Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, May 4, 2017

MPENZI WANGU WA FACEBOOK-22


‘Kuchanganyikiwa kwangu kumenifanya nirudi nyuma sana,  kiukweli
nawashukuru sana kuwa mlikuja kwenye wakati muafaka, kipindi ambacho nilishakata tamaa, nimekuwa nikihangaika kuona haki itatendeka, najua kabisa dada hakuwa hivyo,..lakini najua aliyefanya hadi dada awe hivyo ni wewe msaliti..’akasema

‘Sikuelewi…’nikasema nikigeuza kichwa kumuangalia docta, na docta akawa katulia tu

‘Huwezi kunielewa kamwe, na huu sio muda wa kunielewa, muda utafika utanielewa, na kwa vile wenyewe wanakuja, umesema polisi wanakuja, sawa najua itakuwa hivyo, mtakamatwa, na mkikamatwa mengina yatafuta huko, niliwaambia lakini…’akasema

‘Unajuaje kuwa wanakuja kutukamata sisi…?’ nikauliza

‘Muulize huyo mwenzako atakuwa anajua zaidi , ila nawaonya lolote litakalotokea chonde chonde, sitaki waje kuwagusa wazazi wangu, baba yangu yangu hajapona,unaelewa zaidi docta…’akatulia kama anawaza jambo halafu akasema;

‘Hata hivyo nawashukuru sana..kwa kunisaidia nikapona, bila nyie sijui ingekuwje, nilishafikia hatua na mimi nataka kujiua,… nawashukuru sana, ila sasa nawaomba muondoke,  kabla hamjaiingiza hii familia yangu kwenye matatizo, hamjui tu…’akasema na sasa akaanza kutembea kuelekea ndani..

Kabla hata hajaingia ndani….gari la polisi likawa linakuja kwa kasi…;

‘Polisi hao wanakuja,…’ alisema docta,

Tuendelee na kisa chetu

*****************

 Mara polisi wakafika na gari lao, hata kabla halijasimama vyema askari wawili wakaruka na kutuweka chini ya ulinzi, na baadae wakatoka askari wengine wawili, wakatembea kuelekea mlangoni,..

‘Tunataka kuonana na binti…’akasema askari ambaye alionekana ni bosi wao.

‘Na Binti, binti gani..?’ akauliza docta

‘Binti wa huyu mzee, mzee mwenye nyumba hii, …’akasema , sasa akielekea mlangoni na kuingia ndani…, na mimi nikawa namuangalia docta kuona  kama atachukua hatua gani, maana nilijua na sisi tutakamatwa. Na wakati huo wale askari wawili wakiwa na silaha walikuwa wamesimama wakituangalia sisi

‘Duuh, hawa watu wanataka kufanya nini sasa..?’ akasema docta, akionyesha uso wa mashaka, na mmoja wa wale askari wawili akasema;

‘Msisogee, mkao hapo hapo…’akasema kwa sauti kali, na docta ni kama vile hakujali ile amri yao akawa kama anatembea, halafu akasimama, akaniangalia na mimi nikasema;.

‘Hata sijui….hawajui kuwa wanaweza kumuathiri huyo mzee, si huyo mzee hatakiwi kuingizwa kwenye mshituko tena, …..docta fanya jambo, uwaeleweshe hao watu, hawajui hao, wanatumia nguvu tu…’nikamwambia, lakini docta akawa kasimama tu akingojea

‘Docta…’nikasema kwa sauti, na docta akasema;

‘Subiri…huwezi ukaingilia kazi za watu hivi hivi, hatujui lengo lao ni nini..’akasema na mara tukasikia kilio huko ndani, na hapo docta akataka kukimbilia ndani lakini askari wake wakatuzuia.

‘Mimi ni docta na hao ni wagonjwa wangu, nina haki ya kuhakikisha wanatdea inavyopaswa, ..kama mkinizuia na lolote likitokea mtawajibika nyie..’akasema docta, na aliposema hivyo, yule askari akasogea pembeni na docta akaelekea huko ndani , na mimi nikafuata nyuma..

Tulipofika ndani, tulimuona yule askari akiwa kamshikilia huyo binti mkono, na mkono mwingine baba kamshikilia binti yake…mama akiwa pembeni, ..

‘Sisi watu wa usalama na kazi yetu ni kuhakikisha usalama wa kila raia, na tunapoona raia yupo hatarini, hatuwezi kukaa kimia,…huyu tunaondoka naye, tutamshikilia kwa muda, mpaka hapo tutakapojirizisha, kuwa yupo salama…tuna maana yetu kubwa, hakuna haja ya kuongea zaidi, mengine mtakuja kuambiwa..’akasema huyo askari

‘Sawa kwa usalama wake, …kwa vipi, ujue sisi ni wazazi wake, tuna haki ya kufahamu, huwezi ukaja ukambeba huyu mtoto hivi hivi , kama muhalifu, na kama ni mhalifu tuambie, ana kosa gani..?’ akauliza mzee.

‘Kuna makosa ambayo kwa hivi sasa siwezi kukutajia mzee, ..tuelewe sana, tuna kibali cha kumshikilia huyu yako hiki hapa…’akasema huyo askari, akimuonyesha huyo mzee hicho kibali, na mzee hakutaka hata kukiangalia, akasema;

‘Kama mnataka kumkamata huyu binti, nikamateni mimi, mimi ndio baba yake, na kama labda, …ni matatizo yalitokea kwenye ile nyumba yangu…huyu binti hahusiki maana nyumba ni yangu,.., kwanini mnamkata yeye, mtu alikuwa anaumwa,..siwaelewi lakini,,..’akasema mzee

‘Mzee, usipandishe munkari, matatizo uliyo nayo hayataki..hasira…, chukulia hili jambo kama kazi ya polisi, wana maana yao kubwa tu…, niachie mimi nitalifuatilia hili jambo, na kuhakikisha binti anarejea salama, mimi mwenyewe nitaongozana naye, unanielewa mzee, pamoja kuwa mimi ni dakitari, lakini pia nilisomea sheria..’akasema docta

Binti alivyosikia hivyo, akasema;

‘Baba unaona nilikuambia hawa watu sio watu wema, wanataka kuleta matatizo kwenye hii familia,..inaonekana wao ndio wamewaita polisi ili nikamatwe, hukuona walivyokuwa wananihoji, utafikiri wananishuku mimi kwa jambo fulani,.. sasa mimi baba nakamatwa mimi binti yako…, hujui ni nini kitafuata baadae… haya baba, haya mama, mimi nakwenda kufungwa bila hata kosa…’akasema binti kwa sauti ya huzuni,

‘Binti, hakuna tatizo kubwa…tuamini sisi… hili tunalofanya ni kwa ajili ya usalama wako…’akasema polisi akimshikilia mkono ili waondoke, na baba akawa anazuia..mama naye akawa anafanya hivyo, na docta akamsogelea mzee na kumnong’oneza kitu sikioni…mzee akashtuka, halafu, akasogea , wakati huo binti alikuwa kamshikilia baba yake mkono ili asiondoke.

Baba akawa sasa kama anauondoa mkono wake kwa  binti wake, huku akimuangalia binti yake huyo kwa macho ya mshangao…sasa akionyesha kukubali, binti huyo achukuliwe…kitu ambacho kilimfanya binti ashikwe na mshangao, lakini zaidi ilikuwa mama yake.

Sio binti au mama aliyeliona lile tendo la docta kumnong’oneza huyo mzee, kwahiyo ile hali ya mzee huyo, ya ghafla, ya kuonyesha kukubaliana na polisi, iliwafanya wawili hao, wajihisi vibaya, ..baba anawasaliti, baba hayupo nao,…akili ya kibinadamu ikaanza kufikiri hivyo, na muda huo bab akageukia upande mwingine kama anawapa mgongo.

‘Baba…’binti akaita, baba hageuki,..

‘Mume wangu vipi tena unakubali binti yetu achukuliwe, kuna nini hapa lakini, mbona mimi sielewi, kumetokea nini…?’ mama akauliza kwa huzuni.

‘Tumuachie docta afuatane na hawa watu,najua binti yangu atakuwa salama huko,…najua , hamna shida, mimi nitakuja baadae …’akasema baba, sasa akiwa kasimama pembeni , lakini mama hakukubali…ikawa mshike mshike , baadae mama akasalimu amri binti akachukulia, lakini hakuacha kabisa , akawa bado kama anafuata nyuma, na baadae akamgeukia mume wake..

‘Kama binti yangu atadhurika, kwa lolote lile, sitakusamehe kwa hili…umeniudhi sana, ina maana unakubali binti yako achukuliwe tu, hujui, kwasababu gani, au unajua ni kwanini wanamchukua, niambie sasa…’akasema mke lakini mume akabakia kimia hadi hao watu wakaondoka.

‘Jamani mwanangu, mnampeleka wapi binti yangu…nichukueni mimi kama mnafikiri kuna tatizo…’mama akakimbilia nje hakukata tamaa.

**********

Baadae tulibakia mimi na wawili hao, mama alikuwa kakasirika hataki hata kuongea na mumewe, utafikiri mumewe ndiye aliyesababisha yote hayo, na mimi hata sikuwa najua ni nini kinachoendelea maana docta likuwa hajapata muda wa kunielezea, haya mambo yalitokea kwa haraka haraka.

Baadae simu ikalia, ilikuwa yani simu ya mzee, kabla mzee hajaipokea nikamsogelea,

Angalia namba kwanza ni nani anakupigia, mzee akaiangalia akasema haina jina ni namba ngeni kwake,..nikawaza kwa haraka, nikasema, pokea tu, ila uwe makini,..

‘Halooh, nani mwenzangu..’akasema mzee, na kusikiliza, alisikiliza kwa muda mrefu bila kusema neno, baadae akawa kama anaangalia juu ya nyumba kuzunguka, halafu akakata simu

‘Mhh..hili sasa ni tatizo..’akasema mzee.

‘Ni nani huyo..?’ nikauliza, na mzee akani kwepa swali langu, akamgeukia mkewe na kusema;

‘Mke wangu uwe na subira, kiukweli tupo kwenye matatizo makubwa, sijui nia ya hawa watu nini…mimi sijui nimewakosea nini hawa watu…wangeniambia wanataka nini niwape lakini tuzidi kumuomba mungu tu…sasa nakuomba sana mke wangu uniamini..hebu twende nje kidogo, nataka kukuagiza jambo…’akasema na wakatoka nje.

Mimi nilibakia peke yangu , baadae nikapokea ujumbe wa maandishi kutoka kwa docta, alikuwa akiniagiza mambo ya kufanya,…haraka haraka nikaingia chumba cha mabinti, …nikaanza kutafuta hicho alichoniagiza docta;

‘Laptop…’ nikaangalia huku na kule mle chumbani, kilikuwa chumba cha kike, kila kitu kimepangwa kwa umaridadi,…nikaiona, ilikuwa kwenye kitanda kuna sehemu yake, nikaiona,.. kwa haraka nikaichukua na kuiweka kwenye mfuko wa Rambo, na kwa haraka nikatoka nayo, na kwa muda huo mzee na mkewe wakaingia.

‘Sasa tufanyeje..?’ akauliza mzee

‘Tuwe na subira tu…ila mimi natoka kidogo, nafika hapo dukani, nitarudi sasa hivi, naomba mjitahidi kuwa na subira…, najua mnavyojiskia, lakini hao watu wanatimiza wajibu wao, na uzuri wapo na docta, mimi namuamini sana docta ..’nikasema

‘Nimekuelewa, ila usichelewe..’akasema mzee, lakini mama alikuwa kakasirika tu, kaangalia upande mwingine..mimi kwa haraka nikatoka mle na kutembea hadi sehemu yenye nafasi, nika kaa kwenye kigogo..nilipohakikisha nipo peke yangu, nikaitoa ile laptop.., na kuiwasha.

 Ilikuwa na kifungio(password) nikafanya kama nilivyoagizwa kwenye ujumbe wa simu,.. ikafunguka,..kwanza nikaona vile vitufe mbali mbali, nikatafuta kitufe cha Facebook,…

Nikakifungua, na huko nikatafuta kitufe nilichoagizwa, nikakifungua pia na mara…oh, nilichoona hapo kilinifanya niishiwe nguvu,…..

Mungu wangu, kulitokea  picha ya marehemu, akiwa kakaa peke yake, kashika shavu, na chini yake kuna maandishi;

‘Kwaheri mpenzi wangu, nilikupenda sana,…najua umeshanisahau lakini mimi sijakusau, nilikupenda ndio maana uliponifanyia vile, sikuweza kuvumilia, nikaona njia rahisi ni kujiondoa humu duniani, najua ipo siku utakuja huku tutakutana ..kwaheri ya kuonana…’

Kiukweli nilihsi hali ya uchungu sana, nilitamani kulia,..na kwa chini nikaona picha nyingine,….

Hii picha  ya chini yake, ni ile ya yule msichana akiwa kwenye kaburi, lakini sasa ipo kwa mtindo wa video fupi, na nilipoibofya, ikafunguka,…ilianza na mlio kidogo wa wimbo wa huzuni,…mara akatokea yule mdada kwenye kaburi, akawa kama anatokeza vile kama mtu anayefufuka,kutokea kaburini , hapo ukatokea mlio wa kutisha kama bomu limelipuka….mpaka nilishtuka!

Sura ya huyu mdada sasa haina tofauti na sura ya yule marehemu, nahisi walifanya hivyo ili kuonyesha kuwa huyo ni mtu mmoja,..labda kabdilika kutokana na wakati au huko alipo kumemfany awe hivo…sijui au..hata sielewi wana maana gani,..ile sura ikatoka na kukaja kama kitanda lakini cha maua,..yule mdada akawa kalala kwenye kile kitanda cha mua, huku anatabasamu,.., kalala upande upande,..akiniangalia…hayo …macho, mhh, mbona, yanafanana ..macho macho…

Nikawa nimevutika na hayo macho zaidi.., nikawa nayaangalia, duuh..ukimuangalia macho yake ndio hivyo unakuwa kama unazama ndani yake…na hali hiyo ya kuzama ndani yake iliufanya mwili wangu ulegee, nikawa sina nguvu, akili na mawazo nikajihisi mtu mwingine..

Nikahisi sauti sasa ikiongelewa masikioni mwangu.., sauti tamu yenye mvuto, ni sauto ile ile inayonifanya niliwazike, saut ile iliyonifanya nitokeee kumpenda huyu binti, sauti ya mpenzi wangu wa facebook…lakini ina ujumbe mnzito..

‘Ulisaliti kwa ulionifanyia..sitaweza kukuusahau kwa hilo , sasa unafanya nini, nimekutafuta hupatikani,..hutaki hata kuingia facebook, umesema utakuja kwetu hujafika, kweli unanipenda wewe, au ndio umedanganywa na huyo docta wako kuwa mimi sio binadamu, hahaha, yaani imani yako imegeuzwa, sasa unaamini mambo ya kichwawi, kweli wewe ni mnafiki…’akasema na mimi nikashindwa, kujizuia, nikaaandika kwenye sehemu ya ujumbe.

‘Kweli nakupenda lakini sijui unaishi wapi…na mimi sio mnafiki, siamini mamb hayo natambua wewe upon a ipo siku tutakutana,….’

‘Hahaha, eti hujui ninaishi wapi, kweli wewe ni mwanaume, uwe unampenda mwanamke, halafu ushindwe kujua anaishi wapi, …hahaha, ama kweli wewe ni mmoja wao, mnapenda kuwadanganya akina dada, ujue mimi sidanganyiki, utakuja kunitafuta usinione…’ nilishangaa nilijua ile ni video ya kurekodi, lakini kumbe ni mbashara. Unaandika anaona na anakujibu papo hapo

‘Kwani hapo upo wapi..?’ nikamuuliza.

‘Kule kule nilipokuagiza, uje…na huko huko ndio tutakutana tena kwenye safari yetu ya maisha mapya…, usijali, nahisi muda umeshafika, nakupenda sana mpenzi wangu, ..karibu sana, wazazi wangu wana hamu ya kukuona...’akasema

‘Ahasante, nitafurahi sana..nakupenda na mimi sana, ila safari hii usinidanganye..unanipoteza njia..’nikasema na yey e akatabsamu akawa kama anipiga busu la mbali akiweka mikono..na macho hayo, yakanywea, …akapotea

Yaani ni hali ambayo huwezi kuelezea, ni kama ulikuwa sehemu na yeye, kumetulia kuna ubaridi fulani wa kusisimua mwili na ghafla unarudi sehemu ulipokuwa, joto ..joto kali ..mmh, …!

Baadae ile picha ikawa kama imeyeyuka, na ukumbuke naangalia kwenye laptop kwenye facebook, na chini yake nikaona kitu kingine kikanivutia ingaaje ni tukio la kuhuzunisha…ni picha ya watu wapo makaburini, wanakwenda kuzika, na ilikuwa picha,..na nilipoiangalia sana nikawa kama nazama ndani …ni vitu vy ajabu ina maana ukiiangali aile picha, unazama kuelekea kwenye hilo tukio, unakuwa sehemu ya wale watu

Nikawa kama mmoja wa waombelezaji, nikawa sijui ni nani anayezikuwa, nikajikuta nauliza;.

‘Ni nani kafa..?’nikauliza hivyo lakini akilini, na mara nikasikia suti nyingine ikisema

‘Mlinzi wa nyumba ya mzee,… leo ndio anakwenda kuzikwa, na yeye, viungo vyake vitakuwa biashara..’sauti ikasema

‘Oh, nilisahau…lakini kwanini viungo vyake view biashara kwani,…’nikasema

‘Ndio kawaida,…wala usisumbuke kuuliza kwani hata wewe siku ikifika kama itakuwa hivyo, utafanyiwa hivyo, lakini hutasikia, wala haitakuathiri kitu, maana utakuwa na mimi, si umesema utakuja…?’ sauti ikaniuliza

‘Mhh…sijakuelewa, kuwa na mimi itakuwa hivyo, kwa vipi..’nikasema kwa kuuliza

‘Muda ukifika utajua,..na ukija tutaonana..nitakusubiria..nahisi itakuwa moja ya namna ya kuzoeana, au sio…’sauti ikasema.

 Mara nikarejea kwenye hali yangu, nikakumbuka kuwa nasoma kitu kwenye laptop, sasa nikawa naangalia vitu vingine, na sikujua kuwa wakati mwingine umepita,..baadae nikakumbuka, ooh,

‘Hivi nafanya nini..?’ nikajiuliza,..nikakumbuka kuwa nilielekezwa jambo…

‘Fungu laptop, ingia kwenye facebook, tafuta ….ok, nimefanya hivyo, utaona maagizo yako, halafu nitakupigia simu…’

Sijui ikawaje, nilihis kama sio jambo la kawaida, na sizani kama ..haiwezekani, ndio baaadae ikawa kama akili inafungua, nikakumbuka n akukumbuka huko ni pale nilipohisi kama docta ananionya jambo....

 ‘Usije kuchat na huyo mtu, na kama ukichat naye kwepa sana mambo hayo…usimuangalia macho yake kwa hisia,..ukumbuke ukifany ahivyo, kwa hisia na ukahisi kama unazama ndani ya macho yake ujue, wewe unakuwa ndani yake, anakusoma akili yako…na...utakuwa mtumwa wake…’

‘Mungu wangu..’nikasema hivyo, nilipohisi kuwa nipo kwenye hatari..hatari gani, niliwaza hivyo tu…

 Kitu kilichonishangaza ni kuwa nilipokea ujumbe kutoka kwa docta, kupitia kwenye simu, ukinieleza nifanye hivyo, nilivyofanya, …sasa nimefanya hivyo yametokea mambo hayo ambayo ni kinyume na maagizo ya docta….mbona hivi, imekuwaje..

Hapo akili ikanicheza, fahamu zikawa zinanirudia kwa mbali,..akili ikanijia nikaichukua simu yangu na kuifungua, nikaangalia ujumbe niliotumiwa, ooh, sikuwa nimeangalia vyema sizani kama ujumbe  huo umetoka kwa docta…ni ujumbe kwenye simu …mwishoni ndio aliandika mimi docta, ..

‘Ssshit…’nikasema nilipogundua huo mtego

Hapo nikajua nipo kwenye mtego, nikachukua ile laptop, nikairudishia kwenye mfuko, nikaamua nimpigia simu docta nimuelezee kilichotokea,..kabla sijapiga simu mara. Simu yangu ikalia, nikajikuta nimeipokea, na sauti ikasema;

‘Leo ni siku ya mazishi ya mwenzenu..alikuwa mtiifu,  lakini baadae akakiuka masharti, na dawa ya watu kama hao, kama ilivyo nyie, ni hiyo, najua kila mtu atakufa, lakini kifo kingine ni cha kujitakia, kajitakia, na amekipata alichokitaka..najua hata wewe ndicho unakitaka, sasa subiria zamu yako …’akasema

‘Wewe ni nani..?’ nikauliza kwa haraka.

‘Hahaha, utakuja kuichunguza hiyo namba kwenye simu, kama utapata bahati hiyo na utagundua kuwa mimi ni nani…’akasema

‘Unataka nini kwangu..?’ nikauliza

‘Usijali ninachokita mimi tayari nimeshakipata, ila huyo binti, …namuonea huruma sana,..huko mlipomficha,.. sikutaka kumfanya chochote, ila kwa hali ilivyo, kwa ajili yenu, sizani kama nitakuwa na uwezo wa kumlinda tena, ngoja tuone, …tukimalizana na wewe, nitajua afanywaje…’akasema

‘Kwani wewe ni nani..,ndio wewe sio…?’ nikauliza

‘Hahaha, unataka kujua mimi ni nani, sasa nikuambie kitu, geuka nyuma utaniona mimi ni nani..’akasema na kweli kuna hali iliniashiria kuwa sipo peke yangu, kwa haraka nikataka kugeuka..nimechelewa

Kabla sijafanya hivyo, kitu kigumu kikigonga kichwa changu, na giza likatanda usoni, nikapotea kwenye giza

*********
WAZO LA LEO: Ni muhimu sana kwenye mambo yetu tukawa na  tahadhari, ..ni ili tuwe na tahadhari hiyo kabla ya kila jambo, tumuweke mungu wetu mbele, tuombe, tumuombe yule aliyetuumba, ili jambo hilo liwe kwenye kinga na rehema na baraka zake mola wetu muumba.


 Wengi wetu kutokana na kazi nyingi, kujisahau, au dharau tu,..si unacho,… huwa tunajifanyia mambo yetu bila hata ya kumuomba mola wetu, maana twaona tumepata au tunafanya kutokana na akili zetu, au ujanja wetu, au utukufu wetu, …lakini tukumbuke kuwa yote hayo tunayapata kutokana na rehema , na kudra za mola wetu muumba.  kwahiyo basi, tujijue kama wanadamu tunajukumu la kumuombe na kumshukuru mola wetu kwa kila jambo.

Ni mimi: emu-three

No comments :