‘Baba
nimegundua kuwa matatizo haya niliyo nayo sababu kubwa ni wewe,….’kijana
alimuambia baba yake
‘Nani
kakuambia hayo, ni nani …?’ baba akamuuliza kijana wake akiwa kama kapigwa kofi
usoni.
‘Nimeshajua
kila kitu baba…, unachonifanyia mimi,..na nakupa siku saba, baba mimi nakupenda sana, nawapenda sana wazazi wangu, ...lakini kwanini unifanyie hivi, kwanini baba, sasa baba, japokuwa, nawapenda, japokuwa nyie ni wazazi wangu, lakini kwa hili umevuka mpaka, ..baba,..nakuomba, ... usiporejesha hali
yangu, nitamuambia mama yoote, mbele ya babu na bibi, unasikia mbele yao, …’kijana akasema na kuondoka..
'Mwanangu sikiliza kwanza...we....'alikuwa ameshaondoka.
Ndio nikaamua kuongea na mtaalamu akasema hiyo ni kazi
ndogo kwake, na kwa vile humo ndani kuna binti ambaye anaweza kulifanikisha hilo, basi atakuja...lakini
pamoja na hayo anahitajika mbwa.
Mbwa…ndio mbwa….!!!
‘Mbwa
, mbwa wa nini…?’ nikamuuliza
Tuendelee
na kisa chetu…..
****************************
‘Nilimuuliza
swali hilo, lakini hakunijibu hapo kwa hapo, akasema tutajua huko usiku
ukifika,…’akasema
‘Kwahiyo
huyo mbwa alitoka wapi..ni wewe ulimtafuta, au…?’ akaulizwa
‘Yeye
aliniambia tunahitajika kutafuta mbwa, na hakusema nimtafute mimi, lakini cha
ajabu kulipopambazuka nikasikia mke wangu akilalamika kuwa kuna mbwa yupo hapo
nje na hataki kuondoka, nikakumbuka maneno ya mtaalamu kuwa hilo kafara la
usiku linahitajia mbwa…basi ili kulificha hilo, nikamwambia mke wangu.
‘Huyo
ni mbwa nimepewa na rafiki yangu, atatusaidia kwenye kazi ya ulinzi wa hapa
nyumbani..
‘Mimi
sitaki mbwa, mimi na mbwa tofauiti,…na kwanini mpaka tutafute mbwa, nani
kakuambia kuna tatizo la wezi hapa nyumbani kwetu…’akalalamika mke wangu.
‘Ni
kuwa huyo rafiki yangu kasafiri, na huyu mbwa wake hana sehemu ya kumweka, basi
nikaona nimchukue tu mimi maana ni mbwa aliyefunzwa vyema…, akirudi atamchukua
mbwa wake, tatizo lipo wapi mke wangu…’nikasema na mke wangu akaondoka bila
mabishano zaidi , na huyo mbwa akawa hapo kwetu, sikujua anatakiwa kufanyiwa
nini kwa muda huo,….na sikuwa na uhakika kuwa huyo mbwa ndiye aliyeletwa na
huyo mtaalamu au la…’akasema
‘Ina
maana hukumuuliza huyo mtaalamu wako….?’ Akaulizwa
‘Sikukumbuka
hili hutaamini, mpaka usiku ukafika….ghafla wakati naingia ndani kutoka kwenye
shughuli zangu nasikia mnguromo wa mbwa, nikashtuka, na nilipochunguza vyema
nikamuona huyo mbwa kalala pembeni mwa nyuma karibu na dirisha la mdada….’akasema.
****************
‘Endelea,
ehe mbwa huyo alifanya nini maana hapo unatutisha…na mbwa tena….’akasema mama
Ntilie.
Mimi alipomtaja huyo mbwa, ndio nikamkumbuka vyema, mbwa huyo nilimuona alipokuja, siku hiyo nilikuwa nafanya usafi, mara nikaona mbwa kasimama karibu na geti, mlango wa geti ulikuwa wazi, nikajua katokea nje, nikamfukuza kwa mawe, ili atoke nje, hakuondoka, badala yake akaja kusimama karibu na mlango, na akawa ananitizama ninvyofanya usafi...
Basi mimi nikamuacha nikaendelea na shughuli zangu, na mama mwenye nyumba alipomuona akaniuliza huyo mbwa katokea wapi, mimi nikamwambia sijui...basi akajaribu kumfukuza lakini hakuweza maana huyo mbwa alikuwa akikimbia kuzunguka nyumba, hatoki nje, na alipochoka kumfukuza akamuacha na kumuuliza mumewe kumuhusu huyo mbwa, na sijui waliongea nini.
Cha ajabu cha huyo mbwa, akawa karibu na mimi sana siku ile, na mimi kwa huruma nikampa chakula mchana ule, na usiku akalala nje, karibu na dirisha langu, nakumbuka kweli, usiku alikuwa akitoa mngurumo wa ajabu, kama analia wakati mwingine kama mtoto, au..kama sauti ya mtu hivi analia.....sikumjali sana, maana mimi nimetokea kijijini, milio ya mbwa, paka, ni kitu cha kawaida huko kijijini.
Ila cha ajabu kingine ninachokikumbuka ni kuwa usiku ile niliota ndoto, kuwa huyo mbwa, kaja kulala na mimi, hiyo ni ndoto lakini,...nikajaribu kumfukuza lakini hakutoka, na nikamuacha akalala ubavuni mwangu..ndivyo nilivyokumbuka na mengine yalikuwa yale ya kukabwa, na nakumbuka huyo mbwa ndiye alikuwa akinisaidia, hadi nilipokuwa sikumbuki tena kilichotokea hadi asubuhi,
Kulipopambuzuka huyo mbwa alikuwa hayupo....!
************
Huyo mzee akawa anaendelea kusimulia,...
‘Usiku
sikuwa na raha kwanza kuhusu kijana wangu, nilijiuliza kajuaje,…maana
yanayotokea usiku inakuwa sisi tumelala,na hatuyaoni….na labda kuna mtu
kamuambia, atakuwa ni nan…nikawa najiuliza bila kupata hjibu.
Na
nikakumbuka kuwa kuna kauli ya wakwe zangu kwa pesa zangu ni za kishetani, na
wao wameshanipa muda nijikoshe, kwa kusema ukweli hayo ninayoyafanya, la sivyo
wao wataingilia kati, hawawezi kuona mtoto wao yupo kwenye maattizo wao wakae
kimia,..na pia wao wamesema wameshagundua ninafanya mambo ya kishirikina, na
kwa hilo watahakikisha nazalilika, hilo sikulijali sana, maana vitisho vyao sio
kwa mara ya kwanza, lakini hili la mtoto wangu lilinifanya nisiwe na raha
kabisa.
Mke
wangu siku hiyo alisema atachelewa maana mke wangu kwa shughuli humtoi, na
hakujua kuwa shughuli zake ndizo hawa watu walitumia kufanikisha mambo yao…’akasema.
‘Kwa
vipi, kwani zinawasaidiaje..?’ akaulizwa
‘Mara
nyingi mke wangu akirudi kwenye shughuli huwa kachoka, hana muda wa ibada, yeye
ni kukimbilia kulala, na hao jamaa ndio wanatumia mwanya huo kufanya mambo yao,
sijui wanajuaje kuwa mke wangu leo ana shughuli na ndio wakati wao muafaka wa
kufika…’akasema.
‘Kwahiyo
usiku huo, wakafika, niliwahisi kama kawaida, na kipindi hicho sikuwa nalala
kitanda kimoja na mke wangu, tulikuwa hatuivani kila mtu na kitanda chake,
…’akatikisa kichwa kusikitika.
‘Kwahiyo
mke wako alikuwa hajui kuwa hali yako imerejea kama kawaida, …?’ akaulizwa
‘Sijui,
nahisi hakuwa anajua na aliona nikiwa na wasichana ni kama kujipotezea pesa tu,
ndio maana hakujali sana….’akasema.
‘Basi
nikawa nasubiri nione mtaalamu atakavyonisaidia,…kumbe alikuwa yupo dar, alikuwja kufuatilia matibabu yake,, ….alikuwa
anahangaika na hospitali, na kwa kipindi hicho alikuwa kaandikiwa kwenda
Muhimbili. Kwahiyo haikuwa ile safari ya kutoka huko mikoani, ….’akasema
‘Ulijuaje…?’
akaulizwa
‘Alikuja
kuniambia baadae….’akasema
Usiku
wakafika na kikosi chake, na nilihisi kuwa wapo kamili, kuna hali niliihisi hivyo,
na na ile hali yangu ya kuishiwa nguvu ikanijia, na nakumbuka wakati hali hiyo
inatokea, nikaona mke wangu akihangaika, akipambana pale kitandani, na hata
kabla sijapotezaa fahamu zangu kabisa, nilimuona mke wangu akiinuka kitandani,
ana akawa anatoka nje, ….nikajua itashindikana..na hapo hapo mimi nikazama
kwenye giza…
***************
Mimi
sikujua kilichotokea ule usiku, …ila asubuhi mke wangu alkuwa hayupo,
nikaulizia, wakasema mke wangu aliondoka usiku huo hukalala hapa nyumbani…nikampigia
simu, na akasema;
‘Nipo
kwetu,….’akasema
‘Kwanini…?’
nikamuuliza
‘Sikuweza
kulala usiku, mbwa, alikuwa akitoa mngurumo wa ajabu, kuna milio kama ya
bundi…kuna hali nahsi kuna watu wanaifanyia mabaya, nikaona humo ndani
hakulaliki, ndio nikaondoka…’akasema
‘Sasa
mbona mimi nimebakia humu ndani, kwanini hukuniamuisha…?’ akaulizwa
‘Nilikuaga,
lakini hakusema kitu,…ulikuwa kama unaweweseka weweseka, nikajua ni dharau zako
tu…, nikaondoka zangu, na wakati napita kwa huyo binti nilisikia makelele
fulani , nikajua ni kawaida yake ya kuota , sikutaka kusubiria, nyumba ilikuwa
inatisha muda huo, ajabu nilipotoka nje sikumuona huyo mbwa, wakati nikiwa ndani
nilisikia sauti ya mngurumo kama wa mbwa…’akaniambia.
‘Huyo
mbwa atakuwa alienda wapi, au alikuwa katoka nje…?’ nikamuuliza
‘Mimi
sijui alienda wapi , sikutaka kujua, nikaondoka zangu…’akasema
‘Ni
kijana wetu je, hukutaka kumuangalia, ulijijali mwenyewe…?’ nikamuuliza mke
wangu.
‘Kwanini
nisimjali, nilipotoka nilikwenda chumba chake, na kugonga, hakukuwa na mtu
ndani, nikajua hakulala humo ndani…’akasema mke wangu.
‘Atakuwa
alienda wapi usiku huo..?’ nikamuuliza mke wangu.
‘Labda
alikwenda kulala kwa marafiki zake, alinilalamika kuwa kuna jambo linaendelea
humu ndani, linampa shida, usiku analala kwa shida, na hali yake imekuwa mbaya
sana anahisi tatizo linatokea humu ndani, sikutaka kumuuliza sana mambo hayo,
maana sitaki mambo ya kishirikina,…kwahiyo kuanzia sasa kaamua,kuwa hatalala
hapa nyumbani siku zote…’akasema
‘Atakwenda
kulala wapi, na kwanini hajaniambia mimi mmwenyewe…?’ nikauliza
‘Kasema
anakuja kulala huku kwa babu yake, na hilo la kwanini hajakuambia sio kweli,
kasema kuwa keshakuambia, na kakupa wiki moja umpatie jibu….’akasema
‘Kaniambia
nini, wiki moja ya nini,…kasema hivyo, anataka jibu gani..?’ nikamuuliza,
nikijifanya kushangaa
‘Kasema
wewe unajua ni kitu gani, na kaapa kuwa usipompa jibu atakachokifanya humu
ndani tutakuja kumsikia kwenye vyombo vya habari, sasa labda nikuulize wewe
kuna nini kinachoendelea humo nyumbani kwetu, nisingelipenda kusikia
yanayosemwa na wazazi wangu lakini hali iliyopo inanilazimisha kuamini hayo…’akasema
‘Kwani
wewe hajakuambia ni kitu gani…?’ akaniuliza
‘Kaniambi
wewe unajua kila kitu, sasa ukiniuliza mimi nakushangaa, hamjaongea naye…?’akasema
na kuniuliza
‘Oh,
haya ngoja nitaongea naye..’nikasema
‘Mim
sitarudi hapo nyumbani kwa leo, nitakuwa narudi mara moja moja kuna kazi
naifanya kwanza, …huyo binti atakusaidia saidia kazi za hapo nyumbani,..ila
nakuonya huyo binti wa watu, kama kuna lolote unalomfanyia, sitakusamehe kabisa…muogope
mungu…’akasema.
‘Nimfanyie
nini mimi huyo binti,…., si unanijua nilivyo, hali yangu si unaijua, ukiniona
nastarehe, ni kujipooza tu , ili kuondoa mawazo…’nikasema.
‘Ulivyo
eeeh, unanifanya mimi mtoto mdogo, sioni kinachoendelea, unakumbuka uliniambia
kuwa unajiona umepona, je ulipona nini…kwako wewe kupona imekuwa kama ng’ombe
wa ndani kufunguliwa nje, unaparamia kila mtu, haya endelea na tabia yako hiyo
mbaya, unachokitaka utakuja kukipata, …’akasema.
‘Mke
wangu hayo umeyapatia wapi, hali sasa mbaya, wewe huoni, …?’ akaniuliza
‘Umenisikia
bara bara, na kwa vile hata mtoto wako kakufahamu ulivyo..basi itakuwa rahisi
kwangu, kuchukua hatua muda ukifika, usije kusema sikukuambia,..nasubiria
watoto wengine wakija watoto ndipo kila kitu kitawekwa bayana,, sasa hivi
naogopa kumuumiza kijana wangu…’akasema
‘Ndio
maana umekwenda kwenu, kumbe umeshaanza kuwafuata wazazi wako wanavyotaka au
sio, sas ahuko unafuata nini wakati wazazi wako hali zao ni mbaya…?’
nikamuuliza
‘Nilikuwa
sina sehemu nyingine ya kwenda usiku huo, mimi siwezi kuchukua haya mambo
kiharaka hivyo, ninajua sheria za ndoa, na mimi ni mtu mnzima…muda utafika
utapata nafsi ya kufanya hayo unayoyataka, siku hizi si una nyumba, una pesa,
au…’akasema
‘Mke wangu,
si nimeshakuambia, sasa hivi hali imekuwa mbaya, kuna mambo yamekwenda tofauti
kabisa.. hali imeharibika nyumba , magari yamechukuliwa kulipia
madeni…’nikamwambia mke wangu.
‘Kwanini
leo unaniambia hayo mambo yako…?’ akaniuliza
‘Wewe
ni mke wangu lazima nikuambie mambo yetu ya famalia, nilishakuambia kuwa hali
ni mbaya, hukutaka kuniamini, na…na… haya yote nilikuwa nikifanya kwa ajili ya
familia yetu…’nikasema.
‘Yatakushinda,
ila nakuonya, kama kuna kitu unachokifanya kwa ajili ya wazazi wangu,
utakachokipata utakuja kujuta, hawa ni wazazi wangu, na sijui kwanini
unashindana nao…’akasema
‘Nani
kakuambia hayo mke wangu, hayo ni mawazo yao, kama wameishiwa wameishiwa kwa
mambo yao wasinisingizie mimi…’nikasema.
‘Sio
swala la kuishiwa, kwani kuishiwa imeanza leo, wazazi wangu wamekuwa wakikutana
na mitihani kama hiyo mara kwa mara, na wanakuja kuinuka tena, biashara ndivyo
zilivyo, wao hawafanyi mambo ya kishirikina, kama ya kwako..’akasema,
‘Mambo
gani hayo ya kishirikina mke wangu mbona huniamini, kama ningelikuwa nafanya
hivyo si ungeliniona,..?’ akauliza.
‘Kuna
mtu alikutwa nyumbani kwa wazee akiwa uchi, ..anafanya mambo ya ajabu
alipobanwa sana akasema katumwa kuchukua vitu humu kwa wazazi wangu na
wewe…’akasema
‘What!!…na
mimi kwa vipi, …’nikauliza huku miguu ikiniishia nguvu.
‘Ndio
hivyo huyo mtu kachukuliwa na polisi kupelekwa kituoni,…’akasema
‘Kituo
gani hicho, nitakwenda kumuona maana mimi sijui kitu kama hicho,…’nikasema
‘Kumuona
wapi,…maana hapo walipokuwa wamemfungia, hawakukuta mtu, walikuta mbwa, na huyo
mbwa sawa na huyo niliyemuona hapo nyumbani, sasa najiuliza iweje, mtu ageuke
kuwa mbwa, wewe mwanaume niambie ukweli kuna kitu gani kinachoendelea hapo
nyumbani kwangu…’akasema mke wangu.
‘Mungu
wangu, mi-mi….sijui kitu mke wngu na huyo mtu ni muongo mnafiki tu, usiwasikilize hao watu, na uwe unaniuliza mimi kwanza…’nikasema kumuambia mke wangu.
‘Siku
zenu sinahesabika, najua kuna jambo unalifanya, ... ila jingine tena la muhimu, ni kuhusu huyo binti wa watu, hajui kujitetea, hataki kunieleza ukweli, ila najua kuna kitu mnamfanyia, ...nakuonya tena kuhusu huyo binti wa watu ogopeni hao watu, mayatima,..masikini, hivi hamna huruma nyie watu....sawa ngoja tuone mnachokitaka kitaishia wapi, utakuja kujuta kwa hilo…..’akasema
'Mke wangu achana na mambo hayo ya kishirikina...'akasema
'Na je huyo mbwa bado yupo hapo nyumbani..?' akaniuliza
'Ina maana ndiye unamuogopa, mimi sijamuona hapo nje...'nikasema na yeye akakata simu.
Kiukweli kauli hiyo ilinichoma moyoni, nilijaribu kuvuta hisia,...nikijaribu kuona ni kitu gani hao watu walimfanyia huyo binti...lakini baadae nikapotezea, kujipa matumaini...sio mimi niliofanya hayo japokuwa ni mshiriki, .., shauri lake huyo mtaalamu, na watu wake...hata hivyo sikuwa na raha...niliona mambo yanazidi kuongezeka, ndio nikatoka nje kuhakikisha kama huyo mbwa hayupo kweli,..hakuwepo
'Huyu mbwa kaenda wapi...?' nikauliza lakini hakukuwa na mtu wa kunipatia jibu, binti alikuwa anafanya usafi huko jikoni na sikutaka kuonana naye, nafasi inanisuta...
Baadae ndio nikasema;
'Ngoja nimpigia Mtaalamu simu yeye atanisaidia kwa haya mambo maana naona hali inazidi kuwa mbaya...'nikasema na kuchukua simu yangu kumpigia huyo jamaa
****************
Nikampigia simu mtaalamu..nikapiga simu
ikawa inaita tu, haipokelewi, nikajaribu tena na tena, na nilipotaka kukata tamaa baadae ikawa hewani, na alipopokea sauti niliyosikia ilikuwa ya mgonjwa aliyezidiwa sana.
‘Mtaalamu
vipi, mbona simu hupokei..?’ nikamuuliza
‘Oh,…
mimi naumwa sana hali imekuwa mbaya ghafla, tokea nirudi jana usiku, mambo
hayaendi vyema, nahisi adui yangu huyo…’akawa anaongea sauti ya mgonjwa ambaye
hata kuongea ni shida,
‘Unaumwa
nini….?’ Nikamuuliza
‘Si
nilikuambia naumwa, nimekuja hapa Dar, kwa matibabu, na…hali inazidi kuwa
mbaya, hiyo jana usiku nilifika kwa nguvu za mizimu na kilichonipata huko
kimenizididshia matatizo….’akasema.
‘Kwahiyo,
jana hukufanikiwa , nitamuambiaje kijana wangu sasa , …?’ nikamuuliza
‘Nitakuambia
subiria nipate dawa hali ni mbaya sana…yule mbwa, wamemkamata…na yeye ndiye ooh,
kijana wako, ngoja nitakuambia, su-su--aaah….’simu ikakatika.
NB:
Naishia hapa kwa leo, kuna mambo naweka sawa kuhusu sehemu hiyo inayokuja...ili tuweze kuhitimisha hiki kisa bila maswali megi....
WAZO LA LEO: Ukiishi kwa kutegemea dhuluma, ukawa
unafanya mambo ya kishetani, kula yako, kipato chako, maendeleo yako, mienendo
yako,..hakika wewe ni shetani kimatendo, na kwahiyo wewe unakuwa adui wa
mwenyezimungu, tubia ewe mwana –wa adamu kabla milango ya toba haijafungwa,…
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment