Docta
alikuwa anamfuatilia mpelelezi na alipoona kafika kwenye huo mlango, akatumia
mbinu za kumsaidia, kwa kumfanya mtu wao..yaani, askari wa mkuu-msaidizi..ajifanye kama anatoka
nje, na alijua mpelelezi atachuku nafasi hiyo na kuingia ndani…
‘Ngoja
nione lengo la huyu jamaa, mpelelezi, nahisi kuna kitu anakifuatilia, ngoja
tumuone kitaalamu,…’akasema docta akiendelea kumfuatilia mpelelezi.
Mpelelezi,
alipoingia ndani, cha kwanza alichotaka kukifanya, ni kwenda kwenye kile chumba
alichowahi kumuona yule mdada, alipofika alishangaa kukikuta kipo wazi, kwa
tahadharai akaingia ndani na kuanza kukagua, kwanza kwa macho, pili kwa
vitendo, kwa kuchunguza sehemu zote kama anaweza kupata lolote la muhimu, na alipohakikisha kuwa hakuna kitu kinachoweza
kumsaidia, akageuka kutaka kuondoka, na mara akasikia watu wakiongea..
Sauti
hizo ziliashiria kuwa huenda watu hao wanataka kuja kwenye chumba hicho, na
yeye kwa haraka,akatafuta sehemu, akajificha, na kusubiria…
Haikuchukua
muda, mara hao watu wakaingia, kwanza walisimama mlangoni wakishangaa, halafu
wakaingia ndani…walikuwa watu wawili;
‘Yupo
wapi huyo mdada mwenyewe….’akauliza mtu wa kwanza, japokuwa walikuwa wamevalia
vito usoni vya kuficha sura yao, lakini mpelelezi akawagundua, ni akina
nani,…akasubiria kuona lengo lao ni nini;
‘Alikuwa
humu, huoni jinsi palivyowekwa vyema, maana huyo ni malikia, huyo ndiye , bila
yeye bado hivyo vitu visingeliweza kufanyakazi kama itakiwavyo..’akasema mzee
‘Sasa
yupo wapi, mzee, ….mimi naona una lako jambo, ….’akasema huyo anayeonekana ni
kijana, na huyo mzee akasema;
‘Subiri
kwanza,…..’mzee akasema na kupiga simu, nahisi alikuwa akiulizia
‘Vipi,
mtaalamu msaidizi, mbona vyumba vipo wazi, na hapa alipokuwa mdada, hakuna mtu,
mimi nilitakiwa kuja kumaliza kazi, sasa nitafanyaje kazi….eeh, unasema
haiwezekani, sasa itakuwaje…’akauliza na akawa anasikiliza
‘Hilo
halina shida…niamini, lakini hata vikipatikana, vitakuwa havina maana,…kwahiyo,
unasema, anakuja, ….ohooo, ngoja kwanza, mimi nijuavyo, anapokuja kukutana na
mtu fulani, mtu huyo, hataweza kumuona tena, ndio zake, sasa kama anakuja huku,
anakuja kuonana na nani..na mimi…haaa, kama hanijui, atajiua
sasa…tutaona,…maana bila mimi hakuna kitakachowezekana….’akasema
Baadae
mzee, akakata simu, na kuanza kuongea , hapo akasahau kuwa ana mtu ambaye
hakutaka afahamu undani wake;
‘Huyu
mtu najua,..kwa tamaa zake, anataka kunitumia, animalize, lakin sitakubali,
atajua kuwa kaingi anga za nani..haiwezekani, nimejitolea na kuhatarisha
maishayangu kwa ajili yao…huku wangekujuaje….sasa…kwanini lakini…’akashika
kichwa.
‘Mzee
kwani imekuwaje…’kijana akasema akimshangaa mzee, kwani alimuona uso
ukimbadilika ghafla, akawa mweusi
kupitiliza, na ikawa kama jasho linamtoka.
‘Sikiliza,
huyo jamaa anakuja yeye mwenyewe, sio kawaida yake, na huyo jamaa akija, ….kazi
yake ni kuua, yaani, mfano akija kwako, kwa vile hataki afahamike, akishamaliza
hicho alichokujia, wewe anakumaliza…ndio maana hadi leo hakuna anayemfahamu, hata
mmoja kati yetu…’akasema
‘Hata
huyo kiongozi aliyekamatwa, hamfahamu…?’ akauliza.
‘Huyo
yawezekana …anamfahamu lakini hata yeye anadai hamfahamu..’akasema
‘Na
uchawi wako umeshindwa kumfahamu yeye ni nani….?’ Akauliza
‘Utaalamu
wangu hauwezi kutambua hayo…huyo kakamilika,….anajigeuza kma kinyonga sio mtu
wa kawaida, ulaya anakwenda kama nyumbani kwake,….kiongozi anasafiri sana,
lakini huyo …kazidi…’akasema
‘Anasafiri
kwa hivi hivi au kwa uchawi wake…?’
‘Kwahivi
hivi, leo anaweza kusafiri kwa sura hii kesho nyingine, sio mtu wa kawaida,
mimi simuwezi, ndio maana namuogopa, vinginevyo, ..ningelishamaliza hii kazi
peke yangu…’akasema.
‘Kwahiyo
anakuja kuvichukua hivyo vitu, ..unitume mimi nivichukue halafu kwa ujinga wako
umkabidhi huyo mtu, mbona sikuelewi mzee, kama hivyo vitu vina faida, na unajua
kazi yake ni nini, kwanini umpatie huyo mtu, maana picha ninavyoiona hapa ni
kuwa, mimi utanituma, sijui kwa vipi, nitakwenda kuvileta hivyo vitu,
...mtaniua, hlafu ukishamkabidhi huyo mtu hivyo vitu, atakuua,na wewe,.’akasema
huyo kijana
‘Sikiliza,
sasa…nimeshajua la kufanya, wewe ..tufanye hivi, kabla hajafika, eeh,
tuhakikishe tumeshavipata hivyo vitu, tukishavipata akija tu, tunam-maliza,
unaonaje wazo langu…lakini haiwezekani, sio rahisi kwa huyo mtu, hapa tunaongea
anatusikiliza huko alipo…keshajiandaa…’akasema huyo mzee akiangalia huku na
kule.
‘Unajua
mzee, hilo wazo lako sio baya…, ila sasa, mimi siwezi kukubali kufanya huo
uchawi wako, kabla sijamuona huyo binti,..hilo ndilo lilikuwa sharti letu
muhimu,…kwanza nimuone huyo mdada, mengine hayo yatafuta baadae…si ndivyo
tlivyokubaliana,awali…’akasema kijana.
‘Sikiliza,
..niamini mimi, huyo mdada hajafa…’akasema
‘Sasa
yupo wapi..?’ akauliza
‘Katoka,..najua
hii ni kazi ya docta, kawashinda hao watu wa mitandao, akafungua milango yote,
na watu wote waliokuwa humu ndani wametoka,..walinzi na watu muhimu wote
wamekamatwa, ..ndio maana huyu ‘mkuu, ‘ kaamua kuja mwenyewe kumalizia kazi, na
atakachofanya …ohoo, sijui,….’akatulia
‘Atafanya
nini bwana,…mzee tusipoteze muda, huyo mdada tutampataje maana sijakuelewa hadi
hapo, kutoka kwetu huko ilikuwa ajenda ni hii, sasa umenihadaa, na mimi siwezi
kuendelea kukaa hapa ni lazima niondoke,…kabla huyo jamaa yako hajafika, …’akasema
‘Huwezi
kuondoka,…usijisumbue kwa hilo…..’akasema huyo mzee, na kijana akamuangalia
huyo mzee, hakusema neno hapo na huyo mzee, akasema
‘Ndio
maana nilihisi hali sio ya kawaida, mizimu ina jambo, lakini kwa hivi sasa
siwezi kuongea nayo, ni vigumu sana leo,..sijui nitafanya nini….’akatulia.
‘Sasa
kama unamfahamu huyo mtu, kuwa ni mbaya kihivyo, ni kwanini mnamuahangaikia
yey, ..eti aje kuchukua madaraka, nyie watu mpoje, kwanini usingelishirikiana
na polisi,…ukamaliza kazi, wewe si mtu wa serikali, kwanini ufanye mambo kama
haya, nikushauri kitu,…wakati ni huu, wakuonyesha sehemu yako ya pili ya
undamilakuwili,..’akasema kijana.
‘Kijana
chunga maneno yako..hunijui mimi…’mzee akasema
‘Nakujua
sana mzee, nimeshakujua wewe ni nani,…..nisingelikujua nisingelikubali kuja
hadi huku, wewe ni ndumilakuwili, msailiti…’akasema
‘Tatizo
lako hujui tu…hunijui, hujui kuwa mimi
naweza kuja usiku ukiwa umelala nikakufanyia mambo na hujui …’akasema
‘Sasa
unapata fadia gani, mimi si nimelala, ..fanya ufanyalo, …sijui, sina fahamu
hizo, wewe ndio unajisumbua,na mwisho wa siku utaangamia, makaburi yenu yatajaa
mijoko, mtakufa huku mnanuka, mtaoza mkiwa wazima…adhabu zeni ni nyingi sana,
sijui kwanini hamumuogopi mungu….’akasema kijana.
‘Tunamuogopa
sana, lakini hayo …ni mambo ya kurithi tu, na ukishaingia unakuwa huna ujanja
wa kutoka, kutoka kwake, labda ufe….’akasema.
‘Mzee,..tuspoteze
muda, …mimi nitakusaidia jambo moja, wewe si unavitaka hivyo vitu, sasa kwanza
ungekuwa umenihakikishia kuwa huyo mdada yupo hai, ningelifanya utakavyo,
uvipate hivyo vitu.., lakini sasa..kumbe unakwenda kuwatupia mbwa mwitu,….hata
sikuelewi…mzee, kwa mtaji huo sizani kama nitakuamini….’akaambiwa
‘Kijana
nilikuambiaje tokea awali, mimi nauma na kupulizia, nia ilikuwa kuwapata hawa
watu, nipate na kula yangu, nina maisha mazuri nyumba,..unaona, nikihiajai pesa
napewa, japokuwa ..oh, sina raha, ni maisha ya shida,..’akasema akionekana
mnyonge.
‘Hamna
akili ndio maana, kwanini ulikubali..’akasema.
‘Kijana,
wewe una akili sana, unajua hilo wazo…lakini anatusikia,…hilo la kusema eti
tushikiane na polisi, ni wazo zuri,…,lakini hivyo vitu,…mimi nimeshafungamana
navyo,visipopatikana na mimi nitakuwa matatani…nitaangamia,….ndio tatizo la
haya mambo…’akawa sasa akionyesha dhahiri kuwa keshaanza kuogopa
Kukasikika
sauti, kitu kama kimedondoka, wote wakatega sikio..
‘Umesikia
mzee, ndio mizimu hiyo….’kijana akasema akitega sikio.
‘Mhh…hiyo
sio mizimu, kuna kitu….’akasema huyo mzee akikagua kwa macho.
‘Hebu
kwanza nieleze ulivyofanya, …kuhusu mdada, na inatakiwaje..?’ akaulizwa kijana
akionyesha kutokujali , lakini mzee akawa anaendelea kutafiti kwa macho,
‘Nahisi
kuna mtu humu ndani…’mzee akasema.
‘Mzee
hakuna mtu,..wasiwasi wako tu, …hebu niambie, uliingiaje kwenye anga za hawa
watu….?’ Akaulizwa na mzee akamuangalia kijana, halafu akasema;
‘Mimi
ni mtaalamu wa mambo ya msukule, ..walinihitajia sana, kama nilivyokuambia
awali..nia yao, niwasaidie utaalamu huo, wachangenye na utaalamu wao wa
kidigitali kama walnavyouita, kwa ahadi kadha wa kadha..mimi nikaona hakuna
shida, maana walitega kwa mambo fulani fulani, nisipowasaidia, basi,
wataniumbua,…’akatulia
‘Wajanja
sana,mpaka mzee ukakubali kuwasaidia,…sawa kwahiyo ukawasaidia nini hasa,
kuwafundisha tu huo utaalamu, au kuna mambo mlikuwa mnafanya na wao,…?’
akauliza.
‘Kuwasaidia
sio jambo dogo, kulihitajika kila mara wakitaka kufanya jambo lao linalohitajia
mambo yangu wananiita, kama wanataka labda kuwapata maadui zao au kuna watu muhimu
wanaowahitajia,basi wananiita, napata mapesa mengi tu, lakini unajua tena
mapesa yao ni kishetani, unapata leo keshi huna kitu….’akasema
‘Na
wewe ndio uliwasaidia kuhusu hivyo vitu…?’ akauliza
‘Hivyo
vitu…ndio, bila ya mimi wasingelijua wpi vilipokuwa, bila ya mimi wasingelijua
nhivyo vitu vinatakiwaje, vifanyiwe nini,…nimewasaidia sana, lakini tatizo hawa
watu hawana rafiki wa kudumu, ukifikia muda hawakutaki wanakumaliza….nio sera
yako!’akasema kwa sauti ya chini.
‘Aaah,
mimi sijaelewa jinsi gani ulivyofanya hadi ukaligundua hilo, wapi vilivyo, na
vifanyweje…’akasema huyo kijana.
‘Mambo
ya giza..hayo, siwezi kukuelezea ukaelewa,…ila mimi niliweza kuipata historia
yote ya hivyo vitu…ni mambo ya kale sana, lakini mpaka sasa yanafuata mkono wa
kizazi husika, nikawaelezea namna itakiwavyo…na awali, ilikuwa hivyo vifaa
vifike kwa mama wa huyo binti,..kufauta mila zake, yeye akivishika, anamkabidhi
huyo binti yake..hivyo ndivyo ilitakiwa awali…sasa mimi nikafanya mambo ya na
mizimu…tukabadili badili wee, lakini kwa makafara makali…’akatulia
‘Makafara
ya kuua watu…au si ndio hivyo?’ akauliza
‘Inabidi…mambo
hayo , sio mchezo..niliwaambia lakini, hawakusikia, nia yao ni kuhakikisha
hivyo vitu vinapatikana, hawakujali tena maisha ya watu…, unaona humu ndani,
hiki chumba ndipo nilikabidhiwa kila kitu, na ..hata sisi kufika hapa,…
ilipangwa na mambo yote yangelimazikia humu ndani kama mambo yangeenda vizuri, mdada
akiwepo, na wewe ungeliletwa hapa na kazi ingelimalizika…docta ndiye kaharibu,
huyu docta huyu…ole wake…’akachuchumaa.
‘Sasa
mzee, jiamini, wewe si kigagula,…manachukua watu usiku, mna..wafanya nini sijui
wanaonekana wamekufa kumbe bado…hilo siamini,…labda kidogo nimuone huyo mdada, akiwa
hai, hapo nitaweza kukuamini…’akasema.
‘Tatizo
lako wewe, hujaamuka bado,…’akasema
‘Sasa
mzee, kwanini wakutishe watu wengine, nasikia nyie mnaweza kujigeuza
paka,..akija huyo jamaa akitaka kukuua, unajigeuza paka, au ni geresha zenu,…hahaha,
watu wengine bwana…’akasema kijana kama mzaha.
‘Unasema
nini, unajua wewe kijana, usitake tukaanza kukosana, sikiliza, wewe hujui
hatari iliyopo mbele yetu, humjui huyo mtu, hujui kabisa kinachokusubiria wewe,
na hata mimi .., ogopa, kukutana na huyo mtu…wengine wanamtania kwua ni
izraili,..maana akija kwako, unahesabu siku, …’akatulia.
‘Iziraili,
nyie watu mnakufuru sana….’akasema kijana.
‘Ndio
maana nasema wewe hujajua hatari iliyopo mbele yako…’akasema
‘Na
wewe je…..’akasema
‘Unasikia…’mzee
akatega sikio, akiwa makini kusikiliza
‘Mimi
sisikii kitu mzee, kuna nini, labda ni mizimu yako mzee, au…..?’ akauliza
‘Tutafuta
sehemu nyingine,..hapa tupo wazi sana, mtu akiingia mlangoni tutangulie kwanza
kumuona, na kujiandaa, ..na nahisi huyo
mtu keshaingia tayari ndani ya hili pango la kuzimu, ,..….’akasema huyo mzee, sasa
akimvuta huyo kijana ili wajifiche…
‘Mzee,
mungu ndiye wa kuogopwa, kama kufa kwa kupitia kwa huyo mtu,basi, mungu ndiye kapanga
hivyo, hilo halina mjadala,..mimi, mzee, simuogopi huyo mtu yoyote, wa
kunitishia maisha, namshukuru mungu kwa hilo, siogopi hata ukiwa kigagula,
unasikia, …muhimu nimpate huyo mdada, na wewe nakupatia vitu vyako hiyo ndio
dili, na huyo mtu akija, …polisi watapapambana naye, ..ni kitu kidogo tu mzee…kwanini
unaogopa…’akasema
‘Unajua
hata wakati nafanya kazi ya kukuzimisha wewe, nilipata shida, sana,..wewe na huyo binti
nyota zenu zina nguvu sana,…ilibidi tupata makafara mengi tu,.. lakini mimi
mtaalamu wa mambo hayo, hatimaye nilifanikiwa,,…sasa nashangaa unavyojinadi
hapa, kama ningelitaka kukumaliza…ilikuwa ni kazi rahisi tu, lakini mnahitajika
bado…’akasema mzee.
‘Msingeliweza
mpaka siku ifike mzee.., kama siku imefika,hakuna mwenye ujanja wa hilo, na hata
wewe kama siku yako imefika, basi ujue huyo jamaa akija anakumaliza tu, muhimu,
ni kujitahidi, nikushauri mzee, wangu, unajua tumezoeana sana, japokuwa
..kiukweli mimi siwapendi watu wa aina yenu,..washirikina,…siwapendi kabisa, lakini
kwa hili nitakusaidia, ilimradi tu, nimpate, ok, nimuone huyo binti ambaye
alikufa kimazingara yenu…’akasema.
‘Hahahahaha,
kijana, eti utanisaidia, kweli asiyejua ni kama mtu kwenye usiku wa giza,
unafikia kutamka hivyo kuwa utanisaidia mimi…hahaha, wewe unajua ni kitu gani
kinakuja mbele yako, we acha utani,..lakini ngoja nikuambie jambo,..mimi nataka
ukavichukua hivyo vitu, sasa hivi kabla huyo jamaa hajafika…’akasema.
‘Sasa
mzee kama wewe una uwezo huo kwanini unitume mimi si unakwenda wewe mwenyewe
unavichukua na kurudi tu….?’ Akauliza
‘Mtu
anayeweza kufanya hivyo…kuvichukua huko vilipo ni wewe , wewe uliyeweza
kuvichukua kutoka kwenye mikono ya yule mtu, ndio huyu huyo anayeweza kwenda
kuvichukua huku vilipo na kuvirejesha kwake..huyu auliyevichukua kwake,..kuna
masharti hapo,mwingine akifanya hivyo, sizani kama atafanikiwa…’akasema
‘Kwasababu
gani…?’ akauliza
‘Mazindiko
yake…tangia awali yameshavunjwa, na haitafanikiwa mpaka hayo …yaani wewe
ukavichukue, na kuvirejesha hapa…nikuambie kitu, hii ni siri, sikutakiwa
nikuambie,…wewe ndiwe uliyatakiwa ..umuoe huyo binti, na ukimuoa, yale makutano
yenu yanabariki ile nguvu ya vile vifaa, vikiwa mikononi mwenu…sikutakiwa
niwaambie hili mpaka uvilete kwanza…’akasema.
‘Sawa
mimi sina shida, kwa maana mimi sina umuhimu wa hivyo vitu… muhimu wangu mkubwa
ni huyo mdada, sasa nikuulize kitu, nyie,mnasema mlinifahmu mimi kabla,
mkanitafuta kwa nguvu za giza, …haiji akilini, maana aliyeniltea mimi huku ni
docta, huyu docta ni nani kwenu…’akauliza.
‘Docta..ni
msaliti tu…huyo achane naye, ..atajuta kuzaliwa, ila nguvu zilitumika ili wewe
uje, kuna mambo tulifanya yakutokee, hadi ukavutika..huko kote ulikuwa unazunguka
tu, tulikutafuta kwa kupitia mtandao, wa facebook, ndio tukaweza kukupata
..unajua kuna watu wana nguvu za asili za ulinzi wao,…wewe ni mmojawapo, lakini
hatimaye ukaingia kwenye himaya yetu..huyo msaliti ndio akaharibu…’akasema
‘Kwahiyo
docta mnamfahamu sana..?’ akauliza
‘Kumfahamu
ni baada ya kujitokeza,…mimi nilikuwa simjui…ila hawa watu walipomlisha kwenye
mtandao, wakamgundua kuwa yeye ni nani…kiasili ni mtu wa huku huku..yeye,
alitakiwa awe mshirika, …wa nguvu za giza, lakini alikataa, huko alipokuwa,
angelijiunga, angelikuwa na sisi, hata akiwa huko, si tunakutana…’akasema
‘Oh,
kwahiyo, …mimi najiuliza ni kwanini na yeye avitake hivyo vitu, wakati
anafahamu hana urithi navyo, au..?’ akauliza
‘Hatujui
dhamira yake ni nini, ,..nahisi na yeye kwa vile ana asili fulani na hivyo vitu,
yawez\ekana kagundua namna ya kuvifanya vifanye kazi, kwa kupitia utaalamu wake,
lakini kwa vyovyote vile, ili viweze kufanyakazi,ni lazima vipitie, kwa huyo
dada,akivipata huyo mume atakayemuona ndiye anaibeba ile nguvu yake, lakini sio
mume tu, inatakiwa awe na nyota kama ya kwako…nikuulize kitu, wewe docta
hajawahi kukuambia umuoe huyo
mdada,..najua atakuwa alikuambia hivyo…?’ akauliza.
‘Mdada
yupi sasa..? maana si wapo wawili….’akauliza
‘Kama
huyo wa kwanza alijua kuwa kafariki ni lazima alikushauri umuoe huyo mwingine,
je hajawahi kukuambi ukamuoa binti, wa huyo mzee, ?’ akauliza…na kijana
hakujibu kitu
‘Ndio
maana docta hataki kukuachia, na sisi hatutaki kumuachia huyo mdada…tunapambana
kwa nguvu za asili, na utaalamu wa kisasa…’akasema
‘Mnapambana
wewe na yeye au…?’ akaulizwa
‘Hapana,
wao..mimi sinimekuambia wamenialikatu…kwa ahadi kuwa akifanikiwa na mimi
nitawekezwa kwenye uongozi na masilahi…mimi ninawasaidia kuwaonyesha nguvu za
giza,kwa vile nazifahamu…kiukweli ninazo hizo nguvu,..kutoka kwa mababu, lakini
sihitaji sana hizo nguvu.., nafanya kwa vile mizimu inanitaka nifanye hayo, na
wakati mwingine ni lazima nitoe makafara , ..unajua, tuyaache hayo mazungmzo,
maana masikio yapo mengi, …’akasema
Kukapita
kitambo cha ukimia, na huyo mzee akasema;
‘Haya
mambo yakiisha salama, nitakufundisha kidogo haya mambo yalivyo….’akasema mzee.
‘Unataka
na mimi niwe mchawi, ..hapana mzee…mimi hapana, hayo ni yenu, mimi nitafanya
hicho mnachotaka tu , ili nimpate huyo
binti, basi..’akasema.
‘Hahaha,
…ushaingizwa baba,… huna jinsi, vinginevyo, mauti yatakuandama, ..ni mambo
machache tu, yakikamilika huna jinsi, …ila wewe, una bahati kuwa, bila wewe na
huyo binti haya mambo hayawezi kukaa sawa, ..ndio maana mpaka sasa mpo
hai..vingnevyo, ndugu yangu, …haaa, ..’akatulia akiangalia saa yake.
Mara
kukasikika sauti ya mtu anakuja
‘Nahisi
ndio huyo anakuja..’mzee akasema
NB:
Mazungumo ya huyu kijana na mzee, yamekuwa marefu, nia ni kufichua mambo mengi yaliyokuwa
na utata ndani yake, natumai sasa kila kitu kipo wazi.
WAZO
LA LEO: Inapotokea mtu na mtu mkasigishana ni vyema, mkavuta subira, badala ya kukimbilia kutukanana, na
kuanzisha zogo, hadi kupigana. Kwenye zogo na kutukanana, shetani anapata
mwanya wa kuweka vishawishi vya chuki,
na matokeo yake, wandugu, marafiki, jamii, zinafikia kukosana kabisa.
Wakati mwingine ni heri kwetu, kama mtu utajishusha, na hata kuonekane mjinga,
ilimradi mwisho wa siku mje kupatana,…ni ujasiri wa kuishinda nafsi, ili
kukwepa mfarakano, na visasi visivyoisha. Tumuombe mola wetu atupe subira, na
atujalie nafsi zetu zisijawe na hasira za haraka zenye kuleta migongano na
chuki kwenye mahusiano yetu, baina ya mtu na mtu.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment