Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, April 5, 2017

MPENZI WA FACEBOOK-1



HIKI NI KISA CHA JAMAA YANGU,...anahadithia mambo aliyokutana nayo.., ni mambo haya haya ya Mapenzi ya mitandao,-Kutafuta MPENZI ndani ya FACEBOOK! 

Siku hiyo nilikutana na huyo rafiki yangu, ..nilimuona kabadilika kweli kakonda,..hana raha,…usoni kama hayupo sawa…anatembea na miguuni kavyaa ndala, zimechakaa, sio yule rafiki yangu tena aliyekuwa na gari lake, ..mnadhifu ....(sharobaro au msafi kama wanavyoitaga).

Nikaanza kumsalimia na kumuuliza kulikoni….

‘Mimi sitaki kabisa kujiunga na Facebook,…’akaanza kusema hivyo, na kunifanya nishangae, kwanini kakimbilio huko kwenye mitandao.

‘Kwanini…?’ nikamuuliza

‘Huwezi amini, …nilishachanganyikiwa kabisa, isingelikuwa juhudu za ndugu zangu, sasa hivi labda ningekuwa marehemu…maana nilishaanza kupagawa, …nikawa navua nguo, sasa sijambo, ila naogoap hata kuwa kama zamani, …yaani we acha tu..’akasema.

‘Kwanini…?’ nikamuuliza nikiwa na shauku kubwa.

Unajua mimi nilishakuwa addicted, na face book, ilikuwa simu na mimi, laptop na mimi, na kwenye simu au laptop ni mimi na facebook..na kwenye facebook, …mimi na mpenzi wangu. …’akaanza kusema.

‘Kwahiyo akawaje na huyo mpenzi wako, nakumbuka uliwahi kuniambia una mpenzi na upo mbioni kufunga ndia, sasa imekuwaje, hukunitumia kadi, wewe mbaya wewe...?' nikamwambia .

‘Unajua sikuwahi kumuona ,au kukutana na huyo mpenzi wangu kabla , lakini nilikuwa na uhakika naye, ndio maana siku tuliyokutana nawe nikakuambia nipo mbioni kufunga ndoa naye....'akasema

'Kwani sasa imekuwaje...?' nikamuuliza

'Ni kisa cha aina yake, hakuna anayeweza kuamini hayo yalinikuta..na nawaomba jamani muweni makini sana..hili ni jambo limenikuta mwenyewe na ...ndio maana nasema sitaki tena kuingi ahuko kwenye facebook.....sitaki..sitaki....'akasema

Ina maana alikudanganya..?' nikaamuuliza

'Hapana...alikuwa mkweli tu...na alinipenda sana...lakini we acha tu....'akasema

 'Sasa ilikuwaje mbona unaniacha njia panda, au...alikudanganya, au....?’ nikamuuliza

‘Aheri angelikuwa marehemu, au nimeachana naye ingelikuwa afadhali kwangu…’akasema

‘Sasa tatizo ni nini…?’ nikamuuliza

‘Ni hivi …..’ ndio akaanza kuelezea

*************

‘Mimi nilibahatika kumpata huyo  mpenzi kwenye mtandao wa Facebook,, nikaelewana naye sana, tukawa tunatumiana picha,..yaani haipiti siku bila kuchat naye,..ikawa sio siku tena, haipiti masaa,….mpaka sekunde , hutaamini, sikutamani binti mwingine yoyote zaidi ya huyo,….tuliivana sana, tena sana…

‘Unajua ilifikia muda nalala na simu kitandani, kwani huwa mara nyingi sana tunachat usiku kuliko mchana, kwasababu ya mishughuliko ya kimaisha,, na usiku huwa tunaweka live..ile ya kuchat na video, mnaonana kupitia kwenye video,..na hapo ninachati mpaka nashikiwa na usingizi na ndani ya usingizi naota tupo naye…..

Yaani ilikuwa ni ajabu, kipindi hicho kwangu niliona ni kawaida tu..ni ndoto tu, lakini baadae ndio nilikuja kuona ni kwanini ilikuwa hivyo..

Ikafika muda nikaona ni lazima nimuoe,..tuonane naye uso kwa uso..yeye alisema siwezi kumuoa uso kwa uso mpaka tujuane vyema, kwa kipindi hicho nikaona tumeshajuana kimtandao, sasa tujuane kiukweli,…ikawa ni namna ya kutembeleana, mimi nipajue kwao na yeye ikiwezekana aje kwangu..mimi naishi mwenyewe,

Basi kila nikichat naye nikawa namsihi kuwa nataka nifike nyumbani kwao, nikajitambulishe..

‘Hakuna shida honey…utafika tu, usiwe na haraka..mambo manzuri hayataki haraka…’akasema maana tulishapeana kila jina nzuri la mapenzi, ilibakia tu hiyo ya kuitwa mke wangu au mume wangu…

‘Basi tufanye wikiendi mimi nije kwenu, nitakuja mapema ili tupate muda mnzuri wa kuongea mimi na wazazi wako, baadae tutoke kidogo tuende sehemu mimi na wewe tu…’nikasema

I cant wait….’akasema nikajua amekubali.

‘Nakupenda sana mpenzi wangu…’nikasema

‘Yaani mimi sijui nisemeje, nakupenda sana, my sweetie….’akasema.

Nikiwa nimetarajia kuwa wikiend ndio naenda kwao, usiku wake sasa akaja na kipingamizi kuwa wazazi wake bado hawapo tayari nib ado mapema sana mimi nikaamwambia;

‘Mimi siwezi kulala, siwezi kusubiria tena,  bila ya kuja kuonana na wewe..’nikamwambia

Are you sure unataka kuniona….?’ Akaniuliza swali hilo, nikashtuka kidogo, nikamwambia ;

More than sure, unajuaga jinsi gani ninavyokupendaga…’nikamwambia.

‘But, nakuona haupo tayari yet, unahitajika sana …sipendi wewe ujiingize mapema hivi, nakuona bado bado wewe kama ilivyo mimi bado ni wadogo …’niliposikia hivyo nikamkatiza kwa kusema;

‘Sikuelewi ukisema hivyo ina maana hutaki tuonane, ..nilijua unanipenda sana…na umri wako mbona sawa na kwangu tumepishana kidogo tu …na leo mbona unasema hivyo, tulishakubaliana ati..na, unaongea kama vile wewe ni mkubwa sana…’nikamwambia

‘Hahaha sio hivyo mpenzi…unajua nakuonea huruma, maana ujue ukijiingiza huko mimi nitakuwa nakutegemea wewe, je umeshajiweka sawa, …unajua mimi nakupenda sana, ndio maana sitaki kukuharakishia kihivyo , nataka uwe tayari kwa maisha hayo mengine, si unajua ndoa sio lele mama, na hasa ndoa yangu mimi na wewe …’akasema

‘Hapana mimi nipo tayari, siwezi kukurupuka tu, nimeshajiandaa kwa kila kitu, nina nyumba, nina…wewe utakuja kujionea mwenyewe…’nikamwambia.

‘Najua …una maisha mazuri..lakini maisha mazuru tu hayatoshi, …ndoa, na maisha hayo ya ndoa ni kitu kingine kabisa. Unatakiwa ujiandae, usahau maisha mengine…mimi nakuomba usiharakishe kihivyo…unanielewa…’akasema, sikutaka kubishana na yeye maana nilimpenda na sikutaka kumuuzi.

Basi siku zikaenda baadae tena nikaamua sasa iwe na iwe, ni lazima nikajitambulishe kwa msichana nilitaka anielekeze kwao tu, mimi nitaenda vyovyote iwavyo, basi siku hiyo naye hakutaka kuniudhi akasema;

‘Ok, kama umeamua,na upo tayari sina budi nikuelekeze nyumbani kwangu…’akasema.

‘Sawa..nyumbani kwenu na wazazi wako au sio…kwani ni ndani ndani sana….ulisema kwenu kila mtu anapafahamu a sio…?’ nikamuuliza

‘Ndio lakini ni ndani ndani sana…’akasema

‘Gari haliwezi kuiingia..?’ nikamuuliza

‘Haliwezi…’akasema.

‘Basi mimi  nitachukua pikipiki ili nifike kwa haraka..’nikamwambia

‘Mhh…hapana  wewe chukua dala dala,…sitaki ujiharakishie, kihivyo…wewe chukua usafiri usio wa haraka, ukifika maeneo fulani nitakayokuelekeza vizuri zaidi…, na hapo utafuta maelekezo yangu..hadi utafika nyumbani kwangu…’akasema.

‘Kwako na wazazi wako au sio…?’ nikamuuliza.

‘Usijali utafika tu…nyumbani kwangu…’akasema hivyo, na hiyo ‘kwangu..’ akawa anaitaja sana kuliko awali, awali aliniambia yeye anaishi na wazazi wake, sasa hiyo kwangu ikawa, anyway ..kwa muda huo sikuona ni kitu kisicho cha kawaida.

Basi siku hiyo nikajiandaa kwelikweli…si unajua ukiwa na mpenzi, inavyokuwa na iwe ndio siku ya kwanza ya kutaka kukutana naye, halafu ndio unakwenda kutambulishwa kwa wazazi…unajikagua mara kumi kidogo, …sikuwa na shaka na utanashati wangu, hilo kwangu ni tabia….

Basi  muda ukafika,..nikafanya kama alivyotaka, daladala, japokuwa ni gari langu, hadi nikafika maeneo aliyonielekeza na hapo nikatembea hadi huo mtaa alioniekeza, hapo nikasubiria maelekezo yake na mara, ikaja ujumbe wa maandishi naelekezwa nipitia wapi na wapi..

Mimi ni mkali wa ramani ukinielekeza mara moja siwezi kupotea tena,..basi sikuwa na shaka ..nikaanza kufuatili ile ramani..nikatemba mtaa wa kwanza nikaingia uchochoro, nikatembea bara baraba, kwenye duka kubwa…halafu mti mkubwa wa mbuyu….huyooo, tembea tembea, halafu..unatokea nyumbani kwake.

Naangalia mbele sioni nyumba, …nikageuka kushoto na kulia sioni nyumba kama hiyo, nikaitizama ramani …sijakosea, naangalia hapo nilipoambiwa nitakuta nyumba, sioni zaidi ya  MAKAUBURI….

‘Ohh, huyu honey, kakosea nini..nikajaribu kumpigia simu kwa namba ile ile, lakini sasa simu haipatikani, sio kawaida yake, haijawahi kutokea,…nikarejea ramani, naona sijakosea, na siwezi kukosea mimi, najua vyema ramani…nikasubiria, nikapiga simu , haipatikani…baadaye nimejichokea nikaamua nirudi nyumbani tu…

Nilichoka, maana sio karibu kwa kutembea, niligundua hilo wakati narudi maana wakati nakwenda sikuliona hilo, nilipaona ni karibu tu. 

Nilipofika nyumbani kwangu nikajirusha kitandani, huku nikihangaika kuitafuta ile namba yake,...namba siioni, sio kawaida...nikawa nahangaika wewe...na mara  usingizi mnzito ukanijia,…

**********
2

‘Mpenzi mbona hukufika nyumbani…?’ anaulizwa
‘Nilifuata ramani kama ulivyonielekeza lakini sikuiona nyumba yenu…’nikasema
‘Siwezi kuamini, mbona nyumba yetu ipo wazi kabisa….…’akasema
‘Sikuiona hiyo nyumba honey..nilichoona mbele yangu ni makaburi….’nikasema
‘Hahaha…’akacheka sana, halafu akasema;
‘Sasa ..kwanini hukusogea mbele hadi sehemu niliyokuelekezea..?’ akaliza
‘Ilikuwa makaburini, ningepitaje..huko mbele, unaelewa ninachokuambia, mbele yangu hakukuwa na nyumba kulikuwa na makaburini…..’ nikamwambia
‘Ina maana hunipendi au..?’ akauliza

NB…Niendelee???Ni kisa kifupi tu, subiria sehemu ya pili uone vituko vya dunia, ..kuweni makini jamani ....


WAZO LA LEO: Tuweni makini sana tunapotaka urafiki, na hasa ikiwa rafiki huyo hujawahi kukutana naye kuna zamani iliitwa urafiki wa kalamu, sasa hivi urafiki wa mitandao..ni sawa kwa wenzetu, wao wapo mbali na aina hii ya urafiki, maana kwao kila kitu kipo wazi, kumbukumbu za watu picha zao, anuani, nyumba , mitaa..sisi je..hayo yapo, je ukweli wa taarifa upo…bado tupo nyuma kwa hilo..kwahiyo ni nyema, tukawa makini sana tunapotaka kuchagu rafiki kwa njia hii.
Ni mimi: emu-three

No comments :