Nikiwa ndani ya facebook, nilibahatika kupendana na msichana mmoja, ...tuliwasiliana naye sana, tukajuana lakini kwa kupitia mtandao, tukawa tunatumiana picha, mpaka ikafikia mahali nikataka nikutane naye uso kwa uso...
Hakupendelea hilo wazo, nikajua ni taratibu tu za mwanamke anayejiheshimu, mimi nikamwambia sio kumuona tu, nataka nionane na wazazi wake, ili ikibidi tufunge ndoa..bado aliendelea kusita, lakini hatimaye akaakubali, na ndio nikafunga safari ya kwenda kwao kukutana na wazazi wake.
Kabla ya kukutana na wazazi wake tulipanga kuwa nikutane mimi naye yeye, nyumbani kwake, kwahiyo akanielekeza na cha ajabu ramani aliyonipa, au maelekezo yake aliniyonipa yalinifikisha makaburini...
‘Ohh, huyu honey, kakosea nini, mbona natokea huku makaburini, nahisi kakosea....'nikasema
'Mimi hapo nikajaribu kumpigia simu kwa
namba ile ile tunayowasiliana naye siku zote,.., lakini kwa muda huo hakuweza kupatikana..., sio kawaida yake, haijawahi
kutokea, huwa tukipigiana simu muda wote tunakuwa hewani.
Nilihangaika kutafuta huku na kule kama kuna nyumba mahali hap , au karibu na hapo, lakini sikuona nyumba kama hiyo,...nyumba nyeupe, ina maru maru kuzunguka...nikauliza watu hakuna aliyeitambua nyumba hiyo
Basi baadae nikiwa nimekata tamaa, nikaamua kurejea nyumbani
Hapo ndio nikaota ndoto ya ajabu,...hata hivyo sikuwa na wasiwasi wowote, akili yangu ilikuwa kwa mrembo, nikapanga nionane naye siku nyingine, baada ya kuomba sana, ndio akanikubalia...
Tuendelee na kisa chetu...
*************
‘Mbona hunielewi baby,..i
love you so much…but,…eeh, mimi nahisi ulikosea kuniekeleza…au sio, hapo
uliponielekeza barabara inapitia makaburini, na huko mbele, au hata pembeni hakuna
sehemu za nyumba za watu…, zaidi ya kupita juu ya makaburi ya watu, …’akasema.
‘Mhh, kumbe ulivyokuwa unanisihi hivyo hukuwa na mapenzi na
mimi, nakumbuka mashari yako ya mapenzi ulisemaje, utanitafuta hata kama
makaburini…utanifuata hata kama ni kuzumuni, utanipenda hadi siku kiamani, au
sio…, si ulisema utafika kwetu hata kama ni ndani ya pango, ili unioe, tuwe
pamoja, kweli si kweli…? akauliza.
‘Lakini hiyo ni misemo ya kimapenzi….au …nakupenda sana honey wangu, na niliyasema hayo
nikimaaanisha jinsi gani nikupendavyo, na ya kuwa nitajitahidi nifike pale
ulipo kwa vyovyote vile lakini sasa hujaniekeleza vyema,…nikuambie kitu honye,
tusipoteze muda, wewe nieleekeze tena, naona ulikosea tu, au sio…’nikamwambia.
‘Hapana…naona muda wako wa kukutana na mimi haujafika,
ukifika tutaonana tu…usijali sana mpenzi wangu, …poa, wewe jiandae taratibu, na
hilo halitaki haraka, unasikia..’akaambiwa
‘Hapana mimi nimeshajiandaa sina shaka na hilo….’akasema
‘Usilazimishe jambo ukaja kujijutia baadae…huku unapotaka kuja
kuniona sio njia rahisi, unasikia, …’akasema
‘Basi nitakodi hata ndege…’nikasema nijua ni mzaha wake tu,
unajua hadi hapo sikuwa na mawazo mengine zaidi ya kumpenda huyo binti wa
facebook.
‘Basi kama umedhamiria kweli, ....jiandae ipo siku nitakuambia, ...'akasema
'Sawa honey, usinifane nikasubiri sana....'nikasema
'Basi kesho nitakuelekeza vyema, na safari hii
usiogope, njia ni hiyo hiyo, ukifika hapo, nitakupokea mimi mwenyewe…’akasema na mimi kabla sijamjibu ndio nikazindukana…kumbe alikuwa anaota.
Basi nikajiandaa kwenda kuwajibika kazini kwangu, huku nikitizama kwenye
simu kama nitapata meseji yoyote mpya kutoka kwa huyo mpenzi wangu, lakini
hakutokea kama ilivyokuwa kawaida yetu, nikampigia simu ikawa haipatikani.
Siku hiyo nilifika ofisini nikiwa kama mgonjwa, kisa
sijawasiliana na mpenzi wangu,..baadae mcha mchana hivi ikaingia meseji na
ujumbe na picha, nikaifuingua, mara naona mtu kasimama juu ya kaburi, na ujumbe
unasema;
Anaye yakimbia mauti, mwisho wake, ni hapa, jiandae, na
utamkuta umpendaye anakusubiria, yeye hana haraka, anafika hata kwenye
pango,…gizani hata ndani ya maji,…muhimu jiandae…’
Mimi niliyachukulia maneno hayo kama maneno ya kufurahishana tu kwenye mtandao, sikuwa na wazo lolote
baya kwa huyo binti basi mimi nikaweka maua, na sura za kimapenzi, na kusema;
‘Baby, mbona wanitisha, …mimi kwa ajili yako siogopi kufa,
kwani inzi kufa kidondani ni kawaida tu…' na hakunijibu, nikajaribu kumpigia
hakupatikana, na jioni akanitumia meseji kuwa kaongea na wazazi wake, wamesema
wanahitajia muda wa kunichunguza kwanza.
‘Umesikia, kwa vile umeshatambuliwa kwetu kama mchumba,
inabidi tusiwe kama zamani, kuchat nk..inatakiwa uniheshimu kama mtu wako, sio
hawara au …mpenzi wa kupita, kwahiyo nakuomba tupunguze mawasiliano…’akasema
hivyo.
Kiukweli nilikubali kishingo upande, nikamajibu sawa kama
uonavyo ni sahihi, lakini mimi sitaweza kulala, hata kula kwa ajili yako…
Ilipitia wiki nikawa kama mgonjwa, mpaka watu wakanishangaa,
wakiniuliza nawaambia nyie acheni tu, nampenda sana mpenzi wangu wa facebook…na
siku moja huyo mpenzi wangu wa facebook, akanitumia ujumbe na kuniambia;
‘Sasa wazazi wangu wapo tayari kukutana na wewe…lakini siku
hiyo unatakiwa ufanye yafuatayo...kwanza utakuja tuonane mimi na wewe uso kwa uso, baada ya hapo nitakupeleka kwa wazazi wangu,...
'Sawa itakuwa vizuri sana, nikuone ulivyo, sura yako..tuongee, unijue na mimi nikujue au sio...'nikasema
'Lakini jingine la muhimu, usija na gari lako,...nataka uje na daladala,..wewe wahi asubuhi na mapema, ukifika kituoni utaliona gari linasubiria abiria, na ukae kiti cha mbele…’akasema.
‘Kwanini cha mbele, kama kina mtu je..?’ nikamuuliza
‘Kitakuwa hakina mtu…na itakuwa ni rahisi kwa mimi kukuona ukija, na nafsi yangu itafurahi sana...’akasema.
'Hamna shida upendavyo sweetie...'nikasema.
***************.
Basi siki hiyo nikajiandaa vyema kabisa…cha ajabu kila nguo
niliyokuwa nikivaa niliikuta ina kasoro hii na ile,…sikupenda nguo yenye kasoro, na mimi nilipendelea siku hiyo nivae nguo yenye rangi nyekundu maana siku hiyo ilikuwa siku ya wapendanao...kweli ilinitoa kinamna nitakavyo.
‘Kweli siku muhimu sana, nashangaa amekubali tukutane siku muhimu kama hii...'nikasema huku nikicheza cheza na kujikagua kwa kupitia
kwenye kiyoo kikubwa nilichoweka ukutani. Kiukweli mimi ni mtanashati sana, najipenda , na kupenda kuvaa nguo nzuri
Nilipoona nipo tayari, nikaingia barabarani, …ilikuwa
asubuhi na mapema tu, sikupenda kuchelewa, na haraka nikaelekea kituoni,..kuna
mwenzo kidogo wa kutembea na cha ajabu , njiani nilikutana na vikwazo vingi,
mara nikutane na mtu ninayemfahamu anataka tuongee kuhusu jambo fulani, na
utakuta jambo hilo ni muhimu sana…, mara nikutane na mtu anataka nimsaidia jambo,
mwingine anataka nimuelekeze njia…yaani ni vitu vidodgo vidogo, vya kunifanya
nichelewe
Ikafika muda sasa sijali mtu, anayeniita nakausha , nikajifanya
sijamsikia,..kiukweli nilikuwa najulikana sana, na mimi ni mcheshi kwa watu…lakini
kwa muda huo nikajifanya sina masikio…;.
Na mbele nikakutana na rafiki yangu akaniuliza gari langu
lipo wapi, nikamwambia leo nataka kusafiri na basi, nina sehemu naelekea.
‘Basi subiria kuna dereva wangu anakuja na gari nitakusogeza
mbele…’akasema
‘Hapana, leo sitaki kupanda gari jingine nataka kupanda
daladala tu…’nikasema
‘Kwani unakwenda wapi mpaka uwe na masharti magumu hivyo, …usije
ukawa unadaiwa hutaki kuonekana..’akasema kiutani
‘Hapana, mimi leo nina miadi na mrembo wangu….’nikasema
‘Kuwa makini rafiki yangu, nakuona siku hizi upo bize na
simu,…nimekugundua sana, kama ni marafiki wa mitandao, uwe makini nao sana… ,
hujasikia kuwa warembo wengine ni viini macho…’akaniambia nikageuka
kumuangalia, akacheka na kusema;
‘Hasa warembo wa mitandao, wanaweka picha nzuri lakini kumbe
sio wao, ni watu wengine kabisa…na…na’akasema.
‘Lakini sio huyo wa kwangu mkuu…, wewe hujamuona
tu…’nikasema.
‘Hebu nimuone…’akasema na mimi kwa furaha
nikamuonyesha,..alipoiona ile picha akawa kama anashtuka,…na kurudi nyuma,
mpaka nikashikwa na butwaa.
‘Vipi…umeonaeeh, urembo wake tu umekufanya ushtuke hivyo, je
ukimuona uso kwa uso itakuwaje…’nikasema.
‘Uliwahi kuonana naye uso kwa uso…?’ akaniuliza.
‘Hapana ndio mara ya kwanza, nakwenda kuonana naye…’nikasema.
‘Ndugu yangu mimi nina kipaji, nimezaliwa hivyo…mimi sitaki
kujizoesha sana mambo hayo, sipendi, japokuwa wengi wameniomba nikitumie hicho
kipaji,..huwa naweza kuwatambua watu wabaya,…wenye mapepo na wachawi…sasa huyo
mrembo wako nahisi sio mtu….’akasema.
‘Kwanini…?’ niliuliza hivyo, mara ukaja upepo, wa kutia
mchanga, tukawa tunahangaika kujizuia, na badae huyo jamaa yangu akapata
usafiri wake na kuondoka kabla sijaongea naye zaidi.
‘Huyu mrembo wako
nahisi sio mtu…mijitu mingine bwana, wivu tu,..halafu hizo imani za
kishirikina mimi sizipendi,… eti sio mtu, huyu ni nani…hahaha, watasema sana?’
nikasema nikiiangalia ile picha na tabsamu la mrembo huyo likanifanya
nifarijike, nikaendelea kutembea hadi kituoni.
Nilipofika kwa bahati, nikakuta gari halina watu, wanapiga
debe kuita watu, nikaingia kiti cha mbele kilikuwa na mdada mmoja, nilipoingia
mlangoni mdada huyo akasimama na kushuka,..
Mimi sikumuangalia vyema, nikijua ni abiria tu, nikasogea
hadi kwenye kile kiti..nikataka kukaa, lakini kabla sijakalia hicho hiti,
nikaona alama za damu…damu mbichi kabisa…nikasita kukaa, nikasema;
‘Dereva mbona kiti chako kina damu…?’ nikauliza na dereva
akashtuka na kuangalia ile sehemu, akasema;
‘Huyu dada aliyekaa hapa …..naona kapitiwa, nashangaa
kateremka, nilimuona hayupo sawa, hata ukimuangalia macho yake, unahisi mwili
unasisimuka…’akasema dereva
‘Nilimuona akiteremka kwa haraka…’nikasema
‘Oh, na damu ni ishara ya balaa…’akasema huyo dereva, sasa
akawa amechukua kitambaa na kuifuta huku akilalamika baadae mimi nikaweza kukaa
kwenye hicho kiti, maana nilitaka nisije kumuuzi honey wangu,..na kwa muda huo
sikuwa na mawazo mabaya hata chembe , hapo akili yangu ilikuwa ni namna gani ya
kukutana na huyo mdada.
Gari lilichelewa kidogo mpaka abairia wakawa
wanalalamika,..hata mimi ilibidi nipaze sauti, maana hawakujua nina miadi
muhimu, na badae ndio gari likaondoka,…abiria wakiwa wameshonana kweli
Kila kituo watu wanateremka,
mimi nahesabu vituo,… nilishangaa mbona kumekuwa mbali hivyo, sio kama siku
ile, mpaka ikafika sehemu nikashikwa na usingizi..
Ndani ya usingizi nikawa naota nipo na huyo mdada kaja
kunipokea, na sasa akawa ananipeleka nyumbani kwao, na ajabu iliyoje, tulifika
sehemu ya makaburi akawa sasa ananionyesha …
‘Unaona pale ndipo nyumbani kwangu…’akasema
‘Wapi mbona sioni nyumba..?’ nikamuuliza
‘Hahaha, ina maana huoni…ile pale…’akasema
Na mimi nikakaza macho kuangalia mbele, sikuona kitu, nilichoona zaidi ni kaburi
‘Kaburi..?’ nikamuuliza.
‘Hahahaha….welcome my honey….’akasema na kucheka saana,..
‘Ndugu unakwenda wapi…?’ akaniuliza konda, na kunikatiza
ndoto , nilizinduka nikiwa nahema,..na sikutaka hata kuikumbuka hiyo ndoto,.
‘Kituo cha makaburini…’nikasema
‘Oh, ni kituo kinachofuata…nasikia huko siku hizo kuna mauza
uza…’akasema konda
‘Mauza uza gani…?’ nikauliza.
‘Mhh, watu wanaogopa hata kuongea maana ….nasikia hata
kwenye mitandao kuna namba za ajabu ukitumiwa ukaipokea ..basi hukatizi siku…mitandao
hii ina mambo, mimi sitaki kujiunga na mambo haya, mtu humjui, mnawekeana urafiki…ni
ajabu kabisa…’akasema na mimi nikawa nimetulia.
Basi konda akawa anaongea mambo mengi kuhusu hayo mauza uza,….lakini
mimi akili yangu haikuwa kwenye hayo mauza uza, akili yangu ilikuwa jinsi gani
nitakutana na huyo honye wangu, unajua kupagawa ..mimi nilipagawa kwa huyo
mtoto…nilihisi kausingizinikawa najitahidi nisilale nikaja e kupitishwa, …sijui
ilitokeaje, maana mbele alionekana paka mkubwa mweusi anakatisha njia, dereva
sijuii kwa uwoga, akafunga
breki,…nilirushwa kichwa kichwa kutokea kwenye kiti na kwenda kugonga kwenye kiyoo cha mbele…
Ajabu sasa wakati tendo hili linatendeka, yaani wakati
narushwa kuelekea dirisha, ..mbele yangu nilimuona huyo mdada, mpenzi wa
facebook, akionyesha mikono ya kunipokea, tabasamu tele mdomoni, huku akisema
‘mpenz wangu karibu…karibu nyumbani kwetu…’giza likatanda usoni, sikujua
kilichotokea baadae.
NB: Haya tusome sehemu hiyo ndogo, ili tuende sawa, akili
bado haijatulia lkn nimeona nisiwavunje nguvu wapendwa wangu.
WAZO LA LEO:Kuna mambo
mengine ni ya kufikirika, yapo, lakini hayana uyakinifu halisia, kuna mambo ya
mashetani, uchawi nk…haya hayana sayansi kamili…lakini yapo, na watu wanaathirika
na mambo hayo, na wengine wanafikia hata kuyanunua mambo hayo…mimi najiuliza
iweje…kwanini ujishirikieha na mambo ambayo mwisho wake unaweza kupata shida
nayo. Kitu kama mashetani yana maisha yake, kwanini utake kuyaingilia,huo
unakuwa ni ushirikina!
Muhimu ndugu zanguni, tujue kuwa dunia hii ni mapito tu..ufanye
ufanyalo itafika siku utaachana nayo, kwanini tujihilikishe na mambo makubwa
kupita uwezo wetu.., sisi tunachotakiwa nacho ni kumjua mola wetu na kumuabudu,
tufuate aliyotuamrisha tufanye na tukatazike na yake aliyotukataza, hiyo ndio
njia sahihi nyinginezo ni kujitakia matatizo.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment