‘Wewe
ndio kawaida yako unapenda mizaha mizaha..soda umechelewa kuleta, na bado
unanigandisha,….mimi nakwenda ndani, …’akasema huyo mdada akiwa kainamisha
kichwa chini, na aliposimama mimi nikajitokeza,..tukawa tunaangaliana uso kwa
uso,…
Unajua
kushtuka, mimi nilishikwa na mshituko wa aina yake, …nikajikuta nimekodoa
macho, …siamini ninachokiona mbele yangu,..kwa maana aliyekuwa kasimama mbele
yangu sio mwingine, ni yule mpenzi wa facebook.
Mpenzi
wa facebook,…aliyetaja tuonane na yeye nikajikuta makaburini na safari nyingine
akanitokea tukapata ajali mbaya…nikaja kuambiwa huyo sio mtu ni shetani, mpenzi
wa facebook, tuliyeambiwa ni mtu wa kutengeneza, akiambatishwa na nguvu za
giza,..mpenzi wa facebook…oh, sasa huyu hapa yupo mbele yangu.
Tuendelee
na kisa chetu…
******************
‘Oh,
we-we ni na-niii…?’ nikamuuliza nikishikwa na kigugumizi, mimi sio muoga,
lakini kwa hali hii nilijikuta nikishikwa na kigugumiza cha kutokuamini, ..huyu
ni mtu au..na kama ni mtu , kwanini nikaambiwa kuwa huyo mtu hayupo katika hali
ya kibinadamu.
‘Hahaha,…sasa
hivi unajifanya kuwa umenisahau au?…’akasema na kuuliza hakutaka kuniangalia
machoni tena, akawa kaangalia upande.
‘Mhh…sina
uhakika na wewe, huenda ni mbinu zenu tena hizi …’nikasema.
‘Mbinu
gani,… unakumbuka tuliahidiana nini mimi na wewe…, ukasema utakuja nyumbani,
hukuwahi kufika,…. ukanidanganya, hiyo ndio tabia yako ya kuhadaa mabinti,
eeh,…haya mimi nimekuja mwenyewe,…unasema eti, ni mbinu zenu na nani…?’
akaniuliza.
‘Oh,
siwezi ku-kuamini, wewe ni kweli..hapana, ….msitake kunichanganya…’nikasema.
‘Wewe
mwanaume, mbona unakuwa hivi, unajua mimi sikuzoea tabia hizo, mimi sio mtu
wa…unajua nikuambie kitu,..kama umezoea kuwahadaa mabinti wengine mimi sio aina
hiyo,…ina maana yale uliyokuwa ukiniambia kwenye facebook, ulikuwa unanivunga,
eeh, ongea kama mwanaume..?’ akaniuliza, nikajaribu kumuangali.
Oh ndio yeye, sura, ..oh,..jamani, huyo mdada
wa facebook,.. katoka wapi, nilishaanza kusahau kuwa kuna mtu kama huyu,
nikakumbuka walivyosema kuwa mpenzi wa facebook, walimtengeneza, ..au ni
shetani, au…
‘Mbona
mdogo wake, …..kaniambia nije huku nitakutana na dada yake..sasa nakutana na
huyu mzuka, …sijui, au…hapana hapa kuna jambo, lisilo la kawaida,…’ niliwaza
hivyo huku nageuka huku na kule,kumtafuta ndugu yake yule binti, lakini
hakukuwa na dalili ya mtu mwingine hapo karibu.
‘Unaonekana
una wasiwasi sana, kuna mtu mwingine unatarajia kukutana naye nini,
nimekuvurugia dili yako au sio, sema ukweli, napoteza muda wangu,…?’ akaniuliza
na mimi kwa haraka nikajibu;
‘Ndio…’nikasema
‘Ndio…msichana
au sio, kama kawaida yako,..?’ akaniuliza
‘Mpenzi
wangu, …mchumba wangu…’nikasema
‘Eti
nini,….Hahaha, nilijua tu, nyie wanaume waongo, ina maana kuniambia kote kule
kuwa unanipenda, ilikuwa ni hadaa tu, ukasema hata kulala, hulali kwa kiniwaza
mimi, ukawa ukilala unalala na laptop pembeni, tunaangalia, …oh, kumbe ndivyo
ulivyo eeh, sasa nimeshakujua…’akasema.
‘Sikiliza
kwanza, kipindi hicho nilikuwa sijitambui , sijui ni kwanini, pili, sikujua
mchumba wangu kama bado yupo,..nilijua keshaolewa,….au..kwahiyo sikuwa na
uhakika, nilipokuona wewe, kwa vile ulikuwa unafanana naye nikajua nimepata
badili yake,…’nikasema.
‘Hahaha,
…..unanishangaza sana wewe mwanaume,..kwahiyo unataka kusema nini..?’
akaniuliza akionyesha kukasirika.
‘Nikuombe
samahani tu, kwa vile mchumba wangu keshapatikana, na nilikuja hapa kwa ajili
ya kukutana naye…’nikasema.
‘Una
uhakika gani kuwa huyo mchumba wako, yupo tayari kuolewa na wewe, baada ya yote
haya…una uhakika gani kuwa hajafahamu kuhusu mpenzi wako wa facebook,…, je
nikikuambia nimeshajitambulisha kwake, kuwa mimi ndiye mchumba wako
tuliyekutana naye kwenye facebook, utasemaje…hahaha, utakosa kote, halafu
utakuja kujuta, …’akasema.
‘Hata
kama ….mimi sitajali, ilimradi yupo hai, sitachoka kumsubiria, yeye ndiye
chaguo langu, wewe ilitokea tu, na sielewi, maana nilisikia wewe sio
halisi..lakini hata hivyo, nashukuru kwa kukutana na wewe, ili nikuambie
ukweli, kuwa mimi na wewe basi, sitaki tena mawasiliano na wewe....nisamehe kwa
yote, najua nitakuwa nimekuumiza sana, lakini…’nikasema nikitaka kuondoka.
‘Hebu
subiri kwanza…unataka kwenda wapi, ..hunijui eeh, ulifikiri, wasichana weote ni
wakuchezea, sasa nikuambie kitu, nitakufanya jambo hutalisahau..unasikia…’akasema
akitaka kunisogelea, sikutaka aniguse, japokuwa sina imani na imani za
mashetani, lakini hapo nilitaka kuwa na tahadhari, nakumbuka hayo yaliyotokea
huko nyuma, nikawa nawazia huyo asije akawa shetani kaja kunighilibu.
Alipotaka
kunigusa nikaruka mbali na yeye..nikasema;
‘Wewe
mwanamke vipi…ina maana ..’nikasema;
‘Subiri
, nikuonyeshe kuwa sio wote wana tabia hizo, nataka nikufunze adabu,….’akasema
na mimi nikaanza kukimbia..huku nasema;
‘Samahani
sana, …nielewe tu, mimi sikutaki tena, na kama unataka kunifanya nini, fanya,
mungu atalinda na mashetani, na ubaya wake, ….’ Nikawa nimeshamuacha mbali,
Na
wakati, nipo mbali na huy binti,… mara kwa mbali nikasikia kelele za
kushangilia, kelele hizo zilitokea mlangoni mwa nyumba ya hiyo familia ya mzee,
kwanza nikajisikia vibaya, kuwa wataniona nimesimama na huyo msichana, kwahiyo
nikazidi kukimbia mbali kama nataka kutoka nje ya geti.
‘Hahahaha…….’mara
nikasikia mtu akicheka, akiwa anakuja usawa wangu, lakini sikutaka kugeuka, ila
nilishajua huyo anayecheka ni nani, ..hicho ni kicheka cha mdogo wake, yule
msichana wa kwanza wa huyo mzee.
Nikawa
sasa nipo getini, nataka kufungua mlango wa geti nitoke nje,..huyu mdada
akanijia na kuanza kuongea..huku bado anacheka,…nikawa sielewi kitu, na
aliponikaribia akasema;
‘Umeonaeeh,
huyo ndiye mpenzi wako wa facebook, sasa amua moja dada yangu au huyo mpenzi
wako…’akasema
‘Kwanini
umefanya hivyo..huyu shetani katokea wapi..?’ nikamuuliza
‘Hahaha,
eti shetani, sinimesikia wewe haumini mambo hayo,….’akasema
‘Sikiliza,
sasa naona umevuka mipaka hivi dada yako angeliniona nimesimama na huyo
msichana, unafikiri angelijisikiaje,…na dada yako yupo wapi..?’ akaniuliza.
‘Hahaha….’akacheka,
na akawa anaangalia kule mlangoni ambapo nilisikia sauti ya kushangilia, na
sikutaka kugeuka kuangalia kule…nikasogea kama kutaka kuondoka, na kitu
kikasema niangalie kule mlangoni kabla sijaondoka…kule niliona familia yam zee,
wakiwa wamesimama, wakituangalia..
Hapo,
sasa sikutaka kusimama tena nikavuta mlango, ufunguke niondoke kabisa eneo hili…na
huyu mdada akageuka kuwafuta wenzake huku akicheka, na wakati sasa nimeshatoka
nje, mara nikasikia sauti ya docta,…
‘Wewe,
mbona unaondoka..?’ akaniuliza na mimi sikumjibu nilikuwa sasa nipo kwa nje, na
docta akatoka na kunikabili.
‘Mbona
unaondoka, kuna nini kimetokea..?’ akaniuliza.
‘Sijisikii
vizuri,….’nikasema hivyo tu.
‘Unaumwa..au…lakini
hata hivyo, huwezi kuondoka kienyeji hivyo, …nataka kukuambia jambo…’akasema akinishika mkono ili
anirudishe ndani.
‘Hapana
docta, nielewe tu,…mimi siwezi kurudi tena huko ndani, sitaki kuendelea kuwepo
tena eneo hili…, nimekutana na mambo ya ajabu huko..’nikasema.
‘Mambo
gani…?’ akaniuliza akiniangalia usoni, nikakwepa kuangalia na yeye moja kwa
moja, maana huyu docta anakipaji cha kukugundua unawaza nini mkiangalia moja
kwa moja.
‘Hata
siwezi kuamini,… hivi docta, si ulisikia mwenyewe, kuwa mpenzi wa facebook, ni
vitu walitengeneza tu,…na wewe ukasema ni shetani, au sio..’nikasema na docta
akaniangalia huku amejaa tabasamu usoni, akasema;
‘Hebu
nikuulize kwanza kabla sijajua ni nini lengo la swali lako, hivi kwa mfano kama
huyo mpenzi wa facebook yupo kweli, utafanyaje..?’ akaniuliza.
‘Kwa
vipi, kwanza nijue yupo kweli au hayupo..’nikasema.
‘Kwani
wewe umekutana naye..?’ akaniuliza akionyesha mshangao.
‘Ndio…’nikasema.
‘Una
uhakika…’akaniuliza.
‘Docta,
akili yangu ni timamu, sizani kama imerudia kipindi kile cha kuchanganyikiwa…nina
uhakika ndio yeye, nimemuacha
punde,…docta sielewi haya mambo, kuna nini hapa..’nikasema.
‘Nakuuliza
tena, je kama huyo mpenzi wa facebook yupo upo tayari kuwa naye…?’ akaniuliza,
na kunifanya nihisi kuwa docta anajua kinachoendelea, na ya kuwa wanataka
kunipima kama kweli nampenda mpenzi wa facebook, au huyo mdada wa hapo nyumbani
kwa mzee.
‘Docta
unalifahamu jibu langu tayari, siwezi kuwa muasi kiasi hicho baada ya haya
yote, sizani kama naweza kugeuka nyuma, nitakuwa sio binadamu mwenye utu,
…hapana docta , huyo ni shetani, katokea wapi huyo mdada, au una fahamu haya
mambo, mlionana naye wapi mkaamua kuchezea hivi…’nikasema.
‘Hahaha,
sasa umeshaanza kuamini hayo mambo, naona akili yako imeshageuzwa, nilijua wewe
ni imara, huwezi kutetemeshwa na mambo kama hayo, kwanza nikuulize una uhakika
kweli huyo uliyekutana naye ni binadamu, maana unachozungumza hapa, hakipo,
huyo mpenzi wa facebook, hayupo..…’akasema.
‘Docta,
ina maana huaniamini.. nimekutana naye, nilikuwa naongea naye,..ndio yeye
mpenzi wa facebook,....’nikasema.
‘Hebu
twende huko ndani, ukanionyeshe,…’akasema
‘Docta,…nimemuacha
ndani, na hajatoka, twende…’nikasema na tukaingia ndani tena, na kutembea hadi
pale alipokuwa huyo mdada, hatukukuta mtu, au dalili za kuwepo mtu hapo.
‘Haiwezekani…ina
maana ni shetani….’nikasema
‘Yupo
wapi…?’ docta akaniuliza.
‘Docta,…kwa
kauli yako wewe ulisema huyo msichana ni shetani, na kwa kauli yao mbele ya mahakama
wamesema walitengeneza msichana wa facebook, kuhadaa watu ili watimize lengo
lao..basi huyo waliyemtengeza yupo mitaani, kama ni shetani basi lipo mitaani,…’nikashika
kichwa.
‘Sikiliza
mimi ni rafiki yako, niambie ukweli, je upo tayari kuwa na huyo binti, au la…?’
akaniuliza.
‘Binti
yupi sasa..?’ nikamuuliza.
‘Niambie
wewe…’akasema docta.
‘Docta
kuna nini hapa..nahisi kuna mchezo mnanichezea, mimi sio mjinga kiasi
hicho,..niambie ukweli docta, kwanza ile familia imetokezea pale mlango, ikawa
kama inashangilia,walikuwa wanashangilia nini,…’nikasema na docta akacheka,
halafu akasema;
‘Twende
tukaage tuondoke maana utachanganyikiwa ..nataka nikakupe dawa za kusafisha akili
yako, nahisi haupo sawa, mengine tutaongea huko…’akasema, na sikumbishia,
tukaenda kuaga..lakini tukakuta familia wapo wanaongea na watu wengine na
tusingeliweza kukatisha mazungumzo yao, na mimi nilijitahidi kuficha hisia
zangu, na wao hakuna aliyeonyesha dalili za kutaka kunidadisi, ilikuwa kama
kawaida tu.
*************
‘Twende…’akasema
‘Si
tunaondoka au…?’ nikauliza
‘Hapana
kabla ya kuondoka, kuna jambo nataka tulifanye kwanza…..wakati familia
wanaagana agana na watu wengine ni lazima tuchukua nafasi hii, ni muhimu sana…’akasema.
‘Hapana
docta, mimi sitaki kuongea na mtu mwingine, akili hapa haipo sawa…’nikasema.
‘Wewe
usiharibu mambo, …’akasema na mimi nikamfuata tu kinguvu nguvu, hadi nje tena,
na sasa ilikuwa sehemu nyingine iliyotulia, akasema;
‘Wew
nisubiri hapa, nakuja….’akasema na docta akaondoka, na mara nikasikia mchakato
wa kitu kinakuja,..kwanza nikahisi ni huyo huyo mpenzi wa facebook, moyoni
nikawa namuomba mungu aniongoze, kama kweli mtu huyo yupo, basi anisaidie , na
kama ni shetani aliharibu, lipotee kabisa…
‘Habari
yako…’sauti ikanishtua, ni sauti ya dada mtu, hapo, nikajipa moyo, nikageuka,
na sasa nikawa naangaliana na huyo mdada, msichana ambaye aliteseka kwa ajili
yangu, msichana ambaye ilisadikiwa kuwa amekufa kwa ajili yangu..watu wakasema,
amejiua kwa ajili yangu…lakini kama binadamu unajua tulivyo, unapokuwa
unalinganisha mambo….nikawa namlinganisha na mpenzi wa facebook, sikuweza
kupata jibu ni nani zaidi.
‘Oh,
umekuja, unajua mdogo wako alisema upo kule,…’nikaanza kusema hivyo .
‘Kule
wapi…halafu ikawaje…?’ akaniuliza.
‘Aah,
tuyaache hayo nashukuru sasa nipo na wewe, na…nilitaka niipata nafasi hii,
tuongee, mimi na wewe, ni docta kakutuma uje huku au..?’ akaniuliza.
‘Kwanza
nijibu swali langu kule ulikutana na nani..?’ akaniuliza.
‘Mimi
sijui mdogo wako ana maana gani, kanikutanisha na msichana ambaye sikutaka
kabisa kukutana naye…’nikasema.
‘Msichana
gani huyo…?’ akaniuliza
‘Aaah,
nitashukuru kama hilo utaliacha kama lilivyo, mimi naomba tuongee ya kwetu,
ndilo muhimu kwangu…’nikasema.
‘Ulikutana
na mpenzi wako wa facebook, au sio..?’ akaniuliza.
‘Oh,
ni nani kakuambia,…?’ nikamuuliza.
‘Haah,
bado unaye kichwani,…’akasema na akaonyesha kama kukata tamaa, au…na mimi
nikasema;
‘Mimi
nijuavyo huyo msichana hayupo, ni hadaa tu walitengeneza kuninasa, sasa
nashindwa kuelewa,..na hata hivyo, ..kama yupo basi ni hao wasichana
wanaotafuta biashara tu, siwezi kamwe kujihusisha nao,..mimi nataka tuongee ya
kwetu, mimi na wewe…naomba uniamini….’nikasema.
‘Sawa kama maongezi yako hayana shari karibu
sana, mungu anajua zaidi yaliyopo moyoni mwako kuliko mimi,,..na pili docta
kanichukua juu kwa juu kuja huku, nilijua nakuja kuonana na mdogo wangu , mara
nakutana na wewe..’akasema.
‘Aaah,
kwakweli …akili yangu, imeharibika, ..naomba unielewe tu, mimi nia na lengo
langu ni kuongea na wewe, na sio huyo ..sheta-tani..’nikasema.
‘Mhh..kama
akili yako haipo sawa, mimi naomba uende ukapumzike, usije ukaongea mambo bila
kufikiria,na hata mimi nahitajia kupumzika, au sio, basi mimi naondoka…’akasema.
‘Hapana
usiondoke, nataka tuongee ni muhimu sana…’nikasema’
‘Mimi
siruhusiwi kukaa vichochoroni na wanaume, wazazi wangu wakiniona hivi
hawatakuwa radhi na mimi,..japokuwa
mungu anajua ni nini kilichopo moyoni mwa kila mja wake…niambie ulichotaka
kukisema, nakusikiliza…’akasema.
‘Mimi
kwanza naomba radhi kwa yote yaliyotokea, kiukweli siku ile ulipofika sikuwa na
mimi..’nikaanza kujitetea.
‘Siku
ile ..ipi..?’ akaniuliza akionyesha uso wa mshangao.
‘Siku
ile ulipofika nyumbani kwangu…najua ni muda sana umepita…lakini mimi naona kama
ilikuwa jana…’nikasema.
‘Ok
hayo yalishapita, kama ni hilo tu, mimi
nimeshakusamehe, kabisa, usiwe na shaka na hilo, mungu mwenyewe anajua ni
kwanini ilitokea hivyo…’akasema.
‘Lakini
nilitaka pia kukuelezea ukweli kwa jinsi ilivyokuwa siku ile, kuwa sio kweli
kuwa yule msichana alikuwa ni mpenzi wangu,..alikuja na hadaa zake, na
nakuhakikishia na mungu ni shahidi yangu, sikuwa na ajenda yoyote na yule bint,…’nikasema
akaniashiria kwa mkono.
‘Nimeshakuambia,
sitaki kusikia hayo tena, yameshapita, usisumbuke kujielezea, mimi nimeshajua
kilichotokea, nimeshaambiwa kila kitu, usiwe na shaka na hilo….’akasema
‘Ni
nani kakuambia..?’ nikamuuliza.
‘Na
hilo tena, unataka kujua, hapana,hatukuongea ili nije kukuambia….’akasema.
‘Na
…moyoni mwako umeniamini kuwa mimi sina tabia mbaya kiasi hicho..?’
nikamuuliza.
‘Haah,…nikuambe ukweli kutoka moyoni mwangu, kwa
hali kama ile sio rahisi mtu kukuamini tena..unielewe tu hivyo..’akasema.
‘Mungu
ni shahidi yangu, sina zaidi ya hilo, na sikutaka kusema hayo mbele ya watu,
maana masikio ya wengi yangeliweza kubadili ukweli kuwa fitina,..nimeishi hivi
hivi, sikutaka kuwa na mpenzi maana nilijua wewe ni chaguo langu, sikujua kuwa
kuna jambo limetokea huku nyuma…’nikasema.
‘Sawa
yamtokea mengi tu… na hayo yaliyotokea, yanaweza kubadili mstakabadli mnzima wa
nafsi ya mtu, …na ni vyema ukawa muwazi, ..na hata hivyo ulichoniitia
umeshaniambia au sio, ulitaka kuomba msamaha..mimi nimekusamehe, ..’akasema.
‘Sijaongea
nilichotaka kuongea..’nikasema.
‘Unataka
kuongea nini, mimi ningelikushauri, kama ulivyosema akili yako umetatizwa, ni
bora urudi nyumbani utulia, ili uwe na uhakika na mambo yako, ..japokuwa sijui
unachoataka kuniambia, lakini…..’akatulia.
‘Hapana
siwezi kuondoka mpaka nikuambie ya moyoni mwangu,..sijaweza kuwa na rafiki wa
kweli, …tangia tuachane mimi na wewe…’nikasema.
‘Una maana muda wote huo ulikuwa huna rafiki
wa kike..?’ akaniuliza.
‘Rafiki,.??
Hahaha,….kwa maana ya rafiki, kuongea kupotezeana mawazo..siwezi kusema hakuna,
lakini sijawahi kumtamkia mtu kuwa nakupenda, au nakutaka, ..siwezi kusema ni
kwa ujanja wangu, hapana, nafsi wakati mwingine inatamani kutenda hisia za
mwili, lakini haikuwahi kutokea,…lakini nashukuru mungu amekuwa akiniokoa kwa
namna ya pekee, na hadi sasa simjui mtu moyoni mwangu, mwilini mwangu zaidi
yako wewe…’nikatulia.
‘Mhh,
ujue unaongea na nani,…mimi sina haja ya kuimbiwa mashairi, nakupenda, nakuota
nakuota,…unasema hujawahi kumtamkia mtu kuwa nakupenda, je na huyo mpenzi wa
facebook hukuwahi kumtamkia kuwa unampenda..?’ akauliza na kunifanya nishutike,
nilishasahau kuwa kulikuwa na mtu kama huyo.
‘Ni
nani kakuambia kuhusu huyo shetani,…’nikasema.
‘Leo
hii huyo amekuwa ni shetani, au…?’ akaniuliza
‘Kiukweli
sikuwahi kukutana na huyo mtu kabla, ni leo kwa mara ya kwanza.., ilitokea tu
nikajuana naye kwenye mtandao wa facebook, na nikuambie ukweli, nilivutika naye
kwa vile anafanana na wewe, awali nilijua ni wewe, na nilipoambiwa umefariki…basi
tena, nikajua mungu kaniletea badili yake..na na kiukweli, ..’ nikasita.
‘Hahaha
eti kafanana na mimi, una uhakika na hilo..?’ akaniuliza.
‘Mnafanana,
fanana na yeye, kisura, hata kimwili, lakini sio, kitabia, wewe umemzidi sana
kitabia, unajua mimi nilishamsahau huyo mtu, maana, hao watu wabaya…walisema
walichukua sura yako, wakachanganya na sura ya mama yao…unajua tena, ni mambo
ya kishetani, ya kunipumbaza akili…’nikasema.
‘Sasa
si umeshamuona mbashara, niambie…au bado haupo sawa, ..huyo umemuona, sisi ni
sawa na ndugu zako tupo tayari kukusaidia, umuoe…’akasema.
‘Eti
nini…nimuoe,..hahaha, hunitakii mema, ..hivi kweli kama ungelikuwa ni dada
yangu ungelinishauri kitu kama hicho..hapana, siwezi, ..mimi ninachotaka ni
kukuoa wewe..narudia tena, mimi …’nikasema na akanikatisha kwa kusema.
‘Basi
mimi nikushauri kitu, kwa nia njema, maana usije ukawa unaongea, kwa vile… huku
akili yako ipo kwa mtu mwingine, utakuwa huna raha katika maisha yako ya ndoa,…pata
kwanza muda wa kutosha wa kutafakari hilo,na ni vyema, ukamtafute kwanza huyo
mpenzi wako facebook, ukae naye muongee, ujiridhishe,.. nikwa ushahuri wangu tu..’akasema.
‘Hapana,
moyo wangu upo kwako,..ulipozindukana pale hospitali.., ukafunua macho yako,
ulinifanya nihisi vingine kabisa..nakupenda sana, amini hilo, huyo alikuja
kuighilibu nafsi yangu, sio aina yangu, kabisa...’nikasema.
‘Mimi
namtegemea mungu peke yake, kama ni wewe , kama yupo mwingine nitampokea kama kweli
mungu kapenda iwe hivyo..siwezi kukata kuwa kweli wewe uliutekea moyo wangu kwa
mara ya kwanza, lakini ukauvunja kwa nyundo kubwa sana..nikabakia na jeraha
kubwa.
‘Mhh,
samahani kwa hilo, nisamehe sana, nielewe ndio maana nilitaka nikusimulie
yaliyokuja kutokea hadi ikafikia pale, nisamahe, na nielewe…’nikasema, na yeye
akaendelea kuongea wakati nami naongea.
‘Sasa
kuja kujitibia hili jeraha..mmh.., sijui…ninachopenda kukuambia, ni kuwa uwe na
subira nilitibu kwanza hili jereha moyoni mwangu na siku likipona,..na mungu
akanielekeza kwako, basi.. nitakuja kwako kama siku ile…,au nitakutumia ujumbe
wa maneno kwenye simu, ila usiharakishe kufanya lolote kwangu, mpaka mimi
nikuarifu..sitaki kulazimishana,…tafadhali,..’akasema akitaka kuondoka.
‘Kwahiyo…’nikauliza.
‘Kwahiyo
vipi tena, kwani hujanielewa… nakuomba uondoke hapa wasije kutokezea wazazi
wangu ikawa ni sababu ya mimi kuwakosea tena wazazi wangu, nawapenda sana
wazazi wangu..’akasema na mimi ikabidi niondoke tu.
**********
Baadae
ndio nikakutana na docta akaniuliza ilikuwaje, sikutaka kumuelezea mengi,
nikamwambia;
‘Aaah,
binti kama kawaida yake,..anataka nimpe muda, …anasema nilimuumiza sana siku
ile, kwahiyo anahitajia muda wa kutafakari..’nikasema.
Docta
akasema;
‘Nimeongea
na wazazi wa hao wasichana wawili, nikaamua kuwa mshenga wako japokuwa sio
rasmi..nikawaambia kuwa mimi nachukua dhamana kwako, kama mshenga asiyerasmi,
ila tutakuja tena, kama watanikubalia ombi langu,…
‘Oh
docta…’nikataka kusema na yeye akanikatisha kwa kuendelea kusema;
‘Wakaniuliza
nina maana gani, unajua wazazi wanakuwa makini sana kwa maswala yanayohusu watoto
wao, wanaweza wakajua ni nini , na walijua ni nini nataka, lakini walihitajia
uhakika, basi mimi nikawaambia, kama mjuavyo rafiki yangu alikuwa rafiki wa binti
yenu kwa siri, na hakuwa na nia mbaya, sasa anataka kujibainisha kwenu kuwa
yupo tayari kumposa binti yenu…hapo wakajifanya kushtuka, na kusema;
‘Mhh,
hivyo….lakini mbona haraka hivyo, bint yetu bado hajatulia baada ya mikasa hii
iliyotokea,… unajua tulijaribu kumuulizia hilo,…kama wazazi ikitokea kitu kama
hicho, unapata ishara kuwa binti au kijana wako kakua na anahitajia mwenza,
kwahiyo hatukusita kumuuliza , kuwa yupo tayari kuolewa kwa hivi sasa, akasema
kwa sasa hataki kabisa mambo ya kuolewa..
‘Ehe,
kwasasa unataka nini..usije kusema hivi na wakati una jingine,….’tukamuambia
hivyo na yeye akasema;
‘Lengo
langu kwa hivi sasa ni kusoma zaidi…, sasa nashindwa kukupatia jibu la haraka
la ombi lenu, unielewe hapo, maana japokuwa sisi ni wazazi, lakini muhusika
anahitajika kutupatia majibu yake, kabla hatujasema lolote…’akasema hivyo baba
yake.
Mimi
nikawaambia, ‘kama ni kusoma atasoma tu, anaweza akafanya hivyo akijulikana
kuwa ni mchumba wa mtu, au akasoma baada ya ndoa, hilo halitazuia yeye kutimiza
dhamira yake, mimi nachukua dhamana hiyo kuwa binti yenu hatapata shida,..atatimiza
malengo yake bila wasiwasi, na kiukweli, huyo rafiki yangu na binti yenu,
wanaivana, na sio mimi tu, hata wabaya wenu waliligundua hilo kuwa huyo hawa
wawili nyota zao zinafanana, wakioana mambo mengi yataenda vyema.
‘Basi
sisi tunaomba mtupe muda tutaongea na binti yetu akikubalia, sisi hatuna shaka
na nyie…tumeshajiridhisha kwa hilo’
‘Oh,
sasa mbona itakuwa shida,….’nikasema nikikumbuka kauli ya huyo binti kama
angalizo kuwa nitakutumia ujumbe wa
maneno kwenye simu, ila usiharakishe kufanya lolote kwangu, mpaka mimi
nikuarifu..sitaki kulazimishana,…
‘Hakuna
shida hapa, mimi nawapa siku kadhaa, wakiwa kimia, mimi mwenyewe nitakwenda
huko rasmi…’akasema
Haikupita
siku mbili, nikapokea ujumbe kwenye simu,..maneno machache tu, yakisema;
‘Nimeridhia
ombi lako, japokuwa umevunja sharti langu….’aliandika hivyo tu.
‘Nimevunja
sharti lake, oh, nilijua tu…docta kakurupuka mapema…’nikajisema hivyo.
Nilimuambia
docta, na docta akasema hakuna haja ya kusubiria yeye atafuatilia taratibu zote
kwa haraka, anafanya hivyo kwa vile anatarajia kusafiri nchi za nje…, kuna
mualiko wa kwenda kujiendeleza zaidi na wenzake, na zaidi ni kuwa kapata kazi
huko huko, kwahiyo yeye hatakuwepo hapa bongo mara kwa mara, atakuwa anakuja
kwa likizo tu.
‘Sijui
nitakaa huko kwa muda gani, ila tutakuwa tukiwasiliana, ..ndio maana nataka
kabla sijaondoka, nihakikishe hili limefanikiwa,na zaidi, nilikuwa sitaki
kuwalipisha hiyo familia pesa nyingi, lakini hutaamini kwenye lile jengo,
litapigwa mnada, mke wa mzee, atapewa fungu lake, kwa yote yaliyotokea, na
unajua tena wamiliki wote hawapo duniani…unakumbuka yule mtu aliyekuwa
akiendesha hilo jengo, ndio yule mtaalamu, siku zile alijibadili,..na alikuja kugundulikana
wakati wanampima maiti yake…’akasema.
‘Kuna
kipindi walisema sio Mtanzania…’nikasema.
‘Ndio
kwa jinsi alivyokuwa akifanya shughuli zake pale, alijulikana kabisa kuwa yeye
sio mtanzania,…alijitahidi sana kufanikisha hilo, waliokuwa wanaufahamu huo
ukweli ni hao washitakiwa wawili,…lakini yeye ni mbongo, na ana udugu fulani na
hao washitakiwa wawili…
‘Duuh,
kweli walicheza mchezo, japokuwa ulikuwa mchezo mbaya…’nikamwambia docta hivyo
Basi docta akafanya kazi ya ushenga rasmi,
hakutaka kumtafuta mtu mwingine… na akafanikisha kila kitu,..hatimaye nikafunga
ndoa na huyo binti mkubwa wa mzee… nikaanza maisha kutoka sifuri, nilikuwa sina
kitu, pesa aliyonipa docta niliitumia kwa mahari, na maandalizi madogo madogo,
mke anaingia ndani, tunaanza kupiga mahesabu jinsi gani ya kuishi…hatukutaka
kuishi kwa wazazi wake, au…hapana yeye na mimi tukakubaliana tukaze buti…!
‘Mungu
ametusaidia sana, hatua kwa hatua, tunaanza kujiweka sawa, ..ndio maana
umenikuta katika hii hali rafiki yangu, sikuwa hivi, unanifahamu sana, yote
maisha, na yote ni kwasababu ya mpenzi wa facebook,….’akanimalizia kisa chake
na alipotamka hayo maneno ya mwisho akacheka.
‘Sasa
nikuulize kitu, huyo mpenzi wa facebook yupo kweli..?’ nikamuuliza.
‘Hahaha,…mpenzi
wa facebook,..ni kweli yupo…hutaamini…’akasema.
‘Yupo
wapi,….keshaolewa, mnaonana naye au ulipo-oa, ndio hamukuwahi kuonana naye
tena..?’ nikamuuliza.
‘Hivi
hujanielewa hadi hapo,..huyo mpenzi wa facebook, ni mke wangu…. unajua ni nini
kilifanyika siku ile, …kumbe docta wakati anaongea na wazazi, mimi nipo nje,
akataka kuwaridhisha, kwa kunitega, akawaambia ili wote wahakikishe kama kweli
nampenda binti yao au huyo mpenzi wa facebook, basi wafanye jambo moja, kunipima..
‘Wakamuita
binti, docta akamsomesha ni nini kinatakiwa kifanyike, kwanza binti alikataa ,
lakini wazazi wake waliposhinikiza akakubali,..kufanya hilo igizo, la kunipima
mimi, ..mimi muda huo sijui lolote, sikuwahi kuongea na docta, kuwa nitajibu
vipi,… basi docta kwa vile alikuwa na ule mtandao unaoweza kubadili sura kwa
kuvalisha ngozi, akamvalisha huyo binti sura ya yule mpenzi wa facebook,…nia
yao ni unipima akili yangu….
‘Kwahiyo
ina maana…’nikataka kusema, na yeye akaendelea kusema;
‘Huyo
mpenzi wa facebook, niliyemkuta pale, ni huyo huyo mdada, ambaye sasa ni mke
wangu, alivalishwa hiyo sura, nia ni kunipima, kama kweli nampenda yeye au huyo
mpenzi wa facebook, na nashukuru mungu niliweza kufanya yaliyowaridhisha wazazi
na hata …mke wangu....umenielewa hapo.
Na
ujue wakati naongea na huyo mpenzi wa facebook, wao walikuwa wakiniangalia
kwenye laptop ya docta, mbashara…hata
huyo binti hakujua kuwa tunaangaliwa.. ndio maana walipotoka pale mlangoni wakaanza
kushangilia…sikujua wanashangilia nini, hata huyo binti hakujua hilo…, sikujua
mdogo wake, alipojitokeza mbele yangu alikuwa na furaha gani..kiukweli ilikuwa
ni kitendawili kwangu!
‘Oh,
hongera sana, …mpe salamu shemu, mpenzi wako wa facebook, wa kweli…’nikasema na
tukashikana mikono ya kuagana.
***********Na
hapa ndio mwisho wa kisa hiki*************
WAZO LA LEO: Sio kila king’aacho
ni dhahabu, …na sio kila anayekuchekea ana nia njema na wewe…muhimu tuwe makini
kwenye maamuzi yetu, tumuweke mbele muumba wetu, kwani yeye ndiye anayejua ya
siri na ya dhahiri!
NB:
Nawashukuruni sana nyote mlioweza kukifuatilia hiki kisa hadi mwisho..najua sio
wote watafurahia kila kitu, lakini hivyo ndivyo nilivyoweza kuwakilisha hili
tukio, ama kwa wale waliotaka kumuona au kuwasiliana na docta, ..huyo docta
hayupo hapa nchini kwa sasa…
Ama
kwa hiki kisa.., kama ni kizuri, basi tuelimike sote, na ujumbe uliopo ndani ya kisa hiki uwe ni
shule kwetu, …mojawapo ni kuwa tuwe waangalifu kwenye kutumia hii mitandao ya
kijamii,..mumesikia mtanzania kafungwa huko nchi za nje,…na tujue ukweli
kuwa,.. sio kila kitu unachokiona kipo kama kilivyo,tusiwe wepesi wa kutoa
taarifa zetu zote,..au kuandika mambo kwa pupa, tuelewe tunachokifanya na faida
na hasara zake, kabla ya kuandika au kuweka picha, na zaidi,…tusikurupuke,
kutamani, kwani sio kila king’aacho ni
dhahabu
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment