Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Monday, June 5, 2017

MPENZI WA FACEBOOK-44



Docta, alipokea ujumbe kutoka kwa mtu wake, kuwa kafanikiwa kutengeneza namna kwa kutumia herufi za kikomputa, itakayomuwezesha kurejesha ule mtandao ufanye kazi tena kama awali…
'Sawa ni vyema, hata hivyo nimeshaupata ufunguo wake tayari…’akasema docta
‘Umeshaweza kuufungua huo mtandao..?’ akauliza

‘Bado sijapata muda huo…’akasema docta

‘Ufungue, ukishaufungua uweke hivyo vielelezo vya herufi za kikomputa nilivyokutumia, visaidia kujilinda, na kuulinda huo mtandao usiingiliwe tena…’akambiwa.

'Kwahiyo, ...’docta akataka kuuliza lakini simu ikakata mawasiliano.

Mawasiliano yakakatika, na docta,akahisi kuna tatizo mahali,…lakini hakusubiria, kwa haraka akafungua ule mtandao wa awali, ulipogoma akaingiza ule ufunguo, ni aina ndogo sana ya kitendea kazi cha komputa cha nje(external drive) alipokichomeka tu kwenye komputa, ilijiandika, ..kuwa huo ni ufunguo tawala, unaweza kuingia sehem yoyote iliyifungwa, ikauliza unataka kufanya nini sasa…!

 Docta alichagua kwenye namna mbalimbali zilizoorodheshwa, kuwa anataka mtandao uliofungwa, urudie kufanya kazi, na alipochagua hivyo, mtandao ukaanza kufanya kazi, ukiuliza ushehenezwe habari za zamani na sasa, akasema ndio..ikawa sasa inajaza habari, hadi ikafika mia, na hapo hapo ikasema mtandao upo tayari kutumiwa,…sasa ndio akaweka zile herufi, za kujikinga, ili asiingiliwe, na zilipokamilika, akaweza kuwa mtawala wa mitandao.

 'Sasa tunamaliza kazi...'akasema docta akionyesha tabasamu usoni.

'Cha kwanza ni kuharibu mitandao yao yote mibaya, yenye kuathiri wanadamu,....akazitafuta sehemu hizo, ambao kulifichwa kumbukumbu za watu, akahakikisha kila mmoja karejeshewa kumbukumbu zake, halafu ndio akaziharibu sehemu hizo, zisiweze kufanya kazi tena.

'Chapili ni kuwafungulia wale wote waliofungwa akili zao, warejee kwenye akili zao sahihi, kwa amani na salama..’akasema na kuanza kufungua, na ikasema tayari hao watu wameshafunguliwa na kumbukumbu zao zote..wapo salama.

Na kila mtu anapohakikishiwa kuwa yupo salama, kumbukumbu na picha yake hutokea, na kuonyesha sasa yupo wapi…

Alizifuatilia hizoo picha na majina yao… aliona picha mbali za wahanga wa hao wakubwa kwa wadogo..na ni wale waliopo hai, kama mtu amefariki inaonyesha alama nyekundu kuwa huyo mtu ni marehemu.

 Akawa anafuatilia watu na majina yao, hadi mwisho!

 'Mhh,…. ina maana ni kweli, mbona sijamuona..’akasema akiendelea kutafuta majina tena na tena kwa wale waliofariki, na alipohakikisha kuwa hilo jina halipo, akaona arejee kwenye majina ya waliopo hai,..hayupo,....hii sasa ni ajabu!

‘Mbona huyu mtu hayupo popote, kwanini…?’ akajiuliza sasa akilini akijaribu kuwaza hilo lina maana gani…kama hajafariki alitakiwa awe kwenye majina ya watu waliopo hai…., lakini huko hajaonekana jina lake, na kwenye hata waliofariki pia jina lake halipo...hii ina maana gani…, akajiuliza na hakuweza kupata jibu la uhakika.

 Alipojirizisha,..na kinachoendelea kwenye mtandao,  ndio akaanza kumtafuta  huyo mtu yupo upande gani, na kwanini hajawekwa kwenye huo mtando,  kulikuwa na watu wengi kwenye hilo jengo, na wingi wao ukaongezeeka, kutokana na hao watu waliotokea ndani, hao waliokuwa wafungwa, hawakuwa wanaonekana huko nje,..na cha ajabu wote walikuwa na vazi la aina moja, kutokana na vazi lao walilovaa, watu waliokuwemo kwenye hilo jango, kwa shughuli zao mbali mbali walihisi labda, hilo ni vazi rasmi la wafanyakazi wa hilo jengo.

Cha ajabu hata wafanyakazi wa humo, waliokuwa kwenye shughuli zao mbali mbali, walijikuta wakiwashangaa hao watu pia, na walishindwa kufanya lolote maana hao watu, walikuwa wakitokea ndani,  na hali hii ikazidisha hamasa kwa wateja, na hao wafanyakazi pia, kubakia kuwaangalia hao watu waliokuwa wakitokea ndani.

Hakuna aliyewatambua hao watu kwa haraka, maana miongoni mwao, kuna ambao walikuwa wamepotea siku nyingi, na ndugu zao walishafikiria kuwa huenda wameshafariki, lakini kuna wale ambao walitambulikana kuwa wamefariki wakazikwa, sasa wanatokea, hao ndio itakuwa ni balaa kwa jamaa zao,…je wakionekana na jamaa zao itakuwaje..

Docta hakuwa na muda wa kuwadadisi zaidi yupo ni yupi , inagwaje majina yao yalikuwa yakitokea, kila anamgusa na kiashiria cha komputa….na wakati anawakagua mmoja baada ya mwngine mara macho yake yakatua, kwa mtu mmoja aliyekuwa akiwashangaa hao watu wanatoka ndani…

‘Mpelelezi…’
**************
Docta hakutajia kabisa kumkuta mpelelezi eneo hilo, kwa vile alikuwahajapna vyema, na haitakutakiwa afike eneo hilo tena,kwani jamaa walikuwa wakimtafuta ili wamuue,kwa vile wanahisi ataweza kuongea mambo mengi kuhusu hilo kundi, ndio maana ilitakiwa kama inawezekana aendelee kuumwa hivyo hivyo, mpaka hilo kundi lisambaratishwe, sasa huyu anaonekana yupo kwenye eneo la maadui.

Docta akahisi mwili ukimsisimuka kwa woga,..huyu mtu akipatikana sizani kama watampa hata nafasi ya kujitetea, na hata binti yake ambaye naye yupo kwenye ulinzi mkali, akiwa na mama yake walitakiwa na wao wafichwe seehmu nyeti, lakini wameachiwa kama mitego, ili jamaa wakitaka kuwasogelea tu wakamatwe!

'Huyu mpalelezi kafuata nini huku, na iweje, ina maana keshapona, haiwezekani,..lakini huyu mtu alikuwa hospitalini, kafikaje hapa…’ aliposema hivyo ndio akaitisha namna ya kufuatilia nyendo za huyu mtu, kwa kutumia mtandao, na ndio akagundua kuwa huyu mtu alitoroka hospitalini, na kuja maeneo hayo akitumia bajaji,…

‘Sasa kafuata nini huku kwenye hatari hivi, na bado anaonekana mkono wake haujawa sawa..?’ akajiuliza, na kabla hajapata jibu, simu yake ikawa ainaita, na alipoangalia akakuta ni mkuu anampigia;


‘Naona kuna mambo yanaendelea jumba la biashara ni wewe umefanya vitu vyako nini, mboan hujaniambia kuwa umefanikiwa kurejesha huo mtandao, je ni wewe au kuna namna hawa watu wanatutega,…au kuna nini…maana hata walinzi wangu wameshindwa kujua ni nini kinachoendelea, na walinzi wa ndani wanasema milango yote ya ndani imefunguka..’akasema mkuu.

‘Waambie watu wako wa kule makaburiini, wawe stand by, lolote linaweza kutokea, na wale wa ndani karibu na sehemu hiyo ya makaburini wawe wepesi kuwakagua hao watu,…wanaotoka ni lazima upate taarifa bila kujali ni nani, ama kwa wanaoingia, wawaruhusu tu, lakini wakujulisha kuwa ni nani…’akasema docta

‘Sawa ndivyo wanavyofanya, kwani kuna jambo gani jipya…?’ akauliza mkuu.

‘Kuna watu wawili wameonekana wakiingia kwenye njia ya kupitia kaburini,…ndio nataka kuwafuatilia, sijawagundua bado, je watu wako hawajawaona watu kama hao..?’ akauliza

‘Sijapata taarifa yoyote, ngoja niwaulize, wewe je umeona nini huko…’akasema mkuu.

‘Sawa waambie wawe makini, najua wanaotumia eneo hilo watakuwa watu wanaofahamu sana kundi hilo…’akasema

‘Ni kweli…’akasema mkuu

‘Na huyo mtu wetu wa ndani muwe makini naye, anaweza kutafutiwa njia za kutoroka…ama kwa kupitia kwa wako au..akanbaweza kuja mtu ambaye watashindwa kumzuia…’akasema docta.

 ‘Lakini yupo kwenye kifungo, ..kafungwa vyema mikononi na miguuni,..hawezi kufanya lolote, na nimehakikisha mle ndani kuna kifaa cha kuangalia mienendo yote na hivi sasa namuona, yupo, anaonekana hana raha kabisa…’akasema

‘Sawa…..,. najua hilo…lakini naona kuna ugeni unamfuata hapo, hao watu wawili msiwazuie, tuone wanadhumuni gani, ila uwe …walindwe,…’akasema doctacta
‘Mgeni, gani..ooh, nimekuelewa,… ndio maana hata mimi nataka nielekee huko, sasa wewe fanya hivi, endelea kuwepo hapo kwenye mtandao wako, halafu utanipa habari za nini kinachoendelea huko,ngoja mimi nielekee huko..’akasema

‘Kuna kitu nimeona, mpelelezi katoroka hospitalini yupo huko..’akasema

‘Oh, kwa vipi, katokaje, ..ndio hapo nashindwa kuwaelewa hawa walinzi wangu, kuna uzembe au kuna ndumilakuwili… , inakuwaje wanamuachia mtu…lakini sina shaka naye, ila ninacho-ogopea kwa sasa ni usalama wake, kwa  vile hajapona vyema , na nachelea asije kuharibu mitego yetu..’akasema

‘Ninamfuatilia kwa karibu,..akili yake kwa hivi sasa ipo safi , ila anaonekana na huzuni usoni..kuna kitu kinamsumbua, na hali kama hiyo inaweza ikawa ya kutaka kufanya jambo, likaharibu kila kitu, naona ni bora ukamtuma mtu wako mmoja awe karibu naye, hatua kwa hatua..’akasema docta.

‘Sawa hilo litafanyika mara moja..na vipi uliweza kuvipata vile vitu..salama..?’ akauliza mkuu

‘Vitu gani,…oh, bado, ngoja kwanza kuna kitu kimetokea, …’docta akasema na kukata simu.

**************
Docta alikata simu baada ya kuvutiwa na mtu…alimuona mdada mmoja, mrefu kiasi, ana umbile nzuri kutokana na vali alilovaa kuonyesha kwa nje hivyo, japokuwa halionyeshi kwa ndani yupoje, maana linafunika sehemu zote kutoka juu hadi chini, alikuwa miongoni mwa watu walitokea ndani na inaonyesha hivyo kutokana na mavazi yake….akawa anatembea mwendo wa pole pole, tofauti na wengine ambao walikuwa wakitembea kwa haraka.

‘Yaonyessha huyu bado afya yako haipo sawa,..ni mdada gani huyu,.. au hayupo kwenye orodha ya watu waliokuwepo kwenye huo mtandao hatari, ambao walihitajia kurejeshewa kumbukumbu zao, na ili warejee kwenye afya zao, sasa huyu kulikoni…’akasema docta.

Docta , akavuta sehemu ya kuuliza, je huyo mtu ni nani…lakini ombo hilo halijakamilika, kukatokea tukio jingine lilimfanya asiendelee kuperuzi huko…, huko upande wa makaburini, kuna kitu kikaashiria kuna tukio, akaona ngoja aangalai huko kwanza....akaona jambo, lililomfanya aachane na kumtafuta huyo mdada, kuwa ni  ni nani.

Alipovuta seehmu hiyo ya makaburini, akahisi mwili ukihisi hali ya mashaka makubwa, ndio akasema;

‘Huyu sio ooh,..’  akakunja ngumi kuashiria hasira!

‘Msaidizi wangu..’

‘Huyu mtu kafuata nini huku, mbona hakuniambia anakuja, huku…na hajui kuwa anajipeleka kwenye hatari, huyu mtu kachanganyikiwa nini…’ na mara akaona kuna mtu mwingine nyuma yake…
‘Hii sasa ni hatari…na hapa kwasasa siwezi kumsaidia kwa lolote,, hivi anaelewa ni kitu gani kipo mbele yake,..na huyu mtu anayeongozana naye ni nani huyu,..’akasema na kuchukua simu yake na kumpigia msaidizi wake, lakini simu ya msaidizi wake ikawa haipatikani, akawapigia walinzi wa huko.

‘Huyu msaidizi wangu yupo wapi?’ akauliza

‘Ndio mkuu…eeh, ngoja, maana mimi nilitoka kidogo…’akasema mlinzi na docta akakata simu kwa hasira, akampigia msaidizi wa mkuu wa kituo, akamuulizia kuhusu hilo, na msaidizi akasema.

‘Niajuavyo mimi yupo mle ndani na watu wengine, tuliwaambia wakae hapo kwa usalama wao, sasa sijui kama anaweza kutoka,….kama kafanya hivyo, walinzi watafahamu ..ngoja niwapigia.

‘Wala usihangaike kuwapigia, ..huyu jamaa keshatoka humo, sijui kwanini kafanya hivyo, namuona, na…watume watu wako wawe karibu naye ila wasifanye lolote la kuwazua, kuna kaongozana naye, ..simuamini…’akasema.

‘Ni nani huyo kaongozana naye..?’ akauliza.

‘Sijamtambua bado,..ngoja, ..oh, nitakuambi-a, baadae…..kuna kitu nimekiona ..ok, baadae, nakata simu mara moja..…’docta akakata simu.

 Huku kwenye jengo, akaingia mdada mmoja.., huyu anatokea nje, ni kama pacha wa yule wa ndani , hata kuvalia kwao,ila huyo yupo tofauti usoni..

‘Huyu mdada alikuwa kavaa sawa sawa na hao watu waliotokea ndani,  kavalia vazi jeupe refu, lenye mikono mirefu, na vazi hilo lina kitu kama kofia,..inayoshikiliwa kwa nyuma kutoka kwenye gauni, kofia hiyo ni kama mtandio wa wanawake lakini ni duara, kama kofia, inaonekana inavutoka, unaweza kuivuta hadi sehemu ya shingo, ila sehemu ya mbele usoni inakuwa wazi.

Sasa kwa huyu mdada aliyetoka nje, yeye kavaliwa mawani makubwa ya rangi nyesu ya kufika sehemu kubwa ya usoni, ili mtu usitambulikane sura yake….kilichomvutia docta zaidi ni sehemu ya miguuni, kavalia viatu vya aina yake..

‘Oh..hivi viatu,…vinaonekana vya aina yake, ok…labda, lakini nahisi kuna kuna kitu hapa,..’ akasema hivyo, na hakuataka hisia zake ziwe za kutoka akilini, akawa anaiuliza komputa kw..na kabla jibu halijatokea…mara simu yake ikalia, aliyekuwa akipiga simu alikuwa ni  mkuu, msaidizi wa kitup cha polisi

‘Docta, docta….kuna mtu kafika, na gari na sasa anaelekea eneo la makaburini yawezekana ni yule mtu wetu,..kaja na taxi ya kukodi,walinzi wamejaribu kutafiti kuwa ni nani, lakini hawajaweza kumtambua,kwa jinsi alivyovalia,…nahisi kavalia hivo kuficha sura, kavalia koto refu …kichwani kofia pana, na mawani makubwa ya rangi nyeusi, unaweza kumtafuta kuwa ni nani kwa haraka…’akaambiwa

Ikabidi docta kwanza afanya hiyo kazi, ya mkuu , maana ni muhimu, huyo kwasasa ndiye mkuu wake wa kazi, la sivyo angemkatalia kuwa kuna jambo jingine analifanya,…akawa anamtafuta huyo mtu kwenye mtandao, kweli ..akamuona sasa hivi alikuwa kasha fika maeneo ya mkaburini,…

‘Huyo mtu  ni nani…?’ akajiuliza docta akimkagua kwanza huku akiweka sawa seehmu ya kuuliza,

‘Huyu mtu anaweza kuwa ni miongoni mwa hawa watu …’akasema.

Huyo mtu alichofanya kwanza hakuonyesha wapi anapoelekea, ila ni makaburini, alichofanya yeye, ni kujifanya ni mmoja wa watu waliofika kuzika, kwani kulikuwa na shughuli za mazishi zinaendelea, yeye akafika hapo na kujichanganya, baadae akatoka hiyo sehemu na kuelekea kule kwenye kaburi,..kaburi la binti wa mzee, akaangalia huku na kule alipoona hakuna mtu, akainama na kushika upande wa lile kaburi

 Halafu akainama na kuanza kusukuma,..likawa lile mlango wa juu linasogea kirahisi tu,..na hapo docta akangiwa na hamasa kiasi kwamba alisahau kumpa taarifa mkuu wake, kuwa huyo mtu ni nani, ni kwa jinsi alivyoweza kutambua ni sehemu gani ya kugusa kwenye huo .mfuniko wa juu wa hilo kaburi, na kuweza kuusukuma kwa kirahisi kabisa,..ina maana analijulia hilo kaburi lilivyo.

Haikupita muda, huyo mtu akazama ndani ya hilo shimo la kaburi…, na akawa anavuta ule mfuniko kwa ndani ukajifunga,....sasa hapo docta akawa na hamu ya kumtambua huyu mtu vyema ni nani, akaangalia sehemu aliyoulizia, na maelezo yakaja hivi;-

‘Huyo mtu ni mgeni kwenye mtandao, ila anavyoonekana kajibadili sura,kwa kuvalia kitu cha ziada, na kuficha sura yake halisi,…, ila yawezekana akawa kati ya hawa watu hapa chini; ikatokea orodha ya majina ya watu, na docta hakuwa na nafasi ya kuyakagua, kuwa hao watu ni akina nani huenda akampata mtu anayemfahamu.

Ilichukua muda kuonyesha orodha ya watu, na docta akaachana nayo…akaamua kumuelezee mkuu wake hicho alichokipata…na huku anavuta sehemu za kufuatilia nyendo za huyo mtu, sasa alikuwa kwa ndani, na wakati anafanya hivyo, mara akaona ishara kuwa kuna jambo muhimu kule kwenye jengo la biashara;

 Akaacha kwanza huko makaburini na kuelekea huko kwenye jengo la biashara.


************

 Huku napo alimuona mpelelezi akiwa anamfuatilia yule dada aliyetokea ndani….na yule dada alionyesha kama anataka kutoka nje ya hilo jengo,…na mpelelezi sasa akawa nyuma yake, na huyo mdada hakuonyesha ishara ya mashaka, ila bado alionekana akitembea kwa kuyumba yumba..

‘Itakuwa ni hatari kwa huyu mdada akifika barabarani, anaweza hata kugongwa, anavyotembea ni kama...ok,...'akasema na kumpigia simu mkuu, na wakati anataka kufanya hivyo yule mdada akawa anayumba yumba anataka kudondoka, na mpelelezi akamuwahi na kumdaka.


NB: Nimechelewa kuanza kuandika hii story, lakini kwa matukio, ilikuwa hivyo, najaribu kuyaweka matukio mengi kwa pamoja, japokuwa kila tukio lilikuwa na taarifa yake ndefu tu yenye kutosheleza sehemu nzima ya kisa kwa siku

WAZO LA LEO: Utofauti wa binadamu na wanyama wengine ni tabia, hulka yake ya kutambua baya na zuri. Ukiona mwanadamu anafanya mambo mabaya kinyume na utu, kinyume na mienendo ya wanadamu wenzake, ujua kuna walakini. Sasa iweje sasa mwanadamuu huyo huyo awe anafanya mambo wanayofanya wanyawa wengine wasiojua kutofautisha zuri na baya, wakajizalilisha, wakavaa uchi…eti kwa vile wameofanya hivyo ni wasanii mashuhuri, wenye pesa na kujulikana


Je kama kwa hao wao labda ilitokea bahati mbaya tu, nguo ikawavuka, tutaiga tu, au wakitembea uchi, sisi tutaiga tu, au je kama kwao ni namna ya kutangaza propaganda mbaya zenye muelekezo wakutangaza mauchafu yao, tabia zao chafu,kinyume na maumbile ya mwanadamu, sisi tutaiga tu, kwanini hatutumii akili zetu kutafakari mambo kabla ya kuyafanya, umhimu wake kwa jamii na muonekano wetu ..ni aibu na fedhaha, kama tutakuwa tunaiga bila kutumia akili zetu…itafika sehemu  wanyama wataonekana ni bora zaidi yetu…Tumuombe mola wetu atuepushie na tabia hizo chafu.
Ni mimi: emu-three

No comments :