Mpelelezi
alijiinua pale kitandani, akajinyosha, bado alihisi mwili ukiwa na maumivu kila
sehemu hasa sehemu ya mkono wa kushoto, bado mkono ulikuwa haukubali kunyoshwa,…
bado kulikuwa na matatizo. Alipojaribu kumuuliza docta,…docta akasema;
'Itachukua,muda kupona kabisa, cha muhimu kwa
sasa uwe makini, usijitoneshe, na ingelifaa ukapata mapumziko ya muda mrefu, …yaani
ukiona upo sawa, sisi tutakuruhusu, hata hivyo bado utahitajia kupumzika
nyumbani kama miezi mitatu hivi kabla hujaweza kwenda kazini, jitahidi sana kufuata
masharti, utapona kabisa….’akasema docta.
‘Nikae nyumbani miezi mingine mitatu!!..hapana…haiwezekani,
…?’ akasema Mpelelezi akijikagua
‘Ndio,…inahitajia
kupumzika, kwa kipindi hicho au hata zaidi itategemeana na kupona kwako…hiyo sehemu
ni sehemy nyeti, hiyo risasi iligusa mfupa, na una bahati sana, lakini utapona
kabisa, ni swala la muda tu..’ndivyo docta alivyomuambia, na alipoambiwa hivyo,
akajua sasa kazi basi.., na ndoto zake za kujitahidi afikie cheo kikubwa
zimekwisha..na huenda akizidi kukaa nyumbani, atalipwa nusu mshahara, mshahara
wenyewe ni mdogo!
Aliiwazia familia yake, akawazia watoto wake,
ambao baadae alikuwa ameamua kuwahamisha na kuwapeleka, shule za kulipia,…na
japokuwa imekuwa kazi kubwa kwake kuwalipia wote, na sasa alipojiunga na hilo
kundi, waliweza kumpa pesa akawa analipia,..hakupenda ….
'Unajua
haya maisha ni lazima uwe na malengo, ya mbali,…kwa hivi sasa tutakusaidia
kulipia ada watito wako, tutakuanzishia miradi mbali mbali…miradi hiyo ni kwa
maisha yako ya keshi,…unajua nikuambia kitu,.. hizi kazi zina leo na kesho,
ukitegemea ajira tu…, ipo siku itatokea tatizo….’akaambiwa, kiukweli hakupenda
na huyo mtu hakuchoka, akaendelea kumuelezea.
‘Hizi
kazi zenu hizi , kwanza ni za hatari,..inaweza ikatokea, ukapatwa na matatizo
makubwa ukashindwa hata kujilisha, huku familia inakutegemea,… na hao
unaowatumikia hawatakujali tena, maana umuhimu wako ni pale unapoishika silaha,
ukapambana na wahalifu au sio, hebu fikiria umefikia sehemu huwezi hata
kuishika silaha, itakuwaje ndio maanaa mimi nakushauri hivyo,…utafuta njia
nyingine ya kuingiza kipato...na njia ndio hii…’akaambiwa.
‘Tatizo
njia yenu sio halali, ni haramu…’akamwambia
‘Ni
tafsiri tu….na maneno ya watu, wewe ukifika kwa jamaa yetu, yupo jamaa mtaalamu
anajua jinsi gani y a kukupa mawazo ya kuwekeza, mbinu za kupata pesa, ….mwenyewe
utafurahi,…yeye huyo nina uhakika,… atakuonyesha njia mbali mbali, za kuwekeza
wewe utachagua ipi inakufaa, au sio…kama hupendi hii, kuna nyingine,na…wanaweza
kuutumia utaalam wako..ikibidi..’akaambiwa.
‘Utaalamu
wangu!!!!....hahaha, mimi ni askari na utaalamu wangu ni wa kuitumikia nchi
yangu kwa mambo yahusuyo usalama wa nchi..watautumiaje utaalamu wangu…’akamuuliza
huyu mtu.
‘Wewe
kubali tu …kujiunga…utajulishwa, nina uhakika hutajutia…na sio hivyo, watu
wanavyosema, viitu kma hivyo havipo…lakini kama hutaki haya, usije kunilaumu!
Akamkumbuka jinsi jamaa huyo alivyojitahidi
kumshawishi, ili ajiunge na hilo kundi, na mpelelezi alipoonyesha msimamo wake,
…na baadae ndio wakaanza kumfanyia vitimbwi…mwanzoni hakujua kuwa ni hao watu,
lakini siku moja wakaamwambia waziwazi…, na wakati wanamuelezea hivyo binti
yake yupo mahututi…hana pesa, …ana madeni…
Aliyakumbuka
hayo kwasababu jana usiku alimuota huyo jamaa, jamaa ambaye litumwa kwake
kumshawishi, alijua kuwa huyo jamaa alitumwa kwake , baada ya kulazimishwa
kujiuna na hilo kundi bila hata kupenda, sasa jamaa huyo huyo akamjia kwenye
ndoto,…sasa anaongea kwa kumkebehi...,
'Unaona
sasa wewe, hapo ulipo ni sawa na kilema,… unafikiri nini, wewe ni kilema, mkono
huo mmoja hautafanya kazi maisha mwko tena,..utaalamu wako wa shabaha
hautakuwepo tena….ujasiri wako wa kupigana, wa kufanya mambo kwa haraka, kwa
mikono yako miwili hautakuwepo tena..na kwa namna hiyo, thamani yako kama
askari itakuwa zero…nani atakuthamini kwa hali kama hiyo tena, hakuna.
Hata
wewe mwenye unaujua ukweli huo…umuhimu wa mtu…, muajiriwa ni pale akiwa kazini
na ana afya , ukiwa mgonjwa, muajiri wako atakuona ni hasara, sasa wewe hapo ni
hasara.. watakuvumilia kidogo baadae watakuambia ukapumzike nyumbani, na
kukulipa nusu mshahara, baadae unastafishwa….’akaambiwa na huyo jamaa akiwa
kwenye ndoto.
‘Nilikuambia
haya awali, hukutaka kunisikiliza ukafikiri mimi nataka
kukuchuuza, haya ukaja kuingia kichwa kichwa, wakakutumia, lakini bado
hukutimiza yale yaliyotakiwa ina maana ulikuwa ndumilakuwili au sio..…
ungelikubaliana na mimi, ukajiunga kistaarabu, haya yote yasingelitokea,…
Na
hata kama ingetokea hivyo…maana kazi yako ni ajali mkononi…, ukaumia,..bado
usingelikuwa kwenye hali kama hiyo …mawazo na kujuta,..ukisema ningelijua….maana
sasa ungelikuwa na miradi yako, inajiendesha yenyewe…, hata ukiwa unaumwa, ,
hata ukiwa kitandani…
‘Hebu
sasa, muangalie binti yako alivyo sasa hivi hana raha, mkeo hana raha, watoto
wengine halikadhalika, au wale sio watoto wako ehe……, binti yako hataki,
hata,kuja kukuona, unafikiri ni kwanini…mkeo
anakuja lakini akikuangalia hana raha, unafikiri ni kwanini, na watoto wengine,
wamefukuzwa shule, hawana ada, unafikiri watakuaonaje wewe, ni baba gani wewe…
'Kwasababu
wewe ni baba, asiye na malengo ya mbali,..chukulia mfano binti yako alikuambia nini,
unakumbuka, alikuomba sana, umsomeshe..anataka kusoma awe docta, kufeli kwake
kwa mara ya kwanza sio tatizo, angerudia tena, angelifanya vizuri… ,
ukamwambia, huna pesa za ziada, eti kwa vile hakufaulu kidato cha nne, huku
unajifanya unampenda,…hahaha
‘Wewe
kumpenda mtoto ni kumpa elimu bora…au … angalia watoto wa wenzako wanasoma
shule za fedha,…wana cheo kama chako, kwanini…wanatumia akili ya kuona mbele…sasa
wewe kwann, huna akili
yakufikiria..unafikiria kuua watu kwa risasi tu, au kuwakamata wahalifu au sio…sasa
zawadi yake ndio hiyo…au utasema ulikuwa unaishi kwa jasho lako, su sio…haya
wasomeshe hao watoto, jiulize ni kwanini, utasema mshahara wako ulikuwa hautoshi
au…, kwann usitoshe,...kwasababu hutaki kufikiria mbali, sasa utakula jeuri
yako…’akaambiwa na huyo jamaa akimkebehi kwa ulimi…
Alijaribu kuikwepa hiyo ndoto,lakini kila
akipatwa na usingizi , hiyo ndoto inamrejea tena na tena, na mwishowe akamuota sasa
bint yake mwenyewe kamjia, akiwa kitandani, yeye hajiwezi, binti kaja kusimama
kitandani kwake…hapo anaota , binti yake anasema;
'Baba,
nimejua sasa wewe hunipendi,..hutupendi sisi watoto wako,… kama ungelikuwa
unanipenda, kwanini hukukubaliana na hao wenzako werevu…ukawekeza biashara,…sasa
umeacha mimi nateseka, umeacha mpaka hao wtu wananichukua na kunitesa, haya
wewe ni jabari, askari shupavu, mbona ulishindwa kuniokoa kwenye mikono ya hao
watu...’huyo binti akasema akiwa hana nguvu, mwili umelegea,
‘Sasa
unaniona nilivyo, nipo kama zezeta, sijitambui, sijijui...’ Na aliposema hivyo,
mate yalikuwa yakimtoka kama mlemavu, asiyeweza hata kuzuia mdomo wake….mate
yanajitokea ovyo
Ndoto hiyo ilimfanya Mpelelezi azindukane, na
kukaa kitandani,,,japokuwa macho yaliashiria kuwa bado aan usingizi, madawa
anayotumia yanamchosha…lakini kwa hali aliyoona kwa mtoto wake, na kwa hali
aliyo nayo kwasasa…, akajikutaanashika kichwa,…na bila hata kutegemea akaanza
kulia…hakujua ni kwanini machozi yamemjia ghafla hivyo…akalia sana…, hata
alipochoka , akaanza kujipiga piga na mkono mmoja kifuani…, maana mkono
mwingine hauwezi kuuinua,..mkono huo kwenye kwapa ndipo risasi ilipitia,….
Baadae akatulia, akatuliza mawazo na kuanza
kutafakari, ni nini hatima yake, ni nini amekipta baada ya haya yote,…haya
ukiangalia , kikazi, sasa hivi hataaminika tena, maana, ataonekana alijiingiza
kwenye makundi haramu,..hakuna atakayemuamini tena, hata akielezea ni kwanini…kwani
wanamuuliza kama kulikuwa na tatizo kama hilo kwanini, hakusema...kwann, kwann,
hizi kwann zinamfanya aonekane sio mtiifu tena, hakuweza kutekeleza majukumu
yake vyema kiapo chake cha utii hakukitimiza.
Na sasa akigeukio huko kwa hao watu
waliomshawishi aliangalia kama kuna lolote amepata, amepata nini hakuna…ilikuwa
ni ahadi tu…, utakuwa hivi, tutakufanyiwa hivi,
na zaidi alikuwa akipewa pesa,..lakini cha ajabu hizo pesa, japokuwa
zilikuwa nyingi, zilikuwa kama pesa hewa, ni nyingi, lakini hazishikiki…, ni
pesa chafu, unapata leo, siku kadhaa zimekwisha, pesa gani hizo...alifikia
hatua akawa anamshuku mkewe kuwa labda ndiye anamuibia, lakini haikuwa hivyo,
kumbe zile zilikuwa ni pesa chafu!
Mawazo yakamzidi..akitaka kulala labda
atatuliza kichwa, hakulaliki, kwni akilala anaandamwa na ndoto mbaya….sasa
alitaka atoke nje, angalau akajipe
mazoezi, lakini sasa maumivu yalizidi kwasababu ya kujipiga piga…, akainamisha
kichwa, lakini moyoni akasema, hakuna machozi tena…, hakuna kuwaza tena…,
iliyobakia sasa ni vitendo, akakumbuka usia wa babu yake alipomuambia kuwa
ameamua kujiunga na jeshi la polisi
'Sawa
sawa mjukuu wangu, uwe jasiri kama mimi…, na hata ukienda huko vitani,
usikubali kufa kikondoo, ufe kiume, ..ufe kama chui, au ufe kama paka, unajua
siri ya paka, paka akiona hana upenyo wa kukimbia, anakurukia wewe
mwenyewe..unasikia, usikubali kuwa msaliti, usikubali kuwa mnyonge ukatekwa,
pambana kiume…’.
Alipowaza hivyo akajitutumua..akahisi sasa
mwili ukisisimuka, akitamani atoke nje,…na hakutaka kupoteza nafasi hiyo tena….,
hakujali maumivu tena, hakujali maagizo ya docta tena…akasimama, akajitutumua…akaangalia viatu vyake vipo wapi…akaviona
akainama , akahisi maumivu lakini hakuijali
tena, akavivaa viatu vyake…, akavua zile nguo za hosp, akavaa nguo za
kwake… , akaanza kutoka nje.
‘Sasa
naenda kupambana na hao watu,…ama zangu ama zao…nitakufa ki—ki…, nitaenda
kutimiza wajibu wangu…liwalo na liwe….’akasema lakini akilini akahis kama
anajisuta
‘Utakwenda
kupambana na nani, ….na una silaha gani,….jifikirie kwanza kabla ya kuchukua hatua..wewe
ni askari shupavu, huwezi kuanza jambo bila ya mpangilio…utakufa kizembe wewe…’alipowaza
hivyo, akatulia na kuwaza,
‘Kweli
lazima kwanza niwe na mpango…natakiwa niende wapi, naenda kukutana na adui
yangu wapi, kwanza adui yangu ni nani..hilo lipo wazi, …akakumbuka, sehemu ile
ile alipojeruhiwa na silaha ndipo walipo wabaya wake, hasa huyo aliyemfanya
hivyo, huyo ni lazima ajibu mapigo…jino kwa jino..huyo ndiye wa kwanza,….wengine
watafuta, …’alipofikia hapo hakupotezea muda, ….akaanza kutembea kuelekea nje, ….
Alipofika mlangoni,mara akakutana na mkewe na bint yake…!
Oh….hatimaye
wamekuja, lakini wamekuja kufuata nini…akawaangalia usoni…nyuso zao
hazikuonyesha furaha kabisa,hwakuonyesha kuwa wamekuja kumuona mgonjwa, …maana
yake ni nini, nyuso zao zilionyesha ajenda nyingine,..wanataabika, wana maisha
magumu, hawana matumizi.
Akamuangalia
binti yake…usoni hana furaha, hana furaha kwanini, kwasababu baba anaumwa,
hapana, ni kwasababu anafikiria kuwa , sasa hatima yake imekwisha hatasoma tena…lakini
hata hivyo, kwanini hafanani kma ilivyokuwa kwenye ndoto,…kuwa kawa kilema wa
mwili…yupo salama, lakini usoni , nyoyoni hayupo salama…, kwanini, kwasababu
ana baba asiyejua muelekeo wa mbele….sasa, nitawaonyesha kuwa mimi ni baba gani…’akataka
kuanza kuondoka, lakini akataka kumuangalia na mkewe..
Mkewe kama kawaida, hana furaha..usoni, tokea
awali, hana furaha, atakuwa na furaha gani wakati kila anachokitaka, kinahusu
pesa, na sasa ..na kabla, pesa ilikuwa haishikiki…haya kashauriwa na wenzake
ajiunge na kikundi chenye muelekeo wa kuwekeza, kakataa…..imefika hatua, ….watoto
wanafukuzwa shule…ada hakuna….wewe ni mume gani, …unajiita jasiri, askari shupavu,
mbaona ushupavu wako hausaidiii familia yako…..hayo mawazo yalimfanya azidi
kuchanganyikiwa…akaanza kutembea kutoka nje, hakuna kurudi nyuma hiyo….
Mama
na binti yake wakawa wamesimama, sasa wameshikwa na mshangao huyu mtu anakwenda
wapi, lakini nani ainue mdomo,….wanamuogopa…huyooo, anaelekea nje…huyoo,
akachukua bajaji, huyoo, anaelekea huko huko walipomjeruhi…
**************
Mimi nikiwa sehemu maalumu ambayo tumeambiwa
tukae kwa muda kwa ajili ya usalama wetu, sikuwa na raha baada ya tukio lile….hadi
sasa siwezi kula, nikihisi kile kilichotokea, damu, ....ubongo vilivyonirukia
usoni, vilinifanya nijihisi vibaya…nahisi kama vile
Kiukweli kama kuna tukio litanisumbua sana
akili yangu, ni hilooo..hivyo ulishaona mtu anpigwa riasi kichwani…mbele tobo,
lakini huku nyuma, kichwa kinafumuka…hao atu ni wanyama….Tukio hilo limenifanya
nisiwe na hamu ya kula nyama kabisa, mawazo yakaniandama, hata ule ujasir wangu
wa awali ukawa haupo tena.
Imenisumua
sana hiyo hali, na wakati nawaza hayo, nikakumbuka jambo, nilitaka niongee na
docta, lakini nikasita, nikaona labda, nifuate mawazo ya huyo mzee, labda kweli
anaweza kunisaidia, nikakumbuka jinsi tulivyokutana naye hapo kwenye hilo
tukio..jinsi alivyobadilika pale aliponiona nipo nyuma yake, na alikuwa
akijiuliza je nimesikia yale aliyokuwa akiyaongea, ....
Mimi akilini nikawa nawaza na kujiuliza
inawezekanaje huyu jamaa aliyekuwa rafiki wa karibu wa mzee mwenzake…
'Siamini,
yule mtu anajifanya yupo karibu na mzee mwenzake, kwa vile alikuwa mpangaji
wake kumbe alikuwa na ajenda ya siri, alikuwa akimchunguza na kupeleka taarifa huko kwenye hilo kundi. Ama kweli
adui ya mtu ni mtu…
Yule
mzee alipogeuka na kuona namuangalia kwa macho ya mshangao, akashtuka, lakini
kwa ujanja akajifanya kuniongelesha kwa kusema;
'Hawa
watu bwana wasumbufu kweli…, inabidi niwadanganye, kihivi umesikia
nilivyowaambia hizo ni kamba za kuwaingiza kwenye mkenge, …mimi ni kiongozi
muadilifu,..lazima nifanye kazi y akuwasiaidia polisi, wakifika tu,…wanakutana
na polis,umeona ujanja wangu ee….'akasema na mimi sikumjibu kitu, alipoona nipo
kimia akaendelea kusema:
'Unajua
nilikuwa nakutafuta sana…kuna kitu nilitaka nikuambie, aheri, nimekuona,..unakumbuka
kipindi kile mlipokuja awali, wewe na docta, eeh, mkasema mnamtafuta yule binti
…niliwaza sana, nikajua wewe ulikuwa na mahusiano na yule binti,..nikaunga na
kuunga,nikakumbuka, wale wazee walikuwa wakimtafuta mtu aliyempa…unakumbuka, …na
nikajua, ni wewe, unabisha..’akasema na mim nikabakia kimia japokuwa moyoni
nilianza kushtuka.
Sasa..unajua
tena, hata mimi nilipitia huo ujana,…kama alijiua si yeye, bwana,…huwezi
kumlaumu mtu wakati sio yeye aliyempa sumu au sio…..nikamezea, nikaacha kama
ilivyo,kwanza mumejitolea sana kuisaidia hiyo familia, …lakini muhimu sio hilo…kuna
kitu kingine nilitaka kukuambia…
Akamsogelea
sasa akawa anaongea kwa kunong’ona
‘Unajua
nimegundua kitu,kumbe yule msichana hajafa..yupo hai..niamini mimi nimemuona
mimi kwa macho yangu, ndio hicho nilikuwa nakutafutia, sasa nimekuona,
..unasema tukaliongee hili sehemu tukiwa wawili, maana …unasikia, ni siri…hawajui
watu, na wakijua huyo binti anaweza kuuwawa,..’akasema.
'Unasema
nini….huyo binti yupo hai..'nikamjibu na hapo akapumua akijua keshaniteka
mawazo wangu
'Unajua
hayo matukio yote, yamegubikwa na ushirikina, sasa kama nilivyosikia, huyo bint
hakufa...kuna mazingaumbwe yalichezwa….unataka nikuambie kila kitu…’akasema na
mimi nikakaa kimia, kwanza nikiona kama ni mzaha, au huyu mzee anataka kuniteka
mawazo, ili nisahau hayo niliyosikia akiyaongea, lakini…hapana kuna kitu, …nakumbuka
hata yule kiongozi alipokuwa akiongea na yule mama, kuna kitu aliongea, lakini ….sio
kuwa huyo bint yupo hai….
‘Haiwezekani,hawezi
kuwa hai…’nikasema
‘Kama
huamini, basi nitakwenda mimi na wewe mguu kwa mguu, hadi huko..ila kwa sharti
moja….’akasema huyo mzee
NB: Hapo sasa...k
WAZO LA LEO: Moja ya fundisho la swaumu, ni kuijua njaa ilivyo,...ili ukimuona mwenzako ana njaa ujue jinsi gani anavyojisikia...kuna wenzetu wanaishi maisha ya shida, vita vimewazunguka, mabwana wakubwa wanashusha mabomu kila kona! Wahanga hawa wa vita, hawana sehemu ya kukimbilia, kisa nini...watu wanagombea mali...kisa nini..ubabe., na mengi wanayoyafahamu wao, kuuza silaha nk...sasa hawa watu wasio na hatia, wanakufa kwa njaa,..hawana amani tena, ndani ya nchi yao wenyewe.... sisi huku tunakula na kusaza, na kumwaga, hatujali tena mayatima, hatujali tena wazee, wajane, masikini...tunajaza vyakula vya kila aina mezani, ...je yule yatima, je yule ambaye hana hata cha kufuturia, hata maji, ..umewahi kumfikiria...sasa hivi hata maji ni gharama, mali ya asili ya mungu inauzwa,,...tuikumbuke njaa, ili tuwakumbuke na wenzetu wenye njaa...Ramadhani kareemu, na Ijumaa njema.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment