Nikawa namuomba mungu, na maombi yangu kwa wakati huo yalitoka
moyoni, kauli ya mama ilinigusa sana, nilimuonea huruma mzazi huyo, nilimuona
kama mama yangu kwahiyo wakati natamka haya, ilinitoka kutoka maoyoni japokuwa
…kinamna nyingine sikuwa tayari kwa hilo, kwa vile nilishampenda mpenzi wangu
wa facebook.
‘Nakushika kiganja chako cha mkono,kama ishara ya mshikamano ,kuwa
mimi na wewe kuanzia sas tu wapenzi wa kweli..’nikasema na huku moyoni kidogo
natamani kusita, lakini kuna nguvu ilinivuta nizidi kusema mengi zaidi.
‘Na kwa uwezo wa muumba wetu, ewe mola wetu, ninakuomba kwa rehema
zako, umponye mja wako huyu, aondokane na hicho kifungo cha umauti, na mateso
ya maradhi anayopambana nayo, .. nakuomba mola wetu umjalie mja wako huyu
azindukane kutoka kwenye usingizi mnzito alio nao, azindukane ili tuweze kutimiza
wajibu huo muhimu wa mimi na yeye kuwa kitu kimoja..’ nikatulia kidogo halafu
nikaongezea,
‘Ili mimi nay eye tuje kufunga ndoa…na ili dada yake huko huko
alipo atulie, roho yake itulie, na awe
na makazi mema peponi!...’ nikatulia na kabla sijaendelea ndio nikasikia
‘Aamin….’
Hiyo Amini sikuitamka mimi,..hapo nikashtuka, …
Kiukweli nilisikia sauti ya
kuitikia hivyo, Aamin, na ilikuwa ni sauti ya kike..sauti ambao haikuwa tofauti
na sauti ninayoifahamu mimi,
‘Oh,…’hapo nikasita kuendelea na maombi yangu, huenda
ningeliendelea ningeligundua ni sauti ya nani, kitu kikanivuta kuchunguz kwanza
hilo, ni nani kaitikia aamin, na,..humo ndani hakukuwa na mtu mwingine wa kike
zaidi ya mgonjwa.
Awali kwa akili za haraka nilijua labda ni yule mtu, au kivuli cha
mtu, kinachonifuata fuata, mtu ambaye haonekani, lakini kama ingelikuwa ni huyo
mtu ningemuhisi, maana huyo mu akiwa karibu yangu huwa ninamuhisi,sikuwa na
naihisi hiyo hali, …basi kama hakuna mtu mwingine aliyeitikia hiyo aamni,
atakuwa ni nani mwingine..
Tuendelee na kisa chetu.
**********
Ndio ikabidi badala ya kuendelea kuomba duwa, ikanibidi nigeuza
kichwa kuangalia huku na kule, …sikumuona mtu, hakukuwa na mtu wala ishara kuwa
huyo mtu anayenifuata yupo karibu yangu
Baada ya kuhakikisha kuwa hakuna mtu mwingine ndio nikageuka
kumuangalia mgonjwa wangu, nilihis joto, nilihis mwili kufanya kazi kwenye
mkono niliokuw animeushika, lakini kwa awali akili hiyo haikuwepo, akili
ilikuwa inamtafuta huyo aliyeitikia Aamin.
Ndio nikageuka kumangalia huyo mgonjwa aliyekuwa kalala kitanani,
macho yangu yalitua kichwani mwa huyo mgonjwa, uso ulikuwa wazi, kitambaa
alichokuwa kajifunika huyo mgonjwa sasa hakipo tena…
Nikakumbuka mama akiondoka, huyo mgonjwa alikuwa kafunika uso
wake,..ila sio kwa kitambaa kile cha kufnga moja kwa moja nyuma ya kichwa,
ilikuwa ni leso ndogo tu.., sasa hiyo leso haikuwepo usoni…uso ulikuwa wazi, na
sasa ninachoona ni macho…
Macho yaliyofunguka,…macho yaliyokuwa yakiniangalia mimi, macho
makuwa yaliyojaa nyusii nyingi, kama yamepakwa wanja, …mmh, …lakini sio macho
tu, bali pia na uhai kuwa hayo macho yanaona,..sina uhakika na hilo, ila macho
yalikuwa ymefunguka.
Sikuamini….akili ilikuwa haiamini hicho inachokiona, ni kama vile
ulitaka upate pesa, na sasa unapata dhahabu…, japokuwa ndivyo nilikuwa naomba,
moyoni nilikuwa naomba hivyo, mama wa huyo binti ndio alikuwa anomba hivyo,
baba ..na wengine wanaompenda huyo binti walikuwa wanatamani iwe hivyo…
Lakini kilichonivutia zaidi ni …..macho, eeh, macho, …ya huyo mdada
mgonjwa, yalinivutia sana,..kiasi kwamba nilihisi moyo ukiganda, nikawa
namuangalia tu…na nilichoweza kukisema kwa wakati ule …ni..ni…ni ….
‘Ni ni…ni…’nilijikuta nikisema hivyo,..na kabla sijasema zaidi ndio
mlango ukafunguliwa akaingia docta akiandamana na mama wa huyo binti..
Kiukweli sio kwamba niliathirika na umbile , macho, na uzzuri wa
huyo binti , bali kulikuwa na jingine kubwa, lakini kabla sijaweza kuliweka
wazi, kiakili na…mara ndio wakaingia docta na mama yake huyo mgonjwa.
‘Vipi kuna nini kimetokea mbona upo kama umeona mzuka..?’ aliyeuliza
alikuwa ni docta na huku mama akiwa na hamasa, hakuacha kuendelea kuangalia
pale kitandani, na ukumbuke huyo binti alikuwa katulia vile vile,
ila…macho,….na mama alipomuona vile sijui nisema nini..
‘Mungu mkubwa….mwanangu umeamuka, mwanangu umezindukana, mungu
mkubwa namshukuru mungu, namshukuru mungu siamini…’akasema mama akiinua mikono
juu, na wakati huo docta alikuwa akiniongelesha mimi hakuwa na habari ya
kumuangalia huyo binti kwanza, ila aliposikia kauli ya mama ya kumshukuru mungu,
ndio na yeye macho na akili yake ikaenda
kule kitandani
Kwa haraka docta alimfuata huyo mgonjwa kitandani na kuanza kumpima
pima, na alipomaliza, akasema;
‘Mgonjwa yupo kwenye hali nzuri, muhimu kwasasa ni zoezi la
kuinuka, …mazoezi ya viungo na mengine, maana alikuwa kalala muda mrefu na
viungo vinakuwa kama vimekakamaa, lakini yupo safi na muda tu anaweza hata
kutembea,…’akasema
‘Nimepona mama….’ilikuwa sauti ya mgonjwa na hpo ndio nikajua ndio
yeye aliyetamka yale maneno ya Aamin…nikageuka kumuangalia na yeye huku akiwa
kakumbatiwa na mama yake pale kitandani akanitupia tena jicho…tukaangaaliana,
na hapo hapo nikajua ndio yeye..
‘Umepona mwanangu , siamini, siamini, natamani nikuone ukiinuka
ukitembea, unipe faraja nijisikie na mimi ni mama, nina mtoto, amuka basi
mwanangua…’akasema mama yake akijaribu kumuinua mama yake, lakini binti
akatamka neno lililowafanya wote watulie kidogo.
‘Baba yupo wapi..?’ akauliza huyo binti akiangalia huku na kule...
‘Baba yako yupo, alikuwepo, katoka kidogo, na tukimpatia taarifa,
kuwa umeshapona, atafurahi sana..’akasema mama yake
‘Nataka nimuone baba yangu kwanza…’akasema binti na hapo watu
wakaangaliana.
‘Atakuja kwani una haraka gani na baba yako, naye kachoka
anahitajia kupumzika, alikuwa hapa muda mfupi uliopita….’akasema mama
‘Nataka nimuone baba yangu, yupo wapi, naona kama mnanificha jambo,
najua baba kapatwa na kitu , nataka kuhakikisha, nataka nimuone baba yangu
kwanza, la sivyo mniambie ukweli, babayangu yupo wapi…’akasema hivyo huyo
binti, na aliyeweza kuufunua ukweli alikuwa ni docta, docta akasema;
‘Baba yupo, usijali, .. ila kutokana na hali yako ilivyokuwa, hali ya
baba yako ilibadilika ,akazidiwa ana kuanza kuumwa, na hivi sasa yupo kwenye
hospitali hii hii kalazwa, akipatiwa matibabu, anaendelea vizuri, na nikuembie
kitu, kupona kwako ndio itakuw afaraja ya kumfanya yeye apone haraka, …’akaambiwa
na docta.
‘Basi kamwambieni nimepona, nataka na yeye apone, aje anione,
yawezekana likafanyia leo, sasa hivi…’akasema na docta akasema,
‘Usijali mimi mwenyewe nitakwenda huko, mguu kwa mguu nikampe hiyo taarifa
kuwa umeshapona na unaongea, na hivi karibuni tu utaanza kutembea..’akasema
docta
‘Hapana usiende wewe,…wewe ni docta bado nakuhitajia hapa, mimi
ninataka huyu, masaidizi wako ndio aende, si docta wako msaidizi au nilikuwa
naota..nataka yeye akamwambie baba kuwa nimepona na pia ili aweze kumpa baba
hizo taarifa zingine alizokuwa kiniambia, nataka baba akija hapa alitambue
hilo…’akasema binti.
‘Atambue nini..?’ akauliza mama yake akimuangalia binti yake kwa
mashaka.
‘Kwani hujui mama, hajakuambia tu..?’ akauliza binti, akimuangalia
mama halafu mimi, halafu docta, na kabla docta hajasema kitu mimi nikasema;
‘Sijamwambia mama, unajua ilikuwa sehemu ya matibabu yako, na mama
hajui hayo matibabu, na mengine nitamwambia, …subiri kwanza…si unajua tena kila
kitu kin autaratibu wake,…umenielewa..’nikasema
‘Sawa nimekuelewa, lakini nenda kwa baba kwanza umwambie kuwa
nimeshapona na ikibid kama ni kweli basi uanze kumuambia, au hilo ni haraka
sana,..mimi nakumbuka uliniambaia upo tayari au, haya sawa mimi nitakaa kimia,
…mengine utajua wewe mwenyewe, ila ninataka baba yangu awe afurahi , ili naye
apone haraka, mwambie asipopona haraka na mimi nitashindwa kupona haraka..’akasema.
‘Utapona haraka binti yangu, kwanza ninataka mimi mwenyewe nianze
kukupa zoezi la kuinuka hapo ulipolala, uanze kutembea,…’akasema mama akiwa na
haraka ya kumuinua na docta akasema
‘Mama, bado..subiri, kuna mafuta ya kumkanda..nitakuelekeza jinsi
ya kufanya, inabidi viungo vyote vichuliwe, kabla ya kuanza zoezi la kusimama,
..ni hatua kwa hatua, ..na wewe nenda ufanye ulivyoagizwa..’akasema docta docta
alipoona bado nimesimama nikimkodolea macho huyo binti..
‘Sawa bosi,..’ nikasema huku natembea , huku naangalia nyuma
nikajikuta nagongana na ukuta…docta aliyekuwa akiniangalia akaangua kicheko, na
wengine wakageuka kuniangalia lakini nilikuwa nimeshatoka nje.
**********
Wakati natoka mle ndani akili sasa ilishatulia, nikawa nikiwazia
jinsi gani ya kukutana na huyo mzee, …ukumbuke hasira za huyo mzee dhidi yangu,
japokuwa mpaka sasa hajanitambua kuwa mimi ni nani,..na sina uhakika kama ananifahamu
pili, je akija kugundua kuwa mimi ndiye niliyefanya mabaya kwa binti yake mpaka
akajiua, itakuwaje wakati alishasema mara nyingi kuwa huyo mtu atakuwa halalii
yangu, ama zake ama zangu..
‘Oh, sasa naingie kwenye mtihani mwingine, nakuomba mungi wangu
unipe wepesi, niweze kupambana na mtihani huu, ninajua nimekosa, na nia na
lengo langu ni kutubu, lakini kwa hali ilivyo siwezi kukiri ukweli mbele ya
hawa watu, nahisi itaweza kuleta shida, sasa nifanyeje..
Nikawa nawaza huku natembea huku namuomba mungu wangu..
‘Sasa nifanye nini..nitoroke, lakini siwezi kutoroka maana
nimegundua kitu muhimu sana katika maisha yangu, mpaka sasa hivi siamini…huyu
ni mrembo wa nama gani, huyu..oh, haiwezekani..na nikajikuta nimeshafika chumba
alicholazwa Mzee..na nilipofika mlangoni, maana kitanda cha huyo mzee kilikuwa
karibu sana na mlango nikasikia sauti ikisema;
‘Yaani Docta, siku nikikutana na huyo mtu, ..sizani kama polisi au
nani ataweza kunizuia, ..yaani mpaka nihakikishe na yeye hayupo hapa duniani
tena..’ilikuwa sauti ya huyo mzee .
‘Usiseme hivyo mzee, unajua kauli kama hizo zinaweza kukufunga,
inaweza ikatoke ala kutokea huyo mtu akazurika na jambo jingine watu wakavumisha
kuwa wewe ulisema utafanya hivyo, chunga ulimi wako mzee…’yawezekana ikawa
sauti ya docta.
‘Hilo mimi sijali nimeshatamka hivyo, kama yeye alijiona kidume
basi nitauona huo udume wake,…ngoja nijiweke vyema, sijachoka kumtafuta, ila
nahisi ipo siku atajitokeza tu..’akasema huyoo mzee.
Na mimi nikawa nipo mlangoni, kumbe docta aliweza kuniona nikiwa
nimesimama kule mlangoni akasema;
‘Ni nani wewe upo hapo mlangoni, sio muda wa kuona wagonjwa sa
hizi..’akasema na mimi moyoni nikasema,
‘Sasa kumbe ndio mwanya wa kuondoka hapa na kukimbia moja kwa moja..na kabla sijachuku
maamuzi hayo mara nesi mmoja akaja kwa nyuma na kusema;
‘Mbona huingii, wenzako wanasubiria taarifa yako …wana furaha
kweli, usiwacheleweshe ingia, …’akasema nesi
‘Ni nani huyo …?’ akauliza docta kwa ndani
‘Si huyu msaidizi wa docta rafiki yako…’akasema nesi
‘Vipi lakini huko kuna taarifa nzuri, vipi huyo mgonjwa,…?’akasema
docta na mimi sasa nikawa nimeshaingia ndani hapo alipolazwa Mzee Mashauri.
‘Mambo mazuri kabisa, huwezi amini mgonjwa sasa anaongea,
nimemuacha akiongea na mama yake…’nikasema
‘Kweli eeh, mungu mkubwa, ..ooh, unaniafanya na mimi nitamani
kuinuka hapa, ooh, lakini mwili bado mnzito....’baba akasema akionyesha furaha;
‘Ni kweli baba na hivyo nimekuja kukuchukua, binti yako anasema
asipokuona wewe hataweza kupona vizuri, anataka kuhakikisha kuwa upo
salama..’nikasema.
‘Oh..docta,..inabidi niende,fanya ufanyavo ili niende huko
nikamuona huyo binti yangu,…siwezi kuzuia hiyo furaha, nahisi kupona,..ooh,
mwili bado mnzito, nisaidie docta nisimame…’akasema na docta akataka kusita
lakini baadae akawa anamsaidia huyo mzee na mzee akaweza kusimama.
‘Docta nimepona, nitajikongoja mpaka nifike huko, nataka bint yangu
apone haraka…anione nikiembea mwenyewe na kufika hapo alipo…’akasema na kweli
akaanza kujikongoja, hatua kwa hatua, na kila hatua ikawa inaleta maendeleo ya
hatua nyingine mpaka akaanza kujichanganya.
‘Sasa safi..’akasema docta.
‘Lakini ..naona..’ halafu nikatembea hadi pale nikawa namsaidia
huyo mzee, huku moyoni nikiomba, na kumbe nilikuwa naongea kwa sauti…
‘Ewe mola wangu nakuomba umuwezeshe huyu mzee, baba wa binti, ili
aweze kupona ili aweze kumuwezesha bint yake apone haraka, na wote wapone
haraka, ili iwe furaha kwetu sote, na furaha iweze kufuta yaliyopita..oh, mola
tusaidie kwa maombi yatu…’nikawa naomba hivyo, mara baba akasema
‘Aamini..’ nikashtuka, na kushtuka kule nikawa nimemuachia huyo
mzee, akayumba akataka kudondoka, lakini akajikaza na kuanza kuvuta hatua, moja
mbili tatu…akaanza kutembea vyema, huyoo…hatua kwa hatua, sasa yupo peke yake
bila kushikiliwa.
‘Oh, kijana kweli wewe una kipaji, maombi na duwa zako zimefnaya
kazi, nahisi nguvu ya ajabu, nahisi kupona,..twende mimi nipo tayari…’akasema
na docta muda huo yupo nyuma yetu akitufuata nyuma kwa karibu..
‘Safi kabisa, naona sasa mzee umeshapona, ..jitahidi..’akasema
docta
‘Kama umechoka mzee nikusaidie..’’nikasema
‘Hapana wewe mwenyewe umesema bint yangu anataka kuniona,
nikikitembea peke yangu mnzima ili aweze kupona haraka, …usinishike kabisa,
twende, hatua kwa hatua hakikisha huchezi mbali, ila usiniguse…’akasema sasa
kitembea vyema na huku akinitupia macho na kuniangalia kwa macho yenye udadisi,
akasema
‘Na wewe….sijui nitakupa nini, nimesikia sifa zako kutoka kwa
mwalimu wako, docta kuwa una kipaji cha kuombea watu, …na ninauhakika ndio wewe
umeweza kumuomba binti yangu, sasa anapona au sio, namshukuru sana mungu
kuwezesha nyie kuwepo, maana haya yote ni kwa uwezo wa mungu,…na nikuulize
kitu, wewe umeshaoa, una watoto wangapi?’ akaniuliza
‘Bado mzee, …mimi bado sijaoa, ndio natafuta mke…’nikasema
‘Usiogope kuoa, maana ndoa ni wajibu, na maisha, riziki, mungu mwenyewe atajalia tu kwa neema zake, na
kuoa haraka kuna baraka zake, unapata watoto mapema, na unakuja kufaidi matunda
ya watoto wako ukiwa bado una nguvu…sasa oh, natamani wewe sasa uwe mkwe wangu,
unasemaje…’akasema
Moyoni nikasema;
‘Imejipa, lakinni..mtihani huu…’nilijikuta nikisema
‘Mtihani kwa vipi, humpendi bint yangu kwa vile hajiwezi, wewe sio
ndio utamtibia,.usije kusema nakutupia mzigo, atapona huyo binti…lakini
sikulazimishi, ila nimekupenda sana, sio kama hiyo mihuni mingine inadanganya,
ilimpa binti yangu mimba, na ikaja kumtelekeza hao sio watu., ni wanyama..’akasema
kwa hasira.
‘Mzee, cha muhimu sana ni kusamehe, ili upone vyema, usiposamehe
ukaweka mafundo ya hasira, visasi, kupona inakua vigumu sana, samehe na wewe
utasamehewa..’nikasema nikifuatilia maneno aliyowahi kutamka docta.
‘Ni kweli eeh..sawa, kwa ajili ya binti yangu kama inabidi kufanya
hivyo nitasamehe..lakini huyo mtu lazima nimfanye kitu kibaya…oh, kusamehe
vigumu kijana wangu, tunakaribia, sasa uniache, ila usicheze mbali ukiniona
nayumba tu , usogee..haya fungua mlango..
NB: Naishia hapa
WAZO LA
LEO:
Tujihaidi sana kuweka nyoyo zetu mbali na shetani, shiriki ni namna mojawapo ya
kumpokea shetani, matendo mabaya kama wizi, uwongo, nk,..ni namna nyingine ya
kumpokea shetani kwenye maisha yetu...
Kuna watu wanamkaribisha shetani kwenye maisha yao bila wenyewe kujijua, ukifanya shiriki, ukawa na chuki na wenzako, ukawa
muongo, mwizi, mdhulumaji, na madhambi mengine mbali mbali, ujue wewe umemkaribisha shetani
kuwa rafiki yako..tumkwepe shetani maana shetani ni adui wa mungu, naadui wa
mungu ni adui wetu…shetani kazi yake ni kufarakanisha ndoa, ndugu kwa ndugu,
wazazi na watoto,..marafiki na marafiki, ili wasipatane..tumkwepe na tumuondoe
shetani katika maisha yetu…
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment