Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Saturday, June 10, 2017

MPENZI WA FACEBOOK-48



‘Ni nini hicho…?’ akauliza mdada baada ya kuona alama nyekundu ikitokea kwenye komputa na ikifuatiwa na herufi nyingi zilizojipanga kwa pamoja, hadi zikaajaa kwenye uso wa hiyo komputa..,

‘Ni ishara ya hatari…’akasema huyo jamaa akihangaika kudonoa batani za haiyo komputa ilikuwa ni desk top…, lakini pamoja na utaalamu wake haikuwezekana kufany alolote,…akaishia kusema;.

‘Hatari, hatari..hatari….mungu wangu ….’akasema hivyo na kushika kichwa

‘Hatari gani hiyo…..?’ mdada akauliza mdada, naye akihisi mashaka, akilini mwake isije ikawa ni bomu likaja kulipuka na kuwamaliza wote humo ndani, hakuwa na mawazo mabaya mengine,.. na jamaa sasa akijaribu hata kuzima komputa huku akisema;

‘Mtandao, umekula mzinga,…hapa sina ujanja tena,….umeharibika kabisa…oh, sasa hili ni balaa jingine, hawa jamaa sijui kama watanielewa….’akasema

‘Kwani ni kosa lako, si utawaambi ukweli ulivyo….’akasema mdada.

‘Wewe huwajui hawa watu, wao wanajua kuwa mtu hakosei, ..na hata sio kwamba nimekosea mimi, hii ni virus, imetumwa na…, najua huyu atakuwa ni docta tu, …’akasema

‘Docta, docta atahusikanaje na hilo tatizo, msimsingizie mtu wa watu,…hayo ni mambo yenu mabaya, sasa yanaaza kuwarudia wenyewe…’akasema mdada.

‘Oh, sasa nitafanya nini, na huyu bosi akisikia hivi, na..unaona hii alama hapa,…sasa hii ni hatari, na kiongozi hayupo, …mtaalamu ndiye alikuwa anaweza kupambana na hawa watawala wa hili kundi,…sasa mimi nitasema nini….’akatulia akiangalia alama nyingine ya kama kitaa chekundu, inawaka na kuzimika.

‘Mh….jamaa huyo …keshaingia ndani ya ….jengo, ..unaiona hii, hii ndio alama ya huyo bosi mkubwa, ikialika hivi, ujue yupo karibu, na sio karibu, yupo humu ndani,…’akasema

‘Itakuwa afadhali na mimi nimuone, huyo shetani, na nikikutana naye, sijui..ataniambia wapi dada yangu alipo, na kwanini walimfanyia hivyo,na kwanini wanaifuata fuata familia yangu…aje mimi nipo tayari kukutana naye..’akasema mdada

‘Mungu wangu, wewe dada wewe, hapa ni kuomba tu, dua yako ya mwisho, ilivyo, huyu mtu akikutana nawe, hataki uje umkumbuke, ina maana akija kwako, akimalizana na wewe anakuacha ukiwa maiti…haonekani ovyo ovyo kikazi, …’akasema

‘Kwani yeye, mungu, yeye ni malaika mtoa roho, acheni imani zenu za kishetani…’akasema mdada.

‘Hata sijui nikuambieje..unaona, ni kama anakuja huku….haonekani, anaonekana kwa alama hii,..yupo,na sio mbali..anakuja huku..huyu, oh, sasa mdada, mimi sikai hapa tena…’jamaa akasema akijaribu kusimama, akaanguka, alikuwa kasahau kuwa kafungwa miguu..

‘Unataka kwenda wapi….?’ Mdada akamuuliza akimsaidia kusimama

‘Wewe tuondoke hapa, ..huyu mtu akiingia humu, sizani kama atatuacha hai,….’akasema

‘Usiogope mimi nitapambana naye, na isitoshe, polisi wapo, watamkamata ….’akasema mdada

‘Hawa polisi wenu, hahaha..nisiseme mengi, unajua, hapa walikuwa wakimuogopa mpelelezi, huyo mpelelezi akaja kuwekwa sawa, …akaja huyo msaidizi wa mkuu, …nay eye utasikia, vumbi lake, anajifanya haingiliki, wamesha muanza kwenye familia yake..’akasema

‘Kwa vipi…?’ akauliza

‘Utamuuliza mwenyewe….’akasema akijaribu kujifungua hizo kamba, na mdada hakutaka kumzuia, akawa anamuangalia tu.

‘Dada tafadhali, hii alama inaashiria kuwa huyu jamaa anakuja huku…mimi nakuomba sana unisaidie,…tuondoke hapa, haraka…’akasema, na akageuka kuangalia mlangoni na mdada naye akageuka kuangalia huko……

Tuendelee na kisa chetu
**************


Wakati huo huo mzee na msaidizi wa docta walikuwa wakikodoa macho kuangalia mlangoni, wakisubiria hicho kitakachoingia, ….na mzee akawa anahangaika, ni kama vile mtu anahisi pumzi kumuishia mwilini, …

‘Mzee vipi una nini…?’ akauliza msaidizi.

‘Jamaa akanitupia kombora…ooh,,,kokoko..oohhh…’akawa anahangaika kuzuia kitu , ni kama kameza kitu anajaribu kukitoa lakini hawezi.

‘Kakutupia saa ngapi, na kwanini afanye hivyo, wakati anataka kuonana na wewe ili muweze kufanya mambo yenu….’akasema

‘Si-s-jui kwanini anafanya hivi, nahisi haniamini tena….’akaweza kuongea lakini sasa akawa anatoa jasho jingi,

‘Sasa mzee tufanyeje, maana mimi siwezani na mambo yenu ya kishirikina..?’ akauliza lakini mzee alikuwa kimia akitoa jicho kama vile kaona kitu cha kutisha mbele yake, kijana aangalia huko anapoangalia mzee, lakini yeye hakuona kitu.

‘Mzee, sema..sema kitu nikusaidie, …’akasema, na mara wakasikia sauti ya mtu anatembea kuja muelekeo wa mlangoni, lakini kukatulia hakuonekana mtu, ..ila baada kidogo, kukaanza kuonekana dalili ya moshi…ulianza kidogo kidogo sasa ukawa unakuja kwa kasi.

‘Wewe una leso…?’ akauliza

‘Leso…leso ni moja ya nguo zangu siwezi kutembea bila leso,…!?’ akauliza msaidizi n akuongeza maneno hayo

‘Ziba mdomo wako na pua, hakikisha hufungui, huo moshi ukiingia ndani ya mwili wako unapoteza fahamu, …’mzee akasema na yeye akaziba mdomo wake kwa shida, maana mikono ilikuwa ikimtetemeka…na msaidizi akafanya hivyo hivyo,…ule moshi, ukaanza kutulia kidogo kidogo baadae ukaisha.

Mzee akiwa bado anatetemeka mikono, akatoa vitu ..ilikuwa vichupa viwili vyenye unga unga ndani yake..akatoa unge kwenye kichupa kimojawapo na kumuambia msaidizi, paka hii puani…

‘Hapana mzee, sijawa tayari na mambo yenu, mpaka mtimize masharti yangu…’akasema

‘Paka hii puani, na machoni…sasa hivi hakuna muda tena na mambo hayo, huyu mtu kaja kwa shari, ..keshanichokoza, nataka hizo sumu zake zisikuathiri na wewe…’akasema akihema kwa shida, na msaidizi akafanya hivyo kwa kusita sita, akajipaka, na baadae akauliza..

‘Hivi huyo ni nani, mpaka umuogope hivyo..?’akauliza

‘Ni mwenyewe, yeye hutumia moshi kuzimisha watu…’akasema

‘Oh, kwahiyo…keshafika au sio, safi kabisa huyo huyo ndiye wakumkamata atuambie mdada yupo wapi, la sivyo tunawaita polisi….’akasema.

‘Polisi..hahaha..hivi hujanielewa…sikiliza nikuambie kitu, usitamani kukutana na huyo mtu, ni bora uonekane muogoa, sas ahivi kaja kama yeye, akiwa huko duniani, aah, ni mwema sana,..mimi sijawahi kukutana naye uso kwa uso,..labda akiwa huko duniani, maana huko huwezi kujua yeye ni nani…’akasema.

‘Una maana gani huko duniani, kwani sisi tupo wapi…?’ akauliza.

‘Hahaha..kohokohokoho…aah,….’mzee akawa anakohoa kwa shida, na ikaonekana damu zikitoka mdomoni.

‘Mzee upo sawa kweli, unahitajika ukamuone docta….tutoke hapa, utakufa mzee….’akasema.

‘Tumeshachelewa hapa,..sina dawa ya kunisaidia, ningelikuwa kwangu, huko duniani, ningeliweza kujisaidia, hapa,..hata mizimu imekaa kimia,..nahisi imenisusa, nimeshindwa kutimiza makafara yao..’akasema.

‘Sasa mbona haji…’akasema msaidizi, na mzee akainua uso kumuangalia , uso ulishabadilika,macho yameshabadilika, ..yanatisha..hadi msaidizi akasogea nyuma

‘Mbona umekuwa hivyo, kama shetani….’akasema na mzee akawa kimia.

‘Hawezi kuja hapa kwasasa hivi anajua huku keshamaliza kazi, nahisi sasa hivi anakwenda kwenye mitambo, kuhakikisha kila kitu kipo sawa, …atahakikisha kaharibu kila kitu ili kuondoa ushahidi, au kuna kitu muhimu kakigundua ambacho ni cha maana zaidi ya sisi hapa…..’akasema.

‘Kama nini..kaona nini….?’ Akauliza.

‘Siwezi kujua, labda..kati ya vile vitu vitatu, au yule binti ambaye ni muhimu sana kwake, wewe atakufuata baadae, ….’akasema.

‘Binti gani, huyo ambaye alikuwa marehemu,…safi kabisa,.. kama ni yeye mzee huoni kuwa atatusaidia, akija hapa mimi nitajificha,a kitokeza tu, namvamia kwa nyuma, unaonaje hiyo plani..usiogope mzee, upo kijana ngangari..mimi sasa hivi nina miaka,..ooh, mzee, ishirini tisa…ningelishaoa zamani, lakini ndio hivyo tena.

‘Na-nakujua sana, ni zaidi ya hiyo miaka…sa-sa hatuna mu-da…’mzee akawa anaongea kwa shida..
‘Mzee twende ama tutoke humu, au twende tukapambane tumuokoe binti mikononi mw huyu shetani,…naona na wewe …unatisha mzee, sura imekua kama sio yako….’akasema.

‘Sikiliza kijana sasa sio muda wa kunibishia, nataka nikuokoe kwenye hili janga, najua huko mbele utakuja kunikumbuka na kuniombea, najua nimefanya mengi mabaya, lakini hata zuri moja jamani..haaa, naona wahenga wananiita…unawaona wale….’akasema mzee akiashiria kwa kichwa na msaidizi akaangalia hakuona kitu.

‘Mzee, vipi mbona unaanza kunitisha, mimi sioni kitu …nahisi mwili unasisimuka tu..nywele zinanisimama.

‘Si umesema wewe huogopi…’mzee akasema.

‘Aaah, ni kuhusu afya yako mzee, kwangu usijali..nakuogopea wewe, ila nahis mwili unanisisimuka, ni kama kuna kibaridi fulani hivi….’akasema.

‘Na mimi najalimaisha yako kwa sasa…sasa hivi, sina mdua, sikiliza,…unaona hicho kinapita hapo,…’akasema mzee akiashiria kwa kichwa.

‘Mbona sioni kitu mzee…’akasema akiangalia huku na kule.

‘Sawa subiria utakiona …hicho hicho….ndio yeye, kapita, anaelekea huko juu, nahisi anajua keshatuzimisha, na kwa vile hana umuhimu na sisi kwasasa ndio maana kapita, ila akirudi, atahakikisha kanimaliza na wewe atakuchukua…’akasema.

‘Oh, sasa mambo gani, kwahiyo unasemaje, maana mimi sasa nachoka, lengo letu halijatimia, haya huyo mshenzi keshafika, ..na huyo, nikikutana naye mzee, mimi simpi muda, …chochote nitakachookota ni saizi yake, ..humu ndani kuna nini…’msaidizi akasema akigeuka huku na kule, akaona chuma …ilikuwa nondo fupi iliyokatwa.

‘Sasa mzee mimi nina silaha sema tufanyaje…tutoke nje ukatibiwe au tukapambane kiume..mimi sijali, …kama kufa, tutakufa tu, lakini tusikubali,…tupambane kiume..’akasema msaidizi.

‘Kijana, kijana,…hapa silaha ni nguvu za giza, mwenzko huyo atakuwahi hata kabla hujamkaribia, uliuona huo moshi, akiupilizia…, kama anataka kuku-ua mara moja,anauwasha moto, ..sasa ule moshi unakujia huku unawaka moto…ukikuingia unaunguza vitu vyote ndani ya mwili wako…’akasema.

‘Hatari…’msaidizi akasema, ni kama vile haamini, na mzee akatikisa kichwa, kusikitika, akasema.

‘Kijana…hujui upo wapi, hujui hatari gani ipo mbele yako, upo upo tu, sawa, sio kosa lako, lakini sasa…sikiliza kwa makini, wewe si huogopi…’ mzee akauliza.

‘Kwanini niogope mzee, huo moshi, ukija wa moto, nitaiba mdomo, au sio nitamuomba mungu wa wote, atatulinda, kama siku imefika, basi mungu atupe mwisho mwema, ndio hivyo tu mzee kufa tutakufa sote, siku ikifika haina mjadala, ..ndio maisha ni mzuri, lakini hatuna mamlaka ya kuzuia kifo,..mimi nimeshaanza kuogopa kidogo..sijui kwanini…’akasema.

‘Sasa sikiliza lolote laweza kutokea, kwa hivi sasa …’akasema na akaanza kutoa vitu mfukoni, akatoa vichupa viwili,…

‘Hiki chenye unga mweupe, ni kwa ajili ya kumzindua yule mdada …tuliyekuja kumuona, amehamishwa hapa sijui kapelekwa wapi, nahisi huyo jamaa ndio anamtafuta,..akimpata atakuja kukuchukua na wewe..mimi sizani kama nitaweza kupambana naye tena, keshaniwahi….sasa sikiliza usiongee sana…’akasema alipooana msaidizi anataka kuongea.

‘Huyo mdada hataweza kuzindukana kwenye hiyo hali, ni mpaka umrushie huu unga, huku ukisema maneno haya….’akawa anaghani maneno , kama anaimba vile.

‘Hebu yarudie,….’akasema na msaidizi akayarudia yale maneno vile vile kama alivyokua akisema huyo mzee, uafikiri ndio huyo mzee anayaghani.

‘Safi kabisa, wewe una akili sana…ningelikuwa mzima, ningekufundisha mambo mengi, lakini sitaweza kuwa nawe tena…sikiliza kwa makini maagizo yangu haya, huyo mdada hataweza kuinuka mpaka umtupie huu unga na wakati unafanya hivyo, ughani hayo maneno, halafu umuombe mungu wako, unachokusidia, kwanza kuwa huyo mdada azindukane, halafu hilo lililo moyoni mwako, …muda ukiomba chochote unafanikiwa…’akatulia akichukua kichupa kingine.

‘Na hiki nyekundu rangi nyekundu,..ni silaha, akija adui yako mrushie usoni, ataishiwa nguvu atadondoka…na na- na-…’ mzee akashindwa kuendelea, akaanza kutetemeka.

‘Vipi mzee, ndio mziimu hiyo nini, ….’akasema msaidizi akishangaa kumuona mzee anatoa macho kweli kweli…

‘Si-si-s-kiliza..wewe ondoka hapa mara moja…., akikuona hapa atakuzidi na akivichukua hivyo vitu ndio basi tena….o-o-ndoka, haraka…’

‘Mzee, usiogope, mimi siwezi kufa kabla ya muda wangu…’alipomaliza kusema hivyo tu, yule mzee akadondoka, chini na mara akaanza kutoa mapofu mdomoni yakichanganyikana na damu,..akatikisika kwa muda halafu akawa kimia.

Msaidizi kuona vile,…akageuka kushoto na kulia, alipoona hakuna mtu, huyo akatoka nje,…mara anakutana na moshi,..unakuja kwa kasi, akakumbuka alivyoagizwa, haraka akaziba mdomo, huku anakimbia kukwepa ule moshi…..moshi ukawa unakuja kwa kasi kweli…
Akafika kwenye sehemu ina chumba,akakipiga teke kikafungua na kwa haraka akaingia humo na kufunga mlango, ..akatulia, na kabla hajakaa sawa akashikwa begani…

*************
Sasa huku alipo mdada…

Mlango ukafunguliwa…lakini hakutokea mtu mara moja, kulitangulia moshi…ukawa unatanda kuingia ndani, na mdada akakumbuka jambo, akachukua leso yake akaziba mdomo na …..ule moshi uliingia ndani kwa kasi, akageuka kumuambia huyo jamaa ajifunge mdomoni, lakini akawa kachelewa, ule moshi ukamuingia jamaa akaanza kukohoa na mara, akalala,…..kapoteza fahamu.

Mdada kule kuziba mdomo, na pua, pumzi inamuwia, shida, akaona ni bora  atoke mle, maana ukiwa ndani unaweza kufungua mlango kutoka nje..na mlango ulipofunguka tu,i anakutana na jamaa akiwa kavalia koti refu, usoni kajifunika,,,na kabla hajasema kitu, mdada akainuliwa hewani..kama katoto kwa huyo jamaa, mdada hakuachia pua na mdomo…

Na huyo jamaa akasema;

‘Wewe ndiye nakutafuta kwasasa…nataka hiki kitu…kimoja kwako, baada ya hili sitakuhitaji tena, na huhitajiki tena kwenye hii dunia…utabakia huku huku kuzimu..ukiwa miongoni mwao…’jamaa akawa akawa anaongea huku anamzungusha mdada hewani.

Mara wakaingia askari, wakiwa wameziba midomo yao kwa vifaa maalumu, mikononi wana silaha, jamaa kafanya mambo yake, ule moshi ukaanza kuwaka moto…ukawa uanunguza vile vifaa walivyo vaa hao maskari, na mmoja mmoja akawa anadonoka sakafuni kazimia…

NB: Naishia hapa kwa leo, wikiend njema.

WAZO LA LEO: Sisi wana-damu, ni wakosaji, tunafanya madhambi mengi tu, kwa hiari na mengine kutokana na mitihani tunajikuta tumeyafanya , ikiwa ni pamoja na kuwadhulumu wengine. Mtu anaweza kusema mimi sijamdhulumu mtu, lakini jiulize mambo haya, je hakuna haki ya mtu niliyowahi kuichukua, kwa kudanganya, au kwa namna ya kutaka kupata faida ukamwambia mtu hiki kitu ni kizuri, hakina tatizo lakini kumbe kina tatizo, ili tu upata faida,..hujapunguza kibaba, hujakopa na mpaka leo hujarudisha, au umekopesha kwa riba,  hujamuhadaa mdada, au mkaa ili ukidhi haja za matamanio ya nafsi yako, ukijua unadanganya,..yapo makosa mengi tu! Yote hayo ni dhuluma!.

Ndani ya mwezi huu, tumepewa nafasi ya kutubia madhambi yetu, tutubie kwa kiukweli toba ya kweli, ili iwe ni sehemu ya kujisafisha, na hata mwezi huu wa toba ukiisha tuwe kama nguo safi iliyotoka kufuliwa.

Tumuombe mola wetu atusamehe makosa yetu, na atuongoze njia iliyonyooka, Aamin
Ni mimi: emu-three

No comments :