Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Tuesday, April 18, 2017

MPENZI WA FACEBOOK-8


 Yote haya yalianzia ndani ya facebook, pale nilipompata mpenzi kutoka kwa marafiki wangu wa facebook, na kutokana na jinsi alivyonivutia, kwa sura , umbile na jinsi tulivyokuwa tunaelewana kwenye kuchat, nikahisi yeye anaweza kuwa mpenzi wangu na sio mpenzi tu, bali mwenza wangu wa maisha.

Kutokana na historia ya maisha ya nyuma, nilikuwa nimeamua kutulia na kutafuta mwenza kwa njia nyingine tofauti na ile ya kuhangaika huku na kule, kwani nilishapoteza wapenzi wengi, kwasababu hizi na zile, na wengine niliachana nao kwa njia ambayo inaniumiza hadi leo,...

Mpenzi wangu huyu wa facebook, niliona ndiye chaguo halali, ndiye faraja yangu ndiye mtarajiwa wangu, lakini sikuwa nimekutana naye kabla, simjui ,, ila namafahamu katika mawasiliano ya mtandao

Ikafika muda wa kukutana naye uso kwa uso, ndio matatizo yakaanza kutokea...

Mara ya kwanza kanielekeza nikatokea makaburini, mara ya pili nikapata ajali, na hiyo ikanifanya niwe kama nimechanganyikiwa...wengine wakasema kuwa huyo mpenzi wa facebook, sio binadamu ni shetani, je ni kweli ni shetani...mimi sijui,

Nikawa nimeandamana na docta mtaalamu, akiwa bingwa wa magonjwa ya kawaida ya akili, na pia akiwa mtafiti wa madawa asilia, ikiwemo hilo la kuchanganyikiwa, ...akaamua kuandamana na mim ikiwa ni moja ya tafiti zake, na katik ahiyo safari ndio tukaanza kugundua mengi yaliyojificha...

Mpenzi wangu wa zamani ambaye niliachana naye kwa njia isyo nzuri, ambaye niliwahi hata kuahidiana naye kuwa nitamuoa, lakini kwa mara ya mwishi nikamtelekeza, ...kumbe alishafariki na kufariki kwake, ni kwa kusikitisha, kwani eti alijiua, na walikuja kugundua kuwa alikufa akiwa mja mnzito, je hiyo mimba ilikuwa ni ya kwangu, yasemekana hivyo...kuwa kujiua kwake ni kutokana na mimi kumkataa, ..wakati alishajiaminisha kuwa mimi ndiye mpenzi wake, mimi ndiye mchumba wake, maana nilimuahidi mbele ya kadamnasi na kumvisha pete..

Dhuluma hii niliyomfanyia huyu binti haikuishia kwa binti huyu kujiua tu, ikaendelea kuitafuta familia isiyo na hatia,..mdogo wake binti, baba wa binti, na sijui mama itakuwaje...

Kwa hali hiyo nikajiona mimi ni mkosaji, lakini nitawezake kuikabili hiyo familia, maana baba wa binti ni mkali ajabu, na alishaapa siku ya kukutana na mtu aliyemharibu mtoto wake, ni ama zake ama huyo mtu..sasa nifanyeje,

Na wakati nawazia hilo kunatokea taarifa, kuwa mzee Mashauri, yaani baba wa binti niliyemtenda hadi kuamua kujiua, na binti (mdogo wake huyo marehemu) wapo mahututi hospitalini...kisa ni ile ile dhuluma niliyoifanya...

Tuendelee na kisa chetu..


***************


Tulijikuta tumefika hospitali, na tulipofika hapo, tukawa tunaangalia huku na kule kama tunaweza kumuona mtu tunayemfahamu hususani yule mzee tuliyekutana naye awali. Kufika kwetu hapo ilikuwa ni kutokana na aliyopokea docta kutoka kwa huyo mzee…

Wakati wanaongea na huyo mzee, mimi nilitega sikio kujua ni kitu gani kimetokea tena huko, na mara kwa mara Docta alikuwa akinitupia jicho, na kuzidi kunipa wasiwasi, nikajua kuwa  jambo analoliongelea , linaweza likawa linanihusu na mimi na alipomaliza kuongea na simu akaniambia;

‘Kuna tatizo…’akasema

‘Tatizo gani docta..?’ nikauliza nikiwa na hamasa ya kulifahamu hilo tatizo.

‘Mpenzi wako wa facebook, anazidi kutuingiza ndani ya kiini cha tatizo…’akasema huku akiangalia mbele kama anamtizama huyo mpenzi wa facebook

‘Sijakuelewa docta…’nikasema nilipomuona kabakia kimia, na nilipomuuliza hivyo akatizama saa yake halafu akasema;

‘Yule mzee kanipigia simu kuwa, Mzee Mashauri kadondoka, na kupoteza fahamu…na ni kutokana na hali ya mtoto wake kuzidi kuwa mbaya zaidi…’akasema docta.

‘Sasa kwanini akakupigia wewe, na..tufanyeje docta…?’ nikamuuliza.

‘La kufanya ni kuenda huko…na kanipigia simu kwasababu anasema wananihitaji,…’akasema.

‘Oh, wanakuhitajia kwa vile wewe ni docta au kuna jingine zaidi ya hilo..?’ nikamuuliza.

‘Sijajua,…tutajua tukifika huko…’akasema.

Sikuwa na la kufanya ikabidi niongozane na docta hadi hapo hospitalini.

*************

 Ndipo huyo mzee akajitokea, na usoni kwake kulielezea kila kitu, …kuna jambo nzito, …alitujia na kwa haraka akasema;

'Aheri umekuja docta,…docta ilibidi nikupigia simu baada ya kujulishwa kilichotokea kwa rafiki yangu, mara nyingie wamekuwa wakiendelea na matatizo yao bila kunihusisha kama ilivyokuwa zamani, lakini hili lilipotokea ikabidi waniite kwa haraka…’akasema akimuangilia docta.

‘Ok niambie ….najua ni tatizo, lakini akilini nawazia, mimi nahusikanaje na hili tukio, kama docta au kuna jingine…’akasema docta.

‘Unajua sasa ndio nimeanza kukumbuka vyema, … wakati tunaongea na familia ya Mashauri maana mashauri mwenyewe yupo kwenye hali mbaya…, kuna mtu mmoja alikutaja..Docta wewe ni maarufu sana….’akasema

'Ehe, alisemaje ni kuhusu ugonjwa au kuna jingine…? ‘ akauliza swali hilo tena .

'Ni kuhusu ugonjwa, hususani  tatizo la huyo binti, maana kutokana na hilo tatizo ndio likamsababisha hata baba kuzidiwa,..alishaanza kuumwa umwa, lakini tatizo la binti yake limezidisha matatizo..uzee nao mtihani…’akasema.

‘Oh poleni….’mimi nikajikuta nimesema hivyo.

‘Kiukweli hali yam zee ni mbaya sana, na yupo chumba cha wagonjwa mahututi, na docta anayemshughulikia, niliongea naye, akaniambia nijaribu kutafiti kuwa mzee ana tatizo gani, huko kwenye familia…

‘Kiukweli sikumjibu docta kuhusiana na matatizo ya nyuma, maana sijui, huenda kuna mengine zaidi. Unajua ukishafikia uzee, hutakiwi kuongezewa mizigo ya matatizo, akili imeshachoka, sasa wasiojua wanataka kila tatizo kwa baba , kila tatizo kwa mzee,…hili ni kosa, uzee unatakiwa upunguziwe mizigo ya matatizo….sasa watoto na akina mama wanatakiwa kuliangalia hili sana…’akasema

‘Na akina mama nao wanakuwa na matatizo hayo pia,..wanakuwa wazee pia, au sio, sasa usiseme akina mama wawe waangalifu kwa waume wao, pia wakina baba na wao wawe waangalifu kwa wake zao, uzee una mitihani yake,..muhimu ni kwa watoto wawe makini sana kwa wazazi wao, wasiwabebeshe mizigo mingi wazee wao, kwa kujiingiza kwenye matatizo, kwa kudai mambo juu ya uwezo wa wazee, au kuwaletea wazee wao matatizo au sio…’akasema docta.

‘Ni kweli…’akasema huyo mzee.

‘Sasa ndio hivyo, lakini docta nilichokuitia hapa, sana sana ni huyo binti….’akasema.

‘Kwa vipi, huyo binti ana tatizo gani kubwa sana zaidi ya baba yake…?’ akauliza docta.

‘Hali ya huyo mtoto imezidi kuzorota siku hadi siku,..na tatizo hilo ndilo linamuangamiza sasa rafiki yangu, sasa  docta tafadhali sana, tunahitaji msaada wako, ..'akasema huyo mzee akionyesha ishara ya mikono kumuomba huyu docta.

'Mimi sina shida, japokuwa mimi sipo kwenye ajira za serikalini kama docta, unajua mimi nilishajitoa huko muda mrefu,..na hapa tupo kwenye hospitali ya serikali, mnajua sheria zilivyo…mimi nina hospitali yangu huko mikoni ya binafsi, na matibabu yangu yamekuwa ya mchanganyiko sasa sijui tutafanyaje hapo…’akasema docta.

'Ndio maana tunakuhitajia wewe, kwasababu wewe unaangalia kote kote, tiba za kawaida na tiba mbadala…tunahisi matatizo ya huyu binti, hasa….zinahitajia utalamuw ako zaidi..na nilivyosikia wewe upo tayari kujishirikisha kwenye tiba za asili…’akasema.

‘Sawa ni hivyo japokuwa sijabobea sana kwenye utaalamu huo bado nafanya tafiti zangu….lakini hakijaharibika kitu, …., muhimu kwanza ni kuwaona wagonjwa, ..lakini muhimu ni kujua historia ya tatizo,…sasa nikuulize ni nani hasa anatakiwa kuwa mgonjwa wangu  mzee mwenyewe au binti au wote wawili…..?’ akauliza

‘Hapana kwa mzee tatizo lake ni la hospitalini,…kama walivyompima wanasema kapatwa shinikizo la damu…’akasema.

‘Mhh…nazani tatizo la mzee inawezekana kabisa linatokana na huyo binti, na jinsi ulivyoongea hawa wawili wana tatizo linaloendana, ina maana ili mzee apone, inahitajika binti awe amepona, au sio..?’ docta akasema kama anauliza.

‘Ndio maana tukakuhitajia wewe…’akasema huyo mzee.

‘Hebu niambie ilikuwaje kwa huyo binti,…mpaka mzee anadondoka …kumetokea nini zaidi, binti alizidiwa au kulikuwa na sintifahamu kati ya binti na mzee…?’ akauliza docta.

‘Ni kama nilivyowaambia tatizo lilianzia pale huyo binti alipopewa taarifa ya kuwa ndugu yake kafariki, hakuamini, akachukua gari akitaka kwenda kuhakikisha,… sasa wakati anaelekea huko hospitalini,  akayumba, anasema aliona kitu,...na taarifa nyingine zinasema eti alimuona dada yake,....lakini ni katika hali ya kuchanganyikiwa na ndio akapata ajali…

Sasa ajali hiyo ikazua mengine, maana aliathirika uti wa mgongo, lakini tatizo hilo likaenda mbali zaidi, akawa kama anachanganyikiwa, kila mara anamuona ndugu yake, na akimuona anakuwa akipiga ukelele, ndugu yangu huyu hapa, ..ndugu yangu kwanini unaniacha, mara, ndugu yangu hajafa, yule pale…..kwahiyo imekuwa hivyo, …’akasema.

'Ok...sasa mimi nitawezaje kumuona huyo mgonjwa, maana yupo kwenye mamlaka ya hapa hosp..na siwezi kuanza kumsikiliza au kusikiliza taarifa zake bila kumuona, na kuwaona watu wake wa karibu ni jambo jingine…, je yeye mwenyewe anaongea?’ akauliza.

‘Mhh..kuongea imekuwa ngumu, …anaweza kuongea lakini ni kwa uchache zaidi….anayeweza kuelezea yote kwa undani ni mama yake, maana baba yake hali ndio hiyo, kapoteza fahamu na sasa yupo kwenye chumba cha wagonjwa mahututi, mama alivyo utamuonea huruma, analia mpaka basi, sijui kama unaweza kuongea naye…’akasema.

‘Oh….sasa hilo ni tatizo…’akasema docta na mimi pale nilipo nilihisi maumivu ..nilijiona ndiye mkosaji ndiye chanzo cha hayo yote, nikawa nimeinama chini tu.
‘Sasa tufanyeje docta , maana niliwaambia ninakutafuta…’akasema huyo mzee.

'Sio tatizo,…maana chanzo na sababu zipo wazi,…muhimu ni jinsi gani ya kuliweka kwenye mizani hili tatizo, ili wote walipokee na kulikubali…na…muhimu nipate muda kwanza wa kujua matatizo yote hayo kwa kirefu, na …sijui tufanyaje, maana kuna vipimo vingi natakiwa pia nivichukue kwa huyo mgonjwa,….’akasema.

‘Hilo sio shida docta…, tumeshaongea na docta wa hapa, kasema anakufahamu, na alikuwa mbioni kutushauri tukutafute, yeye keshakuruhusu uje uonane na hao wagonjwa hasa huyo binti ...’akasema.

'Ok, itakuwa vizuri nikionana na huyo docta pia,  kuna mambo ya kitaalamu tunatakiwa tujadiliane mimi na yeye….kwahiyo unasema baba yake alipoona mtoto wake kazidiwa na yeye akadondoka na kupoteza fahamu, si ndio hivyo..?’ akauliza.

'Mhh, ndivyo nilivyoambiwa, unajua  tokea dada yake afariki amekuwa huyo binti amekuwa mtu wa ndani, hawezi kutembea, mpaka kushikiliwa, walivyompima awali, wanasema, pamoja na ajali, lakini pia alipatwa na mshtuko,  ndio maana hayo mengine yanakuja kutokea, unajua tena, wengine wanakimbilia kusema alipatwa na mashetani, sasa hatujui, ni wewe docta unaweza kutusaidia kwa hilo….’akatulia.

‘Ok…mimi nimekuelewa, na nashukuru nipo na kijana wangu hapa, atanisaidia sana, hasa kuhusu huyo binti…’akasema anikiangalia mimi na mzee naye akaniangalia na kutikisa kichwa kama kukubaliana na yeye.
Mimi sikujua docta ana maana gani, nikahisi ni katika hali ya kunifanya nisiwe na wasiwasi au ili watu wasijiulize kwanini naongazana ongazana na yeye.

‘Sasa tunaweza kwenda kumuona huyo binti sasa hivi…?’akauliza docta na aliposema hivyo mimi moyo ukaanza kunidunda dunda…

‘Ngoja tusikie docta atasema nini, ….au..?’ akasema huyo mzee.

‘Sawa…maana wepesi wa hili jambo lifanyike kabla mzee hajazindukana ili akipata unafuu asikie maendeleo ya binti yake…’akasema docta.

‘Unahisi itachukua muda mfupi kwa huyo binti, kurejea kwenye hali yake maana wanasema hivi sasa ndio hajiwezi kabisa…?’ akauliza huyo mzee, na kabla hajajibiwa ndio akaja matu na kusema;

‘Mzee unaitwa…..ndani haraka’, na huyo mzee akasimama, na kumuangalia docta, kama vile anataka kusema waongozane.

‘Wewe nenda kwanza kasikilize wito…’akasema docta, na huyo mzee akaondoka kwa haraka kuelekea huko alipoitiwa, na mimi pale niliposimama nilihisi mwili ukiniisha nguvu, miguu ilikuwa haina nguvu, sijawahi kujisikia hivyo kabla.

Tulibakia pale mimi nikiwa sina amani, nilianza kujilaumu sana, nikijutia yale niliyowahi kuyafanya, sikujua matendo yale, ambalo kwa wakati ule nililifanya nilijua ni mambo ya kawaida tu, kumbe mambo yale niliyokuwa nayafanyia wenzangu, watoto wa wenzangu, yamekuwa ni matatizo makubwa, na pia sikujua kuwa rafiki yule wa facebook angeliweza kunisukumia kwenye hili tatizo.

‘Je rafiki huyo wa facebook anahusikanaje na haya matatizo… maana hafanani kabisa na huyo marehemu…sasa iweje ajiite jina la marehemu, na kujifananisha kila kitu na marehemu…’nikawa najiuliza.

‘Siwezi kukubali kuwa eti sio binadamu, hilo siwezi kamwe kulikubali..’nikasema.

‘Oh, mungu wangu kwanini haya matatizo yaniandame, ina maana ndio mwanzo wa adhabu yangu, …nifanyeje mungu wangu kuliweka sawa hili tatizo, najua nimeshakosa kwa huyo marehemu, najua hiyo ni adhabu naisubiria lakini haya yanayoendelea nitafanyaje ili niweze kuyasimamisha..jamani,…oh mungu wangu nimekosa, nimetubu…’nikasema nawaza sasa nikitaka hata kuinua mikono juu kutubu.

‘Oh, mola wangu,wape subira hao niliowakosea, na kama kuna adhabu, inayonifaa hapa dunia, basi nipatie tu, ili iweze kuwapa faraja hao niliowakosea…namuonea huruma mama wa watu hapo alipo analia, alikuwa akimlilia marehemu , sasa analia ….oh mungu nifanyeje sasa jamni…’nikasema huku nikizungusha zungusha kichwa maana nilikuwa sasa nimechanganyikiwa.

Kitu cha ajabu tokea siku ile nisikie kitu kama sindani ikichoma kichwani mwangu, na kupata maumivu ya kichwa,..ilikuwa kama nimezibuliwa kutoka ndani ya maji, masikio yalizizima na baada ya hapo sijawahi kuona yale marue rue, na ila hali y akumuota huyo binti wa facebook, ikawa imeanza kupotea…

Sas haya…..nikahika kichwa na kuzama kwenye mawazo ya kumuomba mungu…

‘Mungu wangu, najuta na hayo niliyoyafanya, unajua madhaifu yetu sisi wanadamu, na sikujua kuwa katika kutenda vile nitakuwa nimewakosea watu kwa kiasi hiki kikubwa, nashukuru kuwa umenionyesha athari za dhuluma, jinsi gani inavyosambaa, lakini mungu wangu nitafanyaje ili kuzuia athari hii isizidi kuendelea,…’niliposema hivyo nikageuka kumuangalia docta huku macho yakiwa yamejaa machozi.

Kiukweli chozi lilinitoka, nilishindwa kujizuia.

Niliinua macho yaliyojaa machozi na kumuangalia docta, kumbe docta naye alikuwa akinichunguza, nilipomuangalia macho yetu yakakakutana, akatikisa kichwa.. kama kukubali au …, sikujua kutikisa kichwa,kule ilikuwa ishara ya kukubaliana nami, au ilikuwa,kunisikitikia, mimi nikagauka upande mwingine na machozi yakawa yanaendelea kutoka kama maji.

Niliwaza mengi, na kwa mara ya kwanza nilianza kuhisi woga, woga kwa hayo yanayoweza kutokea, maana kama hali ya huyo mzee ipo hivyo, je ikiwa mbaya zaidi, itakuwaje, na je matatizo kama hayo yakihamia kwa huyo mama….oh, sitaweza kuvumilia,….mungu wangu nitafanyaje ….

‘Potelea mbali, mimi sasa nitakwenda kujitambulisha lolote liwalo na liwe, haya ni makosa yangu inabidi niadhibiwe,,…’nikajikuta nikisema kwa sauti, na mara nikahisi mtu ananishika begani…

‘Upo tayari kuadhibiwa…?’ nikaulizwa na mimi bila kumuangalia aliyenishika bega nikasema.

‘Nipo tayari…’nikasema na huyo mtu aliyenishika bega, akaniachia, nikainua kichwa kumuangalia,..hutaamini sikumuona mtu, nikaangalia pale alipokuwa kakaa docta, nikamuona docta akiwa anaongea na yule mzee, kumbe yule mzee alisharudi, kumchukua docta wakati mimi nimezama kwenye mawazo,…na kwa muda huo yule mzee na docta  wakawa wanatembea kueleka huko walipolazwa hao wagonjwa.

Nikawa sasa najiuliza niwafuate au nisubirie pale…

Lakini ni nani huyo aliyenishika  bega…nikageuka huku na kule hakuna mtu aliyekuwa karibu na mimi…nikaanza kuhisi kuwa sipo peke yangu, nikageuka huku na kule…

‘Ni nani wewe…?’ nikauliza, sikuona mtu ila nilihisi kuna mtu yupo karibu yangu..

NB: Samahanini nimechelewa kuiandika sehemu hii kutokana na mitihani ya hapa na pale.


WAZO LA LEO: Mungu ni mwingi wa rehema, anatujua nafsi zetu , na inapofikia kuwa kweli mja wake katubia makosa yake, anamjua , na kusamehe kwake sio tatizo, lakini je ni kweli tumetubia ukweli wa kutubia, hapo ndio taizo,..Tumuombe mungu wetu atusamehe makosa yetu yalipopita na yajayo kwani mitihani ya dunia hutufanya tujiingize kwenye makosa mengi, …
Ni mimi: emu-three

No comments :