Tulifika
kwenye shughuli hiyo, tukakaribishwa kama wageni rasmi, na utambulisho wetu
uliwafanya watu washangilie, tulielezewa kama wapiganaji tuliojitoa mhanga
kuhakikisha tatizo hilo limekwisha, na mzee akasema akazidi kusheneza kwa
kusema;
‘Siwezi
kumlaumu yoyote kwa hili, mimi naliona kama mtihani katika maisha yangu na
familia yangu, mimi sikujua ni nini kilitokea huko nyuma halikadhalika mke
wangu,lakini niseme neno,…hivi tukiamua kila lililofanyika huko nyuma tuwe
tunalipizana kisasi kweli kutakuwa na usalama…, basi tufike mahali tusema
yaliyopita si ndwele tugange yajayo..’
‘Kwa
wale tuliwakosea, tunawaomba sana msamaha, mtusamehe ….maana bila wao
kutusamehe hatutakuwa na radhi mbele ya mungu, na sisi tumewasamehe wale wote tuliowakosea
tukijua kuwa mwanadamu ana mapungufu yake mengi, kama mwanadamu, hatuwezii kuwa
wakamilifu abadana.
Nitumie
fursa hiii kuwashukuru sana wote, na nitakuwa mkosefu wa fadhila,kama
sitwashukuru kipekee docta na msaidizi wake, wao wanakuwa ni sehenu ya familia,
kwa jinsi walivyojitolea kupambana na hili jambo…mungu atawalipa zaidi kwenye
maisha yao.
Kiukweli…,
wapo wengi wa kushururu..wapo askari polisi wamefanya kazi kubwa sana na wote
walihusika kwa namna moja au nyingine wote hao tunawashukuru sana…’akaongea na
mke wake naye akaongea, akaomba msamaha kwa hayo yaliyowahi kutendwa na kizazi
chao, akasema hayo yalikuwa huko, lakini kwa vile imefika hadi kwao, basi yeye
anaomba msamaha kwa niaba ya wazee wake.
Baadae
docta akapewa nafasi ya kuongea, na kabla hajaongea, akachukua mfuko, aliokuja
nao,…
‘Ndugu
zanguni,…mimi sio mrithi wa hivi vitu,..kuna vitu hapa ni mali ya hii familia,
vitu hivi vimetumika kama kichocheo tu, ..ndivyo dunia ilivyo, watu wana chuki
zao, wengine wana visasi vyao, wengine wan hula zao za shari tu, …na wengi wao hawataki
kuyaonyesha hayo matatizo yao bayana, wanatumia miavuli fulani, kama
kisingizio..
Ukichukulia
mfano wa hili tatizo, waliotenda haya, wanadai, kuwa familia yao,… mama yao
alidhulumiwa, ni sawa ilitokea hivyo, huko nyuma,…hayo yameongewa mahakamani,
lakini tujiulize walidhulumiwa na nani,..je huyo aliyefanya hivyo yupo,
..hayupo, kwanini tuiumizeni familia nyingine ambayo haihusiki,..tinafanya
makosa, inabidi kila mtu aubebe mzigo wake mwenyewe.
‘Hao watu, walikuja kutumia vifaa hivi vitatu
kama sababu, kwanini walitumia hivyo,..ni njia ya kuficha maovu yao, ..binadamu
wengine hurithi ubaya, wengine huja kuiga, wengine, wanatafuta upenyo
tu..tujiulize yote haya matokeo yake ni nini, je baada ya kufanikisha hayo, kama
utafanikiwa utaishi mielele, ..
‘Ndugu
zanguni, tusitafute uchochoro wa kuonyesha hisia zetu, tusitumie visingizio hata
vya imani zetu, kuonyesha makucha yetu, ikawa ni visingizio vya kutenda uhalifu
kwa watu wasio na hatua mungu hatakuwa radhi na sisi, na hatuwezi kufanikiwa
kamwe, na mwisho wake ni fedheha tu.
Ama
baada ya kuyasema haya, nitumie fursa hii kuvikabidhi hivi vifaa kwa wenyewe,
wenyewe wanajua ni vitu gani,..na nini cha kuvifanya, ila, kama nilivyosema
tusichukue mambo ya kurithi, ikawa ndio sababu ya kutekeleza matakwa yetu, tukatumia
kama visingizio vya kukidhi tamaa za nafsi zetu, muhimu kwa jambo lolote hebu
kwanza tulifanyie utafiti tuone faida na hasara zake, tujiulize kwanza je sisi
wenyewe tukitendewa hivyo itatufurahisha,…
‘Hivi
vifaa vinatakiwa vikabidhiwe kwa mama wa hii familia, yeye ndiye mrithi wa
asili na yeye ndiye anayeweza kuamua lipi lifanyike kwa vifaa hivyo, wengine
wakiamua kufanya lolote kwa vifaa hivi, wakiwa wanafahamu masharti yake, wata[ata
shida sana, ndio maana wenzetu wakaamua kutumia njia ngumu ya kufanya makafara
ya kumwaga damu za watu wasio kuwa na hatia…
Haitakiwi
kuwakabidhi watoto kwa hivi sasa wakati mzazi wao ambaye ni mmoja wa warithi
bado yupo, .. ‘akasema akiwageukia kuwaangalia hao mabint wawili.
‘Hao
wenzetu, wao waliamua kuwatumia watoto moja kwa moja, baada ya kujua kuwa
wakiamua kuwatumia wazazi, hawatafanikiwa kwa haraka, nayo ilihitajia makafara
pia, ni shidaa…
‘Kwahiyo
huyu mama ndiye sasa atakuwa na mamlaka ya hivi vitu, na akishavipokea, yeye
ndio atakuwa na uhuru wa kuwakabidhi watoto wake, akitaka, au kuviuza..au..atajua
mwenyewe…’akageuka kumuangalia huyo mama.
‘Natoa
kama angalizo tu..linaweza kufuatwa au kuachwa, maana mimi sina mamlaka
hayo,..hivi vitu ni nyeti sana kuliko watu wanavyofikiria, ni vya hatari sana
kama vitafika mikononi mwa watu wenye tamaa mbaya, kama, ilivyotokea kwenye
hilo kundi haramu, hapo bado walikuwa hawajavimilikisha kabisa…, mungu
awasamehe madhambi yao, maana, kama wangevimiliki wakafanikiwa …muda huu tungeliongelea
mengine, kwahiyo vitu kama hivi,...mimi sijui, ngoja tumsikilize mama, ambaye ndiye mrithi halali
atasemaje..
‘Tafadhali
mama mrithi,….’akasema docta akimuashiria huyo mama, na huyo mama akasimama,
kwanza akainama kidogo kwa mume wake, kama kumuomba radhi, au ruhusa ya
kusimama na kuchukua jukumu hilo, na mume wake akatikisa kichwa kuashiria kuwa
amekubali…
Mama
Mrithi akasogea pale alipokuwa kasimama docta, na docta akachukua ule mfuko, na
kuwa kama anamkabidhi huyo mama, huyo mama akawa kama anasita kidogo, na docta,
akavaa kinga za mikononi, na kutoa kifaa kimoja, akamuonyesha na cha pili
akamuonyesha halafu akaukung’uta ule mfuko, kuashiria kuwa hakuna kitu kingine,
ndipo yule mama akaupokea,…lakini kabla ya kuupokea, kwanza akamuomba mungu
ampe kinga, halafu, akasema;
‘Kwangu
mimi, kama nilivyokataa kupokea kikombe cha wazee…watu wanaita mikoba.., na
hiki pia mimi sikipokei, kwasababu gani, haya yaliyovifanya hivi vitu, sijui
undani wake, na je nitawezaje kufanya hayo waliyokuwa wakiyafanya wao wakati
sikuwahi kufundishwa au kuona wakifanya…lakini kwa vile kwa hali ilivyo inabidi
nivipokee, ili sije ikawa kama alivyosema,….docta, vikaingia kwenye mikono
yenye tamaa mbaya..’akatulia.
‘Nawaombeni
watoto wangu mje hapa …’akasema akiangalia pale walipokuwa wamekaa mabinti zake,
watu waliokuwemo wakawa wanawaangalia hao mabinti, wakikumbuki hayo
waliyofanyiwa, hasa huyo mkubwa,
‘Hawa
ni watoto wangu, hii ni sehemu ya familia yangu, sitamuita baba yao kwanza,
maana haya mambo yana masharti yake, nisingelipenda mume wangu mpendwa
akaingizwa kwenye mambo yasiyomuhusu,…kama ni kudhurika, nidhurike mimi
mwenyewe..’akasema, na kila mtu akawa na hamu kujua ni kitu gani huyo mama
anataka kukifanya.
Mabinti
wale wawili wakafike pale mbele, na mama yao akawa anawanong’oneza jambo, na
wao wakatikisa kichwa kukubali,.. baadae yule mdogo, akatoka kidogo, aliporudi
alikuwa kaandamana na mtu akiwa kabeba pipa kubwa, ni aina yamapipa maalumu ya
kuchomea taka-taka, na huyo mtu akalitua lile pipa,..
Yule
mama akamuomba mungu wake akaomba kinga kutoka kwa mola wake kwa hili
alilokusudia kulifanya, na kuomba radhi, kama atakuwa amekosea, lakini yeye
kwake ameona ndio njia sahihi, na kama kuna madhara yoyote basi yampate yeye
mwenyewe, kwa maamuzi hayo…
Alipomaliza
kuomba hivyo, akageuka kumuangalia mume wake, na mume wake akatikisa kichwa
kukubali, ..wenyewe walivyoangaliana walijuana ni nini wanachongea.
Akaingiza
mkono kwenye ule mfuko na kutoa kifaa kimoja wapo akasema;
‘Hii
hapa ni bastola, hii ni ishara ya nguvu, mamlaka, na dhamana ya kulinda utawala
aliokabidhiwa kiongozi na raia zake...ndivyo ilivyokuwa dhamira ya
watengenezaji, hivi vifaa kwa jinsi nijuavyo mimi, lakini ina upande wake wa
pili, ni ishara ya umwagaji damu, vita, mabavu na udikiteta duniani,…’akatulia.
Ni
kwanini ikawa na sehemu mbili, ni kwasababu utawala, ni mtihani, na mtawala
anapimwa kwa hekima zake, sasa yeye akiwa muadilifu, anayewajali raia wake,
hataweza kugeuza upande mbaya, atasimamia upande wa uadilifu, hekima, ..na
kuwaongoza raia wake, kwa mujibu wa sheria,..kinyume chake akipatikana mtawala
mbaya, basi atatumia upande wa pili, ili aogopewe, huu upande wa pili kasimama
shetani..nisingelipenda kuuelezea upande huu zaidi, maana ukiuelezea sana wale
wenye vichwa dhaifu huingiwa na hamasa nao…
Sasa
mimi kama marithi halali wa hiki kifaa.., kwangu mimi nasema iwe mwisho, na
dunia iwe na amani,utawala, na mamlaka yake yarudi kwa raia wenyewe, wao ndio
wakuamua ni nani mtawala wao, na wala usiwe ni utawala wa kurithiana tena, …’ akachukua
ile bastola, akaiangalia, na kwa haraka
akaitumbukiza kwenye pia,…na yule mtu aliyeleta hilo pipa alijua ni nini
cha kufanya.
Akawasha
pembeni mwa lile pipa, na kukasikika mngurumo, kuashiria inafanya kazi, na
haikupita muda,…akaashiria kwa kichwa kuwa tayari…akafunua, kukatokea
moshi,..ulipotulia, akainamisha lile pipa ili watu waone, hakukuwa na kitu
tena, kile kifaa kilikuwa kimeteketea kabisa.Yule mama akatoa kifaa kingine
kwenye mfuko, hiki kilikuwa kidogo tu, akakishika mkononi.
‘Na
hiki hapa,pamoja na udogo wake, ni kikubwa sana kwa matendo yake hasa katika
dunia hii ya sasa,…huu..ni ufungua unaweza kufungua kifungo chochote, ikiwemo,
nyumba, mitambo inayolindwa kwa kutumia mitandao, akiwemo mitandao yenyewe..’akatulia.
‘Ina
maana gani, ina maana hata uweke neno gani la siri, hiki kifaa kinafungua, hii
ni ishara ya pia kwa kiongozi muadilifu kuwa umepewa nchi, na nchi hiyo ina
mipaka, ina masharti, mila na desturi zake, ina mali asili ina mali za watu, na
watu wake, basi wewe funga nyumba hiyo..maana nchi ni mfano wa nyumba yako na
familia yako, uhakikishe umefunga kila kitu ili nchi iwe salama… ukitumia alama
ya ufunguo huu.
Ama
kwa upande wake wa pili, ndio huo utapeli, wenzako wamezalisha, wenzako
wamehifadhi vitu vyao, wewe unatumia kifaa kama hiki kupakenyua maisha ya
wenzako, unaiba mali za wenzako, una-dhuluma,..huko ni kubaya hata kuelezea.
Sasa
mimi kama mrithi halali wa hiki, nasema huu uwe ni mwisho, kila mwenye siri
yake abakie na siri yake….na kila mwenye mali yake halali abakie na mali
yake…na kila mwenye ujuzi wake, autumie ujuzi wake kwake yeye kwa manufaa yake
yeye, na akitaka awasaidie na wengine lakini iwe kwa ridhaa yake,…’akatulia.
Mimi
kama mrithi halali, nakiharibu hiki kifaa kwa manufaa ya vizazi vyetu ambavyo
kwa hivi kwa mfano, wametawaliwa na mitandao, ..wanaweza kuangamizwa kama hiki
kifaa kitaingia kwenye mikono mibaya, watu watatumia hiyo mitandao, na kuweka,
mashetani ndani yake..msiona hii mitandao, mkafikiri ina mema yote..hapana,
kuna mangapi mabaya yapo humo…kizazi kitaharibika kisipojua madhara
yake..mapicha mabaya, yenye kuathiri akili za vizazi vyetu, hii ni moja ya kazi
ya shetani..mungu atulindie vizazi vyetu..
Kwa
haraka akakitumbukiza ule ufungua kwenye pipa, na gesi ikawashwa na kufanya
kazi yake, ilichukua muda kidogo, kuliko ile ya kwanza, kuashiria kuwa kifaa
hicho kina nguvu sana,..na hatimaye kikaharibiwa kabisa..
Alipomaliza
hivyo, akageuka kumuangalia docta, na docta akageuka kumuangalia mzee wa
familia, …na mzee wa familia akasimama.
‘Najua
ni kwanini watu hawa wananiangalia mimi, …hahah, je nikikataa, eti jamani, mimi
nimepewa hivyo vitu kama zawadi, hajalishi masharti yake,…lakini mm, docta
kanishtua, kasema ukijua masharti yake ukakaa nacho,…utapata madhara, na mimi
naogopa hayo madhara, hasa kwa familia yangu.
Ninacho
kifaa chao kimoja,..nilipewa kama zawadi nikiwa jeshini..na sikupewa kifaa
kimoja tu, nilipewa vifaa viwili, ile bastola na hivi viatu…’akaninama na
kuvivua viatu alivuyokuwa kavivaa…na kuendelea kusema;
‘Kiukweli,
kiatu na bastola, nilikaidhiwa mimi kama zawadi..na nisingelijua asili yake
ningeliendelea kuvimiliki..lakini sioni umuhimu wake kwangu, hasa ukiangalia
upande wa pili yake…naona sasa nikiwakilisha kifaa hiki kwa wahusika, na
wenyewe watajua jinsi gani ya kufanya..akasogea pale na kumkabidhi mke wake
hivyo viatu.
Mama
alifanya hivyo, kama vingine…akisema
‘Nasikia
kifaa hiki enzi hizo, mfalme, aliweza kuruka nacho usiku kukagua miliki yake,
kuhakikisha hakuna madhara …kwa ufupi kifaa hiki kinawakilisha usafiri, miundo
mbinu ya namna hiyo…na mengineo, ila kwa upande wa pili, kinawakilisha nguvu za
giza,…’akatulia.
‘Najua
umeshasikia watu wanatembea na ungo…basi kazi ya kifaa hiki kwa upande mbaya
ndio hiyo,.. kifaa hiki usiku unaweza ukaruka nacho, ukafanya mambo yasiyompendezesha
mungu, humo kuna shetani, . ..aah ni hivyo tu, nisiseme mengi..akaviangalia
vile viatu, ni vizuri kwakweli …‘free
size’..
Akakitumbukiza
kwenye pipa,…mpaka vikaharibika kabisa,.. na ikawa ni mwisho wa hivyo vifaa vya
ajabu,..na mwishowe shughuli hiyo kukaendelea shughuli nyingine za kisherehe,
na mpaka ikafikia mwisho wa shughuli hiyo.
************
Baadae,
wakati tunajiandaa kuondoka, mara docta akaitwa ndani, ..nilijua ni kwanini,
docta alifanya kazi hiyo kwa makubaliano ya kuja kulipwa, kwahiyo ilibidi
wakutane na familia hiyo waone watalipana vipi,..mimi sikupenda kuwepo,
nikamuacha docta akaenda peke yake.
Wakati
docta anaongea na hiyo familia mimi
nikatoka nje ya hilo eneo, nikawa napunga upepo,…nikiwaza mambo yangu, maana
binadamu mawazo ni kawaida, sikutaka kuwazia sana maisha ya mbele, …na mara
nikahisi kuna mtu anakuja nyuma yangu, sikuataka kugeuka, nilijua ni docta.
‘Shemeji,..samahani…nilikuwa
nakutafuta huko ndani, kumbe uko huku, oh…’akasema na mimi niliposikia hivyo,
tena nikiitwa shemeji, akili ikaanza kuwaza mengi, namuda huo akawa ameshafika
pale nilipokuwa nimekaa, sikugeuka kumuangalia, akasema;
‘Kwanza
nikushukuruni sana,..kwa hayo mliyotufanyia, tunashindwa hata la kusema, mungu
mwenyewe ndiye atawalipa, ..na pia, aheri nimekuona peke yako, ili nitumie
fursa hii kukuomba unisamehe..’sauti hiyo ilinifanya nigeuka kwa haraka,,
kwanza hiyo kauli,sauti..
‘Mhh,
kwanza nikuuliza kwanini unaniita shemeji..’nikasema kama nauliza
‘Kwani
wewe sio shemeji yangu, najua, na nilijua ipo siku..mungu atawaunganisha wewe
na dada, najua hayo yaliyotokea ilikuwa ni ..mitihani tu..su sio, au kuna
mengine usije ukawa umeshampata mwingine,…niambie ukweli…’akasema
‘Unajua,
hayo unayozungumza, shemeji, ..ilikuwa zamani, sasa hivi, huwezi jua, ..kwangu
mimi, aah, siwezi kukudanganya, sijaweza kuwa na mtu..nipo kama
nilivyo…’nikasema
‘Mambo
si hayo…’akasema.
‘Sikiliza
kwnza…’nikataka kuendelea kusema akanikatisha kwa kusema;
‘Sio
sikiliza mimi namfahamu sana dada yangu anakupenda sana, na hata baada ya hayo
yote bado anakupenda, ..lakini hawezi kukuambia hilo, ..tulikuwa tumetoka na
ndada nje, tukawa tunaongea,…’akatulia.
‘Sawa…’nikasema
‘Na
nikatoka pale nikikutafuta kule ndani sikujua upo huku nje,..’akasema
‘Unitafute
kwa dhumuni gani labda..?’ nikamuuliza.
‘Nilitaka
utumie nafasi hii, uongee na dada, muyamalize, kwa hivi sasa hajui kuwa
nimekuja kukutafuta, ..ila kwanza uniambie ukweli wako kutoka moyoni, ..kama
una mtu wako mwingine unitamkie hapa, na mimi nitajua jinsi gani ya kumalizana
na dada, uwe muwazi, je unamtaka mpenzi wako wa facebook, au dada,…niamini..kwani
sitaki mtu aje kumuumiza dada yangu tena..’akasema.
‘Eti
mpenzi wangu wa facebook,ni nani kakuambia hilo, huyo mtu hayupo, ni geresha
zao hao watu..…haaah,…je una uhakika kuwa dada yako atanisamehe..?’ nikamuuliza.
‘Kwani
ulimkosea nini…?’ akaniuliza hivyo.
‘Oh,
si ndivyo hata wewe uliwahi kusema hivyo..kuwa mimi ni chanzo cha hayo yote
au…’nikasema.
‘Nilisema
vile, …kwa vile sikujua,… sasa nimeujua ukweli…, hata familia yangu sasa ipo
radhi na wewe… hata walipogundua kuwa wewe ulifumwa ukiwa na msichana mwingine,
na ndio ikamuathiri dada…’akasema
‘Lakini
mimi sasa sijawa tayari kuishi na mke, sina mbele wala nyuma, nimefirisika,
nipo-nipo tu..nahitajia muda w kujijenga tena..kwa mfano kwa hivi sasa naishi
kwa mgongo wa docta…’akasema.
‘Hilo
la kuishi mtaishije, lisikutia shaka,labda uniambie ukweli kuwa akili yako bado
inamuwaza huyo mpenzi wa facebook, ama kwa dada,… mimi namafahamu sana dada
yangu kuna kipindi nilimuuliza je akimpata mume asiye na kitu akampenda
itakuwaje, unajua aliniambia nini..?’ akaniuliza.
‘Sijui
labda uniambie wewe..’nikasema.
‘Alisema
hivi, yeye hajali mali, kwasababu mali ni majaliwa ya mungu unaweza kumpata
mume mwenye mali akafirisika, au mali hiyo ikawa sio ya halali, ..lakini ukimpata
mume mwenye upendo wa kweli hiyo ni mali tosha, haifirisiki, na ni halali hadi
mwisho wa maisha yenu, na mume kama huyo mnaweza kujipanga mkajijenga na kufika
mbali zaidi, maana ana upendo wa kweli…’akatulia kidogo.
‘Kiukweli....nilipenda
maneno hayo ya dada…’akasema.
‘Kwahiyo
hata wewe upo tayari kuolewa na mume yoyote, ilimradi umempenda, mkapendana..?’
nikamuuliza
‘Usiniulize
ya kwangu, mimi nipo hapa kwa jili ya dada na wewe, na mpenzi wako wa facebook…’akasema.
‘Oh…hata
sijui nisemeje, unajua naogopa hata kuja kuongea na dada yako nahis nilimkosea
sana,…aah, haya, niambie, maana kama hilo litafanikiwa, sijui nitakushukuruje..’nikasema
na hapo akasogea na kunyosha mkono, sikujua ana maana gani, nikatulia.
‘Nataka
unishike mkono, kwa ishara ya ahadi..kuwa kweli utampenda dada yangu,
utamlinda, mtakuwa naye kwa shida na raha…au kama moyo wako upo kwa mpenzi wa
facebook, basi, hata huyo …sio mbaya, …’akasema na mimi kwanza nikasita, lakini
baadae nikanyosha mikono yangu, ikaishika mikono yake,..nilipomuachia, akaruka
juu na kusema.
‘Yeesss…’kwa
nguvu sana, nikabakia nimeshangaa sikujua kabisa kuwa hilo lipo moyoni kwa huyu
msichana, nilimuangalia alivyofurahi na mimi sasa nikaingiwa na shauku ya
kukutana na huyo dada yake.
‘Kwani
yupo wapi huyo dada yako..?’ nikamuuliza, na akaniashiria kwa mkono kuwa yupo
upande wa pili wa nyumba, halafu akasema;
‘Nenda
..nenda…ila usichelewe ataondoka, nimemuambia nakwenda kuchukua soda ndani …
mkimalizana naye utakuwa na jibu muafaka ….ni nani umpendaye…’akasema na
kuondoka, na mimi nikatembea kuelekea hiyo sehemu, niliyoelekezwa, nikafika
pale alipokaa, alikuwa kainama, kashika
simu, hakujua ni nani anakuja.
‘Na
wewe bwana, …maana yake ni nini kunigandisha hapa nje muda wote huo, hizo soda
ulikwenda kununua dukani,..mimi leo nataka kwenda kulala mapema, sitaki
kusumbuliwa..umeshaleta, umeifungua kabisa..’akauliza na mimi nikakaa kimia.
‘Ndio
kawaida yako..mimi sitaki mzaha hapa,...hata sitaki tena kuendelea kukaa huku nje...mimi nakwenda zangu ndani, …’akasema na aliposimama mimi nikajitokeza, uso kwa uso,…nikajikuta
nashikwa na mshtuko mkubwa, maana aliyekuwa kasimama mbele yangu sio mwingine,
ni yule mpenzi wa facebook…
NB:
Haya naambie...naona imekuwa ndefu sana sehemu hii, nitamalizie sehemu ijayo, tuachane na kisa hiki.
WAZO LA LEO: Kutoa , kusaidia
wengine ni mtihani, mtu anajiuliza hivi mimi mwenyewe maisha ndio haya ya kuunga
unga, nitatoaje hiki kidogo, kumsaidia mtu mwingine....Tunasahau kuwa mpaji ni
muumba wetu, na aliposema utoe usaidie wengine ana maana yake, kutoa huko
inaweza ikawa ni sababu ya wewe kubarikiwa zaidi, …tukumbuke kuwa mkono utoao
ndio unaopokea.
Kwa
waumini wa dini ya kiislamu, tukumbue kutoa zakatul fitry.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment