Mpelelezi akasubiria amri…mpelelezi kwa muda huo alikuwa hana
nguvu zake za kawaida,…watu hao walikuwa wamelegezwa nguvu zao za kawaida.., na
docta alichofanya ni kumwekea nguvu nyingine za kuweza kuhimili hali ya amri
nyingine lakini bado hakuweza kuziondoa hizo nguvu mpaka mtandao uzisafishe na
inachukua mdua kidogo…, lakini kwa vile ile mitambo sasa hivi inamilikuwa na
docta, docta akawa ndiye anamuongoza mpelelezi.
Mpelelezi, akaamrishwa aende kumkagua huyo mdada…ambaye
alimkuta kwenye kile chumba, …,kingine kabla ya kuachana na huyo mdada,
alichoambiwa zaidi ni kufungua pingu alizokuwa,nazo huyo mdada, baadae
akaambiwa aangalie shingoni kwa huyo mdada kuna kitu kavaa kama mkufu, akifungue
na kukiacha humo.humo shingoni.
‘Huyu mdada kama namfahamu….?’ Alijiuliza mpelelezi, lakini
hakuweza kuwaza zaidi, ila akajikuta akimuulia;
‘Wewe ni nani..?’ mpelelezi akauliza, na yule mdada akacheka, ni
kama vile unamuuliza super star, anayejulikana dunia nzima,…na unapomuuliza mtu
kama huyo anahisi kama unamtania tu!
‘Mpenzi wa facebook…’alijiuliza lakini hakuwa na muda , yeye
akavutwa na amri nyingine ya kutoka kwenye hicho chumba
***********
Kama ilivyokuwa,kwa msaidizi wa docta, mpelelezi naye
alikutwa na hayo hayo, kwani docta naye alikuwa akifanya vitu vyake,
kuhakikisha kila aliyewekezwa kwenye hiyo mitandao haramu, ambapo akili na
utashi wa mtu unaondolewa na kuwa mtumwa wa nguvu za giza.
Mpelelezi ambaye alikuwa kwenye hilo jengo la biashara
, akiwa anafanya kazi kwa kufuata anavyoamrishwa na docta, alitoka kwenye kile
chumba alichomkuta yule mdada, na kuelekea huko alipoelekezwa kwingine….
Sasa
alielekezwa kwenye chumba maalumu, ilitakiwa afike hapo mapema, maana hapo ndio
kwenye miongozo ya kila kitu, lakini kwa vile docta alishachukua mamlaka ya
kuongoza mitambo yote, akawa hana wasiwasi, lakini ukumbuke watu hao ni
wataalamu pia, ilipotokea hivyo, na wao wakawa wanatafuta njia ya kurejesha ule
mtambo ufanye kazi kama kawaida.
Docta alishtuka hilo, na alipokumbuka kuwa wenzake wanawe
wakawa wameshaanza kurejesha nguvu zao, ndio akaona kuna umuhimu wa kumtuma
mtendaji wake ambaye ni mpelelezi.
Mpelelezi akaamrishwa,kwenda kuingia kwenye chumba maalumu,
chumba hicho kiliwekwa sehemu madhubuti, na watu wengine hawaruhusiwi kuingia
humo zaidi ya wafanyakazi wa idara hiyo, akafika mlangoni , mlango ulikuwa
umefungwa, na kufungua kwake ni mpaka uwe na namba za siri, ..yeye akaambiwa
asubirie tu, baadae mlango ukafunguka, a ulipofunguka tu, …wakatokea watu wanne
wamevalia majoho meupe kama madocta…
Walikuwa kama hawakutegemea kuonana na mtu, na
walipomuona mpelelezi, sijui kama wanamfahamu maana , walipomuona tu, wakainua
mikono juu…kama kujisalimisha,…mpelelezi akawa anasikiliza amri ya kufanya..
'Angalia shingoni mwao, wavue hiyo mikufu na
uishikilie wewe mwenyewe, hakikisha hupotezi hiyo mikufu…’akaambiwa, na
mpelelezi akafanya hivyo.
Alipomaliza
kuwatoa ile mikufu shingoni, ilikuwa kama kawaondolea nguvu fulani mwilini
mwao, maana ghafla wale watu wakaporomoka na kudondoka chini…wakawa kama
wamepoteza fahamu..
Mpelelezi
hakutakiwa kuwagusa tena, akaambiwa aingie ndani kwenye hicho chumba maalumu.
Na alipoingia akahisi mngurumo wa chini kwa chini, kuashiria kuwa humo ndani
kuna mtambo wenye nguvu, na jinsi unavyofanya kazi ndio unatengeza mngurumo huo…kulikuwa
na baridi sana…
'Angalia kulia kwako, kwa juu, kuna ‘main switch sever’
tafuta kitufe cha kuizima hiyo serve kuu, ‘akaambiwa, na bila kukosea akaiona
hiyo server kuu ambapo kuna nyaya nyingi zinazoelekea sehemu tofauti
tofauti,akaiona ile swicho, akaizima
Na alipoizima mara chumba chote kikawa kimia, ule
mngurumo uliokuwepo humo ndani ukazima…na kukabakia milio ya kulalamika tu,
kuwa mitambo haina nguvu yake ya asili…na umeme!
‘Sasa sogea
mbele kidogo, angalia upande wa kushoto kwako, kuna chumba kipo, kimezungushiwa
viyoo, ni bullet proof hiyo..risasi hzipenyo huko ndani, lakini cha muhimu
kwenye humba hicho ni mashine maalumu ya kutunza kumbukumbu, kama akiba,…umekiona
mlango kumeandikwa…
'Main server room…’
Akaingia kwenye hicho chumba na kumkuta jamaa akiwa na
mihangaiko, jamaa huyo alikuwa kainama chini na aliposikia mtu akiingia
hakugeuka, na kwa vile alikuwa akifanya jambo akiwa kachuchuma, akasema;
'Nimeshindwa
kufanya ‘back up’ kwa haraka, na muhimu kwa sasa ilitakiwa tupate ufunguo kutoka kwa mkuu…’akasema na mpelelezi
kusikia hivyo, akajiukuta akirudia hayo maneno ‘mkuu’!
'Mkuu..', kuna kitu kilimgonga kichwa, na kujikuta
akihis maumivu sio kitu , bali ni hali aliihis kichwani kama anagngwa na kitu.
‘Mkuu, ni nani
huyo…ni mkuu wake wa kazi au ni bosi wa hao watu labda ndio wanamuita boisi wao
hivyo..’akajiuliza bila kupata majibu. Na wakati anawaza hivyo jamaa aliyekuwa
kama kachuchuma au kupiga magoti, akifanya kitu chini ya kuunganisha waya waya
fulani, mara akasimama, kwa haraka akageuka.
Alivyogeuka kwa
haraka, na huku akiinua mkono, bastola tayari ilikuwa mkononi mwake…
‘Wewe ni nani…’Inspecta akaulizwa na inspecta hakusema
kitu alikuwakabakia kimia hawezi kuongea kitu kama hajaambiwa labda iwe ni
jambo la namna ya kipekee, na jamaa alipoona hajibiwi akamuangalia mpelelezi
usoni, huku anatikisa kichwa, huku akisema;
‘Hahaha, kumbe
ni wewe, najua kwanini huongei,..docta huyo anafanya vitu vyake au sio,…..hahaha,…hata
hivyo nimesikia kuwa hivi sasa wewe ni msaliti..na
unafahamu adhabu ya msaliti ni nini kwenye hili kundi,mimi kama mmoja wa
washika dau, nina kura yangu, sihitaji kukuambia ni ipi, ila kwasasa sina jinsi
ni lazima niitekeleze kwa vitendo,…’akasema akitayarisha kufyatua bastola yake,
lakini kabla hajafanya hivyo, akasikia mlio wa hatari kwenye server…
‘Subiri….’akasema akichunguza wapi mlio huo unatokea
huku kashikilia bastola bado akimlenga mpelelezi.
‘Ok, sio tija,…sasa hebu kwanza, niambie ni kitu gani
kimekuleta humu ndani, abda tusema umetumwa au sio…maana wewe unafahamu fika,
watu hawaruhusiwi kuingia humu, ambao
sio wafanyakazi wa idara hii..’akasema huyo jamaa akiwa kama anawaza jambo
Mpelelezi bado hakumjibu kitu, akabakia kasimama tu
'Unajua nilijua wewe ni mjanja sana, sasa ona, …masikini,
binti yako yupo mkononi mwa yule bosi,…unamfahamu alivyo, usoni anatabasamu
anacheka, lakini rohoni ni mnyama, anakuua huku anatabasamu,..ogopa sana watu
wa namna hiyo,…binti yako hana kosa, sasa atauwawa muda si mrefu, na wewe ,
ulitakiwa uwe umeshauwawa, tatizo hivi sasa hatuna mawasiliano, sijui..ok,
..mimi nitamalizia hii kazi, isiwe shida…’akasema huku akiangalia huo mlio
ukizidi kutokea tena.
‘Binti yangu yupo wapi…?’mpelelezi akatokwa na hayo
maneno,
‘Binti yako, hahaha..yupo huko makaburini, kaenda
kutolewa kafara…si unajua mambo hayo yalivyo,…unauliza jibu,…..mimi hapa sijui
kinachoendeleahuko, ila nafahau jambo kubwa, kuwa kuna mtu ,……huyo anayeitwa
docta kaingiza virusi kwenye mtandao wetu….atauliwa kinyama…’akasema
‘Kwanini unataka kuniua mimi….sina kosa, binti yangu
hana kosa…na wewe …’mpelelezi akatulia, mlio ulizidi kuongezeka, na jamaa
anashindwa kuinama kuiangalia kwa chini , maana kashikilia bastola.
'Ungekubaliana na sisi, ungeyafaidi matunda ya kundi
hili…, hebu angalia miradi tuliyo nayo, …ni mingi ajabu, pesa zinaingia kila
siku…na ilivyo, kama tulivyopanga wewe ungekuwa mkurugenzi , familia yako
ingeajiriwa kwenye vitengo vingine kama mameneja, mbona mkeo alielewa tu…sijui
wewe una nin..ni hiyo hulka ya jeshi, mbona wenzako wanayo, na ni zaidi yako,
wapo, wananeemeka tu….’akasema
‘Nakuuliza binti yangu ana kosa gani…?’ akauliza
mpelelezi sasa kwa sauti ya hasira, na jamaa akaweka vizuri bastola….
‘Usiulize majibu….na usinilazimishe kupasua huo ubongo
wako, kabla muda wako wa kufa bado…hii …huu mtambo ungelifunguka, nikajua
kinachoendelea ningelishakuua, lakini je ni kikuua kabla ya muda,..nitaharibu,….lakini
ngoja tuone…’akasema akichungulia huku kashikilia bastoka kwa mikono miwili
akirudi kinyume nyume.
‘Binti yangu yupo wapi…ni kwanini yeye…?’ akauliza
mpelelezi
‘Yupo wapi…tatizo
lako akili yako hapo haipo, ..umeshalogezewa, haujijui…kama ungelikuwa
unajijua,…aah,… bint yako lazma awe kafara, kwani damu yake inaendana na
mizimu....shauri lako, mimi kwa hivi sasa siwezi kuzuia hilo..namuonea huruma tu,
binti mrembo kama huyo anakuja kufa kinyama, unajua wanachokifanya huko….anauliwa
huku anajiona, damu,…inanyonywa,….na shetani…hata sitaki kuona….mtambo
ungelikuwa hai ningekuonyesha …’akasema akiangalia kwenye server.
‘Sasa kama wewe sio mnyama kama wao, kwanini ukajiunga
na kundi hilo..na kama kweli ulimpenda binti yangu, kwanini hujaweza kumtetea, …si
una kura ya dhahabu wewe…kura turufu…?’ akaulizwa
‘Hahahaha, kumbe unanitambua….hahaha, lakini nikitoka
hapa, hakuna atakyenitam bua tena, napotea kabisa kwenye hii dunia,…hahaha…umeuliza
nini vile…’
‘Ok, kuhusu binti yako au sio…?’ akauliza na mlio
ulikuwa ukiendelea kulia, mpelelezi alitamani kuchukua hatua lakini miguu, na
mwili ulikuwa hautaki umezuiwa.
'Kiukweli mimi nilimpenda sana binti yako,…lakini cha
ajabu kabisa akanikataa, ..najiuliza huyo mwanamke anataka nini, wanawake wapo
wengi wananitaka,…kwani, watu wanataka nini, mali ninayo….sura, eeh, mwili…wanataka
nini, sijui..na bint yako kama …kama alivyonikataa yule bint wa yule mzee,..basi
tena…’akatulia.
‘Binti wa mzee…?’ akauliza mpelelezi, akijaribu
kufikiria huyu mtu ni nani…
‘Mimi nilishawaambia yoyote atakayenikataa mimi,
atakumbana na kizimba cha mizimu,…mimi sifanyi kitu, wao wanajua…maana nina
huruma, …lakini mbele ya hiki kitu sina huruma,…huyo binti wa mzee, yupo
wapi,..au binti yako yupo wapi,...wote sasa watageuka kuwa asusa ya mizimu.
'Ninachojua kwa
sasa, na adui yangu mkubwa kwa sasa ni huyo….., sijui docta gani huyo, kaweza
kuiba mitandao yetu, na kuharibu mawasiliano yetu..ameharibu ndoto yetu ya
kutawala dunia kwa kupitia mitandao, kuitawala dunia, watu na
mashetani..hahaha..’akacheka sana, halafu akasema;
‘Unajua ukisoma sana,..ukayajua mambo… unakuwa kama
mwendawazimu..ukimuambia mtu hii ndoto, hakuelewi…lakini wataelewa tu…’akasema,
sasa ule mlio ulikuwa wa kuendelea kuashiria kuwa kama ni tatizo limefikia
kubaya.
‘Aah, unajua umepotezea muda wangu mwingi, sijui
kwanini sikuui tu….kuna kitu hapa… Kuna ufunguo wa kila kitu, `universal key’….unaujua
huo, wengine wanaita magic key…wengine ufunguo Malaya…yaani ni ufungu wa ajabu
sana…huo unatafutwa kila kona, lakini sisi tunao…hahaha…’akacheka, na ghafla
akanyamaza.
Nikuambie kitu, hata kama huyo docta, atachukua
mawasiliano yote…akayamiliki , lakini sis bado tunayo, hii, ‘main server,’…Humu
kumbukumbu zote zipo, hata kama watawashika wote,….wataharibu kila kitu, lakini
bado… je nikuulize kitu, huyo docta anaweza kuharibu, server ya ….giza, maana
sisi tunafanya wazi na gizani, huko anaweza kufika…’akatulia akimuangalia
mpelelezi.
‘Nyie watu mna wazimu…’akasema mpelelezi.
‘Na huyo docta
anajua kuwa wenzake pamoja na elimu hiyo, wana maaskari wasioonekana,
....unawafahamu maaskari hao, wamesambazwa kila kona...kwenye mitandao, kwenye
majumba ya starehe, …na kila sehemu yenye mkono wa pesa..hata majumbani…mwa
watu maalum.., hao atawezaje kuwashinda..au kuwazima…eeh,…’akatikisa kichwa.
‘Sasa hivi
ukiingia kwenye mitandao,eeh… ili uweze kupata nafasi lazima uweke moja ya
herufi zetu,… herufi hizo ni ishara ya maaskari wetu,..zimejengwa na ngucvu za
giza…hebu nikuulize swali, unawafahamu
hao maaskari wetu…?’ akauliza akiwa kama anawaza jambo.
'Hahaha....huwezi
kujibu hilo, maana hakuna anayeweza kuamini hilo…sisi, unajua, tunaweza kuongea
na mashetani...sio raisi kuamini,…na hatutumii …kama wanavyofanya hawa waganga
wa kienyeji,….tunatumia digital.....sayansi tupu…hahaha…kusoma kuzuri….'akawa
anasogea upande, kwani alihisi mlio mwingine, wa hatari kwenye mitambo iliyopo
humo ndani.
'Sio shida, hata kama umezima switch kubwa, bado humu
ndani kuna akiba ya kuhifadhi nguvu …uwezo wake inaweza kuhifadhi nguvu hata
zaidi ya masaa 48, nyie mnajisumbua tu…ngoja kazi imalizike muone maajabu,
maana mumechokoz nyuki….’akasema sasa akionyesha kujiamini.
Mpelelezi, akasikia amri ikimwambia ajitahidi awezavyo
kumzuia huyo mtu asiendelee na hicho anachotaka kukifanya, kwani mpaka sasa, asilimia
80 ya kurudisha mtambo wao umeshakamilika,na ukikamilika itakuwa vigumu
kuwazuia, na huenda …wakawaua wote waliopo kwenye mitandao yao….’akaambiwa
‘Na binti yangu…?’ mpelelezi akajikuta akiuliza kwa
nguvu.
‘Huyo sasa hivi damu inakauka mwilini…wataionyonya
kama …eeh, yaani wanavyofanya, wanatumbukiza mrija hapa shingoni, kwenye huu
mshipa mkubwa, wanazamisha mpira, wanaanza kuvuta damu…zamu kwa zamu, mpaka mtu
anakauka..anavyolia , ..basi shetani linafurahia..hahahaha…’akasema
‘Bint yangu, atauwawa..kinyama hivyo…’akasema na hapo
hakuweza kuvumilia, hakujua jinsi gani alivyoruka hewani, alimshangaza hata
huyo jamaa, na jamaa hata kabla hajafyatua hiyo bastola alihisi mateke mawili
yakitua mwilini mwake, moja kwenye mkono ulioshika bastola na likingine likitua
kifuani.
Jamaa akarushwa
mzima mzima na kutua juu ya meza, iliyokuwa na komputa kubwa inayoongoza ile
server, ..na baadhi ya vitu juu ya meza vikatawanyika…
'Oooh...what, umefanya nini…..'aliguna na kusema kwa
hasira na mpelelezi hakupoteza muda, akachukua chuma cha kutobolea makaratasi
kilikuw akikubwa akambamiza ncho kichwani..na jamaa hapo hapo akapoteza fahamu.
Na mara mpelelezi akahisi mwili ukianza kuisha nguvu…alihisi
vibaya masikio yanakuwa kama yanazibuliwa…
‘ Kumbuka usipozima hiyo server, ndio itakuwa mwisho
wako na mtoto wako..’sauti ikamwambia..
Hapo
akajitutumua, akipepesuka hadi pale kwenye computa ya server,…
‘Bonyeza kitufe cha ‘delete.’ Akaambiwa, na yeye akafanya
hivyo, lakini hakukuwa na mabadiliko yoyote, …na alipoona huyo jamaa kalala juu
ya meza, anamzuia, akamsukumia chini ya meza, kumbe alidondokea karibu na
ilipodondoka bastola, lakini jamaa huyo kwa muda huo, alikuwa hajazindukana.
Mpelelezi akaona alama inaonyesha ujazo wa asilimia
tisini na tano…..akaambiwa
Aakachukua
kipanya cha komputa, akaanza kukichezesha hadi kwenye sehemu inayoonyesha
muendelezo wa hiyo kazi , akabonyeza sehemu ya kuzuia, ..mara ujumbe ukasema,
una uhakika unataka kusimamisha marejeshe ya kumbukumbu zako
‘Bonyeza ndio’
Akafanya hivyo kwa haraka…, na mara ule ujazo ukaanza
kurudi nyuma kwa haraka na alama za asilimia zikawa zinapungua, mapaka sasa
unakaribia sifuri,…
Sasa kumbe yule jamaa chini keshazindukana,…na
alipofungu macho, cha kwanza kukumbuka ni kazi yake kwenye Server…akajaribu
kuinuka akajigonga kwenye meza, na kumfanya mpelelezi ashituke, na kutaka
kuinama kuchungulia chini,…
Yule jamaa alikuwa tayari kashikilia bastola,
akiielekeza kwenye sehemu ya chini ya mpelelezi, juu mapajani, ina maana
akifatua, anaharibu kila kitu….mpelelezi akanywea, na huku mwili ukianza
kumuishia nguvu…
‘Malizia kazi…’sema ndio..kuna ujumbe unasema kazi ya
kufuta imekamilika je ianzishe komputa, ….haikuwa na maana sana, lakini huyo
jamaa aliyeyepo chini angeliweza kurejesha, kama hatachelewa,…
Kosa alilolifanya mpelelezi, jamaa alipodondoka, hakuichukua
ile bastola…sasa ipo mikononi mwa huyu shetani….na mpelelezi alipojaribu
kusogea akiwa kanyosha mkono kubonyesha kitufa cha ‘yes..’ mlio wa risasi
ukasikika….
NB: Na kwa leo tunaishia hapo.
WAZO LA
LEO: Hata tuwe wajanja vipi, elimu, utajiri,..uwezo wa kuongea,
lakini bado hatuwezi kuingilia mamlaka ya mungu, mola ambaye atakalo liwe huwa,
…hana mshikirika, …Tumuombe mola wetu atujalia maisha mema, yenye baraka tele…Aamin.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment