Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, June 7, 2017

MPENZI WA FACEBOOK-45


‘Umekuja…nilijua utakuja tu, nilikuwa na kusubiria, …’sauti hiyo ilinishitua na kunifanya nisimame kwa haraka, na kwa haraka nikageuza kichwa kumtizam huyo mtu aliyeongea kutoak nyuma yangu….
Tuendelee na kisa chetu….

*************

Nilishtuka pale niliposikia sauti hiyo nyuma yangu, na haraka nikakumbuka kauli ya docta;

'Shetani hatakuweza kamwe..hata mchawi hakuwezi, kama nafsi yako utaijengea udhibit wa kuondoa hofu..hofu ndio silaha ya shetani,..na Ili shetani akuingie..au hata hata mchawi, akitaka kukuloga kitu cha kwanza anachokufanyia ni kukuingizia hofu, hofu ambayo, itakufanya uondokane na imani yako ya kumtegemea mungu.


Nilipoyawazia hayo, nikasema kwa ujasiri;


‘Ndio mzee…. nimekuja, nataka nikamuone huyo binti, uliyesema yupo hai....’ nikasema.


'Sawa kama upo tayar, ..hebu sogea pembeni,…ngoja nikuonyesha jinsi ya kufungua huu mlango wa kuzimu…’akasema na kuinama akagusa pembeni akawa kama anakandamiza, halafu akasimama,


‘Sasa unasukuma hivi…’akasukuma, na hiyo sehemu ya juu ya kaburi, ikasogea na kucha uwazi….

‘Umesema huu ni mlango wa nini….?’ Nikamuuliza, na akajifanya kutabasamu , alipogundua. Nahisi alipogundua kuwa kaongea neno ambalo hakutaka kuliongea akasema;


'Wewe huoni hili…kwa kawaida, mtu utaingiaje huku,..hapa watu wengi wanafahamu kuwa ni kabur, lakini kumbe ndani kuna maajabu…eeh, wewe hulioni hili,..humu kuna maajabu…utakuja kujaona, na kawaida mtu ukiingia huku, eeh, kama zio kuzikana, basi wewe ni mfu au sio…’akasema.


'Mzee mbona lugha yalo ni ya kuogofya,...ina maana sisi ndio tunajipeleka kuzimu..au ..’akasema msaidizi, akisita kuingia ndani.

'Usiogope kijana, wewe lengo lako si kukutana na huyo binti, au umeghairi tena…’akasema huyo mzee.


'Mimi sanasana lengo langu ni kukutana na mrembo wa facebook, lakini yeye sizani kama ni marehemu, huku tunakwenda kuhakikisha kama huyo binti wa mzee yupo hai au la, si ndio hivyo…’nikasema.


'Haaah, kumbe...hahaha, haya, ngoja ukajionee mwenyewe, hapo ndio namvulia kofia huyo mtaalamu, masikini wameshamuua, hawa watu bwana…’akasema.


'Unamvumilia kofia Mtaalamu gani huyo…?’ nikamuuliza.

'Tatizo lako wewe unakuwa na hamasa kupitiliza, unisikie… mengine naongea tu, haya zama ndani jizike mwenyewe….’akasema akinisukumia ndani, na yeye akafuatilia, halafu akasema

‘Unaona hicho hapo juu, ni kamba, lakini hii ndio itatusaidia mambo mawili, italifunga hili kaburi,..na sisi tutajizika,…mambo ya duniani, tutatachana nayo, kama tutajaliwa tutaoka nje, kama ndio hivyo, useme dunia bya bye…’akasema

‘Sijakuelewa mzee…’nikasema

‘Wewe kivute hicho kitu usiogope, upo na mimi, haya unaona limejifunga, haya kivute tena,…huoni sasa tutashushwa kwenda chini, kama lifti, utaalamu huo.

 Tulishushwa kidoo tu,, tukawa tupo sehemu ya chini, ndani kwa ndani..

'Sasa…hapa ndio pa kuamua, tunakwenda wapi, huku kuna chumba alipowekwa bosi,..au tuelekee moja kwa moja alipowekwa huyo binti…. kuna mawili chagua moja..’akasema, na mimi nikasema;

‘Unajua tokea awali kuwa mimi lengo langu kwasasa ni huyo binti,..kama kweli yupo hai…’nikasema


'Swadakta,…..umenena vyema kijana,..huku sasa usije ukashangaa nakuita marehemu, hahaha..usiogope,….lakini kwanza kabla hatujaenda huko, nina ombi langu kwanza,....'akasema, huku akisimama.

‘Ombi gani tena mzee….?’ Nikamuuliza

‘Kule duniani, nilikugusia, kuwa ….eeh, ni hivi….unajua mimi nimekuwa nikitaman sana kuvipata vitu vitatu,...


' Vitu gani hivyo mzee…?’ nikamuuliza.


'Ehee,… kuna bastola ya ajabu,…hiyo ni muhimu sana kwangu, kwanza nikuulize, uliionaje hiyo bastola, ile uliyompa, Docta,… ushawahi kuisikia siri yake kabla,…?’ akauliza.


'Hapana….’nikasema


' Ndio maana, maana ungelijua siri yake, sizani kama ungemkabidhi mtu kama yule,…Ile silaha ukiwa nayo, umeshajiandikishia kuwa wewe ni mtawala, ile siri yake toka awali na nembo ya mtawala…enzi za mamabu zetu waliamini hivyo..ili ina mkono wa shetani,…na…amani…’akatulia.


' Kwahiyo wewe unavihitajia hivy vitu kwa vile unataka kuwa mtawala…lakini wewe si mumbe tayari, unataka uwe nani, mbunge, raisi, au….?’ Nikamuuliza.


'Sio lazima niwe mimi..unielewe hapo,…. tunaweza kuiuza kwa mtu tunayefikiria anafaa…huyo keshapatikana, na huyo akiipata ikiwa tayari, basi…dunia itakuwa mkononi mwetu…’akasema


' Kwahiyo kuna mtu unafikiria anafaa kuwa mtawala na ana pesa nyingi za kukulipa..au sio, na huyo ndiye unatak kumkabidhi hiyo bastola….?’ Nikamuuliza.


'Kwa kiifupi ndio...’akasema.


'Ni nani huyo…?’ nikamuuliza.

'Huyo, kwa hivi sasa siwezi kukuambia, wakati muafaka utafika, na huenda ukaona naye, mimi sijawahi kumuona uso kwa uso, namsikia tu….’akasema.


'ndio huyo mkuu nini…?’ nikamuuliza na yeye akatabasamu na kusema.

‘Huyo hatajwi tajwi ovyo….sema kwa vile wewe hujui sifa zake, ….’akasema.

‘Mhh, mnamuabusu au…ni mtu au ni shetani….?’ Nikamuuliza


'Kwanza sikiza,..usipoteze muda wako kunidadisi, ukitatarajia kuwa nitakuambia mambo ukamsimulie docta,au polisi, ujue umeshaingia humu, wewe sasa ni mtu wangu, ninaweza kukufanya nitakavyo…’akasema akipangusa pangusa mikono kama alishika uchafu.

‘Sasa sikiliza, kwa vile wewe lengo lako ni jema tu, wewe unamtaka nani…binti mrembo…na mimi nahitajia nini, hivyo vitu vitatu, kwasasa viwili anavyo, docta,au sio….mimi navihitaia hivyo,… unasemaje, nitavipata au...na kama nilivyokuambia awali, ukiingia humu, umeingia kuzimu, na kila ukiahidi, kitu, nikaumbie ukweli, huwezi kuvunja ahadi, ukivunja mizumu itakuandama…. ukihin, utakuwa mfu…


'Ndio imani zenu hizo….’mimi nikasema.


'Nikuulize tena wamtaka huyo binti au la…., na hii ndio nafasi yako ya mwisho, ukiwa bado hujazama kwenye dimbwi la umauti, na kuusahau ubinadamu…’akasema , nahisi alijua mimi nitaogopa,…mimi nikasema;


'Mzee tumekuja kote huku nia ni hiyo, hayo mengine, siwezi kukuahidi, kwa vile hivyo vitu havipo mikononi mwangu tena…’nikasema.


'Ninafahamu hilo, lakini..nina namna naweza kukuwezesha, ukaenda kuvichukua, ni wwewe tu, ukubaliane na mimi…sitaki kutumia nguvu, ….’akasema.


'Kwa vipi, ina maana unaweza kutumia nguvu kunilazimisha niende kuvichukua, au…?’ nikauliza.


'Wewe nijibu tu, kama upo tayari, kunipatia hivyo vitu, kama upo tyari ukikuali basi nitajua la kufanya, na wewe utakuwa na huyo rafiki yako,…ni mpenzi wako au sio, basi  wewe kubali, kuw upo tayari, ….’akasema.


'Mzee mimi siwezi kukubali wakati, sina namna ya kuvipata hivyo vitu, unajua fika, kwa hivi sasa siwezi kwenda huko alipoweka huyo mtu, ….na kama nikienda, muda, mpka niende nikutane naye, sijui nitamshawishije hadi akubali, ni kitu kigumu sana….’nikasema.


'Mimi ninajua umemkabidhi docta, na wwewe ndiye anayeweza kwenda na kuvipata hivy vitu, kirahisi,….wewe kubaliana na mimi, kuwa upo tayari, mengine niachie mimi…’akasema na nikashindwa kumuelewa,anawezaje kufanya hadi nikavipata hivyo vitu na kumkabidhi yeye,…


Mimi nikawazia, nimdanganye tu, kuwa kama kuna njia hiyo ya kuvipata, basi, nitajua huko mbele kwa mbele, muhimu mimi niweze kumuona huyo binti.


'Mzee, kwanza ni kwanza, ahadi yetu, ni mimi kwanza niweze kumuona huyo binti, ili niweze kusadikisha maneno yako, hili la hivyo vitu limekuja baadae, kwanza timiza ahdi yangu au….na mimi,...nikimuona,…’nikasema na yeye akaangalia juu, halafu akasema

‘Ina maana huniamini…..’akasema

‘Mzee,… kwanza nikuulize, una uhakika, kuwa kweli huyo binti yupo hai au na wewe unakisia tu, huenda ulimuona binti mwingine aliyefananishwa naye, hawa watu wanaweza kumabdili mtu akawa kama yeye….’nikasema.


‘Kijana, hayo ninayokuambia, nina uhakika nayo, na mimi  nisingechukua hatua hii ya hatar, nina uhakika huo..ujue kijana kuingia huku ni hatari..huku ni kuzimuni…’akasema akiangalia juu.


'Ok, …mzee, lakini nilishakuambia awali, mimi sitakiw atu wafu…mimi namtaka huyo binti, ninayemfahamu mimi, mpenzi wa facebook, sio huyo mfu…najua nitamuona lakini kumbe yupo huku kuzimuni hafai huko duniani…’nikasema.


'Sawa, wewe si ndio hivyo, unatamka mpenzi wako wa facebook, wote hao nakuhakikishia utawapata, lakini kwanza ni wewe kutimiza masharti yangu, hayo ni muhimu sana, ..umenielewa,…’akasema sasa akiongoza tuanze kutembea;


'Sawa, twende…’akasema.

‘Haya twende mimi nikimuona, basi nitaangalia namna ya kwenda kuvipata hivyo vitu….’nikasema;


'Aaah..unajua ni hivi, wewe, unakwenda kuvileta, hivyo vitu kwa vile hivyo vitu ndio ufunguo wa kupata mahitaji yako…huyo mdada ili aweze kuongea, ..anahitajia nguvu ya hivyo vitu….’akasema.

‘Sikuelewi mzee, ina maana ni maiti, mnataka kuihuisha au…?’ nikauliza

‘Hakuna mwanadamu wa kuhuisha…labda awe amepewa miujiza na mungu…sisi ni ..mimi ni mtaalamu wa kuagua, ..unajua, nafahamu huyo binti hajafa, ila kafanyiziwa tu, sasa mengina nitakuambia…’akasema.


'Mzee, nikaumbie ukweli, kwangu mimi, hivyo vitu havina thamani kabisa kwangu, sina haja navyo, na wala sijui umuhimu wake. Mimi ninachotaka ni kumuona huyo bint, ambaye alisadikiwa kuwa kafariki…au sio, halafu unielekeze jinsi ya kumpata huyo mpenzi wangu wa facebook,…sawa….’nikasema.


'Huyo binti hajafariki,…hilo liweke akilini mwako,  siri ya yote hayo hadi akawa hivyo, naifahamu mimi, ngoja nikueleweshe sasa, ...'akasema.


'Siri gani hiyo…?’ nikamuuliza.


'Hiyo, nitakuambia ukitimiza makubaliano yetu….unasikia,…’akasema


'Kwahiyo, tukubaliane kitu kimoja uniweke wazi, wewe ni miongoni mwa hao watu, au sio…?’ nikamuuliza.


'Usiniulize maswali ya kunitega, kuwa labda unatafuta ukweli wa kuja kunifunga, hutaliweza hilo, maana kuanzia sasa upo hapa…’akaonyesha kiganja chake cha mkononi…

‘Na unielewe kijana, mimi haya yote ya kuwa na hawa watu, kama nilivyokuelezea awali, kazi yangu ni ujanja, nauma na kupuliza…, ila kiukweli kama huyu jamaa wahili kundi, akibahatika kuupata utawala, …lakini kuweza kwake ni mpaka aipate hiyo bastola, na hivyo vitu vingine….’akasema

' Kwahiyo wewe kumbe, nia na lengo lako ni kuwasaidia, au kumsaidia huyo mtu, ili aupate utawala, sio wewe haswa… au sio...?’ nikauliza

‘Kijana..unauliza sana maswali, unajua hata nikikujibu, ..huna namna nyingine, ushaingia humu ujue utakubaliana na mimi, ..kuna namna nyingi, lakini mimi sitaki kukuumiza, najua wewe sasa ni mtu wangu…nikuulize kitu, unajua ni kwanini ukaja mwenyewe huku…?’ akaniuliza.

‘Nilitaka mwenyewe ndio..nina hamu sana ya kumuona huyo binti…ndio lengo langu…’nikasema

‘Na docta hakupenda kabisa wewe uje huku, unalielewa hilo…’akasema

‘Mimi nimekuja mwenyewe kwa utashi wangu…’nikasema

‘Sawa tusibishane kwa hilo…utakuja kugundua kuwa mimi ndiye nimekuvuta hadi ukaja, na docta hakuweza kukuzuia, maana nina nguvu zangu za kuweza wewe kufanya nitakavyo, lakini sitaki kwa hivi sasa kuzitumia, haina haja, nataka wewe ukubali kwa utashi wako, maana nina imani wewe utakuja kumuona utmakaye, na nyie wawili mtafanikisha jambo, ambalo hata wewe utakuja kulifurahia,….’akasema

‘Sawa mzee, mimi sina shaka,..kwasabau hata ukinisimulia mambo yenu ya kuzimu, uchawi, mimi siujui, na wala siuamini, na …hivyo vitu kama unavihitajia, eeh, kama kuna namna, basi nitavileta, lakini kwanza nimuone huyo binti, hilo ndilo sharti langu…’nikasema

‘Sawa sawa, kwahiyo umekubali…..’akasema

‘Kwa sharti hilo…..unielewe hapo, kwanza kwanza..sio uniletee ujanja ujanja wako wa nguvu za giza, mzee, nikuambie kitu, mimi ..anyaway, twende huko,..ukanionyesha, halafu, uniambia na namna ya kuvipata hivyo vitu, mimi nitakueletea, .havina maana kwangu…’nikasema.

‘Hapo sasa tupo sawa, mizimu wamekusikia,…twende kijana….napenda sana watu wa namna yako majasiri, wanaojiamini,..hahaha.. unampenda sana huyo binti, hata yeye alikuwa anajiamini hivyo hivyo, nikamuambia, haya….sasa hivi watu wanamtambua kama marehemu, lakini….’akatulia, alihisi kitu akatikisa kichwa…

‘Nahisi kuna kitu hakipo sawa….’akasema

‘Unaona , mzee wewe umeanza ujanja ujanja wako…’nikasema

‘Sio kuhusu hilo….mizimu..inaniashiria jambo, hebu kidogo, akasugua mikono yake, ahalafu akanusua, ..halafu akasugua tena, akaniambia
‘Hebu nusa….’akaninyoshea mikono yake

‘Hapana ….mzee, mimi sitaki huo ujanja wako, sitaki uniharibu akili yangu, tuelewane wewe unataka hivyo vitu sawa, kuna namna ya mimi kuvipata , sawa..kama ni hivyo, nionyeshe huyo binti, kama ni ujanja, na mimi nitatumia ujanja wangu, wa asili, …’nikasema

‘Hahaha, huo ujana wao hauna kazi humu ndani..humu eeh, ni milki ya mababu zangu, na hata hao watu, wamekodi..wanalipa pesa nyingi sana, makafara ..ndio usiombe, ni lazima wafanye hivyo, la sivyo, hawatafanikiwa, na wewe upo kwenye miliki yangu, utafanya nitakavyo mimi….’akasema

‘Mzee, unataka kusema nini…’nikasema

‘Sikiliza bwana mdogo, mimi nakupeleka kiungwana, sitaki nikupeleke kinamna ya kukupumbaza, nataka haya yatendeke ukiwa na akili zako, ili baadae tuwe marafiki au sio,…sasa kuna jambo, nataka ulielewe,..twende,, ..usiogope, siwezi kukufany akitu, wewe ni mtu muhimu sana kwenye haya mambo…’akasema na tukaanza kutembea kuelekea huko kwenye sehemu anayosema ndipo huyo binti yupo…

***************

Mpelelezi akamdaka yule mdada kabla hajadondoka…alijitahidi kufanya hivyo kwa mkono mmoja, na kuhakikisha anamuweka chini salama, huku akiangalia huku na kule kuhakikisha hakuna mtu anayemgundua, na pia kuangalia kama kuna mtu atakayeweza kumsaidia, ili akaendelee na kazi yake iliyomleta hapo…wakati hayo yanatendeka, docta anaona, akayasoma mawazo ya mpelelezi,

Docta akapiga simu kwa haraka kwa mkuu-msaidizi , kuwa mpelelezi anahitajia msaada wa haraka. Na mkuu akamjibu;

‘Kijana wangu yupo karibu yake keshaiona hiyo…usijali endelea kunipa habari…

Na wakati huo,…wakati mpelelezi, sasa anageuka huku na kule kutafuta msaada, mara akajitokeza mtu karibu yake,na huyu mtu, akasogea kumkagua huyo mdada, mdada, wakati huo yupo kalala sakafuni, hajitambui,..huyu akasema, kwa kuuliza;
‘Kuna nini, huyu mdada kafanya nini…?’ akauliza akimuinamia kumkagua

‘Huyu dada naona anahitajia msaada, sijui ana tatizo gani!

‘Ok, ok, hebu subiria,…ninapiga simu kumtafuta docta wangu, atashughulikiwa mara moja,au….?’ Akauliza huyo mtu.

‘Sawa, sawa itakuwa vyema, ila…’akasema mpepelezi, na huyo jamaa akamkatisha kwa kusema;

‘Usijali,..bosi,…nimeshapiga simu kuna docta anakuja kumshughulikia…’akasema huyo mtu, na mpelelezi, alijitahidi asiangaliane na huyo machoni ili asije kutambulikana kuwa yeye ni nani,..hata hivyo, kwa tahdhari, akataka kuhakikisha kuwa huyo mdada yupo mikono salama,.. akasema

‘Huyo docta anatokea wapi…?’ akauliza

‘Yupo hapa jirani, ana hospitali yake, lakini kama una docta mwingine, mimi naweza kumzuia huyo asije, unasemaje…?’ akaulizwa na mpelelezi, akaona haina haja, akamuamini huyo mtu, na kusema;

‘Haya, mimi nina mtu namfuata huko ndani, …umesoma hiyo hospitali inaitwaje..?’ akauliza na huyo jamaa akamtajia jina la hospitali ambayo huyo mdada, ikibidi atapelekwa huko…

‘Ok, sawa,..naifahamu, haya nikitoka huko nitakuja huko, …’akasema mpelelezi, na kuanza kuondoka.

‘Lakini bosi si ingekuwa vyema, kama ungesubiria, na ikibidi uongozane na huyo docta, maana hata mimi, sina shughuli, si unajua tena ,au..?’ akauliza huyo jamaa.

‘Mhh..hapana kuna mtu namtafuta huko ndani,..huyu hakikisha yupo salama, mwambie docta mimi nitakuja,..nikitoka huko ndani, ..kiukweli mimi simjui huyo mdada…’akasema mpelelezi, akiona asipoteze muda hapo nje, na akiendelea kubakia hapo atashindwa kufanya kazi yake na anaweza kutambulikana.

Mpelelezi alipoondoka, tu, huyo jamaa akampigia bosi wake simu, kuwa mtu wake, anahitajia mtu mwingine wa kumfuatilia, yeye kabakia na mdada, na akajibiwa kuwa, sawa ahakikishe kuwa huyo mdada yupo salama, mpaka atakapopewa taarifa nyingine.

Huku kwa mpelelezi, yeye kwa haraka…akaendelea na lengo, lakini hakujua kuwa kuna mtu anamfuatilia kwa kutumia mtandao…yeye, akili yale sasa ilikuwa kumtafuta mbaya wake, au wabaya wake, na kukamilisha dhamira yake, huyo mdada akaomba mungu awe kwenye mikono salama, ila akilini alitamani amfahamu huyo mdada, anahisi kama anamfahamu, japokuwa hakupata nafasi ya kumchunguza vyema;

‘Huyu dada nahisi ndio yule …niliyewahi kumuona kule…yawezekana, sina uhakika lakini, hata hivyo nitalijua hilo nikiingia huko ndani,..’akajisemeza hivyo, na kwa haraka akawa anatembea kuelekea ndani , hakukuwa na mtu wa kumzuia,..watu walikuwa wakitembea wengine kuingia, wengine kutoka, ila alishangaa kuona watu waliokuwa na sare kama ile yam dada, na watu walikuwa wakiwashangaa.

‘Sasa nitaingiaje humu..?’ akajiuliza, mara alipofike kwenye mlango ambao ukiingia ndio unaweza kwenda vyumba vya chini,.. na mara ghafla, mlango ukafunguka…mara, akatoka jamaa mmoja akiwa na haraka,

Huyu jamaa wala hakusema neno alipomuona mpelelezi, alimpita huku akiangalia saa kuonyesha kuwa ana jambo muhimu analiwahi, na keshapoteza muda, …mpelelezi, bila kupoteza muda , yeye akaingia ndani, na mlango ukajifunga kwa nyuma yake..hakuangalia nyuma yeye, mbio mbio, kumtafuta mbaya wake..

‘Kwanza kabla ya kukabiliana na huyo, kwanza niende nikahakikisha jambo moja, je kweli huyo mdada ndio yule niliyemuona kule….kama ni yeye,..kuna tatizo,…kama ndio yeye, ..lakini hata kama yeye, mimi sina shughuli na yeye, mimi nataka kuonana na huyo jamaa aliyetaka kuniua na kundi lake….hao..ndio wabaya wangu…

Akafika kwenye kile chumba,…anakuta mlango upo wazi…..

NB: Sehemu ijayo

WAZO LA LEO: Tumemaliza kumi la kwanza, la mfungo, hebu tujikague je kuna chembe ya imani imeongezeka, …jana au juzi uliweza kumsaidia nani, uliweza kujitolea kwa jambo gani, je hukugombea kitu na wenzako, ukasema basi mpeni huyu…nasema hili kwani tulikuwa tunagombea dala dala, kuingia ndani, niliona watu wanavyosukumana kuingia ndani , hakuna aliyejali kuwa kuna watoto, wazee, na  wasiojiweza, kisa wanakimbilia kiti…


 Haya sasa tumeingia ndani, umeonyesha umahiari na ubabe wako,...umekaa huku unawaona, wazee, kuna akina mama wamebeba watoto wadogo, kuna wagonjwa, wamesimama, kwenye viti, umakaa , kwa vile wewe umewahi kuingia kwa ubabe, wao si vijana, wana nguvu..hapo wanatabasamu kuwa wameshinda...wameshinda nini..,kupata viti, hawa wamefunga, kumi la kwanza limeisha,....Huu ni mfano mdogo tu, wa kupima imani zetu kama kweli zimeshaanza kutakasikia, kuna chembe ya upendo ndai yetu,….kiukweli, imani ya  kweli sio kitu cha mchezo…

Tunaambiwa imani ya kweli ni mpaka pale utakapokuwa radhi kumpa mwenzako kitu unachokipenda haswa, ukasema aah chukua wewe kwanza kwa kutoka moyoni..pia, nafsi yako ikajenga kukinai,.... ukarizika na kidogo ulicho nacho,...pia ukawasaidia masikini na wanaohitajia, nk...….

RAMADHANI KAREEM, tumshukuru mungu kwa kulifikia, kumi hili la pili.

Ni mimi: emu-three

No comments :