wewe ulimvamia huyo mgonjwa,…’akasema huyo mama.
‘Kwanini
tudanganye…?’ mimi nikauliza.
‘Wewe
hujui mambo ya polisi,..ukisema hivyo polisi hawatataka kujua chanzo, huyu mama ataswekwa ndani, hadi hapo polisi watakagundua ukweli, na inaweza kachukua muda,... maana
hiyo hali , inavyoonekana ilitokea ghafla, huenda baada ya kumuona huyu mkewe,
akashtuka, au kabla,..mnakumbuka muda ule alibakai kimia, akawa katulia, lakini
ghafla akasema ‘msifungue’ lakini hakuweza kujitikisa zaidi ya kauli hiyo, na
kubakia kimia...'akasema huyo mama muuliza maswali.
'Nimekuelewa ...'akasema huyo mama
‘Mimi
muda wote nilikuwa namtizama mgonjwa, sikuwa na mawazo kwingine,...huyu jamaa , hakutikisika, hata wakati anatamka maneno
hayo ‘msifungue’ hapo akawa anahangaika kujaribu kutikisa angalau kichwa, lakini hakuweza, kwahiyo hiyo ‘stroke’ ilitokea kabla…au ilianza kabla huyoo
mama hajamfikia, kuna wakati, nahisi kuna kitu kilitokea kipindi huyu mama nafungua mlango...'akasema
'Kwa vipi,,,,?' akaulizwa
'Muda huo ndio alionekana kugugumia, ...na uso ulionyesha kutokwa na jasho....nahisi hapo kuna kitu, sasa sijui ni nini hasa, nilimchunguza sana , na ndio maana hata wakati mnaamulia mimi nilikuwa nipo mbali ki mawazo na haikuwa na haja ya kuamua,....'akasema
'Kwanini sasa...?' tukauliza
'Kwasababu jamaa alikuwa hawezi hata kuinua mkono, huyu mama angelijua hilo asingelimvamia, unamvamia mtu ambaye alikuwa hana uwezo wa kujitetea, ....'akasema.
‘Oh,
sasa hili ni nini maanake…?’ nikauliza mimi.
‘Labda
tmama mjnae utusaidie maana muda nao ni muhimu, hatujui kitakachofuata huko mbele....hebu nikuulize masali mawili matatu, kuhusu huyu mtalaka wako...ilikuwaje, mpaka ukaja kuingia mle ndani bila kukuita.
‘Kuna mtu alinipigia simu, akaniambia niende
huko chumba cha docta, nitasikia ukweli, kuhusu kifo cha mwanangu, nikamuuliza
kuna nini, akasema, huko jamaa yangu anaelezea ukweli wote, kuwa, yeye ndiye aliyemuua mwanangu, wakati awali
alikuwa akikana kabisa kuwa sio yeye aliyemuua, mwanangu..mpaka tunaachana
alikuwa hajakiri kosa…’akasema.
‘Ni
nani huyo aliyekupigia simu..?’ akauliza.
‘Mimi sijui,
ni namba tu ilionekana kwenye simu yangu…’akasema.
‘Sasa
lolote likitokea,…ina maana polisi watakuita kukuhoji, uwe makini kwenye
maongezi yako, usije kuongea mambo ya kuhisi,..au, nilisikia, kauli kama hizi, nilihisi, nilisikia ambazo huna uhakika nazo, nikwepe kabisa, ongea hali halisi uliyoiona na kuithibitisha, uwe
makini sana na hayo….’akaambiwa.
‘Kwanini
polsi wanihoji, mimi sijamfanya kitu huyo mgonjwa..., hata pale nilipomvamia, sikumpiga,
nilifika pale na kumvamia, mara tukadondoka wote chini, hakunishika, na nilihsi
mwili wake sio…ni wa baridi..’akasema.
‘Ndio
maana nasema huenda polisi wakakuita kukuhoji, kuna dalili ya taarifa za mbaya, ni hisia zangu tu, sipenzi hivyo, na nyie mkwepe kuongea hisia zenu, nasema hapa kwa vile tupo pamoja, ..hatuombei, lakini nahisi jamaa hataweza kuamuka...'akasema
'Ni kweli, kwa hali ile,.., yawezekana akawa kwenye hiyo
hali kwa mudaa mrefu, maana wengi wanaweza kuwa hivyo kwa muda mrefu, kuna
wengine wanazinduka, kama damu haikugusa ubongo, lakini kama imegusa ubongo,
mmh,sijui…’ akasema huyo mama mwingine.
‘Sasa
hebu tuambie maisha yako na huyo mume wako, maana siku ile niliongea nawewe kwenye simu kwa
haraka haraka, ndio nikakuambia ukija huku tutaongea vyema zaidi…huyu mume wako
alikuwaje…?’ mama akamuuliza lakini kabla hajajibu mara akaja polisi,
****************
‘Ni
nani mke wa yule mgonjwa..?’ akauliza askari , huyu alikuwa askari ambaye
yaonekana kaitwa muda sio mrefu.
‘Ni
mimi afande…’akasema huyo mama.
‘Twende
ndani , kuna maswali tunataka kukuhoji…’akaambiwa, na hapo tukajua kuna jambo
limetokea, na haikupita muda yule mama akarudi, na alionekana vile vile kuwa na
wasiwasi, tukamuuliza kaulizwa nini.
‘Mhh..mimi
nashindwa kuelewa, wananihoji maswali yale yale, ilikuwaje mimi na mume wangu,
kwanini nimekuja huku, hawasemi kuna kitu gani kimetokea kwa mgonjwa, nahisi jamaa hayupo
duniani tena…’akasema huyo mama, sasa kwa sauti ya huzuni.
‘Mhh,
usiseme hivyo, …’akasema mdada
‘Sikupenda huyo jamaa haraka hivyo, nilikuwa sijamalizana naye, nilitaka apate shida kidogo,...hata hivyo jamaa ana roho ya paka, kuna kipindi walikuwa
wakitupiana makombora na huyo anayemuita adui yake,…anadondoka anapoteza fahamu
masaa, lakini baadae anaamuka,….lakini ya safari hii , mhh, ...sijui , hata hivyo sikunda afe haraka hivyo...'akasema
'Lakini muda mfupu ulisikika ukisema hivyo....'akaambiwa.
'Aah, ni hasira, niliwahi kutamka hivyo mara nyingi tu, maana inauma, nyie acheni tu...mimi nilitaka nimsikie kwa kauli yake akikiri kuwa kweli
ndio yeye alimuua mwanangu..baada ya kupata mateso makali,..’akasema.
‘Lakini
wewe ulisema, umesikia akisema, akikiri au…?’ akaulizwa na kabla hajaulizwa yeye akasema.
‘Pale
nilipofika mlangoni nilianza kusikia pale aliposema ‘Kiukweli mimi sikujua, ningelijua nisingelifanya
hilo..alinihadaa…kwanini nimuue mtoto wangu…’akasema.
‘Hebu
nikuulize umesema mume wako alikuwa akitupiwa makombora, ni makombora gani hayo..?' akaulizwa
‘Unajua
yeye huwa anasema eti huwa anapambana na maadui zake, mimi siwajui ni akina nani na hao anaowaita, maadui zake,wanawindana na kutupiana mashetani, ...anasema miongoni mwa hao maadui yake, mmoja wapo ndiye chanzo cha kifo cha mtoto, ndivyo anavyo jitetea hivyo...'akasema
'Huyo adui yake hujawahi kumfahamu.....?' akaulizwa
'Huwa hapendagi kumsema mtu kwa majina, ..hakuwahi kuniambia ni nani, ila wanatupiana mashetani, n ahayo masheani ndio wanaita makombora..'akasema.
'Ni kitu gani utafahamu kuwa katupiwa hayo makombora, ...?' akaulizwa
'Kuna dalili, mfano , ghafla anadondoka, na kuzimia, na ukimuangalia mdomoni, utamkuta na alama za damu, au...anaanguka na kuanza kuweweseka tu,...kama kapagawa....wenyewe wanajua...'akasema
'Na inachukua muda gani mpaka kuzindukana...?' akaulizwa
‘Inaweza ikachukua masaa hata nane, kuna siku tulijua hatazindukana, …’akasema.
‘Kwahiyo kama ulivyosema, ikitokea hivyo, kwanza anadondoka
ghafla, anapoteza fahamu, na inatokea damu mdomoni na puani…si ndio hivyo?’ akaulizwa.
‘Ndio….na
mara nyingi, ikitokea hivyo, nilikuwa namuita rafiki yake mmoja, yeye huyo anajua jinsi
gani ya kumsaidia, basi akija kuna jinsi anamfanyia, haichukui muda, anazindukana hapo hapo au baada ya muda fulani hivi, au
anaweza akachukua hata masaa kadhaa..., lakini baadae anazindukana….’akasema.
'Huyo jamaa yeye yupo wapi, huko huko kijijini, tunaweza kuwasiliana naye kwa hivi sasa..?' akaulizwa
'Mhh, hata sijui...maana hata namba yake kwenye simu...niliyo nnayo ni ya zamani, maana baada ya kuchana na mume wangu, nikaondoka huko, ..na siku nilipokutana naye huyo jamaa alisema simu ya zamani imeharibika,, na sikukumbuka kumuomba namba yake mpya...'akasema
‘Kwahiyo
hili lililotokea lawezekana likawa ni kombora la huyo mwenzake..?’ akaulizwa.
‘Yawezekana,
maana kweli nilipomvamia pale, sikuona akijibu mashambulizi, ndio maana
nikadondoka naye, nilijua yupo sawa, kumbe alikuwa kapoteza fahamu, docta
kasema alikuwa kapoteza fahamu, na pili huyu aliyenipigia simu ni nani, mbona…hata,
sauti kama ni mtu namfahamu..’akasema.
‘Ni
nani unahisi…?’ akaulizwa.
‘Hata
sijui ni nani, ila sio sauti ngeni masikioni mwangu, ngona nitazidi kumfikiria…inaonekana ni mtu ninayemfahmu sana jamaa, na kunifahamu mimi…’akasema
'Au ni huyo raiki yake...?' akaulizwa
'Hapana, sio sauti ya huyo rafiki yake kabisa....'akasema
‘Oh,
sasa itakuwaje…?’ akina mama wakabaki kuulizana
**********************.
‘Jamaa
amefariki…’ilikuwa sauti ya mama , yule aliyekuwa akiongea na docta, na muda
huo alikuwa kaongozana na yule mama mtalaka,…walikwenda naye kumuona docta,
kujua ni nini kinachoendelea.
‘Oh,
mungu wangu, …sasa itakuwaje..?’ akauliza mama mwingine.
‘Hapo
sijui, ila tumeambiwa tusiondoke kwanza, tunahitajika kuhojiwa na polisi…’akasema.
‘Kwanini,
kwani kauwawa, si kafa kifo cha kawaida au polisi wanashuku nini…?’ nikauliza mimi.
‘Kifo
chake kinatokana na mshtuko mkubwa, na kilitokea wakati sisi tunamuhoji,
maswali gani tulikuwa tunamuhoji na kwanini, na kwanini tumefanya hivyo, kwani sisi ni polisi,….ni maswali ya
kawaida lakini tunatakiwa tuwe makini katika kuyajibu...'akasema huyo mama
'Sasa ni hivi, tujiandae kwa hilo, na maswali yanaweza kuwa hivyo, kwa maelezo, tutasema hivi…sisi tulimuita kwa vile
tuna matatizo, na yeye ni mganga, kuna mtu alituelekeza kwake, bahati nzuri tukasikia kaja hapa dar, kuulizia, tukaambiwa kalazwa hapa hospitalini..tuakaja kumuona, tukaomba tuongee naye, …swali
kwanini yeye, ..hapo sasa muwe makini kujibu…
‘Tusemeje…?’
tukauliza.
‘Hapa
hatuwezi kuukwepa ukweli, kuwa matatizo hayo yanatokana na wafanyakazi wetu wa
ndani, na wafanyakazi wetu wa ndani wanafahamiana na huyu jamaa, kwani huko
kijijini kwao ndiye anyetambulikana kwa mambo kama hayo..hapo umemaliza.
‘Je
wakati jamaa anadondoka au anapatwa na mshtuko mlikuwa mnaongea nini, mpaka
ikafikia hivyo, hapo jibu ni rahisi tu, sisi tulikuwa kila mmoja anaelezewa
shida zake..na mara jamaa akaanza kubadilika, na ghafla akakaa kimia, sisi tulijua ndio mambo yake y akiganga, na muda
huo ndio mama mjane akaingia…'akasema
'Ok, tusubiria tu, lakini akiulizia kuhusu huyu mama alipoingia, ...?' akaulizwa
'Yeye aliingia kipindi mgonjwa yupo kwenye hiyo hali, na alipofika kutaka kuongea naye, huyo jamaa akaporomoka chini,...na ndio tukagundua kuwa jamaa hayupo sawa....'akasema
'Mhh....'mimi nikaguna hivyo
'Munielewe hivyo msije kujikanyaga, tukatofautiana maelezo, mkiingiza maneno ,
nahisi..nilisikia, itawapeleka segerea…na ukipelekwa huko unajua shida zake, kuingia rahisi , lakini kutoka, ...ni shida...'akasema huyo mama.
Ni
kweli haikupita muda, tukaanza kuitwa na polisi
*************
Waliitwa hao akina mama kuhojiwa, na bahati nzuri mimi na mwenzangu hatukuitwa, ikawa ni nafuu yetu
Na baaya muda, mara tukaambiwa yule
mama mtalaka wa huyo jamaa akachukuliwa na polisi, kwa maelezo zaidi, kuwa yeye,
anahitajika, kuisaidia polisi, ikabidi sisi tuone jinsi gani ya kumsaidia maana
ni sisi tuliyemchukua huku kutoka huko kijijini kwake kwa ajili ya kuja kutoa
ushahdi.
Taarifa
hiyo ya kifo chake ilitugusa sana, tukikumbuka kuwa ni jamaa tuliyekwisha
kumzoea kwa muda mfupi, na hata kazi tuliyotaka kuifanya na yeye ikawa
haijakamilika, ikabakia swali, je itakuwaje,..hapo vichwa vikaanza kuwaka moto.
‘Kwa hilo lenu
siwezi kulifanya nikiwa humu hospitalini, siwezi kuwadanganya, mimi sina tabia
hiyo ya uwongo, hayo mambo yenu nitaweza kupambana nayo nikiwa majumbani kwenu,
ana kwa ana, na kama kuna mtu kawaambia ataweza haya nendeni mkafanyiwe, lakini
nina uhakika mtakuja kurudi hapa kwangu, na muombe mungu niwe bado sijaondoka,..'
Maneno
haya yakawa yanatucheza akilini, na tulipojaribu kuulizana tufanye nini, jibu
likaja, sisi twende kuonana na huyo jamaa ambaye ni mwalimi wake huyu marehemu..na
kwa bahati nzuri huyu jamaa alikuwa kaja hapa dar, kwa mambo yake binafsi,
tukataka kuhakikisha kuwa hajaondoka…tulipiga simu yake, ambayo huyo mama
muuliza maswali alikuwa nayo, aliipata kipindi anahangaika kutafuta ukweli kuhusu mimi, na matatizo yake na mumewe.
‘Bado
nipo Dar, na …hali yangu kiafya sio nzuri…’akasema, na kweli sauti iliashiria hivyo
‘Unaumwa
nini..?’ akaulizwa.
‘Nina
tatizo la shinikizo la damu, jana ilinikamata mpaka sasa nipo kitandani, kidogo
nina nafuu, …’akasema
‘Oh,
pole sana, sasa tunaweza kuja kukuona…?’ akaulizwa.
‘Kuhusu
nini tafadhali, maana nahitajia kupumzika, maswala ya kazi, sitayafanya kwa hivi sasa, kwanza nataka kuachana nayo kama tulivyowahi kuongea nawe awali…’akasema.
‘Ni
maswala machache tu, ni kazi ndio, unakumbuka nilikuambia kuhusu matatizo ya
mfanyakazi wangu wa ndani, na baadae ukasema kuna madude yamepandikizwa kwenye
nyumba yangu, sasa nataka utusaidia kuyaondoa, kama haiwezekani wewe utuelekeze
kwa mtu mwingine…’tukasema.
‘Mhh..unajua
siku ile hukuniamini, na mambo kama hayo yakiendelea kubakia yanazidi kuleta
madhara, …na yule jamaa aliwaambiaje, hamjawasiliana naye, nasikia yupo huku
Dar, …’akasema.
‘Ndio,
lakini anaumwa…’akasema hivyo, hakutaka kumwambia huyo jamaa, kuwa mwenzake keshafariki.
‘Mbona
…kuna taarifa,ok…..haya mtakuja lini..maana kama nilivyosema hali yangu sio
nzuri, nab ado nipo kwenye michakato ya kuachana kabisa na mambo hayo…’akasema.
‘Kesho
tunakuja…ni muda wako tu….’akaambiwa
‘Sawa,
nitawasubiria…japokuwa kwakweli hali yangu bado sio nzuri...’akaongea kwa sauti inayoonyesha kweli anaumwa
****************
Basi
kesho yake, tulifika sehemu hiyo tuliyoelekezwa kuwa jamaa huyo ndipo alipofikia,
na tulipofika tulikuta watu wamekusanyika, tukauliza kulikoni, tukaambiwa jamaa
mmoja amedondoka ghafla, na hali yake ni mbaya sana…
‘Ni
nani huyo..?’ tukauliza
‘Ni
jamaa mmoja likuja kwa jamaa yake hapa, kutokea mikoani, mara nyingi alionekana
mgonjwa, akiwa ndani, wanasema muda alikuwa yupo sebuleni akiwa kapumzika, alikuwa
akiongea na simu , ghafla, akadondoka, wenyeji wake walikuwa nje, na wao
wanavyosema walisikia kilio kwa ndani, walipoingia wakamkuta jamaa yupo
sakafuni,
‘Ikawaje
sasa…?’ tukauliza
‘Ndio
hivyo kakimbizwa hospitalini..’tukaambiwa,
Basi na
sisi tukaona twende huko huko hospitalini,…tulipofika tukaulizia, kuhuhusu huyo
jamaa tukaambiwa yupo chumba cha wagonjwa mahututi, …hatuwezi kuonana naye.
‘Hali
yake ni mbaya sana…’akasema docta.
‘’Ana
tatizo gani..?’ tukauliza.
‘Shinikizo
la damu, …na limepelekea kiharusi, na kwa uchunguzi wa vipimo, damu imegusa
ubongo,kwahiyo hali yake ni mbaya kwa kufupi…’akasema docta
Akilini
tukasema; yale yale…..
***************
‘Oh,
kwahiyo..?’ ikawa swali la kuulizana tena, na tukasema kwa vile tumefika pale
basi tusubirie tu, ili tujue moja, na baadae tukaenda kumuona docta, docta
akatuuliza sisi ni nani kwake, tukamuelezea, na docta hakutaka kutuficha
akasema;
‘Huyo mzee
amefariki…’tukaambiwa.
‘Kwa
vipi…?’ tukauliza sasa tukichanganyikiwa kabisa, ni kwanini haya yanatokea kwa
watu tuliotegemea watatusaidia kwenye hilo tatizo.
‘Mzeee
kafariki kwa kiharusi,…mshtuko, shinikizo la damu, damu ikavilia kichwani, na
kufariki, zaidi labda mkamuone docta
wake aliyempokea.
‘Sasa na hayo mauchawi jamaa aliyotuwekea
itakuwaje, maana huyo mwalimu wake alisema yeye atatusaidia, nay eye ndio huyo
keshafariki..?’ wakaulizana.
‘Kama
wachawi waliotufanyia hivyo wamefariki , ni nani atafanikisha huo uchawi ina
maana mambo hayo nayo yatakufa, kwanini tuogope uchawi na mungu yupo wa
kutulinda….’wakajipa moyo hivyo
‘Lakini
mnakumbuka kauli zao wote wawili ilikuwaje, kuwa hayo mambo yasipoondolewa
yataanza kuleta matatizo ndani ya familia zetu..’wakasema na hapo ikawa ni
mashaka kwenye nafsi za watu hawa, ikabidi sasa taarifa zifikishwe kwa waume zao.
Mama
mfadhili akawa wa kwanza kumpiga mume wake simu , alipiga simu ya nyumbani,
akijua kuwa mume wake yupo nyumbani, siku hiyo alisema hajisiki vizuri, kwahiyo
atapumzika , hataenda kwenye mihangaiko yake ya kila siku, na alipopiga
akashangaa aliyepokea ni kijana wake, akamuuliza
‘Kwanini
unaongea kinyonge hivyo..?’ akamuuliza
‘Sijisikii
vizuri mama… naona mambo mawili mawili…’akasema
‘Kwa
vipi,..?’ mama akaulizwa kwa wasiwasi sasa.
‘Hata
sijui mama, na alitoka kidogo kununua dawa, alipokua, akawa anaongea ovyoovyo,
kama mtu aliyechanganyikiwa, mimi nikaona nimpe zile dawa zake za kichwa, sasa
hivi amelala, lakini alikuwa kama kapagawa…’akasema
‘Mungu
wangu…na wewe umetumia dawa gani, kwanini na wewe usitumie hizo hizo dawa…?’
akamuuliza
‘Sasa
tukilala wote, ni nani atamsaidia mwenzake,..na ..oh, mama kwani upo wapi, mimi
naanza kuingiwa na mashaka kwanini naona watu wa ajabu..’akasema sasa mama naye
miguu ikaanza kumuishia nguvu
‘Akakata
simu na kuwaambia wenzake,
‘Jamani
mimi naondoka…’akasema
‘Unakwenda
wapi na wewe..?’ akaulizwa
‘Matatizo
yameshaanza nyumbani kwangu tena….’akasema
‘Oh,
ina maana ni kweli, kwangu haitawezekana, mimi namtegemea mungu wangu
atatulinda..’akasema yule mama mwenye nyumba ambapo wote walikutania hapo…,
lakini hata kabla huyo mwenzake hajaondoka, simu ya huyu mama ikalia.
‘Mhh,
simu yangu hiyo, hata sikusindikizi, ngoja niisikilize, utatuambia
kinachoendelea…’akasema akitoa simu yake kwenye mkoba, na sauti ilikuwa ya
askari, ikasema
‘Samahani,
mama, mume wako kapatwa na ajali, alikuwa kiendesha gari kwenye kazi za kila
siku, ghafla akaona kitu mbele yake, kama alivyoniambia maana nilikuwa naye, akajaribu
kukiwepa akagonga nguzo ya umeme, sasa
hivi yupo hopsitalini kapoteza fahamu..’akaambiwa
‘Ok,
hospitali gani..?’ akauliza huyo mama sasa akichukua mkoba wa mwenzake akijua
ndio wake
‘Mkoba
wangu huo mshirika….’mwenzake akasema na simu yake nayo ikaanza kuita…
‘Bado
mimi, mungu wangu wee…..’ilikuwa sauti ya huyo mama mwingine, , mama ambaye alinipeleka hospitalini na
alisema hivyo, baada ya yeye kusikia simu yake ikiita, na aliogopa hata kuipokea..
NB: Je
itakuwaje sasa.....
WAZO LA LEO: Wakati mwingine matatizo yanaweza
kukutokea kwa mfulululizo ya shida, mpaka unachanganyikiwa, na matatizo hayo
yanaweza yakawa yana muelekeo wa jambo ulilolisikia, wewe ulilipuuzia ukasema
ni mambo ya kishirikina, lakini sasa yanatokea kama ulivyoambiwa na watu, au
mtu fulani, Ni muhimu kuendelea kuwa na imani yako kwa muumba wako, wala
usitetereka, kwani mara nyingi,.matatizo haya yanatokea kwa minajili ya
kukupima imani yako, Mungu ni mwingi wa rehema, humpima mja wake kumjua imani
yake kwake, japokuwa anamfahamu . Kwa ma
Ni mimi:
emu-three
1 comment :
Hey there! I'm at work surfing around your blog
from my neww iphone 4! Just wanted to say I love
reading your blog and look forward to alll your posts!
Keep up the excellent work!
Post a Comment