Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Saturday, May 6, 2017

MPENZI WA FACEBOOK-23



‘Mke wangu uwe na subira, kiukweli tupo kwenye matatizo makubwa, sijui nia ya hawa watu nini…' huyu alikuwa mzee akiongea na mke wake ili kumshawishi , binti yake achukuliwe na watu wa usalama, haikujulikana wanachukua kwa madhumuni gani.

'Mke wangu, mimi sijui nimewakosea nini hawa watu…wangeniambia wanataka nini niwape lakini tuzidi kumuomba mungu tu…sasa nakuomba sana mke wangu uniamini..hebu twende nje kidogo, nataka kukuagiza jambo…’akasema na wakatoka nje.


Mimi nilibakia peke yangu , baadae nikapokea ujumbe wa maandishi kutoka kwa docta, alikuwa akiniagiza mambo fulani fulani ya kufanya, …haraka haraka nikaingia chumba cha mabinti, …nikaanza kutafuta hicho alichoniagiza docta;

'Laptop...'

'Ndani ya laptop hiyo niligundua mambo mengi, na ..mojawapo ni kuwa huyo marehemu alijiua kwasababu ya kunipenda...alipoona nina mtu mwingine, na hapo hapo ana mimba, akachukua hatu ya haraka ya kujiua..ndivyo, niligundua, lakini kutokana na maelezo ya laptop,

Lakini sigundua kuwa , kumbe yote hayo, maagizo yote hayo, yalikuwa ni mtego,..mtego wa kuninasa mimi,na kuinasa hiyo laptop, niligundua hayo nikiwa nimechelewa, kwani baadae nilikaribia umauti..

Tuendelee na kisa chetu....

****************** 
 Docta akiwa kituoni, …ni kituo maalumu cha polisi, alihisi mambo sio mazuri,..hakuelewa ni kwanini alikuwa akihisi hivyo, hakutaka kupiga simu huko kwa mzee, kwa tahadhari, lakini kutokana na hiyo hali, ikabidi kwanza ampigie simu msaidizi wake, lakini simu …haikupatikana…, akashangaa, sio kawaida yake, akajaribu tena na tena, hakuweza kumpata msaidizi wake!,  akaona sasa ampigie mzee, na yeye pia simu yake ikawa haipatikani,…

'Mhh,…hapa kuna tatizo, sio bure, hii sio kawaida..nahisi kuna tatizo, sizani kwamba askari walitoa amri watu hawa wazime simu zao, sizani…'akasema akijaribu kupiga tena , na tena, lakini simu zikawa hazipatikani!
Alitaka ampigie simu afande, mkuu wa zoezi hilo ambalo ni la siri kidogo, lakini akilini akaona sio vizuri, kwani kinachoendelea hapo ni hisia zake tu,..

‘Sasa nifanyeje, na muda….muda ni kitu muhimu sana..’akasema

Baadae akamuendea askari wa hapo kituoni, walikuwa sio kwenye kituoni cha polisi hasa,  ni sehemu nyingine  malumu ambayo haitambulikani kama kituo, ila huyo mkuu wa hilo zoezi, aliichagua sehemu hiyo kama kituo maalumu chenye usalama, kwa dharura kama hiyo..na kwa muda ule, Docta alikuwa kabakia kwenye hiyo nyumba ikiwa na walinzi wawili tu. Mlinzi mwingine akaomba kutoka kidogo, akabakia mlinzi mmoja.

Docta akiwa kwenye chumba chake,,…ndio akawa anahangaika kumpigia msaidizi wake, na kwa upande mwingine wa chumba ndipo alikuwa kawekwa huyo binti! Chumba alichokuwa kawekwa huyo binti , kilikuwa imara, na kilifungwa kwa nje..

********

Inavyoonekana mkuu wa zoezi hili aliamua kuchukua hatua hiyo baada ya docta kumuendea na  kumuelezea hiyo kadhia nzima, ya kuuwawa kwa binti wa mzee, na matukio yaliyokuja kutokea baadae,

‘Ni kweli nimesikia taarifa hiyo kutoka kwa mkuu, lakini mkuu anasema , kifo ch ahuyo binti ni mambo ya kimapenzi, wivu….na akanywa sumu..hakutaka kunielezea zaidi…’akasema msaidizi huyo.

‘Lakini ni zaidi ya hayo afande, mimi nililigundua hilo nikiwa kwenye kazi zangu za udakitari kama nilivyokuelezea, na nimegundua kuwa kuna tatizo kubwa,..na huenda likazidi kuwa kubwa,…kama mlivyoona, haya..biashara hiyo ya viungo vya binadamu, sio kitu cha kawaida…’akasema

‘Ndio maana nimetumwa kuja hapa..tutalimaliza hilo, nakuhakikishia…’akasema msaidizi huyo.

Docta aliamua kuonana na huyo msaidizi badala ya mkuu mwenyewe ambaye alikuwa katoka kidogo kikazi, na akaona huyo anaweza kuifanya hiyo kazi zaidi ya mkuu wake, kwani hata hivyo, alishafikia hatua ya kutokumuamini huyo mkuu wa hapo,..hasa kutokana na jinsi alivyoelezea mzee, na hata kwa hisia zake mwenyewe docta, aliwahi hata kumuambia mzee, kuhusu hisia zake hizo

 ‘Kuhusu hili tatizo, hakuna mtu wa kumuamini, kwasababu tatizo hili, limegubikwa na watu wenye pesa, watu wenye imani kazi za giza, za utaalamu wa hali ya juu, na wanatumia vitendea kazi vya kisasa, na yote hayo wao wanayafanya kwa ajili ya pesa,…ni wtu hawajli kuua,..wanakula nyama za watu, …damu n.k..ni binadamu wa ajabu sana..’docta akamwambia mzee.

‘Umeyajuaje hayo yote..docta?’ akauliza.

‘Wakati wengine wanalala,…mimi napitia makabrasha mbalimbali...nawasiliana na wenzangu huko ulaya, unajua huu uchunguzi wa kuoanisha mambo haya ya sayansi na sayansi jamii,..inayohusiana na matatizo ya akili, siyafanyi peke yangu..’akasema

‘Ok, kumbe…’akasema mzee

‘Ndio, nipi mimi na wenzangu huko ulaya, na wao wanaifanyia kazi hii, kuna wachunguzi wameenda huko Nigeria,…huko ndipo kwenye shida zaidi ya mambo haya, na mwisho wa siku tutakutana tuunganishe uchunguzi wetu,..halafu mimi mwenyewe bado naisomea hii kazi ili kupata ujuzi zaidi,…hii ni moja ya masomo yangu,  nafanya uchunguzi usiku na mchana, ..natumia muda mdogo sana wa kulala, ..na kwa ajili hiyo nimeweza kugundua mambo mengi sana…hasa kuhusu hawa watu..’akasema.

‘Na kuhusu huyo mkuu wa kituo hicho hapo mbele, …kiukweli mimi simuamini, sina ushahidi wowote dhidi yake mungu anisamehe tu, , ila kwa jinsi nilivyoongea naye awali na kwa jinsi alivyolichukulia hili jambo, sikumuelewa, na hapo hapo akanitoka,..hili sio tatizo dogo, sijui kwanini hakulichukulia maanani…’akatulia kama anawaza jambo.

‘Kiukweli hata mimi docta, …huyo mtu kanitoka, …alivyolichukulia tatizo la kifo cha binti yangu, sikumuelewa hadi leo, unajua ilifikia mahali nikaamua nifanye uchunguzi wangu mim mwenyewe..nimehangaika, nikapata fununu fulani..’akatulia.

‘Wewe uligundua nini hasa..?’ akauliza docta.

‘Ni likuja kugundua hivyo hivyo, kuwa kuna genge la watu wanatumia vitisho,…wanawarubuni mabinti…wanawaingiza kwenye biashara haramu…na mabinti wengi wanajiingiza tu, wakipata matatizo wanaoumia ni wazazi…kiukweli, awali sikuliamini hili, mpaka liliponikuta mimi…’akatulia.

‘Lakini mzee, unahisi binti yako na yeye aliingizwa huko, …?’ akaulizwa

‘Sasa huo ni ugunduzi wangu, nisingeliweza kuhakiki hilo jambo moja kwa moja, ila nikaona niwaone hao watu wa usalama tuone kama wanaweza kunisaidia,..na kingine ni kuhsu hii mitandao,…hii mitandao ya kijamii, inawaharibu sana vijana wetu, na humo wahuni wameingiza mambo yao…’akatulia

‘Ehe…kama yapi..?’ akauliza docta.

‘Unajua niliwahi kushuhudia tukio moja wanapigisha video za uchi…ni mbaya mbaya, wanasema wanatengeza video za kuuza,..hivi tumefikia huko…sasa angalia wanaosimamia mambo hayo..sio sura zetu, sio watu wa maadili yetu ni kama wametumwa kuja kuharibu…’akasema

‘Umeonaeeh…’akasema docta

‘Mimi nikamuendea huyo mkuu nikamuelezea wee, nikajua labda kanielewa,  lakini hakufuatilia, ila alisema atafuatilia, ..na kuhusu tatizo la mtoto wangu nikamuelezea ni navyo hisi kuwa kwanza tumpate huyo aliyempachika mimba, huyo huyo anaweza kuusaidia, tukimnasa huyo, tukamshikisha adabu tutalimaliza hili tatizo,..’akasema sawa..nikuambie kitu iliishia hapo hapo..ndio nikaamua kulivalia njuga mwenyewe

Nikapata taarifa nikamuendea, nikajikuta sasa mimi nipo matatani,  maana nilienda nikamueleza nilichokigundua, unajua alinisema vibaya ana, akaniambia, naingilia kazi yao, na sasa niifanye mimi mwenyewe na kitakachonipata nisije kumlaumu,…’akatulia.

‘Umeonaeeh, hiyo kauli,, kwa nini alisema hivyo...?' akauliza docta.

'Alinieleze kidogo, kuwa hao watu, kuua kwao si mchezo, wana pesa, na wana elimu ya kujilinda, lakini pia wanatumi anguvu za giza, wanaweza kufanya mambo makubwa ya kumuharibu mwanadamu hata kwa kutumia mitandao...akaniambia hivyo...'akasema mzee

'Halafu ...?' akauliza docta

'Akasema ndio maana yeye analifanyia kazi hilo kwa makini ili aweze kulinasa kundi na kupata ushahidi wa kutosha…'akasema.

'Sasa...?' akauliza docta.

'Sasa...ndio miaka mingapo imepita, hakuna lolote, nikajua anatafuta njia tu za kupoteza muda, ...'akasema

'Unajua kauli yake ya lugha za kukutisha, ina maana fulani, yawezekana alishagundua kuwa kuna watu wabaya, …au anajua jambo kama hilo, ila kuna kitu kinamfanya ashindwe kuchukua hatua,  sasa ni kitu gani,... pesa labda, au shinikizo fulani,.., au  …anyway, tusimshuku vibaya kihivyo, sasa najiuliza ni nani wa kutusaidia hapo…maana inavyokwenda inabidi tuwashirikishe watu wa usalama haya mambo ni nyeti sana..’akasema docta.

‘Hata sijui…’akasema mzee.

‘Sasa tutafanyaje, maana kiujumla hili sio tatizo dogo, na kama kweli unataka hili tatizo liishie, inabidi tulifanyie kazi hasa, jiulize kwanini wewe, una nini kikubwa mpaka wakaingia familia yako…, hii ina maana kubwa sana, kuwa wewe kwako, kuna mdudu mtu anaitafuna familia yako, anakujua ,na anamasihali ya hilo jambo, sasa sijui ni nani, …sijui unanielewa.., na tunapokwenda ni lazima polisi wahusishwe,…’alimwambia mzee.

‘Nakuelewa sana, lakini sizani kama ni ndani ya familia yangu, hilo halipo ila, huyo marehemu, mlinzi nahisi ndiye yeye, maana mimi nilimuamini sana, nilikuwa namuambi akaribu kila kitu, lakini mungu kamuumbua, umeona,..sasa nakuuliza mimi nifanyeje…’akasema

‘Mimi kwa ushauri wangu, ni lazima hili jambo tumpate polisi ambaye atalifanya nje ya polisi..sijui unanielewa hapo..ni kuwa ni kweli polisi wetu ni wazuri lakini anaweza kuwepo mmojawapo mbaya anatumiwa, kwahiyo hata tufanyeje, ..kila hatu taarifa zinavuja na hao maadui wanazidi kutenda makosa..’akasema docta.

‘Lakini utafanyaje hilo, ..bila mkuu au watendaji wake wengine kujua.

‘Mkuu wa kituo, asihusishwe,..hilo linawezekana sio mambo yote anayajua…, lakini matokeo yake yatakuja kuingia ndani ya polisi baadae na yeye atajulishwa rasmi baadae wakati kazi imekwisha fanyika,,,…

‘Sasa kwa vipi maana hapa kichwa kimechoka..’akasema mzee

‘Ndio maana nataka mimi na wewe tushirikiane kwa hili, maana linaweza kuifanya familia yako ikakuchukia,..lakini baadae wataelewa tu…na siwezi kuiacha hii kazi, maana kama nimeianza hii kazi , nikiiacha na mimi nitakuwa hatarini, na ni seehmu ya project yangu, ni kitu muhimu sana kwangu…’akasema docta

‘Kwahiyo tufanyeje..’mzee akazidi kuuliza

‘Nataka kumpata askari ambaye unamuamini, kati yao , lakini kiongozi ongozi hivi,,,wana viongozi wao sio sasa mmojawapo ambaye anaweza kutoa amri kwa watendaji wake wawili , watatu…’akasema.

‘Mhh..hilo hata siwezi kukuhakikishia,…labda huyo mgeni msaidizi wa mkuu, nahisi tukimtumia huyo, anaweza kuaminika,..ila ..kama anawivana na mkuu wake tutakuwa tumelikoroga,bado itakuwa kazi ngumu…’akasema mzee.

************

 Ndio hapo, Docta akamuendea huyo msaidizi wa mkuu wa hicho kituo cha polisi akamuelezea kadhia nzima, na huyo msaidizi wake, akamwambia;

‘Unajua ndio maana nimehamishiwa hapa, na kiukweli sijapata ushiriakiano wowote na mkuu wangu, ..ndio nimekuja na yeye akakumbwa na matatizo y akifamilia, kwahiyo bado sijaweza kukaa naye tukaliongelea, au kuongelea matatizo mengi ayaya hapa, nimekuwa nikipitia kesi mbali mbali,..na mojawapo ni hiyo…

‘Kiukweli nahisi hapa kuna tatizo kubwa…, niliambiwa nilipopata barua ya uhamisho wa kuja hapa na wakuu wangu..huko juu.., nia  kubwa ni kuweza kulisafisha eneo hilo na matatizo mengi yanayotokea hapa, hasa hili, la..imani za kishirikina na kuuza viungo vya binadamu kwa imani hizo, madawa ya kulevya..ujambazi wa hali ya juu…imewatia mashaka wakuu huko na utendaji wa hapaa…nakuambia hili, ..kwa madhumuni maalumu..’akatulia

‘Nakuelewa sana afande..’akasema docta

‘Ninachotaka mimi , nikushirikiana na raia wenye nia njema, ili tuweze kuligundua tatizo, na hasa kiini cha hili tatizo,..ni nani yupo nyuma ya haya yote, ni tatizo na hatutaiweza mpaka kushirikiana na raia,..’akatulia kidogo.

‘Mimi hapo ndio nakosana na mwenzangu, mimi utaratibu wangu wa kazi ni kuwa karibu na raia, najua kutokana na wao nitaweza kuwagundua wahalifu,maana wanaishi nao, wanawafahamu..sasa nashukuri kuwa wewe umekuja na wewe ni docta, wanatu mnaoaminika kisheria…tutashirikiana kwa hili..’akasema.

‘Kwahiyo kwa hili utanisaidiaje..?” akauliza docta.

‘Nitakuambia cha kufanya, …kuna hatua nitazichukua kiutendaji siwezi kukuambia moja kwa moja ni zipi…lakini kuna hatua za dharura, lakini zinaweza zisiwe rasmi…baadae utaona matokea yake, wahalifu wote wa eeneo hili watakamatwa tu…ni kazi ndogo wewe utaona tu, najua tatizo la eneo hili ni kuwa wapo watu wana uwezo wa pesa, na hawa ni hatari,lakini tutapambana..’akasema

‘Nitashukuru sana afande,…sasa mimi nifanye kwa sasa, nikae tu, au niendelee na hicho nilichokianza, kwasababu kama nilivyokuambia hata mimi, nipo kazini nahis utanielewa nikisema hivyo, lakini siwezi kuifanya hii kazi yangu bila kuwahussiha nyie, je unaniruhusu..?’ akauliza docta.

‘Kwanza nikushuru sana,..umefanya jambo kubwa na la hatari, sasa nitakuwa na wewe sambamba..tutashirikiana kwa badhi ya mambo,..nitakuelezea cha kufanya, lakini sio hapa kituoni, tutaonana mahali..’akasema huyo mkuu

Na docta akakutana na huyo afande baadae nje ya kituo, wakashauriana, na lakini hatua zaidi hakuambiwa aliambiwa yeye asubiria na afuate kile atakachoambiwa, hata kama kitaumiza hiyo familia. Na ndio tukio hilo likatokea.

********
 'Nahisi huko kwa mzee kuna tatizo, hizi hisia sio bure,..’docta akawa anawaza akili haitulii, na wakati anawaza hivyo muda huo yupo peke yake, na alipoona hisia hizo zinamcheza chez asana kichwani, akaona asipoteze muda zaidi, kwa haraka akamuendea mlinzi aliyebakia hapo, akamuambia alivyohisi.

'Kwanini, unahisi hivyo, hakuna shida, kaam kungelikuwa an shida wangelikupigia, au wangewaarifu polisi, usiwe na dhana mbaya…?’ akasema huyo askari akionyesha kuwa kachoka na usingizi.

'Nimepigia simu kwa msaidizi wangu hapatikani, simu ya mzee halikadhalika..haipatikani, nahisi kuna tatizo, hisia zangu haziongopi afande…’akasema docta.

‘Kwanini unahisi hivyo, na watu wapo nyumbani kwao,  kama kuna tatizo watapiga wao, na simu kuzima labda ni mtandao au umeme, si unajua umeme wetu huu wa kuunga uunga,..’akasema.

'Niamini mimi afande na tusipoteze muda…huko kuna tatizo, sasa usije kudharau ukaja kujutia, au nimpigie mkuu wako niongee naye mimi mwenyewe..’akasema docta.

‘Sasa ulitaka mimi nifanyeje,… mimi nimepewa kazi ya kuhakikisha mpo salama, na msitoroke,…kazi nyingine hainuhusu mimi,… ok,…au niambie ulitaka mimi nifanyeje…’akasema

'Hapa hakuna jinsi,..ufanyeje , wewe endelea na ulinzi wako, lakini mimi inabidi niende huko..nikajionee mimi mwenyewe, ujue mimi ni docta wa hiyo familia, na ninajua matatizo yao, inawezekana kuna tatizo, haiwezekani namba zao wote zisifanye kazi…’akasema docta

'Lakini huruhusiwi wewe kuondoka hapa unaelewa,…sio kwamba sikuelewi, ila natimiza wajibu wangu,..unakumbuka, mkuu wangu wakati anaondoka hapa ulisikia maagizo yake, sasa wewe unataka kunifukizisha kazi, ..’akasema

'Mpigie bosi wako umueleze hali halisi,..na mimi  niliwaambia muweke mlinzi pale nyumbani kwa mzee, nyie mkadharau, mkasema hakuna tatizo kubwa kiasi hich kwenye hiyo familia, sasa matatizo ndio haya yanaanza..’akasema docta.

'Ok,..ngoja niongee na bosi..’akasema na kuchukua simu yake ili ampigia bosi wake, alifanya hivyo shingo upande;

'Ongea naye, lakini wakati unaongea naye,  mimi ninaondoka, cha muhimu kwako, ni kuhakikisha usalama wa huyo binti, na akizundukana hapo, ..ninajua kabisa itakuwa mshike mshike, ..si umeona mwenyewe alivyo huyo binti, …imebidi tumpige hiyo sindano ya usingizi kwa ajili ya kumtuliza, na hatuwezi kumpiga tena sindano ya aina hiyo , sasa uwe makini…

'Hebu kwanza unajua simu yangu hii,….mmh, lakini hebu kwanza nikuuliza, kama akizindukana na akaanza kusumbua, tutafanyaje…maana ooh, nimechoka kweli, bosi hataki kumleta mtu mwingine, na mimi nikapumzike kidogo, unajua leo siku ya tatu, sijapata kukiona kitanda …?’ akauliza huyo askari, akionekana kachoka kweli, kiukweli huyo askari alikuwa kachoka, alikuwa kafanya kazi muda mrefu bila kupumzika, ilibidi aje askari mwingine kumpokea.

'Wewe ni askari,… huwezi kuniuliza swali kama hilo, ila angalizo kwa huyo binti, huyo binti bado ni mgonjwa, msije kutumia nguvu yoyote, na jingine anaonekana ni mjanja sana, ole wako akuhadae halafu atoroke, …huyo binti kwasasa ni alimasi, anatafutwa na hao watu..’akasema docta.

'Nimekuelewa, ..'akasema huyo askari huku sasa akianza kumpigia bosi wake simu. Na wakati askari huyo akifanya hivyo, docta hakusibiria, haraka haraka akatoka nje, na mbio mbio.., akaelekea kituo cha bajaji.

Huku anatembea huku mawazo tele kichwani…

‘Sasa itakuwaje, huku  huyu binti anahitaji uwepo wangu, hataweza kutulia kama akiniona sipo, na hawa watu hawaelewi tatizo hili lilivyo gumu, hawa watu nimeshawafahamu sana, ni hatari…na huyu binti kwa hali yake, hatakiwi kuongezewa shinikizo la ziada, anaweza kuzidiwa, na kupoteza fahamu tena, na ni hatari ikitokea hivyo mara ya pili, mmh, huu sasa ni mtihani..’akawa anawaza huku anatembea.

‘Na pia nikifika  huko kwa mzee…najua kabisa mama akiniona tu, cha kwanza atauliza kuhusu binti yake,  na kwa hivi sasa hata mimi sijui kinachoendelea, hawa maaskari hawataki kunieleza ,,mmh sasa huyu mama  nitamuambiaje…na hali kama hiyo itazidi kumsononesha baba, ambaye hahitajii mawazao zaidi…inabidi nitafute njia ya kulituliza hili …’akawa anawaza huku anatembea.

'Labda ningewaambia askari wafuatilie  wao wenyewe…hapana kwa jinsi ilivyo…, hili jambo sio la kuwaachia maaskari wengine litavuja, na mkuu akijua kinachoendelea kabla hatujapata ushaidi anaweza kunifunga, na hawataelewana kabisa na msaidizi wake…kwahiyo, ngoja niende huko huko, kwa mzee..’akajipa moyo huo..na sasa akawa keshafika kituoni.

Docta akaingia kwenye boda boda, moja kwa moja hadi kwa Mzee.

Alipofika kwa mzee, akawa anasita hata kupiga hodi, kwanza alihitaji atahadhari, maana hajui kinachoendelea huenda wanafamilia hao wamewekwa chini ya ulinzi, na watu hao wasiojulikana, kwahiyo kwanza alichofanya ni kuvinjari, kukagua na alipojirizisha, ndio akausogelea mlango.

Hakugonga, akafungua kwa haraka, oh, …,aliwakuta wanandoa wawili hao mzee na mkewe, wakiwa wamekaa sebuleni, …na hali aliyowakuta nayo, inaashiria kuwa kuna tatizo, la kutokuelewana au vinginevyo,  maana mama alionekana  kanuna kweli, baba yane kaka kwenye sofa, lakini hakuegemea, ila kainamisha kichwa chini…na docta alipofungua mlango tu, wa kwanza kusimama alikuwa mama;

'Binti yangu yupo wapi?akauliza mama huyo mama, akiwa na macho yenye kuhitaji kupata jibu la haraka.

'Bado yupo kituoni, mimi.nimeomba ruhusa tu mara moja,…’akasema docta akigeuka huku na kule, kama anatafuta kitu, na alipokikosa akasema

‘Msaidizi wangu yupo wapi..?’ akauliza

'Hatujui…’wakasema wote kwa pamoja mke na mume, na docta akazidi kuchanganyikiwa, akatizama saa, halafu akasogea hadi dirishani akawa anaangalia nje, …halafu akawageukiwa wawili hao na kuanza kuwahoji maswali;

‘Mama yeye hakutaka kuulizwa akakimbilia ndani huku akilia;

‘Binti yangu binti….’

NB: tunaendelea sehemu ya pili yake ya tukio hilo, kwenye sehemu ijayo


WAZO  LA LEO: Msomi mnzuri ni yule , kutokana na elimu yake, jamii, inapata faida, na sio hasara, jamii inajifunza kutoka kwake, kwa mema na sio mabaya. Elimu ya mapokeo isiyo na tija kwa jamii, inakuwa sio elimu, bali ni ujuzi tu wa kuongeza jambo katika akili zetu, sasa basi tufikie hatua tuone kuwa elimu yetu inakuwa ya vitendo, yenye tija kwa jamii, isiwe ya vyetu, au kuhesabu kidato, iwe ya kuelimisha, kuleta mabadiliko yenye maana , kuzalisha na kuleta matunda yenye faida kwa jamii.
Ni mimi: emu-three

No comments :