‘Halafu
ndio ukataka kumuoa huyu mdada, au sio,..? ‘akauliza na kubakia kimia, halafu
akainua kichwa kumuangalia mdada, na kukunja uso, mdada atakatabasamu, na
kutikisa kichwa kuashiria kuwa sasa mzee mzima kapatikana.
Sasa
tuanzie hapo, usiogope tupo sawa, au…’ akaambiwa
‘Sawa
tuendelee, tatizo, hayo maswali yako yanajirudia rudia kama kunitega…’akasema
‘Hapana,
ni lazima nikuulize ili nikuamini, mimi hapa nawawakilisha wenzangu sitaki
niwaangushe, umenielewa hapo,, swali langu ni hili…’akasema akimuangalia jamaa
na jamaa naye akamkazia macho.
‘Je
huyu mdada ulimuona wapi kwa mara ya kwanza, ukampenda..na hata kumtaka
kumuoa?’ akaulizwa
‘Mhh,
lakini,….’akatulia kidogo, halafu akasema;
‘Ok,
sawa nitakujibu usije kuniona siwajali wateja wangu..’akasema
‘Sawa
kabisa, haya tujibu…’akaambiwa
‘Kuna
kipindi walikuja na …na.rafiki yake aliyemleta huko kijijini, unajua huyu
alikuwa anaishi mjini na mama yake, waliondoka akiwa mdogo sana, kwahiyo huko
kijijini kwa asili yao, hapajui, alipoletwa ndio nikamuona…’akasema
‘Kwahiyo
kwa mara ya kwanza kumuona sio siku alipokuja kutaka kutibiwa..au sio?’
akaulizwa
‘Nahisi
hivyo…’akasema akiangalia pembeni.
‘Aaah,
jibu swali, wewe ni mtaalamu unajua mambo zaidi yetu, huwezi kuhisi unajua au
hujui sema ukweli wako,…?’ akaulizwa.
‘Ndio
kwani kuna taizo hapo mara ya kwanza nilimuona tu, nikaongea na rafiki yake,
ili anitambulishe kwake, na mara ya pili ndio nikakukutana naye ndio
nikamuelezea lengo langu kuwa mimi nataka kumuoa,….’akasema.
‘Yeye
akakuambiaje?’ akaulizwa.
‘Eeeh,
unajua tena wanawake, hakunijibu hapo kwa hapo,..alisema tu, yeye hajataka
kuolewa kwa sasa, na kitu kama hicho anahitajia muda wa kutafakari…kiukweli
nilishangaa sana, maana sikutegemea…’akasema.
‘Kwanini…?’
akaulizwa
‘Kwa
maono yangu, sikutakiwa kukataliwa…japokuwa hakusema hanitaki hapo hapo…, maana
wengi wananitaka niwaoe, lakini mimi sikutaka kuoa haraka baada ya kukosana na
mke wangu wa kwanza, nilihitaji muda wa kutafakari, na ili niweze kumpata
ambaye tutaendana naye…, sikutaka kukurupuka tena..’akasema.
‘Ni
kweli hayo..kuwa wengi wanakutaka, …mbona awali ulisema watu wanakuchukia, sio
ndio pamoja na hao mabint…?’ akaulizwa na hapo kidogo akasita, na baadae
akasema.
‘Mbona
maswali yako hayalengi swala husika, kwani wewe unahitajia nini hapo, mimi
nilitaka uniulize maswala ya tiba au sio…sasa naona maswali kama ya polisi
unanitia wasiwasi kidogo, lakini mimi isjlai wewe uliza tu..?’ akauliza.
‘Mimi
nina mashaka na wewe kuwa matibabu yako yana walakini, ndio maana nataka
kujirizisha, kwanini huyu mdada alikukukataa, kwanza ulipomtaka umuoe, na pili
huko kwenye matibabu, kwanini…?’ akaulizwa.
‘Mimi
ninavyohisi eeh,…labda, na ndio hivyo yeye alisikiliza maneno ya mitaani…..’akasema
akimtupia jicho mdada, na mdada akawa anatabasamu tu, tofauti na ilivyokuwa
kwangu, nilikuwa nimekunja uso kwa hasira.
‘Maneno
gani hayo ya mitaani mpaka akukatae wakati umesema wewe kwa uaoni wako
asingelikukata,..?’ akaulizwa na hapo akatabasamu na kutikisa kichwa, akasema;
‘Unajua
sasa nimeelewa, nyie mlishaongea na huyu mdada akawaelezea yote wanayoyaongea
watu huko kunihusu mimi, huo ni uwongo, msiwaamini kabisa hao watu, nilimuambia
huyu mdada, asiwasikilize, na akija kwangu atapata kila kitu anachokihitajia,
haamini, sasa….’akasema.
‘Aaah,
kwasasa tunaongea na wewe, sio wao, na hilo unalosema kuwa tunawasikiliza watu
wa huko sio kweli, hatujaongea nao, sisi tumekuja kwako rasmi ili ikiwezekana
tupate huduma yako, sasa jiamini kama docta wa kienyeji, maana wewe ni
mtaalamu, huogopi, au sio…?’ akaulizwa.
‘Watu
kule hasa maadui zangu wamekuwa wakinipakazia uwongo, nahisi huyu mdada
alipofika, na kuwaambia kuwa mimi nataka kumuoa, wakamuambia kuhusu huo uvumi
usio na ukweli…ndio akanikataa, kwasababu hakunikatalia hapo hapo, alisema
nimpe muda, jibu akaja kumpa rafiki yake kuwa hanitaki…’akasema.
‘Hebu
kidogo hapo, huo uwongo wa watu wa mitaani, unasemaje, walikuwa wanakusema
kuhusu nini..?’ akaulizwa hapo akakaa kimia na mama huyu akaliacha hilo swali
na kuuliza swali jingine. Na kabala hajauliza akaingia docta na kuomba kuongea
na mmoja wa akina mama yule aliyeongea naye awali, akamuita kwa nje.
Baadae
huyo mama akarudi, na kusema;
‘Tuendelee,
nashukuru docta katupa muda zaidi, ….’akasema huku akiwaminyia wenzake jicho.
Kuna
kitu kinachoendelea kati ya hawa akina mama…, na huyu mgonjwa alikuwa hajakigundua,
kwasababu wakati wanapeana ishara za macho mara nyingi yeye huwa kainama,
nahisi angeliwaona angeligundua kuwa wenzake wana jambo dhidi yake.
**********
‘ Sasa
kutokana na muda, ..twende haraka haraka, jamani wenzangu huyu mimi
ninavyomuona anaweza kutondolea hili tatizo, kwasababu katutisha sana,…’akasema
‘Sio
nawatisha, ni kweli, ogopeni haya mambo, hayatibiki hospitalini…na hawawezi
kuyaona, utapata shida, unatibiwa huku na kule, kumbe tatizo ni jingine kabisa…mimi
nimewajali sana, mpaka nikachukua hatua hii…’akasema
‘Ni
sawa, .. lakini mimi bado nina Swali,…kuhusu mtalaka wako, umesema yeye
mlikosana naye, bado sijaridhika na huko kukosana naye, unaweza kutufafanulia
kidogo hapo maana mtu anapokosana na mkewe au familia yake, lazima kutakuwa na
walakini kati ya mmojawapo, na hapo ndipo unaweza kumpima mtu..?’ akaulizwa
‘Hahaha…sawa
mimi nitawajibu tu,…unajua kijijini usipokuwa makini, utakosana na kila mtu, na
hasa ukiwa na maendeleo watu wengine watakuonea wivu, nilmuambia mke wangu awe
makini, lakini hakunisiliza mimi ,akawa anawasikiliza watu wa nje, nikamuambia njia ni nyeupe, aondoke zake…’akasema.
‘Hivyo
tu..mbona haiji akilini, hivi kweli mke unampenda, itokee kosa kama hilo,
umuambie nje nyeupe aondoke,..kwahiyo akaondoka kwasababu hiyo..?’ akaulizwa.
‘Kama
kuna mengine, ni ziada tu…, lakini la kwangu muhimu ni hilo, na kwa vile
hakunisikia,..tena na tena, nikaona sasa nimeoa au nimeolewa, nikamkabidhi
kilicho chake, akaondoka, ..kwaheri kabisa, sio kwa kupigana, hapana mimi sina
tabia hiyo…’akasema.
‘Mliwahi
kusuluhishana kwenye mabaraza ya wazee au ilikuwaje, kwenu..?’ akaulizwa
‘Tuliwahi
tena sana, sikupendelea kufanya hivyo…lakini niliona nifuate utaratibu wa
kinyumbani,, na aliyoyaongea hapo kwa wazee, ni yale yale wanayoyaongea watu huko
mitaani..fitina, majungu…iliniuma sana, mke wangu na yeye hataki kuwa upande
wangu akanitetea, na yeye anaunga mkono maneno ya mitaani, kiukweli
nilikasirika, ..na nikaona hanifai..mtu anatoa siri zangu, na zingine sio za
kweli anaongezea na chumvi, hapana nikaona hanifai ….’akasema akitikisa kichwa
‘Kabla
hatujazijua hizo fitina,..maneno ya watu, nk..ngoja turudi kwa huyu mdada,
tunataka tuliweke hili sawa maana tunataka umtibie na yeye, na tunataka na yeye
aondoe chuki , na kama ikibidi , sisi tutamsihi muoane, au sio…sasa ni wewe tu
kujikosha kwetu,…’akaambiwa.
‘Hahaha,
ndio maana nimekubali kuwajibia maswali yenu yote, najua nyinyi ni waelewa, na
mtamuelewesha huyu binti, kwakweli nampenda sana…’akasema
‘Unajua
sisi tunajiuliza tu, huyu na yeye, umsema naye kasikiliza maneno ya nje,
kwahiyo kitabia hana tofauti na mtalaka wako, kwa haraka tunaweza kusema hivyo,..natabia
za mke utaziona mapema,… au sio, sasa kwanini bado umemshinikiza kutaka kumuoa..?’
akaulizwa.
‘Hapana,yeye
kwa muda mfupi niliomchunguza hawezi kuwa kama huyo mtalaka wangu mimi nina
imani tukioana mimi nay eye, atanijulia
, na atanielewa, nimempima nikaona nimuelewi zaidi, unajua yule wa mwanzo, niliongea
wee, nikamkanya, tukasuluhishwa, lakini hakubadilika kabisa, ikafika muda
akasema wazi kuwa hanitaki…’akasema
‘Akasema
kabisa hakutaki, kwahiyo sio wewe uliyemuacha kwa ridhaa yako, ni yeye
alikukataa, au mbona unatuchanganya..?’ akaulizwa
‘Baada
ya kushindwana na kuona msimamo wangu ndio akasema hanitaki, lakini mimi
nilishafikia hatua hiyo kuwa hatutaelewana tena,….nikamuacha…’akasema.
‘Hapo,
bado….unatutia mashaka, tunaogopa kama ukimchukua huyu binti yetu, inaweza
ikawa sawa na huyo mtalaka wako….tuthibitishie, na ukweli wako ndio utatusaidia
kutoa maamuzi, ya kutibiwa kwako na ikiwezekana tumshawishi huyu bint, huenda
akakubali…’akaambiwa.
‘Huyu
nina imani, hatakuwa hivyo..na mimi nitajaribu kujishusha, nimegundua kuwa awali
nilichukulia mambo kwa hasira, …unajua ujana tena, sasa nimeshakua mtu mzima,
hatutakosana kabisa, muhimu asiyasikilize maneno ya mitaani…’akasema.
‘Hivi
hayo maneno ya mitaani ya yepi..?’ akaulizwa na mama mwingine na huyu muuliza
maswali akatikisa kichwa kumuashiria mwenzake asiende haraka hivyo, lakini
swali lilishaulizwa, na jamaa akasema;
‘Achana
nayo…hayana maana hayana ukweli…’akasema
‘Unaogopa
kuyasema…au?’ akaulizwa.
‘Sio
kwamba naogopa kuyasema, unajua vitu vingine uongee ukiwa na ushahidi, mtu
anakuambia eti wewe ni muhuni, unatembea nje, una …warubuni wanawake kwa madawa
wanajileta wenyewe kwako..ni mambo hayo ya uwongo kabisa, mimi sina tabia hiyo
mimi nilikuwa muaminifu kwenye ndoa yangu ,maana kazi yangu inanikataza kufanya
hayo mambo…’akasema
‘Una
uhakika na hilo..?’ akaulizwa.
‘Uhakika
wa lipi hasa..kuwa mimi sina tabia hiyo..ndio ukweli wenyewe kazi yangu
inanibana nisiwe hivyo, sina shaka na hilo na kwanini waseme hivyo,
wangeniambia nimetembea na huyu na yule kama wanavyodai wao, basi angenionyesha
hao watu, lakini alikuwa hana ushahidi, kama hao wapiga domo wa nje, hawana
kazi, kazi zao ndio hizo, ndio maana hawana maendeleo..’ akasema.
‘Kwahiyo
wewe kamwe hujawahi kutembea nje na mwanamke mwingine,…wewe si rijali,..ndivyo
mnavyojiita, aah, sema ukweli bwana,..?’ akaulizwa
‘Hahaha..hayo
tuyaache,….’akasema.
‘Sasa na hilo la kuwa unarubuni wanawake kwa madawa
ni maneno tu, kweli hujatokea kuwapenda, hasa wateja wako maana waganga ndio
zenu akija unampenda, unataka umjaribu, ?’ akaulizwa
‘Hapo
nahisi unanitega…..’akasema
‘Ni
hivi nakuuliza hivyo nikiwa na maana, hata sisi wanawake tunataka hayo madawa,
kuwaweka sawa wanaume zetu,..unayo hayo madawa?’ akauliza.
‘Ninayo
sana…’akasema kwa kujitapa.
‘Na
hayo madawa yanafanyaje kazi…?’ akaulizwa.
‘Ni
kutegemea na wewe unataka nini, kumfanyaje mke au mume wako…wewe unafunguka
unavyotaka.., nataka hivi na vile, na mimi nakutengenezea kabisa, na
inafanikiwa, haina shaka…’akasema.
‘Na unayo madawa ya kumvuta mwanamke akaja
kwako, na ukamfanya utakavyo, au, …ulisema awali hata wabaya wako unapambana
nao kihivyo, si ndio hivyo, mfano umempata mwanamke ukampenda, lakini hataki,
wewe si una dawa za kumpata, au hata kwenda kwake usiku ukamfanyia utakavyo, …?’
akaulizwa.
‘Mhh,
swali lako limekaa kimtego, lakini nikujibu hivi…waganga wanaweza kufanya
madawa ya namna hiyo, na kuwapatia wachawi, ili wao wakatimize malengo
yako,..kama unataka kwenda kwa mtu usiku amelala, basi unafanyiwa hiyo dawa..na
kweli unafika usiku wao hawakuoni, wakiwa wamelala, ukafanya unayotaka
kuyafanya, sasa mimi nawatibia kujikinga na hayo mambo, na hayo mazindiko wanayowawekea
,…’akasema.
‘Ninachotaka
hapa ni uhakika, kuwa hata nyie waganga mnaweza kufanya hivyo,yaani kutengeneza
dawa na kufanya kazi za kichawi…?’ akaulizwa.
‘Tukitaka
ndio tunaweza,…si ninajua dawa zake, pia ninajua zinavyofanya kazi, kwanini
nishindwe kufanya hivyo….’akasema kama kujitambia.
‘Kwahiyo
unakubaliana na mimi kuwa waganga wa kienyeji kama wewe pia ni wachawi …?’ akaulizwa
‘Inawezekana,
siwezi kukataa, kwa msimamo huo…inategemea sasa na tabia ya mtu mwenyewe, au malengo yake ni nini…’akasema
‘Kwahiyo
hata wewe unafanya hivyo, au uliwahi kufanya hivyo…?’ akaulizwa
‘Mimi
kama mimi, kwanini nifanye hivyo, kwanza nimeshakuambia, kazi yangu ina
miiko,siwezi mimi kufanya hivyo, kama ninataka kupambana na mtu, maana wenyewe
kwa wenyewe tunajaribiana, pia kuna maadui zako unataka kuwakomoa, nitafanya
hivyo, lakini kwangu mimi aah, kwanini nisumbuke, ninaweza kufanya hivyo ikinilazimu lakini kwa kupitia kwa mtu mwingine…’akasema.
‘Kwahiyo
wewe ukitaka kumkomoa mtu, au ukitaka kupambana na adui zako, au ukitaka kulazimisha jambo liwe kwa hao unaowaita maadui zako au yoyote yule , wewe huwa hufanyi hivyo peke yako, unawatumiwa watu wengine...sasa unawatumiaje, je utakuwaje na uhakika kuwa kazi yako imefanyika...?' akaulizwa
'Uhakika kwa vipi, maana unayemtuma hawezi kufanya tofauti na wewe..yeye anafuata dhamira yako, anakuwa sio yeye tena hajitambui kabisa.. na wakati mwingine unaweza kuongozana na yeye,, ukitaka kuhakikisha, si ndivyo unataka kujua hivyo au..?’ akasema na kuuliza.
'Kwahiyo wewe mara nyingi unafanya hivyo ukitaka kufanikisha mambo yako, labda kwa maadui zako au kwa mpinzani wako, si ndio hivyo., na mara nyingi kiuhakika na wewe unafika kushuhudia kuwa kazi imefanyika au sio, kwahiyo kila kilichotendeka ambacho kina kuhusu wewe utakuwepo, au sio.....?' akaulizwa
‘Mimi hahaha, wewe bwana wacha kunichanganya, nikuambie kitu,…usitake
kunijua zaidi, ukitaka hayo, utanihisi vibaya bure..., mimi sio mbaya kihivyo, ila
ukinichokoza, kazi yangu ni kubwa wenyewe waulize watakuambia ...hata hivyo najiuliza ni kwanini unaniuliza mswali kunihusu
mimi, au huyu mdada kawaambia nini cha kuwatia mashaka? ’ akauliza.
‘Swali
langu lipo wazi, usiogope kujibu, jiamini, je wewe ukitaka, hasa kwa maadui
zako unaweza kufanya hivyo, au sio…?’ akaulizwa hapo akakaa kimia kidogo.
‘Naona
unaogopa kulijibu hilo swali, kwanini unasita, unaogopa nini…?’ akaulizwa
‘Sio kwamba
ninaogopa, niogope nini, mimi najiamini,…tatizo maswali yako mengi ya sasa yana
mlengo wa kunishutumu hivi, labda mdada kalalamika kwenu...hapana sivyo hivyo mnavyofikiria nyie, kama ningelikuwa na nia mbaya nisingeliwaita kuja kuwasaidia…’akasema akimtupia jicho mdada,
unajua mdada alikuwa kasimama mbele yake, wanakuwa kama wanaangaliana kwahiyo
hakuwa na ujanja ni lazima kila akiinua uso wanaangaliana, na hilo naona
lilikuwa linampa shida.
'Sasa kwanini hujibu swali...?' akaulizwa
‘Kwanza,
unielewe mimi ni mganga wa kusaidia watu, mara nyingi, waganga walivyo,
wanaweza kujaribu madawa yao, kama yanafanya kazi, kwahiyo wanaweza kujigeuza
wachawi pia wakitaka…wengine kwa malengo ya kuthibitisha madawa yao,, au kuonyesha ubabe wao, yote yawezekana japokuwa
sio wachawi, wapo watu wa namna hiyo…’akasema.
‘Na
wewe ni mmojawapo.. au sio?’ akaulizwa, akimuangalia huyo mama huku akicheka, …
‘Hahaha,
hayo tuyaache, maana utataka nikueleze kila kitu ninachokifanya, kitu ambacho
hakiwezekani..kifupi ndivyo ilivyo kwa waganga na wachawi na tofauti zao…, na
ndio maana nawashauri msikimbilie tu watu ovyo, uliza kwanza, huyu mdada
angenisikiliza mimi nahisi sasa hivi angekuwa hana tatizo kabisa…’akasema
‘Kwahiyo kumbe kosa lake ni kutokukusikiliza wewe, ikiwa ni pamoja na kwa vile kakutakaa au sio...?' akaulizwa
'Hapana sio kwa vile kanikataa, kwa vile alipopatwa na matatizo hakutaka kunisikiliza mimi yale niliyomshauri, akaona aende kwa wengine, huko wakamdanganya, ndio walimtibia lakini mengine sio sahihi, hao ni maadui zangu, wanaweza kusema mambo ili kuniharibia.....'akasema
'Nina imani kuwa angekukubalia wewe umuoe, asingelipata hiyo mitihani, au sio…?’ akaulizwa
‘Hahaha,
hapana,.... usije kunifikiria hivyo, kuwa labda kwa vile yeye kanikataa, basi mimi ndiye
niliyemfanyia hivyo, kwanini nifanye hivyo wakati nikitaka naweza kumvuta kwa
namna nyingine,….’akasema
'Kwa namna nyingine kwa vipi..?' akaulizwa
'Hiyo ni siri yangu, siwezi kuwaambia mbinu zangu za kuwashinda maadui zangu...'akasema
'Kwahiyo mtu akikataa matakwa yako, mara nyingi anakuwa adui yako, au sio...?' akaulizwa
'Sio lazima, lakini kama inabidi..lakini sio lazima...'akasema
'Huyu mdada alipokukataa, wakati hapo kijijini wanakuogopa, ukitaka jambo lako unapata, au sio, wewe ni mganga mwenye kuogopwa, na kusifika pia, ..hebu tuambie, alipokukata huyu mdada ulihisi vipi, kukasirika, kuwa kakuzalilisha kwa vile hujawahi kukataliwa au ulijisikiaje..?' akaulizwa
'Kawaida tu...'ni hivyo tu, sina zaidi ya hayo..nimechoka....'akasema akibenua mdomo kwa dharau
'Sema ukweli...kama ulivyoniambia...'akasema mdada, na jamaa akamtupia jicho baya mdada, halafu akakwepesha kumuangalia, na kutikisa kichwa kama kusikitika, hawa akina mama wakawa wanaangaliana huku wanatikisa kichwa kukubaliana kwa ishara, kama vile muda umefika...
************
‘Ndugu
unajua nimekuuliza maswali mengi sana nikitaka kujua jinsi ulivyo…naona na muda
nao umetutupa, tutakuja kufukuzwa humu,nia yangu ya kukuuliza hayo ni kutaka
kukufahamu, jinsi ulivyo,maana sisi kama ulivyosema tuna shida, kama
ulivyotuambia tumewekewa mazindiko au sio, sasa hatuwezi kukurupuka tu kwa mganga, lazima tumuulize maswali tumpime kweli kazi anaiweza, …’akasema
‘Sawa
kabisa, kwahiyo mnasemaje?’ akauliza
‘Lakini
bado najiuliza, sio wewe uliyempigia simu mwenzetu hapa, ukasema kuwa wewe
ulikuwa hivyo ulikuwa mchawi, …kwenye simu, au nimekosea mwenzangu…?’ akageuka
kumuulizia mwenzake, na mwenzake akasema
‘Kanipigia
mwenyewe, hata sijui alivyoipata namba yangu ya simu, maana siku ile sikumbuki
kumpa namba yangu hata mimi nimejiuliza sana…’akasema huyo mama
‘Kuipata
namba ya mtu ni rahisi sana,msituone sisi tupo kijijini mkatudharau... sisi ni wajanja kuliko
hao wenye mitandao wenyewe, tunachoshindwa tu, ni kuiba pesa benki….’akasema
akicheka
‘Ni sawa kama mnaweza kuingia majumbani mwa watu usiku, sizani kama mtashindwa, au sio...sasa hebu tuambie maana hili linaweza kuleta maulizo mengi, ya kutokuaminiana, je uliipataje hiyo namba ya huyu mama..?’ akaulizwa
‘Hiyo
ni siri yangu…siwezi kuwaambia...’akasema akikunja uso kuwa kadhamiria kweli hawezi kujibu hilo swali.
‘Sawa
ni siri yako, kama ilivyo siri, ya jinsi gani uligundua kuwa majumbani kwetu kuna hayo..manini vile...lakini sasa ikibidi utatakiwa kutuambia ukweli maana sio vyema kupata namba
ya mtu bila kibali chake, au kufika majumbani kwa mtu bila kibali, tena usiku…’akaambiwa.
‘Ikibidi,
kwanini unasema ikibidi,…unajua niwaambie kitu, sawa nimekuelewa, kama ikibidi
mimi nitajua jinsi gani ya kujietetea, maana hiyo kauli yako ya ikibidi, ina walakini, mniamini mimi, mimi
lengo langu ni kuwasaidia, sio kuwatapeli, unasema nini, usiku, sijakuelewa hapo….’akasema
‘Tutafiikia huko, kwanza ningelipenda utujibu hili,..wewe ulisemaje wakati ulipompigia simu huyu mwenzangu hapa, .?’ akaulizwa, kwanza
akamuangalia mdada, halafu madamu wake, halafu akatabasamu , lakini tabasamu la
kujiuliza, kabla hajajibu, akatabasamu kidharau, na kusema;
‘Ndio
nilimpigia mimi sikatai,...na lengo langu lilikuwa jema kabisa, mikamwambia kama nilivyoongea awali, kuwa majumbani kwenu kuna
matatizo, yanahitajika kutolewa….’akasema.
'Ulijuaje kuwa kuna matatizo...?' akaulizwa
'Aaah, kwani ukifika kwa mganga, inakuwaje, labda nyie hamjawahi kufika kwa waganga, yeye anaweza kukuambia mambo yote ya nyumbani kwako bila hata ya yeye kufika, ..ni utaalamu wetu ...'akasema
'Na hayo mazindiko yaliwekwaje na nani..?'akaulizwa
'Na wachawi....watu wasio na nia njema na nyie, kwasababu zao ..mimi siwezi kujua ni sababu gani, mpaka niongee na watu wangu...'akasema
'Na wachawi sio....?' akaulizwa
'Ndio ...'akasema
'Sawa sasa hebu tuambie wewe mwenzangu wakati anaongea na simu alikuambiaje, awali kabisa, maana yote hayo tuna ushahidi nayo,..?' akaulizwa
'Si nimeshakuambia...'akasema
'Hakukuambia wewe ni mchawi, ukamjibuje...?' akaulizwa
Ilikuwa kama kazabwa kibao usoni, kwanza akatulia, akageuka kumuangalia huyo mama
aliyeongea naye kwenye simu, na huyu mama akawa kashikilia simu kama kuonyesha ushahidi,...Jamaa akainama chini, na kabla hajasema neno, mimi nikasogea mbele
na kusimama pale aliposimama mdada kwahiyo wote wawili tukawa tunamungalia yeye moja kwa moja usoni
WAZO LA LEO: Uongo wakati mwingine unasuta, kwani
walisema dalili za mnafiki mojawapo ni kuzoea kusema uwongo, hebu tujiulize
mara ngapi tunaongopa, mpaka inafikia sehemu hatuogopi tena, hata kuapa
tunaapa, ‘haki ya mungu, ..’ halafu tukitwa wanafiki tunakasirika. Jamani
tuchungeni sana ndimi zetu, hasa katika jambo hili la kusema maneno yasiyo ya
kweli ili tu kupata umaarufu, au kufanikisha malengo yetu,KUMBUKA unatudanganya
sisi, lakini yupo yule ambaye hadanganyiki, ipo siku utarejea kwake,..Tumuombe
mola wetu atusamehe kwa makosa haya na mengine, na atujalie tuwe wasema ukweli
ili tuweze kuzipata radhi zake.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment