Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, May 18, 2017

MPENZI WA FACEBOOK-30



 Mpelelezi, akazindukana , na kujikuta kalala sakafuni , na alipomuona mkuu wake yumo humo ndani, akasimama kwa haraka na kuweka nguo zake vyema, kuhakikisha yupo kiaskri,  baadae akasema;

‘Docta umenifanya nini mimi mbona nipo hivi..…?’Mpelelezi aliuliza hivyo, pale alipoona wote wanamuangalia yeye,

‘Nimekufanya nini mimi afande…?’ docta akauliza kama anashangaa.

‘Hata sielewi,…'akasema mpelelezi, akijaribu kutikisa kichwa chake, kuna kitu kilikuwa kikimsumbua, na anajua ni kwanini,...hapo hapo akasema;

'Nahisi binti yangu anaumwa...'akasema

'Kwanini...?' akauliza docta

'Kuna hali..ikinijia najua kuna tatizo...'akasema

'Najua ..nilikuambia, hao watu wamewekeza mambo yako kwenye ubongo wako..wameshakufanya mtumwa, jitoe,..kabla hujachelewa...'akasema docta, na mpelelezi akamtupia jicho mkuu, ni kama vile hakutaka hayo docta anayoyaongea yasikiwe na mkuu wake.

'Mhh...'mkuu akaguna hivyo tu.

'Mkuu samahani, ..nataka kufika nyumbani…’akasema mpelelezi

'Una uhakika...kuwa binti yako yupo matatani, au ni sababu nyingine..'akauliza mkuu.

'Hapana mkuu, hali kama hii..ikinitokea ni lazima nitasikia simu ya matatizo..'akasema 

‘Lakini hawajakupigia simu, au walikupigia kabla sijaingia humu ndani…’akasema mkuu

‘Najua tu mkuuu wakati mwingine mke wangu anajihangaisha mwenyewe bila kuniambia lakini hawezi, ..ni mpaka niwepo, mimi najua jinsi gani ya kumtuliza…’akasema

'Unajua kwa vile..unawajua au sio...wanataka nini, sasa mpaka lini,..sawa mimi nakuruhusu uende, lakini uwe makini...kama ukinihitajia nipo..tumetoka mbali, au sio..'akasema mkuu wake

‘Sawa afande ..nimekuelewa...'akasema mpelelezi sasa akionyesha unyonge fulani.

Alipoondoka, wawili hawa wakajua ni nini cha kufanya kila mmoja akakimbilia kwenye seehmu yake, na kazi ikaanza…

Tuendelee na kisa chetu

*************
 Mzee aliona mkewe anachelewa kurudi, akawa sasa anamtafuta kwa kumpigia simy yake ya mkononi,lakini alishangaa, simu ya mkewe  haipatikani, akahisi kuna tatizo, anakumbuka jana usiku, waligombana sana kuhusu binti yao, mkewe amekuwa akimuona mumewe hafuatilii ipasavyo kuhusu bint yao;

‘Kwanini polisi hawataki tuonane na binti yetu, kuna nini wanatuficha…’akasema mkewe.

‘Mimi sijui, wao wanadai ni taratibu zao za utendaji, huyo binti yetu hatakiwi kuonekana na mtu yoyote kwa usalama wake…’akasema mumewe.

‘Hata sisi wazazi wake hatuna haki ya kumuona binti yetu, mimi hapo sitawaelewa, kama huwezi kufuatilia hili, mimi nitaenda mwenyewe kesho, ni lazima wanionyeshe wapi binti yangu alipo, na ana kosa gani..’akasema mkewe.

‘Mke wangu unafahamu hatari iliyopo, nia na lengo lao ni kuhakikish kuwa binti yetu hafahamiki wapi alipo,polisi wanajua ni nini wanakifanya, je….hutaki usalama wa binti yetu…’akasema mumewe.
‘Kwani ni maswala ya usalama au wao wamemshika kwa kisingizio kuwa huenda anahusikana na hao watu wanaowatafuta…si ndivyo walivyofanua au mimi sielewi hapa, kuna kitu gani unanificha…?’ akauliza kwa hasira.

‘Mke wangu, pamoja na hilo…nia na lengo ni usalama wa binti yetu, hiyo shutuma nyingine ni namna tu ya kuwezesha hili, kwa usalama wa binti yetu…’akasema mumewe.

‘Hapana,…nataka nikamuone binti yangu, waniambie wapi alipo nionane naye basi…hapo ndio tutaelewana nao, vinginevyo, mimi nitafika mpaka kwa wakubwa zao…sitaki maelezo zaidi…’akasema na wakalala hivyo..

Na kweli kesho yake, mkewe aliamuka asubuhi sana na kuelekea kituo cha polisi, kutaka kuonana na binti yao….

Sasa jioni imefika, mke hajarudi,…mume kachanganyikiwa.

Mzee kuona mkewe anachelewa, akaamua kumpigia simu mkuu, msaidizi wa mkuu wa kituo, nia ni  kuulizia, kama mkewe alifika huko, na kama alifika, kama anavyofahamu yeye, mbona hajarudi nyumbani;

‘Hajafika huku…’akasema msaidizi huyo na kumfanya mume mtu kushindwa kuelewa.

‘Oh,…alisema anakuja huko kufuatilia maswala ya binti yetu, kama nilivyokuulizia karibu kila siku, sisi kama wazazi tuna haki ya kuonana naye..mkewe wangu ndio kaamua kuja huko yeye mwenyewe…haniamini…’akasema mume mtu.

‘Ndio nakuambia mzee, mkeo wako hajafika huku..’akasema mkuu huyo.

‘Oh ajabu kabisa…tokea asubuhi na sasa ni jioni, atakua kapitia wapi…’akasema mzee sasa akiingiwa na mashaka.

‘Umempigia simu yake ya mkononi..?’ akauliza mkuu huyo

‘Ndio lakini hapatikani…’akasema mzee
‘Ngoja tusubirie, …kama saa moja hivi…, labda kakwama mahali unajua huu usafiri wetu ulivyo, foleni na…’Mkuu akakatisha maneno, kuna kitu alikuwa kakiona kwenye komputa yake, baadae kidogo, akamuuliza mzee;.

‘Mkewe wako alikuwa kavaa nguo gani..?’ akauliza na mzee akamtajia,

‘Ok, ngoja nitakupigia baadaye kidogo, kuna kitu nafuatilia, sawa mzee, mkeo atakuwa kapitia sehemu nyingine, huenda simu yake imekwisha chaji au kuna sababu nyingine, lakini atakuwa salama tu…’akasema huyo mkuuu kukata simu.

Mzee akabakia akisubiria , kama mkuu huyo atampigia simu, lakini ukapita muda hai usiku sasa unaingia,…akawa sasa anaanza kuingiwa na wasi wasi na mashaka…mwishowe ndio akaamua kumpigia docta;

‘Docta, nina mashaka sana, mke wangu hajarudi, alitoka asubuhi, akidai kuwa anataka kumfuatilia mtoto ..nilijaribu kumkanya hakunisikia, sasa usiku unaingia, hajafika hapa nyumbani, ..sijui yupo wapi…’akasema.

‘Umeongea na polisi,..’akaulizwa.

‘Ndio wamesema nisubirie…’akasema.

‘Basi fanya hivyo, mimi siruhusiwi kuingilia mambo yao,..kama nitapata taarifa zaidi nitakupigia,…’akaambiwa na mazungumzo yakaishia hivyo.

*************
 Docta, alikuwa akifuatilia jambo kwenye komputa yake, akaona kitu kilichomvutia  ni muda kabla hajaongea na mzee, na alipoongea na mzee, akasahau kumuulizia jambo, ndipo alipokumbuka, akampigia tena mzee na kumuuliza;

‘Unasema mkeo aliondoka tokea asubuhi, akitegemea kuja kituo cha polisi kumfuatilia binti yake, lakini hajaonekana hadi muda huu, na simu yake haipatikani, nikuulize kitu kwani mkeo alikuwa kavaa nguo gani…’Mzee akashangaa kuulizwa swali kama hilo tena, na yeye akajibu kama alivyomjibu mkuu.

‘Basi,…ngoja niwasiliane na hawa polisi, tuone watafanya nini…’akasema
‘Nimeshawasiliana nao, lakini majibu yao ndio hayo hayo ,subiria tutafuatilia,nahisi kuna jambo ….’akasema mzee na docta hakutaka maelezo zaidi akakata simu.

****************
Akili yangu ilianza kunirejea, na kujikuta nipo kwenye chumba chenye baridi kali sana, sikuweza kuvumilia ubaridi huo…nikataka kuomba mtu apunguze, lakini hakukuwa na mtu karibu,..na wakati huo huo,  nikahisi naitwa, au kuna kitu kinanisukuma niende…, nitokea humo, bila hata ya kufikiria zaidi,nikafanya kama hisia hizo zinavyonituma, …taratibu kama roboti…

Nikatoka nje,..nilipokutana na mwanga wa  nje niliona kama nipo kwenye sehemu ya jangwa, jua kali…nikatamani nikimbie au nirudi nyumbani,..nyumbani nikiwa na maana hapo nilipokuwepo awali…lakini kitu kingine kilikuwa kikiniambia niende…niende, sijui niende wapi ..nikawa natembea tu, tunapishana na watu lakini ni kama vile hawanioni…

Nikafika nje nikaona bajaji,..nikajikuta naiendea na kuingia ndani ya hiyo bajaji, ilikuwa ni kama inanisubiria…nilipoaingia tu kwenye hiyo bajaji ikaondoka…na ilipoanza kuondoka tu,..nikawa sijatambui tena, na nilipozindukana tena, sasa nikajikuta kwenye chumba kingine cha kawaida,…sasa naona, nahisi …najua kinachoendelea…sio kama njozi, ni kama hali halisi.

Nilisikia watu wanaongea kwa mbali, nikataka kujua ni akina nani, lakini sikutaka wanitambue kuwa nimezindukana,…kwahiyo nikawa natembeza macho, na kuyafumba, hadi nikaweza kujua nipo sehemu gani…ni kama hoteli, hakuna baridi kama kule nilipokuwepo awali…

 ‘Huyu hatufai tena,…muda wake wa kafara na binti ulishapita, hawana maana tena kwetu,…ila hawatakiwi kuwepo duniani, watasema mengi,…watakuja kukumbuka, na itakwua balaa kwetu,… ila yule binti bado anahitajika, kwa shughuli nyingine, tunajua ni nini cha kufanya…yeye bado ni mtu wetu huyo, …’ sauti ikasema.

‘Ama kwa huyo, nahisi kwa muda huu alitakiwa awe amezindukana…huyu mchukueni mkam-malize…hakikisha mnachua baadhi ya viungo vyake, kama nilivyowaambia awali, tunavihitajia sana… mabaki ya mwili wake…tupieni wale wanyama wetu…sitaki ije igundulikane, au kubakia salio lolote, hahitajiki kuzwikwa, muelewe hilo…’sauti ikasema
‘Narudia tena…sitaki makosa, huyo hatumuhitajii tulishaharibu awali, sitaki tena kosa hilo lirudiwe,…binti arudi kwao, lakini hakikisheni, hawezi kufungua mdomo, mnajua ni kwa vipi,..’sauti ikazidi kusema.

Haikupita muda mara nikaona nainuliwa juu kwa juu…nikatolewa mle ndani na kuingizwa kwenye gari, na muda huo nimejikausha tu, kama vile sijazindukana, na wao hawakuwa na muda wa kunichunguza.

Niliingizwa kwenye gari la wagonjwa, na kuwekwa kwa nyuma kama mgonjwa tu, kitanda kilichotengezwa ili mtu usiumie,…walikuwa wanne, wawili wakaingia mbele na wawili wengine kwanza walikuja na kuhakikisha nimekaa vyema, wakatoka na kuniacha peke yangu.

‘Nyi wawili mnatosha kuimaliza hii kazi…’sauti ikasema…na gari likaondoka, tukawa tunakwenda, nikiwa hapo, nikawa nawaza nifanyeje…gari likafika kwenye sehemu kama muinuko hivi likawa linakwenda taratibu…hapo nikainuka, nahisi lilisimamishwa na trafiki,…
 Kule mbele nahisi wote wawili waliteremka kwenye gari, wakawa wanahojiwa ….hapo hapo nikajiinua, taratibu nikafungua mlango wa nyuma, ukafunguka kirahisi tu,…kwa haraka nikatoka,..nilikuwa sina nguvu,…lakini nikajitutumua na kutembea nikiwa najizuia wasije kuniona..

Bahati nzuri kwa nyuma kulikuwa na bajaji inatufauta, sikujali ni watu gani au kama ni watu wao, nikasimamisha, na aliposimama tu, sikuuliza nikaingia ndani, ya hiyo bajaji…
.
‘Tafadhali nisaidie nipeleke makaburini…’nikasema na mwenye bajaji alikuwa karibu aruke kwenye bajaji, sijui alinionaje, lakini akafanya kama nilivyomuambia..akanipeleka hadi eneo karibu na huko makaburini….

‘Tafadhali nipe namba yako ya simu,…nitakutumia pesa yako, nipo kwenye matatizo kidogo nielewe ndugu yangu…’nikasema,  na yeye alipoona nimeteremka, kwa haraka akaondoka na bajaji yake, wala hakunipa hata hiyo namba ya simu.
.
Nikaanza kutembea, ujue sasa akili ipo, lakini bado kuna hali nyingine inanivuta nifaney jambo, …ni hali tofauti na ile ya awali,..naona, nahisi, lakini kiutendaji bado kama namilikiwa hivi,…nikawa sasa natembea kuelekea barabara, inayokwenda kwenye nyumba moja, nilipofika hapo,…nikaanza kukumbuka, niliwahi kufika hapo kabla,…kwa muda huo sikujua ni ya nani…nikaingia..na mara nikasikia watu wanaongea..

Nikatega masikio…nikasikia;-

‘Huyu niliwaambia mkishamumaliza,…damu yake ni muhimu na baadhi ya viunbgo vyake,.. msimpe muda..nipo kwenye tambiko..mkisha muua, damu yake,na vingo vyake mpeni dereva, anakuja,..nyie muendelee na shughuli nyingine, muda…ni muhimu sana…’akasema mtu…nikaikumbuka hiyo sauti, niliisikia kule,…

Nikawa nimejificha, baadae wakatoka watu wawili,..watatu,..mmoja mwanamke, ..walikuwa wamevaa manguo meusi..wanatembea taratibu, wakafika kati kati ya chumba, wakasimama, wakawa wanafanya mambo yao, baadae nikasikia wakisema;

‘Damu ipo wapi…’akauliza wakawa wanahangaika, baadae wakapiga simu

‘Unasema nini haonekani, …siwaelewi…basi mmojawenu nahitajia damu yake hapa mara moja…’akasema kwa hasira huku anatetemeka.

‘Wameharibu…wameharibu tena titafanya nini sasa, ..’akawa anaongea huku anatetemeka, na wenzake wakawa kama wanamshikilia kwa muda, baadae akatulia,

‘Sasa tufanyeje…hili ni kosa la pili, ..na la tatu,ina maana mmoja wetu atakuwa ndiye kafara…mnaelewa ilivyo…sasa mtajichagua wenyewe mmoja wenu au mtoto wake anayempenda…’akasema

‘Sasa tufanyaje..?’ wakaulizana

‘Kwani kwenye wale watu wetu,..hakuna anayefaa…?’ wakaulizana..

‘Binti wa mpelelezi bado anafaa, yupoje, muondoeni ila hali, tunamuhitajia akiwa na hali ya kawaida, kafara lake litakuwa ni tofauti, anatakiwa akione kila kitu, hadi tunamumaliza…yeye ni binti mdogo anafaa sana, hahahaha…’akasema na kucheka..

‘Halafu baba yake yupo wapi..?’ akauliza na kuanza kupiga simu, baadae akatulia, na kusema
‘Na baba yake keshaingia makaoni…ila kwasasa ,haaminiki, inabidi amalizwe kabla hajajua kinachotakiwa kufanyika kwa binti yake…’akasema huyo mtu, alikuwa kafunika uso ..huwezi kujua ni nani..

Baadae wakawa wanafanya mambo yao, na  walipomaliza huyo mkubwa wao akasema;

 ‘Sasa hapo tunapoteza muda, kwanza ni hatari…tutawanyike, tutarudi hapa kama ya …saa kumi…itafaa, najua hapo kila kitu kitakuwa  tayari, kila mtu na muelekeo wake…mimi narudi nje ya nchi…’akasema na wakaanza kutoka taratibu, kila mmoja akawa anatokea mlango wake.

‘Ni nani hawa…’sikukubali, kwa haraka nikatoka kuwafuatilia, sasa nimfuatilie nani, nikaona anayefaa ni huyo huyo kiongozi wao, yeye alitokea mlango wa nyuma,…nikamfuatilia kwa mbali,..sijui kwanini , kuna kama kitu sasa kinaniambia fanya hivi..siogopi…nikamuona akiingia kwenye gari,… nikaipata namba ya gari, halafu lilipoondoka tu, nikatoka kwa haraka nikaingia kwenye bajaji.

‘Umeona gari lilitoka sasa hivi…?’ nikamuuliza

‘Ndio….’akasema lifuatilie , na jamaa, utafikiri aliandaliwa, akasema hakuna shida, kazi ya kulifuatilia hilo gari ikaanza, tulilifuatilia kwa mbali, na tukawa tunaingia viunga vya ndani ndani, …na baadae tukafika kwenye jumba moja, lina geti, likafunguliwa na jamaa akatoka na kuingia humo.

Nikawaza nifanye nini, mara wazo likanijia,…nikaona nipige simu, lakini jingine linasema usipige simu ukipiga simu utaharibu…nikabakia kimia,..sijui ilikuwaje mwenye bajaji akanisogelea na kusema, simu yako bosi..
‘Simu yangu kutoka wapi…?’ nikauliza
‘Sijui…’akasema , basi nikachukua simu na kuanza kuongea na mpigaji akasema;
‘Docta..nakufuatilia, endelea kufanya kama inavyokuelekeza, usijali, tupo pamoja

‘Sawa bosi lakini…fanya ufanyalo ukamuokee binti wa mpelelezi, anatafutwa kuwawa,..na baba yake pia…pili nimegundua jambo, nipo nje ya jumba la ..nahisi ndio huyo mkuu…sijui nifanyeje…’nikasema

 Docta, akasema;

‘Nipo pamoja na wewe, usijali, yote hayo yanafanyiwa kazi..’akasema.
‘Kwahiyo sasa nifanyeje..?’ nikauliza.

‘Wewe kaa hapo hapo, kwenye sehemu ambayo hutaonekana, wewe ndiye king’aumizi chetu..kwa kupitia wewe tunaweza kuliona eneo lote hilo…’nikaambiwa
.
Haikupita muda, jamaa mmoja akatoka akiwa kavalia suti…na kuingia kwenye lile gari,nilichogundua ni sauti yake,kuwa ndio yule yule aliyekuwa akiongoza wenzake, sasa hivi sio yule mtu wa ajabu, sasa hivi akawa  kavalia suti yakiheshimiwa

‘Sasa nifanyeje..?’ nikajiuliza
Hali ikaniambia,…

‘Ingia kwenye bajaji mfuatilie…’nikaambiwa.

Nilichukua bajaji, ..tulilifuatilia hilo gari, lilitembea hadi kuingia mjini, likatembea hadi uwanja wa ndege, na gari hilo halikuingia uwanja wa ndege, liliegeshwa nje ya uwanja wa ndege.

‘Sasa sikiliza…subiria hapa hadi ndege ya saa kumi..atakuja mgeni,…’akasema huyo mtu, na kutoka kwenye gari, akawa anatembea kuingia uwanja wa ndege, sasa hapo nikajiuliza nimfuate au la…hali ikaniambia nisiondoke hapo.

Baadae kidogo,nikamuona yule mtu, akitokea uwanja wa ndege kavalia mawani y giza, nikajua labda atarudi kwenye gari, hapana, hakufanya hivyo, sasa akaita taxi.., wakaongea naye kidogo, mara akaingia kwenye hiyo taxi, ..na kuondoka, na mimi nikamwambia mwenye bajaji, aifuate hiyo taxi..

Tukawa tunarudi kule kule…nikajua wapi wanaelekea, ila ahadi ya saa kumi, inakwenda kutimizwa, ..nikawa najiuliza itakuwaje kwa binti na mpelelezi, moyoni nikajipa tumaini kuwa kama alivyosema docta, wakatalishughulikia hilo, lakini sikuwa na amani kabisa..

Tulipofika maeneo yale ya awali, sasa yeye akateremka, na kuanza kutembea kuingia kwenye jengo la mzee, utafikiri ni la kwake, hakuwa na wasiwasi….na mara yakaja magari mengine na baadae gari la wagonjwa…nikaona mtu akitemremshwa….alikuwa binti…

Wakawa sasa wanaelekea ..makaburini…nikakumbuka ahadi yao ya saa kumi…

NB: Haya sasa kisa kinaelekea wapi,…mtajibu wenyewe

WAZO LA LEO: Katika hali halisi watu tunazidiana vipato,… mali, maumbile nak..hii yote ni mitihani ya mungu, yule mwenye nacho na asiye nacho yote ni mitihani kwetu sote.., kwanini ni mitihani, kwasababu yule mwenye nacho, alitakiwa kumpa yule asiye nacho, kwa ziada aliyo nayo.., lakini je inafanyika hivyo.Mtu anaingia kwenye hoteli anaagiza chakula kingi, anakula kidogo tu kingine kinamwagwa, watu wanatenda mambo makubwa ya kufuru, sherehe nk, anafuja haki ya yule aliyestahki..chakula kingi kinamwagwa, sababu ilikuwa si haki ya huyu mtu, mali nyingi zinaharibika, …mabalaa kwa wingi kwasababu huyu mwenye nacho hajataka kutoa kwa wastahiki, anafuja haki ya mtu mwingine iliyopitia kwake kwa niaba tu,..mola anajua ni kwanini ikapitia kwako, mtihani huu…!

Na huyu asiye nacho, alitakiwa awe na subira, huku akitenda mambo yaliyo mema kwa kufanya kazi kwa bidii, maana ni lazima kila mtu afanye kazi kwa kadri ya uwezo wake, na mola atajua jinsi gani ya kumtimizia haki yake,..kutokana na juhudi zake, anazozitenda kwa haki na kwa wema,kutokana na subira yake bila kuingia kwenye kufuru, kutokana ,..na ucha umungu wake wa kweli…, mola atamruzuku mja huyu mwema, kwa kadri mola ajuavyo yeye,…tena kutoka kwa yule mwenye nacho, lakini je subira hiyo ipo..huu ni mtihani kwatu sote. Tumuombe mungu atujalie tuwe wacha mungu wa kweli
Ni mimi: emu-three

No comments :