Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Tuesday, July 18, 2017

DUWA LA KUKU....14


Nilifika nyumbani kwa huyu mzee, ikiwa ni  makao mapya, niliyoambiwa yatakuwa ni y amuda, na humo nikakutana na familia nyingine, ikiwa ya watu wengi kwani mzee huyu alikuwa na watoto wengi tu, na wengi wao alikuwa akiishi nao, hawajaolewa…

 Ukaribisho wangu hapo ulikuwa wa maswali mengi, na yalianzia kwa mke wa huyo mzee, kumbe mama mwenye nyumba wa hapo, hakuwa na taarifa na ujioa wangu, na hata kama alikuw anao, huenda hakukubaliana nao,..na kauli yake ya kwanza naikumbuka sana ilikuwa hivi;

'Naona umeniletea mke mwenza, maana nyie waume hamzeeki…’akasema mke wake akiwa kashika kiuno. Alikuwa mwanamke aliyejaliwa mwili, kwa unene, na huyu akikushika hupurukuti..tofauti na mume wake.

 'Mke wangu, ukisikia kisa na maisha ya huyu binti utamuonea huruma, hapa alipo ni yatima, na mbaya zaidi, tokea anakuwa mkubwa maisha yao yeye na mama yake ni ya umasikini, ya kuomba-omba,  mabarabarani, haya hilo lisitoshe, yule aliyemtegemea,kama mama yake alifariki dunia, kwa kuchomwa moto na wezi..inasikititsiha kwa kweli…’akasema

 'Mhh, na ukaona hapa ndio kituo cha kulelea mayatima au sio, sikatai, hilo ni heri, kama ningelijua mapema, na nikuulize tu,  na huko alipokuwa awali ilikuwaje, si ulisema yupo kwa yule bint yako unayemdekeza, kila anachosema unamkubalia tu…na hata hili nalo umemkubalia, hata bila ya kuomba ushauri wangu…’akasema

'Mke wangu, huko kumetokea mtihani, ndio maana nimeamua kumleta hapa, na ni kwa muda tu, sikujua kuwa leo ninaweza kuja naye hapa….’akajitetea mume mtu.

'Na iwe kwa muda,kweli, maana kama huko wamemshindwa, kwa jinsi nimjuavyo yule bint, basi kuna tatizo, huyu binti anaweza kuwa na …haya ngoja nisiseme mengi nikaja kuonekana nina gubu…’akasema mke wake.

 'Kwa huyu kiukweli hana tatizo, ila yaliyotokea huko ni mambo juu y auwezo wao, hayana haja kuyaselezea zaidi, tupo mbioni kulitatua hilo, najua litaisha na likiisha huyu binti atarejea huko, au tutamtafutia njia mbadala za kumuzesha, ili awe na maisha yake ya kujitegemea..’akasema

‘Hahaha unanichekesha kweli, wewe una watoto hapa, hawana kazi, umeshindwa kuwatafutia njia mabadla za kujiwezesha, leo hii uje kumtafutia huyu..mimi sijui, lakini ipo siri ndani yake, na itakuja kujulikana tu, nawafahamu sana nyie wanaume…’akasema mama huyo.

‘Mke wangu niamini…mkaribishe mgeni, hayo mengine tutaongea wenyewe..hiyo sio tabia nzuri ya kukaribsiha wageni…’akasema mzee huyo.

'Mhh,..haya karibu mgeni samahani kwa lugha yangu, inabidi unizoee, kuwa mimi sina mzaha kwenye wajibu wangu, ukikosea, nitakupasha, na ikibidi nakutimua…na mume wangu, jingine ulisikie kabisa, mimi sitaki kufanyiwa majaribio, maisha yenyewe haya ya kuunga unga, kama umesema ni wa muda, na iwe hivyo,..sio kniletea mizigo humu ndani,mimi nimempokea mgeni kwa vile wewe ni kichwa cha familia, vinginevyo, …haya karibu mgeni…’akasema na kunipokea mzigo wangu.

 Basi nikakaribishwa kama ada, na kuanza kutambulishwa kwa wenyeji wangu, humo kulikuwepo na wasichana wa rika langu, niliwaona wengine wakiniangalia kwa macho ya kininyali, mpaka nikahisi vibaya, lakini niliona ni jambo la kawaida tu , kwani maisha yangu yamekuwa hivyo toka utotoni, kudharauliwa kukashifiwa, kunyanyapaliwa,…nikavumilia tu.

Ila mimi nilijua hali kama hizo ni kwa watu wasiokuwa na uwezo, kumbe hata hawa watu wana tabia hizo,,…nilivumilia tu.., japokuwa kulikuwa na visa vya hapa na pale, vya mauzi, hata wakati mwingine nasingiziw vitu ambavyo sijavifanya mimi, niliendelea kuvumilia tu, nilijua mvumilivu hula mbivu, mpaka wakaanza kuchoka wenyewe, na baadae ikageuka kusifiwa tu.
Nilishangaa tangu nifike hapo ile hali ya kuota ndoto mbaya za kukabwa, au majinamizi sikuwahi kuipata tena nikahisi huenda ni ile duwa na maombi tuliyoyafanya siku ile kabla sijaondoka pale nyumbani, na hata yule binti wa awali aliyetuambia mambo hayo, sikuwahi kuwasiliana naye tena, hali yangu ilirejea kama kawaida, nikawa nalala kwa amani, hilo lilinipa faraja sana…ila mara chache nilikuwa nikimuota mama yangu akinisihi nizidi kuwa na uvumlivu kwani mambo bado magumu, …
‘Mambo gani magumu mama, naona sasa nina amani licha ya hali ya hapa nyumbani, najitahidi kufany akama ulivyonielekeza…’nikamwambia kwenye ndoto.

‘Najua hilo, lakini mitihan yako ni mingi, uvumilivu wako ndio utakupandisha daraja, …usije kuhadaika maana mengi yanayokutokea sio dhamira yako,…ina maana yake…’akaniambia na nilipotaka kumuuliza swali jingine mara nikazindukana ikawa asubuhi, na asubuhi kwangu ni mchaka mchaka wa kazi, nasahau kila kitu kazi ni nyingi, lakini sikupenda kuziacha,…

‘Huyu mgeni ni mchapakazi kweli, hana muda wa kuongea au kubisna na mtu, ukimuambia kitu anakubali tu, na wakati mwingine anasingiziwa ubaya, yeye anakubali tu hata kama sio yeye aliyefanya, na kuomba msamaha…...mmh, kweli kajaliwa ..’wengine wakaanza kusema hivyo

‘Hata hivyo muwe makini naye…’mama yao akawaasa hivyo.
**************m
Siku moja nikiwa sokoni na wenyeji wangu mara nikahisi mtu ananishika bega, kugeuka namuona ni yule binti wa kule nilipotoka, akaniambia kwa ishara ni mfuate, nilishapigwa marufuku nisiwe na huyo binti, hata wakati natoka kule, lakini kwa hapo, nikaona nimfuate nisikie anataka kusema nini…
‘Unasemaje maana siruhusiwi kuongea na mtu…’nikasema
‘Hata mimi, najua tu…wameshachukia sana, lakini ukweli niwapasha,…sasa sikiliza unajua yule mjinga yupo hapa Dar…’akasema
‘Mjinga gani..?’ nikamuuliza
‘Si yule mchawi…..’akasema
‘Huyo aliyetaka kukuoa, au…?’ nikauliza
‘Ndio huyo huyo, kaja anaumwa kweli, sasa najiuliza vipi mchawi naye akaumwa…’akasema

‘Anaumwa nini…?’ nikauliza.

‘Mguu umevimba, utafikiri ana matege…’akasema.

‘Oh, maradhi hayo, ndio umeniitia hicho,…?’ nikamuuliza.

‘Hivi hilo waliona dogo  hata kama anaumwa, hashindwi kupaa usiku na kukujia, ila kuna kitu nataka kukuambia,..’akasema.

‘Kitu gani..?’ nikamuuliza.

‘Nilikwenda sehemu,..nikaambiwa wewe upo kwenye hatari kubwa sana,  unajua na nilipokutana naye kasema  wewe ipo siku utamtafuta, upende usipende….’akasema.

‘Hatari gani,..?’ nikauliza.

‘Na huyo mtaalamu kasema ukisubiria mpaka uanze kuumwa, ndio basi tena, utakwenda na maji…fanya juu chini uje tuonane kabla mambo hayajaharibika,...’akasema.

‘Ni hatari gani hiyo…?’ nikauliza na mara nikasikia nikiitwa, na yule mwenzangu akainama chini na kupotea kwenye makundi ya watu waliopo humo sokoni,hakutaka hao jamaa zangu wamuone, na mimi nikaguka na kuwafuta wenzangu.

‘Ulikuwa unaongea na nani..?’ nikaulizwa.

‘Yule ni msichana mmoja nilisoma naye…’nikadanganya hivyo kitu ambacho sikipendi, nilijisikia vibaya sana kudanganya hivyo nikawa natubu kimoyo moyo.

‘Achana nao, hao watakupoteza, na ukipotea utafute pa kwenda na nakuasa siku nikisikia umeharibikiwa, wala usisubirie kauli yangu, fungasha ondoka..maana nitakuumbua mpaka mitaa yote watafahamu…’akasema mama mwenyeji wangu.


*************

 Siku zikaenda mwezi sasa unapita…, sikusikia lolote kutoka kwa huyo aliyekuwa mfadhili wangu wa awali, mama mwenye nyumba awali alikuwa kilalamika lakini siku zilivyokwenda akawa ananizoea maana niligeuka kuwa mfanyakazi wa ndani, kila kazi naifanya mimi, tena bila kulalamika au kulipwa chochote.

Nilianza kutokujisia vyema, japokuwa nilijitahidi kuficha hiyo hali,..ilikuwa kama kitu kigeni kuingia mwilini mwangu, sikuzoea kuumwa umwa, na nikiwa nyumbani na mama mara nyingi nikijisia kuumwa mama alikuwa akinipatia miti shamba, natafuna, hali inapotea, lakini hii hali ilikuwa ngeni kwangu, sijawahi kujisikia hivyo kabla,.. siku zilivyozidi kwenda hali ikazidi kuwa mbaya, nikaanza kuzidiwa, najisikia vibaya, siwi na hamu ya kula, kizunguzungu…mpaka siku moja nikadondoka na kupoteza fahamu..

Nilipozindukana, wakawa wanajiuliza

‘Au ni hiyo hali aliyokuwa nayo ya kuota majinamizi..?’ wakaulizana

‘Tumpeleke tena hospitalini..?’ wakaulizana

‘Hapo kuna mawili, …nina wasi wasi na huyu mtu, hivi hamuoni anavyonawiri,..kunenepa gani huko, …’sauti ikasema
‘Wasi wasi wako mama, ….mimi naona …’akasita aliponiona najitingisha, kuashiria nimezindukana, na wakanisaidia nikaa vyema, wakaniuliza najisikiaje, niwajibu sasa nina nafuu, ni kichwa tu kinauma, wakanipatia dawa za mauimvu ya kichwa. Baadae hali ikawa nzuri tu.

Baadae baba mwenye nyumba akafika wakamuelezea hali iliyonitokea na yeye akauliza kwanini sikupelekwa hospitalini…

‘Kwasababu alipozindukana, akasema hajambo, na mpaka sasa anaendelea vyema, haina haja ya kumpeleka hospitali tena, kwani bado yupo kwenye dozi, dawa za awali bado hajazimaliza…’wakasema

‘Sawa hebu muangalieni, kama hali hiyo ikitokea tena, basi ni muhimu tumuwahishe hospitalini…’akasema baba mwenye nyumba.
**************
Siku zilivyozidi kwenda nikawa sasa ni mgonjwa kweli…
.
 Kuumwa kukawa tatizo sasa, hata nilivyojaribu kujificha nisionyeshe hiyo hali, lakini ilifikia mahali sasa nashindwa, nikifanya kazi kidogo kizunguzungu,  najisikia vibaya-vibaya tu, kula inakuwa ni shida, kutapika kukaanza, nikawa sasa mtu wa kitandani hapo nikaanza kuonekana ni  mzigo.

'Mama huyu mgeni nahisi sasa ni mzigo kwetu, kwanini haponi, mlimpima magonjwa yote..?’ akauliza binti mmoja akiongea na mama yake, na waliongea baadae baba mwenye nyumba alipokuja mama akalifikisha kwake, na mazungumzo yakawa hivi…

‘Huyu binti kuumwa kwake kumezidi….’akasema mama mwenye nyumba.

 'Anaumwa kama binadamu wengine au sio, binadamu  yoyote kuumwa ni kawaida au…’akanitetea baba mwenye nyumba.

 'Hapana hii hali sio ya kawaida, mimi ni mwanamke na mtu mnzima, huyu bint tunatakiwa tumuhoji vyema kuna jambo …’akasema huyo mama mtu mnzima.

'Kwani unahisi ana nini, nakumbuka ulishaanza kumsifia kuwa ni mfanyakazi mnzuri wa hapa nyumbani ana Tabia nzuri tofauti na ulivyofikiria awali, sasa imekuwaje, au watu kama hawa hawatakiwi kuumwa, mke wangu tuwe makini na wanadamu wenzetu…’akasema baba mwenye nyumba hiyo.

'Sio swala la kuumwa tu, na siwezi kusema hisi zangu kwa sasa, hebu jaribu kuongea naye, umuulize ana tatizo gani, labda mimi nikimuuliza zaidi atasema ninamuonea,…jana nimejaribu kumdadisi, lakini majibu aliyonipatia, nahisi hajielewi,..huu ni mzigo na mtihani, na mimi msimamo wangu upo pale pale…’akasema mama huyo

‘Kwani una mashaka gani na huyo binti mke wangu, tumempa dawa,..si alipima akaonekana ana malaria wengi tu, ana UTI, ana…typhoid, magonjwa yote hayo yameonekana mwilini mwake,…sasa ngojeni amalize dozi tuone matokeo yake kwanza, tukikimbilia hospitalini atazidi kupewa madawa mengine…’akasema baba mwenye nyumba.

'Hata akimaliza dozi, tatizo hilo halitakwisha, ndio maana awali  nilikuuliza huko alipotoka, aliondokaje huko au kuna kitu unanificha mume wangu..?’ akauliza mama mwenye nyumba.

 'Kwani kuna nini unahisi kwanini huaniambii, mimi nitakuficha nini, huko alipotoka tatizo ni kuwa likuwa ikifika usiku anaota ndoto mbaya,  za majinamizi, watu usiku hawalali, ndio wakaona tumlete hapa tuone kama hiyo hali itarudia au tatizo ni nini, na baadae mambo yakikaa sawa tutamrejesha huko…’akasema.

 'Una uhakika na unachoniambia au ni mbinu za kufiachia uovu wenu, kuna nini kilitokea huko alipotokea, mkwe wako alifanya nini,..niambie ukweli mume wangu , maana ukinilazimisha nikagundua ukweli kwa njia nyingine kiukweli hatutaelewana humu ndani, mimi sitkauwa na subira tena, ataondoka humu ndani, hata kama ni usiku…’akasema huyo mama kwa ukali.

‘Mke wangu kwani kuna nini, kwanini wewe huaniambii, una hisia gani kwa huyo binti, kwani ukiniambia mimi kutakuwa na tatizo gani…kwani ulipompeleka hospitalini walimpima ni na nini..?’ akaulizwa.

‘Niliwaambia wampime magonjwa  ya kawaida tu, kama malaria na hayo mengine, kwasababu nilimuhoji kwanza, nijua kama anaweza kuambukizwa magonjwa mengine  aliniambia hana uhusiani na wanaume, mimi nilimuamini kwa vile ulivyosema, kuwa ni mkweli na muaminifu,…kwahiyo mimi sikuwa na mawazo ya tatizo jingine lolote…’akasema
‘Kwahiyo kwa vile katumia dawa haponi, unahisi kaambukizwa magonjwa mabaya,kwa muda mfupi namna hiyo unaanza kumuhisi hivyo, kwani sisi hatujawahi kuumwa zaidi ya mwezi, na baadae tukapona, mke wangu acha hisia mbaya hizo..?’ akauliza baba mwenye nyumba.

‘Kwa hali aliyo nayo naweza kuhisi hivyo na vinginevyo…, mimi sijui lakini, muhimu ni vipimo vitasema, na nakuona una kwepesha kwepesha ukweli, haya kesho tumpeleke hospitali, ukweli utagundulikana huko…’akasema huyo mama mwenye nyumba.

‘Basi wewe umpeleke tu, utaniambia majibu yamekuwaje,..na hata hao madakitari watakushangaa, ndio katoka kupimwa, akaonekana ana malaria, sasa wamrejesha tena,…sawa kwa vile unataka kumjua afya yake zaidi sio mbaya, kwanza kipimo hicho siku hizi ni bura tu…’akasema mume mtu.

‘Mume wangu, na umri huo hujanielewa nina maani gani…, basi kesho inabidi tuongozane, maana naona hutaniamini, hata nikija kukuambia, hahaha, wanaume bwana mnaogopa kuumbuka eeh, hapo hapoo mtakuja kujieleza, ni nani, …’akasema mke mtu…

‘Kwanini tuongozane mimi na wewe, ..kwani mkienda wewe na yeye kuna ubaya gani..au hata kaam unaona anaweza kuzidiwa unaweza kuondoka nab into yako mmoja au unasemaje?’ akauliza.

‘Nataka uwepo wewe mwenyewe, umuwakilisho huyo anayehusika, au kama ni wewe, au mkwe wako, au yoyote, uweze kumuelezea vyema atakavyosema docta, maana mimi sitaweza kuwa naye tena..kama ni hivyo na nin auhakika ni hivyo, sisi tukitoka huko anakuja kufungasha virago vyake kwaheri ya kuonana…’akasema mama mwenye nyumba.

‘Mke wangu mbona sikuelewi…’akasema.

‘Utanielewa tu hiyo kesho…, mimi sitaki mzigo hapa nyumbani, .., unaona hawa mabinti, nilishawapa somo, na wakiona tumelikubali hilo kwa huyi binti, wataona kumbe eeh, ni kawaida tu…, wataambukizwa, na matokea yake tutakuwa na mizigo mingi humu nyumbani,..tuna bahati yamabinti sasa isiwe kugeuka badala ya neema ikawa ni …aah,.. hilo mimi silitaki, nilishawaambia atakaye fanya uchafu wake huko nje.., asije kuniletea matatizo humu ndani, unakumbuka kila siku tunawaasa mabint zetu,  …sasa wewe unataka kulianzisha, hivi utaweza kuibeba hiyo mizigo…’akasema.

‘Mizigo gani mke wangu… atapona tu huyu, hizo ni hisia zako tu, huyu binti kwa maelezo yake hana hata tabia chafu kama hizo..labda awe kaambukizwa na sindano…vinginevyo, sijui…maana huwezi kumsemea mwanadamu mwingine,..ila mimi nina uhakika ni maradhi tu ya kawaida, atapona...sizani kama wamemuambukiza hao…’akasema.

‘Hao akina nani..?’ akauliza mke mtu.

‘Maana mle ndani alikuwa hata kutembea hana tabia hiyo, alisema hana hata rafiki mmoja wa kiume, sasa ataambukizwa magonjwa hayo na akina nani…au unataka kusema nini, kuwa ndugu zetu hao wana maradhi ya kumuambukiza huyu binti, hapana wale ni watu safi kabisa…’akasema.

‘Unafikiria hayo tu eeh, maana unataka kumtetea mkwe wako au sio..au yule kijana wao, maana yule kijana wao naye, siku hizi kabadilika sana, suruwali zinavuka tu..hajisumbui kuzipandisha, anatuonyesha chupi yake, hizi tabia nyingine za kuiga, hazina hata maana, wenzao wanafanya biashara za kutangaza chupi, na mauchafu yao yaliharamishwa, wao wanaona ni fasheni…, ile ni tabia mbobu kabisa, ..mimi humu ndani sitaki mchezo huo, wakiniletea wanaume kama hao nitafukuza…’akasema na mara nikatokea, wakanyamaza.

‘Mhh..lakini mbona ana mwili wake tu, hajakonda..’baba mwenye nyuma akasema nilipopita.

‘Kesho utalijua hilo vyema, mimi sikosei,…hali hiyo ishajionyesha haina kificho tena… huyo binti kaukwaa, na …kama ni zezeta, hatajua wapi alipoubebea huo mzigo…’akasema mama mtu na baba mtu sasa akainama kama anawaza jambo.

‘Usiwaze sana,…kama na wewe ulipitia kidogo, usubirie haki yako… maana baada ya vipimo, siwezi kukufanya uwe unawaza hivyo zaidi, nataka mume wangu uwe na raha, tuwe na maisha yetu na watoto wetu, huo ndio mzigo wetu halali, ..sio kubebeshwa mizigo mingine  ambayo haipo kwenye bajeti yetu, unasikia sasa kama ni mzigo wako, utajua mahali pa kuupeleka…’akasema.

‘Sawa kesho tutakwenda huko hospitalini kupima, maana kwa hivi hatutaelewana…, lakini nilikuwa na mipangilio yangu mingine, unajua kesho ndio i siku ya kwenda kuonana na huyo mkwe na binti yetu kule alipotoka huyu binti…nataka , nijua kama wamefikia wapi, kwasababu wamekuwa kimia, ..sijui wana mipangilio gani, lakini sio tatizo..tutakwenda na nikitoka huko nitapitia huko mara moja.,…’akasema.

‘Utapitia au utakwenda naye…?’ akasema kama anauliza.

‘Hapana itakuwa sio vizuri, kwa vile anaumwa, hapan, huyu mpaka apone, na kama wameshamtafutia sehemu, bado atakaa hapa mpaka apone, ndio ubinadamu…’akasema mume mtu.

‘Sasa hapo utaamua moja, mimi niondoke au huyo hawara wenu aondoke…hilo sina mjadala nalo, kwetu bado kupo, unasikia, kama ulinileta mke mwenza, umtafutie sehemu yake mpaka hapo kitakapojulikana, unasikia, mzee wewe, utaumbuka kweli,..haya wewe jifanye msiri…’akasema mke mtu na mara simu yam zee ikalia, na alipoangalia akasema.

‘Haya, hao wananipigia simu, nahisi wameshapata sehemu au wameamua kumchukua tena akakae nao, subiri niongee nao…’akasema akiweka simu hewani.

‘Hahaha ..mnajidanganya wenyewe

WAZO LA LEO: Katika maisha jitahidi sana kupende wengine, chuki iwe mwiko kwako,  usisubiri wewe kupendwa, kwani yupo anayekupenda kwa vyovyote uwavyo, yeye kakubariki neema zote ulizo nao.

 Jitahidi kusaidia wengine kwa kadri uwezavyo, hata kama una kidogo tu..na usitegemee wewe kuisaidiwa na wengine, kwani ukisaidia wewe hata kidogo,… mola wako atakuzishia barak..na utazidi kupata na kuzidi kusaidia zaidi. Kwani usiposaidia, itafika muda utakuwa hunacho kabisa, na hapo utakosa wa kukusaidia kabisa.

 Jitahidi kusamehe hata kama wewe ndiye uliyefanyiwa ubaya, kwani kusamehe, kunavuta heri nyingi, kamwe wewe usisubiri kusamehewa kwa wale wliokukosea, ..ukumbuke ukisamehe, yupo yule ambaye atakusamehe, siku ambayo msamaha ni kwake tu.


 Tumuombe mola atupe iman thabit ya kumcha mola wa kweli, na kuwa mbali na unafiki, kwani unafiki ni mbaya zaidi ya ubaya.

Ni mimi: emu-three

No comments :