‘Sawa,…mimi nipo tayari, kushirikiana na nyie, mkiwa tayari mniambie, nipo chumbani kwangu mara moja..’binti akasema akiondoka
kuelekea chumbani, na mimi na docta tukabakia pale, na docta akaninong'oneza akisema;
‘Binti anajua jambo…na
hivi sasa huenda anawasiliana na hao watu, najua kwanini anafanya hivyo, lakini
tumpe muda, hata hiyo ya kusema atashirikiana na sisi, sio kweli anachofanya ni
kuvuta muda,…sasa sijui kwanini, kuna hii namba walimpigia, nataka tuipige , tujue
ni nani kabla hajawasiliana nao..mimi natoka kidogo,...’akaniambia kwa sauti ya chini, na kuanza
kutoka nje, mimi nikabakia
Haikupita muda, mara binti akaja akiwa katokea chumbani kwake, alionekana mwenye haraka, na akatuangalia, akagundua kuwa docta hayupo, akasema;
‘Docta kaenda wapi…?’
akauliza akionyesha wasiwasi mkubwa
‘Yupo kaenda
kujisaidia…’nikasema
‘Hapana
nimeshamjua,….kachukua namba ya simu anataka kupiga, kumpigia..hapana asifanye hivyo, ataharibu…’akasema sasa akitaka
kutoka nje
Baba alieyekuwa kimia akasema;
‘Wewe binti niambie kuna
nini unaficha…’baba yake akasema kwa ukali, binti alishafika mlangoni akasema kwa sauti ya huzuni
‘Baba usiwe na wasiwasi, hakuna kitu ninaficha, usinielewe vibaya baba, ili uelewe kuwa, nayafanya haya kwa ajili yenu, nawalinda nyie…baba hawa watu sasa ni hatari kwetu., …’akasema huku akikimbilia nje, baba
akamuangalia mkewe, kama anataka kumuuliza kitu.
Mkewe akawa kamuangalia mumewe kama anasubiria kuulizwa kitu, na alipoona mumewe hasemi neno, hakupoteza muda tena..huyoo..., mbio akamkimbilia mtoto wake kwa kutoka nje…..
Baba naye kuona hivyo, akaijiinua, na haraka akawafuata huko nje..nikabakia peke yangu...
Tuendelee na kisa chetu..
***************
Hata mimi sikuweza
kuvumilia, ikabidi na mimi niwafuatilie huko nje, na niliwakuta wote wamesimama,
binti akionekana mwingi wa mashaka, akiwa bado anaangalia huku na kule
akimtafuta docta,… na wazazi sasa walishamkaribia, na kuanza kumsihi arudi
ndani, atulie, na mimi nilipofika pale waliposimama, nikamuuliza huyo binti;
‘Kwani wewe una mashaka
gani,…sisi tunachotaka ni kuutafuta ukweli, na kama ni madhara tutayapata sisi,
docta keshakuhakikishia kuwa mambo atayamaliza unawasiwasi gani, au kuna jambo
unalolifahamu, ..’nikasema
Yule binti akatulia tu
hasemi jambo, zaidi ya kuendelea kuangalia huku na kule na alipohakikisha kuwa
doct ahayupo karibu akageuka kunikabili…akaniangalia kwa macho yenye hasira,
hakusema neno.
‘Haya twendeni
ndani…’akasema baba mtu, yule binti kwanza akawa katulia, sasa akiwa kageuka
upande wa barabarani,…akawa kama hataki kurudi ndani.
‘Kwani unataka nini
sasa…?’ akauliza mama yake
‘Nimesema twendeni
ndani, …’akasema baba sasa kwa sauti ya ukali, na mdada akawa anageuka kama
kuelekea ndani, na mama yake akasema akimuangali abinti yake..
‘Twende ndani unamjua
baba yako keshabadilika hapo, unataka adondoke chini kwa hasira, …twende
ndani…’akasema mama.
‘Mama nakuja wala usiwe
na shaka na mimi, na wala baba hatadondoka,…ila ni muhimi ningelijua huyo docta
anataka kufanya nini, …’akasema sasa wakawa wanatembea hatua ndogo ndogo
kuelekea ndani, lakini mwendo wa pole.
‘Hebu niambie kuna
tatizo gani..?’ akauliza mama.
‘Mama hakuna
tatizo…..usiwe na shaka na mimi…’akasema na mama yake akasema;
‘Usinidanganye binti yangu
ninakufahamu zaidi ya unavyojifahamu wewe, ukijiigiza ukiwa sawa, mimi
nakufahamu, una tatizo, una kitu kinakusumbua, sasa usipotuambi asisi wazazi
wako, unafikiri, ..’akasema mama yake na
kabla mama hajamaliza binti yake akasema sasa akiwa kasimama;
‘Kwahiyo mama wewe
ulitakaje, maana mimi sio kwamba napenda haya, …ila ni kwa ajili yenu nawapenda
sana wazazi wangu…siwezi nikakaa kimia wakati kuna watu wana nia mbaya,…mimi ni
mkubwa sasa, ni wajaibu wangu kuhakikisha kuwa familai yetu ipo salama, haya
yaliyotokea kwenye familia yetu yananitia uchungu sana, kwanini sisi, kwani
tumewakosea nini hao watu…’akasema kwa sauti kubwa halafu akashusha na kuongea
kwa.
‘Sasa kwanini hutuambii
tatizo ni nini…ili tusaidiane…?’ akauliza mama.
‘Mama hakuna tatizo,…la
mimi . ila nahisi nyie mnalitafuta
tatizo, na mimi siwezi kukaa kimia, hawa watu wawili watatuingiza kwenye
matatizo makubwa sana…, nimefurahi kuwa wametusaidia tumepona, lakini huko
wanapotaka kwenda, naogopa..’akasema.
‘Kwenda wapi sasa..wao
wanachokifanya ni kile ambacho tulikuwa tukikihangaikia kwa muda mrefu,…mnakumbuka
mimi niliwaambia nini, haya yaliyotokea tumuachie mungu, wewe na baba yako
mkasema ni lazima tuutafute ukweli…mnaona sasa, ..kwahiyo matatizo mliyaanza
nyie, wewe na baba yako…’akasema mama.
‘Lakini mama,
tusingeliweza kukaa kimia,…ilikuwa ni wajibu wetu kufanya hivyo…na hata hivyo
…hatuwezi kutulia, nilikuwa na mpango wangu wa amani, wa taratibu, lakini hawa
watu wawili wamekuja kuharibu…’akasema akiniangalia kwa jicho moja.
‘Lakini kwa vipi, wao
wamekuja kusaidia kumtafuta yule ambaye alisababisha binti yetu ajiue, sasa
njia ya kufika huko ndio hii imetufikisha hapa binti yangu, je wewe unataka
tuliachie hivi hivi, na wakati limeshafikia hapa,..’akasema mama.
‘Sasa kwa vile inazidi
kutupeleka kubaya, basi tuachane nayo, kwani mwisho wa siku tutakaoumia ni
sisi,hawa watu watakuwa hawapo,…wao wanachotafuta ni pesa,…unasikia mama, …mimi
najua, lolote tutakalo fanya halitasaidia dada arudi,…hawezi kurudi,
tumeshaombeleza vya kutosha, tumeshateseka vya kutosha, basi ….lakini hivi
wanavyotaka hawa, mama kuna hatari huko mbele wewe hulioni hili..’akasema
‘Sawa twendeni ndani,
tusiwape watu faida…’akasema baba ambaye alirudi na kumsikia binti yake
akiongea, na aliposema hivyo akarudi ndani tena, na sasa mama naye akaelekea
ndani, mimi nikabakia na huyo binti…na nilipona tupo peke yangu, nikamuuliza huyo
binti swali;-
‘Nikuulize swali, hivi
wewe unakubali kuwa dada yako alijiua mwenyewe..?’ nikamuuliza.
‘Si ndivyo
ilivyoonekana, ..’ akasema kwa sauti ya ghadhabu kama vile ninamsumbua.
‘Nyie mlikubaliana na
hilo..?’ nikamuuliza na sasa akainu auso na kuniangalia kwa macho yaliyojaa
hasira, akasema;
‘Haya wewe niambie
alikufaje,..nyie si madakitari, au labda nyie ni wanajimu au waganga wa
kienyeji, tuambieni… mumegunduaje kuwa kama alinyweshwa sumu, ni nani
alimnywesha, au hiyo sumu iliyonekana kwenye vipimo ni ipi, ..ni nani
angelimuewekea maana siku nzimi nilikuwa mimi na yeye, alipokwenda huko
chumbani kwake, ndio yakatokea hayo..’akasema.
‘Nikuulize kitu, nyie
mnalalaje,…yeye ana chumba chake na wewe una chumba chako au sio?’ nikamuliza,
kwanza alitulia kama vile hataki kujibu swali lakini baadae akasema;
‘Awali…tulikuwa
tunachangia chumba kimoja..nyumba ina nafasi ya kila mtu kuwa na chumba
chake,…lakini mara nyingi tulikuwa na wageni, wanandugu, kwahiyo tukawa hivyo,
kulala chumba kimoja, tukazoea hivyo… lakini vinginevyo, kila mtu ana chumba
chake..’akasema.
‘Siku ya tukio, hakukuwa
na wageni, kwahiyo kila mtu alikuwa akitumia chumba chake au sio…?’ nikauliza.
‘Ndio…’akasema sasa
akijibu kwa sauti ya kawaida.
‘Na ilipotokea tatizo,
wewe ndiye uliambiwa uonyeshe dawa mlizonunua madukani…?’ nikamuuliza.
‘Ndio…’akasema.
‘Ukawapa polisi karatasi
ambayo sio yenyewe…’akasema.
‘Sikugundua kwa wakati
ule, maana vikaratasi vyote viliandikiwa hiyo dawa, kulikuwa na vibahasa viwili
mle kwenye kabati,.. vinafanana..’akasema.
‘Ulikuja kugundua baadae
au sio..?’ nikauliza
‘Ndio…’akasema
‘Iilikuwaje mpaka
ukaligundua hilo…?’ nikamuuliza
‘Nilikuwa natafuta dawa,
mara nikakiona hicho kibahasha,…nikagundua ndicho kile dada alipewa,
nikajiuliza imekuwaje,…sikuwa na la kufanya..’akasema
‘Kwanini hukuwaambia
polisi kuwa uligundua kuwa karatsi uliyowapa sio sahihi..?’ akaulizwa.
‘Sikuona umuhimu wake
maana vikaratasi vyote vilikuwa sawa sawa…na nilishaona kuwa polisi hawana
msaada wowote kwetu…’akasema.
‘Wewe si unahitajia dada
yako apatiwe haki yake, sioni ni kwanini usiwaambie polisi maana inawezekana
hizo dawa zikawa na kasoro. Labda ziliisha muda wake, ndio maana zikageuka kuwa
sumu..’nikasema.
‘Hazina kasoro ni zile
zile,..mimi nilizikagua..’akasema.
‘Docta anasema
alipoangalia kwenye kabati, alikuta karatasi nyingine ya dawa hizo hizo, hiyo
nyingine ilitoka wapi..?’ akaulizwa
‘Mimi sijui…kwani
ilikuwa na nini ndani, na kwanini. mbona hakuniuliza alipoiona, sijamuona akiwa
na bahasha nyingine ilikuwaje…hapana hakukuwa na bahasha nyingine sio kweli…’akasema
akionyesha mashaka hapo
‘Naona una
mashaka..naona kama unajua kitu kwa hilo, kwanini hutuambii ukweli tu…’nikasema
‘Ukweli upi,..uliza
swali mimi nitakujibu, ili nafsi yako itulie, ..mridhike, muondoke
zenu…’akasema
‘Sio kwamba hiyo
nyingine ililetwa kuficha ushahidi na ile yenye sumu, ikachukuliwa..?’
nikauliza na yeye kwanza akashtuka, na kusema;
‘Mimi sijui hayo
yanatoka wapi… na usitunge stori kwa jambo kama hili, nikuonye kwa hilo,
…unanielewa, uwe makini sana,..umenielewa?’ akasema.
‘Nakuuliza wewe…unijibu,
hilo halikupangwa ili kuvuruga ushahidi….?’nikasema na kumuuliza.
‘Kwanza sikiliza
usinichanganye, wewe, au nyie ndio tatizo..hasa wewe unayejifanya dakitari
wakati huna hiyo fani…, unajifanya mwema,eti unajua kuombea wakati sio
kweli,..ok, labda yawezekana, lakini wewe sio mtibabu, wewe unatumia mgongo wa
docta wako, nimeshakugundua wewe ni nani, sasa endelea kuchonga-chonga kama
sitakuweka sawa..’akasema.
Kwanza nilishikwa na
namna ya kutahayari, kwa maneno yake hayo, yanaonyesha keshanifahamu mimi na
nani, na sijui kafahamu vipi, lakini nikajifanya kama sijali, nikasema;
‘Kwahiyo unanizuia
nisiseme ukweli,..hupendi sisi kutafuta ukweli wa kifo cha dada yako ina maana
wewe huna haja ya kuutafuta huo ukweli tena, bali wewe nawe una ajenda yako ya siri, au.?’ Nikamuuliza.
‘Nauhitajia sana huo
ukweli…, lakini sio kwa mtindo huo mnaokwenda nao, unaohatarisha maisha ya
wazazi wangu, nimeapa kuwalinda wazazi wangu kwa nguvu zote..limetokea hilola
dada, nisingelipenda litokee tena, labda kwa mapenzi ya mungu…’akatulia.
‘Kwahiyo unataka sisi
tufanyeje, maana lengo letu ni kusaidia…hatuna cha zaidi..’nikasema
‘Kutusaidia au
kujisaidia wewe mwenyewe…’akasema na kabla sijasema neno jingine akasema;
‘Mimi nitautafuta ukweli
kwa njia yangu, nimeshagundua mengi,…, nina uhakika wanaohusika nitawang’amua
hivi karibuni.., pamoja na vitisho vyao, nimeshajua hao watu wanahitaji namna
gani ya kuja kuwanasa..lakini sivyo kama mnavyotaka nyie, mtaitia familia yetu
matatani,,, unanielewa, kwahiyo take care ..’akasema.
‘Huko kuwalinda wazazi
wako kwa njia hiyo ni kwa muda tu, sisi tunataka kuwalinda nyote kwenye njia
sahihi ya kudumu,..na kuhakikisha kundi hilo limesambaratika,.. na hilo
unalosema kuwa umeshanifahamu, sawa kwanini husemi ukweli kuwa mimi ni nani, …mimi
siogopi kwa hilo…’nikasema.
‘Sitaki kusema huo
ukweli, kwasababu wewe na huyo mwenzako mnaujua, sasa kwanini niuseme…na
naikisema …nina uhakika utaharibu mambo mengi,.. maana najua muda wake utafika,
na ukweli huo utabainika…unielewe hapo…’akasema kwa kujiamini.
‘Muda gani huo, na mambo
yanazidi kuwa mabaya..’nikasema
‘Yanakuwa mabaya
kwasababu yenu…vinginevyo, nilishaanza kuyaweka sawa…’akasema
‘Kwa vipi na wewe
ulikuwa unaumwa…?’ nikamuuliza
‘Kuumwa
kwangu..kunatokana na nyie..hamlijui tu, aah, tuyaache hayo,ila..nakuhakikishia
muda ukifika utaumbuka, nitahakikisha unakwenda jela,…unasikia hilo nimeahidi…’akasema
akiniangali kwa macho makali.
‘Kwanini
niumbuke..wakati muda huo ukifika kila kitu kitakuwa wazi, kuwa mimi sihusiki
kwa hivyo mnavyofikiria nyie,…ni kweli labda, nahusika kwa namna ambayo, sikuwa
na lengo baya..lakini sio kihivyo, mnavyofikiria nyie,kwanza unajua wazi kuwa
dadayako hakujiua, au hilo hujaligundua…’nikasema.
‘Hebu tuyaache
hayo..maana kama nyie mnavyochunguza yenu , hata mimi nachunguza kivyangu, …sema
mimi baada ya kuugundua ukweli, ndio nikaanza kuchanganyikiwa…sijui ni wao au
ni kwanini,…nitaligundua tu…ila nilikuja kupata onyo kuwa hiyo ni mwanzo
tu,..nikicheza baba anaondoke…keshaanza, …’akatulia
‘Akina nani hao, mbona
huwataji..?’ nikauliza
‘Siwezi kuwataja maana
sijawajua ni akina nani, na kiukweli …uonavyo kwa nje sivyo ilivyo kwa ndani,
mtawakisia watu wengine kabisa, ambao hawahusiki kabisa, watu ambao ni njaa zao
tu wamenaswa huko…,lakini wenyewe haswa, ni ndoto kuwapata, ..sijui…labda kama
mnamiujiza…’akasema
‘Unajua unanishangaza,
kwanini hutaki kushirikiani na sisi ili tuje kuupata ukweli pamoja,hili ni kwa
manufaaa ya familia yako, sio kwangu, au kwa docta..’nikasema
‘Hahaha, eti sio kwa
faida yenu, una uhakika na hilo….ila nawaonya tena hivyo mnavyokwenda, haiwezi
kuwa na manufaa kwa hii familia abadani, mnachotaka kukifanya kitaiangamiza hii
familia,..’akasema
‘Kwa vipi, ndio maana
naanza kuwaogopa,hamuwajui hao watu walivyo, kuuaa kwao ni kama kuua
mbu..hawajali, na wanaju awatauaje kiasi kwamba hata uchunguzi ufanyike je
hakuna wakuweza kuwagundua…’akasema
‘Kwahiyo wewe unawafahamu..?’
nikamuuliza
‘Sio kwa moja kwa moja…lakini
wapo,…watu wanaongea, hata kwenye mitandao wapo,…ila kumnyoshea kidole kuwa ni
huyu, inakuwa ni vigumu, na kama mwenyewe ukafanya hivyo,..utaingia matatani,
wana wanasheria, wana-ulinzi, wana kila namna ya kujilinda, na ole wako uingie
kwenye anga zao…’akasema
‘Wanaitwaje hao watu kwa
jinsi watu wanavyowasema, ni lazima watakuwa na jina, mahali nk..au..?’
nikamuuliza
‘Huko siwezi kujua maana
hata mimi najiuliza hivyo, nimefanya uchunguzi wangu na kugundua kuwa watu kama
hao wapo kweli..lakini kwenye kificho, ni ni…ndio maana wanaitwa mashetani,
unajua…kwasababu ukiatafuta kwa njia halisi huwezi kuwapata,ila wapo wanafanya
kazi, wanazalisha vyovyote iwavyo, kwa mbinu zao..na wakikuona unafaa
watakuchukua, …’akasema
‘Unafaa kwa vipi…?’
nikamuuliza
‘Oh, unajua unaniuliza
maswali ambayo hata mimi nahangaika nayo, kwanini wanamchukua huyu awe mtu wao,
kwanini, wanaua, kwanini…hayo ndio hata mimi najiuliza…sasa siwezi kukujibu
kihivyo,…ila nijuavyo, kama wakikuona ni tishio kwao, kama wakikuona …basi
hawasiti kukumaliza, lakini kingine wanahitajia wanachama kutokana na sifa
wanazozihitajia wao…urembo, mvuto, akili, kipaji..wanajua wenyewe wakikuona
unafaa, na….watakujaribu, na ikishindikana, wanajua cha kukufanya, ndio hivyo
siwezi kusema zaidi..’akasema.
‘Umewezaje kuyafahamu
hayo…?’ nikamuuliza
‘Kwenye mitandao….humo
wanatumia sana,…na zaidi ni kulinganisha matukio, ..na ujanja ujanja…likikukuta
ndio utajua, lakini kama halijakukuta, huwezi, …haya mambo yapo, na yapo…na …chunga
sana…’akasema
‘Nikuulize kitu, wewe
una mpenzi kwenye facebook..?’ nikamuuliza akaniangalia huku uso umesawajika,
kama anatabasamu lakini ile tabasamu ya dharau, na huku ananikagua nina maana gani…mjanja sana huyu
binti.
‘Mpenzi kwenye facebook
ndio nani…una maana gani mpenzi wa facebook, maana hilo neno tata, kila mtu
anayejiunga na facebook, anakuwa na mpenzi, au ukimuadd mtu anakuwa ni mpenzi
wako wa facebook, au sio…sasa ukiniuliza hivyo nashindwa kukuelewa….’akasema.
‘Wewe umesema
umechunguza na upo mbali kwenye uchunguzi wako, na kama ungelikuwa mbali
kihivyo ungelikuwa umeshaligundua hilo,…kuwa watu hawa wanatumia mitandao
kupata wapenzi wao, au sio….sasa mimi ndio nikakuuliza je unaye mpenzi wako
kwenye facebook..?’ nikamuuliza
‘Sina kama ndivyo
nilivyokuelewa, sina na sina haja naye, wa nini kwanza, wa kunitia kwenye
matatizo..’akasema akikunja uso
‘Ina maana sio
wewe…’nikasema halafu akacheka kuzarau fulani hivyo
‘Hahaha..eti sio mimi,….lakini
una maana gani, sijakuelewa, sijui una maana gani, sio mimi kwa vipi, ni kweli
sio mimi kama ulikuwa na maana yoyote kunihusu mimi, sina mpenzi yoyote,maisha
yangu ndivyo yalivyo…’akasema
‘Basi usijali…utakuja kunifahamu
nina maana gani, siku ukikamilisha uchunguzi wako…ila nina uhakika, una jambo
kuhusu hilo…ama unatumiwa, ama …unafanya kwa vile unajua ufanyavyo hivyo, ndio
unaisaidia familia, lakini sivyo hivyo…nikuambie ukweli…’nikasema
‘Huna swali jingine la
kuniuliza..’akasema akiniangalia moja kwa moja usoni
‘’Huyo anayemiliki super
market, mumeanza lini kufahamiana na yeye..?’ nikamuuliza
‘Mhh..kwanza nikuweke sawa,
kama ni mawazo yak ohayo…wanaume mnapenda sana kukimbilia huko…, mimi huyo mtu
sina mazoea na yeye ya kimapenzi,…zaidi y akuwa awali alikuwa akinifua fuata,
kwa ajili ya kumtaka dada, baadae akanitaka na mimi, nikampiga fully stop…. na
ikafikia sehem akasalimu amri,..unanielewa, kwahiyo dhana yako, kama ndio
hivyo, ifute,…, sio kweli, ..zaidi ya ninavyomsikia kuwa yupo hivyo, ni hivyo
tu sio zaidi....’akasema
‘Unamsikiaje kuwa ni
nani..?’nikamuuliza hapo akakaa kimia kama anawaza jambo, hakusema neno,
nikaona niachane naye huko, nikamuuliza swali jingine
‘Sasa mbona umekubali kuwa
utashirikiana nasi ili uweze kukutana na huyo jamaa, au si ndivyo ulivyokubali
hivyo..?’ nikamuuliza
‘Kwasababau hata mimi
nilikuwa natafuta mwanya huo, ninajua kwa hivi sasa nitaweza kulifanya lile
nililolikusidia nikijua kuna watu wapo nyuma yangu,tutasaidiana nao,..lakini
baadae itakuwa kwa masilahi yangu na familia yangu, siwezi kwenda zaidi kama
mnavyotaka nyie, kwasababu hamjui hicho mnachotaka kukiingia…’akasema
‘Sijakuelewa masilahi
una maana gani..?’ nikamuuliza
‘Nitakuwa nimepata
ushahdi wa kukuweka wewe ndani,..hilo ulielewe, ninajua baada ya hapo kila mtu
atakuwa kakufahamu wewe ni nani..na wewe uliifanyia nini hii familia… na
ikibidi hata huyo docta maana nimeshawajua nyie ni akina nani, kwahiyo huko
najua nitawafahamu mahusiano yenu na hao watu,…’akasema
‘Oh, tunarudi kule kule…kwahiyo
wewe unatushuku kuwa labda tumetumwa kuwachunguza, kwa manufaa ya hao watu au
sio…’nikasema
‘Ndio hivyo, sina zaidi
cha kukuambia kuhusiana na hayo, sijagundua mengine, muhimu nawaombeni,
achaneni na hayo mambo …msije kui-ingiza hii familia yangu kwenye matatizo,
tumeshachoka jamani, hebu na sisi mtuache tuwe kama binadamu wengine,..ndio
ombi langu kwenu, pleaseee!…’akasema
‘Labda wewe ndio uwe
umetumwa na hao watu, au labda, unaogopa tu..kuwa tukiendelea wanaweza kuidhuru
familia yako,lakini vinginevyo,..sisi hatuna nia mbaya, nia ni kukusaidia, wewe
na familia yako..’nikasema
‘Hahaha, eti kunisaidia
mimi na familia yangu, baba alijaribu kwa njia hiyo unaona kilichompata, yeye
hanielewi,..hata mimi nahis ndio hivyo,… sasa nyie…mtawezaje, ndio maana
niliamua kujitolea kwa namna nijuavyo ni sahihi, na nina uhakika nitawashinda
tu,ila sio kwa msaada wenu , …’mara simu yake ikalia mlio nahisi ilikuwa mlio
wa ujumbe wa maneno, maana aliichukua simu yake na kuanza kuiangalia,
‘Sasa unaona nilijua tu,
hivi jamani, hamunielewi, angalia sasa, …nimetumiwa ujumbe huu, hebu
uusome..’akasema akinionyesha kwenye simu yake, kuna picha ya…yule mlinzi akiwa
kalala kitandani, inaonyesha ni hospitali, na maandishi yenye rangi nyeusi
chini yake, yakisema;
‘Waonye hao vikaragosi wako…, kati yao kuna atakamfuata huyu..keshatuambia
yote wanayotaka kuyafanya…, na wewe kama hutaweza kuwafukuza hao watu kwenye
familia yako, usije kutulaumu kwa hilo litakalotokea…’
**********
Wakati nausoma huo ujumbe, ….
Na mara akaja docta, alionekana na huzuni sana
usoni, akamuangalia mdada, na kusema;
‘Vipi, mbona mpo nje..ni
muhimu twendeni ndani maana polisi wanakuja,…’akasema
‘Wanakuja kufanya
nini..?’ nikauliza kabla docta hajajibu mdada akasema;
‘Mnajua nyie mnatuletea
sasa matatizo, haya huo ujumbe una maana gani,..na sasa unasema polisi,…ndio hayo
tulikuwa tunayakwepa, wazazi wangu wanahitaji kupumzika, baba ndio huyo katokea
hospitali hajapata muda wa kupumzika, ….sasa mnazidi kunichanganya, polisi
wanakuja kufuata nini tena..’akasema akimuangalia docta.
‘Ni wajibu
wao,…wanafuatilia kuhusu hiyo kadhia ya hivyo viungo vya binadamu, na
wanatushuku sisi, wanasema au wanataka tukaisaidie polisi, unajua wakisema
hivyo wana maana gani..nisingelipenda hilo , maana tutapoteza muda mwingi kituo
cha polisi, na hatutakuwa na muda wa kuyafuatilia haya mambo,…’akatulia
‘Kwahiyo una maana
tunaweza kuwekwa ndani…?’ nikauliza
‘Ndio maana yake,
jiandae kwa hilo,…na nilijua…tu, ule ni mtego,…lakini hata hivyo, hawana
mshiko…ushahidi wao hauna nguvu, …ila nahisi kuna nguvu nyuma yao, ..si bure,
pesa inafanya kazi…’akasema docta.
‘Kuchanganyikiwa kwangu kumenifanya nirudi
nyuma sana, kiukweli
nawashukuru sana kuwa
mlikuja kwenye wakati muafaka, kipindi ambacho nilishakata tamaa…sasa hayo ya
huko polisi mumejitajia nyie wenyewe ..sitaki waje kumgusa baba yangu,
wawachukue nyie…’akatulia kama anawaza jambo halafu akasema;
‘Hata hivyo, kunisaidia
kupona sio sababu ya kunifanya nishindwe kutimiza wajibu wangu,… nawashukuru
sana, ila sasa nawaomba muondoke, kabla
hamjaiingiza hii familia yangu kwenye matatizo, hamjui tu…’akasema na sasa
akaanza kutembea kuelekea ndani..
Kabla hata hajaingia
ndani….gari la polisi likawa linakuja kwa kasi…;
‘Polisi hao wanakuja,…’
alisema docta, na mdada akakimbilia
ndani, …
NB: Polisi wanakuja
kumata nani…
WAZO LA LEO:
Haki inapogubikwa na dhuluma, ikawa wenye mali, na uwezo wanaaangaliwa kwa
jicho la kulia, huku walala hoi, wananchi wa kawaida wanaangaliwa kwa jicho la
kushoto, na haki ikawa inapindishwa kutegemea na mueleo wa jicho, ujue hapo amani itakuwa kitendawili. …
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment