Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Monday, July 17, 2017

DUWA LA KUKU---13


‘Niambie mke wangu nipo tayari, kukubalia lolote lile, najua nimekukosea sana mke wangu..., na sitaki niendelee kukukosea, nataka nikuonyesha kuwa mimi ninakupenda sana mke wangu...’akasema baba mwenye nyumba akitamani hata kupiga magoti.

Na mke wake ndio akaanza kuongea....


Tuendelee na kisa chetu...


'Wazee wangu, ni kweli mume wangu ana huruma sana, nilimpenda tokea awali kwa tabia hiyo ya huruma na upole, kwasababu hata mimi sipo mbali na yeye, na tabia hiyo ya huruma niliyokuwa nayo mimi  ndiyo iliyonifanya niwe mbali na wazazi wangu !


Kwanini nasema hivyo, …kwasababu sijui ni kwanini, wao kwa mtizamo wao, na siwezi kuwalaumu, ndio kawaida ya kibinadamu, wao wanaamini madaraja ya maisha yapo kuwa kuna watu wa hali ya juu na wa hali ya chini…na kwamba wao kwa vile wapo juu, kwa jinsi wanavyojiona wao hivyo, marafiki wao wa kweli ni wale walio sawa na wao, na wale watakao-oa kwao wawe ni watu wanaojiweza kama wao walivyo…


Kiukweli, sijui ni kwanini tupo hivyo,… kwangu mimi hilo sikulipenda, hasa nikikutana na watu ambao hwakujaliwa kuwa na uwezo, najua wengi sio kwa dhamira yao,…kiukweli mimi nikikutana na masikini, mayatima watoto wa mitaani, naingiwa na moyo wa huruma, najiuliza ni kwanini wao wanateseka hivyo, wakati kuna watu wana mali, wana uwezo uliopitiliza, …sijisifu ila kwetu kwa wazazi wangu tuna kila kitu, tunakula na kusaza, wakati huo huo kuna watu wanateseka…’akasema kwa uchungu.


Hapana mimi sikulifurahia hilo, kwanini tumwage chakula, kwanini tubadilishe magari kama nguo, kwanini, tunaishi maisha ya raha sana, wakati dunia hii ni ya kupita tu, sikupenda hiyo hali, mimi nikawa kila siku naleta watoto wa mitaani, hapo nyumbani kwetu..nawapa chakula nguo..nawasaidia,…, na hilo liliwakera sana wazazi wangu…sio kwamba nawateta wazazi wangu, lakini wengi wenye uwezo wapo hivyo. Isjui kama nakosea!


Mimi nilipokutana na mume wangu, tukawa marafiki, akanielezea maisha yake, nilijawa na huruma na mapenzi yakaanzia hapo, …nilijua huyu ndiye wangu wa kufa na kuzikana, nilitamani kuwa na mume wa namna hiyo, mwenye huruma na upendo, ambaye anawapedna wale wasiojaliwa kupata upendo kwasababu ambazo zipo nje ya uwezo wao, kama mayatima na watoto wa mitaani, tulikuwa mimi na yeye tunalijadili hili mara kwa mara….

Sasa haya yanatokea usoni mwangu,…yamenipa fundisho fulani, kuwa sio vyote ving’aavyo ni dhahabu, sio kwamba wengine wote wanaoteseka wana miyo mizuri, wengine ni kwasababu tu hawajaipata hiyo nafasi,… mtu akipata hubadilika, huwezi kuamini kua ndio yule wa zamani…mimi sitaki maisha hayo….’akasema


‘Lakini mke wangu mimi sijabadilika,…mbona wanasingizia mambo ambayo sio ya kweli….’akajitetea mume wake,lakini yeye hakumsikiliza, akaendelea kuongea kwa kusema;


'Ndio maana,  sasa hivi nataka nipate muda wa kuyatafakari haya yote, nahitajia muda wa kujipima wapi nilikosea, lakini pia, sitaki kumkwaza mtu, sitaki kumuumiza mtu, sitaki mtu anione kuwa nafanya haya kwa vile, hapana, maana sitaki nifanye mambo yenye kumkasirisha mola wangu.


'Ninajua maagizo ya mola wetu ni kusaidiana, kutendeana wema, kujenga udugu wa kiukweli nk..lakini mitihan ikizidi sana mtu hukengeuka, hujikuta akiingia kwenye dhambi bila kupenda, lakini pia sio vyema kujilegeza na kusema nimeshindwa,..hapana mimi bado sijajishindwa, naji….ninajibidisha ndio maana nikafikia maamuzi hayo ambayo nitayateleza ili name nipate muda wa kujijongeza kwenye uhalisia.


Baada ya kuyasema haya, nataka niwaambie nini maamuzi yangu, mume wangu hata kama una matatizo ya kiafya,…labda kama ipo hivyo, siwezi kukubali tu, maana mimi sina kipaji hicho… au hata kama ulilogezewa kama alivyodai huyo mdada maana wengi tunapenda kukimbilia huko, hata kama sio …hata kama kuna njia mbadala, na njia sahihi nyingine, …mimi naamini kuwa mola wetu anatujua sana sisi tulivyo…, ndio maana akatuelekeza njia hiyo, lakini ….hapa nilipofika nasita, na inabidi tufanye hivyo….



Mume wngu, nimeipima nafsi yako, japokuwa sina uwezi huo, ila kwa kile kidogo nilichojaliwa nacho nimekiona kuhusu wewe ulivyo, japokuwa utapinga,… nafsi yako haijatulia, ina muwashawasha wa tamaa za kimwili, kama walivyo wanaume wengi, nyie mnakuwa wa kwanza kutuchoka sisi wanawake, hasa tukianza kuchujuka, ukubali usikubali ndio hivyo…’akasema pale alipoona mume wake anataka kusema neno.


‘Ni kweli nyie wanaume hamzeeki, sisi wanawake tunazeeka mapema, ule urembo wetu unatoweka, lakini kwani hayo ni mapenzi yetu, kwanini mungu alifanya hivyo…najiuliza sana tu, na sio kwamba namlaumu mola wetu,lakini majibu yapo, ndio maana nitachukua maamuzi hayo, na mtu asije kuniona mimi ni mtu wa ajabu sana, hapana na mimi ni mwanadamu..



Nataka unielewe hapo mume wangu…, hata kama utapinga na kujitetea vipi, hili nitakalo kushauri ulifanyie kazi, nilishalifanyia kazi mimi akilini mwangu kwa uoni wangu, na nipo tayari kulibeba hili , japokuwa moyoni nitaumia, sikupendelea iwe hivyo,… lakini mimi nayafanya haya kwa vile nakupenda sana mum ewangu…’akatulia kidogo.


Mimi nayafanya haya kwa vile ninataka wewe uzidi kuwa na furaha, lakini pia furaha yako isiwaumize wengine… sasa ni juu yako kulifanya au kuliacha, nimefikia mamuzi hayo baada ya kupiti utafiti mmoja ya wa njozi, mtu huyo kwa fikira zake na utafiti wake, yeye alisema, ndoto nyingi tunazoota usiku, ni zile hisia zetu za matamanio yetu ya kila siku, kila mtu anatamani kuwa hivi kupata kile hata kama uwezo huo hana,….


Mimi sio …mshirikina, na sipendi imani hizo, ila….kuna mengine unayaona kuwa ni kweli hata bila kupitia huko,
Mtu anataka awe tajiri, au amuoe bint wa sultan ili hali yeye ni masikini, ataota nini hapo , ni lazima usiku ataota ndoto zake, kuwa kafanya hivi na vile akafanikiwa, hata kama haitawezekana kuwa hivyo..maana mipangilio ya mweneyzimungu ina hekima zake, japokuwa sisi hatulioni hilo.


Sasa kuna kitu nilikiwazia sana,  ndoto kama alizosema kiongozi wetu wa dini , kuwa zipo …ndoto za matendo, ya kuwa uliwazalo mchana utakuja kuliota kwa matendo usiku, hata kama mchana ulishindwa kulifanya, basi usiku unaweza kulifanikisha kwa njia ya njozi, na unatenda kwa matendo, hii ni hatari eti…kwa mfano , nachukulia tu kama mfano,…je ukimchukia mtu hadi kutamani afe, usiku utafanyaje,..najiuliza tu  ni nini hatima yake, lakini mungu ni waajabu sana huwalinda waja wake, na haijatokea watu kama hao wakafanya mabaya kiasi hicho cha kuua,… ila wanaweza kufanya madhambi kama hayo aliyoyafanya mume wangu, hahaha hapo unajiwekea alama ya kuuliza…’akasema


Naombeni mnivumilie kwa maneno mengi, lakini nina maana yangu hapo, ili kwa maamuzi yangu msije kuniona nimegeuka kuwa jiwe….


Mume mtu kusikia hivyo, akanyosha mkono kutaka kupata ruhusu ya kuongea, na mkewe akamuangalia bila kusema neno, na yeye akasema;


‘Mke wangu, usfikie kunuhukumu kihivyo,…yawezekana nilifanya ndio, maana ushahidi si unao,…, yawezekana nina matatizo hayo,mimi sijui....lakini ukizidi kuninyanyapaa, ujue nasikia vibaya sana, najiuliza hta mimi, kwanini iwe hivyo, kwanini…hizi kwanini zinaumiza mke wangu…kama tulishakubaliana yaishe, basi, yamekwisha, tuyasahau, na mimi nitajitahidi kujirekebisha…’akasema.


‘Sikunynyapai, lakini ukweli lazima usemwe, na ukisemwa kama hivi utakuwekea kumbukumbu ya kujihami kila ukikusudia kufanya mabaya, ukikumbuka kikao kama hiki, maneno kama hayo, utaogopa,..ndio maana tumeusiwa kukatazana mabaya na kuamrishana mema, nia ni nini, sio kuhukumu mtu hapo, sio kujikweza, nia ni kujengeana kumbukumbu za kujihami…unielewe hapo, mimi nimesomea ualimu na najua ni vipi niwafundishe watu…’akasema mkewe.


‘Ok, sawa, sasa unaonaje ukalisema hilo ulilokusudia kulisema kwasababu kwa jinsi unavyorefusha maneno unanipa shikizo la moyo, nashindwa kujua nini dhamira yako unaanza kuniogopesha hata mimi….’akasema


‘Ni kweli, hata mimi nilipata sana shida kulifikiria hilo…na ni maamuzi magumu kama hayo kwangu mimi, kwa mtu kama mimi, lakini sina jinsi, na…binti ataelewe tu, na ipo siku atakuja kunielewa kwa hili, sasa hivi…itakuwa vigumu na huenda akaniona mtu wa ajabu sana.


‘Baada ya kuyawaza hayo yote, nimefikia maamuzi haya, kuwa hivi sasa, nataka wewe mume wangu, umtafutia huyu binti, sehemu ya kuishi, umtafutie chumba chake, kwa namna utakavyoweza wewe, umuwekezee mradi kwa namna utakavyoweza wewe, na hata ukitaka mfunge ndoa, ili uweze kwenda kwake kwa nafasi, bila kujiiba, si ulimtamani, si ulimpenda, sasa nataka hilo usilifanye kwa kificho na mimi nipo radhi…’aliposema hivyo, mimi nilishtuka, nikatoa macho ya kuogopa.


‘Unasema nini mke wangu, unataka kufanya nini, kunifukuza humu ndani au.?’ Akauliza mume mtu akisimama.


‘Mume wangu mimi sijatamka hilo, na hata siku moja, japokua niliwahi kutamka kwa hasira, kuwa utaondoka humu ndani, lakini mimi sijafikia maamuzi ya kuwa tuachane kwa talaka, kutamka kuwa utaondoka humu ni namna ya kukujenga uelewe wajibu wako, ninachotaka kwa hivi sasa ni wewe usiwe mnafiki, uweze kuifurahisha nafsi na matamanio yako kwa uwazi,…sijui kama  bado sijaeleweka hapo, maana huyo unayemfanyia hivyo yeye ni mwanadamu, kwanini umzalilishe na wakati ipo njia halali, kwanini mfanye kwa siri wakati mnaweza kuifanya kwa dhahiri kwa halali…’akasema.


‘Mimi sijafikiria huko na siwezi kufanya hivyo…’akasema mume mtu.



‘Hili nimelipanga hivyo, kwasababu gani, huyu binti nilikabidhiwa mimi, na yupo mikononi mwangu, na mama yake keshafariki, ni masikini na ni mjane, …na haya yametokea ndani ya nyumba yangu, ndani ya mamlaka yangu, na mimi wakati mwingine ndiye wa kulaumiwa, huenda nimeshindwa kumshibisha mume wangu, huenda…sasa hizi huenda….hapana, na zaidi waliomtendea hayo  ni familia yangu, tunahitajika kuwajibika kwa hilo, lakini pia tunahitajika kuchukua tahadhari..ili yasije kutokea tena makubwa zaidi ya hilo, maana chuki zinakuja kutokea, na chuki, hahaha, zinaweza kuotwa usiku tukaja kuuana humu ndani….’akasema.


‘Kwahiyo, mume wangu kaa ufikirie hilo.., ila kwa huyu binti kuanzia leo, naomba baba, wewe ndio tegemea langu, wewe mara nyingi umekuwa ukinielewa, haya yakiendelea kufanyika, tukiendelea kumpa muda mume wangu kuyafanikisha hayo, kwa jinsi yeye atakavyoona ni sahihi, ninaomba huyu binti aje akae kwako..sikutupii mzigo, mimi bado nitaendelea kumsaidia kwa kadri niwezavyo,..ila hili saa ni jukumu la mume wangu, sio mimi nitamsaidia, ila nitahakikisha misaada hiyo inamfikia mlengwa…’akatulia.


‘Hapana mimi siwezi kulifanya hilo, kama humtaki mtoto wa watu umrudishe huko ulipomchukulia, mimi huyu sijamleta mimi, …’akasema baba mwenye nyumba.


‘Mume wangu uliahidi kuwa nitakachokisema utakitekeleza, ahadi ni deni, sasa kazi ni kwako….’mke mtu akasimama.


‘Mke wangu unataka kwenda wapi hili hatujakubaliana nalo, japokuwa nilikuahidi hivyo….’mume akaanza kulalamika.


‘Mimi nimemaliza, binti fungasha kile kilicho chako, mtaondoka na baba yangu hii leo....nilishaongea naye hili kabla japokuwa sikujua haya yatakuja kuwa hivi,…nimuomba kama kutatokea lolote kama hili, niliwazia hivyo tu, basi huyu binti sio wa kutelekezwa, anahitajia njia nyingine ya kumsaidia, na njia nyingine ndio hiyo..mume wangu usijivunge, huyu  binti umempenda…’akasema na watu humo ndani wakataka kucheka,


‘Hapana mke wangu huko umefika siko…hapana, …hayo ni mawazo yako…’akasema


‘Sisi tutaendelea kulijadi kama mke na mume, lakini maamuzi yangu ni hayo, leo hii huyu binti ataondoka na baba, na ni lazima wewe umtafutie njia ya kujikimu huyu bint, ndio ni mimi nimleta, lakini sikumleta hapa li mumuzalilishe, na adhabu ya kuzalilisha watoto wa watu ni nini…au hujui kuwa huyu naye ni mtoto wa watu…uwajibike kwa hilo..Baba nakuomba unisaidie, sikutupii mzigo, naomba unielewe hivyo, tutazidi kuliongea hili na kulifanyia kazi..’akasema akimuomba baba yake.


‘Aaah, mimi sina tatizo, kuna nafasi kubwa kule kwangu, atakaa ila naomba iwe ni kwa muda, kama ulivyosema, mume wako anahitajika kuwajibika, basi atawajibika, au sio mzee mwenzangu..?’ akasema huyo mzee akimuangalia mzee mwenzake.


‘Eeeeh, yeye atajifunza kwa kupitia njia hiyo, lakin hilo la kuoa, aah, sijui ni yeye mwenyewe, hapo kuna mtego, lakini kama hajatulia, tutamsaidia vipi,..ila la kuoa bado sijaliafiki, ila kumuhudumia huyo binti ni kazi yako mwanangu, na ushukuru kwa hilo, ni wapi utampata mke mwenye hekima kama huyu…ila usije kulichukulia hili jambo kijuu juu, ikawa ndio umepata nyumba ndogo,..huu ni mtihani kwako..kama ni kuoa uoe, sio nyumba ndogo, …’akasema huyo mzee.


‘Nyumba ndogo hata mimi ndio siikubali, ndio maana nimempa nafasi hiyo, kama anataka kumuoa, amuoe, tujue moja, na kama hataki anajivunga huku nafsi inatamani, lazima huduma zimfikie huyu binti,, ni dhamana tuliyokabidhiwa,..ichukulie hii kama ni adhabu kwako kwa kumzalilisha binti wa watu, na jiulize je kama ulipana begu zikaota, itakuwaje, hapo iliwazie kwa makini …huyu binti wa watu ana kosa gani, mim inaniuma sana kuchukua hatua kama hii, lakini najihami, ..hili ni tatizo ..mume wangu hajijuai tu..na kwa hili hata akija ndugu yangu wa kike humu ndani,, itabidi nifikirie mara mbili tatu…’akasema.


‘Mke wangu umefikia huko, huniamini tena…’akalalamika.

‘Sio swala la kuaminiana hapa, imetokea mara ngapi, huyu ni binti wa pili unamfanyia hivyo, huo sasa ni  ugonjwa, ni tatizo ulilo nalo, je akija mdogo wangu wa kike na yeye ukimtamani, usiku itakuwaje, ….hahaha, sio kwamba nacheka kwa furaha, lakini hili ni tatizo, na naomba mungu atujali tuwe kulipatia ufumbuzi wake, bila kufanya makosa ….naogopa sana, tukitoka hapa tunakwenda kumtafuta dakitari, na …jingine .nitafanya uchunguzi  wangu, mungu akipenda, nitakuja kuwapa matokea yake kama ni lazima…’akasema .


‘Mimi naona hapo tumemaliza…’akasema kiongozi wa dini.


‘Tunakusikiliza wewe…’akasema mzee na baba mwenye nyumba akamuangalia kiongozi huyo wa dini, kama vile anasubiria hekima zake za kumuokoa kwa hilo.


‘Unajau hakuna kitu kigumu na rahisi kama kutatua kesi ya wanandoa, lakini ugumu wake na urahisi wake unategemea na wanandoa wenyewe,…mara nyingi, sisi tunatakiwa kuwasikiliza wanandoa, na ni muhimu kila mmoja ukampa nafsi yake, mimi nimependa maamuzi ya huyu mama wa nyumbani...'akasema

'Japokuwa baba wa nyumbani anaona ni gumu sana kwake.., lakini hebu jaribu kulifanya kwanza kama mlivyokubalina hapa ili uone matokea yake, huenda ni heri kwenu, na tumuombe mungu iwe hivyo, mimi naona utafanikiwa tu,,maana binti wa watu akiendelea kukaa hapa, na haya yakiendelea kutendeka, ni dhambi kubwa sana, kazi iliyobakia ni nyie watekelezaji, mzee, ondoka na huyo binti, ili ulete amani kwenye hii ndoa, na..mambo yakikaa sawa, anaweza kurudi tena, …’akasema kiongozi wa dini.


‘Lakini wazee wangu, mimi naliona hili kuwa halijakaa sawa, naona kama mke wangu ananitega…’akasema mume wa familia.


‘Ni kazi yako sasa kuweka sawa hilo wewe ni mume…liweke sawa lisiwe ni mtego kwako, uwe na hekima za kuitunza ndoa yako, na hapo hapo,….uhakikishe huwaumizi wasio na hatia kama huyu binti wa watu, inasikitisha sana kwa haya yaliyotokea, hili sasa lipo mikononi mwako….’akasema kiongozi wa dini sasa akianza kuondoka.


‘Sawa, sina jinsi, nitafanya kama alivyotaka mke wangu, lakini sio kwa kuoa,..mimi bado nampenda mke wangu, haya yaliyotokea najua  ni mtihani kwangu,…nitaanza kuhangaika kumtafutia huyu binti sehemu ili aje kuishi na aanze maisha yake, nitajitahidi kufanya hivyo, nab ado tutaendelea kulijadili hili mimi na mke wangu, nawashukuruni sana wazee wangu…’akasema.

*****************

Mimi pale nikabakia nimeduwaa, sikujua ni nini kipo mbele yangu, sikujua ni nini hatima yangu, sikujua naenda kukabiliana na maisha gani huko mbele, lakini nikaona ni heri tu ,…maana kama hayo yaliyosemwa ni kweli, kuwa na mimi kumbe ilikuwa sio ndoto, ..hapo nikajihisi kama nimepakwa kinyesi, nilitamani nitoke pale nikaoge,…


Lakini pia nikaona ni heri niondoke hapo, maana chuki zilishaanza kunijaa, kwa huyo baba mwenye nyumba, japokuwa kama walivyosema sio dhamira yake, pia chuki kwa kijana wake, aliyejifanya mwema kwangu kumbe usiku wananizalilisha,..


Moyoni nilimuomba mungu anisaidie, kama kuna kosa kwangu, mimi sijui, ..namuomba mungu aniongoze kwenye njia sahihi, nisiwe sehemu ya mitihani kwa watu…nikajikuta nalia, nililia lakini kwa kujificha, na aliyenishtua ni baba wa mama mwenye nyumba.


‘Binti kajiendae tuondoke…’akaniambia, na nilipoinua kichwa nilijikuta nipo na huyo mzee, wengine walikuwa nje wakiagana,


 Baada ya hapo nikafungansha kile kilicho changu, na tukaondoka na baba mkubwa wa mama mwenye nyumba, machozi yalitoka sana nilipokuwa naagana na hawa watu, kwangu mimi pamoja na haya yote, niliwaona kama wazazi wangu…


Mama mwenye nyumba akasema wakati naagana naye,…


‘Unaondoka, sio kwamba nakufukuza, lakini pia iwe ni fundisho kwako, najua kuna kitu umenificha, sasa ni juu yako, kama uliona mume wangu ni mbora kwako, ukamtetea, badala ya kusema ukweli wote, sasa utakuja kuona ukweli wa kusema ukweli, sikuombei mabaya, ila inatakiwa na wewe ukaayanze maisha, ili ujue maisha yalivyo na changamoto zake, na najua, hakuna baya lolote linaweza kutokea huko mbele.., ila likitokea usisite kuniambia, ila lisiwe kuhusu mume wangu au kijana wangu, kwasababu mwenyewe umekiri kuwa hawajakutendea mabaya,..sawa..kwaheri..

Sikuweza hata kumuangalia baba mwenye nyumba machoni au kijana wake, sikuweza hata kuwasemesha, nilipitiliza hadi kwa mzee, ambaye sasa ndiye atakuwa mafadhili wangu, na safari nyingine ya maisha ikaanzia hapo…



NB: Tukutana kwenye sehem uijayo, je itakuwa hitimisho la kisa hiki, au kuna muendelezo wake, ngoja nimuulize msimuliaji je huko kulitokea nini…kwani wakati ananihadithia hilo, alikuwa kambeba huyo mtoto, je huyo mtoto ni wa nani

WAZO LA LEO: Dhambi ni dhambi tu, hata ukitenda kwa siri, ni dhambi!!

Iweje tuwaogope wanadamu wenzetu, kwa kuchelea kuonekana tukitenda madhambi yetu…, tukidhulumu, tukiwanyanyasa, na kuwadhulumu haki zao mayatima na masikini…, tukiwanyanyapaa wasiojiweza na wazee kwa maneno ya kejeli kama vile na sisi hatutakuwa hivyo, ..tukiwadhulumu wafanyakazi haki zao, kwa vile sisi ni wamiliki au ni vingozi tuliopewa mamlaka hayo...nk


 Tunasahau kuwa yule aliyetuumba anatuona, hata kama tumejificha tukitenda  hayo madhambi , tukumbuke yeye aliyetuumba hana mapungufu tuliyo nayo sisi viumbe wake, anayabaini yote, ya siri na ya dhahiri.


 Tumuombe mola wetu atusamehe makosa yetu na atuongoze njia iliyonyooka.

Ni mimi: emu-three

No comments :