HIKI NI KISA CHA JAMAA YANGU,...anahadithia mambo aliyokutana nayo.., ni mambo haya haya ya Mapenzi ya mitandao,-Kutafuta
MPENZI ndani ya FACEBOOK!
Siku hiyo nilikutana na huyo rafiki yangu, ..nilimuona kabadilika kweli
kakonda,..hana raha,…usoni kama hayupo sawa…anatembea na miguuni kavyaa ndala, zimechakaa, sio yule rafiki yangu tena aliyekuwa na gari lake, ..mnadhifu ....(sharobaro au msafi kama wanavyoitaga).
Nikaanza kumsalimia na kumuuliza kulikoni….
‘Mimi sitaki kabisa kujiunga na Facebook,…’akaanza kusema
hivyo, na kunifanya nishangae, kwanini kakimbilio huko kwenye mitandao.
‘Kwanini…?’ nikamuuliza
‘Huwezi amini, …nilishachanganyikiwa kabisa, isingelikuwa
juhudu za ndugu zangu, sasa hivi labda ningekuwa marehemu…maana nilishaanza
kupagawa, …nikawa navua nguo, sasa sijambo, ila naogoap hata kuwa kama zamani, …yaani we acha tu..’akasema.
‘Kwanini…?’ nikamuuliza nikiwa na shauku kubwa.
Unajua mimi nilishakuwa addicted,
na face book, ilikuwa simu na mimi, laptop na mimi, na kwenye simu au laptop ni mimi na facebook..na
kwenye facebook, …mimi na mpenzi wangu. …’akaanza kusema.
‘Kwahiyo akawaje na huyo mpenzi wako, nakumbuka uliwahi kuniambia una mpenzi na upo mbioni kufunga ndia, sasa imekuwaje, hukunitumia kadi, wewe mbaya wewe...?' nikamwambia .
‘Unajua sikuwahi kumuona ,au kukutana na huyo mpenzi wangu kabla , lakini nilikuwa na uhakika naye, ndio maana siku tuliyokutana nawe nikakuambia nipo mbioni kufunga ndoa naye....'akasema
'Kwani sasa imekuwaje...?' nikamuuliza
'Ni kisa cha aina yake, hakuna anayeweza kuamini hayo yalinikuta..na nawaomba jamani muweni makini sana..hili ni jambo limenikuta mwenyewe na ...ndio maana nasema sitaki tena kuingi ahuko kwenye facebook.....sitaki..sitaki....'akasema
Ina maana alikudanganya..?' nikaamuuliza
'Hapana...alikuwa mkweli tu...na alinipenda sana...lakini we acha tu....'akasema
'Sasa ilikuwaje mbona unaniacha njia panda, au...alikudanganya, au....?’ nikamuuliza
‘Aheri angelikuwa marehemu, au nimeachana naye ingelikuwa
afadhali kwangu…’akasema
‘Sasa tatizo ni nini…?’ nikamuuliza
‘Ni hivi …..’ ndio akaanza kuelezea
*************
‘Mimi nilibahatika kumpata huyo mpenzi kwenye mtandao wa Facebook,, nikaelewana
naye sana, tukawa tunatumiana picha,..yaani haipiti siku bila kuchat naye,..ikawa
sio siku tena, haipiti masaa,….mpaka sekunde , hutaamini, sikutamani binti
mwingine yoyote zaidi ya huyo,….tuliivana sana, tena sana…
‘Unajua ilifikia muda nalala na simu kitandani, kwani huwa mara
nyingi sana tunachat usiku kuliko mchana, kwasababu ya mishughuliko ya
kimaisha,, na usiku huwa tunaweka live..ile ya kuchat na video, mnaonana
kupitia kwenye video,..na hapo ninachati mpaka nashikiwa na usingizi na ndani
ya usingizi naota tupo naye…..
Yaani ilikuwa ni ajabu, kipindi hicho kwangu niliona ni
kawaida tu..ni ndoto tu, lakini baadae ndio nilikuja kuona ni kwanini ilikuwa
hivyo..
Ikafika muda nikaona ni lazima nimuoe,..tuonane naye uso kwa
uso..yeye alisema siwezi kumuoa uso kwa uso mpaka tujuane vyema, kwa kipindi
hicho nikaona tumeshajuana kimtandao, sasa tujuane kiukweli,…ikawa ni namna ya
kutembeleana, mimi nipajue kwao na yeye ikiwezekana aje kwangu..mimi naishi
mwenyewe,
Basi kila nikichat naye nikawa namsihi kuwa nataka nifike
nyumbani kwao, nikajitambulishe..
‘Hakuna shida honey…utafika tu, usiwe na haraka..mambo
manzuri hayataki haraka…’akasema maana tulishapeana kila jina nzuri la mapenzi,
ilibakia tu hiyo ya kuitwa mke wangu au mume wangu…
‘Basi tufanye wikiendi mimi nije kwenu, nitakuja mapema ili
tupate muda mnzuri wa kuongea mimi na wazazi wako, baadae tutoke kidogo tuende
sehemu mimi na wewe tu…’nikasema
‘I cant wait….’akasema
nikajua amekubali.
‘Nakupenda sana mpenzi wangu…’nikasema
‘Yaani mimi sijui nisemeje, nakupenda sana, my sweetie….’akasema.
Nikiwa nimetarajia kuwa wikiend ndio naenda kwao, usiku wake
sasa akaja na kipingamizi kuwa wazazi wake bado hawapo tayari nib ado mapema
sana mimi nikaamwambia;
‘Mimi siwezi kulala, siwezi kusubiria tena, bila ya kuja kuonana na wewe..’nikamwambia
‘Are you sure
unataka kuniona….?’ Akaniuliza swali hilo, nikashtuka kidogo, nikamwambia ;
‘More than sure,
unajuaga jinsi gani ninavyokupendaga…’nikamwambia.
‘But, nakuona
haupo tayari yet, unahitajika sana …sipendi wewe ujiingize mapema hivi, nakuona
bado bado wewe kama ilivyo mimi bado ni wadogo …’niliposikia hivyo nikamkatiza kwa
kusema;
‘Sikuelewi ukisema hivyo ina maana hutaki tuonane, ..nilijua
unanipenda sana…na umri wako mbona sawa na kwangu tumepishana kidogo tu …na leo
mbona unasema hivyo, tulishakubaliana ati..na, unaongea kama vile wewe ni
mkubwa sana…’nikamwambia
‘Hahaha sio hivyo mpenzi…unajua nakuonea huruma, maana ujue
ukijiingiza huko mimi nitakuwa nakutegemea wewe, je umeshajiweka sawa, …unajua
mimi nakupenda sana, ndio maana sitaki kukuharakishia kihivyo , nataka uwe
tayari kwa maisha hayo mengine, si unajua ndoa sio lele mama, na hasa ndoa yangu mimi na wewe …’akasema
‘Hapana mimi nipo tayari, siwezi kukurupuka tu,
nimeshajiandaa kwa kila kitu, nina nyumba, nina…wewe utakuja kujionea mwenyewe…’nikamwambia.
‘Najua …una maisha mazuri..lakini maisha mazuru tu
hayatoshi, …ndoa, na maisha hayo ya ndoa ni kitu kingine kabisa. Unatakiwa ujiandae,
usahau maisha mengine…mimi nakuomba usiharakishe kihivyo…unanielewa…’akasema,
sikutaka kubishana na yeye maana nilimpenda na sikutaka kumuuzi.
Basi siku zikaenda baadae tena nikaamua sasa iwe na iwe, ni
lazima nikajitambulishe kwa msichana nilitaka anielekeze kwao tu, mimi nitaenda
vyovyote iwavyo, basi siku hiyo naye hakutaka kuniudhi akasema;
‘Ok, kama umeamua,na upo tayari sina budi nikuelekeze nyumbani
kwangu…’akasema.
‘Sawa..nyumbani kwenu na wazazi wako au sio…kwani ni ndani
ndani sana….ulisema kwenu kila mtu anapafahamu a sio…?’ nikamuuliza
‘Ndio lakini ni ndani ndani sana…’akasema
‘Gari haliwezi kuiingia..?’ nikamuuliza
‘Haliwezi…’akasema.
‘Basi mimi nitachukua
pikipiki ili nifike kwa haraka..’nikamwambia
‘Mhh…hapana wewe chukua dala dala,…sitaki
ujiharakishie, kihivyo…wewe chukua usafiri usio wa haraka, ukifika maeneo
fulani nitakayokuelekeza vizuri zaidi…, na hapo utafuta maelekezo yangu..hadi
utafika nyumbani kwangu…’akasema.
‘Kwako na wazazi wako au sio…?’ nikamuuliza.
‘Usijali utafika tu…nyumbani kwangu…’akasema hivyo, na hiyo ‘kwangu..’
akawa anaitaja sana kuliko awali, awali aliniambia yeye anaishi na wazazi wake,
sasa hiyo kwangu ikawa, anyway ..kwa
muda huo sikuona ni kitu kisicho cha kawaida.
Basi siku hiyo nikajiandaa kwelikweli…si unajua ukiwa na
mpenzi, inavyokuwa na iwe ndio siku ya kwanza ya kutaka kukutana naye, halafu
ndio unakwenda kutambulishwa kwa wazazi…unajikagua mara kumi kidogo, …sikuwa na
shaka na utanashati wangu, hilo kwangu ni tabia….
Basi muda ukafika,..nikafanya
kama alivyotaka, daladala, japokuwa ni gari langu, hadi nikafika maeneo
aliyonielekeza na hapo nikatembea hadi huo mtaa alioniekeza, hapo nikasubiria
maelekezo yake na mara, ikaja ujumbe wa maandishi naelekezwa nipitia wapi na
wapi..
Mimi ni mkali wa ramani ukinielekeza mara moja siwezi
kupotea tena,..basi sikuwa na shaka ..nikaanza kufuatili ile ramani..nikatemba
mtaa wa kwanza nikaingia uchochoro, nikatembea bara baraba, kwenye duka kubwa…halafu
mti mkubwa wa mbuyu….huyooo, tembea tembea, halafu..unatokea nyumbani kwake.
Naangalia mbele sioni nyumba, …nikageuka kushoto na kulia
sioni nyumba kama hiyo, nikaitizama ramani …sijakosea, naangalia hapo
nilipoambiwa nitakuta nyumba, sioni zaidi ya
MAKAUBURI….
‘Ohh, huyu honey, kakosea nini..nikajaribu kumpigia simu kwa
namba ile ile, lakini sasa simu haipatikani, sio kawaida yake, haijawahi
kutokea,…nikarejea ramani, naona sijakosea, na siwezi kukosea mimi, najua vyema
ramani…nikasubiria, nikapiga simu , haipatikani…baadaye nimejichokea nikaamua
nirudi nyumbani tu…
Nilichoka, maana sio karibu kwa kutembea, niligundua hilo
wakati narudi maana wakati nakwenda sikuliona hilo, nilipaona ni karibu tu.
Nilipofika nyumbani kwangu nikajirusha kitandani, huku nikihangaika kuitafuta ile namba yake,...namba siioni, sio kawaida...nikawa nahangaika wewe...na mara usingizi mnzito
ukanijia,…
**********
2
‘Mpenzi mbona hukufika nyumbani…?’ anaulizwa
‘Nilifuata ramani kama ulivyonielekeza lakini sikuiona
nyumba yenu…’nikasema
‘Siwezi kuamini, mbona nyumba yetu ipo wazi kabisa….…’akasema
‘Sikuiona hiyo nyumba honey..nilichoona mbele yangu ni
makaburi….’nikasema
‘Hahaha…’akacheka sana, halafu akasema;
‘Sasa ..kwanini hukusogea mbele hadi sehemu niliyokuelekezea..?’
akaliza
‘Ilikuwa makaburini, ningepitaje..huko mbele, unaelewa
ninachokuambia, mbele yangu hakukuwa na nyumba kulikuwa na makaburini…..’ nikamwambia
‘Ina maana hunipendi au..?’ akauliza
NB…Niendelee???Ni kisa kifupi tu, subiria sehemu ya pili uone vituko vya dunia, ..kuweni makini jamani ....
WAZO LA LEO: Tuweni
makini sana tunapotaka urafiki, na hasa ikiwa rafiki huyo hujawahi kukutana
naye kuna zamani iliitwa urafiki wa kalamu, sasa hivi urafiki wa mitandao..ni
sawa kwa wenzetu, wao wapo mbali na aina hii ya urafiki, maana kwao kila kitu
kipo wazi, kumbukumbu za watu picha zao, anuani, nyumba , mitaa..sisi je..hayo
yapo, je ukweli wa taarifa upo…bado tupo nyuma kwa hilo..kwahiyo ni nyema,
tukawa makini sana tunapotaka kuchagu rafiki kwa njia hii.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment