‘Ehee,
wewe ndiye nakutafuta kwasasa, nashukuru umeniletea kitu muhimu sana kwangu,
japokuwa vingine bado sijavipata hawa washenzi wameshindwa kazi, lakini nitavipata
hivi karibuni, kwako wewe nataka hicho ulichovaa mguuni mwako…’akasema
akimuangalia mdada mguuni.
Mdada
akainama kidogo kujikagua, kabla hajainua uso, akawa keshavamiwa na kuinuliwa
juu kwa juu.
‘Nataka
hivi viatu, unasikia, baada ya kuvipata hivi viatu…, sidhani kama utakuwa na
faida kwangu…mwenye faida kwangu ni dada yako…na sheria na utaratibu wangu
utafuatwa, nitahakikisha, unabakia huku huku kuzimu..ukiwa miongoni mwa mizimu,
unasikia…’jamaa akawa anaongea huku akiendelea kumzungusha mdada hewani.
Mdada
hakujua ni kwanini anafanya hivyo, kumzunguisha hewani, badala ya kumvua viatu,
yeye akaendelea kuziba mdomo na pua,…akichelea huo moshi usije kumuingia, moshi
ulikuwa sio mwingi sana, lakini alishajua madhara yake, alipomuona huyo
msaidizi wa mtandao, alivyofanywa na huo moshi!
Wakati
bado anamzungusha hewani mara wakaingia askari, wakiwa na silaha, wakawa
wanamuelekezea.
Huyo
jamaa hakusituka, alichofanya, kwanza ni kumweka mdada chini, halafu kwa haraka
sana, akawa kama ananyosha mikono juu, na kwenye koti lake sehemu ya viwiko vya
mikono, kulitokea vibomba viwili, vikatoa moshi…na kwa haraka akawa kaam
anakunja mikono mara mbili, kikatokea kibomba kingine cha ziada kikawa kinatoa
moto…
Ule
moshi, ukageuka kuwa moshi wa moto, ukaanza kuungiza vile vifaa walivyovaa
askari, ni kitendo cha haraka sana, hata askari hawakupata muda wa kujihami, na
mara askari hao wakadondoka sakafuni na kazimia…
Mdada
kwa muda ule alikuwa anarudi kinyume nyume, kutafuta upenyo wa kukimbia, na
alipoupata tu…akageuka na kuanza kukimbia…
‘Simama,
nitakumaliza kwa risasi…’huyo jamaa akasema lakini mdada hakusimama, akawa
anakimbia kama anapaa…hata mdada mwenyewe alishangaa kwa jinsi alivyokuwa
akipaa hewani, kwani vile viatu vilikuwa
kama vinampaisha,akiinua mguu, anarushwa kwenda hewani…mbio mbio, na kutokezea
sehemu ya ukumbi mwingine ambao ulikuwa umapangishwa na watu wengine.
Hapo
akasimama, kwa mbali akamuona jamaa akimtafuta,….hakutaka kupoteza muda,
akaanza kukimbia kuelekea nje ya jengo, na mara akajikuta uso kwa uso na Mkuu…
‘Wewe
ulifuata nini huku…mbona mnatupa wakati mgumu kutekeleza majukumu yetu..?’ mkuu
akamuuliza
‘Nilikuja
kumfuata dada yangu…’akasema
‘Dada
yako, dada yako yupi….?’ Akauliza
‘Ndio
bado yupo hai..lakini huyo shetani kanizuia…’akasema
‘Shetani
gani huyo..?’ akauliza
‘Huyo
mkuu wao, manenda huko eeh, haya nendeni mkafe, kama hamjitaki…mimi huko sirudi
tena,…’mdada akasema akigeuka nyuma kwa mashaka.
‘Nenda
kakae kwenye lile gari pale,….’akaambiwa
‘Hapana
mimi narudi nyumbani…’akasema sasa akiangalia usawa wa kupata bajaji, na mkuu
msaidizi hakumzuia, …
****************
Mzee
na mkewe walifika nyumbani, na wakaanza kuongea, maana huko njiani hawakuweza
kuongea, kwa vile walikuwa kwenye gari la askari, ambalo lilitakiwa kuwafikisha
hapo nyumbani, na ulinzi mkubwa uliwekwa kwenye nyumba yao.
‘Hivi
ulimuelewa binti yako…’akasema mzee
‘Kuhusu
nini,kuwa huyo dada yake yupo hai…?’ akauliza mama.
‘Ndio…nahisi
bado akili yake haijamkaa sawa…’akasema mzee
‘Akili
yake ipo sawa, sio yeye tu aliyewahi kusema hivyo,..hata huyo kiongozi wao,
aliniambia hivyo,…’akasema
‘Ukamuamini,
hujui kuwa alikuambia hivyo ili kukuteka mawazo yako…’akasema
‘Aaah,
hata sijui,….kama yupo hai tutampata tu, ilimradi wawakamate hao watu, maana
sitakuwa na amani mpaka nisikie wote wamekamatwa, hasa hao watu wawili wakubwa
zao....nasikia mzee , kafariki, maana huyo naye,..mmh, hata siamini kuwa nay
eye alikuwa miongoni mwa hilo kundi…’akasema mama.
‘Kwanini
usijue na wewe ulikuwa mwanachama…?’ akauliza mumewe
‘Ina
maana hujaniamini..mimi niliingizwa kichwa kichwa kwa ajili ya kuwapata hao
mabinti, lakini mambo yao ya ndani mengi nilikuwa siyajui…nimeipata hiyo
taarifa wakati wananiachia huko gerezani, nikasema kama alikuwa miongoni mwao,
afadhali iwe hivyo….’akasema mke
‘Basi
sasa nimesikia…maiti yake ilikuwa haishikiki…ilioza kwa siku moja…’akasema mzee.
‘Alikuambia
nani..?’ akauliza
‘Kuna
docta mmoja aliyekuwa akishughulia maiti yake…’akasema
‘Ndio
watu waone, jinsi gani wachawi wanavyoadhibiwa hapa hapa duniani, unajua wakati
wanafanya mambo yao wao hujisahau wakajiona wataishi milele, kumbe ipo siku
watarejea kwa mola hakimu wa mahakimu,..…’akasema mama.
‘Huyo
docta anasema wakati wanakwenda kumchukua, walipompima, awali kabisa, walimuona
hajakara roho, lakini mwili umeshaanza kuoza,
alikuja kukata roho baadae, na wanasema kwa hali aliyokuwa nayo, alikuwa
anapata maumivu makali sana…’akasema.
‘Hata
sitaki kumuwazia, maana siwezi kuamini mtu tuliishi naye vyema, alikuwa kama
ndugu yetu , halafu anakuja kutufanyia hivyo, siwezi hata kuamini..’akasema mke.
‘Halafu
sikiliza sasa, kutokana na hali yake, walitaka kumzika haraka haraka,..maana
sio kumzika tena, ni kumfukia,….nasikia hata kaburini lake, lilikuwa na vituko,
kwani waliposhusha kaburini tu….wakiwa wamemuweka madawa makali ya kupunguza
harufu, lakini harufu ya uozo, ilikuwa haiishi..na wakati wanaanza kumfukia,
mara kutokea nyoka kutoka aridhini wakamzunguka,….’akasema
‘Oh,
watu hawajakimbia…?’ akauliza mke
‘Walifukia
kwa haraka haraka wakaondoka, hakuna aliyetaka hata kukaa humo zaidi…’akasema
‘Mungu,
kweli adhabu ya dhalimu, huanzia hapa hapa duniani…’akasema mama
‘Sasa
hawa watoto, maana mimi nimeshaanza kusema watoto, kama vile kweli huyo binti
yetu mkubwa bado yupo hai…’akasema
‘Yupo
hai bwana…’akasema mama, na mara mlango ukagongwa
‘Ni
nani huyo tena, ni askari au ni mgeni..?’ akauliza mama
‘Ngoja
niwapigie simu askari tuwe na uhakika, …
‘Fungua
ni mimi mama, ni mimi baba…’sauti ya kike ikasikika nje.
*********************
Mkuu
akaanza kuwasiliana na watu wake wa ndani lakini hakupata jibu, na mara docta
akampigia simu.
‘Vijana
wangu hawapatikani..’akamwambia docta
‘Wamelishwa
moshi wa huyo jamaa, kama nilivyokuambia wawe makini sana na huyo mtu, ukasema
wamevaa kinga, hizo kinga hazifui dafu na huo moshi wa moto wa huyo jamaa, na
kwasasa ….mkichelewa hamtamuona tena huyo mtu, …’akasema
‘Kwani
kwasasa hivi yupo wapi..?’ akauliza mkuu msaidizi
‘Anarudi
ndani, nahisi anataka kumfuata msaidizi wangu, au bado anamtafuta mdada, binti
wa mzee….’akasema docta
‘Wa
nini…?’ akauliza
‘Wa
nini, kwani kilichomleta humo unafikiri ni nini, yeye anamtaka huyo binti,
awakutanishena msaidizi wangu, ..wakati akiwa keshavipata hivyo vifaa
vitatu,,..akimali hilo basi hatawezekana tena…’akasema
‘Sasa
atavipataje na wewe unavyo huko?’ akauliza
‘Kuna
mzindiko yao walitarajia watayafanya, lakini huyo jamaa hajui kuwa
nimeshayamaliza nguvu, kama mzee angelikuwa hai angeliweza kumsaidia,,lakini
kafanya haraka kumua, msadizi wake wa nguvu za giza.
‘Oh,
sasa unafikiri atafanyaje..?’ akauliza
‘Zaidi
ni kutumia nguvu, lakini hana ujanaj kwa hizi sasa, muhimu ni kujitahidi kuwa
mbali naye hadi tumtege kiaina..’akasema docta.
‘Kwahiyo unataka tufanye nini huku, maana sisi
tulitaka tumuingilie tumshike…’akasema.
‘Mtamshikaje,
huoni, ilivyotokea kwa askari wako, hapo hajataka kuwamaliza angelitaka
angewaua wote…’akasema docta.
‘Kuna
mbinu nyingi za kumkamata, sema nakusikiliza wewe kwa sasa…’akasema huyo mkuu
msaidizi.
‘Ni
kumtega tu….tumsubirie akiingia kumfuata huyo kiongozi, basi tutafunga
mlango,..tatizo ni kuwa askari watakao kuwa humo wanaweza kuuwawa…’akasema
‘Siwezi
kuruhusu askari wangu wauwawe….kama ni hatari kihivyo ni bora tutumie nguvu.
‘Mkuu
ukutumia nguvu, hutafanikiwa, ushahidi wote wa harakati hizi utapotea, na huyo
jamaa ni mjanja, akitoka nje, hutampata tena…naonelea mimi nije huko, najua
jinsi gani ya kuzi-zimisha nguvuu za giza za huyo jamaa.
‘Lakini
ukija huku sisi tutapataje taarifa za ujumla, wewe ukiwa huko ndio unatuona mbashara
kila mtu na katika sehemu tofauti tofauti…’akasema mkuu msaidizi.
‘Usijali,
kazi iliyobakia sasa ni ndogo, muhimu kwasasa wasiliana na muendesha mashitaka
muambie kazi imekamilika, awasiliane na hakimu , kesi hii ifanyike haraka
iwezekanavyo, …’akasema.
‘Hakimu
aliyekuwa akisimimia hii kesi kapatwa na dharura, ..kasafiri, labda tuombe
hakimu mwingine…’akasema.
‘Itakuwa
vyema, …hakimu yule wa kwanza ataikwamisha hii kesi, hakikisha unampata hakimu
mwenye msimamo, maana kesi hii imegubikwa na sintofahamu nyingi…’akasema docta.
‘Hilo
litafanyika, nawasiliane naye tukimaliza mawasiliano na wewe…’akasema.
‘Sawa
vinginevyo, hawa watu watayeyuka na hatutaweza kuwapata tena, na hii inaweza
kuleta balaa kubwa baadae,…’akasema.
‘Kwanini
watayeyuka….sioni ni kwanini tukiwamakata wanakwenda jela kwenye mikono yetu
hawawezi kutoroka tena…’akasema.
‘Mkuu,
haya mambo yasikie tu, hawa watu ni wajanja sana, na daa yao ni hiyo usiwape
muda,..kesi ifanyike haraka iwezekanavyo,..maelezo zaidi ….utayapata huko huko..kwa
hivi sasa siwezi kukupa jibu la uhakika, tusipoteze muda, wewe unaweza kuendelea
na vijana wako, ila wasifanye haraka kutumia nguvu…mimi nakuja huko huko…’akasema
docta.
‘Na
huyo binti wa mzee,…tutamfanyaje…maana askari wanasema bado hajiwezi, anahitajiak
huduma za haraka….kwanini tusimuwahishe hospitalini?’ akauliza huyo mkuu.
‘Huyo
atapona tu,… tiba yake sio ya hospitalini, hapo alipo kalegezwa na madawa ya
mzee marehemu…’akasema docta.
‘Kama
ni madawa ya huyo mzee marehemu, ataponaje na wakati huyomzee mwenyewe hayupo
duniani tena…?’ akauliza
‘Ndio
maana nataka kuja huko..’akasema docta
‘Ok,
sawa ngoja nifanye ulichoagiza…nina hamu sana ya kukutana na hao watu wawili ,
wamenisumbua sana akili yangu, najua wapo wengi, lakini yeye atakuwa ni funzo
kwa wengine wote…’akasema mkuu msaidizi.
‘Ni
kweli,… utakutana nao tu mkuu,…, hutaamini macho yako…’akasema docta,na kukata
mawasiliano
**************
Msaidizi wa docta, akachukua leso yake,
akaziba mdomo na puani, huku sasa akiukimbia ule moshi, ulikuwa kama
unamkimbiza, alipofika mbele akaona mlango wa chumba ukifunguka, nay eye bila
kujiuliza akaingia kwenye hicho chumba ule moshi, ukapita..yeye akafunga mlango….na
wakati anajiuliza;
Mara
akashtuka mtu anamshika begani, akageuka kwa haraka, akakutana uso kwa uso na
askari.
‘Usijali
upo mahali salama….nimepewa taarifa unakuja..pole na majanga…’askari akasema,
na msaidizi akageuka na kuwaona askari kama watano wapo humo ndani, na pembeni
alikuwepo yule kiongozi aliyekamatwa awali, aliyeweza kupata bastola na ufunguo
kwake, ..na jamaa alimuangalia kwa macho yaliyojaa hasira,
Akakumbuka
jinsi gani alivyoweza kumshinda ujanja huyu jamaa…na kuvichukua hivyo vitu kwa
kirahisi akimuacha akikamatwa na polisi….hakutaka kuliwazia hilo sana, akageuka
na kusema kimoyo moyo;
‘Oh..hii maana yake ni nini…’akatulia kwa muda.
Wakati
yupo na hao askari humo ndani, ndio wazo likamjia, akaamua kuwasha simu yake,
ambayo muda mwingia alikuwa kazima, ilipowaka tu, akakutana na mlio wa siku
anapigiwa,..
‘Wewe
hebu zima simu yako….’akasema askari mmojawapo.
‘Oh,
samahani napokea taarifa muhimu kutoka kwa docta na mkuu msaidizi…’akasema na
yule askari kabakia kimia…
‘Docta
hapa….sasa fanya hivi …rudi pale ulipotoka, kamuokoe mpelelezi, kabla
hajavamiwa na hao watu, kuna wasaidizi wameitwa wa huyo jamaa kuja kumkomboa
kiongozi wao,yeye mwenyewe anaonekana hataki kujionyesha, kajificha kwenye
chumba kimojawapo, hakikisha ukienda kumchukua mpelelezi uwe umeziba mdomo na
pua..’akaambiwa
‘Kwanini
wasiifanye hiyo kazi hawa maaskari
‘Sina
uhakika nao, wewe fanya nilichokuambia, nina maana yangu…’akaambiwa na msaidizi
hakupoteza muda, akatoka mle,..askari hawakumzuia inaonekana walishaambiwa
wamruhusu atoke..
Haraka
haraka msaidizi, akatoka mle, hakukuwa na moshi tena, akarudi kule, na kweli
alimkuta mpelelezi kalala sakafuni, akamshika, ..akajitahidi mpaka akamuweka begani,
akaanza kutoka naye, kwa haraka hadi kule kwenye chumba alichokuwa awali..na
alipofika tu, docta akampigia simu
‘Sasa
chukua huo unga kidogo aliokupa huyo mzee, mpake puani…’akaambiwa akafanya
hivyo, na mara mpelelezi akazindukana,…
‘Kuna
nini…’mpelelezi akauliza
‘Mapambano
yameanza, …’akasema msaidizi na mpelelezi, kwa haraka akasimama na kujinyosha, akageuka
kuwaangalia maaskari waliokuwemo, nahisi alitaka kuwamba silaha, lakini
akajizuia
Simu
ikapigwa tena alikuwa ni docta
akamwambia,…
‘Sasa
jitahidini mtoke hapo, waacheni hao askari, wataendelea kufanya yao, sisi
hatuingiliani na wao, …mkitoka hapo, tembeeni hatua chache, karibu na chumba
mlipokuwa awali, mkifika hapo, nitawafungulia chumba, mtaingia humo, na humo
mtapata maelekezo zaidi,fanyeni haraka kidogo, kabla hao watu walioitwa
hawajaingia huko.,…’akasema.
‘Sawa bosi…’akasema msaidizi, yeye na
mpelelezi wakatoka na kunza kurejea kule walipokuwa awali, na kabla hawajasogea
hatua chache…, mara kwa mbele wakaona askari wakija.
‘Hawa
wanaonekana kama sio askari…’akasema msaidizi, na mpelelezi, akaguna kwanza
halafu akasema;
‘Ni
kweli, hawa watakuwa watu wao wamevaa sare za usalama…sasa hapa hatuna muda wa
kupoteza tugeuka turudi kwa haraka…’akasema mpelelezi.
Wale
watu waliovalia ki-askari walipowaona hawa watu wawili wakaanza kuwafuata,
ikawa sasa kazi ya mpelelezi na msaidizi kurudi mbio, hadi chumba kile
walipotokea, walipofika tu mlango ukafunguliwa wakaingia.
‘Mnakuja
kuvamiwa…’wakasema , kuwaambia askari waliokuwemo humo ndani.
Askari
wakajiweka tayari, na mara docta akapiga simu,…
‘Ni
kweli hao sio askari, ni watu wa huyo jamaa, mumefanya vyema kukimbia kurudi ,
sasa ni kazi ya hao askari kupambana nao,…sasa wewe fanya hivi, kwenye hicho
kichupa chenya unga mwekundu ulichopewa, nenda kampake huyo kiongozi wao,aliyeshikiliwa
na polisi, fanya haraka,..’akaambiwa, na msaidizi akafanya hivyo.
Alipomsogelea
huyo jamaa, alikuwa kafungwa imara kabisa, na alipomuonamsaidizi anakuja akiwa
kashikilia kichupa , akajua ni nini anafanyiwa, akainamisha kichwa kuficha uso
wake, lakini akisaidiwa na askari akainualiwa uso, na alipopakwa huo unga
puani, akalegea,… na kupoteza fahamu.
Docta,
akasema,
‘Kwahivi
sasa huyo sio tishio kwenu kwa muda,…ni mtu hatari sana huyo akipata mwanya, na
ilivyo, anatakiwa kufikishwa mahakamani akiwa hivyo hivyo…’
Huko
nje kukawa kunasikika milioa ya risasi,na haikupita muda, askari wakaja na
kusema,
‘Tumeshawamaliza,..iliyobakia,
sasa ni kumtoa huyu mtu hapa ndani…’akasema kiongozi wa kundi hilo linalomlinda
huyo mshukuwa ambaye alikuwa kiongozi wa shughuli nyingi za hilo kundi.
‘Wasimtoe
mpaka nifike..’docta akasema kwenye simu akiongea na msaidizi na msaidizi
akamuambia mpelelezi.
Mpelelezi
akasogea mbele ya huyo jamaa na kusema;
‘Huyu
mtu hatoki hapa kwa hivi sasa.
‘Kwanini…mnazuia..?’
akauliza askari mmojawapo
‘Afande
huyu ni lazima tumtoe humu, ni hatari akiendelea kukaa humu ndani,..’akasema
‘Nimesema
huyu hatoki humu, …nieleweni hivyo..’akasema mpelelezi na kukawa na kubishana
fulani hivi hadi mkuu alipopiga simu, kuwa huyo mtu asitolewe humo ndani.
Na
haikupita muda, kiongozi wa kikosi hicho cha humo ndani akaamriwa atoke
akaonane na mkuu….alionekana kakasirika, lakini amri ya mkuu ni moja, …
‘Huyu
atakuwa ni kibaraka…’akasema msaidizi wa docta
‘Wapo
wengi…’akasema mpelelezi
‘Unawafahamu…?’
akauliza msaidizi
‘Sio
rahisi kuwafahamu, watu hawa wana mtindo wa kuhakikisha watu walichukuliwa
kwenye usalama, hawajuani…ni siri ya mtu mwenyewe…’akasema
‘Kwanini
sasa umekuja huku na wewe bado unaumwa…?’ akaulizwa
‘Ninataka
kusafisha jina langu, ..najua sitaeleweka, lakini nilifanya mengi kwa masilahi
ya familia yangu, nikakiuka amri za kazi yangu…’akasema
‘Mimi
sioni kosa lako, maana ulifanya kwa masihali ya familia, usingelifanya hivyo
familia yako ingedhurika, au sio…?’ akasema msaidizi.
‘Kwako
wewe hulioni hilo kosa, lakini ndani ya sheria za kazi yetu ni kosa kubwa, kuna
makosa nimeyakiuka, na sizani kama itakuwa rahisi kwangu kusamehewa…’akasema
‘Usijali
, tutakusaidia,…’akasema msaidizi, na mara simu ikalia, alikuwa ni docta tena
‘Nimeshafika
nipo huku nje, …na namuona jamaa yao, anatoka kwenye kile chumba sasa hivi
kavalia kama askari, keshajua kuwa kazungukwa, sasa muwe makini sana…nilitaka
mfike kwa mdada lakini haitawezekana kwasasa.
‘Sasa
tufanyeje,…?’ akauliza.
‘Nakuja
huko huko ndani, TUMALIZE KAZI….’akasema docta kwa kujiamini kabisa.
NB:
Tutamalizia sehemu ijayo... kama hitimisho la kisa hiki!
WAZO LA LEO: Mtu anapokalia kiti
cha dhuluma, hujisahau akaona yeye ni yeye tu, na watu kama hawa ukiwagusa
wanasema ‘Unajua mimi ni nani…’ mimi ni nani maana keshajitolesha kuwa yeye ni
juu ya sheria, lakini wapi , hata siku moja dhuluma haidumu,…
Jamani
tusijisahau kihivyo, hata kama tunazo, tunautawala, au sisi ni mabosi kwenye
ofisi, tukaanza kuwanyanyasa wenzetu , tukawadhuluma wengine haki zao, kwa kutumia ubosi wetu...
Hala hala ndugu bosi...kumbuka hili,...hata kama utafanikiwa sasa hivi,
ukawanyamazisha hao wanyonge, ukafanya ulichofanya, ...wanyonge wakakosa haki yao, wewe ukaonekana bosi mwema, kwa
tajiri wako, hujashinda, maana huo sio mwisho wa dunia..., haki, ya mtu ipo pale pale…,
na mungu atairejesha kwa huyo mnyonge kwa namna ambayo huwezi kutegemea kabisa..na wewe utalipwa mabaya kutokana na dhuluma yako hiyo, wangapi wangapi tumewaona.... Tumuombe mungu
atulinde, na atuongoze kwenye njia sahihi, anayoirizia yeye mwenyewe,…Aamin.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment